MTOTO ANAEFANANA NA ALBINO ATEKWA NA KUUAWA

Loveness Maliaki (11), mtoto wa darasa la nne shule ya msingi Osunyai Sombetini, anayedaiwa kufanana na watu wenye ulemavu wa ngozi (Albino), ametekwana kuuawa na kunyofolewa viungo vyake vya siri, pua na macho kutobolewa.

Mama wa marehemu, Mary Kilongo (37), alisema walimpata mtoto huyo akiwa amefichwa chini ya uvungu, kwenye nyumba mbovu ya udongo inayomilikiwa na Henry Ally (58) ambaye wakati wa tukio hilo inadaiwa hakuwapo.

"Wakati wakitoka shule jioni akiwa ameongozana na wenzake huyo kijana (anamtaja mtuhumiwa) Tunamfahamu, aliwafuata watoto akiwa anaendesha baiskeli yake akawaambia kuwa kuna hela yangu imetumwa kwa M-Pesa kwenye simu yake,"

alieleza na kuongeza: "Akawataka wamfuate wakaichukue, alimkatalia basi akaamua kumchukua marehemu kwa nguvu na kumpandisha kwenye baiskeli yake na kuondoka naye, hivyo wale waliobaki wakaja kunieleza."

Mjomba wa marehemu, Mohamedi Kilongo, alisema alipouangalia mwili wa marehemu ulionekana kama alinyogwa shingo, kwani alikuwa na alama

Chanzo:East Africa Radio!