RAIS MORSI AHUKUMIWA KIFUNGO CHA MIAKA 20 JELA

Rais wa zamani wa Misri Mohamed Morsi amehukumiwa kifungo cha miaka 20 jela kwa makosa ya kusababisha kuuliwa waandamanaji mwaka 2012.

Rais wa Zamani wa Misri Mohamed MorsiKorti ya makosa ya jinai mjini Cairo imetoa hukmu hiyo wakati Morsi na watuhumiwa wengine katika kesi hiyo-wengi wao wakiwa viongozi wa chama cha Udugu wa kiislam-wakisimama ndani ya tundu la vigaendani ya ukumbi wa mahakama katika chuo cha mafunzo ya polisi mjini Cairo.

Kesi yao inahusu matumizi ya nguvu yaliyotokea nje ya kasri la rais mwezi decemba mwaka 2012.

Wafuasi wa Morsi waliwashambulia waandamanaji wa upande wa upinzani na kusababisha machafuko yaliyopelekea watu wasiopungua 10 kuuwawa.

Jaji Ahmed Youssouf ameachilia mbali madai ya kuchochea mauaji ya waandamanaji wawili na mwandishi habari mmoja machafuko hayo yaliporipuka mbele ya kasri la rais-madai ambayo wadadisi wengi walikuwa wakifikiriaa yangepeleka Morsi kuhukumiwa adhabu ya kifo.

Mbali na Mohamed Morsi, wakuu wengine 12 wa chama cha Udugu wa kiislamu na wafuasi wa itikadi kali akiwemo Mohammed el Beltagy na Essam el Erian, nao pia kila mmoja amehukumiwa kifungo cha miaka 20 jela.

Akitoa hukmu hiyo jaji Ahmed Youssouf ameyataja majina ya mtuhumiwa wote na kufafanua:
"Mohammed Mohamed Mursi, Mohammed el Baltagy na Essam el Erian wamehukumiwa kifungo cha miaka 20 jela kwa ushiriki wao wa kuchochea mauwaji ya umma wa wamisri na tuhuma za kulidhuru taifa la Misri."

Morsi na watuhumiwa wenzake walinyoosha vidole vinne-alama inayokumbusha malalamiko yaliyofanywa katika msikiti wa Rabaah al Adawiya ambako polisi waliingia kwa nguvu wakawauwa mamia ya waandamanaji wafuasi wa Morsi Agosti 14 mwaka 2013.


*Kesi zilisosalia dhidi ya Morsi hazitaharakishwa

Morsi anakabiliwa na kesi nyengine nne pamoja na wanachama wenzake wa udugu wa kiislamu, tangu alipopinduliwa na wanajeshi decemba mwaka 2013.

Morsi na wenzake wana nafasi ya kukata rufaa dhidi ya hukumu ya leo.

Wadadisi wanahisi viongozi wa Misri hawatofanya pupa kusikiliza kesi nyengine kwakua hakuna ghasia majiani na wafuasdi wa Udugu wa kiislamu hawakusayiki kwa wingi ili kuepusha wasikamatwe..