WATANZANIA WAHUSISHWA NA MAUAJI YA ALBINO MALAWI

Mauaji ya watu wenye ulemavuwa ngozi (Albino) yameendelea kuharibu taswira ya ya nchi na jumuiya ya kimataifa baada ya taarifa kudai kwamba wahalifu wa Tanzania wanahusishwa na unyama huo nchini Malawi.

Kwa mujibu wa habari iliyochapishwa wiki iliyopita kwenye Nyasa Times, gazeti la Malawi likiwa na kichwa cha habari Albino "wanawindwa kama wanyama" kwa viungo vya mwili nchini Malawi, mwanaharakati alikaririwa kwenye habari hiyo akisema, baada ya Tanzania kuanza jitihada za kupambana na vitendo hivyo, wahalifu hao wamehamia Malawi sasa.

Shirika la Watu wenye Ulemavu wa Ngozi nchini Malawi (APAM) lilikaririwa katika habari hiyo ya gazeti hilowakisema, watu wanaojihusishana uuzaji wa viungo vya albino wamepata soko Malawi baada ya kuona ugumu wa biashara hiyo nchini Tanzania.

"Wale ambao wako katika biashara ya kuuza viungo vya albino… wameanzisha soko nchini Malawi, kwa sababu imekuwa vigumu kufanya biashara nchini Tanzania," Boniface Massah aliliambia gazeti hilo.

"Tunawinda kama wanyama, huna uhakika kuwa unaweza kuwaamini marafiki au ndugu,"alisema rais wa APAM Massah, ambaye anapiga kampeni za haki za albino Malawi.

Kwa mujibu wa takwimu nchini Malawi, kulikuwa na mauaji ya albino wawili mwaka 2014 na moja 2013.
Gazeti hilo limeeleza kuwa Malawi na watu wapatao 10,000 wenye ulemavu wa ngozi.