MARTIN NOOIJ ATAJA KIKOSI KUJIANDAA NA MICHUANO YA COSAFA

Kocha Mkuu wa Timu ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars), Mart Nooij leo ametangaza kikosi cha wachezaji 28.

Kikosi hicho kitaingia kambini katika hoteli ya Tansoma iliyo eneo la Gerezani jijini Dar es salaam, kujiandaa na michuano ya kombe la COSAFA na kuwania kufuzu kwa AFCON na CHAN mwezi Juni mwaka huu.

Katika orodha hiyo ya wachezaji 28 watakao ripoti kambini jumatatu mchana, watapimwa afya zao na madakatari wa timu ya Taifa, na kisha watakaokuwa fit atachagua wachezaji 20 watakao kwenda kwenye michuano ya COSAFA nchini Afrika kusini.

Wachezaji walioitwa ni magolikipa: Deogratius Munish (Yanga), Aishi Manula, Mwadini Ali (Azam),

Walinzi: Shomari Kapombe, Aggrey Morris, Erasto Nyoni (Azam), Nadir Haroub, Oscar Joshua, Kelvin Yondani (Yanga), Abdi Banda, Hassan Isihaka (Simba), Salim Mbonde (Mtibwa Sugar) na Haji Mwinyi (KMKM).

Wengine ni viungo: Amri Kiemba,Salum Abubakar, Frank Domayo (Azam), Said Juma, Salum Telela, Hassan Dilunga (Yanga), Said Ndemla (Simba), Haroun Chanongo (Stand United) na Mwinyi Kazimoto (Al Markhira).

Washambuliaji ni Ibrahim Ajib (Simba), Mrisho Ngasa, Saimon Msuva (Yanga), John Bocco, Kelvin Friday (Azam) na Juma Luizio (Zeco United).

Taifa Stars inatarajiwa kuondoka nchini siku ya jumatano, Mei 13 saa 1 jioni kwa shirika la ndege la Fastjet kuelekea nchini Afrika Kusini katika mji wa Rusterburg - North West Province ambapo ndipo michuano ya COSAFA CUP itafanyika kuanzia Mei 17 mpaka Mei 31 mwaka huu.

WAHAMIAJI WATIKISA SOKA ITALIA

*Timu ya weusi tupu yapanda daraja

Timu ya soka nchini Italia inayoundwa na Waafrika wahamiaji tupu imepanda kutoka daraja la chini kabisa nchini humo.

Timu hiyo, Koa Bosco, ilishinda kwenye mechi ya mtoano Jumapili na hivyo kuwa juu kabisa ya msimamo wa ligi katika Jimbo la Calabria Kusini. Maana ya jina la timu hiyo ni Watumishi wa Madhabahu.

Shirikisho la Soka la Italia lina mfumo wenye ngazi tisa, kuanzia Serie A ambayo ni Ligi Kuu hadi ile ya mwisho, Terza Categoria, ambayo ni ya ridhaa na ambako Koa Bosco wanaondoka.

Wanaounda timu hii ni wahamiaji na wakimbizi kutoka nchi mbalimbali, zikiwamo Senegal, Ivory Coastna Burkina Faso. Jimbo waliloweka makazi ni moja ya maeneo masikini zaidi nchini Italia.

Wengi wa wachezaji wa timu hii huishi kwenye mahema au makontena katika kambi inayoendeshwa na Serikali ya Italia ikaribu na mji wa Rosarno, kusini mwa nchi.

Timu hiyo iliundwa na Padre wa Kanisa Katoliki, Roberto Meduri na inaendeshwa na kufundishwa na Wataliano wa eneo hilo.

"Si rahisi kuendesha mradi wa aina hii, kuna magumu mengi. Vijana hawa wamepiga hatua kubwa, ni ushindi na ni wazi kwao kwamba maisha ya kila siku yanasonga mbele," Mkurugenzi wa Koa Bosco, Domenico Bagala ananukuliwa na jarida la Il Calcio akisema.

Anaeleza kwamba kuanzia asubuhi hadi alasiri wahamiaji hao hufanya kazi kwenye mashamba yaliyo jiranina pia kwenye bustani za machungwa.

Haikuwa rahisi kwa timu hii kupanda daraja, kwani wachezaji walikuwa wakikashifiwa kwa sababu ya rangi yao, kwa mfano Machi mwaka huu wakicheza ugenini zilitokea fujo na wachezaji wao wakatupiwa mawe kutoka majukwaani.

Mechi hiyo ilivunjwa na baadaye timu zote zikaadhibiwa, ambapo wenyeji, Vigor Paravati waliambiwa kwamba hawakuonesha kitendo cha kimichezo.

Hata hivyo, tangu kupanda kwao daraja watu kutoka maeneo mbalimbali wamekuwa wakiwatumia salamu za pongezi na sifa.

Kocha wao, Domenico Mammoliti, amekuwa akitundika mtandaoni baadhi ya salamu hizo, akieleza mwenyewe kufarijika na kwamba huu ni mwanzo wataendelea kupanda madaraja.

Tayari timu hiyo imeanza kuwa na mvuto kwa klabu kubwa kamaJuventus, ambapo Mkurugenzi wa Juve, Pavel Nevded majuzi alialika kikosi chote na viongozi kwenye Makumbusho ya Juventus.

Hapo walikutana na wachezaji wa Juventus na wakabadilishana jezi kama kutakiana heri na pia kuwapongeza Koa Bosco kwa hatua waliyopiga.

Padre Meduri anasema awali alipounda timu hiyo alikuwa na nia ya kuwachanganya wageni katika jamii, kujenga urafiki na kusitisha hali mbaya iliyokuwapo, ambapo fujo zilipata kuua watu 53 kujeruhiwa baada ya Waafrika wawili kupigwa risasi 2010.

Ni mara chache Koa Bosco hupata ufadhili wa kifedha, lakini kwa kupanda daraja na kuanza kujulikana sehemu nyingi, wanatarajia mambo mazuri baadaye.

Hata hivyo, watu wa maeneo ya jirani wamekuwa wakikusanya na kutoa msaada wa mablangeti na mavazi ya kuwatia joto wachezaji.

Eneo wanaloishi lina ukosefu wa ajira na nahodha wa timu hiyo anayetoka Ivory Coast,Yaya Diallo, anaamini ni vyema Waafrika wengine wakabaki nyumbani ambako wanaweza kufanikiwa kuliko hatari ya kusafiri kwenda Italia.

Italia huwa na wahamiaji wengi ambao husafiri kwa boti kutoka Afrika wakipitia pwani ya Libya, na wengi hufia baharini katika kile wanachosema ni kwenda kutafuta maisha Ulaya.

PACQUIAO ASHUTUMIWA KWA UDANGANYIFU

Manny Pacquiao ameshutumiwa kwa kudanganya kuwa alikuwa akiumwa bega kabla ya pambano dhidi ya Floyd Mayweather. Pambano hilo lilipigwa Las Vegas,Marekani.

Iwapo Mfilipino huyo atakutwa na hatia, adhabu atakayopata kwa mujibu wa sheria itakuwa kifungo jela cha kati ya mwaka mmoja na miaka minne, na faini ya kufikia dola za Kimarekani $5,000 (£3,305).

Tume ya Michezo ya Nevada, NAC, imesema Pacquiao, mwenye umri wa miaka 36, hakutangaza kuwa majeruhi katika fomu ya maelezo kabla ya pambano.

Lakini Pacquiao anasema alikuwa muwazi na mpango wa matibabu ulikuwa umekubaliwa.

Pacquiao alisema kupigwa kwake kumetokana na maumivu - akidai kuwa alishindwa kutumia mkono wake wa kulia katika pambano hilo- lakini taarifa ya pamoja iliyotolewa na Team Pacquiao na mapromota wake Top Rank imesema Shirika la Marekani la Kuzuia Matumizi ya Dawa za Kuongeza Nguvu Michezoni, Usada, lilijulishwa juu ya sula hilowakati wa kambi ya mazoezi ya mwana masumbwi huyo na pia katika usiku wa pambano.

Wamesema daktari mmoja wa Usada alizuia matumizi ya dawa moja ya kuzuia maumivu usiku wa pambano, lakini NAC haikuruhusu kutolewa kwa sababu hawakujua kuhusu kuumia bega.

Taarifa hiyo imesema: "Hii inakatisha tamaa kutokana na ukweli kwamba Team Pacquiao ilieleza kuhusu Pacquia kuumia bega na matibabu kwa Usada, ambao waliidhinisha matibabu na Manny aliorodhesha dawa katika fomu yake ya kabla ya pambano."

NAC imesema kambi ya Pacquiao haikulazimika kueleza kuhusu kuumia kwa bondia wake, lakini mkurugenzi mtendaji wao Bob Bennett amesema: "si tu kwamba hakujaza fomu kikamilifu,ni kwamba hakuwa mwaminifu. "Saa mbili kabla ya pambano walitaka dawa ya kutuliza maumivu. Suala hilo lilituweka katika mazingira magumu sana."

DANGOTE ATAKA KUINUNUA ARSENAL

Mtu tajiri barani Afrika Aliko Dangote amesema kuwa bado anataka kuinunua kilabu ya Arsenal licha ya kushindwa kufanya hivyo mwaka 2010 alipotaka kununua hisa za kilabu hiyo.

Bilionea huyo kutoka Nigeria ni tajiri mara nane ya alivyokuwa wakati alipojaribu kununua hisa za klabu hiyo na kwamba shabiki huyo wa Arsenal bado hajatupilia mbali ndoto yake ya kutaka kuinunua kilabu hiyo ya London Kaskazini.

''Bado nina matumaini kwamba siku moja nitainunua timu hiyo',' alisema Dangote mwenye umri wa miaka 58.

''Naweza kuinunua bei ambayo wamiliki wake itakua vigumu kukataa'', huku akiongezea kuwa ''najua mpango wangu''.

La kushangaza ni kwamba Dangote ametaja hadharani kwamba Arsene Wenger anafaa kubadilisha mbinu yake akisema kuwa timu hiyo inahitaji mwelekeo mpya.

Dangote ambaye ana thamani ya dola bilioni 15 ni tajiri zaidi ya Stan Kroenke ambaye anamiliki hisa nyingi katika kilabu hiyo na Bilionea raia wa Uzbek Alisher Usmanov ambao wamekuwa wakipigania udhibiti wa kilabu hiyo katika miaka ya hivi karibuni.

WAKIMBIZI TOKA BURUNDI WALIOINGIA NCHINI WAFIKI 1852

Idadi ya watu wanaoingia nchini kutoka Burundi kukimbia machafuko ya kisiasa kupitia mkoani Kigoma, imezidi kuongezeka kutoka 1,645 hadi kufikia 1,852.

Kati ya hao, 1,252 tayari wameshasajiliwa kama wakimbizi rasmi na kupelekwa katika kambi yaNyarugusu, wilayani Kasulu.

Hayo yalibainishwa na msemaji wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Isaac Nantanga, wakati wa mahojiano na NIPASHE.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na wizara hiyo juzi, hadi kufikia Aprili 30, mwaka huu, mkoa huo ulikuwa umeshapokea idadi ya watu 500 walioingia kupitia vijiji sita vya Kibuye, Kagunga, Kosovo, Kakonko, Sekeeye na Kigaye.

Kwa mujibu wa msemaji huyo, haliya usalama katika maeneo ya mipakani, imeimarishwa na kutoa wito kwa wakazi wa maeneo hayo kutoa taarifa kwa uongozi wa vijiji iwapo kuna mgeni asiyefahamika kufika maeneo hayo.

Kwa upande wake, Afisa wa Idara ya Uhamiaji Mkoa wa Kigoma, MauriceDavid, alisema hadi juzi jioni idadi ya wakimbizi walioingia mkoani humo ilifikia 1,645.

David alisema wakimbizi kutoka Burundi walianza kuingia mkoani humo Aprili 26, mwaka huu kupitia wilaya za mkoa huo na idadi kwenye mabano kuwa ni Buhigwe (156), Kigoma Vijijini (1,155), Kibondo (260, Kasulu (195) na Nyarugusu (64) ambao walikwenda moja kwa moja katika kambi hiyo bila kupitia katika vituo vya Uhamiaji.

Hata hivyo, aliongeza kuwa idadi ya wakimbizi waliofika kabla ya kuzuka upya kwa vurugu hizo nchini humo ilikuwa 46, lakini hadi jana mkoa mzima ulikuwa umepokea jumla ya wakimbizi takribani I, 852.

Burundi imekumbwa na vurugu kutokana na maandamano yanayofanyika kwenye mji mkuu wanchi hiyo Bujumbura, kwa wananchikupinga hatua ya Rais Pierre Nkurunziza kutaka kugombea tena urais kwa muhula wa tatu kinyume cha katiba ya nchi hiyo.

Katiba ya Burundi inataja muda wa urais kuwa ni vipindi viwili, lakini Rais Nkurunziza anadai kusimamia makubaliano ya Mkataba wa Arusha kwamba kipindi chake kilianza pale mkataba huo uliposainiwa, hivyo muda aliokuwa madarakani kabla ya kusainiwa usihesabiwe.

Chanzo: NIPASHE

CHENGE ATINGA KORTINI NA MAWAKILI 10

Mbunge wa Bariadi Magharibi, Andrew Chenge, amefungua kesi ya kikatiba dhidi ya Baraza la Maadili ya Viongozi wa Umma na maazimio ya Bunge kuhusiana na malalamiko ya ukiukaji wa maadili ya uongozi.

Chenge, anatuhumiwa kupokea fedha kutoka kwa Kampuni ya VIP Engineering and Marketing Ltd Sh. bilioni 1.6.

Chenge aliitwa katika Baraza la Maadili ya Viongozi wa Umma kuhojiwa kuhusiana na tuhuma hizo ambazo ni kinyume cha maadili. Hata hivyo, alipinga akisema kuwa baraza hilo halina mamlaka ya kumhoji kwa kuwa liko katika Mahakama ambayo ina mamlaka kuliko baraza, na kueleza kuwa atafungua kesi ya kupinga mahakamani.

Katika maombi yake, lililowasilishwa masjala kuu ya Mahakama Kuu Tanzania, Kanda ya Dar es Salaam, Chenge ameorodhesha sababu 13 za kupinga mwenendo wa baraza na mapendekezo yaliyowasilishwa na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) na Kamati ya Bunge na Hesabu za Serikali (PAC) kuhusiana na shauri hilo.

Kwa mujibu wa hati yake ya maombi, anadai kwamba mwenendo wa Baraza na maazimio ya Bunge ya Novemba 29, mwaka 2014, yalikuwa ni kinyume cha amri iliyotolewa Novemba 25, mwaka 2014 ikisimamisha kwa muda kuwasilishwa na majadiliano ripoti iliyohusiana na uhamishaji wa fedhaza akaunti ya Tegeta Escrow.

Kesi hiyo imepangwa mbele ya jopola majaji watatu likiongozwa na Stella Mugasha, Augustine Mwarija na Dk. Fauz Twaib.

Majaji wamewaelekeza walalamikiwa ambao ni Tume ya Maadili ya Baraza la Maadili na Mwanasheria Mkuu wa Serikali kuwasilisha majibu yao Mei 8 na Mei 21, mwaka huu kesi hiyo itasikilizwa.

Jopo la mawakili 10 linalomwakilisha Chenge katika kesi hiyo linawajumuisha Deogratias Ringia, Wilson Ogunde, Jamhuri Johnson, Michael Ngalo, Respicius Didace, Okare Emesu, Cuthbert Tenga, Dosca Mutabuzi, John Nyange na Stephano Kamala.

Katika maombi yake, Chenge anaiomba mahakama kutoa amri yakudumu ya kuizuia Tume na Baraza kuendelea au kutafakari kuanzisha malalamiko yoyote dhidi yake kuhusiana na ripoti za CAG na PAC.

Kadhalika, anaiomba mahakama kutoa azimio kwamba malalamiko yaliyoanzishwa na tume kupitia baraza lake ni batili kutokana na ukiukaji wa taratibu na kwamba majadiliano ya Bunge na maazimio yake hayakuwa sahihi, hayakuwa ya kisheria, na kwa hiyo yalikuwa batili.

MGOMO WATIKISA TENA

Takribani siku 22 zikiwa zimepita tangu madereva wagome kutoa huduma za usafiri nchi nzima, leo wametangaza mgomo mwingine kutokana na ukimya dhidi ya madaiyao kwa serikali.

Madereva hao jana walitoa tamko lakuwapo kwa mgomo huo kupitia vyama vyao, huku wakikanusha kwamba watagoma sambamba na kuandamana.

Walisema leo watakuwa kwenye ofisi zao za muungano wao zilizopo Ubungo, jijini Dar es Salaam na hawatatoa huduma za usafiri.

Akizungumza na NIPASHE jana, Katibu wa Umoja wa Madereva na Chama cha Malori, Rashid Salehe, alisema, mgomo upo pale pale kwa madai kuwa bado kuna mambo ambayo yameendelea kuwa kikwazo kwao.

Alisema iwapo serikali haitatoa majibu ya kuridhisha, leo hawataingia barabarani kutoa huduma za usafiri.

Alisema jana walifanya mkutano wa madereva jijini Dar es Salaam huku ajenda kubwa ikihusu mgomo huo.

Alitaja baadhi ya sababu zinazowafanya wagome kwa mara nyingine kuwa ni serikali kutotekeleza madai yao likiwamo lakupewa ajira rasmi na waajiri wao.

"Msimamo wetu upo palepale kwamba kesho (leo) hatutaendesha magari..madereva wanaambiwa wezi, tunataka mikataba iboreshwe…tutakaa hapa hata ndani ya siku saba hadi serikali ije na kutoa majibu yanayoridhisha. Tunataka tupatiwe mikataba inayoeleweka na waajiri wetu mbele ya serikali," alisema na kuongeza:"Tumekaa katika kikao cha leo (jana)kwa ajili ya kuangalia maazimio ya kikao tulichokaa Aprili 29, mwaka huu…katika kikao hicho zaidi ya madereva 40 walisema hawana hela."


TABOA WAIPAANGALIZO SERIKALI

Katibu wa Chama cha Wamiliki wa Mabasi Tanzania (Taboa), Enea Mrutu, alisema walipata taarifa zotekuhusu mgomo huo na kueleza kwamba wanaotangaza mgomo huo siyo madereva walioajiriwa.

Kwa mujibu wa Mrutu, madereva hao ndiyo waliosababisha magari yao kutoingia barabarani Aprili 11, mwaka huu na kuitaka serikali kuingilia kati suala hilo, vinginevyo leo magari hayataweza kuingia barabarani.


DARCOBOA: MGOMOUWE WA HIARI

Mwenyekiti wa Wamiliki wa Daladala Dar es Salaam (Darcoboa), Sabri Mabrouk, alisema chama hicho kina taarifa kuhusu mgomo huo, lakini akaeleza kusikitishwa kwake kwa namna madereva wa vyombo vya usafiri wanavyowahusisha wao akisema hawahusiki.

Kutokana na hilo, Mabrouk aliomba mgomo huo usiwe wa lazima bali wa hiyari kwani si vyema kuwahusisha wao wanaohusika na daladala tena ndani ya mkoa na kupewa vitisho vya kupigwa mawe endapo gari lolote litakaidi agizo hilo.

"Serikali iangalie suala hili, kama kuna jambo lipo nyuma ya pazia basi liwekwe wazi….kama ni wa mikoani kwa nini wanatuhusisha sisi, tusitafute kuwasumubua wananchi," alisema mwenyekiti huyo wa Tarcoboa.

SUMATRA: WANANCHI WATASUMBULIWA

Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Udhibiti Usafiri wa Nchikavu na Majini (Sumatra), Gilliard Ngewe, alisema, suala hilo lipo katika wizara husika na kwamba kufanyika kwa mgomo huo kutaathiri wananchi kutokana na kukosa huduma za usafiri.

Hata hivyo, gazeti hili lilimtafuta Waziri wa Uchukuzi, Samuel Sitta (pichani), bila mafanikio kutokana na simu yake kutopatikana, huku Naibu wake, Charles Tizeba, akisema: "Naomba mnitafute kesho..nipo msibani."NIPASHE pia lilimtafuta Waziri wa Kazi na Ajira, Gaudensia Kabaka na Naibu wake, Makongoro Mahanga, lakini simu zao hazikuwa hewani.

Kamanda wa Kikosi cha Usalama Barabarani, Mohamed Mpinga, alikaririwa na vyombo vya habari juzi akisema amepokea ujumbe mfupi wa simu kwamba leo kuna mgomo.

Tishio la mgomo wa leo ni mwendelezo wa mgomo mwingine mkubwa ambao ulidumu kwa takribani saa saba kwa mabasi kutokuruhusiwa kutoka katika kituo kikuu cha mabasi yaendayo mikoani na nje ya nchi cha Ubungo, Aprili 11, mwaka huu.

Madai ya mgomo huo ambao uliletaadha kubwa kwa wananchi yalikuwa ni kupinga ucheleweshwaji wa malori kwenye mipaka hususani ya Tunduma ambako hukaa kwa zaidi ya siku 26 licha ya kulipiwa kila kitu bandarini.

Mengine ni kupinga sheria namba G 31 ya mwaka 2015 ambayo inazungumzia faini ya Sh. 300,000 au kifungo cha miezi 21 kwa madereva wanapofanya makosa barabarani. Pia kupinga madereva kutakiwa kwenda Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT) kila baada ya miaka mitatu kwa ajili ya kujinoa.

Madai mengine yalikuwa ni wamiliki wa magari kutowashirikisha madereva katika mikataba yao ya kazi.

Hata hivyo, mgomo huo ulisitishwa baada ya serikali kupitia kwa Waziri Kabaka kufuta sharti la kwenda chuoni kila baada ya miaka mitatu.

Pia aliahidi kulipatia ufumbuzi sualala mikataba yao katika kikao kilichotarajiwa kufanyika wiki iliyofuata.


CHANZO: NIPASHE

RAIA 800 WA BURUNDI WAINGIA TANZANIA WAKIKIMBIA MACHAFUKO NCHINI KWAO

Idadi ya watu wanaokimbilia nchini kutafuta hifadhi kutokea Burundi imezidi kuongezeka huku Serikali ya Tanzania ikithibitisha kuwa jumla ya watu 800 wameingia na kuorodheshwa.

Raia hao wanakimbia machafuko ya kisiasa nchini humo yaliyoanza hivi karibuni.

Aidha, kwa mujibu wa Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Isaac Nantanga, watu 51 waliongia nchini wiki iliyopita kupitia mkoani, Kagera wamerudishwa makwao kutokana na kukiuka sheria na taratibu za uhamiaji.

Nantanga alisema wakimbizi hao walirudishwa Burundi kwa sababu kabla ya kuingia nchini walitokea Rwanda na huku akisisitiza kuwa sheria na taratibu za Umoja wa Mataifa (UN) haziwahesabu kama wakimbizi kamili.

"Watu 51 waliongia nchini wiki iliyopita kutokea Burundi na kuingia mkoani Kagera wamerudishwa kwao kutokana na kuingia nchini kupitia Rwanda tofauti na sheria za Uhamiaji zinavyoelekeza," alisema Nantanga.

Aliongeza kuwa kati ya wakimbizi 800 waliongia nchini kupitia mkoaniKigoma, 720 tayari wamepelekwa katika kambi ya Nyarugusu iliyopo wilayani Kasulu mkoaoni humo.

Nantanga alisema mpaka Aprili 30, mwaka huu katika mkoa wa Kigoma watu 500 waliingia kupitia vijiji sita ambavyo ni vya Kibuye, Kagunga, Kosovo, Kakonko, Sekeeye na Kigaye.

Mkuu wa mkoa wa Kagera, John Mongella, jana alithibitisha kuwa kuna raia wa Burundi wanaoingia mkoani humo, lakini alisema kutokana na kutokuwapo kwa kambiya wakimbizi, wamekuwa wakipelekwa mkoani Kigoma ambako kuna kambi ya kuwahifadhi.

"Wapo baadhi wanakamatwa na kurudishwa nchini mwao, lakini wengine tunawakabidhi mkoa wa Kigoma ambao kwa sasa una kambi kwa ajili ya kuwahifadhi, hata tukisema wakae hapa hatuna mahala pa kuwahifadhi," alisema Mongella.

Alisema kwa sasa mkoa wa Kagera hauna mpango wa kufungua kambi kwa ajili ya kuwahifadhi wakimbizi hao, na kutumia fursa hiyo kuwataka wananchi kutowapokea nakuwahifadhi watu hao na badala yake watoe taarifa wakati watakapoona wameingia katika maeneo yao.

"Waharifu nao wanaweza kutumia fursa hiyo kuingia, ninachowaomba wananchi wasijiingize katika masuala ya kupokea watu na kuwahifadhi, badala yake wawakabidhi kwa wenyeviti au maafisa watendaji walioko katika maeneo yao," alisema Mongella.

Burundi imekumbwa na vurugu kutokana na maandamano yanayofanyika kwenye mji mkuu wanchi hiyo Bujumbura, wakipinga hatua ya Rais Pierre Nkurunziza kutaka kugombea tena urais kwa muhula wa tatu, baada ya kumaliza muda wake wa mihula miwili.

Katiba ya Burundi inataja muda wa urais kuwa ni vipindi viwili, lakini Rais Nkurunziza anasema kwa mujibu wa makubaliano ya Mkataba wa Arusha, kipindi chake kinaanza pale mkataba huo uliposainiwa, hivyo muda aliokuwa madarakani kabla ya kusainiwa usihesabiwe.

Anasema kuwa, muhula huu ndio utakuwa kipindi chake cha pili na cha mwisho.

Hata hivyo, upinzani unapinga na yamekuwepo maandamano kuanzia Jumamosi ya kupinga hatua hiyo, natayari watu kadhaa wametiwa nguvuni na baadhi wanadaiwa kupoteza maisha.

CHANZO: NIPASHE

VIKONGWE WAKAMATWA NA MAGOBOLE

JESHI la Polisi mkoani Katavi linawashikilia watu tisa wakiwemo vikongwe wa miaka 80 na 70 baada ya kukamatwa wakiwa na bunduki tatu za kienyeji aina magobole, risasi zake 15, mtambo wa kutengenezea silaha, baruti na sare za Jeshi la Wananchi la Ulinzi na Usalama (JWTZ).

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Katavi ,Dhahiri Kidavashari alitaja vitu vingine vilivyokamatwa kufuatia msako mkali unaoendelea wilayani Mlele ni vipande tisa vya nondo, vyuma vya kutengenezea risasi na mafuta ya kiboko yaliyohifadhiwa kwenye chupa.

"Mafanikio haya yametokana na ushirikiano mzuri kati Jeshi la Polisi, askari wa Tanapa na raia wema ambapo wamekuwa wakiendelea kutoa taarifa za uhalifu na wahalifu na kufanikisha katika ukamataji," alieleza.

Alidai kuwa silaha hizo zilikuwa zikimilikiwa kinyume cha sheria na zilikuwa zikitumika katika visa vya kijangili na uhalifu mwingine wilayani Mlele.

Akizungumza kwa njia ya simu, aliwataja watuhumiwa hao kuwa ni pamoja na Lazaro Zakaria (63) aliyekamatwa akimiliki gobole bila kuwa na kibali, Shaaban Mussa (52) gobole bila kuwa na kibali na Robert Kaumba (80).

Wengine ni Hamisi Rehani (70) alikamatwa akiwa na mtambo wa kutengenezea silaha aina ya gobole bila kuwa na kibali, Benedict Simon (52) akiwa na risasi 15 za gobole, vipande tisa vya nondo, vipande vyamiti, mtutu mmoja na baruti ndani ya chupa na Shaaban Mussa (52) alikamatwa akiwa na risasi moja ya gobole bila kibali.

Kwa mujibu wa Kidavashari, katika msako huo pia jeshi hilo lilimtia mbaroni Esther John (21) akiwa na sare ya JWTZ na vyuma viwili vya kutengenezea risasi na Mashaka George (32), alikamatwa akiwa na mafuta ya kiboko aliyoyahifadhi kwenye chupa.

Alieleza kuwa watuhumiwa wote, wanashikiliwa na Jeshi la Polisi kwa upelelezi na watafikishwa mahakamani baada ya upelelezi kukamilika.

WATU WAWILI WAUAWA KWA RISASI MJINI TEXAS

Polisi mjini Texas wanasema kuwa wamewapiga risasi na kuwaua watu wawili waliokuwa nasilaha, waliowashambulia walinda usalama kwa risasi, walipofika katika eneo la hafla moja yenye utata ya uchoraji wa vibonzo vya kuwakejeli waislamu na mtume Mohammed.

Duru za habari zasema kuwa kisa cha ushambuliaji wa risasi kimefanyika katika sherehe moja, iliyokuwa ikifanyika mjini Dallas, mahala ambapo waandalizi walikuwa wakiendesha onyesho hilo.

Hafla za Sherehe hiyo iliyoandaliwa na kundi moja la kisiasa la kihafidhina, ambalo limekuwa likikejeli Uislamu, lilikuwa litoe zawadi nono ya dola milioni kumi kwa mchoraji kibonzo mahiri zaidi, atakayeibuka mshindi kwa kumchora mtume Mohamed.

Mwanasiasa kutoka Uholanzi Geert Wilders -- ambaye anafahamika kwa matamshi yake dhidi ya kuwadunisha waislamu, alikuwa msemaji mkuu katika hafla hiyo.

Aliyeshuhudia ameiambia BBC kuwa, aliwaona maafisa wa polisi wakimtia mbaroni mshukiwa wa tatu, ambaye alionekana kuwa hana silaha.

Kikosi cha kutegua mabomu pamoja na ndege za helikopta za polisi zimefika mahali hapo kwa sasa.

MKUU WA MAJESHI BURUNDI AWAONYA WANASIASA

Mkuu wa majeshi nchini Burundi Meja Jenerali Prime Niyongabo ametoa wito kwa wanasiasa kutotumia jeshi la taifa kwa manufaa yao ya kisiasa.

Jenerali Niyongabo amekariri tangazo lililotolewa na waziri wa ulinzi Jumamosi kuwa jeshi la nchi hiyo litahakikisha kuwa mkataba wa Arusha umetekelezwa kikamilifu na kuwa jeshi hilo halitumiwi na mtu au chama chochote cha kisiasa.

Kuhusiana na maandamano yanayoendelea, mkuu huyo wa jeshi amesema kuwa maandamano hayo sio halali na wanaichi wanapaswa kutumia mbinu za sheria zilizopo kutatua mizozo yao.

Wakati huo huo Meja Jenerali Niyongabo amesema jeshi hilo litasalia kuwa lenye nidhamu ya hali ya juu na tiifu kwa taifa la Burundi na wala sio kwa mwanasiasa yeyote.

Ameongeza kusema kufikia sasa jeshi limefanya kazi nzuri kuhakikisha kuwepo kwa usalama nchini Burundi na katika mataifa mengine wanakohudumu katika vikosi vya Umoja wa Mataifa na Muungano wa Afrika.

Mkuu huyo wa majeshi amesema wanajeshi wataendelea kushirikiana na polisi kushika doria ili kuhakikisha amani na utulivu vinakuwepo nchini Burundi.

Huku hayo yakijitokeza muungano wa upinzani umesema kuwa maandamano yataendelea siku ya Jumatatu baada ya mapunziko ya siku mbili.

Upinzani umepinga hatua ya rais Pierre Nkurunziza ya kuwania muhula wa tatu kama rais.

Viongozi wa upinzani wanasema kuwa Rais Nkurunziza ni sharti atekeleze mkataba wa Arusha ambao ulimaliza mapigano ya wenyewe kwa wenyewe nchini Burundi.

Lakini chama tawala cha CNDD FDD kimepinga madai hayo na kusema kuwa Rais Nkurunziza anatumikia muhula wake wa kwanza kwa sababu, miaka mitano ya kwanza ilikuwa kipindi cha mpito na hakuchaguliwa na raia kama inavyohitajika kisheria.

Wakaazi wa mji mkuu wa Bujumbura wameshuhudia uhaba mkubwa wa bidhaa muhimu kama vile petroli, na kadi za simuza muda wa mazungumzo huku kukiwa na misururu mirefu katika vituo vya kununua mafuta.

Idadi kubwa ya raia wa Burundi wamekimbilia nchi jirani kwa hofu ya kuzuka mapigano zaidi.

MATEKA WASIMULIA MATESO YA BOKO HARAM

Wanawake na watoto waliokuwa wakishikiliwa mateka na kikundi cha Kiislam cha Boko Haram kaskazini mwa Nigeria wamesema baadhi yao waliuawa kwa kupigwa mawe na wapiganaji wa Boko Haram wakati jeshi lilipokaribia kuwaokoa.

Walikuwa wakizungumza siku moja baada ya karibu mateka mia tatu kuokolewa kutoka msituwa Sambisa na kuwapeleka katika kambi ya serikali.

Mwanamke mmoja ambaye alijifungua akiwa mateka ameelezea namna wapiganaji hao walivyomkata koo mumewe wake mbele yake, kabla mwanamke huyo kutenganishwa na watoto wake wengine watatu.

Mwandishi wa Associated Press ambaye aliotembelea kambi hiyoamesema wengi wa watoto waliokolewa walikuwa wanaugua utapiamlo mkali.

Jeshi la Nigeria limesema limewaokoa zaidi ya watu mia saba katika kipindi cha wiki moja iliyopita wakati wa mapigano makali yanayoendelea dhidi ya Boko Haram.

MELI YA TANZANIA YAKAMATWA NA TANI 3 ZA COCAINE UINGEREZA

Kwa mara nyingine, Jina la nchi limeendelea kuchafuka baada ya Meli ya MV Hamal iliyosajiliwa Tanzania kukamatwa barani Ulaya ikiwa imebeba shehena ya dawa za kulevya aina ya cocaine yenye uzito wa tani tatu.

Kama dawa hizo haramu zingeuzwa mitaani nchini Uingereza, zingekuwa na thamani ya Sh1.5 trilioni, kiasi ambacho nchi wafadhili zinatarajiwa kuichangia Tanzania kwenye bajeti ya mwaka 2015/16.

Matukio mengine yaliyoichafua nchi ni la meli ya mizigo ya Gold Star iliyosajiliwa Tanzania ambayo ilikamatwa Septemba 2013, jirani na Kisiwa cha Sicilia katika Bahari ya Mediterranian nchini Italia wakati ikielekea Uturuki ikiwa na tani 30 za dawa za kulevya aina ya bangi zenye thamani ya Pauni 50 milioni za Uingereza (sawa na Sh125 bilioni). Tukio jingine ni lile la Watanzania wawili kukamatwa na dawa za kulevya zenye uzito wa kilo 150 na thamani ya Sh6 bilioni kwenye Uwanja wa Ndege wa Oliver Tambo, Afrika Kusini.

Kiwango hicho cha dawa zilizokamatwa kimeweka rekodiya ukubwa wa mzigo wa dawa hizo haramu nchini Uingereza. Awali shehena ya cocaine iliyokuwa kubwa ilikamatwa Septemba mwaka jana ikiwa na mzigo wenye thamani ya Sh 450 bilioni.

Kwa mujibu wa vyombo vya habari vya Uingereza, meli ya MV Hamal ilikamatwa kwenye Bahari ya Kaskazini na baada ya kupekuliwa kwenye bandari ya Arberdeen nchini Scotland, ilikutwa na shehena ya dawa za kulevya aina ya cocaine.

Meli hiyo yenye urefu wa mita 32 na uwezo wa kubeba tani 422, ilikamatwa na askari wa kikosi cha majini cha Royal Navy waliokuwa kwenye meli ya HMS Somerset pamoja na askari wa uhamiaji wa Border Force waliokuwa kwenye meli ya Valiant, karibu kilomita 160 mashariki mwa mji wa Aberdeen Alhamisi baada ya kupewa taarifa na kitengo cha makosa ya jinai, NCA.

Baadaye, meli hiyo ilipelekwa bandari ya Aberdeen, ambako maofisa wa Border Force wenye stadi maalumu ya upekuzi, waliipekua meli hiyo kwa kusaidiana na polisi wa Scotland.

John McGowan – afisa mwandamizi wa uchunguzi wa NCA, alisema: "Upekuzi wa meliulikuwa mrefu na unaosababisha maumivu, na uliofanywa na watu wenye utalaamu mkubwa wa kufanya kazi kwenye mazingira magumu.

"Matokeo yake ni ugunduzi huu mkubwa – unaoaminika kuwa mkubwa kuwahi kutokea kwenye rekodi nchini Uingerezana ambao unaweza kuwa na thamani ya mamilioni ya fedha."

Hata hivyo, rekodi za mtandao wa shughuli za baharini unaonyesha kuwa katikati ya Februari, meli hiyo ilikuwa Uturuki na wiki mbili zilizopita ilianza safari kutoka visiwa vya Tenerife nchini Hispania na ilipokamatwa ilikuwa inaelekea Hamburg, mji wa pili kwa ukubwa nchini Ujerumani ikitazamiwa kufika jana usiku.

Meli hiyo imekutwa na watu tisa wenye umri kati ya miaka 26 na 63 wote raia wa Uturuki na wameshitakiwa kwa kukutwa na dawa za kulevya. Washitakiwa wote hawakusema lolote waliposomewa mashtaka yao. Washitakiwa hao ni Mustafa Ceviz, 54, Ibrahim Dag,47, Mumin Sahin, 45, Muhammet Seckin, 26, Umit Colakel, 38, Kayacan Dalgakiran,63 na Emin Ozmen, 50, wote wanatoka jiji la Istanbul. Wengine ni Abdulkadir Cirik, 31, anayetoka Mersin na Mustafa Guven, 47, kutoka Yozgat, nchini Uturuki. Walifikishwa mahakamani Jumatatu.

MIKOPO YA WANAFUNZI HESLB YAIVA

Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB), jana imetoa mwongozo kwa wanafunzi wahitaji wanaotarajia kuomba mikopo na ruzuku kwa mwaka wa masomo 2015/2016 unaotarajiwa kuanza miezi michache ijayo.

Kwa mujibu wa mwongozo huo, ambao unapatikana katika tovuti ya Bodi (www.heslb.go.tz), waombaji wamepewa miezi miwili kuwasilisha maombi yao kuanzia Jumatatu (Mei 4) hadi Jumanne (Juni 30, 2015).

Mwongozo huo uliotolewa na Mkurugenzi Mtendaji wa HESLB, George Nyatega, unasema wanafunzi wote wahitaji wa mkopo na ruzuku wanapaswa kuwasilisha maombi yao kwa njia ya mtandao kupitia mfumo maalum kupitia mtandao unaojulikana kama"Online Loans Application and Management System" ulioanzishwa na HESLB kwa ajili ya kupokea maombi hayo.

Mfumo huo unapatikana kupitia tovuvi ya Bodi au kwa kufungua kiunganishi chake (http://olas.heslb.go.tz).Mwongozo huo pamoja na mambo mengine, unafafanua kuwa waombaji wa mara ya kwanza wanapaswa kulipa ada ya maombi ya Sh. 30,000 na kisha kutumia namba ya muamala na kuingia katika mtandao na kuanza kujaza fomu za maombi.

"Waombaji wa mara ya kwanza wanapaswa kulipa ada ya maombi ya Sh. 30,000 ambayo inalipwa mara moja tu na haitarudishwa kwa njia ya M-Pesa," inasisitiza sehemu ya mwongozo huo.

Aidha, imesisitizwa kuwa wanafunzi wenye mikopo na wanaoendelea namasomo katika taasisi mbalimbali za elimu ya juu, hawapaswi kuwasilisha maombi tena.

Kwa mujibu wa Nyatega, Bodi imewasihi waombaji na wadau wengine kuusoma na kuuzingatia mwongozo huo wakati wote wanapofanya na kuwasilisha maombi.

HESLB ilianzishwa kwa Sheria ya Bunge Na 9 ya mwaka 2004 na kuanza kazi rasmi mwezi Julai, 2005ili, pamoja na majukumu mengine, kutoa mikopo kwa wanafunzi wahitaji waliodahiliwa katika taasisi za elimu ya juu.

Aidha, jukumu jingine la Bodi ni kudai na kukusanya mikopo yote iliyotolewa kwa wahitimu wa taasisi za elimu ya juu kuanzia mwaka 1994 wakati Serikali ilipoanza kukopesha wanafunzi.

WATU WATATU WAUAWA SHAMBULIZI LA BOMU BURUNDI

Watu watatu wameuawa katika shambulizi la bomu lililowalenga askari polisi nchini Burundi ambapo zaidi yawatu mia sita wametiwa mbaroni wakati wa maandamano na ghasia za kupinga raisi wa taifa hilo Pierre Nkurunziza kuwania muhula wa tatu wa kiti cha urais.

Mkuu wa Polisi nchini humo Generali Andre Ndayambaje amesema kuwa maafisa wawili wa polisi waliuawa na mmoja kujeruhiwa katika wilaya ya Kamenge ya mji mkuu wa Bujumbura.

Shambulizi kama hilo linatajwa kutekelezwa katikati mwa jiji hilo ambapo maafisa watatu walijeruhiwa.

Afisa mmoja wa polisi ambaye aliomba jina lake lisitajwe alisema kuwa ni wazi kuwa waandamanaji wameanzisha mashambulizi ya ghafla na ameongeza kuwa ikiwa raia hao wanataka vita watakiona cha mtema kuni.

UKAWA WATOA TAMKO JUU YA NJAMA ZA KUAHIRISHA UCHAGUZI

Vyama vinavyounda umoja wa katiba ya wananchi UKAWA vimetoa msimamo wao juu ya njama za kuahirisha uchaguzi mkuu unaotakiwa kufanyika OCTOBA mwaka huu na kwamba hawako tayari serikali iliyopo madarakani iongezewe muda,huku ukiitaka tume kutoka hadharani na mpango maalum na ratiba nzima ya maandalizi ya uchaguzi mkuu badala ya kuishia kusema kuwa uchaguzi uko pale pale.

Akielezea msimamo huo jijini dar es salaam mwenyekiti wa NCCR-MAGEUZI Mh. James Mbatia amesema endapo tume ya uchaguzi itaendelea na utaratibu uliotumika mkoani njombe itatumia zaidi ya miaka 10 kuandikisha na kuongeza kuwa kwa sasa suala la kura ya maoni liwekwe pembeni na serikali isitishe mambo yote yasiyokuwa ya msingi ielekeze nguvu zake kwenye zoezi la uboreshaji wa daftari la wapiga kura ili limalizike kwa wakati.

Kwa upande wake mwenyekiti wa chadema Mh Freeman Mbowe amesema hakuna mgawanyiko ndani ya ukawa licha ya kuwepo kwa changamoto za hapa na pale na kwamba tayari wameshafanya mgawanyo wa majimbo kwa asilimia 95 ambayo wamekubaliana isipokuwa majimbo 12 ambayo bado wanavutana lakini bado wako kwenye masahauriano.

Mwenyekiti wa CUF Prof. Ibrahimu Lipumba amesisitiza kuwa UKAWA haiungi mkono jaribio lolote la kufanya marekebisho ya katiba ya sasa kwa lengo la kuongeza muda wa utawala uliopo madarakani kwani kwa kufanya hivyo ni kwenda kinyume na katiba ya nchi na ukiukwaji wa sheria huku akiitadharisha serikali kutokuipeleka nchi kwenye machafuko yanayotokea burundi hivi sasa.

RAIS KIKWETE AKANA NJAMA ZA KUMMALIZA DK.MENGI

RAIS Jakaya Kikwete ameshtushwa na taarifa za kuhusishwa na mikakati ya kummaliza Mwenyekiti wa Makampuni ya IPP, Dk. Reginald Mengi. Kauli hiyo ya Rais Kikwete imekuja siku chache baada ya Dk. Mengi kudai kuwa kiongozi huyo wanchi ameapa kupambana naye kama ilivyoripotiwa na moja ya magazeti ya kila wiki nchini.

Kauli ya Rais Kikwete ilitolewa jijini Dar es Salaam jana na Mkurugenzi wa Mawasiliano Ikulu, Salva Rweyemamu, alipokuwa akitoa ufafanuzi wa mambo mbalimbali kwa waandishi wa habari.

Madai ya Dk. Mengi yalitokana na taarifa za gazeti hilo, zikidai kuwa Rais Kikwete aliyasema maneno hayo baada ya kukutana na aliyekuwa Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC), Zitto Kabwe ambaye alimweleza mkakati wa mfanyabiashara huyo wa kutaka kupambana naye baada ya kung'atuka madarakani.

Baada ya maelezo aliyotoa katika hotuba yake, waandishi walitaka kujua msimamo wa Ikulu juu ya madai ya Dk. Mengi, ambapo Rweyemamu alisema: "Wakati niko Jordan ndio tulipata habari kuwa mzee Mengi amesema hayo aliyosema, kila mtu akiwapo rais alishangazwa sana na kauli hiyo." Alisema kwa muda mrefu Rais Kikwete hajafanya kikao chochote na Zitto wala kuwasiliana naye kwa njia ya simu. "Hata wakati wa Escrow hakuwasiliana naye kwa sababu alikuwa nje ya nchi," alisema Rweyemamu.

Alisema Dk. Mengi ana mawasiliano ya Rais Kikwete na ni marafiki, hivyo ilitarajiwa baada ya kupata taarifa hizo angewasiliana naye.

Rweyemamu alisema hivi sasa kunauzushi mwingi nchini, hivyo siyo jambo jema mfanyabiashara huyo kusikiliza maneno ya watu kwani kufanya hivyo atakosana na watu wengi. Aprili 15, mwaka huu Dk. Mengi alituhumiwa kutaka kuiangusha Serikali ya Rais Kikwete na kumshughulikia baada ya kumaliza uongozi wake Oktoba, mwaka huu.

Dk. Mengi alisema habari hiyo imempa hofu kubwa juu ya mustakabali wa maisha yake kutokana na kile kilichoandikwa kuwa Kikwete aliapa atapambana naye. "Hofu yangu kubwa inasababishwa na Ikulu na Maelezo kwa kukaa kimya kwa zaidi ya wiki tatu bila kutoa ufafanuzi. "Ikulu na Maelezo wako makini katika kutoa ufafanuzi wa haraka wa jambo lolote linalomhusu Rais Kikwete, lakini katika hili nashangaa kuona taasisi hizo zimeamua kukaa kimya na kuacha tuhuma hizo kusambaa," alisema Dk. Mengi.

Aprili 18, mwaka huu naye Kiongozi wa Chama cha ACT-Wazalendo, Zitto Kabwe, alisema watu waliotajwa katika wizi wa fedha za Escrow wasitapetape kutafuta mchawi wakati wao ndio wezi wenyewe.

Kutokana na hali hiyo amesema suala la kumuhusisha mfanyabishara huyo kuwahonga wabunge ili kuishughulikia Serikali ni sawa na porojo. Kauli hiyo aliitoa mjini Shinyanga alipokuwa akihutubia ambapo alisema hatorudi nyuma katika kusimamia haki za Watanzania na kama kuna mtu ana chembe ya ushahidi wa jambo hilo apeleke kwenye vyombo vya dola kwa hatua za kisheria.

JK kimya kimya Jordan Rweyemamu alisema pia kuwa Jumamosi ya juma lililopita Rais Kikwete alisafiri kwenda nchini Jordan bila kutoa taarifa kwa umma kutokana na jambo hilo kuwa nyeti hali iliyochangiwa na mazingira ya mkutano aliokwenda kuhudhuria.

Alisema Rais Kikwete alikwenda nchini humo kwenye mkutano ambao pamoja na mambo mengine walizungumzia masuala ya ugaidi ambayo kwa sasa yamekuwa tishio duniani. "Ule mkutano ulitakiwa uwe wa siri kutokana na uzoefu wa Jordan na mambo ya ugaidi na pia majirani zake ambao ni Syria, Israel, Iraq na mataifa mengine," alisema. Sheria ya mtandao Rweyemamu alisema Rais Kikwete ataisaini sheria ya makosa ya mtandao licha ya baadhi ya wadau kuipinga.

Alisema sheria hiyo ilipitia hatua zote muhimu ikiwa ni pamoja na kupitishwa na Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

"Lazima rais aisaini kwa sababu ilipitia hatua zote muhimu ikiwa ni pamoja na kupitishwa na Bunge," alisema Rweyemamu.

WAKIMBIZI 152,572 WAPATIWA VYETI VYA URAIA

Waliokuwa wakimbizi wa Burundi nchini Tanzania zaidi ya 152,572 walioingia nchini humo tangu mwaka 1972, wamekabidhiwa vyeti vya uraia wa Tanzania na kuwa huru kuishi kama Watanzania wengine.

Wakimbizi hao walikuwa wameomba uraia wa Tanzania mwaka 2008 na kupewa na waziriwa mambo ya ndani mwaka 2010, sasa ni halali kuchagua na kuchaguliwa katika nafasi mbalimbali za uongozi zikiwemo za udiwani na ubunge.

Akizungumza wakati wa ugawaji wa vyeti hivyo, mkuu wa makazi ya Mishamo, Frederick Nisajile alisema ugawaji wa vyeti hivyo ulianza Novemba 24 mwaka 2014 katika makazi ya Katumba mkoani Katavi magharibi mwa Tanzania ambako watu 56,554 walipewa vyeti vya uraia na baadaye kuhamia katika makazi ya Ulyankulu mkoani Tabora, magharibi mwa Tanzania ambako wakimbizi 43,453 tayari wamepewa vyeti hivyo.

Kwa upande wake msemaji wa wizara ya mambo ya ndani, Isaack Nantanga amesema hatua ya Tanzania kuwapa uraia wakimbizi hao ni kutokana na hiyari yao na kwamba serikali ya Tanzania ilishauriana na Burundi na hatimaye kukubaliana wapatiwe uraia wanaotaka wa kuwa Watanzania.

Hata hivyo si mara ya kwanza kwa Tanzania kutoa uraia kwa wakimbizi wanaoishi Tanzania kwa muda mrefu.

Tanzania imefanya hivyo kwa wakimbizi waBurundi na Somalia ambao wameishi Tanzania kwa miaka mingi.

RAIS MORSI AHUKUMIWA KIFUNGO CHA MIAKA 20 JELA

Rais wa zamani wa Misri Mohamed Morsi amehukumiwa kifungo cha miaka 20 jela kwa makosa ya kusababisha kuuliwa waandamanaji mwaka 2012.

Rais wa Zamani wa Misri Mohamed MorsiKorti ya makosa ya jinai mjini Cairo imetoa hukmu hiyo wakati Morsi na watuhumiwa wengine katika kesi hiyo-wengi wao wakiwa viongozi wa chama cha Udugu wa kiislam-wakisimama ndani ya tundu la vigaendani ya ukumbi wa mahakama katika chuo cha mafunzo ya polisi mjini Cairo.

Kesi yao inahusu matumizi ya nguvu yaliyotokea nje ya kasri la rais mwezi decemba mwaka 2012.

Wafuasi wa Morsi waliwashambulia waandamanaji wa upande wa upinzani na kusababisha machafuko yaliyopelekea watu wasiopungua 10 kuuwawa.

Jaji Ahmed Youssouf ameachilia mbali madai ya kuchochea mauaji ya waandamanaji wawili na mwandishi habari mmoja machafuko hayo yaliporipuka mbele ya kasri la rais-madai ambayo wadadisi wengi walikuwa wakifikiriaa yangepeleka Morsi kuhukumiwa adhabu ya kifo.

Mbali na Mohamed Morsi, wakuu wengine 12 wa chama cha Udugu wa kiislamu na wafuasi wa itikadi kali akiwemo Mohammed el Beltagy na Essam el Erian, nao pia kila mmoja amehukumiwa kifungo cha miaka 20 jela.

Akitoa hukmu hiyo jaji Ahmed Youssouf ameyataja majina ya mtuhumiwa wote na kufafanua:
"Mohammed Mohamed Mursi, Mohammed el Baltagy na Essam el Erian wamehukumiwa kifungo cha miaka 20 jela kwa ushiriki wao wa kuchochea mauwaji ya umma wa wamisri na tuhuma za kulidhuru taifa la Misri."

Morsi na watuhumiwa wenzake walinyoosha vidole vinne-alama inayokumbusha malalamiko yaliyofanywa katika msikiti wa Rabaah al Adawiya ambako polisi waliingia kwa nguvu wakawauwa mamia ya waandamanaji wafuasi wa Morsi Agosti 14 mwaka 2013.


*Kesi zilisosalia dhidi ya Morsi hazitaharakishwa

Morsi anakabiliwa na kesi nyengine nne pamoja na wanachama wenzake wa udugu wa kiislamu, tangu alipopinduliwa na wanajeshi decemba mwaka 2013.

Morsi na wenzake wana nafasi ya kukata rufaa dhidi ya hukumu ya leo.

Wadadisi wanahisi viongozi wa Misri hawatofanya pupa kusikiliza kesi nyengine kwakua hakuna ghasia majiani na wafuasdi wa Udugu wa kiislamu hawakusayiki kwa wingi ili kuepusha wasikamatwe..

ETHIOPIA YAANZA SIKU TATU ZA MAOMBOLEZO

Ethiopia imeanza siku tatu za maombolezi ya kitaifa kwa heshima za raia wake waliouawa na wanamgambo wa kundi la Islamic State nchini Libya.

Bendera zitapepea nusu mlingoti wakati nalo bunge la nchi hiyo likikutana kujadili hatua ambazo litachukua kufuatia mauaji hayo ya raia wake zaidi ya ishirini.

Msemaji wa serikali Redwan Hussein, alisema kuwa waathiriwa hao wanaaminika kuwa wahamiaji waliojaribu kusafiri kwenda barani ulaya.

Mungano wa Afrika ambao una makao yake makuu nchini Ethiopia ulilaani mauaji hayo na kusema kuwa utafanya mikakati ya kuhakikisha kuwepo usalama nchini Libya.

Wanamgambo wa Islamic State walitoa kanda ya video ambayo inakisiwa kuonyesha mauaji hayo yanayoonyesha watu hao wakipigwa risasi na kukatwa vichwa.

DK. MENGI AHOFIA MAISHA YAKE

Mwenyekiti wa Makampuni ya IPP, Dk. Reginald Mengi amesema anahofia usalama wa maisha yake, kufuatia habari iliyoandikwa katika gazeti moja la kila wiki kwamba, Rais Jakaya Kikwete aliapa kupambana naye jambo ambalo limempa hofu kubwa.

Kadhalika, amelalamikia Kurugenzi ya Mawasiliano Ikulu na Idara ya Habari Maelezo kwa kukaa kimya nakuacha kutoa ufafanuzi dhidi ya tuhuma hizo, huku taarifa hizo zikiendelea kusambazwa.

Akizungumza na waandishi wa habari jana jijini Dar es Salaam, Mengi alisema kuwa tuhuma zilizotolewa dhidi yake kuwa yeye nikinara wa kuhujumu serikali ya Rais Kikwete siyo za kweli.

Dk.Mengi alisema amesoma kwa masikitiko makubwa habari iliyochapishwa Machi 23, mwaka huu na gazeti la Taifa Imara, yenye kichwa cha habari 'Zitto amchongea Mengi kwa JK' ambapo pamoja na mambo mengine inasema kuwa Zitto Kabwe amemchongea Dk. Mengi kwa Rais Kikwete kwamba ndiye kinara wa kuhujumu serikali yake.

Alisema habari hiyo ambayo chanzo chake kimeelezwa kwamba ni Ikulu,iliendelea kueleza kuwa Zitto alikutana na Rais Kikwete muda mfupi baada ya kuwasilisha bungeni ripoti ya Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) kuhusiana na kashfa ya Escrow ambayo Zitto alikuwa ni mwenyekiti wake.

"Habari hiyo inasema kwamba katika mazungumzo yake na Rais Kikwete Zitto amenukuliwa akimueleza mkuu huyo wa nchi kuwa anayesababisha serikali yake iyumbe kila mara ni Mengi," alisema Dk. Mengi.

Dk. Mengi alisema habari hiyo ambayo nakala yake ameiambatanisha kwenye taarifa yake, inasema yeye Zitto , binafsi amekuwa akishawishiwa na Dk. Mengi kuiangusha serikali ya Rais Kikwete.

Hata hivyo, Dk. Mengi alisema katika habari hiyo Zitto alikwenda mbali zaidi kumueleza Rais Kikwete kuwa Dk. Mengi ameapa kuwa Rais Kikwete akimaliza muda wake wa Urais atamshughulikia kwa nguvu zake zote.

Alisema habari hiyo imeeleza kwamba baada ya maelezo hayo, Rais Kikwete aliapa kupambana na Dk. Mengi na akamshukuru Zitto kwa kumpa taarifa hizo.

Mengi alisema tuhuma zilizotolewa kuhusu nia yake ya kutaka kuiangusha serikali ya Rais Kikwete na kumshughulikia baada ya kumaliza muda wake wa uongozi, zimemshtua sana na tamko la kwamba Rais Kikwete aliapa kuwa atapambana na yeye zimempa hofukuhusu mustakabali wa maisha yake.

Alisema kuwa hofu yake kubwa inasababishwa na Ikulu na Idara ya habari Maelezo kukaa kimya kwa zaidi ya wiki tatu bila kutoa ufafanuzi wowote.

"Najua umakini wa Kurugenzi ya Mawasiliano Ikulu na Idara ya habari Maelezo katika kutoa ufafanuzi wa haraka wa jambo lolote linalomhusu Rais, lakini katika hili nashangaa kuona taasisi hizo zimeamua kukaa kimya na kuacha tuhuma hizo kusambaa,"alisema Dk. Mengi.

Aliongezea kusema kuwa," hofu yangu inazidi kuwa kubwa kwa sababu Rais ni Mkuu wa Majeshi ya ulinzi na usalama. Kauli yake kama ilivyonukuliwa na gazeti hili kwamba atapambana na mimi inawezekana kuchukuliwa kama agizo kwa vyombo vya dola kuniangamiza," alisema.

Alitolea mfano mwaka 1170, AskofuMkuu wa Canterbury nchini Uingereza aliuawa baada ya walinzi wa mfalme kusikia mfalme akisema"hakuna anayeweza kuniondolea huyo mkorofi?". Walinzi wake wakadhani mfalme ameagiza wamuue Askofu huyo na wakamuua, alisema.

CHANZO: NIPASHE

MWANDISHI WA HABARI APIGWA RISASI UKRAINE

Mwandishi maarufu wa Ukraine ameuawa kwa kupigwa risasi mjini Kiev na watu waliokuwa wameficha nyuso zao.

Oles Buzyna alifahamika sana kwa maoni yake ya kuunga mkono Urusi na amefanya kazi yauchapishaji akishirikiana na serikali ya rais Viktor Yanukovych aliyeondolewa madarakani nchini Ukraine.

Kifo chake kimekuja siku moja baada ya mwanasiasa mwenye kupendelea Urusi, Oleh Kalashnikov kuuawa katika shambulio linalofanana.

Rais Poroshenko ametaka uchunguzi ufanyike haraka, amesema mauaji haya dhidi ya watu maarufu yamefanyika makusudi na maadui wa Ukraine.

KIJANA JELA MIAKA 30 KWA KUMLAWITI MWANAFUNZI

MAHAKAMA ya Wilaya ya Tabora imehukumu Masudi Nassor (20) kifungo cha miaka 30 jela baada ya kupatikana na hatia ya kumlawiti mwanafunzi wa kike wa shule ya msingi mwenye umri wa miaka tisa.

Akitoa hukumu hiyo jana Hakimu Mkazi wa Mahakama hiyo, Bahati Chitepo alisema kwamba ametoa adhabu hiyo ili iwe fundisho kwa watu wengine wenye nia kama hiyo kama kijana huyo mdogo.

Alisema kitendo alichofanya kijana huyo mwenye nguvu ya kufanya kazi na kupata mwenzi wake wanayelingana umri inaonesha wazialifanya hivyo makusudi.

Hata hivyo Hakimu Chitepo alisema kwamba ushahidi uliotolewa mbele ya Mahakama hiyo kutoka kwa mganga aliyemhudumia mtoto huyo katika Hospitali ya Kitete unaonesha wazi kwamba mshtakiwa alimwingilia mtoto huyo kinyume na maumbile yake na kumsababishia maumivu makali.

Kabla ya kutolewa kwa hukumu hiyo Mwendesha Mashitaka wa Serikali aliiomba Mahakama hiyo itoe adhabu kali kwa mshitakiwa huyo kwa kile alichoeleza kuwa hilo ni kosa lake la pili hivyo adhabu hiyo itakuwa fundisho kwa watu wengine wenye nia mbaya.

Awali Mwendesha Mashitaka alieleza Mahakama hiyo kwamba mnamo Januari 22, mwaka huu majira ya asubuhi katika Kata ya Kiloleni, Manispaa ya Tabora, Nassor akiwa anaendesha baiskeli alikutana na mlalamikaji akiwa anakwenda shuleni na kuomba lifti.

Baada ya kumpandisha kwenye baiskeli Nassoro alikwenda naye kwenye pori la Kalunde ambapo alimlawiti mara tatu na kumtelekeza huko kisha kukimbia lakini alikamatwa na askari Jeshi aliyekuwa dori katika kambi hiyo nakumfikisha Polisi.

Hata hivyo mshitakiwa huyo aliiomba Mahakama hiyo impunguzie adhabu kwani anaishi na babu yake mlemavu wa mguu na wazazi wake wote wamefariki.

WATANZANIA KURUDISHWA TOKA YEMEN

Tanzania imetangaza kuwarejesha nchini raia wake wanaoishi Yemen, kufutia mapigano yanayoendelea nchini humo.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe alitangaza uamuzi huo wakati akizungumza na Balozi wa Tanzania nchini Yemen, Ali Ahmed Saleh, jana.

Waziri Membe alisema ni jukumu la Serikali kuhakikisha kuwa Watanzania hao ambao wengi wao ni wanafunzi, wanarejea nyumbani salama.

Awamu ya kwanza ya kurudisha Watanzania ilianza siku chache zilizopita chini ya uratibu wa Ofisi zaUbalozi wa Tanzania mjini Mascut, Oman.

Kwenye awamu hiyo Watanzania 25 walirudishwa nyumbani huku jitihada za kuandikisha wengine zikiendelea.

"Nimeruhusu matumizi ya fedha ya dharura ili kuhakikisha ndugu zetu walioko kwenye hatari na machafuko ya Yemen wanarejeshwa salama nyumbani mara moja," alisema Membe.

RAIS ZUMA ASHTUSHWA NA GHASIA ZA NCHINI MWAKE

Rais wa Afrika Kusini, Jacob Zuma, ameshutumu ghasia zilizopo nchini humo hivi sasa ambapo wahamiaji wageni wameshambuliwa.

Ametaja ghasia hizo kama za kutisha na zisizokubalika.

Watu watano wameuawa tangu juma lililopita ambapo wamelaumiwa na wenyeji kwa kufanya kazi wanazostahili kufanya wao.

Akihutubia bunge leo alasiri, RaisZuma alisema mashambulizi hayo yalikiuka haki za kibinadamu kama vile haki ya kuwa hai na kuheshimiwa.

Awali maelfu ya raia wa Afrika Kusini wamefanya maandamano katika mji wa Durban kulalamikiakile walichotaja kama ukatili dhidi ya Waafrika wengine.

Katika maeneo yanayopakana na Johannesburg, wenye maduka wenye asili ya kutoka Ethiopia, Somalia na maeneo mengine ya Afrika walifunga biashara zao, wakiogopa kuwa mali yao itaporwa.

WATU 10 WATIWA MBARONI KWA KUHISIWA KUJIHUSISHA NA UGAIDI

POLISI mkoani hapa imewatia mbaroni watu zaidi ya tisa wanaojihusisha na uhalifu wakiwa na milipuko hatari na zana za milipuko, wakiwa wamefichwa ndani ya Msikiti wa Suni kata ya Kidatu, wilayani Kilombero, mkoani Morogoro.

Licha ya kukamatwa kwa watuhumiwa hao, mwingine ameuawa kwa kuchomwa moto na wananchi wenye hasira baada ya kumshambulia na kumkata kwa jambia shingoni askari polisi mwenye namba F. 3323 Koplo Nassoro.

Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Morogoro, Leonard Paulo, alithibitisha jana na kusema watu hao walikamatwa juzi majira ya saa 3.30 usiku katika kitongoji cha Nyandeo, Kijiji cha Chicago, kata na tarafa ya Kidatu, wilayani Kilombero mkoani Morogoro.

Hata hivyo, alisema Polisi walipofika katika msikiti huo waliuomba uongozi wa msikiti kuwatoa watu wote waliokuwa msikitini ili kuweza kubaini watu ambao wanatiliwa mashaka.

Kwa mujibu wa Kamanda huyo, waumini wote walitakiwa kutoka nje ya msikiti wakiwa na mabegi yao, nandipo katika ukaguzi na upekuzi huo walifanikiwa kuwakamata watu hao wakiwa na milipuko hatari.

Hata hivyo, alisema kukamatwa kwao ni baada ya Polisi kupokea taarifa za siri zinazohusu watu hao kujihusisha na vitendo vya uhalifu na pia alimtaja aliyefariki katika tukio hilo kuwa ni Hamad Makwendo mkazi wa Manyasini, Ruaha wilayani Kilombero ambaye ndiye anadaiwa kuwa mwenyeji wa watuhumiwa hao wengine.

Akielezea zaidi alisema, baada ya kupokea taarifa hizo, Polisi ilifuatilia na kwamba, katika ufuatiliaji huo waliona pikipiki mbiliza matairi matatu aina ya Bajaj zikielekea katika mji wa Mkamba eneo la wilaya ya Kilombero ambazo ziliwapotea na baada ya kitambo kidogo, Bajaj hizo zilirudi tena zikiwa na abiria mmoja.

Alisema, Polisi waliokuwepo eneo hilo walisimamisha bajaj moja na iliposimama, mtu mmoja akiwa na jambia mkononi aliruka kwenye bajaj na kuanza kukimbia ndipo askari walipoanza kumkimbiza.

Kwa mujibu wa Kamanda huyo, mtuhuyo alipogeuka alimshambulia kwakumkata na jambia shingoni askari mwenye namba F. 3323 Koplo Nassoro na ndipo askari mwenye namba E. 9245 Koplo Chomola alipompiga risasi ya mguuni upandewa kulia mtuhumiwa huyo.

Alisema wananchi walifika eneo la tukio na baada ya kuona askari ameumizwa ndipo walipomchoma moto mtuhumiwa na kusababisha kifo chake.

Alisema baada ya tukio hilo, taarifa zilifikishwa mkoani na ndipo Polisi mkoa walikwenda eneo la tukio wakiwa na timu ya askari na kwa kushirikiana na wananchi wa eneo hilo ndipo walipokamatwa watuhumiwa zaidi ya tisa waliokutwa ndani ya Msikiti wa Suni uliopo Kidatu.Kwa mujibu wa Kamanda wa Polisi wa Mkoa, vitu vilivyokutwa katika mabegi hayo ni pamoja na milipuko 30 aina ya 'Water Explosive Gel', bendera nyeusi yenye maandishi ya Kurani na Kiswahili yenye maneno Mungu Mmoja; nyaya, majambia, bisibisi, nguo za jeshi, misumeno yachuma, spana piperange, madaftari na vitabu mbalimbali vikiwemo vya risiti.

Vitu vingine walivyokutwa navyo ni vifaa vya kuficha uso 'mask' na kitambulisho kimoja chenye jina la Ramadhani Hamis kinachojieleza ni Ofisa wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA).

Hata hivyo, alisema kwa mtuhumiwa aliyeuawa na wananchi alikutwa na risasi sita kati ya hizo tano zikiwa za bunduki aina ya SMG na risasi moja ya bunduki aina ya Mark IV, pamoja na nyaya mbili za umeme zikiwa kwenye mfuko mdogo wa kijeshi.

Kwa mujibu wa Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro, watuhumiwa wanaendelea kuhojiwa ambapo askari aliyekatwa na jambia shingoni amelazwa Hospitali ya Kiwanda cha Sukari Kilombero na hali yake inaendelea vizuri.

MGANGA WA JADI AKAMATWA NA NYARA ZA SERIKALI

Jeshi la Polisi Mkoa wa Katavi linamshikilia mganga mmoja wa Jadi kwa tuhuma za kumkamata akiwa na ngozi mbili za chui na mkia wa nyumbu akiwa amehifadhi ndani ya chumba chake cha kulala.

Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Katavi Dhahiri alimtaja mtuhumiwa huyo aliyekamatwa na nyara hizo za Serikali kuwa ni Kabichi Nhulu (39)Mkazi wa Kijiji cha Kakese Tarafa ya Misunkumilo Wilaya ya Mpanda Mkoani hapa.

Alisema tukio la kukamatwa kwa mtuhumiwa huyo lilitokea hapo majira ya saa kumi na mbili jioni nyumbani kwa mtuhumiwa katika Kijiji cha Kakese.

Alifafanua kuwa mtuhumiwa huyo alikamatwa kufuatia taarifa za kilizotolewa kwa jeshi la polisi kutoka kwa raia wema kuwa mtuhumiwa huyo anamiliki nyara za Serikali visivyoalali.

Alieleza baada ya taarifa hizo kulifikia jeshi la polisi lilifika kijijini hapo kwa lengo la kufanya upekuzi kwenye nyumba ambayo anaishi mtuhumiwa huyo.

Kidavashari alisema baada ya polisi kufanya upekuzi ndani ya nyumba ya mtuhumiwa Kabichi Nhulu alikamatwa akiwa na ngozi mbili za chui na mkia wa nyumbu akiwa amehifadhi ndani ya chumba chake cha kulala akiwa ameficha chini ya uvungu wa kitanda.

Mtuhumiwa anaendelea kushikiliwa na jeshi la Polisi kwa mahojiano zaidi na anatarajiwa kufikishwa mahakamani baada ya upelelezi kukamilika ili aweze kujibu tuhuma inayomkabili.

Chanzo: KATAVI YETU

AJARI ZAUA WATU 866 KATIKA MIEZI MITATU

JESHI la Polisi nchini, limesema Watanzania 866 wamefariki dunia katika kipindi cha miezi mitatu, kutokana na ajali za barabarani.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, Kamanda wa Kikosi cha Usalama Barabarani, Mohammed Mpinga alisema kuanzia Januari hadi Machi mwaka huu, ajali 2,116 zimetokea katika maeneo mbalimbali nchini.

Alisema katika ajali hizo, watu 866 wamepoteza maisha na wengine 2,363 kujeruhiwa, ambao baadhi yao wamepata ulemavu.

Hata hivyo nje na kipindi hicho, ajali nyingine zilizotokea kuanzia Machi 11 hadi April 12, mwaka huu zimesababisha vifo vya watu wengine 103 na hivyo kufanya idadi ya watu walipoteza maisha katika kipindi cha miezi mine kuwa 969.

Akizungumzia sababu za ajali hizo, Kamanda Mpinga alisema ni mwendo kasi usiozingatia alama za barabarani na kufutika kwa baadhi ya michoro barabarani.

Alisema sababu nyingine, ni baadhi ya wamiliki wa vyombo vya moto kuhamasisha mwendo kasi kwa madereva wao, abiria kushabikia nabaadhi ya wadau wa usalama barabarani kutowajibika ipasavyo.

Kamanda Mpinga, alisema uzembe wa madereva, ubovu wa barabara na uoni hafifu kwa baadhi ya madereva ni miongoni mwa sababu zinazochangia ajali nyingi kutokea.

Alisema kuwapo kwa tatizo la utelezi, ulevu na uchovu, unaosababishwa na mvua inayoendelea kunyesha nako kumeongeza idadi ya ajali.

"Utumiaji wa dawa za kulevya ni sababu nyingine ambayo inasababisha ajali nyingi," alisema.

Huku akionekana kusikitishwa na matukio hayo, Kamanda Mpinga alisema tatizo jingine ni ubabe wa madereva wanaoendesha magari makubwa ya mizigo kutothamini magari ndogo, waenda kwa miguu, bajaj pamoja na pikipiki wawapo barabarani.


HATUA KALI

Kuhusu hatua, Kamanda Mpinga, alisema madereva wote waliosababisha ajali za hivi karibuni watachukuliwa hatua, ikiwa ni pamoja na kunyang'anywa leseni zao.

Alisema ajali nyingine zitakazo tokea baada ya hizo, wamiliki wa vyombo husika watafungiwa kampuni zao.

Alitoa wito kwa watumiaji wa barabara kuchukua hadhari, madereva kuwa makini msimu huu wa mvua.

Kutokana na hali hiyo, amewataka wamiliki wa mabasi yanayokwenda safari za mbali kuajiri madereva wawili watakao safiri ili kumpunguzia dereva uchovu.

Aliomba Bunge Ili kukomesha au kupunguza wimbi la ajali hizo, Kamanda Mpinga ameliomba Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kubadilisha sheria zilizopo za usalama barabarani ambazo zinatoa adhabu ndogo kwa watu wanaosababisha ajali.

Alisema uchunguzi uliofanywa na kikosi hicho, umebaini wamiliki wa mabasi wamekuwa wakihamasisha madereva wao kwenda mwendo kasi kwa kujali maslahi yao kibiashara zaidi.

Miongoni mwa ajali zilizogusa mioyo ya watu ni ile iliyotokea Machi 11, mwaka huu katika Kijiji cha Changarawe Wilaya ya Mufindi mkoani Iringa ambapo watu 50 walipoteza maisha, huku 20 wakijeruhiwa kutokana na basi la Majinja kugongana na lori.

Katika ajali nyingine iliyotokea maeneo ya Mikumi Mbugani mkoani Morogoro Machi 17, mwaka huu na kuhusisha basi la Fm Safari na lori aina ya Scania, watu wawi walipoteza maisha na nane kujeruhiwa.

Ajali nyingine ilitokea Machi 19, mwaka huu eneo hilo hilo la Mikumi na kuhusisha basi dogo aina ya Tata linalojulikana kwa jina la Msanga Line lililogongana na basi la Luvinzo na kusababisha vifo vya watu saba na majeruhi 17.

Ajali nyingine ni ile iliyotokea Aprili3, mwaka huu iliyokuwa imebeba mashabiki wa timu ya soka ya Simba ambao walikuwa wakielekea mkoani Shinyanga, ambapo iliua watu saba na kujeruhi 22.

Mbali na ajali hizo, ajali nyingine iliyotokea mkoani Tanga eneo la Mkata ilihusisha basi la Ratco, Ngorika na gari dogo aina ya Paso ambapo watu 10 walipoteza maisha pamoja na kujeruhi wa 12.

Pia Aprili 12, mwaka huu mkoani Morogoro kulitokea ajali katika milima ya Hiyovi ambapo basi la Nganga Express lililogongana na Fuso na baadaye kuwaka moto na kusababisha watu 19 kupoteza maisha, huku wengine 10 wakijeruhiwa.

17 WAUAWA SHAMBULIO LA AL SHABAAB

Watu 17 wameripotiwa kuuawa na wengine 20 kujeruhiwa vibaya wakati wanamgambo wa Kiislamuwa Al Shaabab waliposhambulia majengo ya wizara ya elimu mjini Mogadishu, Somalia.

Mwandishi wa BBC Mohammed Moalimu, amesema kuwa wavamizi hao walilipua bomu lililotegwa ndani ya gari kwenye ukuta wa jengo hilo Kulingana na msemaji wa idara ya usalama wa ndani Mohammed Yusuf watu 8 waliuawa na wavamizi hao huku wanajeshi wawili wakipoteza maisha yao.

Askari mmoja ni wa muungano wa majeshi ya umoja wa Afrika.

Msemaji huyo anasema kuwa wavamizi hao walikuwa ni 7 wawili waliojilipua langoni huku wengine watano wakikabiliwa na maafisa wa usalama.

Walioshuhudia wanasema wavamizi hao walitumia bomu lililotegwa ndani ya gari kabla ya wavamizi kadhaa kuingia ndani yajengo wakiwa wamejihami kwa bunduki za rashasha.

Msemaji wa wa kitengo cha mashambulizi cha kundi la wapiganaji wa Al Shabaab Sheikh Abdiasis Abu Musab, amethibitisha kuwa ni wao waliotekeleza shambulizi hilo na kuwa ''wapiganaji wetu wamekwisha ingia ndani ya jengo hilo lenye wizara ya elimu''

Mapigano yanaendelea hadi sasa ndani ya jengo hilo baina ya majeshi ya serikali na wapiganaji hao kulingana na mwakilishi wa polisi.

Wapiganaji wa Al shabaab wametekeleza mashambulizi kama haya katika siku za hivi punde.

Mwezi uliopita wapiganaji wa Al Shabaab walishambulia hoteli moja mjini Mogadishu uvamizi huo ulikamilika siku mbili zilizofwatia.

Waandishi wa habari walioshuhudia matukio kabla ya uvamizi huo wanadai kuwa kulikuwa na milipuko miwili mikubwa kabla ya milio ya risasi kuanza kusikika kutoka jengo hilo.

Hakuna kundi lililothibitisha kutekeleza shambulizi hilo lakini Al shabaan imekuwa ikitumia mbinu kama zilizotumika leo.

Kundi hilo la waislamu linapinga serikali iliyoko sasa ambayo inaungwa mkono na majeshi ya Umoja wa Afrika.

OBAMA KUIONDOA CUBA KATIKA ORODHA YA UGAIDI

Rais Barack Obama amesema ataiondoa Cuba kutoka orodha ya Marekani ya nchi zinazofadhili ugaidi duniani.

Taarifa kutoka Ikulu ya Marekani imesema hatua hiyo inakuja huku kukiwa na jitihada za kujenga uhusiano kati ya Marekani na Cuba.

Uwepo wa Cuba katika orodha hiyo pamoja na nchi za Syria, Iran na Sudan kilikuwa kigezo cha Cuba katika mazungumzo yake na Marekani ya kufungua ofisi za balozi kati ya nchi hizo.

Seneta wa chama cha Republican Marco Rubio ameishutumu Ikulu ya Marekani kwa uamuzi huo, akisema kuwa Cuba bado ni taifa linalofadhili ugaidi.

"Wanawahifadhi Wamarekani ambao wanakimbia mkono wa sheria, akiwemo mtu aliyemuua afisa wa polisi huko New Jersey zaidi ya miaka 30 iliyopita," amesema Bwana Rubio, Mmarekani mwenye asili ya Cuba ambaye alizindua kampeni yake ya uchaguzi wa rais wa Marekani 2016.

"Ni nchi ambayo pia inaisaidia Korea Kaskazini kukwepa vikwazo vya silaha vilivyowekwa na Umoja wa Mataifa."

Bwana Obama alitangaza tukio la kihistoria la kurejesha uhuasiano kati ya Marekani na Cuba mwezi Desemba 2015 lakini vikwazo vya kibiashara vya Marekani dhidi ya Cuba vinabakia, na vinaweza kuondolewa tu na baraza la Congress.

ASASI ZISIZO ZA KISERIKALI 53 ZAMUANDIKIA BARUA RAIS ASISAINI MUSWADA

Asasi zisizo za kiserikali 53 zimemwandikia Rais Jakaya Kikwete,barua ya kumuomba asisaini Sheria ya Takwimu ya 2015 na Sheria ya Makosa ya Mtandaoni zilizopitishwa na Bunge hivi karibuni ili kuruhusu kufanyiwa marekebisho kwanza.

Kwa majibu wa barua hiyo iliyosainiwa na asasi 53 na mtandao wa asasi za kiraia ambayo NIPASHE imeona nakala yake, zinataka sheriahizo zirudishwe bungeni kuondoa vifungu vinavyokwenda kinyume na Katiba ya Jamhuri ya Muungano ya mwaka 1977 na haki za binadamu kwa ujumla.

"Tunashauri kabla ya kutia saini sheria hizi upate muda wa kusikilizakilio cha jamii juu ya ubaya wa sheria hizi kwa mustakabali wa taifa. Sheria hizi zikipitishwa katika utawala wako zitatia doa dhamira yako nzuri ya kuongeza wigo na uhuru wa habari na ushiriki wa wadau katika maendeleo ya kitaifa,"alisema.

Barua hiyo imeeleza sababu za kumtaka Rais kutosaini sheria hizo kuwa ni, malengo ya Sheria ya Takwimu siyo tu kuratibu takwimu za kitaifa, bali umetoa madaraka makubwa kwa Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) kama kitovu cha utoaji wa takwimu nchini.

"Maana yake ni kwamba taasisi zote za serikali, mashirika binafsi, taasisiza elimu ya juu, vyuo vikuu na taasisi za utafiti hazitakuwa na uhuru wa kutoa matokeo ya tafiti wanazozifanya bila ya kibali au ridhaa ya NBS" ilisema barua hiyo.

Imesema pia sheria hiyo imeweka adhabu kali kwa vyombo vya habari,asasi za kiraia, taasisi za utafiti na vyuo vya elimu ya juu vitakavyotenda makosa yaliyoainishwa katika sehemu ya tatu ya sheria.

Kuhusu Sheria ya Makosa ya Mitandao, barua hiyo imesema itaminya kwa kiasi kikubwa uhuru wa wananchi kuwasiliana na kupashana habari endapo itasainiwa bila marekebisho.

"Ni dhahiri sheria hii imelenga kufuta kabisa uhuru wa mawasilianona matumizi ya mitandao ya kijamiikama Facebook, WhatsApp, Jamii Forums, Twitter, blog… Kupitishwa kwa sheria hii bila kufanyiwa marekebisho kutasababisha Watanzania wengi kutiwa hatiani bila sababu, lakini pia kutaondoa kabisa uhuru wa habari nchini" iliongeza kusema.

CHANZO: NIPASHE

RADI YAUA 6 YAJERUHI WENGINE 15

Wanafunzi sita wa shule ya msingi, wamefariki dunia kwa kupigwa na radi na wengine 15 wamejeruhiwa miongoni mwao vibaya kufuatia mvua kubwa iliyoambatana na upepo mkali na radi kunyesha katika Manispaa ya Kigoma/Ujiji jana.

Tukio hilo lilitokea jana saa 5:00 asubuhi katika Shule ya Msingi Kibirizi iliyopo kwenye manispaa hiyo.


KAULI YA MGANGA

Kaimu Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Mkoa wa Kigoma ya Maweni, Dk. Fadhili Kibaya, alisema alipokea maiti za watu wanane zikiwamo za wanafunzi sita wa Shule ya Msingi Kibirizi na moja ya mwalimu wao jana saa 6:00 mchana.

Alisema maiti nyingine ni ya mwanaume mkazi wa Bangwe katika manispaa hiyo. Alisema mbali ya maiti, pia alipokea majeruhi 15.

Dk. Kibaya aliyataja majina ya wanafunzi waliofariki dunia kuwa ni Yusuf Athumani (8), Hassani Ally (9),Fatuma Silei (7), Zamuda Seif (8), Warupe Kakupa (10) na Shukurani Yohana (7) ambao ni wanafunzi wa Shule ya Msingi Kibirizi.

Alisema wengine waliofariki dunia katika tukio hilo la kusikitisha ni mwalimu wa shule hiyo, Elieza Mbwambo (25) na Focus Ntahaba (35), mkazi wa Bangwe katika manispaa hiyo.

Dk. Kibaya alitaja wanafunzi waliojeruhiwa katika tukio hilo na ambao wamelazwa wodi namba nane hospitalini hapo kuwa ni Mahamoud Sijafiki (10), Najimu Rajabu (9) na Khatibu Amani (9).Aidha, alisema wengine watano wako kwenye chumba cha uangalizi maalum (ICU) na wengine walitibiwa na kuruhusiwa kurudi nyumbani kwao.


MWALIMU ANENA

Kwa upande wake, Mwalimu wa Shule ya Msingi Kibirizi, Emmanuel Wilbert, alisema mwalimu aliyefariki dunia alitoka darasa la tatu na kuingia ofisi ya walimu na kukaa akiendelea na shughuli zake kama kawaida.

Wilbert alisema baada ya muda mvua kubwa iliyoambatana na upepo mkali na radi huku walimu wengine wakiwa madarasani wakiendelea na vipindi, ilipiga radi iliyosababisha kifo cha mwalimu na wanafunzi hao waliokuwa madarasani.

Alisema baada ya tukio hilo, wanafunzi na walimu walikimbia ovyo na mwalimu mwingine Merina Serilo, alipigwa na radi na kujeruhiwa. Hata hivyo, alisema hali yake inaendelea vizuri.


KAULI YA KAMANDA

Kwa upande wake, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kigoma, Ferdinand Mtui, alithibitisha kutokea kwa tukiohilo na kueleza kuwa masuala ya radi hayazungumziki.

WANAFUNZI KIU WAGOMA

Wanafunzi wa vitivo vya Sayansi ya Afya wa Chuo Kikuu Kishiriki cha Kampala-tawi la Dar es Salaam (KIU), wamegoma kuendelea na masomo baada ya kubaini kuwa kozi wanazosoma katika chuo hicho hazijasajiliwa katika ya bodi mbalimbali kama taratibu na sheria zinazoelekeza.

Walianza mgomo huo tangu Ijumaa iliyopita baada ya kugundua kuwa kozi wanazofundishwa hazijasajiliwa katika Bodi ya Mafamasia, Bodi ya Maabara na Baraza na Madaktari.

Walisema jana chuoni hapo kuwa wamekuwa wakiendelea na masomo bila kugundua kama kozi wanazochukua hazijasajiliwa katika bodi hiyo huku uongozi wa chuo ukikaa kimya.

Waziri wa Afya wa Serikali ya Wanafunzi (KIUSO), Kenedy Murunya, alisema walibaini kuwa kozi wanazosoma hazijasajiliwa baada ya kwenda katika ofisi za bodina kuelezwa kuwa hazijasajiliwa. Wanafunzi waliokumbwa na tatizo hilo ni wale wanaochukua Shahada za maabara, udaktari na upasuaji.

"Wanafunzi walipokwenda Tume ya Vyuo Vikuu (TCU) waliambiwa kuwa tume imeshafanya asilimia 50 ya usajili wa chuo hicho na asilimia 50 nyingine zilizobaki zinatakiwa zishughulikiwe na bodi husika za usajili," alisema.

Mwakilishi wa Kitivo cha udaktari (SUGA)), Martin Augustine, alisema 2013 wakati wanaanza masomo waliambiwa na uongozi wa chuo kuwa kozi zao zimesajiliwa bila kujua walikuwa wanadanganywa na uongozi wa chuo hicho.

Alisema mwaka huu walikwenda Bodi ya Madaktari Tanganyika wakaambiwa kuwa bado kozi yao haijasajaliwa kutokana na uongozi wa KIU kuzembea kutuma nakala muhimu zitakazofanikisha usajili.

Alisema Ijumaa baada ya mgomo wawakilishi wa vitivo vya sayansi wangazi zote za masomo walifanya kikao na uongozi wa chuo chini ya OCD wa Ilala kujadili matatizo ya usajili na uongozi na kuwa cha ajabu wawakilishi hao hawakupewa majibu yanayoridhisha hali iliyosababisha mgomo huo kuendelea.

Alisema tangu mgomo uanze Jeshi la Polisi limeweka kambi likiangalia hali ya usalama wa chuo.

Alisema Septemba, 2014 walikwenda Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi kwa lengo la kumuona Waziri, Dk. Shukuru Kawambwa, lakini hawakumuona hivyo kumwandikia barua ili awape majibu ambayo hadi sasa hawajapatiwa.

Alisema wanaendelea kulipa ada kubwa japokuwa serikali ilikiagiza chuo hicho kushusha ada cha kushangaza Baraza la KIU ambalo lipo Uganda lilikataa maagizo ya serikali.

Alisema wanafunzi wa udaktari mwaka wa pili wanalipa Sh. milioni 8 wakati wa mwaka kwanza wanatozwa Sh. milioni 6.7, maabarash. milioni 4.8, Famasia milioni 5.4 huku wa mwaka wakilipa sh. milioni3.8.Kwa mujibu wa Waziri Mkuu wa KIUSO, Elisha Mushi, mgomo huo unajumuisha wanafunzi wa vitivo vya sayansi pekee wakati vitivo vya biashara na sharia vinaendelea na masomo.

Jitihada za kumpata Rais wa KIUSO, Elias Mbogo pamoja na Waziri wa Elimu, Answari hazikufanikiwa baada ya kuambiwa kuwa wote wamekwenda Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii kupata ufumbuzi wa matatizo ya wanafunzi.

Hata hivyo, Naibu Waziri wa Elimu wa Kiuso, Fadhilina Kassim, alisema anachofahamu yeye kuwa chuoni hapo kuna mgomo wa wanafunzi, lakini mwenye dhamana ya kuzungumzia suala hilo ni Waziri wa Elimu au Waziri Mkuu.

Afisa Masoko na Uhusiano wa KIU, Keneth Uki, alithibitisha kuwapo kwa mgomo wa wanafunzi hao huku akisisitiza kuwa vitivo vingine vya sayansi vimeshakamilika usajili ingawa kitivo cha wanafunzi wanaochukua Famasia tu ndio kozi zao hazijakamilisha usajili katika Baraza la Famasia Tanzania.

Wanafunzi hao wanaiomba wizara husika iwapatie ufafanuzi kuhusiana na suala hilo pamoja na uhalali wao KIU kwa kuwa walijiunga na chuo hicho kupitia TCU na NACTE.

NEC YASEMA BVR 1600 KUWASILI MUDA WOWOTE

Tume ya Taifa ya Uchaguzi (Nec), imesema vifaa BVR Kts 1,600 vinatarajiwa kuwasili wakati wowotekuanzia leo.

Kadhalika, Nec imesema itatoa ratiba ya uandikishaji kwa mfumo wa Biometric Voters Registration (BVR), kwenye mikoa ya Lindi, Mtwara, Iringa na Ruvuma.

Mikoa hiyo ni yenye watu 4,809,428kwa mujibu wa Sensa ya watu na makazi ya mwaka 2012 na kati yao watu 2, 599,205 ndiyo wenye sifa ya kupiga kura hadi kufika siku ya uchaguzi mkuu mwishoni mwa mwezi Oktoba mwaka huu.

Mwenyekiti wa Nec, Jaji Mstaafu Damian Lubuva (pichani), alisema aliliambia NIPASHE kuwa baada ya vifaa hivyo, 248 vilivyowasili hivi karibuni na 250 vilivyokuwa vinatumika mkoani Njombe, vitatumika kwenye mikoa hiyo kwa pamoja.

Aidha, alisema ratiba ya uandikishaji kwenye mikoa hiyo itatolewa wakati wowote wiki hii ili kuwafanya wananchi wa maeneo husika kujitokeza kwa wingi kushiriki.

Jaji Lubuva alisema Nec ina uhakika wa kuandikisha Watanzania wenye sifa ya kupiga kura katika daftari la kudumu la wapiga kura hadi Julai, mwaka huu na kwamba uchaguzi mkuu ni lazima ufanyike.

Akizungumzia uwezekano wa kugawanywa kwa majimbo na kata za uchaguzi, alisema utaratibu huo ni wa kawaida na unafanyika kila mwaka wa uchaguzi mkuu.

"Kwa sasa tunaangalia maeneo ya utawala wa serikali, mipaka na kujua kama kuna ongezeko la mgawanyo wa maeneo ndipo tuweze kutangaza maeneo mapya ya uchaguzi," alisema.

Alisema kwa sasa wako kwenye mchakato na wakati wowote baada ya kukamilisha watatangaza kama kuna ongezeko la maeneo ya uchaguzi kwa ngazi ya kata na majimbo.

CHANZO: NIPASHE

TANZANIA KUMENYANA NA UGANDA MICHUANO YA CHAN

Tanzania itachuana na Uganda wakati Kenya itakipiga na Ethiopia katika michuano ya kufuzu ya Afrika kwa wachezaji wa ndani (CHAN) kufuatia ratiba ya michuano hiyo iliyotolewa na Shirikisho la mpira wa miguu barani Afrika, (CAF), Mechi hiyo ya awali itachezwa kati ya Juni 19-21 wakati ile ya marudiano itachezwa kati ya July 3-5 mwaka huu.

Fainali za CHAN zitafanyika nchini Rwanda kuanzia January 16 mpaka February 7, 2016.

Michuano hiyo, kwa mujibu wa ratiba ya CAF, itashirikisha timu 42, ambazo zitashindana katika kanda 6 na fainali zake zitachezwa na nchi 16 tu wakiwemo timu mwenyeji.

Uganda kwa sasa ipo nafasi katika nafasi ya 84 ya viwango vya FIFA, wakati Tanzania ipo nafasi ya 100.

Ratiba ya kufuzu ya CHAN ni kama ifuatavyo

Kanda ya Magharibi A.

Guinea Bissau vs Mali

Mauritania vs Sierra Leone

Guinea vs Liberia

Senegal vs Gambia


Kanda ya Magharibi B

Ghana vs Ivory Coast

Nigeria vs Burkina Faso

Niger vs Togo


*Kanda ya kati

DR Congo vs Jamhri ya Kati (CAR)

Cameroon vs Congo

Chad vs Gabon


*Kanda ya Kati Mashariki Hatua ya awali

Tanzania vs Uganda

Djibouti vs Burundi

Ethiopia vs Kenya


*Kanda ya Kusini

Zimbabwe vs Visiwa vya Comoro

Lesotho vs Botswana

Namibia vs Zambia

Msumbiji vs Seychelles

Afrika ya Kusini vs Mauritius

Swaziland vs Angola


*Kanda ya Kaskazini

Libya vs Tunisia

Morocco vs Libya

MARUBANI WAZIKUNJA KWENYE CHUMBA CHA KUONGOZEA NDEGE

Katika hali isiyokuwa ya kawaida, wakati dunia bado ikiwa na kumbukumbu mbaya ya ndege yashirika la ndege la Ujerumani na vifo vya abiria 150 ndaniye,kituko kingine kimegubika tasnia ya urubani baada ya marubani wawili kuondolewa kwenye zamu ya urushaji ndege kufuatia madai yawawili hao kuzikunja katika chumba cha kuongozea ndege.

Marubani hao hurusha ndege za shirika la ndege la India, Air India walishushwa katika ndege yao baada ya rubani msaidizi kumshambulia captain wake ama nimwite rubani kiongozi.

Hata hivyo ili kulinda hadhi ya shirika la ndege la India, maafisa wa juu wa shirika hilo walidai kuwa marubani hao wawili walirushiana maneno na hawakuingiana mwilini.

Msemaji wa shirika hilo la ndege amedai kwamba marubani hao wawili wote waliondolewa kwenye zamu zao na maswali tele yaligubika msuguano wa marubani hao,na kitengo cha nidhamu cha shirika hilo la ndege kilipewa jukumu mara moja kuwaketisha marubani hao kujua chanzo cha sintofahamu hiyo na hatimaye kuyamaliza.

Lakini askari wa ngazi za juu nchini India wamedai kwamba chanzo cha mzozo huo kilianzia pale Rubani kiongozi alipomtaka rubani msaidizi kurekodi mwenendo wa ndege hiyo ikiwemo idadi ya abiria waliokuwemo kwenye ndege hiyo kabla haijaanza safari yake.

Ndege hiyo inadaiwa ilikuwa ifanye safari kutoka Delhi kuelekea Jaipur na baada ya kutua salama wafanyakazi wa ndege hiyo waliarifiwa juu ya tukio hilo.

Tukio hili limekuja siku chache tubaada ya rubani wa shirikisho la ndege za kukodi nchini India kumuandikia waraka mkurugenzi kuu wa mamlaka ya anga nchini humo akielezea msongo wa mawazo unavyowatesa marubani.

Katika barua hiyo rubani huyo alielezea namna marubani wanavyozongwa na mambo na chanzo ni mishahara midogo, masuala ya kifamilia, hayo ndo baadhi aya vyanzo vya matatizo yanayozonga vyumba vya marubani.

Kwa taratibu za mamla za anga rubani anapaswa kuwa mtulivu kwa namna yoyote,na inawezekanaje rubani wa shirika la ndege la India afanye kazi wakati akiwa amevurugwa?

RADI YAPIGA KANISANI, YAUA WATANO

Watu watano wamefariki dunia papo hapo katika kijiji cha Shilabela, kata ya Bwanga, wilayani Chato, mkoa wa Geita, baada ya kupigwa na radi wakati wakiendelea na ibadaya Sikukuu ya Pasaka.

Tukio hilo lilitokea juzi jioni kwenye Kanisa la Assemblies of God Tanzania (AGT) na kujeruhi watu wengine 18 wakati wakiwa kwenye maadhimisho ya sikukuu ya kufufuka kwa Yesu Kristo, Pasaka. Kati ya majeruhi hao, wanne wamelazwa katika Zahanati ya Bwanga, wilayani Chato.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Geita, Joseph Konyo, akizungumza na NIPASHE jana, alithibitisha kutokea kwa tukio hilo na kuwataja waliofariki ni Daud Merdad (20), Daud Lazaro (20), Saimon Marco (15), Haile Shija (20) na Monica Sumuni (19).

Kamanda Konyo aliwataja majeruhi watatu waliolazwa Zahanati ya Bwanga ni Mabula Mathias (8), Fabian Ezekiel (10) na Edina Leonard (21).

Mganga Mfawidhi wa zahanati hiyo, Deogratias John, alisema majeruhi 18 walipokelewa katika zahanati hiyo, lakini 14 walitibiwa na kuruhusiwa kurejea nyumbani baada ya hali zao kutengemaa.

Akizungumzia tukio hilo, Diwani wa kata hiyo, Mahobe Chiza, alisema nikubwa na la aina yake lililotokea wakati wananchi hao wakisherehekea sikukuu ya Pasaka.

"Walikuwa katika sikukuu ya Pasaka, lakini bahati mbaya mvua iliyokuwa ikinyesha ilisababisha radi kupiga nakuwadhuru waumini hao," alisema Chiza.

Naye Mchungaji wa kanisa hilo, Deus Mhangwa, alisema kanisa lake limepata msiba mkubwa wakati wa maadhimisho ya sikukuu ya Pasaka, ambayo ni siku ya kukumbuka kufufuka kwa Yesu Kristo baada ya kusulubiwa msalabani.

"Kila nafsi itaonja mauti, lakini tukio hili limewaachia simanzi kubwa waumini wa kanisa pamoja na wananchi kutokana na kupotea kwa nguvu kazi ya kanisa na taifa kwa ujumla," alisema Mchungaji Mhangwa.

CHANZO: NIPASHE

SHAMBULIZI LAFANYIKA CHUONI NCHINI KENYA

Takriban watu sita wameuawa baada ya watu watano wanaodaiwa kufinika nyuso zao kushambulia chuo kikuu cha Garrissa Kaskazini mashariki mwa Kenya.

Watu hao wanadaiwa kuingia katika taasisi hiyo mwendo wa saa kumi asubuhi wakati ambapo waislamu walikuwa wakifanya sala yao ya alfajiri.
Hatahivyo maafisa wa polisi wanasema kuwa shambulizi hilo lilifanyika mwendo wa saa kumi na moja unusu.

Mwandishi wa BBC mjini humo anasema kuwa walinzi wawili waliuawa katika lango la chuo hicho huku maafisa wawili wa polisi waliokuwa wakilinda chuo hicho pamoja na wanafunzi wakijeruhiwa.

Walioshuhudia wanasema kuwa kumekuwa na majeruhi mengi ndani ya chuo hicho.

Mwandishi wetu anasema kuwa wapiganaji hao bado wako ndani ya chuo hicho na wamewateka nyara watu kadhaa.

Jeshi la Kenya KDF ,maafisa wa polisi na magari ya ambulance yamewasili katika eneo la tukio ambapo kumekuwa na ufyatulianaji wa risasi.

Jeshi la Kenya KDF ,maafisa wa polisi na amabulansi wamefika katika eneo la tukio na sasa wameingia ndani ya majengo ya chuo hicho ambapo kumekuwa na ufyatulianaji wa risasi kati ya washambuliaji na maafisa wa jeshi.

Wanafunzi 27 wamefanikiwa kutoroka na sasa wako katika kituo kimoja cha kijeshi.

Kufikia sasa hakuna kundi ambalo limekiri kutekeleza shambulizi hilo ijapokuwa kundi la wapiganaji wa Somalia Al Shabaab limeshukiwa kutekeleza shambulizi hilo.

Chuo hicho ndio taasisi ya kipekee ya masomo ya juu katika eneo hilo kilichofunguliwa mwaka 2011 na kiko takriban kilomita 350 kutoka mji mkuu wa Nairobi.

MTIKILA ATAKA MAHAKAMA YA KADHI ISIJADILIWE

Mwenyekiti wa Democratic Party (DP), Mchungaji Christopher Mtikila, ameiomba Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Dar es Salaam, kutoa amri kwa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kusitisha kujadili suala lolote linalohusu kuanzishwa kwa Mahakama ya Kadhi.

Mtikila aliwasilisha maombi yake jana mbele ya jopo la majaji watatu likiongozwa na Mwenyekiti, Jaji Richard Mziray, anayesaidiana na Jaji Lawrence Kaduri na Said Kihio.

Kesi ya msingi ambayo Mtikila anaomba Mahakama ya Kadhi isiruhusiwe nchini, ilipangwa kutajwa jana.

Upande wa Jamhuri uliongozwa na Mawakili wa Serikali Wakuu, Gabriel Malata na Kasori Sarakikya, ulidai kuwa utawasilisha majibu ya maombi ya Mtikila leo.

Mtikila alidai kuwa anaomba kuwasilisha hati ya dharura mahakamani akitaka bunge hilo lisijadili wala kuzungumzia suala la Mahakama ya Kadhi.

"Ina maana suala hili baada ya kufunguliwa mahakamani linajadiliwa huko nje ya Mahakama?," alihoji Jaji Mziray na kuitikiwa na Mtikila.

Jopo hilo lilisema upande wa Jamhuri uwasilishe majibu ya maombi ya Mtikila kwa njia ya maandishi leo na kesho kesi hiyo itatajwa.

Mtikila alifungua kesi ya madai kupinga kitendo cha serikali kupeleka muswada bungeni wa kutunga sheria ya kuanzishwa kwa Mahakama ya Kadhi, kwamba kuanzishwa kwake ni kinyume cha Katiba ya nchi.


Mtikila ameiomba Mahakama itoe amri kwamba wale walio kwenye mamlaka ya serikali akiwamo Waziri Mkuu, Mizengo Pinda; Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Mahusiano naUratibu), Mary Nagu; Waziri wa Katiba na Sheria, Dk. Asha-Rose Migiro; Mwanasheria Mkuu wa Serikali, George Masaju na Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika, Stephen Wasira na wenzao, watoe sababu kwa nini wasifungwe kifungo kisichopungua miaka mitano ikiwa watashindwa kujieleza.

Pia, Mtikila kupitia hati yake ya madai iliyopewa usajili namba 14 yamwaka huu, ameomba Mahakama itoe amri ya vigogo hao kufungwa kifungo hicho kutokana na kuchezea Katiba ambayo ni sheria mama ya nchi.

Katika hati yake, Mtikila pia anaiomba Mahakama itoe amri kwamba Mahakama ya Kadhi na Jumuia ya Kimataifa ya Kiislamu (OIC), itangaze kuwa ni haramu kwenye ardhi ya Tanzania.

Pamoja na mambo mengine, Mtikila anadai kuwa suala la serikali kuandaa Muswada wa Kiislamu na kuuwasilisha bungeni na kitendo cha Bunge kukubali zaidi ya kuukataa ni sawa na uhaini, kinachofanywa na waliopanga kuupeleka muswada huo bungeni.

Anaendelea kudai kuwa kitendo hicho ni sawa na uvunjifu mkubwa wa viapo vya viongozi hao walivyoapa wakati wa kushika nafasiza uongozi wa umma na ni kinyume cha kifungu cha 19 cha Katiba ya nchi kinachoeleza kwamba masuala ya dini na kuabudu yatakuwa ni ya mtu binafsi na kuongeza kuwa uendeshaji wa mambo au taasisi za kidini hazitakuwa sehemu ya mamlaka ya nchi.

CHANZO: NIPASHE

MSHINDI WA URAIS KUTANGAZWA

Mwenyekiti wa Tume Huru ya Uchaguzi nchini Nigeria INEC, Attahiru Jega, amesema kuna uwezekano wa kumtangaza mshindi wa uchaguzi wa rais nchini humo ifikapo leo jioni kama zoezi la kuhesabu kura litamalizika mapema.

Jega amesema kuwa jumuiya ya kimataifa inaweza kuipongeza Nigeria jinsi ilivyoendesha uchaguzi mkuu.

"Tuna amini zoezi la kupiga kura limeenda vizuri ingawa kumekuwepo na changamoto mbalimbali lakini hatuwezi kuzipuuzia.
Ni hakika haukuwa muda kamilifu lakini tunaaminikwa ujumla tumefanya vizuri, japokuwa bado tunayo nafasi ya kuzidi kuboresha upigaji kura. Ndiyo maana tuliwaalika waangalizi vikiwemo vyombo vya habari na waangalizi wengine wa uchaguzi, ili kuweza kutangaza habari za uchaguzi na tunaweza kujifunza kutokana na ripoti zitakazotolewa na vyombo hivi pia tunaweza kuendelea kuboresha mchakato wa uchaguzi", amesema Jega.

Upigaji kura umeendelea kwa siku mbili kutokana na kutokea hitilafu katika kadi za kielektroniki na kuchelewesha usajili kwa baadhi ya wapiga kura.

Matokeo ya awali yamepangwa kutangazwa ndani ya saa 48 baada ya uchaguzi.

15 MBARONI JARIBIO LA KUMTOROSHA GWAJIMA

JESHI la Polisi linawashikilia na kuwahoji watu 15 kwa tuhuma za kutaka kumtorosha kutoka Hospitaliya TMJ Askofu wa Kanisa la Ufufuo na Uzima lililopo jijini, Dar es Salaam, Joseph Gwajima aliyelazwa hapo tangu usiku wa kuamkia juzi.

Gwajima amelazwa ikielezwa hali yake ilibadilika wakati akihojiwa na makachero wa Polisi waliokuwa wanamhoji baada ya kujisalimisha baada ya kutakiwa kufanya hivyo kutokana na kufunguliwa jalada la malalamiko ya kumkashifu Askofu Mkuu wa Kanisa Katoliki, Jimbo Kuu la Dar es Salaam, Mwadhama Kardinali Polycarp Pengo.

Kukamatwa kwa watu hao, wakiwemo wachungaji sita, mhadhiri mmoja wa Chuo Kikuu chaDar es Salaam (UDSM) na mwanafunzi wa udaktari katika Chuo Kikuu cha Kimataifa cha Matibabu na Teknolojia (IMTU), Dar es Salaam kumethibitishwa na taarifa ya Kamishna wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Suleiman Kova.

Katika taarifa yake, amesema watu hao wanatuhumiwa kwa makosa ya kula njama pamoja na kujaribu kumtorosha Askofu Gwajima ambaye amelazwa katika Hospitali ya TMJ kwa matibabu.

Alisema saa tisa na nusu usiku wa kuamkia jana, watu 15 walifika hospitalini hapo kwa lengo la kumuona mgonjwa huyo.

"Askari ambao wapo katika lindo hilo waliwatilia mashaka watu hao hivyo waliwakatalia kuingia. Na hapo walijaribu kutumia nguvu, lakini walikamatwa," alisema.

Kova alisema baada ya kuwapekua, watu hao walikutwa na begi lenye bastola aina ya BERRETA yenye namba CAT5802 ikiwa na risasi tatu, risasi 17 za Short gun na vitabu viwili vya hundi.

Alisema begi hilo pia lilikuwa na hati ya kusafiria yenye jina la Gwajima Joseph Mathias yenye namba AB 544809, kitabu cha hundicha Benki ya Equity, nyaraka mbalimbali za kampuni ya PUMA, chaja ya Simu na Tablets, suti mbili na nguo za ndani.

Aliwataja waliokamatwa ni Chitama Mwakibambo (32), fundi seremala mkazi wa Gongo la Mboto, Mchungaji Edwin Audex (24) mkazi wa Kawe Maringo, Adam Mwaselele(29), mhandisi na mkazi wa Kawe Maringo, Frederick Fusi (25) mkazi wa Mbezi Beach.

Wengine mwanafunzi wa chuo cha IMTU, Frank Minja (24) mkazi wa Mbezi Beach, Emmanuel Ngwela (28) mkazi wa Keko juu ambaye ni mlinzi shirikishi, Geofrey William (30), Mhadhiri UDSM mkazi wa Survey Chuo Kikuu, Mchungaji Mathew Nyangusi (62) mkazi wa Mtoni Kijichi, mchungaji Boniface Nyakyoma (30) mkazi wa Kitunda.

Pia wametajwa Geofrey Andrew (31), dereva mkazi wa Kimara Baruti, Mchungaji David Mgongolo (24) mkazi wa Ubungo Makoka, Mfanyabiashara George Msava (45) mkazi wa Ilala Boma, Mchungaji Nicholaus Patrick (60) mkazi wa Mbagala Mission, George Kiwia (37) ambaye ni dalali wa magari na mkazi wa Tandale Uzuri na mchungaji Yekonia Bihagaze (39) mkazi wa Kimara Stop Over.

Kova alisema upelelezi wa shauri hilo unaendelea kwa madhumuni yakubaini sababu za njama hizo sambamba na kujua mbinu zote zilizotumika kutaka kufanikisha jaribio la kumtorosha Askofu Gwajima.


Pengo Asamehe

Wakati hayo yakiendelea, jana Pengo aliwatangazia waumini wake kumsamehe Gwajima na pia kuwataka waumini wake pia wamsamehe.

Akizungumza katika Kanisa Katoliki la Mtakatifu Joseph ambako iliendeshwa misa ya Jumapili ya Matawi, alitoa msamaha kwa Gwajima na kusema kuwa hana chuki na mtu yeyote.

Aidha, Pengo alisema hawezi kuingilia hatua ya Polisi kumhoji kiongozi huyo wa Kanisa la Ufufuo na Uzima.

Gwajima: Niombeeni Aidha, katika Kanisa la Ufufuo na Uzima, Askofu Gwajima amewaomba waumini wake wamuombee kwa Mungu apone haraka ili aweze kuendelea na kazi aliyotumwa na Mungu ya kuhubiri Injili.

Taarifa iliyotolewa na kusomwa kanisani kwake imedai kuwa kiongozi huyo anaendelea vizuri na afya yake imeanza kuimarika. Alisema waumini wake wamuombee kwa Mungu apone haraka ili kuendelea na kazi aliyotumwa na Mungu ya kuhubiri injili.Kiongozi huyo bado amelazwa kwenye chumba cha wagonjwa mahututi katika hospitali ya TMJ iliyopo Mikocheni jijini Dar es Salaam na anaendelea kupatiwa matibabu ya karibu na madaktari kutokana na hali yake kubadilika mara kwa mara.

Hata hivyo, kwa taarifa iliyotolewa na daktari anayemtibu askofu Gwajima, Fortunatus Mazigo, alisema hali ya mgonjwa inaendelea vizuri japokuwa alikataa kusema ni nini tatizo linalomsumbua hadi akamilishe kukusanya taarifa ya vipimo vyote ambavyo vingine bado majibu yake hayajapatikana na huenda kila kitu kikawa hadharani leo.

Chanzo:Habari Leo

BABA AWABAKA MABINTI ZAKE

Mkazi mmoja wa Miembe Saba wilayani Kibaha mkoani Pwani amekamatwa na polisi akituhumiwa kuwabaka watoto wake wawili wadogo kwa zaidi ya miaka miwili sasa.

Habari zilizolifikia gazeti hili, zilisema kuwa katika tukio hilo ambalo limethibitishwa na polisi na watoto wenyewe, baba huyo alianza kuwafanyia binti zake vitendo hivyo mwaka 2013 kwa siku ambazo mkewe ambaye nimama wa wasichana hao hakuwapo hadi usiku wa Machi 19, mwaka huu. Kwa sasa tunayahifadhi majina ya familia hiyo.

Watoto hao mmoja mwenye umri wa miaka 15 anayesoma darasa la saba na mdogo wake mwenye umri wa miaka 11 aliyeanza kubakwa akiwa darasala tatu.

Kwa mujibu wa watoto hao, baba huyo alikuwa anamuita mmoja wa watoto wake chumbani kwake na kumtaka alale na mdogo wao wa kiume wakati huo akiwa na mwaka mmoja na binti akipitiwa na usingizi humvua nguo za ndani na kumwingilia huku akimtaka kukaa kimya na kuvumilia maumivu.

Mke wa mtuhumiwa huyo, ambaye amekuwa akizimia mara kwa mara kutokana na kulia baada ya kubaini mchezo huo, alisema aligundua watoto wake wanabakwa Ijumaa iliyopita baada ya mmoja wa mabinti zake hao kumweleza kuwa baba yake alikuwa amembaka Machi 19, mwaka huu.

Alisema kabla ya binti huyo kumweleza hivyo, alimwomba asimpige kwani kuna kitu anataka amweleze, japo ni kibaya lakini yeye amechoshwa na kimekuwa kikimuumiza kichwa.

"Alisema kila ninapokwenda katika biashara zangu, anatamani nisiwe ninawaacha hapo, nikamwahidi sitamfanya kitu ili mradi aseme ukweli tu," alisema mama huyo.

Baada ya kuhakikishiwa kulindwa, ndipo binti huyo aliposimulia jinsi ambavyo baba yake amekuwa akiwafanyia na kuwatishia wakipiga kelele atawaua.

"Niliposikia mwili ulisisimka na ghafla binti yangu mwingine naye akatokea akilia na kuniambia, 'hata mimi baba ananifanyiaga hivyohivyo kila siku unapokuwa umepeleka mboga sokoni Kariakoo," alisema mama huyo.

Mwanamke huyo ameomba sheria ichukue nafasi yake katika tukio hilo kwa kuwa ni la kinyama na pia wataalamu wa saikolojia wamsaidie binti yake mdogo wa darasa la tano kwani yeye ameathirika zaidi.

Daktari aliyewapima watoto hao, ameshauri binti huyo mdogo apate ushauri zaidi ili kurudisha akili yake katika hali ya kawaida.


Simulizi za watoto

Wakizungumza nyumbani kwao jana watoto hao, walisema babayao alikuwa akiwatishia kuwakatakata kwa panga au kuwakaba koo humohumo chumbani endapo wangethubutu kumweleza mtu yeyote kitendo wanachokifanya.

"Tulikuwa tumeingia kwetu kulala na wadogo zangu, nikasikia ananiita nikambembeleze mtoto eti anamsumbua, nilikwenda nikambembeleza akalala, wakati nashuka kitandani kurudichumbani kwetu baba akanivutakwake akanivua, akasema anachokifanya ni suna kwa hiyo hataki kelele, akisikia atanikaba nife."

"Niliumia sana na asubuhi mama alirudi nikajitahidi kweli asijue na hata shule sikwenda, jioni mama aliondoka tena baba hakuniita siku hiyo lakini baada ya siku tatu aliniita tena ikawa vilevile navumilia. Siku zilivyozidi unaweza kukuta kwa wiki naitwa hata mara nne siku ambazo mama hayupo nyumbani," alisema.

Watoto hao walieleza kuwa baadaye baba huyo alihamia kwa binti mdogo kwa staili ileilena kila mmoja alikuwa akiitwa kwa zamu na kwa vile kila mmoja alijua ni siri yake na baba. Kutonaka na woga wa kuuawa, hakuna aliyemweleza mwenzake hadi katikati ya mwaka jana mmoja wao alipomweleza mwenzake na baadaye kumweleza mama yao.

"Baba alikuwa anasema atatuua bila hata mtu kujua na tutaozea shambani, hata nikiwa katika siku zangu baba ananiingilia hivyohivyo, naugua kila mara UTI, mdogo wangu naye kila mara UTI, tukaamua liwalo na liwe kama kufa basi ila mama ajue," alisema mtoto huyo huku akibubujikwa na machozi.

Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa wa Miembe Saba, Hamis Shomari alisema kabla ya kupelekwa kituo cha polisi Kongowe Jumamosi iliyopita, watoto hao waliitwa shuleni hapo na kuhojiwa kila mmoja peke yake na wote walikiri kuanza kubakwa mwaka 2013 na baba yao na kwamba tabia hiyo iliendelea hadi Machi 19 usiku alipobakwa binti mdogo kwa mara ya mwisho na Machi 20 walipoamua kumweleza mama yao.

Kamanda wa Polisi mkoani Pwani, Ulrich Matei alisema wanamshikilia mtuhumiwa huyo na kwamba wasichana hao wamefanyiwa vipimo mbalimbali na majibu ya daktari yamethibitisha kuwa wamebakwa na sehemu zao za siri zimeharibiwa, hivyo wanaendelea na matibabu.


Chanzo: Mwananchi

GWAJIMA ASAKWA NA POLISI KWA KUMKASHIFU PENGO

POLISI Kanda Maalumu ya Dar es Salaam wamefungua jalada la uchunguzi dhidi ya tuhuma za Askofu Josephat Gwajima wa Kanisa la Ufufuo na Uzima za tuhuma za kumkashifu Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu la Dar es Salaam la Kanisa Katoliki, Mwadhamana Polycarp Kardinali Pengo.

Taarifa iliyotolewa jana na Kamandawa Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Suleiman Kova ilisema Askofu huyo anatakiwa kujisalimisha Kituo Kikuu cha Polisi, ofisi ya Mkuu wa Upelelezi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam kwa mahojiano.

"Tumepokea malalamiko ya kukashifiwa na kutukanwa hadharani kwa Mwadhama Polycarp Kardinari Pengo ambaye ni kiongoziwa Kanisa Katoliki nchini Tanzania," alidai Kamanda Kova na kuongeza kuwa kashfa na matusi hayo, yamefanyika kupitia mitandao mbalimbali ya kijamii.

Aidha, alidai kwamba kuna sauti iliyorekodiwa (audio) na picha za video (video clip) zikimuonesha Askofu Gwajima akimkashfu na kumtukana Kardinali Pengo katika hali ambayo pia imewaudhi watu wengine.

Alidai taarifa ya kumtaka Askofu Gwajima ajisalimishe haraka, inatokana na juhudi za kawaida ili kumpata kushindikana.

"Ni muhimu kwa Askofu Josephat Gwajima kuripoti yeye mwenyewe badala ya kutafutwa au kukamatwa ili ajibu tuhuma hizo kutokana na nafasi yake katika jamii," ilisema taarifa ya Kamanda huyo.

MBARONI KWA KUKUTWA NA VIUNGO, MIFUPA YA ALBINO

WATU wawili wanashikiliwa na Jeshi la Polisi mkoani Kagera kwa kosa la kukutwa na viungo mbalimbali vya mwili ikiwemo mifupa mitatu ya mtu mwenye ulemavu wa ngozi (albino).

Kamanda wa Polisi mkoani Kagera Henry Mwaibambe alisema kuwa tukio hilo limetokea juzi katika kijijicha Kyota kata ya Kimwani wilayani Muleba mkoani humo baada ya jeshi hilo kuweka mtego kwa watuhumiwa hao ambao walikuwa wanatafuta wateja wa viungo hivyo.

Aliwataja watuhumiwa hao kuwa ni James Rutozi (66) mkazi wa Kimwani ambaye ndiye aliyekuwa anahifadhi viungo hivyo na Emanueli Kaloli (50)ambaye pia ni mkazi wa Kimwani aliyekuwa anatafuta mteja wa viungo hivyo.

Alisema mara baada ya kupata taarifa kuwa kuna watu wanauza viungo hivyo kwa Sh milioni 3 waliweka pesa za mitego na kujifanya wao ni wateja na ndipo walipowakamata watuhumiwa hao wawili ambao walikutwa na mfupa mmoja na walipowabana zaidi ndipo walitoa mifupa miwili.

Alisema mnamo mwaka 2006 katikakijiji cha Rushwa kata ya Mushabago wilayani Muleba, Zeulia Jestus akiwana miaka 24 mwenye ulemavu wa ngozi (albino) alifariki dunia muda mfupi baada ya kujifungua na ndipo watuhumiwa hao walifukua kaburi hilo mwaka 2008 kwa maelekezo ya mganga wa jadi.

Alisema pia walipotaka kujiridhisha jeshi hilo liliomba kibali mahakamani ili kufukua kaburi hilo mnamo Machi 23, mwaka huu lilipofukuliwa liligundulika kuwa viungo hivyo vimetolewa katika mwili wa marehemu huyo.

Aidha, jeshi hilo linamtafuta mganga wa jadi aitwaye Mutalemwa Revocatus ambaye ametoroka kabla hajakamatwa ambaye ndiye aliyewashawishi wafukue hilo kaburina kuwapa dawa ya kinga ili wasidhurike wakati wanafukua.

Aliongeza kuwa mnamo mwaka 2008 wananchi wa kata hiyo ya Mushabago walitoa taarifa kwa Jeshila Polisi kuwa kaburi alilozikwa marehemu Zeulia lilifukuliwa na watu wasiojulikana baada ya kugundua tukio hilo.

CCM WAMUONYA TENA LOWASSA

CHAMA Cha Mapinduzi (CCM), kimesema vitendo vinavyofanywa na Mbunge wa Monduli na Waziri Mkuu wa zamani Edward Lowassa niukiukwaji wa Katiba na kanuni za chama hicho.

Aidha, kimesema vitendo vinavyofanywa na Lowassa ni kampeni za wazi za urais anazoendesha kabla ya muda kufikana hivyo kukiuka Katiba na kanuni za CCM na kuonya kuwa kama ataendelea na kampeni hizo haramu atapoteza sifa za kugombea nafasi ya urais.

Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye alitoa ufafanuzi huo baada ya waandishi wa habari waliopo katika msafara wa Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinanakutaka ufafanuzi wa kinachoendelea mjini Dodoma kwa makundi tofauti kwenda kwa Lowassa kwa madai ya kumshawishi agombee urais katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka huu.

Nape akizungumzia suala hilo alisema, "Anachokifanya Lowasa ni kuvunja kanuni na kiburi, ni matendo ya wazi ya kampeni, bila shaka anajua adhabu yake. Matendohayo yanaweza kumpotezea sifa za kuwa mgombea kupitia CCM.

"Katibu huyo wa Itikadi na Uenezi CCM Taifa aliongeza kuwa Lowassa ni miongoni mwa wanaCCM ambao walipewa adhabu na CCM mwaka mmoja uliopita kwa kuanza kampeni kabla ya wakati na mpaka sasa bado wapo kwenye kipindi cha uangalizi wakati vikao husika vikiendelea na tathmini dhidi yao. Nape alisisitiza kuwa matendo yanayoendelea hivi sasa ni dhahiri kuwa ni kiburi kisicho na maana dhidi ya CCM."

Lowasa anajua utaratibu wa Chama katika kuwapata wagombea wake kwa ngazi mbalimbali kuanzia udiwani mpaka urais hivyo kuendelea na matendo ambayo yanatafsiri ya wazi kuwa ni kampenini kiburi cha wazi. "Kwa matendo hayo ya Lowassa labda dhamira iwe ni kuomba ridhaa ya kuwania nafasi ya Urais kupitia chama kingine na si CCM."

Nape alisema ni vyema wagombea wa ngazi mbalimbali wakahakikisha wanazingatia Katiba na kanuni za chama hicho ili wasiingie kwenye kundi la kutokuwa na sifa ya kuomba ridhaa ya kugombea udiwani, ubunge na urais.

"Tunaendelea kukumbusha na kusisitiza kwamba wale wote wenyenia ya kugombea kupitia chama chetu kuheshimu kanuni na tararibu za kupata ridhaa kugombea kwa ngazi ya chama chetu," alisema Nape.

Lowassa amedaiwa kuwa amekuwa akitumia makundi mbalimbali kufanya kampeni ambapo alianza nakikundi cha wajasiriamali jimboni Monduli mkoani Arusha ambapo walienda nyumbani kwake kumuomba agombee.

Hatua hiyo ilifuatiwa na mashehe 50 kutoka wilaya ya Bagamoyo mkoani Pwani ambao nao walikwenda nyumbani kwa Lowassa Dodoma kwa lengo la kumshawishi agombee urais.

Baadaye walifuata wachungaji ambao nao walifunga safari hadi nyumbani kwa Lowassa Dodoma na kusema wameamua kumuomba Lowassa agombee urais kwa madai kuwa ana maono makubwa dhidi ya Tanzania.

Baadhi ya wachungaji hao walimwambia Lowassa wanaamini kuwa yeye ndio chaguo sahihi kwao na ndio maana wameamua kufunga safari na kumshawishi huku wakieleza kuwa kila mtu ametumia nauli yake kufika Dodoma.

Kwa upande wake Lowassa, akizungumza na wachungaji hao waliofika nyumbani kwake, alisema anafarijika kuona makundi mbalimbali yakifika nyumbani kwake kumshawishi agombee.

Alinukuliwa na vyombo vya habari juzi akisema pia kuwa hakuna kundi ambalo analituma au kulipa fedha kwa ajili ya harakati za kutaka kugombea urais.

Hata hivyo, tayari baadhi ya makadawa CCM ambao wamo kwenye orodha ya kutaka kugombea urais, wametoa malalamiko yao kuwa kinachofanywa na Lowassa si sahihi.

Naibu Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, January Makamba alisema kuwa kitendo chakuandaa watu kwa ajili ya kuanza kampeni si cha kiungwana na kwamba kila mgombea anaweza kufanya hivyo, lakini wanaheshimu kanuni na Katiba za chama chao.

January amenukuliwa kwenye vyombo mbalimbali vya habari na mitandao ya kijamii akieleza wazi kuwa anaweza kutengeneza makundi kwa ajili ya kuonesha Watanzania kuwa anahitajika, lakini akasema hizo ni propaganda ambazo hazina tija kwa Taifa.

"Kama mgombea anakubalika kwa Watanzania kwanini atumie fedha nyingi kutafuta makundi ili aonekane anakubalika? Alihoji January katika ujumbe wake aliousambaza katika mitandao mbalimbali ya kijamii.

LOWASSA AMPUUZA JANUARY

Mbunge wa Monduli (CCM), Edward Lowassa, amesema watu wanaosema anawalipa watu wanaomshawishi awanie nafasi ya urais kwenye uchaguzi mkuu ujao, ni upuuzi na uongo na kwamba hawezi kuwajibu kwani kufanya hivyo ni kuwapa sifa wasizostahili.

Lowassa aliyasema hayo nyumbani kwake jana mjini hapa, kufuatia baadhi ya vyombo vya habari, kumnukuu Naibu Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, January Makamba, ambaye ametangaza nia ya kuwania urais, akisema baadhi ya watu wanatumia vibaya umaskini wa Watanzania kwa kuwakusanya na kuwapa fedha ili waseme wanawashawishi wawanie urais.

Akizungumza mbele ya wachungaji 110 wa makanisa ya Kipentekoste kutoka sehemu mbalimbali nchini jana, Lowassa alisema hana uwezo wala sababu ya kuwagharimia watu wanaofika nyumbani kwake kumshawishi na kwamba wengi wanafanya hivyo kwa mapenzi yao na Mungu wao.

"Najiunga na mwenzangu (Mwenyekiti wa CCM Shinyanga, Khamis Mgeja) kusema leo (jana) kuna mtu kwenye magazeti amesema maneno ya hovyo hovyo kidogo, ambaye nikimjibu nitakuwa nampa heshima kwa hiyo nampuuza, sina uwezo wa kuwagharamia watu wote hawa waje nyumbani kwangu na wala sina sababu," alisema.

Alisema makundi yanayomshawishi awanie nafasi hiyo wanafanya hivyo kwa utashi wao, mapenzi yao kwa taifa na Mungu wao na kwamba 'lugha nyingine tofauti ni upuuzi tu na uongo.

'Awali, Mgeja alisema watu wanaosema kuwa wanaofika nyumbani kwa Lowassa wanalipwa, ni walioishiwa hoja, wamefilisika na sasa wanatapatapa na kwamba kuwajibu watu hao ni kuwapa sifa wasizostahili kwani baadhi yao wanahitaji muda mrefu wa kujifunza siasa.

"Nimekaa muda mrefu kwenye siasa, wengine bado wanahitaji wapate muda wa kujifunza na katikasiasa hatuwajui ni wapi walipotokea,wakipata muda mzuri wajifunze, wawe na adabu, watulie kuliko kuzusha maneno ambayo huna uhakika nayo, ambayo ni dhambi kubwa sana," alisema Mgeja. Alisema wakati wa sherehe za miaka 38 ya CCM mkoani Ruvuma, Mwenyekiti wa chama hicho, Rais Jakaya Kikwete alitoa rai kuomba wananchi na wana CCM wakiona mtu anayefaa kuwa kiongozi wamshawishi, hivyo wanachokifanya siyo makosa.

"Tusihukumiane kwenye hili, Mgeja na wengine wamefika nyumbani kumshawishi, ndivyo tulivyoombwa kwamba tukiona ana uwezo tumshawishi, mpeni nguvu, mjengeni suala hili ni kubwa linahitaji dua na maombi.
Kama viongozi tumeona kwa maana tunafahamiana, nani anafaa kupokea kijiti na kutupeleka mbele,niungane na Watanzania wenzangu na mimi kusema tunaona kwamba hakuna mwingine zaidi ila Mheshimiwa Lowasa," alisema Mgeja.

Aidha, Lowassa alizungumzia ujio wa wachungaji hao nyumbani kwakejana, akieleza kuwa umeandika historia katika maisha yake kwani hakutegemea kupokea kundi kubwakama hilo la watumishi wa Mungu.

Alisema watu ambao wamemfuata kumshawishi amewaambia kuwa nafasi ya urais ni kubwa na inahitaji maombi.

"Ninachoomba wachungaji mmekuja nawashukuruni sana, mkapige magoti mpaka yachubuke, hatimaye niweze kusema nayaweza yote katika yeye anitiaye nguvu," alisema.

Mapema, Mratibu wa ujio wa Wachungaji hao, Mchungaji Benedickto Kamzee, kutoka Kanisa la Glory of Christ la Katavi, alisema wamefikia uamuzi huo bila kushinikizwa wala kushawishiwa na mtu yeyote.

"Hakuna aliyetushawishi, hata siyo maaskofu wetu, hili suala halina msukumo wowote zaidi ya msukumo wa Mungu," alisema.

Kamzee alisema wachungaji hao wanatoka kwenye madhehebu ya EAGT, TAG, PEFA na KLPT kutoka maeneo mbalimbali nchini.

Wachungaji hao waliingia nyumbani kwa Lowassa wakiwa na mabango yaliyoonyesha maeneo waliyotoka.

Maeneo hayo ni pamoja na Meatu, Makete, Karatu, Busega, Bariadi, Bukombe, Igunga, Chakechake, Mafia, Karagwe, Nachingwea, Temeke, Kinondoni, Rombo, Monduli, Kilwa, Mkuranga Kasulu na Bunda.

Wengine wanatoka Handeni, Ngara, Iramba, Mpanda, Bagamoyo, Same, Masasi, Kibondo, Kilombero, Rungwe, Mwibara, Kisarawe, Nachingwea na Kilolo.


WANAFUNZI, WAFANYABIASHARA WANENA

Wakati huo huo, wanafunzi wa vyuo vikuu na wafanyabiashara mjini hapa waliokwenda kwa Lowassa juzi kumshawishi agombee, wamesema kwa Lowassa hakukuwa na ubwabwa wala soda na kwamba kauli ya Makamba inaonyesha kuwa Lowassani kiongozi anayefaa ndio maana watu wanampinga.

Rais wa Kitivo cha Imformative katika Chuo Kikuu cha Dodoma, Goodluck Philip, alisema wanafunzi walikwenda kwa Lowassa kwa utashi binafsi na bila shinikizo na kwamba kauli ya kuhongwa imewadhalilisha.

Alisema kauli hizo zinalenga kuwatisha watu wakati msingi wa kufanya hivyo ni wa kidemokrasia.

Naye mwenyekiti wa wafanyabiashara mjini Dodoma, Norbati Pangaselo, alisema wapinzani wa Lowassa wanatakiwa kujenga hoja badala ya kuzusha uongo kwa nia ya kumchafua.


WAZAZI WAJA JUU

Mbio za uchaguzi wa urais zimeanza kukichanganya CCM, kufuatia Jumuiya ya Wazazi kutoa tamko kali la kutaka kuwachukulia hatua wenyeviti na makatibu wa mikoa wa jumuiya hiyo na wajumbe wa Baraza Kuu la Jumuiya waliokwenda nyumbani kwa Lowassa kumshawishi agombee urais mwakahuu na kumpatia Sh. 600,000 wakidai ni kwa niaba ya baraza hilo.

Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi Taifa, Abdallah Bulembo, akizungumza na waandishi wa habari jana mjini Dodoma, alisema CCM ina maadili na taratibu zake kwa wanachama wanaotaka kugombea urais mwaka huu.

"Viongozi 20 wa jumuiya waliokwenda kwa mgombea mmoja(Lowassa), wakae kwenye vyombo vya habari wakanushe hawakwenda kwa niaba ya Jumuiya ya Wazazi ndani ya mwezi huu na kwamba kukanusha huko hakuzii kuwahoji kwenye kikao cha maadili" alisema Bulembo.

Alisema vikao vya maadili vya jumuiya hiyo vitakaa kuwajadili na wakibainika kufanya makosa wanaweza kuchukuliwa hatua ambao ni pamoja na kufungiwa uanachama miezi sita, 12 na 18 au kufukuzwa kabisa uanachama.

Kwa mujibu wa kanuni ya Jumuiya ya Wazazi toleo la Mwaka 2008 kifungu cha 83 Ibara ndogo ya 11, Baraza la Wazazi Taifa litakuwa na uwezo wa kumfukuza au kumsimamisha uongozi kiongozi yeyote ambaye uongozi wake huteuliwa na Umoja wa Wazazi.

Bulembo alisema viongozi watakaojadiliwa na ikibainika wamekiuka kanuni watakumbwa na adhabu hiyo ni wenyeviti wa wazazi mkoa wa Kilimanjaro, Simiyu, Mwanza, Mbeya , Morogoro, Shinyanga, Kusini Unguja na Mkoa wa Mara.
Wajumbe wa Baraza Kuu watakaojadiliwa ni kutoka mkoa wa Tanga, Mbeya, Dodoma, Ruvuma namkoa wa Njombe wakati Makatibu wa Jumuiya wanatoka mikoa ya Kusini Unguja, Morogoro na Shinyanga.

Alisema siyo kosa kwa kiongozi au mwanachama yeyote kuonyesha mapenzi kwa mtu yeyote anayetaka kugombea urais, lakini taasisi ya chama haiwezi kuwa na mgombea wake itakuwa imekosa sifa.

"CCM ina jumuiya tatu, Jumuiya ya Vijana, Wazazi na Wanawake, jumuiya mojawapo inaposema ina muunga mkono mgombea fulani haifai kubaki tena katika CCM kwa sababu kazi ya jumuiya hizi ni kufanya kazi za chama kutegemeana na maelekezo," alisema.

Alisema unapozungumzia taasisi ambayo ni Jumuiya ya Wazazi yenye wanachama zaidi ya 2,300,000 Tanzania nzima, hivyo anapotokea kiongozi mmoja anasema anazungumza kwa niaba ya wanachama hao ni hatari na anavunja maadili ya chama ambacho hakiruhusu taasisi kujihusisha na mgombea yeyote.

Bulembo alisema CCM itatoa mgombea wake baada ya mkutano mkuu kwa kazingatia vikao vya chama, hivyo wale wote waliokwenda kwa Lowassa watachukuliwa hatua kwa kuitumia jumuiya kwa matakwa yao .

"Lakini hawa wagombea urais napenda niwaase, kama wanataka kugombea ndani ya CCM wafuate taratibu za chama na kusoma vitabu vinavyoelezea miiko ya chama, lakini unakuta mgombea anakusanya watu Mbeya na maeneo mbalimbali jamani anataka nini?" alihoji.


CHANZO: NIPASHE