TANZANIA KUMENYANA NA UGANDA MICHUANO YA CHAN

Tanzania itachuana na Uganda wakati Kenya itakipiga na Ethiopia katika michuano ya kufuzu ya Afrika kwa wachezaji wa ndani (CHAN) kufuatia ratiba ya michuano hiyo iliyotolewa na Shirikisho la mpira wa miguu barani Afrika, (CAF), Mechi hiyo ya awali itachezwa kati ya Juni 19-21 wakati ile ya marudiano itachezwa kati ya July 3-5 mwaka huu.

Fainali za CHAN zitafanyika nchini Rwanda kuanzia January 16 mpaka February 7, 2016.

Michuano hiyo, kwa mujibu wa ratiba ya CAF, itashirikisha timu 42, ambazo zitashindana katika kanda 6 na fainali zake zitachezwa na nchi 16 tu wakiwemo timu mwenyeji.

Uganda kwa sasa ipo nafasi katika nafasi ya 84 ya viwango vya FIFA, wakati Tanzania ipo nafasi ya 100.

Ratiba ya kufuzu ya CHAN ni kama ifuatavyo

Kanda ya Magharibi A.

Guinea Bissau vs Mali

Mauritania vs Sierra Leone

Guinea vs Liberia

Senegal vs Gambia


Kanda ya Magharibi B

Ghana vs Ivory Coast

Nigeria vs Burkina Faso

Niger vs Togo


*Kanda ya kati

DR Congo vs Jamhri ya Kati (CAR)

Cameroon vs Congo

Chad vs Gabon


*Kanda ya Kati Mashariki Hatua ya awali

Tanzania vs Uganda

Djibouti vs Burundi

Ethiopia vs Kenya


*Kanda ya Kusini

Zimbabwe vs Visiwa vya Comoro

Lesotho vs Botswana

Namibia vs Zambia

Msumbiji vs Seychelles

Afrika ya Kusini vs Mauritius

Swaziland vs Angola


*Kanda ya Kaskazini

Libya vs Tunisia

Morocco vs Libya