IDADI YA WALIOKUFA KUTOKANA NA JOTO YAONGEZEKA INDIA

Idadi ya watu waliopoteza maisha kutokana na ongezeko la joto nchini India imefikia 1,412 huku joto likifikia takriban nyuzi joto 47.

Watu 550 walikufa katika miji ya Andhra na Pradesh huku wengine zaidi ya 215 wakishindwa kukabiliana na joto hilo mjini Telangana.

Msimamizi shughuli za majanga nchini humo Saada Bhargavi amesema kuwa vifo katika jimbo la Telangana vimefika watu 215 tangu kuanza kwa joto hilo kali hapo Mei 15.

Mamlaka ya hali ya hewa nchini India ilitangaza kuwa hali ya joto katika majimbo ya Telangana na Andhra Pradesh inategemewa kuwa nyuzi joto 29 na 41 kwa siku zijazo.

Mji mkuu wa India, New Delhi umefikisha nyuzi joto 45.5 mpaka sasa.