KITWANGA APONDA NDEGE ZA ATCL

ALIYEKUWA Waziri wa Mambo ya Ndani, Charles Kitwanga, jana aliponda aina ya ndege mpya zilizonunuliwa na serikali kutoka Canada kwa ajili ya kufufua Shirikala Ndege Tanzania (ATCL).

Kitwanga alisema ndege hizo si tu hazina mwendo, lakini pia ilikuwa niajabu kununuliwa kwa fedha taslim wakati duniani kote ndege hununuliwa kwa kulipa kidogo kidogo wakati mteja akiendelea kuzitumia.

Serikali imelipa kwa Bombardier Aerospace fedha za ndege mbili za Q400 zinazotumia injini za pangaboi; zenye uwezo wa kubeba abiria 70.

Kitwanga ambaye ni Mbunge wa Misungwi (CCM), alieleza kushangazwa na kitendo cha Serikali kununua ndege hizo ambazo amesema zinatoka kwenye kampuni ndogo ya mtu binafsi, na kuhoji ubora wake.