Taifa Stars Yaifumua Morocco

Taifa Stars imefanya kile Watanzania walichowatuma baada ya kuwalaza
Simba wa Atlas kwa mabao matatukwa moja. Kipindi cha kwanza Stars
walicheza kandanda la kuvutia na kupoteza nafasi nyingi za wazi huku
Mbwana Samatta akionekana kuwa mwiba mkali kwa beki ya Morocco muda
wote. Katika kipindi cha pili, Thoma Ulimwengu akitokea benchi
alifunga bao la kwanza baada ya kuunganisha mpira wa kona, Dakika ya
66 ilikuwa ni Mbwana Samatta ambaye alimchambua golikipa wa Morocco na
kufunga bao la pili na kuongeza bao la tatu katika ya 80. Stars
iliendelea kushambulia kwa kasi huku ikigonga mwamba mara mbili.
Dakika ya 90 Morocco ilipata baola kufutia machozi na hivyo mchezo
kuisha kwa 3-1. Kwa sasa Msimamo wa Kundi C baada ya Mechi ya Jana
kati ya Ivory Coast na Gambia na Leo kati ya Tanzania na Morocoo,
Jumla zimechezwa Mechi Tatu tatu.
Ivory Coast 7 Points
Tanzania 6 Points
Morocco 2 Points
Gambia 1 Point