DEREVA WA ROLI ASABABISHA AJARI, KUKATIZA RELINI WAKATU TRENI IKIPITA

Ubishi wa madereva wapitao barabara inayokatisha reli nusura igharimu maisha ya watu baada ya dereva wa maroli la mafuta lililokuwa likitokea mikoani kukaidi ishara ya mshika kibenedera wa shirika la reli na kusababisha ajali kubwa baina ya roli hilo na Treni.

Ajali hiyo imetokea majira ya saa tisa mchana na walioshuhdia ajali hiyo wameiambamia ITV kuwa kabla ya kutokea ajali hiyo dereva mwenye roli namba T.507 AVW lililokuwa na tera lake alisimamishwa kuahiria kuja kwa Treni lakini akakaidi hivyo kusombwa kisha kuburutwa na Treni umbali wa unaokadiriwa mita 60 pembeni mwa reli.

Alipoulizwa dereva wa Treni hiyo yenye namba 7321 aligoma katakata kuzungumza kwa madai kutokuwa na mamlaka ya kuongelea.

Mashuhuda walioshuhudia wamesema ukaidi wa dereva wa roli ndio uliochangia ajali hiyo lakini wakalilaumu shrika la reli kuacha kufunga barabara kwa vyuma inapotokea treni kuja na maafa kama hayo yamekuwa yakitokea mara kwa mara.

Katika hali ingine jeshi la polisi lililazimika kuifanya kazi ya ziada ya kuzuia watu wasikaribie tera la roli hilo wakihofia kutokea mlipuko kutokana na tera hilo kuhisiwa lilikuwa na mafuta na petroli.

Chanzo:ITV