WAKIMBIZI TOKA BURUNDI WALIOINGIA NCHINI WAFIKI 1852

Idadi ya watu wanaoingia nchini kutoka Burundi kukimbia machafuko ya kisiasa kupitia mkoani Kigoma, imezidi kuongezeka kutoka 1,645 hadi kufikia 1,852.

Kati ya hao, 1,252 tayari wameshasajiliwa kama wakimbizi rasmi na kupelekwa katika kambi yaNyarugusu, wilayani Kasulu.

Hayo yalibainishwa na msemaji wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Isaac Nantanga, wakati wa mahojiano na NIPASHE.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na wizara hiyo juzi, hadi kufikia Aprili 30, mwaka huu, mkoa huo ulikuwa umeshapokea idadi ya watu 500 walioingia kupitia vijiji sita vya Kibuye, Kagunga, Kosovo, Kakonko, Sekeeye na Kigaye.

Kwa mujibu wa msemaji huyo, haliya usalama katika maeneo ya mipakani, imeimarishwa na kutoa wito kwa wakazi wa maeneo hayo kutoa taarifa kwa uongozi wa vijiji iwapo kuna mgeni asiyefahamika kufika maeneo hayo.

Kwa upande wake, Afisa wa Idara ya Uhamiaji Mkoa wa Kigoma, MauriceDavid, alisema hadi juzi jioni idadi ya wakimbizi walioingia mkoani humo ilifikia 1,645.

David alisema wakimbizi kutoka Burundi walianza kuingia mkoani humo Aprili 26, mwaka huu kupitia wilaya za mkoa huo na idadi kwenye mabano kuwa ni Buhigwe (156), Kigoma Vijijini (1,155), Kibondo (260, Kasulu (195) na Nyarugusu (64) ambao walikwenda moja kwa moja katika kambi hiyo bila kupitia katika vituo vya Uhamiaji.

Hata hivyo, aliongeza kuwa idadi ya wakimbizi waliofika kabla ya kuzuka upya kwa vurugu hizo nchini humo ilikuwa 46, lakini hadi jana mkoa mzima ulikuwa umepokea jumla ya wakimbizi takribani I, 852.

Burundi imekumbwa na vurugu kutokana na maandamano yanayofanyika kwenye mji mkuu wanchi hiyo Bujumbura, kwa wananchikupinga hatua ya Rais Pierre Nkurunziza kutaka kugombea tena urais kwa muhula wa tatu kinyume cha katiba ya nchi hiyo.

Katiba ya Burundi inataja muda wa urais kuwa ni vipindi viwili, lakini Rais Nkurunziza anadai kusimamia makubaliano ya Mkataba wa Arusha kwamba kipindi chake kilianza pale mkataba huo uliposainiwa, hivyo muda aliokuwa madarakani kabla ya kusainiwa usihesabiwe.

Chanzo: NIPASHE