MWANDISHI WA HABARI APIGWA RISASI UKRAINE

Mwandishi maarufu wa Ukraine ameuawa kwa kupigwa risasi mjini Kiev na watu waliokuwa wameficha nyuso zao.

Oles Buzyna alifahamika sana kwa maoni yake ya kuunga mkono Urusi na amefanya kazi yauchapishaji akishirikiana na serikali ya rais Viktor Yanukovych aliyeondolewa madarakani nchini Ukraine.

Kifo chake kimekuja siku moja baada ya mwanasiasa mwenye kupendelea Urusi, Oleh Kalashnikov kuuawa katika shambulio linalofanana.

Rais Poroshenko ametaka uchunguzi ufanyike haraka, amesema mauaji haya dhidi ya watu maarufu yamefanyika makusudi na maadui wa Ukraine.