RAIS KENYATTA AKWAMA KWENDA NIGERIA

Rais Uhuru Kenyatta alisitisha ziara yake ya kwenda Nigeria siku ya Alhamisi masaa kumi na moja baada ya kuibuliwa maswali dhidi ya idadi kubwa ya maafisa ambao aliungana nao kwenye safari hiyo.

Badala yake, Kenyatta alimtuma makamu wa rais William Ruto kumuwakilisha katika kuapishwa kwa rais mpya wa Nigeria, Jenerali Muhammadu Buhari, leo.

Safari ya rais ilisitishwa siku moja baada ya maafisa 84 wa serikali ambao waliungana naye kuvujishwa kwenye vyombo vya habari. Maswali yaliulizwa kuhusu ukubwa wa ujumbe huo.

Hii ni mara ya pili kwa Kenyatta kusitishiwa safari zake, mwezi uliopita, ndege yake iligeuka angani katika hali ya kushangaza wakati akielekea Marekani baada ya kuhitajika kuitisha mkutano wa biashara nchini kwake.

Taarifa za kugeuka kwa ndege yake hazikuelezwa kwa kina japo inadaiwa kuwa ndege hiyoiligeuka ikiwa anga la Ethiopia.