KIONGOZI WA UPINZANI BURUNDI AUWAWA

Kiongozi wa chama kidogo cha upinzani nchini Burundi ameuawa kwa kupigwa risasi.

Mwili wa Zedi Feruzi pamoja na wa mlinzi wake ulipatikana nje yanyumba yake kwenye mji mkuu Bujumbura.

Mauaji ya mwanasiasa huyo yanafanyika wakati wanaharakati wa upinzani nchini humo wamesitisha kwa siku mbili maandamano yao dhidi ya rais Pierre Nkurunziza kupinga uamuzi wake wa kuwania urais muhula wa tatu.

Uamuzi huo ambao wengine wanasema kuwa unaenda kinyume na sheria umesababisha kuwepo kwa jaribio la kumpindua, maandamano ya wiki kadha na kuhama kwa zaidi ya watu 100,000 kutoka nchini humo.