WATU WATATU WAFARIKI WAWILI KATI YAO WAHISIWA KUWA MAGAIDI

Watu watatu wamefariki dunia wawili kati yao wanasaidikiwa kuwa ni kundi la magaidi pamoja na raia mmoja baada mapigano kutokea kufuatia msako uliofanywa na jeshi la polisi kwa kundi la vijana wanaojinadi kuwa ni magaidi wapato 50 waliokuwa na silaha mpakani mwa mkoa wa Tanga na Morogoro kupitia msitu wa mziha turiani wilayani Mvomero.

Kamishina msaidizi wa jeshi la polisi mkoa wa Morogoro(ACP) Mussa Marambo akizungumza na waandishi wa habari ofisi kwake amesema jeshi la polisi mkoa wa Morogoro wakishirikiana na askari wa mkoa wa Tanga linawashikilia watu sita wanaojinadi kuwakundi la magaidi kufutia msako mkali uliofanyika baada kuona kundi la vijana wasiojulikana watokako wakiwa na silaha mbalimbali za moto wakielekea mkoani morogoro na wamekimbilia katika misitu.

Kwamujibu wa matroni wa zamu katika hospital ya Bwagala Turiani Lidya mhina akizungumza amethibitisha hospitali imepokea maiti mbili ambazo si raia wa Tanzania pamoja na majeruhi mmoja raia ambaye alifariki muda mfupi wakati akipatiwa matibau na askari mmoja aliejeruhiwa amelazwa anaendelea kwa matibabu katika hospitali hiyo.