WATU WATATU WAFIA BAHARINI

Watu watatu mkoani Mtwara wamepoteza maisha kufuatia kuzama kwa mtumbwi waliokuwa wakisafiria katika Bahari ya Hindi kutoka Kitongoji cha Mwale kuja Mtwara Mjini kwa ajili ya shughuli zao za kila siku.

Kwa mujibu wa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mtwara, Zelothe Stephen aliyeongea na waandishi wa habari katika Hospitali ya Rufaa ya Ligula akiwa ameongozana na uongozi wa mkoa, alisema ajali hiyo ilitokea saa 5 asubuhi mita kama 100 kutoka eneo la ufukwe wa kienyeji baada ya mtumbwi waliokuwa wakisafiria kupatwa na misukosuko.

Zelothe alisema ajali hiyo imesababisha vifo vitatu, majeruhi 21 wakiwemo watoto wadogo wawili kati ya mwaka mmoja na kuwataka wananchi kuwa makini na vyombo wanavyotumia kusafiria ikizingatiwa kwa sasa hali ya hewa siyo nzuri kutoka na na mvua zinazoendelea kunyesha.

Aliwataja waliopoteza maisha kuwa ni Mwanahamis Juma (31) na Habiba Masoud (13) wote wakazi waMwalena Rahma Abdul (25) mkazi wa kitongoji cha Ngw'ale.

Naye Mkuu wa Mkoa, Kanali Mstaafu Joseph Simbakalia alieleza kuwa ajali hiyo imesikitisha sana nakwamba kifo hakina matarajio kwani waliokumbwa na mkasa huo walikuwa wakienda kwenye shughuli zao za kila kujitafutia kipato.

Mganga Mkuu wa Hospitali ya Rufaa ya Ligula, Dk Shaibu Maarifa alikiri kupokea majeruhi na maiti za ajali hiyo na kusema kuwa wanawahudumia ipasavyo ili waweze kurudi katika hali zao za kawaida.

Mmoja wa majeruhi walionusirika katika ajali hiyo, Sophia Kassim (28) alimwambia mwandishi wa habari hizi wakati wa mahojiano kuwa mtumbwi waliokuwa wakisafiria ulijaza watu kupita kiasi na kwamba abria wote walikuwa wanawake isipokuwa dereva na msaidizi wake.

NASSARI AUMBUKA BUNGENI

Mjumbe wa Bunge Maalumu la Katiba, Joshua Nassari, juzi alijikuta akiumbuka bungeni baada ya kushindwa kutaja kanuni aliyoitumia, kuomba mwongozo.

Hali hiyo ilitokea muda mfupi kablaya wajumbe kupiga kura za kumchagua Mwenyekiti wa Bunge hilo.

Kuumbuka kwa mjumbe huyo ambaye pia ni Mbunge wa Arumeru Mshariki, kulitokana na Mwenyekiti wa Muda wa Bunge hilo, Pandu Ameir Kificho, kumtakakutaja kanuni aliyoitumia.

Hata hivyo, baada ya kusita kwa muda Nassari bila kutaja kanuni aliyoitumia, alisema wajumbe wengi hawajasikia utaratibu unaotumika katika upigaji kura kwa sababu walichelewa kwenye msongamano wa watu getini.

"Wengi wetu tumeingia tukiwa tumechelewa kwa sababu wengi tunapita katika geti moja. Ningependa ufafanuzi wako kuhusuaina ya kura tunayokwenda kupiga ni ya wazi au ya siri,"alisema.

Hata hivyo, kificho alimjibu kuwa kura zitakazopigwa kumchagua mwenyekiti zitakuwa ni za siri.

Hatua hiyo imekuja muda mfupi baada ya Bunge hilo kupitisha kanuni za uendeshaji wake ambapo hata hivyo nyingine bado zimekuwa na mgongano wa maridhiano kwa baadhi ya wajumbe kutaka ufafanuzi zaidi.

JK AWAAPISHA VIONGOZI BUNGE LA KATIBA

Rais Jakaya Kikwete jana aliwaapisha Katibu na Naibu Katibu wa Bunge Maalumu la Katiba, hali inayoonyesha kuwa kazi ya Bunge sasa imeanza.

Walioapishwa ni Yahaya Hamisi Hamad ambaye anakuwa Katibu na Dk Thomas Kashilila anashika nafasiya Naibu Katibu wa Bunge hilo.

Shughuli za kuapishwa kwa makatibu hao, zilifanyika katika Viwanja vya Ikulu ndogo iliyoko eneo la Uzunguni mjini Dodoma na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali.

Viongozi hao ni Waziri Mkuu Mizengo Pinda, Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Balozi Seif Idd, Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Ombeni Sefue, Mwenyekiti Mteule wa Bunge , Samuel Sitta na Makamu wake Samia Suluhu Hassan.

Baada ya kiapo hicho, Rais Kikwete alikutana na Pinda, Sitta na Suluhu.

Hata hivyo mazungumzo yao yalikuwa ya faragha.

Akizungumzia nafasi yake Katibu waBunge, Yahaya Hamad, alikiri kuwa kazi iliyoko mbele yake ni kubwa lakini ana matumaini makubwa kwamba ataifanya kwa uadilifu mkubwa wa hali ya juu.

Hamad alisema changamoto kubwa anayoiona ni mwingiliano wa masilahi ya wanasiasa kwa sababu wengi wametanguliza misimamo ya vyama.

"Mimi ningewashauri wanasiasa kuacha kila kitu ili tuweze kufanya kazi ya watu iliyotuleta Dodoma, ili tuweze kupata Katiba nzuri itakayodumu kwa muda mrefu. Wanasiasa lazima wakubali kuwa nchi kwanza na vyama baadaye," alisema Hamad.

Kwa upande wake Dk. Kashillilah alisema atatumia uzoefu wake kumshauri na kumsaidia katibu na wenyeviti wa Bunge ili ndoto ya kuwa na Katiba nzuri itimie.Hata hivyo, alikanusha madai kwamba Katiba Mpya haitapatikana kutokana na kelele za wanasiasa.

KIJANA MMOJA AMEKUFA BAADA YA KULIPUKIWA NA SIMU

ALI Bakari Ali (20) mkazi wa Kisima Majongoo mjini Unguja amekufa baada ya simu yake aliyokuwa akitumia ambayo ilikuwa imeunganishwa na chaja ya umeme kupata hitilafu.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mjini Magharibi Unguja, Mkadam Khamis Mkadam alithibitisha kutokea kwa tukio hilo ambapo alisema Ali alikufa baada ya kupata mshtuko wa umeme unaotokana na simu yake iliyokuwa imewekwa katika chaja ya umeme huku akifanya mawasiliano.

"Ni kweli tumepata taarifa ya kifo cha kijana Bakari Ali ambaye alikuwa akisikiliza simu yake iliyokuwa imewekwa katika chaja ya umeme na kusababisha mshtuko mkubwa," alisema.

Kamanda Mkadam alitoa wito kwa wananchi na kuwataka wakati wanaposikiliza simu zao kwanza kuziondoa katika umeme ili kuepusha ajali.

AHUKUMIWA KUNYONGWA MPAKA KUFA

MAHAKAMA Kuu ya Tanzania Kanda ya Sumbawanga imemhukumu Malambi Lukwaja (47) mkazi wa Kijiji cha Igalula Tarafa ya Kabungu Wilaya ya Mpanda Mkoa wa Katavi kunyongwa hadi kufa, baada ya kupatikana na hatia ya kuua kwa kukusudia.

Mshitakiwa alitiwa hatiani na mahakama hiyo kwa kumuua kwa kukusudia Ibrahim Juma (44) mkaziwa kijiji hicho cha Igalula. Inadaiwa alitumia shoka kumchinja kisha kuufukia ardhini mwili wa mdai wake.

Hukumu hiyo ilitolewa jana katika kikao cha Mahakama Kuu kilichofanyika katika mahakama ya wilaya ya Mpanda na Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Sumbawanga, Jaji Kasukulo Sambo.

Awali Mwanasheria wa Serikali wa Mkoa wa Katavi, Njoloyota Mwashubila alidai mahakamani hapo kuwa mshitakiwa alitenda kosa hilo Julai 9 mwaka 2009 katika muda usiofahamika.

Ilidaiwa mahakamani hapo kuwa siku hiyo ya tukio marehemu alimuaga mkewe aitwaye Hamisa Hassan kuwa anakwenda nyumbanikwa mshitakiwa Malambi Lukwaja ili kuchukua magunia yake ya mpunga ambayo alikuwa akimdai ambapo walikubaliana amlipe magunia hayo ya mpunga baada yakuvuna.

Mwanasheria huyo wa Serikali aliieleza mahakama hiyo kuwa tangu siku hiyo alipoondoka marehemu hakurudi nyumbani hivyo kusababisha mke wake apateshaka na kutoa taarifa kwa ndugu wa marehemu juu ya kutoonekana kwake kwa kipindi cha wiki tatu.

Alieleza ndugu wa marehemu walipopewa taarifa hizo waliamua kumfuatilia nyumbani kwa mshitakiwa ambapo aliwaeleza marehemu alifika kwake na alishaondoka nyumbani kwake baada ya majibu hayo ndugu hao waliamua kurudi nyumbani.

Mwashubila alidai kuwa wakati ndugu hao wa marehemu wakiwa wanarudi nyumbani waliitwa na jirani yake na mshitakiwa ambae aliwatahadharisha kutojenga mazoea ya kwenda kwa mshitakiwa kwani kuna mtu mmoja alikwenda hapo na hajaonekana tena.

Alieleza baada ya kuelezwa hivyo ndugu hao walikwenda kutoa taarifa kwenye uongozi wa kijiji na kisha walimkamata mshitakiwa na kumpeleka kituo cha Polisi cha Mpanda.

Mwanasheria huyo aliendelea kueleza baadhi ya wanakijiji walibaki nyumbani kwa mshitakiwa wakiendelea kumhoji mkewe ambae aliwaeleza marehemu siku hiyo aliondoka na mumewe kwenda shamba, lakini kesho yake mshitakiwa alirudi akiwa peke yake na alipojaribu kumuuliza mume alikuwa mkali.

Ilidaiwa mke huyo wa mshitakiwa aliamua kuwapeleka lilipo shamba lao la mpunga na walipofika walishituka kuona kuna eneo limefukuliwa ambapo waliamua kulifukua eneo hilo ghafla waliona miguu ya marehemu ndipo walipotoa taarifa polisi ambao walifika kwenye eneo hilo na kuendelea na ufukuaji mwili wote wa marehemu ukiwa umechinjwa na kiwiliwili chake kutenganishwa na kichwa ambapo kwenye kichaka waliiona baiskeli ya marehemu na nguo zake.


Chanzo: Habari leo

WANAFUNZI DARASA LA SABA WAOANA

MWANAFUNZI aliyehitimu Darasa la Saba mwaka jana, jina tunalo amefikishwa katika Mahakama ya Hakimu wa Wilaya ya Nkasi mkoani Rukwa, kwa madai ya kumuoa msichana waliyekuwa wakisoma naye darasa moja mwenye umri wa miaka 15.

Binti huyo alifanikiwa kupata nafasiya kidato cha kwanza Shule ya Sekondari Chala wilayani Nkasi, lakini ameshindwa kujiunga kwa kuwa ni mke wa mtu. Wawili hao walikuwa wakisoma Shule ya Msingi Kacheche kijijini Kacheche wilayani Nkasi.

Mshitakiwa ambaye kwa sasa ni mkulima katika kijiji cha Kacheche alifikishwa mahakamani hapo jana mbele ya Hakimu wa mahakama hiyo, Ibrahim Mgalamalira ambapo alikana shtaka hilo. Mtuhumiwa alidai kuwa anafahamu kuwa amemaliza elimu ya msingi, lakini hakuwa na taarifa kama alikuwa amechaguliwa kujiunga na elimu ya sekondari mapema mwaka huu.

Awali Mwendesha Mashtaka, Mkaguzi Msaidizi wa Polisi, Hamimu Gwelo alidai mahakamani hapo kuwa mtuhumiwa alimuoa msichana huyo, Februari 24, mwaka huu na kuishi naye nyumba moja kijijini Kacheche kama mume na mke kwa siku sita hadi alipotiwa nguvuni Machi 3, mwaka huu.

"Msichana huyu bado ni mwanafunzi kwa kuwa alichaguliwa kujiunga Kidato cha Kwanza katika Shule ya Sekondari Chala wilayani hapa lakini ameshindwa kuendeleana masomo kwa kuwa alikuwa ameolewa na mtuhumiwa ambaye sasa amemkatisha masomo yake," alidai mahakamani hapo Mwendesha Mashtaka.

Ilidaiwa mahakamani hapo kuwa mshtakiwa alipohojiwa kwa mara ya kwanza kabla ya kufikishwa mahakamani hapo, alikiri kumuoa msichana huyo kwa kuwa alifahamu kuwa ameshamaliza darasa la saba mwaka jana.

Hakimu Mgalamalira aliamuru mshtakiwa arudishwe rumande baada ya kushindwa kutimiza masharti ya dhamana ambayo alimtaka awe na wadhamini wawili wenye mali zisizoweza kuhamishika zenye thamani isiyopungua Sh milioni moja. Shauri hilo limeahirishwa hadi Machi 26, mwaka huu litakapotajwa tena.


Chanzo:Habari leo

ANELKA ATEMWA NA WEST BROM

Ishara aliyofanya anelka ya msanii wa ufaransa M'bala

Mchezaji wa klabu ya soka ya West Brom, Nicolas Anelka amefutwa kazi kwa kosa la utovu wa nidhamu.

Klabu hiyo iliamua kuchukua hatua hiyo baada ya Anelka kutangaza kupitia mtandao wa kijamii kuwa anaacha kazi.

Anelka alisema kuwa anaondoka katika klabu hiyo baada ya kukosa kutatua tofauti zilizopo kati yake na Albion kuhusu ishara yake yenye utata ambayo inasemekana kuwa ya kibaguzi dhidi ya wayahudi.

Mshambuluaji huyo mwenye umri wa miaka 35, alipigwa marufuku kutocheza mechi tano na kutozwa faini ya pauni 80,000 na shirikisho la soka Uingereza,kwa kufanya ishara hiyo, baada yakuingiza bao dhidi ya klabu ya West Ham mwezi Disemba.

West Brom imechukua hatua ya kumfuta kazi Anelka kutokana na ishara hiyo na pia kwa sababu ya matamshi yake kwenye mtandao wa kijamii.

Awali aliachishwa kazi mwa mudana Albion, wakati klabu hiyo ilipokuwa inafanya uchunguzi wake binafsi.

Mapema siku ya Ijumaa, Anelka alitangaza kwenye mitandao ya kijamii kuwa anaondoka katika klabu hiyo.

Aliandika: "kufuatia mazungumzo kati yangu na maafisa wa klabu, kuna masharti kadhaa ambayo wamenipa kabla ya kujiunga tena na klabu hiyo, Masharti ambayo siwezi kuyakubali.''

Hata hivyo klabu ilisema kuwa masharti yaliyotolewa kwa Anelka ni pamoja na kumtaka awaombe msahama mashabiki , wadhamini na jamii kwa ujumla kwa athari iliyotokana na ishara yake aliyoifanya Disemba tarehe 28 na pili akubali kutozwa faini.

MARTINEZ KUMRITHI WENGER

Kocha wa Everton, Roberto Martinez ameanza kufikiriwa na wakubwa wa Arsenal kuwa ndiye chaguo sahihi la kumrithi Arsene Wenger.

Martinez, Mhispania aliyeoa mke Mwingereza alijiunga na Everton akitoka Wigan Athletic walioshuka daraja msimu uliopita, lakini anawavutia sana wadau wa Emirateskwa tabia zake uwanjani na hata nje.

Hata jinsi alivyopokea kipigo cha mabao 4-1 kutoka kwa Arsenal wikiendi iliyopita kwa namna ya kipekee akionesha heshima na utulivu badala ya hasira na fujo, kimemwongezea maksi miongoni mwa wakubwa wa Arsenal.

Hata hivyo, kukubalika huko kwa Martinez hakumaanishi kwamba Wenger anaondoka kesho au keshokutwa, hapana. Wenger anakaribia kuanguka saini kwa ajili ya kuendelea kuwanoa Arsenal kwa miaka mingine miwili.

Hata hivyo, wamiliki na wajumbe wa Bodi ya Wakurugenzi wa Arsenal wameamua kuanza kufikiria mrithi wa Wenger ili wasikutwe na mshangao wakikosa la kufanya ikitokea siku Wenger kweli anaondoka.

Kwa hiyo wamekuwa wakikuna vichwa juu ya nani angeweza kuwa chaguo lao, na jina la Martinez linashika namba moja kwa sasa, wakipendezwa na aina ya soka analowafundisha vijana wake, pasi kama zile ambazo washabiki wa Arsenal wanazipenda na wamezizoea chini ya Wenger.

Kadhalika Martinez ni muumini wa kuhamasisha kuendeleza ukuzaji vipaji kupitia timu za vijana, falsafa ambayo Arsenal wamekuwa nayo kwa muda mrefu na hata nyota waowengi waliowakimbia walikuwa mazao yao.

RWANDA NA A.KUSINI ZALIPIZANA KISASI

Serikali ya Rwanda imesema hatua ya kuwatimua maafisa sita wa ubalozi wa Afrika Kusini mjini Kigali ni ya haki na ilizingatia uchokozi ambao ulianzishwa na serikali ya Afrika Kusini yenyewe kwa kufukuza maafisa watatu wa ubalozi wa Rwanda.

Waziri wa mambo ya nje na ushirikiano wa kimataifa ,Bi Louise Mushikiwabo, kupitia mtandao wa kijamii wa Twitter ameeleza kwamba Rwanda ilikuwa na haki zote kuwafukuza mabalozi wa Afrika Kusini mjini Kigali ikizingatia hatua ambayo nchi hiyo ilianzisha yenyewe kwa kuwatimua maafisa wa ubalozi wa Rwanda mjini Johannesburg.

Katika ujumbe wake mfupi kwenye mtandao huo Bi Mushikiwabo, anailaumu Serikali ya Afrika Kusini kwa kutochukua hatua dhidi ya wanyarwanda waliokimbilia nchini humo ambao serikali ya Rwanda inawatuhumu kuendelea na hujumaza kigaidi dhidi ya Rwanda na kwamba Pretoria haijatekeleza muafaka uliofikiwa awali.

Kulingana na kiongozi huyo kupitia mtandao wa twitter, mahusiano mema kati ya Rwanda na Afrika Kusini yatafikiwa wakati suala la kisheria kuhusu wanyarwanda waliokimbilia nchini humo itapata ufumbuzi.

Wakati haya yakiarifiwa ,mjumbe maalum wa Rais Baracka Obama wa Marekani katika mataifa ya ukanda wa maziwa makuu, Russ Feingold, alisema kuwa Marekani inafuatilia kwa karibu mzozo huo ambao alielezea waandishi kwamba mataifa ya Rwanda na Afrika ya kusini hayana budi kumaliza tofauti zao kwa njia ya kidiplomasia.

Mjumbe huyo alikutana na waandishi wa habari muda mfupi baada ya kukutana na Rais Paul Kagame.

Miongoni mwa wanyarwanda waliokimbilia Afrika ya kusini ni Generali Kayumba Nyamwasa ambaye amekuwa akilaumu utawalawa Rwanda kwa kuhusika na mashambulizi kadhaa dhidi yake ambayo amenusurika.

Kwa upande mwingine Serikali ya Rwanda inakanusha vikali kuhusika na tuhuma hizo.

Kayumba Nyamwasa anajulikana kama mtu aliyetangaza wazi kupiga vita utawala wa Rwanda na anatuhumiwa kuhusika katika mashambulizi ya hapa na pale yanayogharimu maisha ya watu na mali.

WASIWASI WA UDUKUZI FACEBOOK

Mwanzilishi wa Facebook Mark Zuckerberg amesema kuwa amezungumza na Rais Barack Obama kumwelezea kero lake kuhusu udukuzi unaofanywa na serikali kwa mitambo ya Dijital.

Zuckerberg mwenye umri wa miaka 29, amesema kuwa serikali ya Marekani inapaswa kupigia debe internet badala ya kuwa adui wa mitandao ya kijamii.

Matamshi yake yanakuja siku moja baada ya ripoti kuwa shirikala ujasusi la Marekani ilibuni mtandao bandia wa Facebook ili kuweza kuvamia mitambo ya Kompyuta inayotumiwa kwa uchunguzi.

Shirika la NSA lilisema kuwa taarifa hiyo sio ya kweli.

Mnamo mwezi Septemba, Zuckerberg alisema kuwa Marekani ilikosea sana taarifa zilipoibuka kuwa inafaya udukuzi kwenye mitandao.

Mwanateknolojia huyo alisema kuwa huenda ikachukua muda mrefu sana kwa mageuzi yoyote kufanyika.

Zuckerberg alisema, "wakati wahandisi wetu wanapofanya kila hali kuboresha usalama kwenye mtandao, kwetu ni kama tunawalinda kutokana nawahalifu kwenye mitandao, sio serikali yetu.''

"Serikali ya Marekani lazima ipigie debe Internet sio kuwa adui wa mtandao. Lazima waelezee wanachokifanya la sivyo, watu hawatakuwa na imani tena na serikali.''

Shughuli za shirika la ujasusi la Marekani lilijipata motoni baada ya ufichuzi kutolewa na aliyekuwa jasusi wakati mmoja Edward Snowden, mwaka jana.

Ufichuzi wake ulionyesha kuwa shirika hilo lilikuwa linakusanya taarifa za simu za watu, kufanya udukuzi na kuvamia mitandao ya watu.

RWANDA YAHUSISHWA NA UVAMIZI A.KUSINI

Afrika Kusini imewatuhumu wanadiplomasia watatu wa Rwanda waliofurushwa kutoka nchini humo kwa kuhusika na mauaji na njama ya mauaji dhidi ya wapinzani wa serikali ya Rwanda wanaoishi Afrika Kusini.

Waziri wa sheria wa Afrika Kusini, Jeff Radebe amesema kuwa ana ushahidi wa kutosha unaowahusisha watatu hao na vitendo vyinavyokiuka sheria.

Wanadiplomasia hao, walifurushwa siku ya Ijumaa baada ya kutokea uvamizi nyumbani kwa Generali Kayumba Nyamwasa aliyekuwa wakati mmoja mwandani wa Rais Kagame, mjini Johannesburg.

Rwanda ambayo nayo iliwafurushwa wanadiplomasia sita wa Afrika Kusini kutoka mjiniKigali, imekanusha madai ya kuhusika na njama hiyo.

Msemaji wa Bwana Radebe, Mthunzi Mhaga, aliambia BBC kuwa uchunguzi ulibaini kuwa watatu hao walihusika na uvamizi huo na mashambulizi mengine dhidi ya watu wanaoonekana kuwa wapinzani wa serikali ya Rwanda wanaoishi nchini Afrika Kusini.

Watu waliokuwa wamejihami, walivamia nyumba ya Luteni Generali Nyamwasa, mkuu wa zamani wa majeshi ya Rwanda wiki jana lakini hakuwepo nyumbani wakati wa uvamizi huo.

Wavamizi hao walifanya msako ndani ya nyumba hiyo na kuondoka wakiwa wamebeba Komputa na stakabadhi kadhaa.

Generali Nyamwasa ameponea majaribio mawili ya kumuua ikiwemo kupigwa risasi mjini Johannesburg mwaka 2010 baadaya kutoroka Rwanda.

Alitafuta hifadhi nchini Afrika Kusini baada ya uhusiano wake na Kagame kuvunjika.

Januari mwaka huu mwili wa aliyekuwa jasusi mkuu wa Rwanda, Patrick Karegeya, ulipatikana ndani ya hoteli moja mjini Johannesburg akiwa na alama za kunyongwa.

Maafisa wa zamani wa serikali ya Rwanda waliokimbilia usalama wao katika nchi za Magharibi ikiwemo Uingereza na Marekani wanasema kuwa maafisa wa usalama wa serikali wametishia kuwaua.Muda mfupi baada ya kifo cha Karegeya Rais Kagame alionya kuwa wale ambao wanasaliti nchi hiyo watakiona cha mtema kuni.

Afrika Kusini ilikuwa wakati mmoja mshirika mkubwa wa Afrika Kusini na hata kununua silaha kutoka kwake, lakini uhusiano kati ya nchi hizo umeendelea kuzorota kila kukicha kufuatia mashambulizi dhidi ya waliokuwa maafisa wa Rwanda waliokimbilia nchini humo.

ALIYEKUWA RAIS WA SIERRA LEONE AFARIKI DUNIA

Bwana Kabbah anasifiwa zaidi duniani kwa kurejesha amani nchini Sierra Leone baada ya mapigano ya wenyewe kwa wenyewe.

Amefariki nyumbani kwake akiwana miaka 82.

Alhaji Ahmad Tejan Kabbah alizaliwa February 16, 1932. Aliongoza Sierra Leone katiya mwaka wa 1996 hadi 1997 na kisha tena mwaka wa 98 hadi mwaka wa 2007.

Katika miaka mingi ya utu uzima wake, alihudumu kama mtaalamu wa uchumi na sheria. Alifanya kazi kwa miaka mingi na shirika la maendeleo la Umoja wa mataifa UNDP. Baada ya kujiuzulu kutoka umoja huo mwaka wa 92, alirudi zake nchini Sierra Leone na kujiingiza katika siasa za nchi hiyo.


*Maisha yake ya siasa

Mnamo mwaka wa tisini na sita, bwana Kabbah alichaguliwa kuwa kiongozi wa chama Sierra Leone's People's Party (SLPP) na kuwania urais kwa tikiti ya chama hicho mwaka wa 96.

Katika kinyanganyiro hicho, alishinda na kuwa rais kwa 59% ya kura na kumpiku mpinzani wake mkuu John Karefa-Smart wachama cha United National People's Party (UNPP) aliyepata 40% tu ya kura.

Waangalizi wa kimataifa walitangaza kuwa uchaguzi huo ulikuwa huru na wa haki.

Kikubwa atakachokumbukwa nacho ni hotuba yake ya kuapishwa mjini Freetown, alipoahidi kumaliza kabisa mapigano ya wenyewe kwa wenyewe, jambo alilotekeleza baada ya kuwa rais.

Bwana Kabbah ni wa kabila la Mandingo kiasilia na ndiye aliyekuwa rais wa kwanza wa kiislamu wa Sierra Leone. Alizaliwa katika kijijji cha Pendembu, wilaya ya Kailahun mashariki mwa Sierra Leone, japo udogoni mwake alikulia mji mkuu wa Free town.


*Utawala wa Kabbah

Sehemu kubwa ya uongozi wa Kabbah ilishawishiwa na mapigano ya wenyewe kwa wenyewe yaliyotokea nchini Sierra Leone kwa muda mrefu, huku akikumbwa na mapinduzi yamuda yaliyofanywa na wanamgambo wa United Front wakiongozwa na Foday Sankoh. Mapinduzi hayo yalim'ngoa madarakani kati ya Mei 97 hadi March 98.

Hata hivyo alirejeshwa madarakani kufuatia usaidizi wa kijeshi kutoka kikosi cha Jumuiya ya Kiuchumi ya Afrika Magharibi (ECOWAS) kilichoongozwa na Nigeria.

Awamu ya pili ya machafuko ya ndani na mauaji ilisababisha kuingiliwa na Umoja wa mataifa pamoja na Uingereza nchini humo mwaka wa 2000.


*Harakati za amani

Katika wadhifa wake kama rais, Kabbah alianzisha mazungumzo na wanamgambo hao wa RUF ili kumaliza mapigano hayo ya ndani. Alisaini mikataba kadhaa ya kusitisha mapigano na kiongozi wa waasi Foday Sankoh, ukiwemo ule mkataba wa mwaka wa 1999 wa mjini Lome' ambapo kwa mara ya kwanza waasi hao walitekeleza na kusitisha kabisa mapigano na mashambulio dhidi ya serikali.

Na pale mkataba huo ulipovunjika baadaye, Kabbah alifanya kampeini kuomba usaidizi kutoka Umoja wa Mataifa, Uingereza, Jumuiya ya ECOWAS na hata Muungano wa Afrika, AU ili kurejesha amani.

Kabbah alitagaza rasmi kumalizika kwa vita vya ndani vya Sierra Leone mwaka wa 2002. Maelfu ya raia wa Sierra Leone walikimbia katika barabara kuu zanchi hiyo kusherehekea hatimaye kupatikana amani.

Miaka michache baadaye Kabbah alipata ushindi wa rahisi sana kuongoza nchi hiyo kwa muhula mwingine wa miaka mitano alipopata 70% ya kura na kumpiku mpinzani wake mkuu Ernest Bai Koroma wa chama cha All People's Congress (APC). Hapopia, waangalizi wa kimataifa walitangaza uchaguzi kuwa huru na wa haki.

WACHINA MIAKA MITANO JELA AU FAINI YA MILIONI MOJA

RAIA wawili wa China wamehukumiwa kifungo cha miakamitano jela au kulipa faini ya Sh milioni moja baada ya kukutwa wakisafirisha meno ya tembo.

Qui Wu (30) na Zou Zhihong (51) ambao walikutwa na meno ya tembo, zilizotengenezwa kama bangili na kinyago.

Akitoa hukumu hiyo, Hakimu Janeth Kinyage alisema washitakiwa watatumikia kifungo cha miaka mitano au kulipa faini.

Zhihong aliomba mahakama impunguzie adhabu, kwa kuwa ana matatizo ya moyo na ana familia inamtegemea na mama yake ni mzee.

Mwendesha Mashitaka Nassoro Katuga alidai Februari 23 mwaka huu eneo la Uwanja wa Ndege wa Mwalimu Julius Nyerere (JNIA) Wilaya ya Ilala, raia hao wa China walikutwa na vipande nane vya bangili, vilivyotengenezwa kwa meno ya tembo vyenye thamani ya Sh 249,600.

Pia, mshitakiwa Zhihong alikutwa na bangili mbili na kinyago, vilivyotengenezwa kwa meno ya tembo yenye kilogramu 0.25 yenye thamani ya Sh 240,000.

JELA MIAKA 10 KWA KUMPA MIMBA MWANAFUNZI

MAHAKAMA Kuu Kanda ya Dodoma imemhukumu mfanyabiashara wa mbuzi, Adam Shaban Hole (46) kwenda jela miaka 10 baada ya kumtia hatiani kwa kosa la kumpa mimba mwanafunzi, kushiriki kumtoa mimba na kusababisha kifo chake.

Mshitakiwa mwingine katika kesi hiyo, Godlisten Raymond (37) ambaye kwa wakati huo alikuwa tabibu, alipewa adhabu kama hiyo ya miaka 10 jela baada ya kupatikana na hatia ya kumtoa mimba na kusababisha kifo cha mwanafunzi.

Mwanasheria wa Serikali, Neema Mwanda alidai katika mahakama hiyo, mbele ya Jaji Mfawidhi, Cresentia Makuru kuwa tukio hilo ni la Septemba 7, 2006 katika Zahanati ya Tumaini mjini Singida.

Alidai kuwa Hole, ambaye ni mkaziwa kijiji cha Kintandaa Wilaya ya Ikungi mkoani hapa, alimpa mimba mwanafunzi, Hamida Athuman (16) kisha kushiriki kumtoa hatua iliyosababisha kifo chake.

Mwanafunzi huyo aliyekuwa darasala saba kwa wakati huo, alifariki siku chache kabla ya kufanya mtihani wake wa kumaliza elimu ya msingi.

Ilidaiwa mahakamani hapo kuwa mfanyabiashara huyo, ambaye ana mashine ya kusaga nafaka kijijini hapo, katika kipindi hicho hicho, alimpa mimba mwanafunzi mwingine, Rukia Juma aliyekuwa anasoma darasa moja na Hamida.

Ilidaiwa kuwa baada ya kutolewa mimba, Rukia alilazwa Hospitali ya Mkoa wa Singida, ambapo alipatiwa matibabu sahihi na hivyo kuepuka kifo.

Mwendesha Mashitaka, Neema Mwanda aliiomba mahakama hiyo itoe adhabu ya kifungo cha maisha jela kwa washitakiwa ili iwe fundisho kwao na kwa watu wengine wenye tabia kama hiyo.

Wakili Deus Nyabiri kutoka Dodoma aliyekuwa akimtetea mshitakiwa wa kwanza, Godlisten Raymond aliiomba mahakama impe mteja wake adhabu nafuu, kwa kuwa hilo lilikuwa ni kosa lake la kwanza.

Wakili Raymond Kimu ambaye alikuwa anamtetea Hole, aliiomba mahakama hiyo impe mteja wake adhabu ndogo au imwachie huru, kwa kuwa baada ya kuwapa mimba wanafunzi hao wawili, alikimbiwa na mke na kutengwa na familia yake.

Hata hivyo, Jaji Mfawidhi Makuru alisema katika hukumu yake kuwa kwa mazingira ya kawaida, kosa walililotenda washitakiwa, hawastahili huruma ya mahakama yoyote nchini.

WAZIRI MKUU AZUILIWA KUSAFIRI

Kiongozi wa mashtaka Nchini Libya Abdel-al-Qader Radwan amemzuia Waziri mkuu wa taifa hilo aliyevuliwa madaraka, Ali Zeidan, kusafiri nje ya taifa hilo hadi pale uchunguzi dhidi yake utakapo kamilika.

Anatuhumiwa kwa madai ya ubathirifu wa pesa za umma.

Bwana Zeidan amesimamishwa kazi mapema siku ya Jumanne na Bunge la taifa hilo, baada ya Wabunge kudai kuwa meli ya mzigo ya Korea Kaskazini iliyokuwa imezuiliwa baada ya kunaswa ikibeba mafuta ghafi toka bandari moja linalokaliwana waasi huko Libya, ilivunja nanga na kusafiri baharini.

Kura ya kutokuwa na imani na Bwana Zeidan iliitishwa baada ya meli hiyo iliyokuwa na bendera ya Korea Kaskazini kuabiri na kufikia maji makuu ya mipaka ya kimataifa baharini.

Mafuta hayo yalikuwa yamenunuliwa kutoka kwa waasi wanaodhibiti bandari ya Al- Sidra.


*Wabunge hawana imani na Waziri Mkuu

Bunge la Libya limemuachisha kazi Waziri huyo mkuu, baada ya kupitisha agizo la kutokuwa na imani naye.

Hilo limeafikiwa baada ya meli ya Korea Kaskazini kuingia katika bandari ya taifa hilo na kuondoka na mafuta ghafi bila idhini ya serikali.

Makundi ya wapiganaji yamekuwa yakidhibiti baadhi ya bandari ya taifa hilo mashariki mwa taifa, tangu Julai mwaka jana na kuuza mafuta nje ya taifa.

Mwaandishi wa BBC Rana Jawad anatuarifu kutoka Tripoli.

Bunge la Libya limekuwa likijadiliana namna ya kumtimua Waziri mkuu Ali Zeidan kwa miezi kadhaa sasa.

Wabunge 200 wa taifa hilo walipiga kura na kupata maoni 124 iliyotosha kumuondoa madarakani.


*Serikali ya mpito

Waziri wa sasa wa ulinzi Abdullah Al-Thani amechukua mahala pake kama kama kaimu waziri mkuu.

Anatarajiwa kuhudumu kwa kipindi cha majuma mawili, kuruhusu bunge kukubaliana kumteuwa mridhi wa wadhifa huo.

Chama cha Libya National Congress, tume ya kwanza ya uchaguzi ndio yenye majukumu ya kumteuwa waziri mkuu mpya.

Lakini shinikizo kali limekuwepo Nchini humo la kutaka Bunge livunjwe.

Bwana Zeidan amekuwa akilaumu baadhi ya wanasiasa katika tume hiyo, hasa kutoka ndani ya vyama vya kiislamu ya kutaka kumtimua toka uongozini.

Hatua hiyo ya hivi punde inatazamiwa kuibua maswala mbalimbali ya udhibiti wa uongozi Nchini Libya, inapojikakamua kutafuta uungwaji mkono kutoka pembe zote za Nchi.

LOWASSA AKERWA NA MITANDAO

(Noti ya Sh.500 Iliyowekwa picha ya Lowassa)

Waziri Mkuu aliyejiuzulu, Edward Lowassa amekerwa na tabia ya baadhi ya watu wanaosambaza uzushi katika mitandao ya kijamii kwa kutumia jina lake.

Lowassa alisema kuna watu wanaoendeleza kusambasa picha yanoti ya Sh500 yenye picha yake huku wakiongeza maneno mabaya juu yake.

Katika taarifa iliyotolewa na ofisi yake, Lowassa alisema, "Kitendo hicho siyo utani, bali ni dhihaka na dharau kwa alama za Taifa na mamlaka ya nchi."

"Hizi ni alama za Taifa ambazo zinatakiwa kulindwa na kuheshimiwa na watu wote, si busara kwa hao wanaozichezea kuendelea kufanya hivyo, kwani ni dharau kubwa kwa Taifa' alisema.

Katika noti hiyo ya Sh500 inaonekana upande wa kulia wa noti hiyo picha ya Edward Lowassa, huku ikikaribiana na ngao ya Taifa huku ikionyesha kuwa ilitolewa na Benki Kuu ya Tanzania..

Alisema anaheshimu maoni ya watu na nguvu ya mitandao ya kijamii, lakini anasisitiza umuhimu kwa wananchi hao kutumia nguvu hiyo ya mitandao kwa kujadili maendeleo ya nchi badala ya kuzusha mambo yasiyo na tija. Kwa nyakati tofauti, picha hiyo imekuwa ikisambaa katika mitandao mbalimbali ya kijamii ikiwamo ya Facebook, Instagram, Whatsapp, na Twitter huku kukiwa na maneno kama "timu Lowassa" na mengineyo.

Ikumbukwe kuwa Lowassa yupo katika adhabu ya kutoshiriki katika masuala yoyote yahusianayo na kampeni za chinichini za urais, baada ya kamati ya maadili ya CCM)kutoa hukumu yake mwezi uliopita.

Adhabu hiyo pia iliwakumba wengine watano wakiwamo Waziri Mkuu wa zamani, Frederick Sumaye, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Uhusiano na Uratibu), Stephen Wassira, Naibu Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, January Makamba na aliyewahi kuwa Waziri wa Nishati na Madini, William Ngeleja.

Moja ya sababu ya adhabu hiyo ya miezi 12 ilikuwa ni kuanzisha kampeni za chinichini za kugombea urais mwaka ujao nje ya muda uliopangwa, ambapo baadhi ya wanachama akiwamo Lowassa walituhumiwa kuhusika kuandaa makundi na fulana za kujinadi.

JE ARSENAL KUWAONDOSHA THE BAVARIANS KWAO?

Michuano ya kuwania kombe la klabu bingwa barani Ulaya kuendelea leo usiku huku kukiwa na mechi mbili.

Arsenal, inaelekea, Bonn, kutoana jasho na mabingwa wa Ujerumani, Bayern Munich ambayo ilishinda mechi ya raundi ya kwanza kwa mabao mawili kwa nunge katika uga wa Emirates.

Hata hivyo Arsenal itakosa huduma za mcheza kiungo wake Kieran Gibbs ambaye kwa sasa anauguza jeraha la mkuu na mshambulizi Yaya Sanogo, lakini mlinda lango Laurent Koscielny, ambaye alikuwa akiuguza jeraha la paja anatarajiwa kurejea.

Kipa Lukasz Fabianski naye atachukuwa mahala pa Wojciech Szczesny, ambaye amesimamishwa kucheza kwa muda baada ya kupewa kadi nyekundu wakati wa mechi ya raundi ya kwanza.

Mwaka uliopita Arsenal iliishinda Bayern kwa magoli mawili kwa bila katika mechi ya marudiano lakini ilibanduliwa nje ya mashindano hayo baada ya kupoteza raundi ya kwanza 3-1.


Katika mechi nyingine ya marudiano leo usiku itakuwa kati ya Atletico Madrid na AC Milan.

Madrid ilishinda awamu ya kwanza kwa bao moja kwa bila.

Mario Balotelli huenda akajumuishwa kwenye kikosi cha wachezaji kumi na mmoja wa AC Millan, baada ya kuuguza jeraha la mgongo alilopata siku ya Jumamosi dhidi ya klabu ya Udinese.

Atletico nayo inamkaribisha mchezaji wake aliyefunga idadi kubwa yua magoli Diego Costa huku ikijaribu kufunzu kwa robo fainali ya kombe hilo kwa mara ya kwanza kwa zaidi ya miaka kumi na saba iliyopita.

Na ili kufuzu, mabingwa hao mara saba wa Ulaya ni sharti waandikishe historia ya kuwa timu ya tatu katika historia ya kombe hilo kuwahi kushindwa nyubani katika mechi ya raundi ya kwanza na ishinde mechi ya marudiano ugenini.


*BARCELONA KUIMALISHA MPIRA SOMALIA

Klabu ya soka ya Hispania Barcelona, imezindua mpango wakutoa mafunzo kwa makocha wa Somalia.

Mpango huo ujulikanao kama Futbal Net unalenga kuimarisha soka miongoni mwa vijana nchini Somalia, huku nchi hiyo ikijaribu kujiondoa kutoka katika vita vya wenyewe kwa wenyewe.

Kamati ya michezo ya Olimpiki pia inaunga mkono mpango huo.Wanatumai kufungua vituo kadhaa vya mafunzo kote nchini humo.

Soka na michezo mingine ilikandamizwa na kundi la wanamgambo la Al Shabab kabla ya kuondolewa mjini Mogadishu miaka mitatu iliyopita.


*MASHABIKI KUTIZAMA MPIRA BURE

Mashabiki wa soka nchini Afrika Kusini watapata fursa ya kutizama mechi za ligi kuu ya England, katika bustani mpya itakayo funguliwa mjini Johannesburg mwisho wa mwezi huu.

Mechi tano, ikiwemo ile kati ya Arsenal na Manchester City itaonyesha moja kwa moja kwenye runinga kubwa katika bustani hiyo tarehe 29 na 30 mwezi huu.

Hafla hiyo ambayo haitatoza ada yoyote, inaandaliwa kwa mara ya kwanza na mashabiki elfu kumi na mbili wataruhusiwa kuingia ndani ya bustani hiyo ya Zoo LakeSports Club kila siku.

Mashabiki hao pia watapata fursa ya kukutana na wachezaji wa zamani wa timu ya taifa ya AfrikaKusini, Bafana Bafana akiwemo Mark Fish na Lucas Radebe.

Vile vile wachezaji wa zamani wa Liverpool, Robbie Fowler na mchezaji wa zamani wa Chelsea na nahodha wa Ufaransa Marcel Desailly watakuwepo.

Wakati wa hafla hiyo mashabiki watakuwa na fursa ya kuona na kupiga picha kombe la ligi kuu ya Premier ya England.

WAANDAMANA DHIDI YA UN

Zaidi wa raia elfu moja wa Sudan Kusini, wameandamana katika mji mkuu wa nchi hiyo Juba, dhidi ya Umoja wa Mataifa, wakiishutumu kwa kuwapa waasi wanaopambana na serikali silaha.

Waandamanaji hai wamemtaka mjumbe maalum wa Umoja wa Mataifa nchini humo Hilda Johnson kujiuzulu.

Siku ya Ijumaa, serikali ya Sudan Kusini, ilisema kuwa ilinasa msafara wa magari yaliyokuwa yakisafirisha silaha ambazo huku zikidai kuwa zilikuwa zikisafirisha misaada ya chakula.

Umoja wa Mataifa umekanusha shutuma hizo, lakini imekiri kuwa imekiuka mkataba waliosaini na serikali ya nchi hiyo, kwa kusafirisha silaha wakitumia magari badala ya ndege.

Taifa la Sudan Kusini, limekumbwa na mzozo wa kisiasa tangu Desemba mwaka uliopita, wakati wanajeshi watiifu kwa makamu wa rais wa zamani wa nchi hiyo Riek Machar, kuanzisha mapigano katika kambi kuu ya jeshi mjini Juba.

Mazungumzo ya amani kati ya wawakilishi wa serikali ya Sudan Kusini inayoongozwa na Salva Kirrna makamu wake wa zamani RiekMachar, yanaendelea mjini Addis Ababa, Ethiopia.

MELI YA KOREA KASKAZINI YAKAMATWA LIBYA

Wakuu nchini Libya, wamesema kuwa wameikamata meli moja iliyokuwa na bendera ya Korea Kaskazini, ikiwa na shehena haramu ya mafuta katika bandari inayodhibitiwa na waasi.

Msemaji wa shirika la kitaifa la mafuta, amesema kuwa meli hiyo ilisimamishwa ilipokuwa ikijaribu kungoa nanga na kwa sasa inasindikizwa katika bandari inayodhibitiwa na serikali ya Libya.

Maafisa wa serikali ya Libya waliisimamisha Meli hiyo ya Korea Kaskazini ilipokuwa ikiondoka kutoka bandari inayodhibitiwa na waasi siku ya Jumatatu ikiwa imesheheni mzigo usio rasmi wa mafuta ghafi.

Jeshi la nchi hiyo limethibitisha tukio hilo.

Waasi wa zamani wanaotaka kuitenga eneo la Libya Mashariki, wamekuwa wakimiliki bandari ya Al-Sidra na vituo vingine muhimu vya kuuzia bidhaa nje katika eneo hilo tangu Julai mwaka uliopita.

Mnamo siku ya Jumamosi, walianza kupakia shehena ya mafuta yasiyosafishwa ndani ya meli hiyo ya Korea Kaskazini iitwayo Morning Glory, iliyokuwa imetia nanga katika bandari ya Al-Sidra.

MAREKANI WASUSIA MAZUNGUMZO NA URUSI

Maafisa wa Marekani wamesema kuwa Waziri wa mambo ya nje John Kerry, amekataa kukutana na Rais wa Urusi, Vladmir Putin, mpaka pale Moscow itakaporidhia mapendekezo ya Marekani kuhusu kumaliza mzozo nchini Ukraine.

Kerry amemwambia waziri wa mambo ya nje wa Urusi kuwa uvamizi wa kijeshi wa Urusi mjini Crimea umefanya mazungumzo ya kufikia muafaka kuwa magumu mno.

Maafisa wa Marekani wamesema ikiwa kura ya maoni iliyopendekezwa itapigwa mwishoni mwa juma kuhusu kuridhia kwa Crimea kuwa sehemu ya Urusi, hakuta kuwa nasuala jingine la kuzungumza.

Maafisa hao wamesema kuwa ikiwa hali itafikia hivyo, Marekani itaiwekea Urusi vikwazo vikali.

MISHAHARA YA RAIS, MAKAMU NA MAWAZIRI KUPUNGUZWA KWA 20%

Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta, ameamuru maafisa wakuu watendaji wa mashirika ya serikali kukubali mishahara yao kukatwa kwa asilimia 20, la sivyo waachishwe kazi.

Akiongea kwenye kongamano la kitaifa kuhusu gharama kubwa ya matumizi ya serikali, Rais Kenyatta alisema kuwa hatua yake na naibu wake pamoja na baraza la mawaziri kupunguza mishahara yao kwa asilimia 20 haikuwa kwa sababu ya kufurahisha watu.Kadhalika Kenyatta ameongeza kusema kuwa uchumi wa nchi hauwezi kuwa mzuri ikiwa kila mtu anataka nyongeza ya mishahara badala ya kuzingatia kupunguza gharama ya maisha nauzalishaji wa bidhaa.

''Wakuu wa mashirika ya serikali watatakiwa kukubali mishahara yao kupunguzwa kwa asilimia 20. Kuna wakenya ambao wanaweza kushikilia nyadhifa hizo kwa pesa ndogo ikilinganishwa na zile wanazopata wakuu hao,'' aliongeza kusema Kenyatta.

Kenyatta amesema matumizi ya pesa za serikali ni ya juu mno na kwamba hayawezi kudhibitiwa ikiwa baadhi ya wafanyakazi wa sekta ya umma wataendelea kupata mishahara mikubwa.Rais alisema lazima safari za kwenda nje ambazo zinafanywa na baadhi ya wafanyakazi wa serikali, kupunguzwa. Wakati huohuo, Rais aliwataka wabunge kukubali mishahara yao kukatwa kwani ni baadhi ya wabunge anaopokea mishahara mikubwa duniani.

Swala la mishahara ya wabunge ni swala tete sana nchini Kenya.

Rais Kenyatta, alisema kuwa serikali inatumia kati ya dola dilioni 4.6 kwa mishahara ya wafanyakazi wa umma na kutumia dola bilioni 2.3 kwa maendeleo.

AHUKUMIWA MIAKA 30 JELA KWA KULAWITI

Mahakama ya Wilaya ya Mpanda Mkoa wa Katavi imemuhukumu Wiliamu George 32 Mkazi wa Mtaa wa Nsemlwa Wilaya ya Mpanda kifungo cha miaka 30 jela baada ya kupatikana na hatia ya kumlawiti kijana mwenzie 22 Mkazi wa Mtaa wa Mpanda hoteli baada ya kumnywesha pombe ya kienyeji kupita kiasi.

Hukumu hiyo ilitolewa na Hakimu mkazi mfawidhi wa Mahakama ya Wilaya ya Mpanda Chiganga Ntengwa na hukumu hiyo kuvuita hisia za watu mbalimbali wa maeneo ya mjiwa Mpanda na Mkoa wa Katavi.

Hukumu hiyo ilitolewa na Hakimu wa mahakama hiyo baada ya mahakama kuridhika na ushahidi uliotolewa mahakamani hapo wa upande wa mashitaka na upande wa utetezi Katika kesi hiyo hapo awali mwendesha mashita mkaguzi wa jeshi la polisi Ally Mbwijo alidai mahakamani hapo kuwa mshitakiwa alitenda kosa hilo hapo Novemba 21 mwaka jana majira ya kumi na mbili jioni katika mtaa wa Mpanda Hotel.

Mshitakiwa siku hiyo ya tukiokabla ya kutenda kosa hilo la kumlawiti kijana huyo alidaiwa kunywesha pombe ya kienyeji aina ya komoni walikuwa wakichanganya na bia nyumbani kwa mwamke aliyekuwa akiwauzia pombe aliyetambulika kwa jina moja la Lita katika mtaa huo wa Mpanda hotel.

Ilielezwa na mwendesha mashita Ally Mbwijo kuwa mshitakiwa baada ya kuona mwenzake ametoka nje kwenda kujisaidia alimwagiza dukani Lita aende akamnulie sigara.

Aliileza mahakama baada ya kijana huyo ambae jina lake limehifadhiwa kurudi ndani aliendelea na kunywa pombe ambayo alikuwa imeisha kwenye chupa yake na ndipo alipoteza fahamu na mshitakiwa alitumia nafasi huyo kumwingilia kinyume cha maumbile yake huku akiwa amemlaza kwenye kochi.

Mwendesha mashitaka alieleza Lita alipotoka dukani alimkuta mshitakiwa akiwa amekaa karibu na kijana huyo ambae alikuwa amevuliwa nguo yake ya saruali na akiwa ajitambui na sehemu zake za matakoni zikiwa na mbegu za kiume.

Mshitakiwa baada ya kufanya kitendo hicho siku iliyofuata alimtuma mama yake mzazi aende kwa kijina huyo akamwombee samahani kwa kile alichoeleza kuwa anahofia kufungwa jela.

Baada ya mama mshitakiwa Wiliamu George kumwombea msamaha kwa kijana alilawitiwa alikubali kumsamehe mshitakiwa kwa kuhofia kupata aibu.

Mshitakiwa baada ya kusamehewa alianza kumtangaza kijana huyo kwa rafiki zake na kuwafahamisha kuwa kijana huyo ni shemeji yao kitendo ambacho kilimkasilisha kijana huyo na kuamua kwenda kituo cha polisi kutoa taarifa ya kulawitiwa kwake na Mshitakiwa Wiliamu George.

Hakimu mkazi mfawidhi Chiganga Ntengwa kabla ya kutowa hukumu hiyo aliiambia mahakama kuwa mahakama imemtia hatiani mshitakiwa Wiliamu George kwa kosa la kumwingilia kijana huyo kinyumbe na maumbile yake hivyo mahakama inatowa nafasi kwa mshitakiwa kama anasababu ya msingi ya kuishawisha mahakama impunguzie adhabu aieleza mahakama hiyo.

Katika uetezi wake mshitakiwa aliiomba mahakama imwachie huru kwani yeye hakutenda kosa hilo na pia umri wake bado ni kijana mdogo na wazazi wake bado wanamtegemea maombi ambayo yalipingwa vikari na mwendesha mashitaka.

Hakimu Chiganga baada ya kusikiliza utetezi huo aliiambia mahakama kuwa mshitakiwa amehukumiwa na mahakama baada ya kupatikana na hatiaya kumwingilia kinyume na maumbile kijana huyo na anahukumiwa na adhabu ya kifungu cha sheria namba 235 sura ya 20 ya mwaka 2009 hivyo Wiliamu George mahakama imehukumu kutumikia jela kuanzia jana kifungo cha miaka 30 jela.

Chanzo: Katavi yetu

JUHUDI ZA KUTAFUTA NDEGE YA MALAYSIA ZAENDELEA

Wakati juhudi za kuisaka ndege iliyopotea ilipokuwa ikisafiri kutoka Malasyia kuelekea Uchina zikiendelea, ndege moja ya Vietnam imeripoti kuwa imeona kitu kinachofanana na mlango wa ndege kwenye ufuo wa bahari ya Kusini mwa Uchina kwenye mwambao wa taifa hilo.

Hata hivyo hakuna thibitisho kuwa mlango huo ni wa ndege iliyopotea ya Malaysia, iliyokuwa na abiria mia mbili na thelathini na tisa.

Uchunguzi kuhusiana na kilichosababisha kupotea kwa ndege hiyo mapema siku ya Jumamosi, inawalenga abiria wawili wanaodaiwa kuwemo ndani ya ndege hiyo, waliotumia paspoti iliyoibiwa.

Stakabadhi hizo mbili za kusafiria kutoka Italia na nyingine Australia inaaminika kuibwa nchini Thailand.

Idara ya polisi ya Kimataifa, Interpol, inasema kuwa ni mapema mno kuhusisha pasi zilizoibwa na kutoweka kwa ndege hiyo.

Na huku kushughuli za kuisaka ndege hiyo zikiendelea, Msemaji wa shirika la ndege la Malysia amewaambia jamaa ya watu waliokuwemo katika ndege hiyo, kujiandaa kwa taarifa mbaya.

Amesema kufikia sasa hakuna mawasiliano yoyote na ndege hiyo masaa 30 sasa tangu itoweke.

Wakuu wa Malysia wanasema jumla ya meli 30 na ndege 44 kutoka mataifa tisa tofauti duniani, yamejiunga katika shughuli za kuitafuta ndege hiyo.

Kamanda William Marks wa kikosicha saba cha jeshi la wanamaji la Marekani, ametuma ndege aina ya USS Pinckney kusaidia katika usakaji huo.''

Jambo la kwanza kufanywa ni kukadiria mahala na kwa sasa tunalenga mawasiliano ya mwisho kutoka kwa ndege hiyo kabla ya kutoweka na mawasiliano ya rada.

Kutoka hapo tunahesabu mwendo kasi yaupepo na mawimbi. Kutoka hapo tunagawanya na eneo na tunatafuta kutumia kila kifaa tuliyonayo na hiyo siyo tu kutumia vifaa kutoka Marekani lakini pia kutumia meli na anga kutoka mataifa mengine ya dunia." Alisema kamanda huyo.

Ameonya kuwa shughuli hiyo ya kutafuta ndege hiyo inakumbwa na changamoto nyingi.

MWANAMKE AHUKUMIWA KWA KOSA LA KUMSHAMBULIA POLISI

MWANAMKE mmoja amehukumiwa na mahakama ya wilaya ya Musoma, mkoani Mara, kutumikia kifungo cha miaka mitano na miezi sita jela, baada ya kupatikana na makosa ya kutoa matusi na kushambulia askari polisi wawili waliokuwa wanataka kumkamata.

Aliyekumbwa na adhabu hiyo ni Mary Jumanne, mkazi wa mjini Musoma, ambapo pia ameamriwa kuwalipa fidia ya shilingi laki moja kila mmoja askari polisi hao.

Hukumu hiyo imetolewa juzi na hakimu mwandamizi Richard Maganga, wa mahakama ya wilaya ya Musoma, baada ya kuridhika na ushahidi uliotolewa mahakamani hapo na upande wa mashitaka.

Awali, imedaiwa mahakamani hapona mwendesha mashitaka wa serikali, Jonas Kaijage, kuwa mshitakwa huyo alitenda kosa hilo machi 3, mwaka huu, mjini Musoma.

Kaijage alisema kuwa mshitaikiwa huyo aliwashambulia na kutoa lugha ya matusi askari polisi wawili, PC. Hamis na WP.Kuruthumu kutoka ofisi ya afisa upelelezi wa mkoa wa Mara, waliokuwa wamekwenda kumkamata akikabiliwa na kosa jingine la kutoa lugha ya matusi.

Alisema kuwa baada ya polisi hao kutaka kumkamata ndipo mwanamke huyo alipowatukana nakisha akamshambulia askari wa kike WP.

Kuruthumu na kumsababishia maumivu makali mwilini mwake. Mshitakiwa huyo baada ya kusomewa mashitaka yake alikiri kutenda makosa hayo huku akiomba mahakama hiyo impunguzie adhabu, ombi lililotupiliwa mbali na mahakama hiyo.

Kufuatia ushahidi huo hakimu Maganga alihukumu kifungo cha miaka mitano kwa kosa la kushambulia askari na kifungo cha miezi sita jela kwa kosa la kutoa lugha ya matusi.


Source:Habari leo

ITV, STARTV NA RFA VYAPEWA ONYO

MAMLAKA ya Mawasiliano Tanzania(TCRA) imevipa onyo kali vyombo vya habari vya Independent Television (ITV), Star Tv na Radio Free Africa (RFA) kwa kutangaza maudhui yanayoelezwa kuchochea uvunjifu wa amani na kuzuia wananchi kulipa kodi.

Aidha, sambamba na onyo hilo, piaimevitaka vyombo hivyo kuwasilisha kwa mamlaka hiyo miongozo yao ya kuchuja vipindi wanavyorusha hewani baada ya kubaini baadhi yao hawakuwa na miongozo hiyo na kuwataka wazuiewatangazaji kuingia na miziki yao binafsi studio.

Onyo hilo lilitolewa jana, Dar es Salaam na Mwenyekiti wa Kamati ya Maudhui ya TCRA, Magreth Munyagi, ikiwa ni sehemu ya hukumu kwa vyombo hivyo kwa kukiuka Kanuni za Utangazaji za mwaka 2005 na kuhatarisha mshikamano wa Taifa, usalama wa Taifa na maadili bora.

Akisoma hukumu hiyo mbele ya waandishi wa habari katika Makao Makuu ya TCRA kabla ya kuwakabidhi wahusika, Munyagi alisema Kamati ya Maudhui ya TCRA inayosimamia maadili na maudhui ya utangazaji nchini ilibaini ukiukwaji wa kanuni hizo mwaka jana na mwaka huu na kabla ya uamuzi huo, ilikutana na wahusika kwa majadiliano na kufikia muafaka.

"Hivyo kwanza, kamati inatoa onyo kali kwa wahusika, pili, inawataka kuwasilisha mwongozo wa uchujaji wa vipindi vyao kwa mamlaka na tatu, ikiwa watarudia kosa hili, hatua kali zitachukuliwa dhidi yao.
Wahusika wana uhuru wa kukata rufaa dhidi ya uamuzi huu katika kipindi cha siku 30 baada ya tamkohili," alisema Munyagi akisoma hukumu hiyo.

Akifafanua kuhusu uvunjifu huo wakanuni, Munyagi alisema kituo cha televisheni cha ITV na Star Tv kwa nyakati tofauti vilirusha hewani tangazo la taasisi ya Policy Forum linalohamasisha wananchi kutolipa kodi katikati ya taarifa za habari za usiku (saa 2:00 hadi 3:00) kinyume cha kanuni namba 5(a) na 6(b) za kanuni hizo.

Kuhusu RFA, alisema Juni 27 mwaka jana katika kipindi cha "Sindano tano za moto" kilichorushwa kati ya saa mbili hadisaa tatu asubuhi na radio hiyo, mtangazaji alipiga wimbo wa msanii Nashi (MC) inayoamsha hisia za uchochezi wa kisiasa, maandamano na uvunjifu wa amani kutokana na maudhui ya wimbo wenyewe.

Kufuatia majadiliano na pande zotembili, Munyagi alisema wahusika walikiri kutoa maudhui hayo kupitia vyombo vyao ambapo katika majadiliano Mkurugenzi wa ITV na Radio One, Joyce Mhavile alieleza kuwa, wao hawakuona uvunjifu wa amani katika tangazo hilo, bali elimu kwa umma kuhusu misamaha ya kodi na uwajibikaji wa serikali na jamii.

Aidha, Kampuni ya Sahara Media Group inayomiliki Star TV na RFA, kupitia Mkurugenzi wake Anthony Dialo na Meneja Mipango na Utafiti, Nathan Lwehabura, walikiripia kutumia muziki na tangazo hilona kuiomba TCRA isiwape adhabu kali kwa kuwa hawakuwa na mwongozo wa kuchuja muziki na maudhui kabla ya kuyarusha kwa jamii.

Akizungumza jana na waandishi mara baada ya hukumu hiyo, Lwehabura alisema hatua hiyo ni changamoto kwa vyombo vyote vya habari kwa kuwa wao binafsi hawakuona kosa kutokana na ukweli kwamba hata baadhi ya viongozi wa serikali huzungumza wazi wazi kuhusu misamaha ya kodi lakini wanaheshimu uamuzi wa TCRA na tayari wamesitisha matangazo hayo.

"Tumekiri kwamba tulitangaza maudhui yaliyosomwa, lakini hili linazungumzika na pia ni suala la mjadala kwa wanahabari wote, StarTV na ITV ni kama kondoo wa kafara tu, tunapaswa kujadili nini ni uchochezi maana hili la kodi hata Bungeni linazungumzwa, tumejifunza unapopata tangazo kutoka taasisi hizi binafsi, lazima utafsiri kama ni uchochezi ama la,"alisema Lwehabura.

ICC YAMPATA NA HATIA GERMAIN KATANGA

Mahakama ya kimataifa ya jinai ICC imempata na hatia ya uhalifuwa kivita mbabe wa kivita kutoka Jamhuri ya kidemokrasi ya Congo, Germain Katanga.

Hata hivyo Katanga hakukutwa nahatia katika shtaka la udhalilishajiwa kijinsia.

Alituhumiwa kuhusika na mauaji ya wanavijiji zaidi ya 200 mwaka 2003 katika jimbo la Ituri lenye utajiri wa dhahabu, kaskazini mashariki mwa Congo.

Katanga ni mtu wa pili kupatikana na hatia ya uhalifu wa kivita katika mahakama ya ICC tangu ianzishwe mjini The Hague, Uholanzi mwaka 2002.

Katika shambulio hilo lililotokea mnamo Februari 24, 2003 watu 200 waliuawa katika kijiji cha Bogoro karibu na mpaka wa Uganda,Katanga wakati huo akiwaKamanda wa kundi la waasi la Patriotic Resistance Force of Ituri(FRPI) lililotekeleza mauahi hayo.

Mwendesha mashtaka amesema nia yao kuu ilikuwa kuangamiza kijiji kizima.

Germain Katanga kwa jina la utani Simba alikanusha mashtaka hayo yote dhidi yake .

MWANAJESHI FEKI ATUPWA JELA MIAKA MITATU

MAHAKAMA ya Wilaya ya Bunda mkoani Mara, imemhukumu kifungo cha miaka mitatu jela mwanamume aliyejifanya askari wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na kufanya utapeli.

Bakari Saibo (32) mkazi wa Mwenge jijini Dar es Salaam, alihukumiwa na Hakimu wa Mahakama ya Wilaya ya Bunda, Said Kasonso, baada ya kuridhika na ushahidi uliotolewa mahakamani na upande wa mashitaka.

Awali, Mwendesha Mashitaka wa Polisi, Masoud Mohamed, alidai kuwa mshitakiwa huyo alitenda kosa hilo Februari 28 mwaka huu, saa 12:15 jioni.Alidai mshitakiwa huyo akiwa katika eneo la nyumba moja ya kulala wageni iitwayo Mori iliyoko mtaa wa Posta mjini Bunda, alijitambulisha kwamba ni askari wa JWTZ.

Aidha alidai mshitakiwa alijitambulisha kwa Kamira Nkengemkazi wa mtaa huo aliyemtilia shaka na kutoa taarifa Polisi. Alidaimbali na kujitambulisha hivyo, pia alimtapeli Nkenge nguo zake zenye thamani ya Sh 100,000 na kwamba baada ya polisi kupata taarifa hiyo, walimkamata na kumpeleka mahakamani hapo.

Hakimu Kasonso alisema kosa la kwanza la kujifanya mwanajeshi wa JWTZ, anamhukumu kutumikia kifungo cha miaka mitatu jela na kosa la pili la utapeli anamhukumu kifungo cha miaka miwili jela.

Adhabu hizo zatazitumika kwa pamoja. Kabla ya hukumu kutolewa mwendesha mashitaka wa Polisi, aliiomba Mahakama hiyokutoa adhabu kali kwa mshitakiwa, kwani tabia hiyo inachafua sifa za majeshi.

MTU MMOJA AFARIKI NA WENGINE 38 KUJERUHIWA

Mtu mmoja amefariki dunia na wengine 38 kujeruhiwa, kati yao 14 vibaya, baada ya magari matatu waliyokuwa wakisafiria, kugongana, mawili uso kwa uso, huku jingine likijaribu kukwepa ajali, katika eneo la Bwawani, barabara kuu ya Morogoro-Dar es saalam, wilayani Bagamoyo mkoani Pwani.

ITV imefika eneo la tukio na kushuhudia magari mawili kati ya yaliyohusika na ajali, yakiwa yameharibika vibaya, hasa sehemu ya dereva, ambapo mkuu wa usalama barabarani Chalinze mkoani Pwani, Inocent Sule, amesema chanzo cha ajali ni basi la abiria, mali ya kampuni ya Linowele class, lililokuwa likitokea dar es salaam kuelekea malinyi wilayani ulanga, , likiendeshwa na mtu aliyefahamika kwa jina moja la musa kujaribi kulipita gari jingine lililokuwa mbele na kukutana uso kwa uso na tenka la mafuta aina ya Iveco, ambapo dereva wa tenka, ali hassan ngoma, mkazi wa korogwe mkoani tanga, amefariki dunia papo hapo, huku yule wa basi hali yake ikiwa ni mbaya sana na la tatu mali ya kampuni ya adventure aina ya nisan diesel, lililokuwa likitokea Dar es salaam kuelekea Kigoma liliyagonga magari hayo yaliyokuwa yamepata ajali.

Mashuhuda wa ajali hiyo, wakiwemo majeruhi walionusurika kifo katika ajali hiyo, ambao baadhi yao wamekimbizwa kupatiwa huduma ya kwanza katika zahanati ya magereza bwawani, wamezungumzia kuhusiana na namna walivyobaini ajali hiyo, huku mganga wa zahanati ya sekondari ya magereza Bwawani, Lazaro Mdeka, akikiri kupokea majeruhi 38, na 14 hali zao ni mbaya na wamekimbiza hospitali ya rufaa ya mkoa wa morogoro kwa matibabu.

Katika hospitaliya mkoa wa Morogoro, huduma za kuwapokea na kuwahuduma majeruhi hao zimekutwa zikiendelea, huku wengi wakishindwa kuzungumza kutokana na hali mbaya.

Chanzo:ITV

NDUGU WAWILI WATUHUMIWA KUMUUA MPENZI WA MAMA YAO

NDUGU wawili wa kiume wa familia moja wilayani Mlele mkoa wa Katavi, wanatuhumiwa kumuua mpenzi wa mama yao kwa kumchinja, kisha kutelekeza mwili wake porini. Wakazi hao ambao mmoja ni mtoto mwenye umri wa miaka 16 ni wakazi wa Kitongoji cha Milumba Kata ya Kibaoni na aliyeuawa ni Kitungulu Luhende (65).

Inadaiwa mama yao, Sai Mponje (65) ambaye ni mjane anayeshikiliwa na polisi kwa sasa, alikuwa na uhusiano wa kimapenzi na Luhende, jambo ambalo watoto hao hawakufurahishwa.

Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Katavi, Dhahiri Kidavashari alitaja watuhumiwa hao ni Nyengu Kashele (19) na nduguye mwenye umri wa miaka 16.

Mtoto huyo anashikiliwa wakati Nyengu amejificha kusikojulikana. Mwili wa marehemu uligundulika Machi 3, mwaka huu saa 3:30 asubuhi katika milima ya kitongoji hicho cha Milumba ukiwa umeharibika.

Mwili huo uligundulika kutokana na msako uliofanywa na askari wa jadi(sungusungu) kwa kushirikiana na polisi na wananchi. Kidavashari alisema Februari 22, mwaka huu saa 2 asubuhi, Luhende ambaye pia ni mkazi wa kitongoji hicho cha Milumba, alimuaga mkewe kwamba anakwenda kijiji cha Kirida ambako ana mke mwingine.

Hata hivyo, Kamanda alidai kuwa badala ya kwenda kijijini Kirida, aliko mke wake mwingine, kwanza alipitia nyumbani kwa rafiki yake katika kitongoji hicho cha Milumba, aitwae Milembe Katembeni ambako aliacha pikipiki yake yenyenambari za usajili T449 BAF. Inadaiwa kisha alikwenda moja kwamoja kwa Sai (mama wa watuhumiwa).

Kamanda alisema tangu hapo hakuonekana hadharani hadi mwili ulipokutwa umetelekezwa eneo la milimani huku pembeni kukiwa na leseni yake ya udereva.

Akielezea sababu za kuanza kumtafuta, Kamanda alisema baada ya kutorejea kwa rafiki yake kuchukua pikipiki, Katembeni aliingiwa wasiwasi ndipo Machi 2 , mwaka huu aliamua kutoa taarifa kwa kiongozi wa sungusungu na kisha polisi, na msako ukaanza.

MCHUNGAJI ASHIKILIWA KWA MAUWAJI

MCHUNGAJI mstaafu wa Kanisa la Anglikana, Usharika wa Mfarasi kata ya Madilu wilayani Ludewa, mkoani Njombe, Petro Chambachamba (87) anashikiliwa Polisi akihusishwa kwenye kesi ya mauaji.

Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Njombe, Fulgence Ngonyani, amesema jana kuwa Chambachamba pamoja na watu wengine wanane, wamekamatwa wakihusishwa na mauaji yaliyotokea Februari 25, mwaka huu saa 8 mchana katika kijiji cha Mfarasi.

Alisema watu hao wanatuhumiwa kuchukua sheria mkononi kwa kumpiga hadi kumsababishia kifo Boniface Mtweve (35), mkazi wa kijiji cha Ilininda kilichoko kata ya Madilu wakimtuhumu kuiba simu tatu mali ya Nuru Ngairo.

Kamanda alisema kwa kupitia taarifa za siri kutoka kwa wakazi wakijiji hicho, Februari 28, watu hao walikamatwa na kufikishwa mikononi mwa dola. Wengine waliokamatwa ni Linus Chaula, Stanley Katembo, Ery Mwapinga, Kedimoni Mwapinga, Phillimon Mgimba, Richard Mvalla, Meshack Mgaya na Nuru Ngairo.

"Ushahidi wa awali unawahusisha watu hao tisa akiwemo mchungaji huyo, hata hivyo wanaweza kuachiwa huru endapo baadaye wataonekana kutohusika na tuhuma hiyo na uchunguzi unaendelea," alisema Kamanda.

Hata hivyo, waumini wa usharika huo wamedai vyanzo vya taarifa za Polisi zinazomuhusisha mzee huyo katika kesi hiyo, ni vya uongo na wameomba aachiwe huru.

Zaidi ya wananchi 600 wa kijiji hicho, juzi walishiriki mkutano maalumu wakishutumu kuchukuliwa kwa mchungaji pamoja na watuhumiwa wengine.

Katika mkutano wa kijiji uliofanyika katika kijijini Mfarasi, Mwenyekiti wa Kijiji hicho, Petro Mwapinga alisema, " inasikitisha Polisi walivamia kijijini hapa usiku wa manane na kuwakamata ndugu zetu bila kushirikisha uongozi wa kijiji."

Ofisa Mtendaji wa Kijiji hicho, Samwel Mtewele alisema wote wanaotuhumiwa kuhusika katika mauaji hayo, ni wale waliotoa taarifa katika kituo cha Polisi cha Lugarawa wilayani Ludewa, kwamba nyumba zao zilivunjwa na mali zao mbalimbali ziliibwa.

Msaidizi wa Askofu Mkuu wa Kanisala Anglikana Dayosisi ya Kusini Magharibi, Michael Lugome, alieleza kushangazwa na hatua ya Polisi kumkamata mchungaji huyo na wenzake.

"Taarifa tuliyopewa na Kijiji inaonesha kwamba kabla ya mauajihayo, Mchungaji wetu mstaafu na watuhumiwa wengine, walivunjiwa nyumba zao na mali zao kuibwa; taarifa hizo zilipelekwa Polisi, na askari walipaswa kuzifanyia kazi taarifa za wizi huo," alisema Lugome.

"Hili ni tukio la aina yake na yawezekana likawa la kwanza; lakini tuna maswali ya kujiuliza ni wapi na katika mazingira gani tukiohilo lilitokea na watu hawa akiwemo mzee huyo wa miaka 87 alishirikije katika tukio hilo," alisema Mwenyekiti wa Idara ya Uinjilisti ya Dayosisi hiyo, Nicholaus Mgaya.

Mke wa Mchungaji huyo, Lea Chambachamba, alisema mumewealikuwa nyumbani wakati watu wenye hasira kali kijijini hapo wakimpiga mtuhumiwa.

Alisema kabla ya tukio hilo, nyumba yake ilivunjwa na vitu kuibwa ambavyo inadaiwa mtuhumiwa huyo aliyeuawa, alikutwa navyo.

"Polisi hawajatenda haki, mume wangu ana miaka 87, mimi nina miaka 70; mzee wa umri huo anawezaje kwenda kwenye kundi lenye watu wengi na kushiriki kumshambulia mtu?" alisema.


Source: Habari Leo

JUHUDI ZA KERRY ZAGONGA MWAMBA

Juhudi za marekani kuwakutanisha kwa mara ya kwanza ana kwa na mawaziri wa mashauri ya nchi za kigeni wa Urusi na Ukraine kuhusu mzozo unaoendelea katika jimbo la Crimea zimegonga mwamba.

Ingawa waziri wa mashauri ya nchi za kigeni Marekani John Kerry amekanusha kwamba palikuwa na nia ya kumkutanisha mwenzake wa Urusi Sergey Lavrov na waziri mpya wa mashauri ya nchi za wa Ukraine Andrii Deschchytsia iwapo wawili hao wangekutana mjini Paris ingekuwa ni mafanikio makubwa ya kidiplomasia.

Sergei Lavrov alikataa kukutana na waziri huyo mpya wa Ukraine kwa sababu Urusi haitambui utawala mpya wa mjini Kiev.

Akizungumza mjini Paris Bwana Deschchytsia amesema licha ya vuta nikuvute hiyo anaamini kwamba kuna dalili ya mafanikio katika mashauri." Kwa hiyo baada ya kuwa hapa siku nzima mjini Paris, inaonekana kwamba tunaendeleana mashauri yetu na tunaamini kwamba tutapata mwafaka.

Ninaelekea mjini Brussels kukutana na waziri mkuu kujadili hatua zaidi za kuchukua. Shukran.

"Na alipoulizwa na mmoja waandishi wa habari ni kwa nini hakuweza kukutana na waziri wa mashauri ya nchi za kigeni wa Urusi Sergey Lavrov hivi leo, bwana Deschchytsia alijibu- ''kamuulize Lavrov mwenyewe.''

Hata hivyo bwana Lavrov alifanya mazungumzo ya kina na waziri wamashauri ya nchi za kigeni wa Marekani John Kerry na mawaziri wengine wa umoja wa ulaya. Bwana Kerry alitaja mkutano huokuwa mgumu lakini akasema ana ujumbe atakaoupeleka kwa rais Obama na mazungumzo yataendelea.

Waziri wa mashauri ya nchini za kigeni wa Ufaransa Laurent Fabius kadhalika alielezea matumaini ya mazungumzo hayo kufanikiwa."

Tumekubaliana kuendelea na mashauri kwa sababu mambo bado na hali sio rahisi anasema bwana Fabius. Lakini tunayo furaha kwamba siku ya leo mjini Paris imeturuhusu kuanzisha mikakati.''

Kwa upande mwingine rais wa Urusi Vladmir Putin alifanya mazungumzo kuhusu mzozo huo na chanzela wa Ujerumani Angela Merkel kwa njia ya simu.

Wakati huo huo Mwakilishi mkuu wa Umoja wa mataifa huko Crimea, Robert Serry, amelazimika kukatiza ujumbe wake baada ya kutishiwa na watu waliojihami alipokuwa akitoka katika makao makuu ya jeshi la wanamaji la Ukraine katika bandari ya Simferopol.

MVUA ZINAZOENDELEA KUNYESHA DAR ZAZUA MAAFA

Mvua zinazoendelea kunyesha jijini Dar es salaam, zimesababisha maafa kutokana na baadhi ya magari kupinduka barabarani mengine kukwama kwenye mashimo na msongamano wa muda mrefu kutokana na magari kuteleza na miundombinu ya barabara kuharibika.

Akizungumza katika eneo la tukio Kongowe Mzinga jijini Dar es Salaam kondakta wa lori lililopinduka katika barabara hiyo Casmir Michael amesema chanzo cha ajali hiyo ni baada ya mwenye daladala kusimama ghafla mbele ya lori lao ndipo breki za gari lao kukataa na tairi kupoteza mwelekeo kisha gari kupinduka.

Baadhi ya mashuhuda wa ajali ya haisi wamesema chanzo ni baada ya haisi kuigonga gari nyeupe iliyokuwa imeharibika barabarani lenye namba za usjaili T591 CGP na kushindwa kushika breki saa chache kabla halijatumbukia mtaroni kwa kuwa mbele kulikuwa na shimo kubwa lililochimbika baada ya kunyesha kwa mvua.

Nao madereva waliokumbwa na adha ya mrundikano wa foleni barabani wameiomba serikali kutengeneza makarabati imara na barabara za pembeni ili magari yaweze kupita kwa urahisi zinapotokea ajali kwenye barabara hiyo.

Imeshuhudiwa gari la magereza nalo likiwa limenasa kwenye barabara ya pembeni hali iliyowalazimu askari magereza kushuka kwenye gari lao kisha kulisukuma walipokwama wakiwa njiani kuelekea wilayani Mkuranga mkoani Pwani kusindikiza mahabusu wao.

KIJANA AJICHINJA MPAKA KUFA(SAHAMANI KWA MUONEKANO WA PICHA)

AMA kweli duniani kuna mambo kwani dereva na abiria wa basi la Manchester ambalo namba yake haikujulikana mara moja, lililokua likitoka Lindi kwenda jijini Dar es Salaam walijikuta wakiangua vilio baada ya kumuona mwenzao akijichinja hadi kufa kwa kisu ndani ya gari hilo.

Kwa mujibu wa chanzo, tukio hilo la kusikitisha lilitokea saa tisa alasiri, Jumatano wiki iliyopita mara basi hilo lilipofika katika hoteli moja ya Nangulukulu kwa ajili ya kupatia chakula.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti na waandishi wa habari hii jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki iliyopita, baadhi ya abiria walioshuhudia tukio hilo walisema kuwa mara walipofika katika hoteli hiyo, kila mmoja alitawanyika kwa lengo la kujipatia chakula na baadhi yao walienda maliwatoni akiwemo marehemu huyo.

Walisema kwamba marehemu huyo ambaye jina lake halikupatikana mara moja, wakati wa kushuka hakuonekana na kisu aina ya sime lakini baadaye abiria wachache waliotangulia kwenye gari, walimshuhudia akiwa ameshika sime hiyo mkono pasipokujua aliipata wapi.

"Hata sisi tulishangaa kumuona akiwa karibu na usukani wa dereva huku akizamisha sime tumboni kisha kuichomoa na kujichinja shingoni hadi pale alipokuwa akivuta koromeo na kuning'inia.

"Tulichanaganyikiwa kwani ni kitu ambacho hatukukitarajia na wala hatujawahi kushuhudia tukio kama hilo la mtu kujichinja hadharani, tulibakia kutokwa machozi huku akina mama wakipiga yowe, hakuna mtu aliyethubutu kumsogelea kumuokoa kwani kila mmoja alimuogopa.

"Tulishindwa kupanda basi hilo kwani ni tukio la ajabu pia ndani kwa mbele kulikuwa kumetapakaa damu, ghafla alidondoka chini ndani ya gari, aliomba kalamu na karatasi ili kuandika ujumbe.

"Dereva alichukua kalamu na kipande cha karatasi na kumpa, alianza kuandika huku damu ikimbubujika tumboni na shingoni, hatukujua alichokiandika, aliishiwa nguvu taratibu akadondoka.

"Abiria walimsogelea na kumuinua na walimueleza kuwa atubu kwa Mungu kosa alilolifanya kabla hajafa, alipiga magoti na kuomba, ghafla alidondoka tena.

"Kaka yake ambaye alikuwa akisafiri naye kuelekea Dar es Salaam alichanganyikiwa kwani hakutegemea kuwa mdogo wake angejiua, kwani alisema hana historia ya kuugua ugonjwa wa akili.

Polisi walipigiwa simu na walifika kumchukua lakini baada ya muda mfupi akawa amefariki dunia.

"Sisi abiria wengine tuliendelea na safari kuelekea Dar es Salaam ambapo marehemu na kaka yake walibakia huko mkoani Lindi.

"Mara tulipofika Dar es Salaam dereva alitusihi tukae kimya kwa dakika moja na kuomba kutokana na tukio lililotupata, tulifanya hivyo baadaye kila mmoja alitawanyika na kuelekea kwake,"kilisema chanzo kwa sharti la kutoandikwa jina gazetini.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Lindi, ACP Renatha Mzinga alipoulizwa mwishoni mwa wiki iliyopita kuhusiana na tukio hilo alikiri kutokea.

"Ni kweli tukio hilo lilitokea lakini kwa sasa sina data kwani nipo njiani nikitokea Nairobi, Kenya kikazi kuelekea Lindi, mara nitakapofika huko ofisini ndipo nitapata tukio zima lilivyokuwa,"alisema Kamanda Mzinga.


Chanzo: Jf

WAWILI WANUSURIKA KUFA BAADA YA KUFUKIWA NA KIFUSI KWA SIKU TANO

Watu wawili wamenusurika kufa baada ya kufukiwa na kifusi kwa siku tano katika machimbo ya dhahabu mkoani Geita na kuokolewa wakiwa katika hali mbaya.

Eneo hilo lipo chini ya leseni ya mgodi wa dhahabu wa Geita na shimo hilo lilikuwa likitumika zamani ambapo kwa sasa halitumiki, mara kwa mara vijana waishio katika mji wa Geita na vijiji vya jirani hufika eneo hilo kuchimba ili kuweza kuambulia angalau masalia ya mchanga wenye dhahabu hata hivyo uongozi wa mgodi huo kwa kushirikiana na jeshi la polisi wamekuwa wakijitahidi kuwazuia vijana hao kutofika eneo hilo kwa kuwa si salama.

Daktari mfawidhi katika hospitali ya wilaya ya Geita Adam Sijaona amethibitisha kupokelewa kwa vijana hao amesema hali zao zinaendelea vizuri, ambapo kwa upande wa mgodi wa dhahabu wa Geita wamewataka viongozi na wananchi waishio kandokando ya mgodi huo kuwaelimisha vijana wao kutovamia maeneo hatarishi kama hayo.

Imedaiwa kwamba kuna baadhi ya wanasiasa ndio wanaowashawishi vijana hao kuvamia maeneo ya uchimbaji yasiyo rasmi ili kuweza kujiongezea mvuto kwa wapiga kura ambapo jeshi la polisi limewataka wananchi kutovunja sheria kwa shinikizo la wanasiasa.

WAISLAM WALAANI KUCHANWA KWA KORAN

Mamia ya waislam wamefanya maandamano katika mji mkuu wawa Mauritania Nouakchott, baadaya kuenea kwa taarifa kuwa Koran imechanwa msikitini.

Imam ameripoti kuwa watu wanne waliokuwa wamefunika nyuso zao waliingia msikitini , wakachana nakala za Koran na kuzitupa chooni.

Polisi walifyatua mabomu ya kutolea machozi kutawanya umati wa watu waliokuwa na jazba, na mtu mmoja aliuawa, duru za polisi zilieleza.Mauritania ni taifa la kiislam , likiwa na idadi ndogo ya wakristo.

Imekuwa mshirika muhimu wa nchi za magharibi katika kampenidhidi ya al-Qaeda na makundi mengine ya wanamgambo yanayoendesha harakati katika kanda hiyo.

Mwandishi wa habari Hamdi Mohamed El Hacen aliyeko mjini Nouakchott anasema waandamanaji walichoma vizuizi na maduka mengi na masoko yalifungwa jana siku nzima.

Mamia ya waandamanaji walikusanyika kati kati mwa mji mkuu na nje ya msikiti wakipaza sauti "Mungu ni mkuu" wakidai wahusika wakamatwe na kuhukumiwa kifo kwa madai ya kukufuru uislam, alisema.

PUTIN: URUSI HAIJAPELEKA MAJESHI UKRAIN

Rais Vladimir Putin wa Urusi, amesema bado hakuna haja kwa nchi yake kupeleka majeshi nchini Ukraine.

Bwana Putin amesema Urusi ina haki ya kutumia njia zote kulinda raia wake walioko mashariki mwa Ukraine.

Amekanusha taarifa kwamba majeshi ya Urusi yamewazingira raia wa Ukraine walioko katika jimbo la Crimea, bali ni watu wanaoiunga mkono Urusi na ambao wanajilinda wenyewe.

Bwana Putin amesema kuondolewa madarakani kwa RaisViktor Yanukovych katika mji mkuu wa Ukraine, Kiev ni "ukiukaji wa katiba na uporaji wa madaraka kijeshi.".

Amesema wapiganaji hao wameitumbukiza Ukraine katika"vurugu". Pia amesema wapiganiautaifa na wapinga usemiti wanarandaranda katika mitaa ya Kiev na miji mingine.

Amesema iwapo watu wanaozungumza Kirusi mashariki mwa Ukraine watahitaji msaada wa Urusi, basi Urusi itakubaliana na ombi lao.

"kama tutaona hali hii ikianza kutokea maeneo ya mashariki, tuna haki ya kutumia kila njia" amesema.

Bwana Putini amesema katika jimbo la Crimea watu wenye silaha wanaoiunga mkono Urusi na raia wamezingira kambi za kijeshi za Ukraine, sio askari wa Urusi.

"Majeshi ya eneo hilo kwa ajili yakujilinda" ndiyo yanayohusika na kuchukuliwa kwa majengo ya serikali katika Crimea, amesema.

Ukraine imesema Urusi imepeleka maelfu ya askari katika eneo la Crimea hivi karibuni.

Uhasama umeongezeka katika kituo cha kijeshi cha Belbek karibu na Sevastopol, mji wa bandari ambao ni kambi ya majeshi ya majini ya Urusi.

Akizungumzia kupinduliwa kwa Bwana Yanukovych, Bwana Putin amesema kiongozi huyo aliyeondolewa madarakani nchini Ukraine alikubali matakwa yote ya wapinzani.

Bwana Putin amesisitiza kuwa Bwana Yanukovych bado ni rais halali wa Ukraine.

Amesema kuna mambo matatu ya kumwondoa madarakani rais, ameyataja kuwa ni kifo, kujiuzuluau kushtakiwa.

Bwana Yanukovych alikimbilia Urusi, na Bwana Putin aliwaambia waandishi wa habari:

"Sifikiri kama ana mustakabhali mwema kisiasa".

Urusi ilimsaidia kwa sababu za"kibinadamu", amesema,

"vinginevyo angekuwa ameuawa".

WABUNGE WA BUNGE LA KATIBA WATOFAUTIANA

Wajumbe wa bunge la katiba wamekuwa na mtazamo tofauti wa kuwasilisha mapendekezo ya vifungu vya rasimu ya kanuni za bunge vilivyo na matatizo baada ya baadhi ya wabunge kuonyesha kutokubaliana na pendekezo la mwenyekiti wa muda lililotaka wawasilishe kwa maandishi kwa kamati ya kanuni.

Hatua hiyo ya wajumbe ilizua kutokusikilizana kwa baadhi ya wajumbe na mwenyekiti huku wajumbe wengine wakisimama na wengine kuwasha vipaza sauti bila ya utaratibu hali iliyomlazimu wa mwenyekiti wa semina ya wajumbe kuzungumza.

Katika semina hiyo baadhi ya wajumbe wameshauri rasimu hiyo ipitiwe kurasa kwa kurasa huku wengine wakipongeza utaratibu wa mwenyekiti wa muda unaotaka mapendekezo yawasilishwe kwa kamati ya kanuni kwa maandishi.

Katika hatua nyingine, baadhi ya wajumbe wamelalamikia wajumbe wa kamati ya kanuni kuzingatia zaidi hoja za makundi makubwa na kuziacha hoja za watu wachache katika kutengeneza rasimu ya kanuni za bunge maalum.

DARAJA LA KIGAMBONI LAKAMILIKA KWA 45%

Daraja la Kigamboni limekamilika kwa zaidi ya asilimia arobaini na tano na matumaini makubwa ya kumalizika kwa ujenzi huo kwa muda uliopangwa Julai mwakani yakionekana huku nyumba zilizokuwa zinazuia ujenzi huko zikibomolewa kwa nguvu na serikali.

Akizungumza na ITV jijini Dar es Salaam meneja mradi huo injinia Karim Mattaka amesema ujenzi huo umeshaanza kuleta matumaini makubwa kutokana na nguzo mbili zilizokuwa zinakwamisha kuwa tayari na zoezi linaloendelea ni kuhamisha maji katika maeneo yalinayochimbiwa nguzo hizo sambamba na kuchimbia nguzo kubwa za kupokea baraja hilo upande wa barabara ya Mandela.

Aidha injinia Karimu amejaribu kufafanua mfumo wa barabara na daraja hilo namna utakavyotumika baada ya kukamilika na kuwahakikishia watanzania ujenzi huo utakamilika kwa wakata kama mambo yataenda kama yalivyopangwa.

Mwenyekiti serikali ya mtaa wa Vijibweni Bw. Athman Ally akielezea kuhusiana na hatua iliyochukuliwa na serikali ya kuvunja nyumba za baadhi ya wakazi waliogomea fidia amesema wao walipewa taarifa na mwanasheria mkuu na baadaye akatakiwa kwenda kusimamia zoezi la uvunjaji wa nyumba hizo.


Chanzo:ITV

CHAMA CHA ALLIANCE FOR CHANGE AND TRANSPARENCY(ACT) CHATAMBULISHWA

KILE kinachotafsiliwa kuwa Demokrasia nchini imeanza kukuwa kutokana na wingi wa vyama vya kisiasa nchini vinaanzishwa, hivi leo chama kipya cha kisiasa nchini kimeanzishwa chama hicho kinajulika kama ACT,(Alliance for change And Transparency)maana yake ni Umoja wa Mabadiliko na Uwazi.

Hayo, yamethibitishwa leo Jijini Dar es Salaam na Mwenyekiti wa Chama hicho kipya, Limbu Lucas Kadawi Wakati akitambulisha Chama hicho kwenye Mkutano na Waandishi wa Habari, ambapo alisema wamefikia maamuzi ya kuanzishwa chama hicho kutokana na Malengo mahususi ya kuwaleta watu pamoja.

"Tumeanzisha chama hichi cha kisiasa kwa malengoma hususi ya kuwaleta watu pamoja watanzania wanaoamini kwamba nguvu ya Pamoja inaitajika katika kuleta mabadiliko ya kweli ya kisiasa katika nchi hii, na kwamba uwazi na uadilifu ni tunu ambazo taifa hili linaitajika kwa sasa na Baadaye"alisema Limbu

Limbu alisema chama hicho cha ACT kinatakuwa kinaongozwa na misingi mikuu mitano ambayo ndio itakuwa nembo ya chama hicho.

"ACT tutakuwa na inaongozwa na misingi mikuu mitano ambayo ni Uzalendo,Usawa,Uadilifu Uwazi na uwajibikaji pamoja na Demokrasia ya Kweli" Alizidi kuongezea Limbu.

Limbu ikumbukwe Mwaka 2010 alikuwa Mwanachama wa cha Wananchi CUF na aligombania Ubunge kupitia Chama hicho kwenye Jimbo la Temeke na Alibwagwa kwenye uchaguzi huo na Mbunge wa CCM kupitia Temeke, Mr Mtevu na Baada ya Hapo na kwenda kuanzishwa chama cha ADC kabla ya kuanzishwa chama hichi.

Aliwataka wananchi wakiamini chama hicho kuwa ni Chama kitakachowaletea maendeleo.

Kwa upande wake Katibu mkuu Taifa wa Chama hicho Samsoni Mwigamba alisema Chama hicho kwa sasa kimeanda mipango mikubwa ya kuhakikishwa kinashinda kwenye Chaguzi Mbalimbali Zinazokuja.

"Kwa sasa ACT Tanzania imekwisha Kukamilisha Rasimu ya awali ya Katiba ambaye iliwezesha kupata usajili wa Muda na Zoezi la kuandikishwa wananchama katika mikoa kwa ajali ya kuomba usajili wa kudumu kwa mujibu wa sheria limekwisha kamilika"

"Tumewapata Wanachama katika mikoa yote ya Tanzania Bara,hata ivyo tumechagua mikoa kumi ambayo tungependa Msajili akahakiki kama sheria inavyotaka"alisema Mwigamaba.

Ikumbukwe Samsoni Mwigamba kabla ya kujiunga na chama hichi cha ACT alikuwa mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA Mkoani Arusha na pia alikuwa mhasibu Mkuu wa Chama hicho na Baada ya hapo Chama chake cha Chadema kilimvua uwanachama kwa kile chama hicho kinadai kuwa Mwigamba alikuwa anafanya Uasi katika chama hicho, ambapo Kamati kuu ilimvua uwanachama pamoja na Wananchama wengine akiwemo Ziito Kabwe pamoja na Dk Kitara Mkumbo.

Wachambuzi wa Masuala ya Kisiasa waliozungumza na Mwandishi wa Mtandao huu walisema chama hicho kipya cha kisiasa nchini uwenda kikawa kimeanzishwa kwa mahususi ya kuwachukua wanachama waliokuwa wamevuliwa uwanachama kwenye vyama tofauti vya kisiasa nchini, huku wachambuzi hao wakihoji kwanini chama hicho cha kisiasa kimeanzishwa sasa, wakati vyama vya kisiasa nchini vikiwa katika hali ya sitofamu.

Ambapo Kauli hiyo ilipingwa vikali na Mwenyekiti wa Chama hicho cha ACT alisema chama hicho wala hakina uhusiano wowote na Mtu wala mikoa bali chama hicho kinawahusishwa watanzania wote.

WABUNGE WASHAMBULIWA LIBYA

Wabunge wawili nchini Libya walipigwa risasi na kuumizwa baada ya kundi la waandamanaji kuwashambulia bungeni katika mji mkuu wa Tripoli.

Walioshuhudia tukio hilo, walisema kuwa wawili hao walipigwa risasi walipojaribu kutoroka kutoka katika eneo hilo.

Waandamanaji hao waliokuwa na ghadhabu walilishambulia bunge hilo, huku wakitaka bunge lifungwe na tarehe mpya ya uchaguzi wa mapema itangazwe.

Kumekuwa na wimbi la maandamano nchini humo kutokana na uamuzi wa bunge la nchi hiyo kuahirisha tarehe ya uchaguzi hadi baadaye mwakani.

Waliolishambulia bunge siku ya Jumapili walisema kuwa walighadhabishwa pia na "kutekwa nyara" kwa waandamanaji waliokuwa na kikao nje ya bunge.

Walisema kuwa waliohusika na utekaji nyara huo walikuwa chini ya uongozi wa waasi wanaotumikia amri ya bunge.

Waandamanaji hao ambao wengi wao ni vijana walijihami kwa visu na vijiti, wakalishambulia bunge huku wakiwa na ujumbe kwa wabunge kwa kuimba "jiuzulu, jiuzulu", kwa mujibu wa taarifa ya ashirika la habari la AFP.

Bunge la nchi ya Libya limeshambuliwa mara kadhaa kwa zaidi ya mwaka mmoja sasa.

Nuri Abu Sahmein ambaye ni spika wa bunge hilo aliambia kituo cha televisheni cha Al-Nabaa kuwa maandamano yaliyokuwa ya amani, yalivurugwa na watu waliojihami.

"Wabunge wawili walipigwa risasi pale walipojaribu kutoweka mahali hapo kwa kutumia magariyao," alisema.

Haikuwezakana kubaini papo hapo idadi ya wabunge walioumia.

Picha zilizotumwa kwenye mitandao ya kijamii zinaonyesha waandamanaji wakivuta kile kilichokusudiwa kuwa kiti cha Spika wa bunge hilo nje ya bungena kukichoma.

Mwandishi wa BBC Rana Jawad ambaye yuko Tripoli anasema kuwa bunge la Libya limeshambuliwa mara kadhaa na makundi tofauti, yakiwemo makundi ya waasi katika kipindi cha mwaka mmoja uliopita.

Uchaguzi uliokuwa wa amani ulifanywa na nchi ya Libya katika mwezi wa Julai mwaka jana, ila bado nchi hiyo ya kaskazini mwa Afrika ingali inang'ang'ana kupata utulivu, miaka mitatu baadaye tangu kufurushwa kutoka maamlakani kwa aliyekuwa rais, hayati Muammar Gaddafi.

OSCAR PISTORIUS AKANA MASHITAKA

Mwanariadha wa Afrika Kusini Oscar Pistorius amekanusha mashitaka ya kumuua mpenzi wake wakati kesi yake ikianza kusikilizwa mjini Pretoria.

Pistorius ambaye ana ulemavu wa miguu na ambaye hutumia miguu bandia ameshitakiwa kwa kumuua mpenzi wake na mwanamitindo Reeva Steenkamp.

Oscar amesema alimpiga risasi marehemu kimakosa kwani alidhani alikua mwizi.

Katika siku ya kwanza ya kesi hiyo jirani wa Oscar Michelle Burger , ameambia mahakama kuwa alisikia mwanamke akipiga mayowe mapema asubuhi tarehe14 mwezi Februari mwaka 2013.

Bwana Pistorius amekanusha madai dhidi yake kuwa alimuua mpenzi wake Reeva Steenkamp.

Alimpiga risasi na kumuua Steenkampe aliyekuwa na umri wa miaka 29 mwanamitindo na muigizaji akisema kuwa hakumuua kwa maksudi.

Jirani ya Oscar alisema kuwa kiliocha mwanamke huyo kilifuatiwa na milio ya risasi ''alipiga nduru akitaka msaada. Pia alisikia mwanamume akipiga mayowe naye akiomba msaada, ''alisema mwanamke huyo.

Alisema punde alipopiga simu kutaka msaada kutoka kwa polisi hapo ndipo alisikia milio ya risasi.

Kukamatwa kwa Pistorius kulishangaza wengi nchini Afrika Kusini.

Pistorius mwenye umri wa miaka 27 alishinda dhahabu katika michezo ya Olimpiki ya walemavu mjini London mwaka 2012 na pia alishindana katoka michezo rasmi ya olimpiki.

Kesi hiyo ilicheleweshwa wa dakika 90 kwani mkalimani wa lugha ya Afrikaans hakuwepo mahakamani.

Pistorius inasemekana alionekana mtulivu alipowasili mahakamani.

Pistorius anasema kuwa alimpiga risasi Reeva kwa bahati mbaya akidhani alikuwa jambazi aliyekuwa amevamia nyumba yake. Mauaji yake yalitokea siku ya Valentines mwaka jana.

Wiki jana mashirika ya habari za michezo, yalipata idhini ya kupeperusha kesi ya Pistorius moja kwa moja kutoka mahakamani.

CHATU AMSHINDA MAMBA NA KUMMEZA

Chatu ameshinda vita vikali dhidi ya Mamba Kaskazini mwa mji wa Queens Land, kupigana na Mamba, kumpinda na kisha kumla.

Tukio hilo lilishuhudiwa katika ziwa Moondarra, karibu na mlima Isa na kunaswa kwa kamera na wakazi wa eneo hilo siku ya Jumapili.

Nyoka huyo mwenye urefu wa futi 10, alijipinda kwa Mamba na kuanza kupambana naye majini.

Hatimaye, Nyoka huyo alifanikiwa kumshinda Mamba na kumtoa nje ya maji na kisha kumla.

Nyoka alimvuta Mamba na kumtoa ndani ya Maji Chatu huyo alianza kumla Mamba na kushangaza wakazi Baada ya mlo huo mkubwa Nyoka alijiendea zake

Tiffany Corlis, mkazi wa eneo hilo, alishuhudia pambano hilo na kupiga picha hizi."lilikuwa jambo la ajabu sana, '' aliambia BBC

"Tulimuona Nyoka akipambana na Mamba , alifanikiwa kumbana mamba hasa katika sehemu ya miguu ili kumdhibiti.''
"Pambano lilianzia ndani ya maji.

Mamba alikuwa anajaribu kuweka kichwa chake juu ya maji wakati mmoja ingawa Nyoka alikuwa amembana sana.''

"Baada ya Mamba kufa Nyoka alijikunjua, na kuja mbele ya Mamba huyo na kuanza kumla,'' alisema Tifanny.

Bwana Corlis alisema kuwa ilimchukua nyoka muda wa robo saa kumla mamba huyo.

''Bila shaka Nyoka huyo alishiba vyema, na hatujui alikokwenda, baada ya mlo wake,'' alisema mama huyo ambaye hakutaka kusuburi kumuona Nyoka tena.

Mtu mwingine aliyeshuhudia pambano hilo Alyce Rosenthal, alisema kuwa wanyama hao wawili walipambana kwa karibu saa 5. Hatimaye wote walionekana wachovu.

''Sio kitu unachoweza kuona kila siku,'' alisema Alyce.

WACHAPANA MAKONDE MSIKITINI KUMPINGA IMAMU

katika hali ambayo haikutarajiwa waumini wa Dini ya Kislamu wanaosari katika Msikiti wa Mji wa Zamani uliopo katika mtaa wa Mji Mwema Wilayani Mpanda wamepigana makonde ndani ya Msikiti kutokana na na pande mbili kupingana baini yao juu ya nani awe Imamu wa Msikiti huo.

Tukio hilo la aina yake liltokea hapo Februari 21 mwaka huu majira ya saa nane mchana mara baada ya kumalizika kwa ibada ya Ijumaa iliyofanyika katika Msikiti huo iliyokuwa ikiongozwa na Shehe Hussein Mkumba.

Hali ya hewa ndani ya msikiti huo ilibadirika mara baada ya swala hiyo ilipomalizika ambapo Kaimu Shehe Mkuu wa Mkoa wa Katavi Ally Hussein ambae pia ndiye shehe mkuu wa wilaya ya Mpanda aliposimama na kuwaeleza waumini hao kuwa hatua inayofuata ni ya kumkabidhi hati ya Uimamu mpya wa msikiti huo Yassin Kasote.

Baada ya kuuli hiyo Shehe Ally Hussen alianza kusoma hati hiyo kitendo ambacho kiliwaudhi baadhi ya waumini hao ambao hawakubaliana kuongozwa na Imamu Yassin Kasote ambaye alichaguliwa hivi karibuni katika uchaguzi uliofanyika Januari 29 baada ya kumshinda mgombea mwenzake wa nafasi hiyo Muajiri Mzee.

Wakati akiendelea kusoma hati hiyo kundi hilo linalompinga Kasote liliokuwa likiongozwa na Ally Kibauka Mawisa walikwenda kufunga milango ya misikiti huo na kutangaza kuwa hatoki mtu humo ndani Baada ya kufunga milango walimfuate Kasote wakimtaka awapatie hati ambayo alikuwa amekabidhiwa na viongozi wa Bakwata waliokuwa wameongozwa na Kaimu shehe wa Mkoa wa Katavi kitendo ambacho Kasote kakukubaliana nacho.

Shehe Kasote alipoona anataka kupolwa hati hiyo alianza kuwashambulia kwa makonde hali ambayo iliwafanya waumini wanao muunga mkono nao kuungana nae hali ambayo ilisababisha mapingano kuanza baina ya pande hizo mbili.

Hata hivyo wakati mapingano yakiwa yanaendelea baadhi ya waumini waliokuwa ndani ya msikiti huo wakiwemo askari polisi wa Dini hiyo waliweza kufanikiwa kufungua milango ya msikiti huo na kufanikiwa kumaliza vurugu hizo na kisha makundi hayo yote mawili walikwenda kituo cha polisi cha mpanda mjini kutoa taarifa kuhusiana na vurugu hizo.

Kwa upande Kaimu Shehe Mkuu wa Mkoa wa Katavi Shehe Ally Hussen amewaomba waumini wa Dini hiyo ya Kislamu wawe na utulivu wakati wa kipindi hiki cha mgogoro huo.

Amesema kikubwa anachotaka waumini wa Dini hiyo ni kuhakikisha wanaendeleza amani katika msikiti huo sio kuleta machako ndani ya msikiti na nje ya msikiti.

Nae mmoja wa kundi linalompinga Imamu mpya alisema wao hawako tayari kuongozwa na Imanu Yassin Kassote kutokana na uchaguzi uliofanyika wa kumchagua ulikiuka taratibu za katiba yao.

Jeshi la polisi Mkoa wa Katavi limekiri kuwepo kwa vurugu kwenye ibada hiyo siku hiyo ya tukio katika msikiti huo wa Mji wa Zamani.

AFIKISHWA MAHAKAMANI KWA KUFUKUA KABURI

Mkazi wa kijiji cha Ikola Wilayaya Mpanda Mkoa wa Katavi Richard Clavery 34 amefikishwa Mahakamani katika mahakama ya Wilaya ya Mpanda kujibu tuhuma za kufanya vitendo vya ushirikina wa kufukua kaburi la mwanamke aliyekufa Mtuhumiwa alifikishwa kizimbani hapo Februari 25 mwaka huu mbele ya Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakamaya Wilaya ya Mpanda Chiganga Ntengwa na kusomewa mashitaka na mwendesha mashitaka Godfrey Luzabila.

Mwendesha mashitaka alidai Mahakamani hapo kuwa mtuhumiwa alitenda kosa hilo hapo Februali 18 mwaka huu majira ya saa nne usiku nyumbani kwa Lenada Sakafu Mwendesha mashitaka Luzabila aliiambia mahakama kuwa siku hiyo ya tukio mtuhumiwa alifika nyumbani kwa Lenada Sakafu na kufukua maiti ya mdogo wake na Lenada aitwaye Tabu Omera ambae alikuwa amefarii siku tatu kabla ya tukio hili.

Aliendelea kuieleza Mahakama siku hiyo Lenanda alikuwa nyumbani kwake pamoja na majirani na ndugu zake wakiendelea kuomboleza msiba ghafla alitokea mtoto wake aitwaye Brandina na kuwaeleza kuwa ameona mtu nje akifukua kaburi la marehemu ambae alikuwa amezikiwa kwenye eneo la nyumba yao.

Alieleza ndipo watu hao walipoamua kutoka nje na kumkuta mtuhumiwa Richard Clavery akifukua kaburi hilo huku akiwa amevua nguo zake zote ambazo alikuwa amezitundika kwenye msalaba wa kaburi hilo na walipomsemesha mtuhumiwa alijifanya kupandisha majini.

Mtuhumiwa baada ya kusomewa mashitaka alikana na Hakimu Mkazi Mfawidhi Chiganga Ntengwa aliharisha kesi hiyo hadi hapo machi 6 na mtehumiwa alipelekwa lumande baada ya kushindwa kutimiza mashariti ya mdhamana ambapo alitakiwa adhaminiwe na mtu mmoja kwa dhamana ya shilingi milioni moja.

Chanzo: KATAVI YETU

WANAFUNZI WA KIKE WAPATWA NA UGONJWA WAKUANGUKA

WAZAZI na walezi ambao watoto wao wanasoma katika Shule ya Msingi Inyonga wilayani Mlele, mkoani Katavi wameitaka Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii kutumatimu ya wataalamu wa afya kuchuguza ugonjwa wa ajabu unaowakumba wasichana wanaosoma katika shule hiyo.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti na gazeti hili, wazazi hao wameelezea kupata hofu ya afya ya watoto wao wanaosoma katika shule hiyo, baada ya kukumbwa na ugonjwa huo wa ajabu ambao unasababisha waanguke wakiwa shuleni huku wakiweweseka na kupiga kelele.

"Tunaiomba Serikali iingilie kati ili kunusuru maisha ya watoto wetu hawa ambao sasa hawasomi tena, tunaomba watume wataalamu wa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii kuja huku kufanya uchunguzi wa kitabibu ili kubaini ugonjwa huu," anasema mmoja wa wazazi hao, Isabela John.

Isabela alisema wasichana hao wanaosoma darasa la tatu hadi la saba wakiwa na umri wa miaka katiya 12 na 16, wamekuwa wakishambuliwa na ugonjwa huo kwa zaidi ya miezi minne sasa.

"Ajabu ni kwamba watoto wetu hawa wanakumbwa na ugonjwa huu wa ajabu ambao hata wataalamu wa afya wilayani hapa wamekiri kuwa kila wanapowachunguza kitabibu watoto hawa hawaoni ugonjwa wowote. Isitoshe watoto hawa wakifika nyumbani, hawashambuliwi na ugonjwa huo isipokuwa pale wanapokuwa katika eneo hilo la shule," alisema mzazi mwingine, Patrick Ndolezi.

Wazazi wengine waliohojiwa na gazeti hili wamekiri kuwahamisha watoto wao wanaosoma katika shule hiyo wakihofia afya zao na wakiri kuhusisha ugonjwa huo na imani za kishirikiana kwamba shulehiyo imekumbwa na pepo wabaya.

Akizungumza kwa njia ya simu na gazeti hili, Mganga Mkuu wa Wilayaya Mlele, Dk Admihabesi Koni, alisema ugonjwa umewastaajabisha hata wataalamu wa afya wilayani humo kwani unawakumba wasichana tu wanaosoma katika shule hiyo wakati wanasoma pamoja na wenzao wa kiume."

Watoto hao wakikumbwa na ugonjwa huo hakika wanakuwa na nguvu ya ajabu, ni vigumu watu kuwathibiti kirahisi …Ugonjwa huu ulianza kwa wasichana wanaosoma darasa la tano, sita na saba lakini sasa umewakumba pia wanafunzi wa kike wanaosoma darasa la nne na la tatu.

"Lakini wanafunzi wa kike wanaosoma darasa la kwanza na la pili hawajakumbwa na ugonjwa huuna wamekuwa wakiendelea na masomo yao shuleni hapo kama kawaida," alisema.

Kwa mujibu wa Dk Koni, wanafunzi hao wanapokumbwa na ugonjwa huo wamekuwa wakifikishwa hospitalini kwa matibabu na kutibiwa kwa kudungwa sindano za 'valium' ambapo baadae wakizinduka hushikwa na butwaa na kuhoji walipo na kwa nini wamefikishwa hapo.

"Sisi wataalamu wa afya hatuamini kama ugonjwa huu unahusu imani za kishirikina, isipokuwa wanapofika hospitali kwa matibabu tunawakagua kitabibu na kuthibitisha kuwa hakuna dalili za ugonjwa wowote uliowakumba," alisema.

Aliongeza kuwa jitihada kadhaa zimeshafanyika ili kunusuru hali hiyo kwa viongozi wa madhehebu mbalimbali ya dini kuitwa kufanya ibada maalumu, lakini hali haijabadilika.

"Kulikuwa na uvumi uliozagaa kuwashule hiyo imekumbwa na mapepo wachafu na majini, hivyo waganga wa jadi walifika shuleni hapa na kufanya vitu vyao lakini wapi bila ya mafanikio yoyote yale," alisema Dk Koni.

Katibu Tawala wa Wilaya ya Mlele, Ephras Tenganamba alipozungumza na gazeti hili, amesema jitihada kadhaa zimefanyika bila mafanikio na hata baada ya kuwahamishia wanafunzi hao katika Shule ya Sekondari Inyonga jirani na shule hiyo, bado watoto hao waliendelea kuanguka huku wakipiga kelele.


Chanzo: Habari leo

OFISI ZA CHADEMA MPANDA ZAFUNGWA

MGOGORO wa uongozi ndani ya Chadema, umeingia katika hatua nyingine baada ya makada wa chama hicho wanaopingana kimisimamo, kufunga ofisi za chama hicho mjini Mpanda kwa zaidi ya wiki sasa.

Makada hao wamegawanyika na kuwa na kambi mbili tofauti, ambapo kila upande umeweka kufuli lake na walinzi wake, kuhakikisha hakuna atakayevunja na kuingia ofisini humo.

Ofisi za chama hicho ambazo ziko katika Mtaa wa Mji wa Zamani mjini hapa, kabla ya kufungwa zilikuwa zikitumiwa na viongozi wa chama hicho ngazi ya wilaya na mkoa pamoja na viongozi Jimbo la Mpanda Mjini ambalo kwa sasa Mbunge wake ni Said Arfi (Chadema).

Mvutano huu wa uongozi uliibuka mwanzoni mwa wiki iliyopita, ambapo viongozi wa chama hicho waliosimamishwa hivi karibuni, walifika ofisini hapo ili waendelee na shughuli zao za kiofisi na kukutaofisi zimefungwa kwa kufuli linginetofauti na waliloliweka wao.

Baada ya kubaini hivyo, viongozi hao wa Jimbo la Mpanda Mjini, walilazimika kuwahoji wenzao wa wilaya kulikoni ofisi za chama hicho kufungwa kwa kufuli lingine, tofauti na hilo, ndipo walipojibiwa kuwa wao si viongozi tena, kwa kuwa tayari wamesimamishwa uongozi.

Pia, uongozi wa wilaya wa chama hicho, wanadaiwa kuwajibu wenzao hao kuwa kwa kuwa wamesimamishwa uongozi, hawana mamlaka tena ya kufanya shughuli zozote za chama ndani ya ofisi hizo.

Hivi karibuni kikao cha maridhianoya chama hicho kilichofanyika kwenye ofisi cha chama hicho zilizopo katika mtaa wa Mji wa Zamani mjini hapa, kiliwasimamisha uongozi baadhi yaviongozi waandamizi wa chama hicho mkoani hapa na wengine wawili kusimamishwa uanachama.

Kikao hicho kilichoongozwa na Makamu Mwenyekiti wa Chadema Kanda Magharibi, Masanja Katabi, kiliwasimamisha uongozi Mwenyekiti wa Chadema wa Mkoa wa Katavi, John Malack, Katibu Mwenezi wa chama hicho mkoani hapa, John Matongo na Mwenyekitiwa Jimbo la Mpanda Mjini, Seif Sipia.

Wengine ni Katibu Mwenezi wa Jimbo la Mpanda Mjini Joseph Mona, ambaye pia ndiye Katibu wa Mbunge, Arfi na Katibu Mwenezi wa Jimbo la Mpanda Mjini, Godfrey Kapufi.

Mbali ya kusimamishwa uongozi, kikao hicho kimependekeza Kapufi na Diwani wa Kata ya Makanyagio, Idd Nziguye wavuliwe uanachama, kama ilivyokuwa kwa akina Dk Mkumbo na Mwigamba.

Pia, kikao hicho pia kiliazimia Arfi achunguzwe, wakimtuhumu kudhamini mkutano wa hadhara uliofanyika katika viwanja vya Maridadi mjini hapa, unaodaiwa kutumika kuwakashifu Lema na Mnyika.

ACT YASHUSHA BENDERA ZA CHADEMA

Chama cha Alliance For Change and Transparency Mkoa wa Kigoma, kimeshusha Bendera ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA tawi la Ujiji stendi ya zamani na kupandisha bendera ya (ACT) wakati wa uzinduzi rasmi wa matawi sita katika manispaa ya kigoma ujiji.

Akizungumza na wananchi wa eneo hilo, Katibu wa ACT Mkoa Athuman Kabogo alidai lengo la kushusha bendera hiyo ni hatua ya kukataa kugeuzwa kuwa vibaraka wa watu wengine kwa kukosa haki ya kuhoji na kuwania nyadhifa za chama hicho nahivyo kuanzisha ACT kama chama cha wanyonge kinachoweza kuwasikiliza na kutoa haki kwa kila mmoja Kabogo aliwataka wanachama wahitaji, wachukue kadi za ACTili chama kipate usajili kamili kwa mujibu wa sheria, kanuni na taratibu husika pamoja na kutoa michango endelevu,ikiwa ni jitihada za makusudi kuhakikisha chama kinasonga mbelekwa maslahi ya Taifa.

"Wananchi nyie ni chachu ya chama kuwepo kwenye mchakato wa uchaguzi mdogo wa wenyeviti wa serikali za mitaa kwa kukiamini na kukipatia ridhaa kiweze kuletamabadiliko ya kimaendeleo" alisema Juma Ramadhan aliyekuwa katibu kampeni wa CUF kigoma.

Kwa upande wa Katibu ACT Kanda Magharibi Wiston Moga alisema, lengo la chama ni kuleta mabadiliko kwenye ulingo wa siasa, ambapo wao wamedhamiria kutetea maslahi ya umma kwa lengo la kuondoa mfumo wa maslahi binafsi ambayo ni chachu ya vyama vya siasa kushindwa kuleta mabadiliko chanya kwa wananchi.

Katika ziara hiyo ya uzinduzi wa matawi ya chama husika, ACT kimefanikiwa kufungua matawi kwenye kata sita kati ya kata 19 zilizopo katika manispaa ya kigoma ujiji, huku baadhi ya viongozi kutoka UPD, CHADEMA na CUF wakijiunga na chama hichokwa kudai wanahitaji chama chenye uchungu na kukabilianana changamoto za wanyonge.

Hata hivyo wanachama 3500 wa chama cha Democrasia na Maendeleo Chadema katika tawi la Ujiji mkoani Kigoma wamehamia chama kipya cha Alliance For Change and Transparency (ACT).

Chanzo:Kigoma Yetu

SAMUEL ETO'O ANA UMRI WA MIAKA 39

KOCHA, Claude Le Roy, amesema alizungumza na Samuel Eto'o kwenye simu na kwamba alikasirikasana kwa kitendo cha umri wake kuhojiwa.

Kocha wa sasa anayemnoa straika huyo wa Cameroon kwenye klabu ya Chelsea, Jose Mourinho, kwenye mazungumzo yake ya kawaida tu natajiri mtengeneza saa wa Uswisi ambayo yalinaswa kwa siri na kurekodiwa, alisema hafahamu umri halisi wa Eto'o kama ni miaka 32 kama ilivyo kwenye pasipoti yake ya kusafiria au ni miaka 35.

Kabla ya kufikia kwenye kuhoji umri wa Eto'o, Mreno Mourinho alikuwa akijadili uwezo wa mastraika wake kwenye klabu ya Chelsea na mustakabali wa kunyakua ubingwa msimu huu.

Mourinho alilalamika kwamba washambuliaji wake wote wanamwangusha kutokana na kushindwa kufunga mabao. Washambuliaji waliopo kweye kikosi cha Chelsea wote ni makini; Demba Ba, Fernando Torres na Eto'o, lakini wote hao wamekuwa butu na kushindwa kufunga mabao.

"Tatizo la Chelsea hakuna wafungaji," alisema Mourinho. "Ninaye Eto'o, lakini umri wake ni miaka 32, pengine inaweza kuwa 35, huwezi kujua," alisema Mourinho.

Kocha, Le Roy, aliyewahi kumnoa Eto'o kwenye kikosi cha Cameroon, anasema straika huyo hakupendezwa na kauli ya Mourinho kumsema kwamba umri wake ni mkubwa kuliko unaotambulika rasmi.Eto'o amesisitiza kwamba umri wake ni miaka 32. Jumatano iliyopita, Chelsea ilikuwa na mechi muhimu ya Ligi ya Mabingwa Ulaya dhidi ya Galatasaray na kwamba iliaminika kwamba baada ya mchezo huo, Mourinho na Eto'o watahitaji kuwekana sawa.

Lakini, wakati Eto'o akisisitiza kwamba umri wake ni miaka 32, kama ulivyoandikwa kwenye pasipoti yake, mke wa zamani wa staa huyo ameibuka na kuchafua zaidi hali ya hewa baada ya kueleza kwamba umri wa supastaa huyo wa zamani wa Barcelona ni mkubwa kuliko hata uliotajwa na Mourinho.


*MKEWE AFICHUA

Mrembo, Anna Barranca, ambaye alizaa na Eto'o mtoto mmoja, amefichua wazi na kusema umri wastaa huyo ni miaka 39.

Mourinho alihisi Eto'o anaweza kuwa na umri wa miaka 35, lakini mwanamke huyo wa Kitaliano ametoa kali baada ya kudai kwamba Eto'o amepunguza miaka saba ya umri wake wa kweli.

Anna anasema: "Nadhani Samuel umri wake si miaka 35 ni zaidi ya 39. Samuel alizaliwa 1974 na sasa ana umri wa miaka 39."

Anna umri wake wa sasa ni miaka 43, mtoto aliyezaa na Eto'o anaitwa Annie.

Baada ya mjadala wa umri wa Eto'o kushika kasi, gazeti la The Sun lilimtafuta aliyekuwa mke wa staa huyo na kufanya mahojiano naye ilikufahamu ukweli halisi, ndipo mwanamke huyo alipasua kwamba Mcamerooni huyo ana umri wa miaka 39.

Anna na Eto'o walimzaa Annie wakati mchezaji huyo alipokuwa akiichezea Mallorca. Kuna wakati fulani, mwanamke huyo aliwahi kumlalamikia mchezaji huyo kutokana na kushindwa kutoa huduma kwa ajili ya malezi ya mtoto.


*TABIA YA ANNA

Mwanamke huyo anayefanya kazi saluni, anadaiwa kuwahi kuuza habari zake kwenye gazeti akimtuhumu Eto'o kwamba hana anachokifanya kwa mtoto wake na kwamba haishi kwa kutegemea pesa za mwanasoka huyo.

Mrembo huyo alisema Eto'o amekuwa akishindwa kutimiza wajibu wake wa kumlea mtoto wao,kabla ya sasa kuibuka na kusisitiza kwamba umri wa mchezaji huyo si miaka 32 na kwamba umri wake ni zaidi ya miaka 39.


*ETO'O ANG'AKA

Kwenye hali ya kuonekana kuwa na hasira, Eto'o alijifanya kupuuza kauli ya Mourinho kudai kwamba staa huyo ana umri mkubwa baada ya kusisitiza kwamba ataendelea kufunga mabao hata kama atafikisha umri wa miaka 50.Staa huyo kwa kejeli alisema aliweza kuifunga 'hat-trick' Manchester United licha ya kuwa na umri huo mkubwa, hivyo suala la kufunga mabao kwake ni jambo la kawaida.

"Mimi ni Samuel Eto'o, nitasemaje sasa?" Alisema alipozungumza na Sky Sports News baada ya mechi dhidi ya Galatasaray.

"Kama kwenye umri wa miaka 36 na 37 naweza kuifunga mabao matatu Manchester United kwenye mechi moja, hiyo ina maana kwamba naweza kuendelea kutikisanyavu hadi nitakapokuwa na umri wa miaka 50. Mimi sijali kitu, kitu muhimu kwangu ni kujitolea kwa nguvu zote katika kuisaidia timu yangu ili kutwaa mataji."

Kwenye mchezo dhidi ya Galatasaray, Eto'o aliingizwa katika dakika 68, kuchukua nafasi ya Torres ambaye alifunga bao kwenye sare ya bao 1-1 katika mchezo huo wa kwanza wa hatua ya mtoano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya uliofanyika Istanbul, Uturuki, Jumatano iliyopita.


Chanzo:Mwanaspoti