DAESH WATANGAZA VITA DHIDI YA TALIBAN

Kundi la kigaidi la Daesh limetangaza vita dhidi ya kundila Taliban la nchini Afghanistan.

Shirika la habari la IRNA limemnukuu mkuu wa kundi la Daesh nchini humo, Abdurrahim Musallam Dust akisema kuwa, kundi la Taliban ni mwakilishi wa Shirika la Kijasusi la Pakistan ISI na ametangaza vita dhidi ya kundi hilo.

Kabla ya hapo, kundi la Daesh ambalo linaendesha vita katika nchi za Iraq na Syria liliwataka wanamgambo wa Taliban wajiunge na kundi hilo ili kupambana na kuangusha serikali za nchi hizo.