GAMBIA YAMTIMUA MWAKILISHI WA EU

Serikali ya Gambia imemtimua mwakilishi wa muungano wa Ulaya Agnès Guillaud kutoka nchini humo.

Amepewa saa 72 kuondoka nchini humo na hakuna sababu iliyotolewa ya kufukuzwa kwake.

Muungano wa Ulaya umekuwa ukiilaumu Gambia kwa ukiukaji wa haki za binadamu na mwaka uliopita ulizuia msaada wa karibu dola milioni 15 kwa nchi hiyo.

Shutuma nyingi zimeelekezwa kwa sheria zinazopinga mapenzi ya jinsia moja nchini humo.