MABINTI 12 WAKAMATWA KWA UNGA NDANI YA SIKU 30

Licha ya kampeni kubwa ya kupambana na kuzuia usafirishaji, uuzaji na matumizi ya dawa za kulevya nchini, bado Watanzania wameendelea kufanya biashara hiyo na katika kipindi cha siku 30 mabinti 12 wamekamatwa wakisafirisha dawa hizo ndani na nje ya nchi.

Taarifa zilizolifikia gazeti hili na kuthibitishwa na Kamishna wa Kikosi cha Kupamba na Dawa za Kulevya nchini, Godfrey Nzowa zinaonyesha kuwa idadi kubwa ya Watanzania waliokamatwa katika kipindi hicho ni mabinti wenye umri mdogo.

Kwa mujibu wa taarifa hizo, mabinti wanane wamekamatwa katika Uwanja wa Ndege wa Hong Kong na wanne katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Dar es Salaam.

Kamishna Nzowa alisema ingawa vyombo vya habari na wafungwa walioko Hong Kong wamejaribu kuwashauri Watanzania wasifanye biashara hiyo, bado wamekuwa na 'shingo ngumu.'

Alisema Januari 23, wanawake wawili, Rehema Ndunguru (31) na Moyo Ramadhani (31) walikamatwa katika Uwanja wa Ndege wa Julius Nyerere wakisafirisha dawa hizo kwenda Hong Kong.

"Rehema alikuwa amemeza pipi 78 ambazo ni sawa na kilo 1.2 na Moyo alitoa pipi 86 sawa na kilo 1.5," alisema Kamanda Nzowa.

Alisema Februari 12, mwaka huu alikamatwa mwanamke mwingine Munira Mohamed (27) akiwa amemeza pipi zenye uzito sawa na kilo 1.

Februari 9, mwaka Halmati Tango (21) alikamatwa akiwa na pipi 76 zenye uzito sawa na kilo 1.3.

Nzowa alisema Halmat alikuwa akisafirisha dawa hizo kwenda Nigeria wakati Munira alikuwa akizipeleka Mombasa.


Hong Kong

Wakati huo huo, Padri John Wotherspon aliyekuwa nchini kwa ajili ya kampeni ya kuwazuia vijana wa Kitanzania kusafirisha dawa za kulevya amelieleza Mwananchi kuwa wanawake wanane wa Kitanzania pia wamekamatwa katika uwanja wa ndege wa Hong Kong katika kipindi hicho hicho.

Padri Wotherspon alisema baadhi ya wanawake hao wamekiri kusikia na kuona barua za wafungwa wa China zilizoonya kuhusu biashara hiyo lakini wakachukua uamuzi wa kuzibeba. Kati ya wanawake hao wanane, mmoja alikuwa amemeza kete 135 za dawa za kulevya aina yaheroin na mwingine alikuwa amemeza kete 86.

"Kwangu mimi vita inazaa matunda, tunapowakamata ina maana tunazuia," Nzowa. kusambazwa kwa mzigo," alisema.


Chanzo: Mwananchi