ASKARI POLISI APORWA SMG KWA PANGA

Matukio ya kuvamia askari wakiwa lindoni, vituo na vizuizi vya polisi nchini yameendelea kulitafuna Jeshila Polisi na safari hii, Askari wa Kikosi cha Tazara, Jijini Dar es Salaam, ameporwa SMG na kujeruhiwa vibaya.

Tukio hilo lilitokea juzi usiku saa sita kwa watu wanaosadikiwa ni majambazi wakiwa na silaha za jadi kumvamia askari huyo akiwa kwenye lindo la Tazara na kupora silaha hiyo.

Kwa mujibu wa taarifa kutoka eneo la tukio, watu wawili wakiwa na silaha za jadi, nyakati za saa sita usiku walivamia eneo hilo na kupora silaha hiyo na kutokomea nayo.

Taarifa hizo zinafafanua kuwa askarihuyo alijeruhiwa vibaya sehemu mbalimbali za mwili na amelazwa hospitali kwa matibabu zaidi, ingawa jina lake halikutajwa wala hospitali aliyolazwa.

Kamanda wa Kikosi hicho, Kamanda Bieteo, akizungumza na NIPASHE kwa njia ya simu, alithibitisha kuwepo kwa tukio hilo na kusema kuwa hawezi kutoa ufafanuzi kwa simu bali kwa taarifa ya maandishi.

"Tukio lipo ni kweli wamemvamia askari akiwa lindoni kumjeruhi na kumpora silaha…siwezi kutoa ufafanuzi zaidi kwa simu, leo nitatoa taarifa kwa maandishi," alisema.

Alipotakiwa kueleza zaidi alijibu kwamfupi: "Nitafute kesho (leo), nitaandaa taarifa ya maandishi, sipotayari kueleza kwenye simu."

Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Suleiman Kova, alipoulizwa, alithibitisha, lakini akamuelekeza mwandishi kuwasiliana na Kamanda Bieteo.

Januari 21, mwaka huu, usiku huko kituo cha Polisi Ikwiriri - Rufiji majambazi wakiwa na bunduki walivamia kituo cha Polisi na kuwaua askari wawili na kupora bunduki aina ya SMG 2, SAR 2, Anti Riot gun moja, Shotgun moja na risasi 60.

Machi 30, mwaka huu barabara ya Kilwa kwenye kizuizi cha Polisi eneola Shule ya Sekondari St. Mathew Kongowe kata ya Vikindu Wilayani Mkuranga, majambazi wasiofahamika wakiwa na mapanga na silaha zingine za jadi walimuua askari mmoja kisha kupora bunduki moja aina ya SMG ikiwa na risasi 30.

Hivi karibuni, Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mathias Chikawe, alisema idadi ya matukio ya uvamiziwa vituo vya polisi imeongezeka kutoka sita kwa mwaka 2014 hadi nane kwa mwaka 2015.

Alisema katika matukio hayo jumla ya askari saba waliuawa kwa mchanganuo kwenye mabano Chamazi (2), Mkuranga (2) na Ushirombo (3)Bunduki zilizoporwa ni bunduki 22 na mchanganuo wake ni Chamazi (2), Mkuranga (1), Ushirombo (17) na Tanga (2).

CHANZO: NIPASHE