Askari Auwawa na Waendesha Bodaboda

BREAKING NEWS: Mauaji ya Askari
Wananchi na waendesha bodaboda wa wilaya ya Namtumbo mkoani Ruvuma,
wamemuua askari polisi baada ya mwendesha boda boda mwenzao kuuliwa na
askari polisi.
Mwendesha boda boda huyo aliyeuliwa inasemekana ni wale wavunjaji wa
sheria za barabarani, baada ya kufanya kosa la kuvunja sheria
walikimbizana na askaripolisi na ndipo askari polisi alipoachia risasi
iliyomuua dereva boda boda huyo.
Baada ya tukio hilo waendesha boda boda wa eneo hilo kwa kushirikiana
na baadhi ya wananchi walianza mashambulizi ya silaha za jadi dhidi ya
askari hao na hatimaye kumuua askari mmoja.


SOURCE: Radio One.