RAIS ZUMA ASHTUSHWA NA GHASIA ZA NCHINI MWAKE

Rais wa Afrika Kusini, Jacob Zuma, ameshutumu ghasia zilizopo nchini humo hivi sasa ambapo wahamiaji wageni wameshambuliwa.

Ametaja ghasia hizo kama za kutisha na zisizokubalika.

Watu watano wameuawa tangu juma lililopita ambapo wamelaumiwa na wenyeji kwa kufanya kazi wanazostahili kufanya wao.

Akihutubia bunge leo alasiri, RaisZuma alisema mashambulizi hayo yalikiuka haki za kibinadamu kama vile haki ya kuwa hai na kuheshimiwa.

Awali maelfu ya raia wa Afrika Kusini wamefanya maandamano katika mji wa Durban kulalamikiakile walichotaja kama ukatili dhidi ya Waafrika wengine.

Katika maeneo yanayopakana na Johannesburg, wenye maduka wenye asili ya kutoka Ethiopia, Somalia na maeneo mengine ya Afrika walifunga biashara zao, wakiogopa kuwa mali yao itaporwa.