MISRI: HAMAS SI KIKUNDI CHA UGAIDI

Mahakama nchini Misri imefuta hukumu ya awali ambayo ilikitajachama cha Hamas cha Palestina kama kikundi cha kigaidi.

Imefuta hukumu hiyo kwa sababu mahakama iliyotoa hukumu hiyo haikuwa na uhalali wa kufanya hivyo.

Misri inaonekana kama ni msuluhishi mwenye nguvu kwenye mzozo kati ya Israel na Hamas, ambayo inatawala eneo la ukanda wa Gaza.

Lakini tangu kuondolewa madarakani kwa rais Mohamed Morsi ,uhusiano baina ya Misri na Hamas umedondoka.

Hamas ilikuwa ni chama dada cha Muslim Brotherhood ambacho nichama cha rais Morsi.

Na sasa Muslim Brotherhood imepigwa marufuku nchini Misri.