UKAWA WABADILIKA

VIONGOZI wanaounda kile kinachoitwa Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa), wamesema hawako tayari kushiriki Uchaguzi Mkuu ujao wa mwaka kesho huku nchi ikiwa na Katiba ya zamani, hivyo keshokutwa wanatarajiwa kuingia katika mazungumzo kunusuru mchakato mzima wa Katiba.

Wameeleza kuwa, kwa kutambua muda mfupi uliobaki kati ya mchakato wa Katiba kumalizika na Uchaguzi Mkuu, watafanya mazungumzo hayo kwa faida ya Taifa na wananchi waliojitokeza kwa wingi kuwasihi warejee katika Bunge Maalumu la Katiba linalotarajiwa kurejea kwa siku 60 kuanzia Agosti 5, mwaka huu.

Awamu ya kwanza ya Bunge hilo ilikutana kwa siku 70, lakini kutokana na wajumbe kusigana kwa mambo kadhaa, yakiwemo ya kiitikadi na kutoaminiana, liliahirishwa Aprili 25 mwaka huu ilikupitisha Bunge la Bajeti bila kuwepo na sura ya kukamilika karibuni.


Akizungumza jana jijini Dar es Salaam, mmoja wa viongozi wa umoja huo ambaye ni Mwenyekiti wa Taifa wa Chadema, Freeman Mbowe alisema wana imani kuwa taifa linahitaji Katiba mpya hivyo watajadili katika mazungumzo hayo ya Jumatatu ili kuwawezesha kupatanjia mbadala iwapo mchakato huo utakwama.

Akifungua kikao cha Kamati Kuu ya chama hicho, Mbowe alisema kwa niaba ya uongozi wa Ukawa wanapongeza hatua ya taasisi, viongozi wa dini na watu mbalimbali kuwasihi kurudi katika Bunge la Katiba, na kwamba wako tayari kufanya mazungumzo kuhusukurejea bungeni.


Alisema hata kama kwenye mazungumzo hayo watakubaliana kurejea bungeni na wakiwa katika bunge hilo kutajitokeza maamuzi yakutaka kulivuruga bunge, hawatasitakuchukua hatua kama ya awali.

"Napenda kuwataarifu wananchi kuwa Ukawa tuko tayari kwa mazungumzo kwa nia ya kunusuru mchakato wa Katiba kuendelea kama walivyotusihi watu mbalimbali, lakini tutaenda katika mazungumzo hayo Jumatatu kwa kuhakikisha mchakato huo hautanajisiwa," alisema.


Alidai kuwa wao kama chama cha siasa wamepata habari za ndani zinazodai kuwepo kwa njama za kuvuruga mchakato huo ili kuendelea kutumika kwa Katiba ya zamani, jambo alilodai kuuliza dhamira hizo katika mazungumzo hayo.

"Sisi hatuko tayari kuona uchaguzi ujao unafanyika kwa kutumia Katibaya zamani na tume ya uchaguzi iliyopo, hivyo tutahakikisha tunakwamua hali hii ili mchakato uendelee," alisema Mbowe na kuongeza kuwa, watu mbalimbali wamekuwa wakiwasihi Ukawa kurejea bungeni bila kuzungumza kwa nini waliamua kutoka nje ya bunge na kwanini mchakato huo unatishia kukwama.


Alisema viongozi wa Ukawa wamejadiliana na kufikia maamuzi kuwa hawakatai mazungumzo, bali wanachopinga ni kurudi Bungeni kabla sababu iliyowafanya watoke haijafanyiwa kazi huku akieleza kuwa mwenye mamlaka ya kuokoa mchakato huo ni Rais Jakaya Kikwete.

"Hatuwezi kuwa wanasiasa wa kuzirabali mazungumzo ni kitendo cha uungwana wa kawaida katika uongozi pale inapotokea kutoelewana kwa kuangalia tatizo nakufanyia kazi kwa ajili ya kunusuru mchakato na kurudi katika mchakato," alisema.


Alisema katika mkutano wa awali kujadili jinsi ya kunusuru mchakato huo walikubaliana kila chama kuweka bayana vikwazo vya mchakato ambapo chama tawala na Ukawa kila moja walitoa sababu zao.

Mbowe alisema baada ya kutoa taarifa zao watazijadili katika kikao hicho cha kamati kwa siku mbili, ikiwa ni pamoja na hali ya siasa nchini, mchakato mzima wa katiba pamoja na suala la uchaguzi wa serikali za mitaa na kisha kutoa taarifa kesho.


Naye, Mjumbe wa Kamati hiyo, Profesa Mwesiga Baregu alisema jambo la msingi ni Ukawa kurejea bungeni na kukubaliana katika bunge hilo kuongozwa na agenda zilizo chini ya sheria kwa kujadili kilichopo katika Rasimu ya pili na kujadili nje ya rasimu ni kuvunja sheria.

Alisema pia Ukawa wanatakiwa kuwa makini na wanaotaka warejee bungeni kwani siyo kila mmoja nia yake ni njema.

Chanzo: Habari leo

WANAKIJIJI MAKETE WATAKA BANGI ILUHUSIWE

Huku harakati za kutaka matumizi ya Bangi kuhalalishwa zikishika kasi katika sehemu mbali mbali duniani, Tanzania haijaachwa nyuma.

Wanakijiji katika wilaya ya Makete , mkoa wa Njombe Kusini Magharibi mwa Tanzania wanataka serikali iweke sheria ambayo itaweza kuhalalisha matumizi ya mmea huo.

Wanakijiji hao zamani walikuwa wakitumia mbegu za mmea huo kukaanga na chakula lakini siku hizi wanalazimika kuzitumia kwa usiri mkubwa wakihofia kukamatwa na polisi.

Mwenyeketi wa Halmashauri ya wilaya ya Makete Daniel Okoka amesema matumizi ya Bangi katika wilaya hiyo hayajaanza leo, tangu zamaniwatu kitamaduni walikuwa wakitumia Mbegu za Bangi kukaanga na chakula.

Na kama mmea huo ungekuwa na tahri kubwa kiafya, basi watu wengi wilayani humo wangekuwa vichaa.

Miti ya mimea hiyo pia ilikuwa ikitumiwa kutengeza kamba ambazo anasema zilikuwa za nguvu sana.

Lakini kwa sababu ya sheria kali, matumizi ya Bangi au Marijuana yanafanywa kichinichini katika wilaya hiyo.

NDEGE YATUA KATIKATI YA BARABARA

Shughuli ziliathirika leo wilayani Mityana baada ya ndege kutua kwa dharura katika barabara ya magari ya Mityana.

Ndege hiyo N604AR, iliyokuwa imewabeba wanajeshi wa Marekani, ilituakatika eneo la Kiwawu umbaliwa kilomita 22 kutoka wilaya ya Mityana.

Kwa mujibu wa mtandao wa Nation, kamishna wa wilaya Joel Walusimbi, alithibitisha tukio hilo akisema rubani wa ndege hiyo alilazimika kutua katikati ya barabara

Polisi walisema kuwa ndege hiyo ilikuwa inaelekea mjini Juba Sudan Kusini kutoka uwanja wa ndege wa Entebbe.

DUNIA YAMKUMBUKA MANDELA

Hii leo ni siku ya kimataifa ya kusherehekea maisha ya hayati Nelson Mandela.


Wananchi wa Afrika Kusini wamekuwa wakifanya shughuli mbali mbali za kijamii kumkumbuka.

Moja ya shughuli hizo imekuakufanya usafi.

Waziri wa Mambo ya nchi za njee wa A-Kusini pamoja na kikosi cha mabalozi kadha wanaoishi A-Kusini wameweza kufanya usafi katika kituo kimoja cha magari ya abiria (Daladala) mjini Pretoria.


Huu ulikuwa wito wa Rais Jacob Zuma kwa raia wa afrika ya kusini kulisafisha taifa lao.

Lakini baadhi yao wamelalamika wakisema kuwa hiyo ni kazi ya serikali.


Ili kuadhimisha kuzaliwa kwake mamilioni ya watu pia wamejitolea kutumia dakika 67 za mda wao kufanya mambo mema ili kuadhimisha miaka 67 aliyotumia kama mwanaharakati wa kisiasa.

Vuguvu hilo lilianzia mjini Johanesburg na New York mnamo mwaka 2009 lakini sasa linasimamia mataifa 126.


Bwana Mandela, aliyefariki mwaka jana alisifika sana kwa kupigana vita dhidi ya utawala wa mzungu.

Aliishi grezani mwa miaka 27 kabla ya kuwa rais wa kwanza mzalendo nchini Afrika Kusini mwaka 1994.


Kabla ya kifo chake aliugua homa ya mapafu kwa mda mrefu, ugonjwa ambao mara kwa mara ulikuwa unazuka mwilini mwaka hata baada yamatibabu.

Mnamo siku ya Alhamisi, vitu vinavyosimulia maisha yake vilinadiwa kama kumbukumbu kwa maisha yake na kuchangisha pesa ili kusaidia shirika la kibindamu.

AMUUA MTOTO WA MIAKA TISA KISHA KULA UBONGO WAKE

MAUAJI ya kutisha yanaendelea kuuandama mkoa wa Kilimanjaro, baada ya kijana Laurance Flavian (20), mkazi wa Marangu Mashariki kumuua Mwanafunzi wa darasa la Pili katika Shule ya Msingi Marangu Hills, Francis Fortunatus (9), kwa kumkata mapanga sehemu za kichwani na kula ubongo wake, kisha na yeye kujikata uume wake na kusababisha mauaji hayo.


Akizungumza Kamanda wa polisi mkoani humo, Robert Boaz, amesema tukio hilo limetokea leo Ijumaa Julai 18, 2014 saa7:15 asubuhi katika eneo la Marangu Pentekoste katika Wilaya ya Moshi mkoani humo.


Amesema mtoto huyo ambaye pia ni mwanafunzi wa darasa la pili katika Shule ya Msingi Marangu Hills alikutwa na mauti wakati akielekea shuleni na kuwa kijana huyo (Laurance Flaviani), alianza kumshambulia kwa kumkata na mapanga sehemu za kichwani nakutoa ubongo wake na kuula hali iliyomsababishia, kufariki dunia papo hapo.


Kwa mujibu wa taarifa ya Kamanda Boaz, kijana huyo baada ya kumuua mtoto huyo nayeye alijijeruhi kwa kuukata uume wake, na kukimbizwa katika Hospitali ya Kilema ambapo alikufa wakati akipatiwa matibabu kutokana na kutokwa na damu nyingi kaatika sehemu aliyojikata.

"Mtoto huyu akielekea shuleni asubuhi ghafla kijana huyo ambaye nay eye sasa ni marehemu, alianza kumshambulia kwa kumkata kwa panga kichwani bila sababu yeyote, hali iliyosababisha kifo cha mtoto huyo papo hapo"Kamanda Boaz.

Aidha, amesema chanzo cha mauaji hayo hakijajulikana na kuwa taarifa za awali kuhusu tukio hilo kinasadikiwa kuwa kijana huyo alikuwa na ugonjwa wa akili na kwamba kabla ya kutenda tukio hilo alikuwa akifanya vurugu na kuvunja vioo vya nyumba yao za watu katika eneo hilo.


Mashuhuda wasimulia

Hata hivyo, taarifa kutoka eneo la tukio zinasema kijana huyo baada ya kutekeleza mauaji hayo ambapo inadaiwa mtoto aliyemuua ni mtoto wa bosi wake wake na kwamba baada ya kuukata uume wake alianza kuula kama nyama choma huku akikata kipande kimoja baada ya kingine.

Mmoja wa mashuhuda wa tukio hilo, Tetrula Kimario, amesema kijana huyo ambaye alikuwa akifanya kazi ya kutengeneza Sanamu za mapambo katika kiwanda kilichopo Marangu Pentekoste, na kuwa Julai 17, 2014 alianza kubadilika kwa kufanya vitu visivyoeleweka ambapo tajiri yake ambaye ni Baba wa mtoto aliyeuawa alimchukua na kumrudisha nyumbani kwao karibu na alipokuwa anaishi mwanzoni.


Amesema, ilipofika leo asubuhi mtoto wa bosi wake alitoka kwenda shule, ndipo kijana huyo alipomkata kichwa na kisha kuanza kula ubongo wake, ambapo watu walifikia katika eneo la tukio waliamua kumpiga kwa mawe hadi polisi walipofika katika eneo la tukio.

Kumbukumbu zinaonyesha kuwa, mkoa huo umekumbwa na matukio ya mauaji na unyanyasaji wa watoto waliochini ya umri wa miaka kumi na nane (18).

NDEGE YA MALAYSIA YADAIWA ILISHAMBULIWA


Kuanguka kwa ndege ya Malaysia si ajali,bali shambulio la kigaidi yasema Ukraine


Maafisa nchini Ukraine wanasema kuwa ndege ya abiria iliyoanguka nchini humo ilidunguliwa katika eneo la mashariki mwa taifa hilo ambako waasi wanaoiunga mkono Urusi wamekuwa wakipigana na vikosi vya serikali.
Wanasema abiria wote 298 waliokuwa katika ndege hiyo ya shirika la Malaysia iliyokuwa ikisafiri kutoka Amsterdam kuelekea Kualar Lumpur wameufariki.
Wengi wa abiria hao walikuwa ni raia wa Uholanzi.
Rais wa Ukraine Petro Poroshenko alitaja tukio hilo kama kitendo cha ugaidi.
Maafisa wa Ukraine walichapisha kile walichotaja kuwa mawasiliano ya simu yaliyonaswa kati ya waasi wakiwaeleza maafisa wa Urusi kwamba ni wao ndio waliohusika katika kuindungua ndege hiyo.

Waziri wa mashauri ya nchi za kigeni wa Ukraine, Pavlo Klimkin, amesema kuwa serikali ina ushahidi wa kutosha kwamba ndege hiyo ilidunguliwa.
Takriban Abiria 300 wa mataifa mbalimbali wamefariki baada kuanguka kwa ndege hiyo.


' Tulinasa pia mawasiliano ya simu kati ya magaidi hao wakizungumzia kundunguliwa kwa ndege hiyo.
Kwa sasa tunatafsiri sauti zao na kisha tutaziweka kwenye mtandao wa internet ili kuthibitisha hilo."
Hata hivyo sauti hizo zilizonaswa bado hazijathibitishwa na upande uliohuru na waasi hao wamekanusha kuhusika wakisema kuwa ni wanajeshi wa serikali ndio walioidungua ndege hiyo.
Kadhalika marekani imesema kuwa inaamini ndege hiyo ililipuliwa angani na wala halikuwa tukio la ajali.

Makamu wa rais Joe Biden hata hivyo amesisitiza kuwa Marekani bado inatafuta maelezo.
''Ndege ya Malaysia iliyokuwa ikitoka Ulaya magharibi kuelekea Kuala Lumpur, yaelekea ilipokuwa ikivuka karibu na mpaka kati ya Ukraine na Urusi, nasema yaelekea kwa sababu hatuna taarifa za kina, nataka kuwa makini na kile ninachosema yaelekea ilidunguliwa, ilidunguliwa na wala sio ajali. Ililipuliwa kutoka angani. Tunaona ripoti kwamba huenda raia wa Marekani walikuwa kwenye ndege hiyo na bila shaka huo ndio wasiwasi wetu wa kwanza.''
Rais wa Urusi, Vladimir Putin, amesema kuwa Ukraine inapaswa kuwajibika katika tukio la udunguaji wa ndege hiyo.

Msemaji wa serikali ya Urusi amesema kuwa mkasa huo haungetokea ikiwa Kiev haingeimarisha harakati zake za kijeshi mashariki mwa Ukraine.

MSHUKIWA WA UGAIDI KENYA AKAMATWA TANZANIA

Mmoja wa watuhumiwa wa matukio ya ugaidi nchini Kenya, Jihad Gaibon Swaleh, amefikishwa mahakamani nchini Tanzania.

Mshukiwa huyo amesomewa mashtaka ya kufadhili vitendovya kigaidi nchini Kenya.


Pamoja naye watuhumiwa wengine 16 ambao wanadaiwa kuendesha vitendo vya kigaidi nchini Tanzania pia wamefikishwa mahakamani hii leo wakikabiliwa na tuhuma za kula njama ya kutenda makosa ya kigaidi nchini Tanzania.

Washtakiwa wote 17 wamerejeshwa rumande baada ya kusomewa mashtaka ya vitendo vya kigadi nchini Tanzania pamoja na nchi jirani ya Kenya.


Upande wa mashtaka ukiongozwa na mwendesha mashtaka ambaye ni wakili wa serikali mwandamizi Prosper Mwangamila ulidai mbele ya Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dares Salaam, kuwa kwa kutumia mtandao wa facebook aliweza kushawishi watu wengine kuwasiliana kwa lengo la kutafuta vifaa vya kulipua mabomu nchini Kenya na kusababisha majerahi, hofu na Vifo.


Jihand Gaibon Swaleh ambaye amesomewa mashtaka mawili hakuruhusiwa kukiri wala kukana mashitaka yanayomkabili kutokana na kwamba mashitaka hayo yanaangukia katika makosa ya ugaidi ambayo kwa mujibuwa sheria nchini Tanzania mahakama ya Hakimu Mkazi haina mamlaka ya kuendesha kesi za namna hiyo.

Katika kesi ya awali kutajwa mahakamani hapo washtakiwa wengine 16 walisomewa mashtaka mawili ikiwemo kula njama kutenda kosa pamoja na kushawishi wenzao kushiriki katika vitendo vya kigaidi katika sehemu mbali mbali nchini Tanzania.


Ni makosa ambayo wanadaiwa kutenda kati ya Januari mwaka 2013 na Juni 2014 katika maeneo tofauti Tanzania.

Katika kesi zote mbili dhidi ya washtakiwa hao Upande wa mashtaka uliiambia mahakama iliyokuwa chini yahakimu mfawidhi wa mahakama hiyo bi Hellen Riwa kuwa upelelezi bado unaendelea na hivyo kuiomba mahakama kuahirisha kesi hizo hadi mwishoni mwa mwezi huu waJulai.


Awali mapema asubuhi msemaji wa jeshi la polisi nchini Tanzania Bi Advera John Bulimba aliwealeza waandishi wa habari kuhusu tuhuma dhidi ya washtakiwa hao.

Hii ni mara ya kwanza kwa kundi kubwa la watuhumiwa kufikishwa mahakamani kwa pamoja wakikabiliwa na tuhuma za makosa ya kigaidi huku mtandao wa kijamii wa facebook nao ukitajwa kuhusika katika kutawanya taarifa za kuwezesha kutenda makosa hayo.

UFAULU KIDATO CHA 6 JUU

UFAULU katika mtihani wa Kidato cha Sita mwaka jana, umeongezekakwa asilimia 8.13 huku shule za mikoani zisizo na majina makubwa zikichomoza katika orodha ya kumibora.Matokeo hayo yalitangazwa jana naBaraza la Mitihani Tanzania (Necta),huku yakionesha baadhi ya shule kongwe kama vile Tambaza ya jijiniDar es Salaam, zikiwa zimeshika mkia.

Katika mkutano na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, Kaimu Katibu Mtendaji wa Necta, Dk Charles Msonde alisema katika mtihani huo uliofanyika kati ya Mei5 na 21, mwaka jana, ufaulu umeongezeka kwa asilimia 8.13 ikilinganishwa na matokeo ya mwaka jana.

Jumla ya watahiniwa 38,905 sawa na asilimia 95.98 ya waliofanya mtihani huo wamefaulu. Mwaka jana wanafunzi waliofaulu walikuwani 44,366 sawa na asilimia 87.85.

Kaimu Katibu Mtendaji alisema wanafunzi waliofaulu, wasichana ni 12,080 sawa na asilimia 97.66 wakati wavulana ni 26,825 sawa na asilimia 95.25.

Shule Bora

Katika matokeo hayo, shule zilizofanya vizuri ni Igowole (Iringa), Feza Boys (Dar es Salaam),Kisimiri (Arusha), Iwawa (Njombe), Kibaha (Pwani), Marian Girls (Pwani) Nangwa (Manyara), Utawa (Mbeya), Kibondo (Kigoma) na Kawawa (Iringa).Ufaulu wa shule hizo umepangwa kwa kutumia kigezo cha wastani wapointi (Grade Point Average – GPA)na mchanganuo kwa kuzingatia idadi ya watahiniwa wasiopungua 30.

Kumi za mwisho

Kwa upande wa shule 10 za mwisho, pamoja na Tambaza, Dk Msonde alizitaja nyingine kuwa ni Ben Bella (Unguja), Fidel Castro (Pemba), Muheza High School (Tanga), Mazizini (Unguja), Mtwara Technical (Mtwara), Iyunga Technical (Mbeya), Al-Falaah Muslim (Unguja), Kaliua (Tabora) naOsward Mang'ombe (Mara).Wanafunzi BoraAkizungumzia walivyopatikana wanafunzi waliofanya vizuri zaidi, Kaimu Katibu Mtendaji huyo wa Necta, alisema waliangalia wastani wa GPA kwenye masomo ya tahasusi pamoja na wastani wa alama za jumla walizopata.Wanafunzi hao waliofanya vizuri katika masomo ya Sayansi kitaifa na shule zao kwenye mabano ni Isaack Shayo (St. Joseph Cathedral),Doris Noah (Marian Girls), Innocent Yusufu (Feza Boys), Placidl Pius (Moshi), Benni Shayo (Ilboru), Abubakar Juma (Mzumbe),Mwaminimungu Christopher (Tabora Wavulana), Chigulu Japhaly (Mzumbe), Hussein Parpia (Al-Muntazir Islamic Seminary) na Ramadhani Ally Msangi (Feza Boys).

Kwa upande wa wasichana 10 bora kwa masomo ya sayansi kitaifa, watano wametoka Shule ya Marian.Nao ni Doris Noah, Monica Mtei, Wema Kibanga, Deborah Mlawa na Doreen Kashushura.

Wengine ni Frida Mbilinyi, Gloria Kweka (Msalato), Aisha Mnjovu, Mulhat Said (Feza) na Heavenlight Munis (St Mary Goreth). Wavulana 10 bora kwa masomo ya Sayansi kitaifa na shule zao kwenye mabano ni Isaack Shayo (St Joseph Cathedral), Innocent Yusuf, Ramadhan Msangi (Feza), Placid Pius (Moshi), Benini Shayo (Ilboru),Abubakar Juma (Mzumbe), Mwaminimungu Christopher (Tabora Boys), Chigulu Japhaly (Mzumbe), Hussein Parpia (Al Muntazir Islamic Seminary) na Lusekelo Kihesya (Mpwapwa).

10 bora

Biashara Watahiniwa 10 bora kwa masomo ya Biashara ni Jovina Leonidas (Nganza), Nestory Makendi (Kibaha), Imma Anyandwile (Umbwe), Thersia Marwa na Grace Chelele (Loyola), Betria Rugila (Baobab), Jaqueline Kalinga (Weruweru), Tajiel Kitojo (Arusha), Shiriya Ramaiya (ShaabanRobert) na Mwanaidi Mwazema (Weruweru).

Lugha, Sanaa

Watahiniwa kumi bora wa masomoya Lugha na Sanaa ni Lisa Mimbi (St. Mary Goreth), Rosalyna Tandau(Marian Girls), Joseph Ngobya (St. Joseph Cathedral), Aneth Mtenga na Idda Lawenja (Marian Girls), Edna Mwankenja( Kisimiri), Catherine Kiiza ( St. Mary Mazinde Juu), Nancy Adonswai (Mwika), Mohamed Salmin (Mwanza) na Idrisa Hamisi (Mwembetogwa).

Ubora wa ufaulu

Msonde alisema ubora wa ufaulu kwa kuangalia madaraja waliyopata watahiniwa wa shule unaonesha kuwa jumla ya watahiniwa 30,225 sawa na asilimia 85.73 wamefaulu katika madaraja I - III wakiwemo wasichana 9,954 sawa na asilimia 90.59 na wavulana 20,271 sawa na asilimia 83.53.

Daraja kwa Kwanza ni wanafunzi 3,773, wavulana 2,232 na wasichana 1,541, Daraja la Pili ni wanafunzi 9,631ikiwa wavulana ni 6,179 na wasichana 3,452.Daraja la Tatu ni wanafunzi 16,821 ikiwa wavulana ni 11,860 na wasichana 4,961, Daraja la IV: wanafunzi 4,420 ikiwa ni wavulana 3,474 na wasichana 946 na Daraja 0: wanafunzi 612, wavulana wakiwani 524 na wasichana 88.

Ufaulu Kiswahili

Msonde alisema ufaulu wa watahiniwa wa shule katika masomo yote 14 ya msingi umepanda ikilinganishwa na mwaka 2013. Ufaulu wa juu kabisa ni ule wa somo la Kiswahili ambao ni asilimia 99.88 ya watahiniwa wote wa shule waliofanya somo hilo wamefaulu.Alisema ufaulu katika masomo ya Sayansi (Physics, Chemistry, Biology na Advanced Mathematics)umeendelea kuimarika kwa kulinganisha na ufaulu wa masomohayo mwaka 2013.

Gredi za ufauluAlisema watahiniwa wa shule waliofaulu ni wanafunzi 34,645 sawa na asilimia 98.26 ya waliofanya mtihani, wasichana wakiwa ni 10,900 ambayo ni asilimia 99.2 na wavulana 23,45 sawa na asilimia 97.84.

Mwaka 2013 watahiniwa 40,242 sawa a asilimia 93.92 ya watahiniwa wa shule walifauu mtihani huo. Mtahiniwa anahesabiwa kuwa amefaulu somo kwa kupata angalau gredi D (alama 30) katika somo husika.Hivyo, kiwango cha juu cha ufaulu katika somo ni gredi A na cha chinikatika somo ni Gredi D. "Ufaulu katika gredi A, B+, B na C utakuwa ni Principal Pass," alisema Kaimu Katibu Mkuu wa Necta.Kulingana na mpangilio huo, Daraja la Kwanza ni poiti 3-7, la Pili8-9, Tatu 10-13 na Daraja la Nne mtahiniwa atakuwa amefaulu kwa kuwa na angalau D mbili au principal pass moja.Aliyepata Sifuri ni aliyepata ufaulu chini ya D mbili. Uzito wa alama katika Gredi; A=1, B+= 2, B=3, C=4, D=5, E=6 na F=7.

Watahiniwa wa Kujitegemea Alisema watahiniwa wa Kujitegemea waliofaulu ni 4,260 sawa na asilimia 80.73 ya watahiniwa 5,277 waliofanya mtihani.Mwaka 2013 watahiniwa wa kujitegemea 4,124 sawa na asilimia 53.87 walifaulu mtihani huo. Msonde alisema Baraza limezuia matokeo ya watahiniwa 150 wa shule ambao hawajalipa ada ya mtihani hadi watakapolipa, watahiniwa tisa waliopata matatizo ya kiafya."Watahiniwa husika wamepewa fursa ya kufanya mtihani kwa masomo ambayo hawakuyafanya kwa sababu ya ugonjwa katika Mtihani wa Kidato cha Sita Mei, 2015.

Alisema watahiniwa 29 wa shule ambao walipata matatizo ya kiafya na kushindwa kufanya mtihani kwa masomo yote. Watahiniwa husika wamepewa fursa ya kufanya Mtihani wa Kidato cha Sita Mei, 2015.

Msonde alisema Baraza limefuta matokeo yote ya watahiniwa wawiliwaliobainika kufanya udanganyifu katika mtihani. Matokeo Ualimu Katika hatua nyingine, matokeo ya walimu waliofanya mtihani mwaka 2014 yanaonesha watahiniwa katika ngazi ya Cheti, Stashahada na Stashahada ya Ualimu Ufundi, hakuna mwanafunzi aliyepata alama za juu.Dk Msonde alisema watahiniwa 4,161 sawa na asilimia 85.71 ya watahiniwa 4,899 waliofanya mtihani wa Stashahada ya Ualimu mwaka 2014 wamefaulu.Kati ya watahiniwa hao, wasichana ni 1,401 sawa na asilimia 83.64 na wavulana 2,760 sawa na asilimia 86.79.Alisema katika hao waliofaulu, hakuna aliyepata daraja la juu (distiction). Waliopata daraja la credit ni watano, pass 4,156, wanaorudia mtihani ni 658 na waliofeli ni 36.Akizungumzia matokeo ya mtihani wa Stashahada ya Ualimu Ufundi, Msonde alisema "watahiniwa wote watatu waliofanya Mtihani wa Stashahada ya Ualimu Ufundi wameshindwa baadhi ya masomo, hivyo watarudia masomo waliyoshindwa katika Mtihani wa Mei 2015.

Bofya hapa Kuangalia matokeo http://www.necta.go.tz/matokeo2014/ACSEE.htm

WEZI WA CHUMA WAIBA RELI

Sehemu ya njia ya reli iliyoibwa


Wezi wa chuma nchini Afrika Kusini wameiba karibu kilomita kumi za chuma kwenye njia ya reli na kusababisha uharibifu wa thamani ya dola milioni 2.3.
Sehemu kubwa ya chuma ya reli imeibwa katika muda wa miezi michache iliyopita. Njia hiyo ya reli hutumiwa na magari ya moshi kutoka mjini Johannesburg kwenda mjini Nigel. Taarifa hii ni kwa mujibu wa jarida la The Star.
Watu watano wamefikishwa mahakamani baada ya kukamatwa na walinzi ambao hushika doria katika sehemu hiyo wakiibaa chuma hiyo.
"ni wataalamu wa kuiba hao. Hakuna dalili ya wao kukosea hata kidogo,'' asema Thumbu Mahlangu,mwanakamati ya usafiri.
Msemaji wa usafiri wa reli Mike Asefovitz anakubaliana na hilo.
''Hawa wezi sio watu wadogo. Chuma hizi huwa ni nzito na kuweza kuzing'oa unahitaji mashine kubwa.''

Chuma hizo zina thamani ya dola 120,000 katika soko la vyuma kuu kuu.
Wizi huo umesababisha mabehewa mapya 34 kuegeshwa tu katika kiwanda kwani hazina pa kutumiwa. Kiwanda hicho sasa kinahofia watu zaidi ya 700 huenda wakapoteza kazi zao.
Nchini Afrika Kusini wizi wa vyuma ni tatizo kubwa sana kiasi cha kuleta hasara ya mamilioni ya dola kwa uchumi wa nchi.

JELA KWA KUMTUMIA OBAMA BARUA YENYE SUMU

Richardson ameigiza katika vipindi vya 'The Vampire Diaries' na 'The Walking Dead.


Muigizaji mwanamke nchini Marekani aliyemtumia Rais Barack Obama barua iliyokuwa na sumu ya Ricin amefungwa jela kwa miaka 18.
Shannon Richardson, mwenye umri wa miaka 36, kutoka Texas, pia alimtumia meya wa New York Michael Bloomburg barua nyingine iliyokuwa na sumu hiyo hiyo.
Alidai kuwa mumewe waliyeachana naye ndiye alituma barua hizo katika njama ya kumlimbikizia madai hayo.
"sikuwa na nia ya kumdhuru mtu, '' Shannon aliambia mahakama.
Alikiri kosa la kumiliki na kutengeza sumu hiyo mwezi Disemba.

Jaji alimpa hukumu kubwa zaidi ikilinganishwa na kosa lake na pia kutakiwa kulipa faini ya dola 367,000.
Richardson, mama mwenye watoto sita, ameigiza katika vipindi kama 'The Vampire Diaries' na 'The Walking Dead.'
Viongozi wa mashitaka wanasema kuwa mwanamke huyo aliagiza bidhaa za kutengeza sumu hiyo kupitia kwa mtandao kisha akatuma barua tatu zilizokuwa zimepakwa sumu hiyo.
Shannon mwenye watoto sita aliomba mahakama kumhurumia kwa kumpa adhabu ndogo


Kulingana na viongozi wa mashitaka, moja ya barua alizomtumia Obama , ilikuwa na maandihsi haya: "kilicho ndani ya barua hii, hakiwezi kulinganishwa na mipango yangu kwako bwana Rais. ''
Barua nyingine iliyopokewa na meya Bloomberg, anayeunga mkono kudhibitiwa kwa bunduki, ilisema, '' mpige risasi mtu yeyote atayekuja kuchukua bunduki za mtu aliyetuma barua hii.''
Barua ya tatu iliyokuwa na kemikali hiyo ya sumu, ilifunguliwa na bwana Mark Glaze, mkurugenzi mkuu wa idara inayofadhiliwa na Meya ya kupambana na silaha haramu.
Richardson katika kumtaka jaji kumhurumia, aliomba msamaha akisema, '' mimi sio mtu mbaya. Sina nia ya kumdhuru mtu yeyote.

Aliomba msamaha na huruma na kusema tayari anahisi ameadhibiwa vya kutosha kwa kunyang'anywa watoto wake sita

ISRAEL NA HAMAS WAKUBALIANA KUSITISHA MASHAMBULIZI KWA MUDA

Vuguvugu la kupigania Uhuru wa Palestina, Hamas, na Israel zimekubali kuheshimu makubaliano ya kusitisha mapigano katika ukanda wa Gaza kwa muda wa saa tano baadaye hivi leo baada ya siku tano za mapigano makali.


Baada ya ombi la umoja wa mataifa jeshi la Israel limesema kuwa litasitisha mashambulizi kati ya saa nneasubuhi hadi saa tisa kwa saaza Gaza, ili kuwaruhusu wakaazi kupata chakula na huduma muhimu.

Msemaji wa Hamas Sami AbuZukhri amethibitisha kuwa vuguvugu hilo kadhalika litasitisha mashambulizi ya roketi dhidi ya Israel wakati huo.


Msemaji wa shirika la umoja wa mataifa linalowasaidia wakimbizi wa Palestina Christopher Gunnes amesema kuwa ni matumainiyake kwamba usitishaji huo wa mapigano utatoa fursa ya kusuluhisha matatizo yanayoikabili gaza.

Hapo jana jumatano jazba zilizidi pale watoto wanne wa kipalestina wote kutoka familia moja waliuwawa katika shambulizi la mizinga kutoka Israel wakati wakicheza kwenye ufuo wa bahari huko Gaza.


Israel imesema ilikuwa ikiwalenga wapiganaji wa Hamas na kwamba vifo hivyo ni matokeo ya mkasa mkubwa wa mapigano hayo.

Naye rais wa Marekani Barrack Obama amesisitiza kuwa Israel ina haki ya kujilinda.

WANASAYANSI WAELEZA FAIDA ZA 'USHUZI'

Wanasayansi katika chuo kikuu cha Exeter, nchini Uingereza, wanasema kuwa wamegundua harufu mbaya kama vile ya kujamba japo inachukiza kwa pua, ina manufaa makubwa kwa afya ya binadamu


Wanasayansi hao wanasema kuwa harufu hiyo mbaya inaweza kuwa kinga dhidi ya magonjwa ya moyo na akili na hata Saratani, Gesi au harufu mbaya ambayo hutokana na chakula kinachosagwa tumboni mwako inaweza kulinda baadhi ya viungo vya mwili wako.

Ndio! athari ni kile ambacho unakidhania: Eti watu wanauchukulia utafiti huu kumaanisha kuwa harufu mbaya inayotokana na mtu kujamba inaweza kuzuia magonjwa fulani mwilini kama vile saratani.


Utafiti huo uliochapishwa katika mtandao wa chuo kikuu cha Exter uligundua kuwa gesi hiyo inayojulikana kama Hydrogen Sulfide ambayo pia hupatikana katika Mayai yaliyooza, inaweza kuwa muhimu katika kutibu baadhi ya magonjwa.

"Ingawa gesi ya hydrogen sulfide inajulikana kuwa na harufu mbaya na hupatikana katika Mayai yaliyooza pamoja na harufu ya mtu kujamba, hutengenezwa mwilini na inaweza kuwa kana tiba kwa magonjwa fulani," alisema daktari Mark Wood, profesa wachuo hicho cha Exeter.


Hata hivyo gesi hiyo ina athari mbaya ikiwa katika viwango vikubwa , kwa mujibu wa utafiti huo

Watafiti wanasema licha ya harufu hiyo mbaya ya kujamba kuchukiza, ina uwezo mkubwa wa kupunguza uwezekenano wa mtu kupatwa na magonjwa kama vile, saratani, kiharusi, mshtuko wa moyo na kuumwa na mifupa.

ASKARI WA JWTZ AFARIKI MAZOEZINI MLIMA KILIMANJARO

Ofisa mmoja wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) amefariki dunia na mwingine amesagika mguu baada ya mawe kuporomoka wakati wakipanda Mlima Kilimanjaro katika mazoezi.


Wanajeshi hao ni miongoni mwa maofisa 263 wa JWTZ waliopanda mlima huo mrefu kuliko yote barani Afrika kwa makundi kuanzia Julai 12, mwaka huu kupitia njia ya Rongai iliyopo wilayani Hai.

Habari za uhakika zilizopatikana jana zilieleza kuwa tukio hilo lilitokea jana saa 10:00 alfajiri katika urefu wa mita 5,000 kutoka usawa wa bahari wakati maofisa hao wakitoka eneo la Hans Meyer wakikaribia kilele cha Gilmans.


Mkuu wa Hifadhi ya Mlima Kilimanjaro (Kinapa), Erastus Lufungulo alilithibitisha kutokea kwa maafa hayo na kueleza kuwa mawe hayo yaliporomoka kutoka juu ya Hans Meyer na kushuka hadi eneo la Jamaica.


Aliyefariki dunia katika ajali hiyo wametajwa kuwa ni Cadet MT 104948 Malata Thomas Kitene (26) baada ya kupata majeraha ya kichwa na Cadet MT 105896 Gabriel Makenge (32) ambaye amevunjika na kusagika mguu wa kushoto.


"Baada ya kupata taarifa za tukio hilo, kikosi chetu cha uokoaji kilikwenda eneo la tukio na kushiriki kazi ya uokoaji, lakini taarifa zaidi kuhusu ziara ya maofisa hao mnaweza kupata kwa wasemaji wa JWTZ," alisema.

Hata hivyo, msemaji wa JWTZ, MejaErick Komba hakupatikana jana kuzungumzia tukio hilo.


Majeruhi pamoja na maiti ya ofisa hao waliteremshwa kutoka kileleni jana saa 4:00 asubuhi na kupelekwa moja kwa moja Hospitali ya Rufaa ya KCMC iliyopo mjini Moshi.

Taarifa zaidi zilisema maofisa hao walipanda mlima huo ikiwa ni utaratibu wa kila mwaka kwa ajili ya mazoezi ya ukakamavu.

WATUPWA JELA MAISHA KWA UBAKAJI

Mahakama nchini Misri, imewahukumu maisha jela wanaume saba na wengine wawili kifungwa miaka 20 au zaidi kila mmoja kwa kuwabaka wanawake wakati wa sherehe za kutawazwa kwa Rais Abdul Fattah al-Sisi.


Watuhumiwa walipatikana nahatia kwa makosa mengine mengi ikiwemo jaribio la ubakaji na udhalilishaji wa wanawake.

Bwana Sisi aliamuru waziri wake wa mambo ya ndani kuchukua hatua kali dhidi ya watuhumiwa wa ubakaji na dhuluma nyinginezo za kingono baada ya wanaume hao kukamatwa kwa kuwashambulia wanawake katika medani ya Tahrir.


Duru zinasema kuwa hukumuhiyo, huenda ikaodnoa wasiwasi kuwa maafisa nchini Misri hawachuku hatua kali dhidi ya vuisa vya dhuuma za kingono.

Kulikuwa na ghadhabu miongoni mwa umma baada ya kanda liyomuonyesha mwanamke aliyekuwa uchi akibururwa katika barabara za mji mkuu Cairo.


Kanda hiyo iliwekwa kwenye mitandao ya kijamii.

A court in Egypt has sentenced seven men to life in prison and two others to 20years for sexual assaulting women last month.

HABARI NJEMA VITA DHIDI YA UKIMWI

Kuna uwezekano kuwa janga la ukimwi huenda likadhibitiwa ifikapo mwaka 2030, kulingana na ripoti iliyotolewa na shirika la Umoja wa Mataifa la kupambana na ukimwi.

Ripoti hiyo imesema kuwa idadi ya visa vya maambukizi mapya na vifo kutokana na HIV, vimeendelea kushuka.


Hata hivyo, shirika hilo linataka juhudi zaidi za kimataifa kufanywa kwani za sasa hazitoshiNa shirika la misaada la Medecins Sans Frontieres limeonya kuwa watu wanaoishi na virusi hivyo hawapati dawa za kutosha.

Kwa mujibu wa shirika hilo watu milioni 35 wanaishi na virusi vya HIV.


Ripoti hiyo ilionyesha visa vipya vya maambukizi milioni2.1 vilitokea mwaka 2013. Idadi hii iko chini kwa asilimia38 ikilinganishwa na mwaka 2001.


Vifo kutokana na HIV pia vimepungua kwa asilimia 5 katika miaka mitatu iliyopita. Kwa sasa watu milioni 1.5 hufariki kutokana na ugonjwahuo kila mwaka.

Afrika Kusini na Ethiopia zimepiga hatua katika kupunguza vifo vya wagonjwawa HIV.

PICHA YA SIKU

Kuelekea fainali ya kombe la dunia leo katika dimba la Maraccana kati Germany vs Argentina pia kuna upande mwingine ni kati ya Papa Francis anaetokea Argentina dhidi ya Papa Benedict ya 16 ambae ni mjerumani. Je wataangalia mechi hii pamoja?

BINTI WA MIAKA 10 ABAKWA NA WANAUME WAWILI KWA ZAMU

JESHI la polisi mkoani Ruvuma linawatafuta wakazi wawili wa kijiji cha Silo kata ya Linda wilaya ya Nyasa kwa tuhuma za kumbaka msichana wa miaka 10 , mwanafunzi wa darasa la pili katikashule ya Msingi Luhekitiki wilayani humo.

Kamanda wa polisi mkoani hapa, Mihayo Msikela alimtaja mtuhumiwa wa kwanza kwa jina moja la Damas ambaye kwa kushirikiana na mwenzake ambaye hakufahamika walimbaka mwanafunzi huyo nyakati za usiku katika kijiji hicho.


Tukio hilo lilitokea juzi usiku ambapo Damas akiwa na mwenzake, walimrubuni mtoto huyo kwa pipi na kumvuta kichakani kabla ya kumbaka.

Alisema mwanafunzi huyo alikuwa katika sherehe za ngoma kijijini hapo.


Alieleza kuwa watuhumiwa hao baada ya kufanikisha lengo lao hilowalikimbia na kumuacha mtoto huyo kichakani akipiga kelele kabla ya kuchukuliwa na wasamaria ambao walitoa taarifa kwa babu yake (jina limehifadhiwa) ambaye naye alitoa taarifa ya tukio hilo polisi.

Baada ya polisi kufika kijiji hapo nakumchukua mtoto huyo walimfikisha hospitalini kwa ajili ya uchunguzi na aligundulika kufanyiwa kitendo hicho.


Chanzo: Habari leo

BINTI ACHINJWA KAMA KUKU

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Singida, Geofrey Kamwela WATU wasiojulikana wilayani Manyoni wamemchinja mithili ya kuku binti mmoja anayekadiriwa kuwa na umri wa miaka 16.

Diwani wa Kata ya Manyoni Mjini, Hamis Masabuni alisema tukio hilolilitokea juzi asubuhi katika eneo laMitoo kwenye mashamba ya Magereza, Uwanja wa Ndege wa zamani.


Alisema siku ya tukio, yeye alipata taarifa ya simu kutoka kwa raia wema hivyo ikambidi aende huko kushuhudia kulikoni na mara alipofika eneo hilo alikuta mwili wa marehemu ukiwa umelala chinina kuchinjwa mithili ya kuku.

Diwani huyo amelitaka jeshi la polisi kufanya uchunguzi wa kina juu ya tukio hilo ili kubaini wauaji wa binti huyo ili hatua za kisheria ziweze kuchukuliwa dhidi yao.


Muuguzi wa zamu katika hospitali ya wilaya ya Manyoni, Getruda Njughuda amekiri kuupokea mwili wa binti huyo.

Naye Kamanda wa Polisi Mkoa wa Singida, Geofrey Kamwela alisema kuwa polisi inaendelea na uchunguzi kuhusu tukio hilo.

BUNGE LA UINGEREZA KUJADILI MSWADA WA KUJIUA

Askofu mkuu wa zamani wa Cantebury Lord Carey amesema kuwa ataunga mkono sheria ambazo zitahalalisha watu wanaougua kupitia kiasi nchini Uingereza na Wales kupata usaidizi wa kujiua.


Katika taarifa yake ndani ya gazeti la Daily Mail Lord Carey ameondoa pingamizi yake dhidi ya mswada huo kufuatia hali inayowakumba watu wanaougua.

Lakini Askofu mkuu wa Cantebury anayehudumu kwa sasa Justin Welby ameutaja mswada huo kama ulio na makosa na hatari kubwa.

Wabunge wataujadili mswada huo siku ya ijumaa.


Mswada huo uliowasilishwa na mbunge wa chama cha leba Lord Falconer utawapa fursa watu wazima nchini Uingereza na Wales kupata usaidizi wa kujitoa uhai.

Fursa hiyo itashirikisha wale walio na chini ya miezi sita kuishi.


Madaktari wawili watalazimika kuthibitisha iwapo mgonjwa anaugua kupitia kiasi na kwamba wameafikia uamuzi wao wenyewe wa kujitoa uhai.

Takriban wabunge 110 wameorodheshwa kuzungumza wakati bunge litakapojadili mswada wa wanachama binafsi siku ya ijumaa.


Wakati Askofu Lord Carey alipokuwa Askofu mkuu wa Cantebury, alikuwa miongoni mwa watu waliopinga mswada wa Lord Joffes wa kuwasaidia wagonjwa wanaougua kupitia kisia kujitoa uhai ambao ulipingwa katika bunge la mabwana mnamo mwaka 2006.

Anasema kuwa inawezekana kuwa mcha mungu na vilevile kuwasaidia wale wanaotaka kujitoa uhai.


Lakini katika taarifa yake hii leo katika gazeti la Daily Mail Lord Carey alisema ''ukweli nikwamba nimebadilisha uamuzi wangu''.

MWANAMKE ALIYEFICHA MTOTO KWA NJIA ZA KISHIRIKINA AFIKISHWA MAHAKAMANI

MKAZI wa kijiji cha Marambeka wilayani Bunda, Minza Pama (80), anayetuhumiwa kuiba mtoto kwa njia ya ushirikina na kumficha uvunguni mwa kitanda chake kwa muda wa siku saba, amefikishwa katika mahakama ya wilaya hiyo nakupelekwa mahabusu kwa kukosa dhamana.

Mwanamke huyo amefikishwa katika Mahakama hiyo juzi mbele ya Hakimu Mkazi Mfawidhi, Safina Simufukwe na kusomewa mashitaka ya kuiba mtoto kwa nia ya kutaka kutenda kosa.

Mwendesha mashitaka wa polisi, Masoud Mohamed alidai mshitakiwa huyo anatuhumiwa kumuiba Yateke Ramadhan (9) na kumficha nyumbani kwake uvunguni mwa kitanda kwa muda wa siku saba, bila kumpa chakula chochote.


Mtoto huyo baada ya kupotea katika mazingira ya kutatanisha akiwa matembezini, wananchi wa kijiji hicho na vijiji jirani walianza msako wa kumtafuta na Julai 3, mwaka huu, walimkuta akiwa amefichwa uvunguni mwa kitanda cha kikongwe huyo akiwa hajitambui.

Baada ya kumpata wananchi walianza kushambulia mwanamke huyo, ambapo aliokolewa na polisi waliowahi kufika katika eneo hilo, ambapo pia askari polisi mmoja alijeruhiwa kwa bahati mbaya kwa kupigwa jiwe kichwani na wananchihao waliokuwa na jazba.


Aidha, ilielezwa kuwa wananchi hao walimwamru kikongwe huyo kumzindua mtoto huyo ili aweze kurudia hali yake ya kawaida na ndipo akammwagia dawa kichwani na kuzinduka.

Mtuhumiwa huyo alikana mashitaka yake na kupelekwa mahabusu baada ya kushindwa masharti ya dhamana, ambapo kesi yake itatajwa tena mahakamani hapo Julai 22, mwaka huu.


Chanzo: Habari leo

WASICHANA SABA WABAKWA KISHA WANYONGWA

WASICHANA saba wamepoteza maisha wilayani Nachingwea mkoani Lindi baada ya kubakwa nakunyongwa kisha kuwekewa vijiti na chupa kwenye sehemu zao za siri.

Wasichana hao wamepoteza maisha kwa nyakati tofauti katika kipindi cha miezi minne iliyopita na wamekuwa wakipigiwa simu nyakati za usiku na kukutana na waliwapigia simu ambapo hubakwa na kunyongwa na kisha katika sehemu za siri kuwekewa vijiti au chupa.


Mkuu wa Mkoa wa Lindi, Ludovick Mwananzila amebainisha aina hiyo ya mauaji jana wakati alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari katika Hospitali ya Mkoa ya Sokoine.

Mwananzila alikuwa amekwenda hospitalini hapo kuwatazama majeruhi ambapo alifafanua kuwa mauaji hayo yanaendelea na juzi mtu mwingine aliuawa katika mazingira hayo.


Alisema, "serikali ya wilaya ilishatoa namba za simu kuwa unapopigiwa simu mtoto wa kike fanya juhudi kumjulisha mwenzakoau piga simu kituo cha polisi ili kuweza kukabiliana na watu hao wanaotoa roho za watu".


Mwananzila alisema kuwa binti mmoja aliweza kupigiwa simu na kundi hilo, aliamua kupiga simu kituo cha polisi na kuweka mtego baada yeye kutoka nje, polisi walikuwa wameshazingira maeneo hayo na wauaji wale walimfuata ndipo huyo binti alianza kuvutana nao na hatimaye Polisi waliwatia mbaroni watu hao. Mkuu huyo wa mkoa aliwaonya mabinti hao na kusema: "ni makosa kwa wasichanakutoka nje baada ya kupigiwa …"kinachotakiwa kwanza mjulishe mwenzako, lakini unafanya siri madhara yataweza kukutokea, hususani watoto wa kike".


Alisema mauaji hayo yana ishara ya imani ya kishirikina. Hata hivyo uchunguzi unaendelea kufanyika. Alisema suala hilo liko ndani ya uchunguzi hivyo ni vizuri kufanyia kazi kwanza na kuwataka wananchi wawe na subira.

BUNDUKI YA FFU YATUMIKA KATIKA UJAMBAZI

TUKIO la ujambazi ambalo liliua watu watatu wanaosadikiwa kuwa majambazi, limechukua sura mpya baada ya silaha waliyokuwa wakitumia majambazi hao kugundulika kuwa ilikuwa ikimilikiwa na askari wa Kikosi cha Kutuliza Ghasia (FFU), Sospeter Peter Manyika ambaye kwa sasa yuko rumande.


Kukamatwa kwa Manyika kumethibitishwa na Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Arusha, Liberatus Sabas lakini hakuwa tayari kusema chochote juu ya kuwekwa rumande kwa askari huyo.

"Ni kweli tulimkamata (Manyika) baada ya kufanya uchunguzi na kugundua kuwa silaha waliyokutwa nayo majambazi ni mali yake," alisema bila ya kufafanua chochote.


Vyanzo vya habari kutoka ndani ya jeshi la polisi vilisema kuwa Manyika alikamatwa Julai 9 mwaka huu akiwa kazini Ngorongoro, baadaya kubainika kuwa silaha hiyo ilikuwa mali yake.

Habari ziliendelea kusema kuwa Manyika ambaye ni dereva wa gari kubwa la FFU anamiliki silaha aina ya shotgun namba A 947514 M – Pump Action iliyotengenezwa Marekani.


Siku ya tukio la kuuawa kwa majambazi hao watatu ambao walikuwa wakitumia gari aina ya Toyota Corolla lenye namba za usajili T 762 CWE, walikuwa wanakwenda kupora fedha katika kampuni ya Arusha Ceramic Centre inayojishughulisha na utengenezaji wa vigae.

Majambazi hao waliuawa Julai 4 mwaka huu saa 10:20 jioni jirani na Kiwanda cha Bia (TBL) eneo la Njiro Jijini Arusha na silaha hiyo ilikuwa na risasi tatu.


Majambazi hao walitambuliwa kwa majina ya Selemani Walii(25) mkazi wa Kaloleni Jijini Arusha, Walter John (30) na mdogo wake Fred John (21) wote wakazi wa Sekei wilayani Arumeru mkoani Arusha.

CHEKA APANDISHWA KIZIMBANI

Baada ya tuhuma zakumdunda meneja wake, hatimaye bondia wa ngumi za kulipwa anayeshikilia mkanda wa WBF, Francis Cheka, amepandishwa kizimbani katika mahakama ya hakimu mkazi mkoa wa Morogoro, akikabiliwa na shtaka la shambulio la kudhuru mwili na kujeruhi.

Cheka amefikishwa kwa mara ya kwanza katika mahakama ya hakimu mkazi mkoa wa Morogoro, na kusomewa shtaka, na mwendesha mashtaka wa polisi, Aminata Mazengo, mbele ya hakimu wa mahakama hiyo Said Msuya, akidaiwa mnamo julai 02 mwaka huu, bila halali na akijua kufanya hivyo ni kosa kisheria, amempiga kwa ngumi maeneo ya kichwani na tumboni, Bahati Kabanda maarufu kama Masika, na kumsababishia maumivu makali.

Cheka anadaiwa kutenda kosa hilo kwa kabanda ambaye alikuwa ni meneja wa baa yake ya Vijana Social iliyopo sabasaba katika manispaa ya Morogoro baada ya kudaiwa kutoridhishwa na mahesabu ya mauzo, ambapo mahakama ilitoa masharti ya dhamana, ikimtaka kuwa na wadhamini wawili kwa kila mmoja kuweka dhamana ya maandishi ya shilingi milioni moja, ama aende rumande, taratibu za dhamana zilikuwa zikiendelea.

WATU 20 WANAOCHOCHEA MAUAJI AFRIKA YA KATI

Shirika la kupigania haki za kibinadamu lenye makao yake mjini Washington Marekani Amnesty International limewataja watu 20 inayowatuhumu kwa kuendeleza mauaji ya kimbari katika jamhuri ya Afrika ya kati CAR.


Viongozi wa kadhaa wa makundi ya waasi pamoja na marais wawili wa zamani wamo katika Orodha hiyo ambayo Amnesty International inasema ndio wanaochochea kufadhili na kuendeleza mauaji ya halaiki nchini humo.

Aliyekuwa rais wa taifa hilo Francois Bozize aliyeng'olewamadarakani na kundi la wapiganaji wa Seleka chini yauongozi wake Michel Djotodia, mwezi Marchi mwaka uliopita pamoja na Djotodia mwenyewe wametajwa.


Djotodia aliyeongoza makundi ya waislamu wachache(Seleka) alishurutishwa kunga'atuka madarakani na viongozi wa mataifa jirani mapema mwaka huu, lakini kuondoka kwake kukaibua changamoto nyengine kwani sasa makundiya wapiganaji wafahamikao kama Anti-Balaka walianza kuwavamia na kuwauwa Waislamu ambao walidaiwa kuwaunga mkono wapiganaji wa Seleka.


Robo ya idadi ya wananchi wa taifa hilo milioni 4.6 walilazimika kutoroka makwao kuepuka mapigano

Katika Ripoti hiyo yenye kichwa '' Time for Accountability'' Amnesty inasema kuwa viongozi hao wanaoongoza mauaji hayo hawana uwoga wowote kuwahuenda wakachukuliwa hatuana mtu yeyote kwa serikali yataifa hilo ni hafifu sana kwa sasa.


Aidha kuweko kwa zaidi ya maafisa elfu 7 wa kulinda amani nchini humo hakujasaidia chochote kwani kwa sasa vita vimekuwa kuuwa na kulipiza kisasi.

Kwa mujibu wa Christian Mukosa jumuiya ya mataifa inapaswa kuwachukulia hatu kali wale waliotajwa kwani nawao pia wamewanyika amani watu wa jamhuri ya Afrika ya kati.


Amnesty imemtaja kiongozi wa kijeshi wa kundi la Seleka Nourredine Adamkuwa mtuhumiwa mkuu wa visa vya mauaji,ubakaji na mauaji ya halaiki yaliyotokea kati ya Desemba mwaka wa 2012 hadi Januari mwaka huu.Kundi hilo bado linadhibiti kaskazini mwa taifa hilo ambako Amnesty inetrnational inadai visa vya ukiukaji wa haki za kibinadamu vinaendelea kwa kulipiza kisasi dhidi ya watu wasiokuwa wakislamu.


Kwa Upande wa Anti Balaka, Amnesty International imeonya kuwa kundi hilo silo lile lililodhaniwa kuwa ni kundila vijana bali sasa limegeuka na kuwa kundi lenye uwezo mkubwa kijeshi na kuwa linajumuisha wanajeshi aliokuwa wakihudumu wakatiwa enzi za uatawala wake aliyekuwa rais wa taifa hilo Francois Bozize.

Aidha Anti Balaka imewalazimisha waislamu wengi kutoroka mji mkuu wa Bangui ambapo wengi waliuawa.


Kwa sasa Amnesty International inasema kuwa shirika la Umoja wa mataifa linaloshughulikia maslahi ya wakimbizi linaendelea kuwahamisha waislamu kutoka maeneo chini ya Anti-Balaka na kuwapelekea maeneo chini ya utawala wa Kundi la Seleka ambapo wanakubalika.


Vilevile Kidole cha lawama kimewaelekea wanajeshi wa kulinda amani kutoka Chad ambapo Amnesty inasema kuwa waliwauawa wakaazi wa mji wa Bangui mwezi Machi.

Rais wa serikali ya mpwito Catherine Samba-Panza, ameiomba mahakama ya jinai ICC kuchunguza tukio hilo.

TANZANIA NA ALGERIA KATIKA UBIA WA GESI

TANZANIA na Algeria zinakamilisha majadiliano ya kuanzisha kampuni ya ubia, itakayohusika na ujenzi wa miundombinu ya kusambaza umeme.


Pia, itaanzishwa kampuni ya ubia ya kujenga mtambo wa kusindika gesi ya majumbani (Liquefied Petroleum Gas-LPG) na kuiuza kwawananchi kwa kutumia mitungi.

Makubaliano hayo yamefikiwa katika ziara ya kikazi ya Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo na ujumbe wake nchini humo.


Ziara hiyo ya waziri, inalenga kufuatilia utekelezaji wa makubaliano ya awali ya kushirikiana katika kubadilishana uzoefu kwenye masuala yanayohusu sekta za nishati na madini, kutokana na Mkataba wa Makubaliano ya ushirikiano uliosainiwa Desemba 2 mwaka jana nchini humo.


Kwa mujibu wa makubaliano katika mkutano baina ya Mawaziri wa Nishati na Madini wa Tanzania, Profesa Muhongo na wa Nishati na Migodi wa Algeria, Youcef Yousfi, Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) na la Algeria (KAHRIF) yameagizwa kukamilisha majadiliano ya ujenzi wa miundombinu ya kusambaza umeme.


Aidha mawaziri hao wenye dhamana ya nishati na madini, waliagiza kampuni za mafuta na gesi, likiwemo Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC), kukamilisha majadiliano yakuanzisha kampuni ya ubia ya kujenga mtambo wa gesi na kuuza gesi hiyo kwa wananchi kwa kutumia mitungi. TPDC pamoja na kampuni za mafuta na gesi za Algeria ambazo ni Naftal na Sonatrac, zimeambiwa kampuni zote za ubia zinatakiwa kuanza kazi ifikapo Januari mwakani.

Katika ziara hiyo, Waziri Muhongo na ujumbe wake wamepata nafasi ya kutembelea mtambo wa kufua umeme wa kutumia gesi asilia wa Hamma, ambao unamilikiwa na serikali ya nchi hiyo kwa asilimia 100.


Mtambo huo una uwezo wa kuzalisha megawati za umeme 418, na uwezo wa kutumia mafuta ya dizeli na gesi kwa nyakati tofauti.

Miongoni mwa maofisa walioongozana na Waziri Muhongo ni pamoja na Kamishna Msaidizi wa Nishati anayeshughulikia masuala ya umeme, Luoga na wataalamu kutoka Wakala wa Jiolojia Tanzania (GST), TPDC na Tanesco.

IDADI YA MAKANISA KUDHIBITIWA

Bunge la waakilishi nchini Burundi, limepitisha mswada unaodhamiria kupunguza ongezeko la makanisa nchini humo.


Utafiti wa serikali uliofanywa mwaka jana, ulipata madhehebu 557 ya waumini wa kikristo wanaofanya ibadazao nchini humo.

Sheria hiyo mpya itahitaji makanisa kuwa tu na waumini 500 pamoja na jengo nzuri linalotumiwa kama kanisa.


Makanisa ya kiivanjelisti, yalianza kuongezeka kabla nabaada ya vita vya wenyewe kwa wenyewe ambavyo vilimalizika 2005 ambapo karibu watu 300,000 waliuawa.


Mwandishi wa BBC mjini Bujumbura, Prime Ndikumagenge, anasema kuwa mswada huo uliungwa mkono na wabunge wote katika bunge la waakilishi na huenda usipingwe utakapowasilishwa kwa baraza la Senate.

Ikiwa hautafanyiwa mabadiliko yoyote, mswada huo utahitajika kutiwa saini na Rais ishara ya kuudhinishana kuufanya sheria mpya katika siku 30, la sivyo urejeshwe kwa bunge la waakilishi kurekebishwa.


Pindi itakapotiwa saini, makanisa yatapewa mwaka mmoja kufuata sheria hiyo na masharti mapya.

Kwa kanisa la kigeni kusajiliwa , lazima wamiliki kuonyesha kuwa iliwahi kuwana waumini 1,000.

'Kashfa makanisani'

Ni jambo la kawaida kuona waumini wakiwa wamepiga kambi kando ya barabara katika mahema wakifanya ibada siku za Jumapili.

Mtu yeyote anaweza kujitangaza kama muhubiri na kumekuwa na kashfa kadhaa zikihusisha kanisa ndogo ndogo.

Baadhi ya wahubiri wametuhumiwa kwa kuwanyanyasa waumini.


Kuna kisa kimoja ambapo muhubiri aliwaambia wanawake wasio na uwezo wa kushika mimba kulala naye ili awazalishe.


Idadi kubwa ya watu nchini Burundi ni wakristo, wakati wengine wanafuata itikadi za kitamaduni.


Wakati wa mjadala kuhusu swala hilo bungeni, mbunge mmoja kwa jina Jean Minani, aliwatakia waumini wenye imani ambazo sio za kidini kuruhusia kuabudu watakavyo.

Lakini waziri wa mambo ya ndani alipuuza imani hizo na kuzitaja kama za kijadi na zisizokubalika.


Rais wa Burundi Pierre Nkurunziza - ambaye zamani alikuwa muasi, alichaguliwa kama Rais mwaka 2005 na ni mlokole huku mkewe akiwa muhubiri katika kanisa la kiivanjelisti.

CHINA YAIPATIA SUDAN KUSINI SILAHA

Inaripotiwa kuwa China imetuma silaha zenye thamani ya dola milioni 38 nchini Sudan Kusini licha ya nchi hiyo kukabiliwa na mzozo ambao huenda utaitumbukiza katika baa la njaa.

Nyaraka zilizogunduliwa na wataalamu wa masuala ya ulinzi zinaonyesha kuwa makombora, bunduki za rashasha na risasi viliwasili nchini Sudan Kusini mwezi uliopita kupitia bandari ya Mombasa nchini Kenya.


Wanadiplomasia wanakadiria kuwa Sudan Kusini inatumia mamilioni ya dola kwa ulinzi.


Kwingineko, muungano wa ulaya umewawekea vikwazo viongozi na kupiga tanji mali ya wakuu wa kijeshi wa nchi hiyo kwa tuhuma za kukiuka makubaliano ya kusitisha vita ambayo yangeleta mazingira ya amani na kuziia mauaji ya maelfu ya wanachi.


Baraza la Muungano huo, halikuwataja wawili hao katika taarifa yao wala kutajapande wanazounga mkono.

Marekani imechukua hatua sawa na hizo dhidi ya viongozi kutoka pande zinazo zozana.


Vita vilizuka mjini Juba Disemba mwaka jana kati ya serikali na wapiganaji wa aliyekuwa makamu wa Rais Riek Machar.


Mgogoro huo bila shaka umetonesha kidonda katika taifa hilo changa zaidi duniani tangu kujitawala mwaka 2011.

MAJASUSI WA MAREKANI WAWATIA HASIRA WAJERUMANI

Hofu zimeanza kutanda kwenye ulimwengu wa kidiplomasia kwamba mahusiano ya kijadi kati ya Marekani na Ujerumani yanazidi kuathirika, kutokana na kashfa nyengine ya ujasusi wa Marekani dhidi ya Ujerumani.

Katika siku ya pili ya majadiliano mjini Washington, ujumbe wa bunge la Ujerumani umesema kwamba kashfa hii mpya ya ujasusi inaweza kusababisha mgawanyiko wa kudumu kati ya washirika hao wawili.


Akizungumza na waandishi wa habari katika jengo la ubalozi wa Ujerumani mjini Washington, mwenyekiti wa kamati ya mambo ya nje ya Bunge la Ujerumani, Norbert Roettgen, ameonya juu ya kile alichokiita "mgogoro wa chini kwa chini" kati ya nchi yake na Marekani.


Roettgen amewaambia waandishi hao kadhia hizi mbili zimesababisha madhara makubwa sana kwa mahusiano kati ya nchi yake na Marekani, na kwamba haoni dalili yoyote ikiwa Marekani itabadili msimamo wake hivi karibuni.

Ujerumani inataka Marekani isaini makubaliano ya kutokufanyiana ujasusi, lakini Roettgen amesema hilo "si jambo lenye uhalisia" kwa Marekani.


*Marekani yataka mazungumzo

Hata hivyo, msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Ujerumani, Martin Schaefer, amesema kwamba tayari Marekani imeonesha nia ya kulizungumzia suala hili kwa upana zaidi. "Balozi wa Marekani ameelezea nia ya kuzungumzia maswali haya na mwakilishi wa Wizara yetu ya Mambo ya Nje, nasi pia tulitaka kuzungumza naye," alisema Schaefer.


Ujumbe huo wa Bunge la Ujerumani, Bundestag, uko nchini Marekani kujadiliana hatima ya mahusiano kati ya pande hizo mbili,chini ya kivuli cha ukosefu wa kuaminiana uliozushwa na kashfa hizo za ujasusi.


Mjini Berlin, wizara ya ulinzi ya Ujerumani imeanzisha uchunguzi wa pili wa ujasusi, baada ya wiki iliyopita kukamatwa kwa mfanyakaziwa Shirika la Usalama wa Ndani (BND) akishukiwa kuitumikia pia CIA. Msemaji wa wizara hiyo, Kanali Uwe Roth, amethibitisha kufanyika kwa uchunguzi huo.


"Ninaweza kuthibitisha kwamba kuna uchunguzo wa Ofisi ya Mwendesha Mashitaka Mkuu wa Serikali ya Shirikisho ambao uko chini ya wizara ya ulinzi. Siwezi kusema mengi zaidi lakini naweza kuwaambia kwamba tunaichukulia kesi hii kwa umakini mkubwa," Roth aliwaambia waandishi wa habari.


*CIA haikumfahamisha Obama

Gazeti la New York Times linasema hata Rais Barack Obama hakujulishwa na CIA juu ya kadhia hii, ingawa alifanya mazungumzo kwa njia ya simu na Kansela Angela Merkel wa Ujerumani siku ya tarehe 3 Julai.


Kwa mujibu wa gazeti hilo, hivi sasa maafisa wa Ikulu ya Marekani wanahaha kumsaka afisa wa CIA aliyekuwa dhamana wa kadhia hiyo kujua ni kwa nini hakuijulisha Ikulu hiyo.

Ujumbe wa bunge la Ujerumani ulio Marekani tayari umeshakutana na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje, Victoria Nuland, na mwenyekiti wa Kamati ya Ujasusi ya Senate, Dianne Feinstein.


Binafsi Feinstein anatafautiana sanana CIA, ambayo mapema mwaka huu aliituhumu kwa kuingilia uchunguzi wa bunge juu ya programu ya uwekaji kizuizini na kuwahoji washukiwa chini ya utawala wa George Bush.

ISRAEL YAZIDISHA MASHAMBULIZI GAZA

Watoto watano wa kipalestina ni miongoni mwa watu 21 waliouwawa katika mashambulizi ya leo ya angani yanayofanywa na Israel katika ukanda wa Gaza, hii ni kulingana na wataalamu wa afya katika ukanda huo.


Vifo hivyo vimeongeza idadi ya watu waliouwawa kufikia 80 tangu Israel ilipoanzisha mashambulizi ya angani siku ya Jumanne, dhidi ya Ukanda wa Gaza.

Akizungumza na shirika la habari cha AFP msemaji wa huduma za dharura Ashraf al-Qudra amesema katika shambulizi la hivi karibuni mtoto wa miaka mitano aliuwawa wakati bomu kutoka Israel lilipofyetuliwa Kaskazini mwa Ukanda wa Gaza, katika mji wa Beit Lahiya.


Aidha mauaji mengi zaidi yalishuhudiwa katika mji wa Khan Yunis ambapo mkahawa mmoja ulishambuliwa wakati watu walipokuwa wakiangalia mechi ya kombe la dunia kati ya Argentina na Uholanzi, watu wanane waliuwawa huku wengine 15 wakijeruhiwa.

Saa moja baadaye ndege mbili za kivita za Israel zikashambulia nyumba mbili katika mji huo huo wa khan Yunis na kusababisha mauaji ya wanawake wanne na watoto wanne.


*Ban Ki Moon alaani Mashambulizi ya Mashariki ya Kati

Hata hivyo mpaka sasa hapajakuwepo na mauaji yoyote ya raia wa Israel lakini Hamas imezindua mawimbi ya makombora, katika maeneo kadhaa nchini Israel.


Kwa upande wake Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki Moon anayetarajiwa kulihutubia baraza la usalama la umoja wa mataifa juu ya mgogoro wa Mashariki ya Kati, amelaani mashambulizi ya angani huku akiihimiza Israel kusimamisha mashambulizi.

"Kwa mara nyengine tena nalaani mashambulizi ya angani yanayofanywa na Israel katika ukanda wa Gaza, mashambulizi kama haya hayakubaliki na ni lazima yasimamishwe, pia namuomba Waziri Mkuu Netanyahu kusimamisha mashambulizi na kuheshimu majukumu ya kimataifa ya kulinda raia," alisema Ban Ki Moon.


Naye balozi wa Palestina katika Umoja wa Mataifa awali alisema Baraza hilo la usalama la Umoja wa mataifa linajikokota kushughulikia mgogoro unaoendelea.


Huku hayo yakiarifiwa Misri imefungua mpaka wake wa Rafah ilikuwapokea raia wa palestina waliojeruhiwa.

Hospitali Kusini mwaeneo la sinai linalopaka na Gaza pamoja na Israel zipo tayari kuwapokea raia hao waliojeruhiwa. Hii ni kulingana na shirika la habari la Misri MENA.


Mshindi wa tuzo la amani la Nobel Desmond Tutu pia ameongeza sauti yake katika mgogoro huu wa Mashariki ya kati na kusema viongozi wa Israel na Palestina wanabidi kuacha kulaumiana kama watoto katika mgogoro wa muda mrefu kati ya nchi hizo mbili.

KATIBU MWENEZI CCM ATUPWA JELA MWEZI KWA KUDHARAU MAHAKAMA

ZIARA ya Makamu Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Taifa, Philip Mangula mkoani Kigoma, imemponza Katibu Mwenezi wa chama hicho Wilaya ya Uvinza mkoani hapa, Majaliwa Zuberi na kujikuta akitupwa jela mwezi mmoja.


Zuberi, alihukumiwa kifungo hicho na Hakimu wa Mahakama ya Mwanzo, Kata ya Nguruka, wilayani Uvinza, William Mugisa kwa kosa la kudharau mahakama.


Inaelezwa kuwa wakati mahakama ikiendelea na shughuli zake jana asubuhi, Zuberi alikuwa akifanya maandalizi ya kumpokea Mangula kwenye ukumbi wa CCM Social Hall ambao uko karibu na mahakama hiyo, kwa kupiga nyimbo za kukisifu na kukipamba chama hicho.


Kutokana na kitendo cha kupiga muziki kwa sauti ya juu, Hakimu Mugisa aliagiza akaitwe katibu huyo na kumtaka akazime nyimbo hizo kutokana na kuingilia shughuli za mahakama na kumpa dakika tano akatekeleze, lakini aliporejea ukumbini aligoma.


Kutokana na kukaidi amri hiyo, Hakimu Mugisa aliagiza askari wakamkamate na kumpandisha kizimbani na kukumbana na adhabu hiyo ya kwenda jela mwezi mmoja kutokana na kuidharau mahakama.

MSICHANA AKUTWA NDANI YA SANDUKU LA CHIPS

Kituko hiki kilitokea huko pandeza Yombo Vituka Dar-Es-Salaama mchoma chips kama kawaida baada ya kumaliza biashara yake alifunga kabati lake kwa kufuli na kwenda kulala.

Cha kushangaza alivyo amka asubuhi na kuja kufungua kabati lake, alikuta huyu dada kalala ndani ya kabati akiwa hajitambui na bila hata kula mabaki ya chips na mishkaki kama unavyoona.

Kitu kilicho waacha majirani midomo wazi wasijue la kufanya.

Na hadi sasa bado haijajulikana aliingiaje ndani ya kabati hilo lamuuza chips kwani aliondoka bila hata kusema chochote.


Chanzo: Dsm Yetu

KAMATAKAMATA YAIBUKA ZANZIBAR

Kumeibuka kamatakamata ya watu wanaotuhumiwa kuhusika na milipuko ya mabomu katika maeneo mbalimbali ya Mji wa Zanzibar na baadaye wahusika husafirishwa nyakati za usiku kwenda Tanzania Bara, imefahamika visiwani humu jana.


Madai hayo yametolewa na familia za watu hao wakati walipozungumza na waandishi wa habari Kikwajuni Welesi mjini hapa na kudai watu kadhaa wameshakamatwa na kusafirishwa kwa ndege chini ya ulinzi mkali.

Aisha Othman mkazi wa Tomondo, alisema mume wake Hassan Bakar Suleiman alikamatwa usiku wa manane akiwa amelala.


"Niliwasikia watu usiku wakiita jina la mume wangu na kumtaka atoke nje kwamba ana wageni wake, tulipochungulia dirishani tulibaini kuwa ni polisi waliokuwa na silaha,"alisema Aisha.

Anasema mume wake aligoma kutoka kwa kuhofia usalama wake, lakini alikubali baada ya kushawishiwa na jirani yake ambaye naye aligongewa mlango na polisi hao.


Aisha alisema Naibu Sheha alitumika kumshawishi mume wakeatoke nje kwa kumuhakikishia usalama wake lakini alipotoka alitiwa pingu na kuingizwa katika gari la polisi.


Swalha Hamid Hemed naye alisema mume wake, Nassor Hamad Abdallah na mke mwenzake, Salma Khamis walisema mume wao alichukuliwa usiku kwa kishindo kilichoambatana na kupigwa risasi hewani.


Mke mwengine wa Nassor Abdallah, Salma Khamis, mkazi wa Tomondo alisema askari hao walifika nyumbani kwake wakimtafuta mume ambaye hakuwapo wakati huo.


"Baada ya kumkosa, walimchukua mtoto wao Hamad Nassor na kumpeleka Makao Makuu ya Polisi Zanzibar," alisema Khamis.


Watu wengine wanaodaiwa kukamatwa ni Naasor Hamad Mpendae, Said Salum (Kwarara), Said Kassim (Kikwajuni), Hassan Bakari (41), Hussein Bakari (41) wakazi wa Tomondo, Salim Ali Salim (Kiembe Samaki), Muhamed Isihaka (Tomondo), Rashid Ali Nyange (Kibweni) na Antar Humud (Kiembesamaki).


Naibu Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai Zanzibar, Yussuf Ilembo alikiri jana kukamatwa kwa watu hao.

NIGERIA WAFUNGIWA NA FIFA

Nigeria imepigwa marufuku ya kushiriki mashindano yeyote ya kandanda yanayoandaliwa na shirikishola soka duniani FIFA.


Hatua hii imeafikiwa baada ya maafisa wa serikali kuwaondoa wasimamizi wa shirikisho la soka nchini Nigeria NFF ofisini.

Marufuku hii inamaanisha hakuna klabu yeyoye ya soka nchini Nigeria inaweza kushiriki mashindano yeyote ya Kimataifa.


FIFA ilikuwa imeionya Nigeria kuwa ingeichukulia hatua ifikiapo Jumanne kama Shirikisho la NFF halijarejeshewa madaraka yao lakini Serikali ikapuuza makataa hayo.


Mwishoni mwa juma Serikali ya Nigeria ilikuwa imemteua afisa mshikilizi kuongoza shirikisho hilo hadi uchaguzi wa huru na wa haki utakapofanyika kulingana na taarifa ya wizara ya michezo.

FIFA katika taarifa imeonya kuwa marufuku hiyo itaondolewa tu iwapo maafisa waliochaguliwa watarejeshwa mamlakani.


Marufuku hiyo itaathiri timu ya taifa ya Super Eaglets ya wasichana wasiozidi umri wa miaka 20 ambayo inapaswa kushiriki mchuano wa kombe la dunia iwapo marufuku hiyo haitaondolewa ifikapo juma lijalo.(Julai15


Msemaji wa serikali hata hivyo alisema kuwa hatua iliyochukuliwa dhidi ya NFF ilifuata kanuni kwani hata kiongozi wa shirikisho la soka la Nigeria Aminu Maigari alikamatwa na polisi punde baada ya kurejea nyumbani kutoka Brazil.


Mahakama ya Nigeria ilikuwa imeamua kuwa Maigiri hakuwa anastahili kuendelea kuiongoza NFF haswa baada ya matokeo duni huko Brazil.


Wajumbe wa NFF waliafiki kauli ya mahakama ya kumn'goa mwenyekiti huo madarakani lakini lakini kwa sasa erikali ya Nigeria inasubiri mawasiliano kutoka FIFA baada ya kutuma ithibatiya mkutano maalum uliofanyika na wajumbe wa shirikisho la soka la NFF.


Mabingwa hao wa Afrika walishindwa katika mkondo wa pili wa kombe la dunia na Ufaransa.


Hiyo ilikuwa ni mara ya tatu kwa timu hiyo kufuzu kwa mkondo wa pili baada ya kufuzu mwaka wa 1994 na 1998.

AL SHABAB WASHAMBULIA IKULU

Ikulu ya Rais iliwahi pia kushambuliwa mwezi Februari


Vikosi vya serikali Somalia vimefanikiwa kuidhibiti upya ikulu ya rais katika mji mkuu Mogadishu baada ya wapiganaji wa Al Shabaab kuishambulia.

Maafisa wanasema washambuliaji wapatao watano kutoka kundi la al-Shabab - waliuawa walipoingia katika eneo la ikulu hiyo.


Washambuliaji hao wanadaiwa kulipua bomu lililotegwa kwenye gari karibu na langu kuu la Ikulu hiyo.

Waziri wa habari wa Somalia Mustaf Dhuhulow


Waziri wa habari na mawasiliano wa Somalia Mustaf Dhuhulow ameambia BBC kuwa tayari mmoja wa washambuliaji hao amekamatwa na anahojiwa na polisi.

Waziri Mustaf amesema, '' Walishambulia ikulu ya rais saa za jioni. Alikuwa watu washambuliaji watatu pamoja na dereva wao.

Washambuliaji hao waliuawa lakini dereva wao alipata majeraha madogo na anazuiliwa na polisi na kuhojiwa.

Walijaribu kuvamia Villa Somalia lakini wakakomeshwa. Tutawapa maelezo zaidi baadaye. Na tutaweza kutoa maelezo zaidi kwa raia wa Somalia na dunia nzima.''

Shambulio la Al shabaab Mogadishu


Hii ni mara ya pili kwa Al Shabaab kuvamia ikulu ya rais mjini Mogadishu mwaka huu japo mara ya kwanza walifanikiwa kuingia ndani.

Rais Hassan Sheikh Mohamoud hakuwepo wakati wa shambulio hilo.

Kundi la wapiganaji wa kiislamu Al shabaab limefukuzwa kutoka mjini Mogadishu tangu mwaka wa 2011 lakini limekuwa likifanya mashambulio ya kuvizia tangu wakati huo.

Wanamgambo hao wanaaminiwa kufanya mashambulio kadhaa pia katika nchi jirani ya Somalia kama vile Kenya, Uganda na Tanzania kama njia ya kulipiza kisasi kwa kuingia majeshi ya Umoja wa Afrika nchini Somalia.

WANAFUNZI WALIOUA MWALIMU WAHUKUMIWA MIAKA 6 JELA

VIJANA wawili waliokuwa wanafunzi wa Shule ya Sekondari ya Chemchem wilayani Mkalama katika Mkoa wa Singida, wamehukumiwa kifungo cha miaka sita kila mmoja baada ya Mahakama kuwatia hatiani kwa kosa la mauaji ya mwalimu wao. Mahakama Kuu Kanda ya Dodoma inayoendesha vikao vyake mjini Singida, ilitoa hukumu hiyo jana.


Waliohukumiwa ni Shani Mtua na Mohammed Salimu ambao wakati walipotenda kosa hilo, mwaka 2008, walikuwa Kidato cha Tatu na walikuwa na umri wa miaka 18 kila mmoja.


Ilielezwa mahakamani kwamba kulikuwa na washitakiwa wengine wawili katika kesi hiyo; Emmanuel Daud na Michael Msengi, walikufa wakiwa mahabusu wakisubiri kesi yao kusikilizwa na Mahakama Kuu.


Hukumu ilitolewa na Jaji Rehema Mkuye baada ya washitakiwa hao kukiri shitaka la kuua bila kukusudia walilofanya katika Kijiji cha Mpambala, Tarafa ya Kirumi Wilaya ya Mkalama.


Awali, Mwanasheria wa Serikali, Zakaria Elisaria aliyekuwa anasaidiwa na Karen Mrango, alidai mahakamani kwamba washitakiwa walihusika na mauaji ya Rajabu Idude (49), aliyekuwa Mwalimu wa Nidhamu shuleni hapo. Ilidaiwa walifanya mauaji hayo Agosti 2008.


Mwanasheria huyo wa Serikali alidai chanzo cha mauaji hayo ni mshitakiwa wa kwanza , Shani, kupewa barua ya kusimamishwa masomo kwa wiki mbili kutokana nautovu wa nidhamu na kisha akashawishi wenzake watatu kumpiga mwalimu huyo.


Zakaria alisema wanafunzi hao walimvizia mwalimu huyo katika kichaka cha karibu na shule yao wakampiga ngumi na mateke, kisha wakamjeruhi mwilini kwa kisu alichokuwa nacho mshitakiwa wa kwanza.


Inadaiwa kutokana na kipigo hicho, Mwalimu Idude alipiga kelele na mwanawe aliyetajwa kwa jina la Maye Rajabu, alifika haraka kwenye eneo la tukio, lakini akakuta ameshakufa.


Wanafunzi hao (washitakiwa) hawakukutwa katika eneo hilo lakini msako ulifanyika usiku huo na wanafunzi wanne walikamatwa.

Baada ya kuhojiwa kuanzia ngazi ya mlinzi wa amani kwenye kijiji hicho hadi jana mahakamani, walikiri kosa.


Kwa upande wake, Wakili wa washitakiwa, kutoka Kampuni ya Uwakili ya Kim & Company, Raymond Kimu, alimwomba Jaji Mkuye kutoa adhabu nafuu dhidi ya wateja wake, kutokana na kuonesha ushirikiano wa kutosha tangu siku waliyokamatwa. Aidha, alidai washitakiwa walifanya kosa hilo kutokana na kusukumwa na umri mdogo wa utoto.


Alidai ni wakosaji wa mara ya kwanza, wanajutia kosa hilo na kwamba wamekaa jela kwa muda mrefu wa miaka sita, hivyo wamejifunza kutokana na mauaji hayo.


Akitoa hukumu, Jaji Mkuye alisema hakuna ubishi kwa yote aliyosema wakili wa utetezi. Hata hivyo alisema, anadhani sababu hizo siyo kibali kwa washitakiwa hao kupanga na kutekeleza mauaji dhidi ya mwalimu wao aliyekuwa anasimamia nidhamu.


"Nadhani kosa walilofanya haliwezi kukubalika kwa jamii hata kidogo…fujo zimekuwa zikitokea kwenye mashule na vyuo, hata kusababisha vurugu kiasi cha kuathiri utendaji…, kufuatia kosa hili, kila mmoja atatumikia kifungo cha miaka sita jela," alisema Jaji Mkuye.


Chanzo: Habari Leo

WASHINGTON RUHUSA BANGI

Matumizi ya Bangi kwa ajili ya kujiburudisha yamehalalishwa katika jimbo la Washington nchini Marekani.

Washington ni jimbo la pili nchini Marekani kuhalalisha Bangi , baada ya Colorado, ambako jimbo hilo linajipatia mamilioni ya dola kila mwezi kwa kutoza ushuru biashara za Bangi kwa wanaoitumia kujiburudisha.

Hata hivyo utaratibu wa kuuza bidhaa hiyo utadhibitiwa ipasavyo katika jimbo hilo.

Ni maduka 25 pekee yaliyoruhusiwa kuuza Bangi hadi sasa, ingawa maafisa wanaamini kuwa idadi ya maduka huenda ikaongezaka na kufika miamoja.

Katika sehemu zingine za Marekani, majimbo 23 yanaruhusu matumizi ya Bangi kwa sababu za kimatibabu.

MASHAMBULIZI YAZIDI PWANI YA KENYA

Watu wasiojulikana wameteketeza nyumba saba katika eneo la kuhifadhi wanyama mjini Lamu , ingawa hakuna vifo vimeripotiwa katika shambulizi la hivi karibuni.

Washambuliaji walifanya uharibifu mkubwa kwa kuteketeza magari na ofisiTakriban familia 500 zinatoroka na kukimbilia usalama wao katika maeneo jirani ambako mashambulizi mengine mawili yalitokea mjini Lamu na katika eneo la Tana Delta na kusababisha vifo vya watu 29 mwishoni mwa wiki.

Chanzo cha familia hizi kuanza kutoroka makwao kabla hata ya kuwazika jamaa zao, ni swala linalowatia wasiwasi maafisa wakuu.

Wengi walilazimika kulala nje ya gereza la Hindi baada ya kutoroka mashamba yao.

Familia nyingi pia zimepiga kambi nje ya lango kuu la Kambi ya jeshi iliyo karibu na eneo hilo.

Wengi wanahisi kuwa salama katika kambi hizi kinyume na hali ilivyo nyumbani kwao.

Msemaji wa shirika la Red Cross,Waita Wariko, aliambia BBC kuwa watu wengi wameshuhudiwa wakihama makwao kutafuta maeneo salama.

Licha ya hali hiyo, watu hao wameombwa kurejea makwao, lakini hawana imanina polisi hususan kuhusu usalama wao.

Makamu wa Rais William Ruto, aliyezuru eneo hilo Jumapili, alitoa makataa ya saa 48 kwa maafisa wakuu wa usalama kuwasaka washambuliaji , wakiwa hai au wafu la sivyo, wafutwe kazi.

Hakuna mshukiwa hata mmoja amekamatwa mpaka sasa.

Mauaji hayo yamesemekana kuchochewa na swala tete la umliki wa mashamba na kunawasiwasi wa kutokea mashambulizi ya kulipiza kisasi kutoka kwa jamii moja ambayo watu wake wengi walishambuliwa hivi karibuni.

MAMA AKIRI KUWAUA WATOTO WAKE

Mama mmoja amekiri kuwaua watoto wake watatu kwa sababu ya ulemavu wao.

Tania Clarence, mwenye umri wa miaka arobaini na miwili alikiri kosa hilo la kuwaua watoto wake watatu wakiwemo vijana pacha wa miaka mitatu na msichana mmoja mwenye umri wa miaka minne kwa misingi kuwa wanawe walikuwa walemavu mno.

Baba ya watoto hao alikuwa ameenda Afrika Kusini wakatiwa mauaji hayo.

Mama huyo ambaye ametoka eneo la New Malden kusini Magharibi mwa London,alikana kufanya mauaji hayo. Watoto hao ambao walikuwa na ugonjwa wa uti wa mgongo,walipatikana nyumbani kwao tarehe 22 Aprili mwaka huu.

Ugonjwa huo wa kimaumbile husababisha watoto kuwa na uwezo mdogo sana wa kusongesha mwili na pia huwa hawaishi kwa mda mrefu.

Mwanamke huyo alitibiwa kwa majereha aliyoyapata kwa kujikata na baadaye kushitakiwa tarehe ishirini na nne Aprili.

Alizuiliwa katika hospitali ya matibabu ya akili na tarehe ya kesi kupangwa siku ya ishirini na tatu Februari mwaka ujao katika korti iyo hiyo.

8 WAJERUHIWA MLIPUKO ARUSHA

Watu wanane wamejeruhiwa mmoja akiwa hali mahututi kufuatia mlipuko katika mkahawa mjini Arusha Tanzania Mlipuko huo ulitokea Jumatatu jioni na polisi wangali wanachunguza kilichousababisha.

Kwa mujibu wa shirika la habari la AFP, mlipuko huo ulitokea Jumatatu jioni na kuwajeruhi watu wanane huku mmoja akiwa hali mahututi.

Haijulikani kilichosababisha mlipuko huo.

Kufika sasa afisaa mkuu wa shirika la ujasusi nchini humo anakutana na wandishi wa habari. Taarifa zaidi punde tutakapozipata.

WATU WATATU WAMEKUFA KWA MOTO NA KUJERUHI WENGINE 40

Watu watatu wamefariki na wengine zaidi ya 40 wamejeruhiwa wakati gereza moja liliteketea moto magharibi mwa Rwanda, karibu na mpaka wa DRC.

Tukio hili linatokea mwezi mmoja baada ya gereza jengine, Muhanga, kuteketea moto katika jimbo lililopo kusini mwa Rwanda.

Ajali hiyo ya moto imeripotiwa kutokea majira ya jioni (Jumatatu) katika gereza la Nyakiriba, katika wilaya ya Rubavu mpakani naJamhuri ya Kidemokrasia ya Congo.

'Uokozi haukutosha'

Akiongea na BBC kwa njia ya simu mkuu wa wilaya hiyo, Sheikh Hassan Bahame, amesema kuwa juhudi za uokozi zimefanyika haraka ilamahabusu 3 walifariki na wengine 44 kupatwa na majeraha ya moto.

Majeruhi walifikishwa mara moja katika hospitali kuu ya wilaya.

Amesema kuwa kutokana mazingira ya milima ambapo gereza hilo limejengwa, imekuwa vigumu kwa wazima moto kufanya kazi yao kwa wepesi na haraka.

Shekh Bhame ameelezea hasara iliyojitokeza.

'' Hasara kubwa abayo imetokea ni kifocha hawa wafungwa. Na majeraha waliyopata wafungwa wengine. Kuna vituvingi vimeharibika na hatujajua idadi yake bado.''

Sheikh Bahame ametahadharisha kuelekeza lawama la shambulio la kigaidi akisema kuwa japo inatia shaka, ni muhimu uchunguzi zaidi kufanywa.

''Hata sisi tunajiuliza, mbona mambo haya yametokea, na juzi tu yametokea Muhanga?Inatakiwa uchunguzi wa ndani zaidi ufanywe. Lakini uhakika badohatujapata.'' Amesema Sheikh Bahame.

Uchunguzi umeanzisha kujua chanzo cha moto, pamoja na ule moto katika gereza la Muhanga mwezi mmoja uliopita.

WAPIGANAJI WA KIPALESTINA WAUWAWA GAZA

Wanamgambo tisa wa kipalestina wameuawa katikamashambulizi ya angani yaliyofanywa na Israel katika ukanda wa Gaza.


Kundi la Hamas limesema kuwa wapiganaji wake sita waliuawa katika shambulizi moja karibu na eneo la Rafah Kusini mwa nchi hio.


Mashambulizi hayo yanajiri baada ya kurushwa kwa roketi kutoka ukanda wa Gaza kwenda Kusini mwa Israel ambapo wanajeshi watatu waliuawa.


Kundi la wanamgambo la Hamas linasema kuwa wapiganaji wake sita waliuawa wakati wa mashambuzi hayo na wengine watatu kuuawa eneo tofauti.

Hamas wanasema kuwa watalipiza kisasi mauaji hayo.


Hali ya wasi wasi imetanda tangu kuuawa kwa kijana mpalestina Mohammed Abu Khdeir.


Mnamo siku ya Jumapili, polisi waliwakamata washukiwa sita wa kiyahudi kufuatia mauaji ya kijana huyo wakisema kuwa walimuua kwa sababu ya uraia wake.


Taarifa zaidi bado hazijatolewa kwa sababu kesihiyo imebanwa kuzungumziwa.


Mauaji ya Abu Khdair yalitokea kufuatia mauaji ya vijana watatu wa kiyahudi katika eneo la West Bank. Miili yao ilipatikana wiki moja iliyopita.


Israel inasema kuwa wapiganaji wawili wa kipalestina waliwateka nyara vijana hao kisha kuwaua, ingawa Hamas imekanusha kuhusika na mauaji hayo.

WANAUME NA WAVULANA WATOROSHWA PWANI YA KENYA

Idadi kubwa ya watu wameanza kuhama mji wa Hindi, karibu na eneo la Lamu, Pwani ya Kenya.

Mji huo ulishambuliwa na wapiganaji wa Al Shabaab na kuwaua watu 29.


Mashambulizi hayo yametokea chini ya mwezi mmoja tangu mashambulizi mengine kutokea eneo jirani la Mpeketoni ambako zaidi yawatu sitini waliuawa.


Inaarifiwa wakaazi wanawatorosha wavulana na wanaume kwa sababu ya hofu kuwa wao ndio wanalengwa kwa mashambulizi washambuliaji wanapofika kutekeleza mashambulizi.

Wakaazi wanahamia maeneoya Mpeketoni na Malindi kutafuta hifadhi.


Wamelalamikia serikali kwa kukosa kuwapa ulinzi wa kutosha kwani siku moja kabla ya mashambulizi walikuwa wamehakikishiwa usalama wao ingawa kesho yake mashambulizi yakawakuta.


Hata hivyo mkuu wa kaunti ya Lamu, Miiri Njiri, ameiomba serikali kupeleka wanajeshi wa KDF pamoja na polisi wa kupambana na ghasia katike eneo zima la Lamu ili kulinda usalama wa wananchi.


Naibu Rais William Ruto, ametoa makataa ya saa 48 kwa maafisa wakuu wa usalama katika pwani ya Kenya kuwakamata washambuliaji waliofanya mauaji mwishoni mwa wiki Polisi wanalaumu kundi la MRC linalotaka eneo la Pwani kujitenga na Kenya licha ya AlShabaab kukiri kufanya mashambulizi hayo.


Mashambulizi ya Jumamosi yalitokea karibu na eneo la Mpeketoni ambako watu 65 waliuawa mwezi jana , katika mauaji ambayo kundi la Al Shabaab pia lilikiri kuyatekeleza.


Serikali hata hivyo ilidai kuwa mashambulizi hayo yalichochewa kisiasa wala hayakutekelezwa na kundi la Al Shabaab.


Mashambulizi ya mara kwa mara na kudorora kwa hali yausalama katika eneo la Pwanini changamoto kubwa kwa sekta ya utalii ambayo imepata pigo kubwa

AL SHABAB WAMUUA MBUNGE

Wanamgambo wa Al Shabab wamedai kuwa wamemuua kwa kumfyatulia risasi mbunge maarufu mjini Mogadishu.


Ahmed Mohamud Hayd aliuawa baada ya kutoka hotelini ambapo katika tukio hilo, mlinzi wake pia aliuawa na katibu wa Bunge alijeruhiwa,mashuhuda wameeleza.


Kundi la Al-Shabab, ambalo lina uhusiano na al-Qaeda, limeapa kuendelea na mashambulizi zaidi katika kipindi hiki cha mwezi mtukufu wa Ramadhani.


Wanamgambo hao walipoteza ngome yao mjini Mogadishu na kuchukuliwa na Vikosi vya Umoja wa Afrika mwaka 2011,lakini wameendelea kutekeleza mashambulizi ya mabomu namauaji mjini humo.

Msemaji wa kundi hilo Abdulaziz Abu Musab amesema kuwa kundi lake limetekeleza mauaji kama ilivyopangwa na kuwa wataendelea kuwafuatilia Wabunge wengine ikiwa hawataachana na Bunge.


Al-Shabab imekua ikipigania kuunda taifa la kiislamu nchini Somalia.

ACHINJWA MBELE YA MKWE WAKE

MKAZI wa Kijiji cha Mwamkulu wilayani Mpanda, Suzana Kingi (40),ameuawa kikatili na watu wasiofahamika kwa kuchinjwa akiwa katika chumba alicholala, huku mkwe wake akishuhudia.


Kamanda wa Polisi Mkoa wa Katavi, Dhahiri Kidavashari, alisema jana kuwa mauaji hao ya kinyama, yanahusisha imani za kishirikina nayalitokea juzi usiku wa manane nyumbani kwa marehemu katika Kijiji cha Mwamkulu.


Kidavashari alisema usiku huo wa tukio, Suzana alikuwa amelala peke yake nyumbani kwake, jirani na nyumba walimolala wake wa mwanawe, Paul Charles, ambao ni Maria Kanyungiro na Maria Nsabi.


Ilidaiwa kuwa wakati mke wa kwanza, Maria Kayungiro akiwa chumbani kwake, alisikia mama mkwe akikimbia kutoka nyumbani kwake akienda kwenye nyumba walimokuwa wamelala wakweze, huku akipiga mayowe ya kuomba msaada akisema 'mama nakufa .... nakufa... nisaidieni.'

Mama mkwe wake alipofika katika nyumba walimolala wakweze, alisukuma kwa nguvu mlango wa chumba alichokuwa amelala mke wa pili, Maria Nsabi na kuingia chumbani huku akihema kwa hofu na akiendelea kupiga mayowe.


Kamanda Kidavashari alidai kuwa watu hao, ambao hawakufahamika mara moja wakiwa na silaha za jadi yakiwemo mapanga, walikuwa wakimfuata kwa nyuma wakimfukuza.


Inadaiwa wauaji waliingia ndani ya chumba hicho, wakitumia mwanga wa kurunzi na kumkuta Suzana amejilaza na mke huyo wa pili wa mwanawe kitandani.


Kwa mujibu wa madai ya Kamanda Kidavashari, wauaji hao walianza kumshambulia Suzana kwa mapanga na hatimaye kumchinja.

Chanzo: Habari leo

ANYONGWA KWA CHANDARUA NA WEZI

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kagera, Goerge Mayunga Mzee Furgensi Batura (72), Mkazi wa Kijiji cha Nyamiyaga Kata ya Bugomora Wilaya ya Kyerwa mkoani Kagera ameuawa kwa kunyongwa kwa chandarua na wezi nyumbani kwake na kumuibia kahawa.


Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kagera, Goerge Mayunga alisema kuwa mauaji hayo yalitokea usiku wa kuamkia jana baada ya wezi hao kuvamianyumbani kwake na kumkuta nje ya nyumba yake akilinda kahawa na mjukuu wake, Shukuru John (16).


Mayunga alisema baada ya wezi hao kuvamia nyumbani hapo, walimfunga mzee huyo na mjukuu wake kwa chandarua shingoni.


Alisema mzee huyo alikufa baada ya chandarua hicho kumnyonga shingoni na mjukuu wake kunusurika nawezi hao kuiba magunia saba ya kahawa yenye thamani ya Sh. 700,000.


Alisema polisi wanawashikilia Wakazi wawili wa Bugomora na kuendelea kuwasaka wegine kwa tuhuma za mauaji hayo na wizi wa magunia hayo ya kahawa.


Mayunga alisema Spelius Lukokerwa aliyekutwa na kahawa hiyo inayodaiwa kuibwa nyumbani kwake alikufa baada ya kufikishwa kituo cha afya Murongo kutokana na kipigo alichokipata kutoka kwa wananchi.

Chanzo: NIPASHE

BALOZI WA LIBYA NCHINI AJIUA KWA KUJIPIGA RISASI

Msemaji wa serikali hapa nchini Assa Mwambene amekiri kutokea kwa kifo cha Balozi Msaidizi wa Libya nchini bwana Ismail Nwairat kwa kujipiga risasi mwenyewe majira ya saa saba usiku katika chumba cha ofisi za ubalozi huo.


Mwambene alisema kuwa mpaka sasa haijafahamika kifo cha balozi huyo kimetokana na nini, ila wafanyakazi wa karibu katika ubalozi huo wamesema kuwa walisikia mlio wa risasi chumbani kwake, na walipojaribu kufungua mlango ulikuwa umefungwa na wakatumia nguvu ya kuvunja mlango huo na kufanikiwa kumkuta balozi yupo katika haliya mbaya.


Aidha walimuwahisha katika hospital ya Ami iliyopo Oysterbay na baada ya nusu saa madaktari walithibitisha kuwa amefarika dunia.


Serikali imesikitishwa na kifo hicho na wanafanya utaratibu wote wa kuusafirisha mwili wa marehemu kuupeleka nchini kwao kwa ajili ya mazishi.

JESHI LA POLISI LAWASHIKIRIA ASKARI WATATU KWA TUHUMA ZA MAUAJI

Jeshi la polisi kanda maalum ya Tarime na Rorya, linawashilia askari wake watatu kwa tuhuma za kumpiga hadi kumuua kijana mmoja Kitandika Ryoba mkazi wa Sirari, baada ya kumkamata kwa madai ya kumkuta akivuta bangi na kucheza kamali katika eneo hilo la Sirari mpakani mwa Tanzania na Kenya.


Jeshi hilo la polisi limechukua hatua hizo siku chache tu baada ya mamia ya wananchi wa mji huo mdogo wa Sirari kufanya vurugu na maandamano makubwa huku wakichoma tairi za magari katika barabara kuu ya Sirari, Tarime -Mwanza, vurugu ambazo zililenga kulitaka jeshi hilo kueleza chanzo cha kifo cha kijana huyo, anayedaiwa kuuawa kisha mwili wake kwenda kuhifadhiwa katika chumba cha maiti cha hospitali ya wilaya ya Tarime bila ya ndugu na jamaa zake kujulishwa kuhusu tukio hilo.

Kamanda wa polisi wa kanda maalum ya Tarime na Rorya kamishina msaidizi mwandamizi wa polisi Justus Kamugisha, amesema jeshi hilo linawashikilia askari wake hao watatu kwa mahojiano ambao walimkamata kijana huyo kabla ya kuuawa kwa kipigo, wakati jeshi hilo likisubili majibu ya uchungizi wa sehemu ya mwili wa marehemu ambayo yamepekelekwa kwa mkemia mkuu wa serikali.

Wakizungumza katika mazishi ya kijana huyo, ambayo yamefanyika katika mji mdogo wa Sirari,baadhi ya viongozi wa halmashauri ya wilaya ya Tarime na vyama vya siasa, wamewataka askari wa jeshi hilo kubadilika katika utendaji wao wa kazi, kwani wamesema kitendo cha polisi kuua ovyo raia kwa kisingizi kuwa ni watuhumiwa kinachochea chuki kati ya jamii na jeshi hilo.

HOUSE GIRL AMUUA BOSS WAKE KWA KISU

Binti wa kazi za ndani (house girl) anayejulikana kwa jina la Valetina Kerenge (17) amemchoma kisu Bosi wake cha sehemu ya juu ya titi la kulia kwa madai ya kunyanyashwa na tajiri yake huyo.


Kamanda wa polisi Mkoani Singida (SACP) Geofrey Kamwela alisema tukio hilo limetokea jana eneo la Sabasaba Kata ya Utemini Manispaa ya Singida saa 4 asubuhi.


Kamanda Kamwela alimtaja marehemu kuwa ni Asha Juma (24) ambaye ni Karani wa Mahakama ya Wilaya ya Singida.


Baada ya marehemu kuchomwa kisu na msichana wake huyo, alifanikiwa kutoka nje ya nyumba na kukimbilia kwa majirani kwa ajili ya kuomba msaada, lakini wakati majirani wakiwa katika harakatiza kumpeleka hospitali, alianguka chini na kufa papo hapo."Alisema Kamanda Kamwela

MBOWE NA SLAA HAWANA SIFA ZA KUGOMBEA TENA CHADEMA

Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa imesema Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe na Katibu Mkuu, Dk Willibrod Slaa hawana sifa za kugombea tena uongozi wa chama hicho kwa kuwa wanabanwa na katiba yao.


Akizungumza jana ofisini kwake baada ya kuzungumza na Mbowe, Msajili Msaidizi, Sisty Nyahoza alisema walipata malalamiko na kuyafanyia kazi, ikiwa ni pamoja na kupitia kumbukumbu walizonazo na kubaini kuwa kipengele cha ukomo wa uongozi kiliondolewa kinyemela katika katiba ya chama hicho.


Alisema kwa kawaida vyama vyote vinapofanya mikutano huwapelekea muhtasari, hivyo Chadema nacho kiliwapelekea kumbukumbu ya Mkutano Mkuu wamwaka 2006, lakini hakuna sehemu yoyote iliyoondoa ukomo wa uongozi.


"Hivyo, hawa tayari wana vipindi viwili, wakichaguliwa katika uchaguzi unaokuja hatutawatambua. Wakitaka wabadili katiba kwa njia halali ambayo ni ya mkutano mkuu na si vinginevyo," alisema.


Alipoulizwa kuhusu suala hilo, Mbowe alisema hakuwa tayari kulizungumzia, akieleza kwamba amefika kwenye ofisi hiyo ya Msajili kwa masuala mengine.

"Siwezi kulizungumzia suala hilo kwa sasa, likifikishwa kwenye Kamati Kuu ndipo nitalielezea," alisema Mbowe.


Baadaye Ofisa wa Habari wa Chadema, Tumaini Makene alisemakwamba Msajili alimwita Mbowe ili kumshawishi asaidie wajumbe wa Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) warejee katika Bunge la Katiba.


"Mwenyekiti alibainisha kuwa msimamo wa Ukawa upo wazi kwamba hawatarudi katika Bunge hilo hadi pale maoni ya wananchi yatakapoanza kujadiliwa na msimamo huo hautabadilika," alisema Makene akimkariri Mbowe.

Makene alisema baada ya kutoa msimamo huo, hakuna maongezi mengine yaliyoendelea baina ya Mbowe na Msajili.


Alipoulizwa iwapo Msajili alionyesha nia pia ya kuushawishi upande wa pili wanaotaka serikali mbili, Makene alisema hawezi kufahamu, japo kwa nafasi yake, Mutungi ana uwezo wa kufanya hivyo.


Alipoulizwa iwapo Msajili pia alizungumzia suala la ukomo wa uongozi linalodaiwa kubadilishwa kinyemela, alisema:

"Kuhusu hilo Chadema tunafuatilia kwa kina taarifa zinazozagaa zikionyesha correspondence (barua) zinazotoka kwa Msajili wa Vyama juu ya Chadema na tutakapokamilisha tutatoa taarifa."


Gazeti hili jana lilichapisha taarifa iliyonukuu barua ya Msajili wa Vyama vya Siasa, Jaji Francis Mutungi kwenda kwa Katibu Mkuu wa Chadema, ikieleza kuwa kipengele hicho katika Ibara ya 6.3.2 (C) kiliondolewa kwenye katiba bila idhini ya mkutano mkuuwa chama hicho.

Jaji Mutungi alisisitiza kuwa mkuu wa chama hicho ndiye wenye mamlaka ya kurekebisha katiba, hivyo baada ya kupitia muhtasari wa Mkutano Mkuu wa mwaka 2006 suala la kuondoa kipengele cha ukomo wa uongozi halikuonyesha kujadiliwa katika mkutano huo.


Hata hivyo, akizungumza kwa simu juzi, Katibu Mkuu wa Chadema, Dk Willibrod Slaa alisema kipengele hicho kiliondolewa kwa vikao vya chama ambavyo ni wilaya na mkoa.


Hoja hiyo iliwasilishwa na aliyekuwa Mwenyekiti wa ChademaMkoa wa Arusha, Samson Mwigamba na ambaye sasa si mwanachama wa chama hicho.


Chanzo: Mwananchi

AMUUA MPENZI WAKE, NAE AJICHOMA KISU

MKAZI wa Mtaa wa Majengo 'B' mjini hapa, Cesilia Clement (22) ameuawa kikatili kwa kuchomwa kisu mwilini na mpenzi wake, aliyemtuhumu kutomjali baada ya kuwa na mahusiano ya kimapenzi na mwanamume mwingine.


Mtuhumiwa aliyefahamika kwa jina moja la Kanu, ambaye ni mkazi wa Kigoma naye amejijeruhi vibaya kwa kujikata koromeo, alipojaribu kujichinja baada ya kubaini kuwa amemuua mpenzi wake Cecilia.


Pia, mtu huyo anadaiwa kujichoma kisu tumboni. Taarifa kutoka eneo la tukio na zilizothibitishwa na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Katavi, Dhahiri Kidavashari zinaeleza kuwa mtuhumiwa huyo ni mfanyabiashara wa mpunga.


Taarifa hizo zilisema mtu huyo anatuhumiwa kutenda uhalifu huo saa mbili asubuhi nyumbani kwa shemeji wa marehemu, aitwaye Mashaka Hanja katika Mtaa wa Majengo "B" mjini hapa.


Ilidaiwa kuwa katika uhai wake, Cesilia alikuwa akiishi kwa dada yake, ambaye ni mke wa Mashaka Hanja na alikuwa na mahusiano ya kimapenzi na Kanu, ambaye alikuwa amepanga katika nyumba hiyo.


Mashuhuda na majirani wa Mashaka, walidai kuwa siku hiyo yatukio, Cesilia aliamka saa mbili asubuhi na kuanza kufagia uwanja wa nyumba hiyo ya shemeji yake Mashaka.


Inadaiwa kuwa wakati Cecilia akiendelea kufanya usafi katika nyumba hiyo, Kanu alitoka nje ya chumba alichopanga katika nyumba hiyo na kumwita Cesilia, kisha wote wakaingia ndani ya chumba chake.


"Tulimsikia Kanu akimwita Cecilia, kisha tukawaona wote wakingia katika chumba alichopanga Kanu, ndipo ghafla tukasikia Kanu akifokakwa sauti kubwa, akimshutumu Cesilia kuwa siku hizi amekuwa hamjali kabisa, kwa kuwa ana mahusiano na mwanamume mwingine " alidai mtoa taarifa.


Inadaiwa baada ya mabishano ya muda mfupi, wapangaji na majirani walisikia Cesilia akipiga mayowe ya kuomba msaada. Lakini, jitihada zao za kuufungua mlango wa chumba hicho cha Kanu, zilishindwa kwani ulikuwa umefungwa kwa ndani.


"Tulijaribu kumsihi Kanu afungue mlango, lakini alikaidi ndipo tukalazimika kuchungulia dirishani na kushuhudia jinsi Kanu akimshambulia Cecilia kwa kisu, akimchoma sehemu mbalimbali zamwili wake ....huku Kanu akiwa ametapakaa damu mwili mzima " anadai mmoja wa mashuhuda. Kwa mujibu wa Kamanda Kidavashari, askari Polisi walifika eneo hilo la tukio, baada ya kutaarifiwa.


Alisema polisi walikuwa na silaha, ambapo walivunja mlango wa chumba hicho cha Kanu na kuushuhudia mwili wa marehemu ukiwa umelala kwenye dimbwi la damu sakafuni, akiwa tayari mfu.


Ilidaiwa kuwa Kanu naye alikuwa amezirai, baada ya kujijeruhi vibaya shingoni na tumboni kwa kisu, baada ya kubaini kuwa amemuua mpenzi wake.


Kwa sasa Kanu amelazwa katika Hospitali ya Wilaya ya Mpanda, mjini hapa, kwa matibabu akiwa chini ya ulinzi mkali.


Kamanda Kidavashari alidai kuwa mtuhumiwa huyo, atafikishwa mahakamani baada ya kutibiwa na kupona.

Uchunguzi wa tukio hilo bado unaendelea.


Mwili wa marehemu umehifadhiwa katika chumba cha kuifadhi maiti katika Hospitali ya Wilaya ya Mpanda ili ufanyiwe uchunguzi wa kitabibu, kabla ya kukabidhiwa ndugu wa marehemu kwa maandalizi ya maziko yake.

USA KUONGEZA VIKOSI 200 IRAQ

Rais Barak Obama ametangaza kuwa anatuma vikosi 200 zaidi , na pia helikopta zisizoKuwa na ruban nchini Iraq.


Katika barua yake wa baraza la Cogress rais Obama amesema kuwa vikosi hivyo vitatoa msaada wa nyongeza na usala kwa ubalozi mjini Baghdad.


Rais Obama amesema vikosi hivyo vya ziada vimepewa mafunzo kabambe ya kijeshi na majukumu yao makuu yatakuwa kuwalinda raia wa Marekani na mali zao huko Iraq.


Wataungana na wanajeshi wengine wa Marekani walioko Badghad wanaolinda ubalozi wa Marekani.


Katika barua yake kwa bunge la Congress, Obama amaesema amepeleka pia helicopters, na ndege zisizo na rubani kuimarisha ulinzi huo.


Tayari Marekani washapeleka washauri wakijeshi wapatao 180 kufanya kazi na jeshi la Iraq.


Obama kupeleka pia ndege za kivita zisizo na rubani 'drones' huko Baghdad

Hata hivyo idadi ya jumla ya wanajeshi wa Marekani nchini Iraq ni kama 750 pekee.


Huku mapigano yakiendelea kuchacha huko Iraq rais Obama amesisitiza hatapeleka majeshi ya ardhini nchini lakini hatua ya kufanya mashambulizi ya angani dhidi ya kundi la wapiganaji wa ISIS huenda ikachukuliwa.


Wakati huohuo Balozi wa Saudi Arabia katika umoja wamataifa amekana madai ya Waziri mkuu wa Iraq , Nouri Maliki kwamba nchi yake inatoa usidizi wowote kwa kundi la ISIS na pia kupinga nadharia kuwa usaidizi wa Saudia kwa waasi wa Syriaumechangia kuliinua kundi hilo la ISIS.


Tangazo la kundi hilo la ISIS hapo jana kwamba wataunganisha ardhi walizoziteka huko Iraq na Syria ndio waunde eneo mojawanalolitaja kama 'Islamic Caliphate' litakalotawaliwa na sheria kali za kiislamu, liwawatia tumbo joto mataifa mengi ya mashariki ya kati namataifa ya kizungu hasa Marekani.


Kwa kipindi cha mda mfupi ISIS imeweza kushambulia na kuyateka maeneo makubwa kwa kasi iliyowashangaza wengi huku serikali za nchi husika zikishindwa kukabiliana nao.


Kuzuka kwa kundi hili kunaleta tisho jipya katika mashariki ya kati ambayo tayari inayumbishwa na vita na vizozo mbalimbali ya kisiasa.

KOCHA MKUU WA NIGERIA ABWAGA MANYANGA

Kocha wa Nigeria coach Stephen Keshi amejiuzulu wadhfa wake katika timu hiyo.


Keshi amejiuzulu punde baada ya timu ya Super Eagles kuondolewa kutoka kwenye kipute cha kombe la dunia ilipolazwa 2-0 na Ufaransa.


Kocha huyo mwenye umri wa miaka 52 alichukuwa wadhfa huo mwaka wa 2011 na akaiongoza timu hiyo kufutwaa ubingwa wa afrika mwaka uliopita.


Nahodha wa timu hiyo Joseph Yobo aliyejifunga bao la pili la Ufaransa naye pia ametangaza kustaafu.


Hii haitakuwa mara ya kwanza kwa Keshi kujiuzulu wadhfa wakae,mwaka wa 2013 Keshi alikuwaradhi kujiuzulu lakini akashawishiwa kusalia kama kocha na waziri wa michezo wa Nigeria.


Chini ya uongozi wake Super Eagles imefuzu kwa mara ya kwanza katika mkondo wa piliwa kombe la dunia tangu mwaka wa 1998 licha ya kukumbwa na migomo ya mara kwa mara ya wachezaji wake wakidai malimbikizi ya marupurupu yao.


Kuondoka kwake kumefikisha idadi ya wakufunzi waliojiuzulu kufuatia matokeo duni katika kombe la dunia kutimia makocha 6.


Makocha wengine waliondoka ni pamoja na LuisSuarez, wa Honduras, Carlos Queiroz wa Iran's , Alberto Zaccheroni wa Japan , Cesare Prandelli wa italia na Sabri Lamouchi wa Ivory Coast.


Keshi, aliwahi kuhudumu kama kocha wa Mali na Togo.

POLISI WAWILI WAUAWA KWA BOMU KARIBU NA IKULU

Mabomu mawili yamelipuka karibu na Ikulu ya Rais mjini Cairo, nchini Misri na kuwaua maafisa wawili wa polisi.

Bomu la kwanza lilimuua afisa wa polisi na kuwajeruhi wengine watatu.


Bomu la pili lililipuka maafisa wa polisi walipokuwa wanajaribu kulitegua na kumuua polisi mwingine.

Wapiganaji wa kiisilamu wanadaiwa kutega mabomu hayo katika eneo hilo wiki jana.


Shambulizi hili limetokea katika siku ya maadhimisho ya maandamano ambayo yalisababisha jeshi kumpindua aliyekuwa Rais Muhammad Morsi.


Mkuu wa ulinzi wa mjini Cairo ameambia BBC kuwa mkuu wa idara ya kutegua mabomu Generali, Alaa Abdel Zaher, alikuwa miongoni mwa wale waliojeruhiwa.


Wakati huo huo, naibu mkuu wa ulinzi amesema kuwa wataalamu wa kutegua mabomu walitegua mabomu mengine mawili yaliyopatikana nje ya ikulu yaRais. Abdul Fattah al-Sisi.


Hata hivyo ratiba ya Rais Abdul Fattah al-Sisi haikubadilishwa kutokana na mashambulizi hayo.


Mashambulizi ya mara kwa mara yamesababisha vifo vyamamia ya watu wakiwemo maafisa wa usalama tangu Morsi kuondolewa mamlakani tarehe 3 mwezi Julai.


Wapiganaji wa kiisilamu wameongeza mashambulizi katika kujibu operesheni ya kijeshi dhidi ya wanachama wa vuguvugu la Muslim Brotherhood, ambapo zaidi ya watu 1,400 wameuawa na wengine 16,000 kujeruhiwa.

RAIS WA URUGUAY AWATUKANA MAAFISA WA FIFA

Rais wa Uruguay Jose Mujica amewatukana maafisa wa FIFA kwa kuwaita ''kundi la watoto wa Mbwa'' au "a bunch of old sons of bitches".


Hii ni baada ya maafisa wa shirikisho hilo kumpiga marufuku mchezaji wa nchi hiyo Luis Suarez.

Mchezaji huyo aliitaja adhabuhiyo ya marufuku ya miezi minne ikiwemo kutocheza mechi 19 za kimataifa kama adhabu ya kinazi.


Suarez alipata adhabu hiyo ambayo inasemekana kuwa kali sana kuwahi kutolewa katika historia ya kombe la dunia kwa kumuua mchezaji wa Italia Giorgio Chiellini.


Rais Mujica anasifika kwa kutotafuna maneo yake pamoja na ukali wa matamshi yake.


Aliyatoa matamshi yake kupitia televishini ya taifa alipokuwa anawapokea wachezaji wa timu hiyo baada ya kubanduliwa nje ya michuano ya kombe la dunia katika awamu ya muondoano.


Rais huyo alifunika mdomo wake kwa mshutuko wa kile alichosema , lakini wandishi wa habari tayari walikuwa wamemrekodi.

Pia aliwaambia kuyachapisha matamshi yake alipohojiwa ikiwa alitaka kujirekebisha.


Rais huyo alisema kuwa FIFA ilimuadhibu Suarez kwa sababu ya maisha yake ya zamani ambayo yalikuwa ya unyonge.


Pia alitaja adhabu hiyo kama aibu kubwa sana kwa historiaya FIFA.