UJERUMANI: WAHAMIAJI NI MUHIMU

Maafisa nchini Ujerumani wanasema kuwa idadi inayozidi kuongezeka ya wakimbizi wanaowasili kutoka nchini kama syria watasaidia kujaza pengo la ukosefu wa wataalamu.

Mwenyekiti shirika la ajira nchini Ujerumani aliliambia gazeti mojakuwa watu wanaokimbia syria, wengine wameelimika na hivyo wanakaribishwa nchini Ujerumani.

Wakimbizi 350,000 watarajiwa kutafuta ajira nchini ujerumani mwaka huu.

Ujerumani hupokea maombi mengi ya hifadhi kuliko nchi yoyote katika muungano wa ulaya na idadi hiyo inazidi kuongezeka.