MAGUFULI NDIYE MGOMBEA WA URAIS CCM

Chama Cha Mapinduzi (CCM) kimemtangaza daktari John Magufuli kuwa mgombea wake wa kiti cha Urais katika uchaguzi mkuu wa ujao.

Daktari John Magufuli, alisajili asilimia 87.1 % ya kura za wajumbe, hiyo ikiwa ni kura 2104.

Bi Amina Salulm Ali alimaliza katika nafasi ya pili akiwa na asilimia 10.5 % ya kura zote ikiwa ni sawa na kura 253.

Dk. Asha-Rose Migiro akijizolea asimilia tatu ya kura ya wajumbe ama kura 59(2.4%).

Kufuatia ushindi huo Daktari Magufuli ndiye atakaye kuwa mgombea urais wa chama hicho katika uchaguzi mkuu ujao unaotarajiwa kufanyika Oktoba mwaka huu

Mpaka sasa haijafahamika nani atakuwa mgombea mwenza.

Hata hivyo tetesi zilizoenea zinaashiria kuwa Amina Salum Aliana nafasi kubwa ya kuchaguliwa kuwa mgombea mwenza kutokana na kwamba yeye ndio amekuwa wa pili katika kinyang'anyiro hicho.

Pia ikizingatiwa kwamba yeye ni mtanzania mwenye asili ya Zanzibar.