WATANZANIA KURUDISHWA TOKA YEMEN

Tanzania imetangaza kuwarejesha nchini raia wake wanaoishi Yemen, kufutia mapigano yanayoendelea nchini humo.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe alitangaza uamuzi huo wakati akizungumza na Balozi wa Tanzania nchini Yemen, Ali Ahmed Saleh, jana.

Waziri Membe alisema ni jukumu la Serikali kuhakikisha kuwa Watanzania hao ambao wengi wao ni wanafunzi, wanarejea nyumbani salama.

Awamu ya kwanza ya kurudisha Watanzania ilianza siku chache zilizopita chini ya uratibu wa Ofisi zaUbalozi wa Tanzania mjini Mascut, Oman.

Kwenye awamu hiyo Watanzania 25 walirudishwa nyumbani huku jitihada za kuandikisha wengine zikiendelea.

"Nimeruhusu matumizi ya fedha ya dharura ili kuhakikisha ndugu zetu walioko kwenye hatari na machafuko ya Yemen wanarejeshwa salama nyumbani mara moja," alisema Membe.