MGANGA WA JADI AKAMATWA NA NYARA ZA SERIKALI

Jeshi la Polisi Mkoa wa Katavi linamshikilia mganga mmoja wa Jadi kwa tuhuma za kumkamata akiwa na ngozi mbili za chui na mkia wa nyumbu akiwa amehifadhi ndani ya chumba chake cha kulala.

Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Katavi Dhahiri alimtaja mtuhumiwa huyo aliyekamatwa na nyara hizo za Serikali kuwa ni Kabichi Nhulu (39)Mkazi wa Kijiji cha Kakese Tarafa ya Misunkumilo Wilaya ya Mpanda Mkoani hapa.

Alisema tukio la kukamatwa kwa mtuhumiwa huyo lilitokea hapo majira ya saa kumi na mbili jioni nyumbani kwa mtuhumiwa katika Kijiji cha Kakese.

Alifafanua kuwa mtuhumiwa huyo alikamatwa kufuatia taarifa za kilizotolewa kwa jeshi la polisi kutoka kwa raia wema kuwa mtuhumiwa huyo anamiliki nyara za Serikali visivyoalali.

Alieleza baada ya taarifa hizo kulifikia jeshi la polisi lilifika kijijini hapo kwa lengo la kufanya upekuzi kwenye nyumba ambayo anaishi mtuhumiwa huyo.

Kidavashari alisema baada ya polisi kufanya upekuzi ndani ya nyumba ya mtuhumiwa Kabichi Nhulu alikamatwa akiwa na ngozi mbili za chui na mkia wa nyumbu akiwa amehifadhi ndani ya chumba chake cha kulala akiwa ameficha chini ya uvungu wa kitanda.

Mtuhumiwa anaendelea kushikiliwa na jeshi la Polisi kwa mahojiano zaidi na anatarajiwa kufikishwa mahakamani baada ya upelelezi kukamilika ili aweze kujibu tuhuma inayomkabili.

Chanzo: KATAVI YETU