WAZIRI MKUU WA SERBIA APIGWA MAWE BOSNIA

Waziri mkuu wa Serbia Aleksandar Vucic,amepigwa mawe na kufukuzwa na raia wa Bosnia katika hafla ya ukumbusho wa miaka 20 ya mauaji ya halaiki ya watu katika mji wa Srebrenica Waziri huyo alilazimika kutorokea maisha yake bada ya kutupiwa chupa mawe na matusi.

Mashamblizi hayo yalitokea bwana Vucic alipokuwa akiondoka kwenye hafla hiyo iliyoandaliwa katika makaburi ya takriban wahanga 136 wa mauaji hayo.

Inaaminika kuwa waziri Vucic aligongwa na jiwe kichwani.

Vikosi vya majeshi ya Bosnia Serbia viliwaua wanaume 8000 waisilamu na wavulana wa Srebrenica baada ya kuvamia kambi ambayo ilistahili kulindwa na umoja wa mataifa.

Mauaji hayo yanadaiwa kuwa ndiyo yaliyoisababisha Yugoslavia kuvunjika.

Hii leo sherehe hizo zitakamilika kwa maziko ya waathiriwa136 ambao mabaki yao yalitambuliwa hivi majuzi kwa kutumia DNA.

Rais wa zamani wa marekani Bill Clinton ni mmoja wa wale wanaodhuruia maadhimisho hayo.

Awali waziri mkuu Vucic alikuwa ametoa risala za rambirambi japo aliepuka kukiri kuwa yalikuwa mauaji ya halaiki.