WAKRISTO WAKIMBIA KANISA

WAKRISTO nchini Ujerumani wanazidi kujiondoa katika makanisa yao wakiudhiwa na utoajiwa zaka (kodi ya kanisa) ambayo wanaona ni kubwa.

Imeelezwa kuwa katika majimbo ya Bavaria na Baden Wurttemberg sadaka (zaka) ni asilimia nane ya mapato halisi.

Maeneo mengine ya Ujerumani sadaka ni asilimia 9. Kwa mujibu wa taarifa zinazopatikana mtandaoni zinasema kwamba mwaka huu kumekuwepo na kundi kubwa linalojiondoa katika Ukristo (Ukatoliki na Uprotestanti) nchini humo.

Waumini elfu kumi wa Kiprotestanti wamejiondoa kutoka Kanisa la Berlin, idadi inayoelezwa kuwa kubwa kuliko waliojitoa mwaka 2011 na 2012 wakichanganywa pamoja.

Aidha ukanda wenye Ukatoliki mkubwa wa Bavaria,Wakatoliki 14,800 walijiondoa kati ya Januari na Juni mwaka huu ukilinganisha idadi ya waliojiondoa 2013 kwa mwaka mzima. Zaka ya kanisa nchini humo hukatwa moja kwa moja na Hazina ya Ujerumani.

Mpaka mwaka huu walipa kodi walitakiwa kujieleza kuhusiana na zaka lakini kuanzia mwaka ujao zaka hizo zitakatwa moja kwa moja na benki zao. Kutokana na mabadiliko hayo ya sheria, benki zitalazimika kujua madhehebu ya wateja wao.

Pamoja na masuala ya sadaka, masuala mengine yanayosababishawatu kujitoa ni ndoa ambapo imeelezwa wengi wa wanandoa walioachana wameenda kuoa au kuolewa kwingine, na wanajitoa wakihofia adhabu ya kufungiwa kiimani.

Pamoja na waumini kupungua makanisa hayo yamekuwa yakiingiza fedha nyingi za kanisa. Mwaka jana Kanisa Katoliki lilikusanya euro bilioni 5.5 (Sh trilioni 11.5) wakati makanisa ya Kiprotestanti yalikusanya euro bilioni 4.8 (Sh trilioni 10).

MAHAKAMA IMEWATIA HATIANI WALIOJARIBU KUMUUA JEN. NYAMWASA

Mahakama nchini Afrika ya Kusini imewatia hatiani watu wanne kwa kujaribu kumuua Jenerali Faustin Nyamwasa, aliyewahi kuwa mshirika wa karibu wa Rais Paul Kagame wa Rwanda, ambaye alipigwa risasi nyumbani kwake jijini Johannesburg miezi michache baada ya kutorokea huko akitokea Rwanda.

Nyamwasa anasema utawala wa Kagame uliwakodi watu hao ili wamuue, madai ambayo Rwanda inayakanusha, ingawa serikali imekuwa ikituhumiwa kwa kuwafuatilia wakosoaji wake  wanaoishi nje.

Mkuu wa zamani wa usalama wa taifa wa Rwanda, Patrick Karegeya, aliuawa huko huko Afrika ya Kusini mwaka 2013 na uchunguzi wa kifo chake bado unaendelea.

YANGA WAMSHITAKI OKWI TFF

Klabu ya Young Africans imemshitaki mchezaji Emmanuel Okwi kwa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) na kuwasilisha nakala kwa shirikisho la soka Barani Afrika (CAF) na shirikisho la soka duniani (FIFA) kwa kuingia mkataba na timu nyingine wakati akiwa bado ana mkataba wa miaka miwili.

Akiongea na waandishi wa habari makao makuu ya klabu ya Yanga mitaa ya Twiga/Jangwani, mwenyekiti wa Yanga Bw Yusuf Manji amesema wameshangazwa nakitendo hicho kilichofanywa na viongozi wa Simba , wakala wake na mchezaji mwenyewe.

"Emmanuel Okwi awali tulishapeleka malalamiko TFF na kuwapa nakala CAF na FIFA juu ya kufanya mazungumzo na timu ya Wadi Degla FC ya nchini Misri na kufikia klabu hiyo kutuma ofa ya kutaka kumnunua bila kuwasiliana na uongozi wetu" alisema Yusuf.

Ikiwa hilo tunasubiria majibu kutoka TFF jana mchezaji huyo amesaini mkataba mwingine, hii inaonyesha ni jinsi gani mchezaji huyu kuna watu walikua wanamrubuni,kwa kusaini mkataba mwingine kitu ambacho amekiuka sheria za FIFA za usajili.

Baada ya kuona jana amesaini mkataba na Simba, Yanga tulichokifanya leo ni kuandika barua nyingine TFF juu ya suala hilo na kuomba kulipwa fidia ya US Dollar 500,000 (sawa na TZS 800,000,000/=) kutoka kwa klabu yaSimba, wakala wake na mchezaji mwenyewe aliongeza "Manji"Aidha uongozi wa Yanga umeiomba TFF kuwa imelipatia ufumbuzi sualahilo ndani ya siku saba, na kama siku saba zikipita basi uongozi wa Yanga utakwenda moja kwa moja FIFA na ikishindakana mahakama ya soka CAS.

Lengo sio kuikomoa timu ya Simba,bali tunachotaka ni sheria ifuatwe, Okwi alikua ameitumikia klabu ya Yanga kwa kipindi cha miezi sita tu, na kuwa amebakiza mkataba wa miaka miwili mpaka msimu mwishoni mwa msimu wa 2015/2016.

Mchezaji anayekutwa na kosa la kusaini sehem mbili adhabu yake nikufungiwa kucheza soka kuanzia mwaka mmoja na kuendelea huku klabu husika ikifungiwa kusajili kuanzia miaka mwili na kuendela nakushushwa daraja au adhabu zote kwa pamoja.

WATU KUMI WAFARIKI PAPO HAPO NA WENGINE SABA WAJERUHIWA KATIKA AJALI JIJINI MBEYA

WATU kumi wakiwemo watoto wawili wamefariki dunia papo hapo na wengine saba wamejeruhiwa vibaya katika ajali iliyohusisha magari mawili.

Ajali hiyo ilitokea jana majira ya saa nne asubuhi ikihusisha gari ndogo ya abiria maarufu daladala lenye namba za usajili T 237 BFB aina Toyota Hiace na gari kubwa aina ya Fuso lenye namba za usajili T 158 CSV.

Kwa mujibu wa mashuhuda wa ajali hiyo wamesema ajali hiyo ilitokea maeneo yaMbalizi baada ya Hiace iliyokuwa ikitokea Mbeya mjini kuelekea Mbalizi kulivaa Fuso ilikuwa ikiingia barabarani.

Walisema inasemekana dereva wa Hiace gari yake ilimshinda kutokana na kutelemka mlima mkali wa Mbalizi inagawa pia walimtupia lawama dereva wa Fuso ambaye alikuwa akiingia barabarani bila kuchukua tahadhari.

Muuguzi Mkuu wa Hospitali teule ya Ifisi Mbalizi, Sikitu Mbilinyi, ambako Majeruhi na marehemu walikimbizwa hapo alithibitisha kupokea majeruhi 7 ambapo alisema kati yao ni wanawake 3 na wanaume 4.

Alisema kati ya majeruhi hao wawili wamepewa rufaa kwenda hospitali ya Rufaa Mbeya kutokana na kuhitaji msaada zaidi huklu wengine wakiendelea kupatiwa msaada wa haraka ili kunusuru hali zao.

Mbilinyi aliongeza kuwapia wamepokea miili ya marehemu 10 wakiwemo watoto wawili na Wanawake wanne na Wanaume wanne.

Hata hivyo majina ya majeruhi na marehemu hayajaweza kupatikana mara moja kutokana na kuwa katika hali mbaya ambapo Dereva wa Fuso akitokomea mara baada ya tukio.

Source: MBEYA YETU BLOG (http://mbeyayetu.blogspot.com/2014/08/breaking-news-tukio-katika-picha-watu.html?spref=fb&m=1)

GARI YA ULINZI WA RAIS YAIBIWA?

Taarifa za kutatanisha za kuibiwa kwa gari la ulinzi wa Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta zimeibuka nchini humo.

Taarifa hii ilitolewa na baadhi ya vyombo vya habari ingawa msemaji wa Rais Kenyatta ameikanusha taarifa hiyo akisema kuwa gari lililoibiwa lilikuwa la idara ya polisi likiendeshwa na inspekta mkuu wa polisi.

Gari hilo lililokuwa lisemekana kuwa na uwezo wa kuhimili risasi, liliibiwa usiku wa Jumatano na kwamba aliyekuwa analiendesha gari hilo alikuwa afisa wa polisi.

Kwa mujibu wa taarifa iliyochapishwa kwenye mtandao wa Daily Nation ikimnukuu mtu anayesemekana kuwa dereva wa gari hilo la kifahari alilazimishwa kuvua nguo zake kabla ya kupokonywa gari hillo.

Gari lenyewe lilikuwa na nambari ya usajili ya kibinafsi.

Ni gari la polisi au la Rais?

Kwa mujibu wa msemaji wa Rais, gari hilo aina ya BMW 735 la mwaka 2000, lilikuwa linaendeshwa nainspekta wa polisi alipovamiwa na wanaume wanne waliokuwa wamejihami karibu na eneo la Ruai viungani mwa mji mkuu Nairobi.

Msemaji wa Rais Manoah Esipisu amekanusha madai kwamba gari hilo lilikuwa moja ya magari ya ulinzi wa Rais Uhuru Kenyatta kama ilivyokuwa imenukuliwa na baadhi ya vyombo vya habari

Bwana Manoah amesema kuwa Inspekta aliyekuwa anaendesha gari hilo aliporwa dola mia saba na simu yake gari hilo lilipoibiwa saa tatu usiku.

Alitekwa na majambazi hao kwa karibu saa tano kabla ya kumwachilia usiku wa manane.

Alisema kuwa wezi hao walitoweka na gari hilo ambalo alisema hutumiwa kwa shughuli za polisi na kwamba tayari msako umeanzishwa ingawa gari hilo bado halijapatikana.

Kadhalika alikanusha kuwa gari hilo lilikuwa la ulinzi wa Rais na kwamba lenyewe lilikuwa na uwezo wa kuhimili risasi.

Visa vya wizi wa magari na utekaji wa madereva sio jambo geni nchini Kenya ila kilichowashangaza wengi ni kwamba je vipi gari la ulinzi wa Rais liibiwe?

Bwana Manoah amesema takwimu zinaonyesha visa vya uhalifu vimepungua hasa katika jiji kuu Nairobi katika miezi ya hivi karibuni na kwamba ulinzi unaendelea kuimarishwa.

JAJI AHOJI WINGI WA KESI ZA SHEIKH PONDA

Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam imemtaka katibu wa Jumuiya na Taasisi za Kiislamu Tanzania, Sheikh Issa Ponda aeleze sababu za kuwa na kesi nyingi, huku akihusishwa na matukio mbalimbali ya uhalifu nchini.

Pia mahakama hiyo imeamuru vyombo vya dola kuacha kuwazuia wafuasi wake kuingia mahakamani kusikiliza kesi zake, na kushauri kama wana wasiwasi nao, waweke mashine za ukaguzi katika mlango wa kuingilia mahakamani hapo.

Mwenendo huo wa Sheikh Ponda ulihojiwa mahakamani hapo na Jaji Augustine Shangwa juzi kabla ya kuanza kusikiliza rufaa yake ya kupinga hukumu ya Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, iliyomtia hatiani katika kesi ya jinai, mwaka 2012.

"Sheikh Ponda, sijui ni kwa nini unakesi nyingi kiasi hiki. Kwenye Mahakama ya Hakimu Mkazi (Kisutu) una kesi, Mahakama Kuu una kesi. Nani yuko nyuma ya kesi zako? Je! Serikali inakuchukia?" alihoji Jaji Shangwa.Licha kumhoji Sheikh Ponda maswali hayo, alimweleza kuwa kama atakuwa na jambo la kuzungumza, atampa nafasi siku nyingine rufaa yake itakapotajwa. Pia Jaji Shangwa alimshauri apunguze mapambano.

"Ikiwezekana uyapunguze (mapambano) maana dunia hii si yakupambana nayo," alisema Jaji Shangwa na kusisitiza kuwa lazima ajiulize kwa nini ana kesi nyingi.

Jaji Shangwa aliendelea kusema: "Jambo likitokea Zanzibar, wewe umo; likitokea Morogoro umo; likitokea Dar es Salaam umo. Bahati mbaya kuna kikundi cha Uamsho kinadaiwa kulipua mabomu na kuua watu, nasikia na wewe unatajwa kuhusishwa."Hata hivyo baadaye Jaji Shangwa alimuuliza Ponda kama ana la kueleza kuhusu wingi wa kesi zinazomkabili.

Sheikh Ponda alidai kuwa kesi hizo ni mzigo anaotwisha kutokana na kutetea kile alichokiita masilahi, huku akijitetea kuhusu hukumu ya kesi iliyomtia hatiani ambayo amekata rufaa kuipinga, akieleza kuwa eneo analodai kuvamia ni mali ya Waislamu.

Hata hivyo, Jaji Shangwa alimkata kauli akisema anayoyaeleza yanapaswa kusemwa na mawakili wake katika rufaa hiyo kama alikuwa na hatia au la. Alimtaka aeleze ni kwanini anakabiliwa na kesi nyingi.

Hata hivyo, wakili wake Juma Nassoro alisimama na kuieleza Mahakama kuwa si kwamba mteja wake ana kesi nyingi, bali anakabiliwa na kesi mbili tu moja iliyokuwa Mahakama ya Kisutu ambayo ndiyo wameikatia rufaa na ile iliyoko Mahakama ya Hakimu Mkazi Morogoro.

Awali, wakati akivipiga 'stop' vyombo vya dola kuwazuia wafuasi wake kuingia mahakamani, Jaji Shangwa alisema: "Huyu Sheikh Ponda ana wafuasi wengi, wanahitaji kuja kusikiliza kesi yake. Vyombo husika visiwazuie, waacheni waje wasikilize kesi ya Sheikh wao." Pia aliwaonya wafuasi hao kuacha mapambano na vyombo vya dola.

JWTZ KUWACHUNGUZA MAKOMANDO WA NEPAL

JESHI la Wananchi Tanzania(JWTZ), limeshtushwana taarifa za kuwepo kwa makomandoo wa kijeshi kutoka nchi ya Nepal ambao waliingia nchini kinyemela kwa madai ya kutafuta kazi.

Pia, JWTZ imesema taratibu za mwanajeshi kwenda kuajiriwa sehemu nyingine ya nchi haipo karibu duniani kote, hivyo suala hilo wanalifuatilia kwa karibuili kupata undani wake, ambapo hati za kusafiria za makomandoo hao zikiwa zinashikiliwa, huku Serikali ikibeba jukumu la kuwahudumia.

Akizungumza na gazetihili jana kwa njia ya simu,Mkurungenzi wa Idara ya Mawasiliano JWTZ, Luteni Kanali Erick Komba alisema kwa mujibu wa kanuni za jeshini kwamba, mwanajeshi kutoka nchi moja kwenda nyingine suala halipo.

Hata hivyo, Komba alisema inawezekana kukawa na makubaliano maalumu ya nchi au katika jumuia za kusaidia kijeshi, ndipo wanajeshi waliokubalika nchi na nchi hutolewa kwa lengo la kazi maalumu, kama ilivyo kwa vikosi vya kulinda amani ambavyo JWTZ hushiriki.

"Wanajeshi kwa kawaida haajiriwi kama wafanyakazi wengine, ila huteuliwa na jopo maalumu na baada ya kuridhishwa, hupewa nafasi ya kujiunga na jeshi, hivyoni mapema kulisemea na ningeomba uwasiliane na watu wa uhamiaji kwa maelezo zaidi,"alisema Luteni Kanali Komba.

Mkuu wa Idara ya Uhamiaji Dar es Salaam, Grace Hokororo alisema tayari wahamiaji 12 wa Nepal wametumiwa tiketi kutoka kwa ndugu zao na wanatarajiwa kusafirishwa kurejea kwao Septemba 2, mwaka huu.

Alisema wanawashikilia wahamiaji 50, ambapo 12 kati yao ndiyo walioletewa tiketi na waliobaki wanaendelea kuhifadhiwa kama walivyokutwa kwenye nyumba ya mzee mmoja ambaye hakumtaja jina lake.

"Tumefi kia hatua ya kumwomba mzee atusaidie kuwatunza kwenye nyumba hiyo walimokamatiwa, wakati taratibu nyingine zikifanyika, ikiwa pamoja na kuwatafut amawakala wawili waliowaleta nchini," alisema.

Hokororo alisema mawakala waliowaleta wahamiaji hao,walifahamika kwa majina ya Ali Hamidu Ali au kwa jina lingine anajulikana kama Ali Prosper Ngurigwa ambaye ni Mtanzania akishirikiana na raia wa Nepal, Devi Ram Dhamala akiwa na pasipoti 4277471.

Alisema kwa mujibu wataarifa zilizopatikana kutoka kwa wahamiaji hao, zinasema waliletwa nchini baada ya kurubuniwa kuwa, kuna kazi zenye ujira mzuri watakazo pata pindi wakifika Tanzania."

Kuna gharama walilipa, pia kulipa tiketi ya kwenda na kurudi, lakini cha ajabu walipofi kahapa nchini kupitia uwanja wandege, walipelekwa Kijitonyama na Tegeta kwa mafungu na kula yao ikawa ya shida hadi suala hilo lilipofahamika hadharani.

"Hatuwezi kuwaweka ndani kutokana na sheria zilizopo za ndani na nje ya nchi, kwa vile watu hao walidaganywa kwa lengo la kupata ajira, hivyo wanakuwa waathirika wa janga hilo," alisema na kuongeza kwa sasa Serikali imechukua hatua ya kuwahudumia hadi watakapo ondoka nchini.

Makomandoo hao walikamatwa juzi maeneo ya Tegeta jijini Dar es Salaam wakiwa wamehifadhiwa katika nyumba mbili tofauti, huku wakiwa na sare za kijeshi la Nepal.

Chanzo: Jambo Leo

MAJAJI WATATU KUAMUA HATMA YA BUNGE LA KATIBA

JOPO la Majaji watatu linatarajia kusikiliza ombi kwa Mahakama itoe amri ya kusimamisha Bunge Maalumu la Katiba lililofunguliwa na Mwandishi wa Habari, Said Kubenea katika Mahakama Kuu, Kanda ya Dar es Salaam.

Jopo litakalosikiliza ombi hilo linaongozwa na Jaji Augustine Mwarija. Wengine ni Jaji Dk Fauz Twaib na Jaji Aloysius Mujulizi lakini bado halijapangiwa tarehe yakusikilizwa.

Kubenea aliwasilisha ombi hilo mwishoni mwa wiki iliyopita dhidi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG) kupitia kwa wakili wake Peter Kibatala, akiomba Bunge hilo lisimamishwe hadi Mahakama itakapotoa tafsiri sahihi ya Bunge hilo kuhusu mamlaka iliyonayo na kama ni sahihi kwenda kinyume na Rasimu.

Katika ombi hilo, Kubenea anaiomba Mahakama itoe amri hiyo wakati wakisubiri uamuzi wa Mahakama kuhusu tafsiri sahihi kama Bunge hilo linaweza kwenda kinyume na Rasimu pia tafsiri kuhusu mamlaka ya Bunge hilo.

Aidha anaomba Mahakama itoe tafsiri ya kifungu cha 25(1) na (2) cha Sheria ya Mabadiliko ya Katiba ya Nchi ambacho kinaeleza mamlaka ya Bunge hilo.

Ombi hilo lililowasilishwa chini ya hati ya dharura limeungwa mkono na hati ya kiapo ya Kubenea ambapo anaeleza, Desemba Mosi, mwaka 2011, Bunge la Tanzania lilipitisha mabadiliko ya Katiba na kuanza maandalizi ya kupata Katiba mpya.

Hati hiyo inadai kuwa Tume ya Mabadiliko ya Katiba iliundwa kwa ajili ya kusimamia mchakato huo, ambapo Rais alitoa maelekezo kwaTume hiyo kukusanya maoni kwa wananchi kwa ajili ya kuandaa Rasimu ya Katiba mpya.

Kwa mujibu wa hati hiyo, Tume ilianza kutekeleza kazi hiyo kwa kukusanya maoni kwa wananchi kupitia mikutano na njia nyingine ikiwemo Mabaraza ya Katiba katikawilaya zote ambapo wananchi 33,537 walitoa maoni.

Tume iliandaa Rasimu ya pili ya Katiba na Desemba 8, 2013, iliikabidhi kwa Rais ambapo Rais kwa mamlaka yake alielekeza Bunge Maalumu kujadili Rasimu hiyo.

Anadai baada ya kuanza kwa Bungehilo wajumbe walitofautiana kutokana na kuingizwa kwa hoja ambazo hazipo kwenye Rasimu ndipo wajumbe wengine ambao ni Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) wakatoka bungeni kwa madai Rasimu hiyo haiwezi kufanyiwa marekebisho kama wajumbe walivyokuwa wanadai.

Chanzo: Habari leo

POLISI WAMKAMATA MPIGA RISASI WANAWAKE ARUSHA

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha Liberatus Sabas amesema jeshi hilo linamshikilia mtuhumiwa wa matukio ya kuwapiga risasi wanawake jijini Arusha.

Mtu huyo ni Adam Mussa, mwenye umuri wa miaka 30, mkazi wa Majengo Jijini Arusha ambaye amekamatwa na bastola mbili zikiwa na risasi kumi.

Akiongea na waandishi wa habari ofisini kwake, Kamanda Liberatus Sabas amesema mtuhumiwa huyo alikamatwa Agosti26 mwaka huu, majira ya usiku, nyumbani kwake Majengo Juu.

Kamanda Sabas amesema baada ya kumkamata mtuhumiwa na kumhojiambapo alikiri kuhusika katika matukio yanayoendelea jijini Arusha ya upigaji wanawake risasi na moja kati ya silaha hizo iliibiwa ndani ya gari la mfanyabiashara Seleman Bakari Msuya mkazi wa Sombetini, baada ya watu wasiojulikana kuvunja kioo cha gari na kuichukua.

Mtuhumiwa anatarakiwa kufikishwa mahakamani mara baada ya upelelezi kumalizika.

Kamanda Sabas ametoa wito kwa wananchi kuendelea kutoa siri za mtandao huo uliozuka ghafla mwezo Agosti mwaka huu na kujeruhi na kuua wanawake wenye magari mjini Arusha, ambapo hadi sasa tayari watu nane wanashikiliwa kwa kuhusiana na matukio hayo.

DROO YA LIGI YA MABINGWA ULAYA

Group A: Atlético, Juventus, Olympiacos, Malmö

Group B: Real, Basel, Liverpool, Ludogorets

Group C: Benfica, Zenit, Leverkusen, Monaco

Group D: Arsenal, Dortmund, Galatasaray, Anderlecht

Group E: Bayern, Man City, CSKA, Roma

Group F: Barcelona, PSG, Ajax, APOEL

Group G: Chelsea, Schalke, Sporting, Maribor

Group H: Porto, Shakhtar, Athletic Club, Bate Borisov

WANAMGAMBO KUCHUKULIWA HATUA LIBYA

Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa limepitisha azimio linalotoa wito wa kusitisha mapigano nchini Libya haraka iwezekanavyo na kuweka vikwazo dhidi watu wanaohusika na ghasia zinazoendelea nchini humo kati ya makundi yawanamgambo wanaopingana.

Balozi wa Libya katika Umoja wa Mataifa ameliita azimio hilo kama"msingi", lakini ameonya kuwepo kwa vita vya wenyewe kwa wenyewe.

Orodha ya watakaokabiliwa na vikwazo vya uchumi bado haijaamuliwa.

Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa limeshtushwa na kuongezeka kwa mapigano katika ya makundi ya wanamgambo na vikundi vya kijeshi.

Mapigano ya karibuni yamejikita katika uwanja wa ndege wa kimataifa, Tripoli, ambao kwa sasa unadhibitiwa na wanamgambo kutoka Misrata na miji mingine yakiwa chini ya mwavuli wa "Mapambazuko ya Libya", ikiwa ni pamoja na makundi mengine ya kiislam.

Yameuchukua uwanja huo kutoka mikononi mwa kikundi cha wanamgambo wenye makaazi yao katika mji wa Zintan, licha ya tuhuma za mashambulio ya anga kufanywa na Misri na Muungano wa Falme za Kiarabu wakililenga kundi lenye uhusiano na makundi ya wanamgambo wa Kiislam.

Pia Libya inakabiliwa na mgogoro wa kisiasa, kwa viongozi wawili wanaopingana na mabunge ambayo yanaendesha shughuli zao katika sehemu mbili tofauti za nchi, kila bunge likiungwa mkono na makundi ya wanamgambo wenye silaha.

Uzuiaji wa silaha waimarishwa Jumatano, Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kwa kauli moja walipitisha azimio ambalo linatishia kuwawekea vikwazo, kama vile utaifishaji wa mali, kuzuia safari dhidi ya viongozi wa makundi ya wanamgambo na wafuasi wao.

Marekani imeishutumu Misri na Muungano wa Falme za Kiarabu kwa kufanya mashambulio ya anga yakilenga vikundi vya wanamgambo vyenye uhusiano na wapiganaji wa Kiislam.

Azimio hilo limesema kuwa vikwazo vitawalenga watu binafsi na makundi yanayohatarisha usalama wa Libya au kupuuza mageuzi ya kisiasa nchini humo.

Pia azimio limeimarisha upigaji marufuku silaha, amri ambayo tayari imewekwa ambapo mtu au kundi anayetaka kuingiza silaha Libya atahitaji idhini ya mauzo yoyote ya silaha au kibali cha kusafirisha silaha kwenda nchini humo.

ARFI ATAMANI UKAWA WARUDI BUNGENI

MBUNGE wa Mpanda Mjini, ambaye ni mjumbe wa Bunge Maalumu la Katiba, Said Arfi (Chadema), ameelezea matamanio yake kuona wajumbe wa Bunge Maalumu la Katiba, wa kundi la Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa), kurudi bungeni.

Amesema kwa hali inavyokwenda sasa, mapendekezo ya upande mmoja wa chama tawala ndiyo yanayopita na kuongeza: "Tungekuwepo wote ndani ya Bunge hili, lisingewezekana kwa sababu tungepinga kwa nguvu zaidina hata kuhakikisha Bunge haliendelei."

Akizungumza na waandishi wa habari jana mjini hapa, Arfi alisema kuondoka kwa Ukawa ndani ya Bunge, ni sawa na nyani aliyekabidhiwa shamba la mahindi lisilo na mlinzi.

Alipoulizwa kama wajumbe wa kuteuliwa wa Kundi 201, wangeweza kusaidia kutetea baadhi ya hoja za Ukawa, alisema wajumbe wa kundi hilo wanaangalia maslahi ya makundi yao zaidi na ya wananchi kwa ujumla.

Pamoja na kutokuwepo nguvu ya ajenda za Ukawa, Arfi alikiri kuwepo kwa mabadiliko mazuri yaliyofanyika katika Rasimu ya Pili ya Katiba mpya, yatakayo nufaisha wananchi hasa wakulima, wafugaji na wavuni.

Arfi, ambaye amejitapa hajutii uamuzi wake wa kushiriki Bunge hilo, akipingana na wajumbe wenzake wa Ukawa, alitaja mazuri hayo kuwa ni pamoja na haki za wakulima, wafugaji na wavuvi kumiliki ardhi, haki ya hifadhi ya jamii, haki ya makazi na haki ya afya, chakula, maji safi na salama.

Hata hivyo, Arfi alidai amepanga kwenda mahakamani ili kupata ufafanuzi juu ya alichoita Bunge hilo kuachana na rasimu ya iliyokuwa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, iliyokuwa chini ya Mwenyekiti Jaji Joseph Warioba.

Amedai kuwa kinachofanyika sasa ni kuandika rasimu nyingine ili iendane na muundo wa serikali mbili ambao ndio CCM wanaoutaka, kazi ambayo imekuwa rahisi kwa sababu hakuna upinzani wa kutosha kuzuia.

Hata hivyo, tayari Mwenyekiti wa Bunge Maalumu, Samuel Sitta, alishatoa ufafanuzi kuwa msingi wamajadiliano yote tangu Bunge hilo limeanza, ni Rasimu ya Katiba iliyowasilishwa na Tume ya Mabadiliko ya Katiba Mpya na hakuna rasimu nyingine inayojadiliwa isipokuwa hiyo ya Tume."Maana ya rasimu ni andiko ambalo halijajitosheleza … anayekabidhiwa rasimu, anayo hakina mamlaka ya kuirekebisha. Vinginevyo kujadili rasimu hakuna sababu.

"Itakuwa ni jambo la ajabu na lisilona mantiki yoyote kuwa taasisi iliyopewa mamlaka ya kujadili rasimu, ikishaijadili iiache ibaki kama ilivyokuwa wakati ilipowasilishwa," alisema Sitta.

Hata hivyo, Arfi alisema kutokana na mwandishi wa habari Said Kubenea kupitia mwanasheria wake, Peter Kibatala kufungua kesi Mahakama Kuu kutaka mahakama kuzuia kuendelea kwa Bunge la Maalumu la Katiba, anasubiri ushauri wa wanasheria wake kuhusu azma yake ya kufungua kesi hiyo.

Kuhusu Muungano, Arfi alisema kwa sasa wajumbe wanajadili namna ya kuboresha Muungano kwa kupunguza kero zake, ikiwemo kuanzishwa kwa Makamu wa Rais watatu; wa kwanza ambaye atatokana na Mgombea Mwenza, wa pili Rais wa Zanzibar na wa tatu Waziri Mkuu.

Alitaja jambo jingine la kuboresha Muungano kwa kuondoa kero kuwani kuanzishwa kwa mabunge matatu ya Jamhuri, Zanzibar na Tanganyika.

Kwa sasa Bunge Maalumu la Katiba linaendelea na vikao vya kamati yakupitia rasimu ya Katiba na kesho kutwa kamati hizo zinatarajiwa kukamilisha kazi zao kupisha kamati ya uandishi chini ya Mwenyekiti Andrew Chenge kuandaa maoni ya kamati zote na Septemba 2, mwaka huu majadiliano yataendelea ndani ya Bunge maalumu kwa ajili ya utungaji wa Katiba mpya.

Chanzo: Habari Leo

MIZENGO PINDA AUTAKA URAIS

Waziri Mkuu, Mizengo Pinda ameingia rasmi katika mbio za kuwania urais kupitia Chama ChaMapinduzi (CCM), hatua ambayo imebadili mwelekeo wa kinyang'anyiro cha nafasi hiyo kubwa ya uongozi nchini kuelekea Uchaguzi Mkuu 2015.

Gazeti hili limethibitisha kwamba Pinda tayari ameamua kujitosa kuwania nafasi hiyo kupitia CCM ambayo tayari inawaniwa na makada wa chama hicho wasiopungua 15 na baadhi yao wameishatangaza nia zao kwa nyakati tofauti.

Habari kutoka ndani ya CCM zinasema uamuzi wa Pinda kuwania urais mwaka mmoja tu kabla ya uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba mwakani, umesababisha kiwewe miongoni mwa wagombea na kunakifanya kinyang'anyiro hicho kuchukua sura mpya.

Kiongozi mmoja mwandamizi wa CCM aliliambia gazeti hili siku chache zilizopita mjini Dodoma kuwa: "Na sisi tumesikia kwamba PM (Waziri Mkuu) amejitosa na kama ni kweli atawasumbua wagombea wengi kutokana na rekodi yake hasa katika uadilifu."

"Yeye (Pinda) ana faida tatu kubwa; kwanza hana kundi katika chama, anaelewana na watu wote, pili nafasi yake ya uwaziri mkuu inampa nafasi ya kufahamika kwa watu wengi na tatu rekodi yake ya uadilifu, hana kashfa za ovyoovyo, labda kama ataharibu dakika hizi zamwisho," alisema kiongozi huyo ambaye aliomba jina lake lihifadhiwe.

Wengine ambao wamekuwa wakitajwa kuwania uraia kupitia CCM ni Waziri Mkuu wa zamani Edward Lowassa na mtangulizi wakekatika nafasi hiyo, Frederick Sumaye, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Kazi Maalumu), Profesa Mark Mwandosya, Mbunge wa Songea Mjini, Dk Emmanuel Nchimbi na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe.

Wegine ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Uhusiano na Uratibu), Steven Wassira na Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki ambaye pia ni Mwenyekiti wa Bunge Maalumu, Samuel Sitta.

Wengine wanaotajwa ni Waziri wa Uchukuzi, Dk Harrison Mwakyembe, Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Profesa Anna Tibaijuka na Waziri wa Katiba, Asha-Rose Migiro.

Pia wamo Waziri wa Maliasili na Utalii, Lazaro Nyalandu, Naibu Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, January Makamba, Naibu Waziri wa Fedha, Mwigulu Nchemba, Mbunge wa Sengerema, William Ngeleja, Mbunge wa Msalala, Ezekiel Maige na aliyewahikuwa Balozi wa Tanzania nchini Ujerumani, Balozi Ali Karume.


Wasomi

Profesa wa Chuo Kikuu cha Mzumbe, George Shumbusho alisema wingi wa wanaojitokeza kutaka kuwania urais ni njia ya kuunda mtandao utakaomwezesha mtu fulani au mmoja kunyakua tiketi hiyo.

"Watu wanapiga kampeni katika harambee kwa njia ya kutengeneza mitandao, kwani ukifika wakati wa chama kumpitisha mgombea, asiposhinda ataibuka na kuwaeleza kuwa mnaoniunga mkono mimi muungeni fulani," alisema.

Naye Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Richard Mbunda alisema kujitokeza kwa idadi kubwaya wanaowania nafasi ya urais, kutatoa fursa ya wananchi kutambua udhaifu wa kila mmoja jambo litakalowezesha kupatikana kwa mtu sahihi wa kupeperusha bendera ya chama hicho.

"Wakiwa wengi, kila mmoja atataka kuonyesha umahiri wake na sisi ambao ni wananchi watawaliwa tutaweza kutambua upungufu wa kila mmoja, jambo litakalosaidia kupatikana kwa mtu sahihi," alisema Mbunda


Kambi ya Pinda

Uchunguzi uliofanywa na gazeti hili kwa siku kadhaa mjini Dodoma ambako vikao vya Bunge Maalumu vinaendelea umebaini kuwa kambi ya Pinda inaongozwa na Mwenyekitiwa Mamlaka za Mitaa Tanzania (ALAT) ambaye pia ni Meya wa Jiji la Dar es Salaam, Dk Didas Masaburi.

Inadhaniwa kuwa Dk Masaburi atatumia ushawishi wake kwa viongozi wa mamlaka za miji na wilaya zinazoongozwa na wenyeviti wa halmashauri na mameya wa miji, manispaa na majiji kumuunga mkono mgombea huyo ambaye piahivi sasa Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa ziko chini ya ofisi yake.Wiki hii kundi la wafuasi wa Pinda likiongozwa na Dk Masaburi lilikuwa mjini Dodoma likijaribu kutafuta kuungwa mkono na makada viongozi wa CCM ambao walikuwa wakishiriki kikao cha Kamati Kuu ya chama hicho pamojana wale walioko katika Bunge Maalumu. Habari zinasema mbali na Dodoma, tayari kambi hiyo imeshafanya vikao kadhaa jijini Dares Salaam na Visiwani Zanzibar lengo likiwa ni kutafuta kuungwa mkono na makada wa CCM katika sehemu hizo. Hivi sasa nguvu za Pinda zinaelekezwa katika mikoa mingine nchini kwa lengo hilohilo. Kutokana na kasi ya kambi yake, wafuasi wa baadhi ya wagombea wameanza kufuatilia mwenendo wao kwa lengo la kukusanya ushahidi wa kile wanachokiita 'rafu' zinazochezwa ili kupata ushahidi unaoweza kutumika dhidi ya mgombea huyo wakati mchakato wa uchaguzi ndani ya CCM utakapoanza mapema mwakani.

Itakumbukwa kwamba makada watano wa chama hicho ambao ni Lowassa, Membe, Makamba, Wassira na Ngeleja wanatumikia adhabu na wapo chini ya uangalizi wa chama hicho baada ya kutiwa hatiani kwa makosa ya kuanza kampeni za urais kabla ya muda kutangazwa.

Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana alisema hivi sasa ni mapema mno kusema ni lini mchakato wa kupata wagombea wa nafasi za uongozi ndani ya chama hicho utaanza na kwamba wakati mwafaka ukiwadia wananchi watafahamishwa.


Uwezo, udhaifu wake

Hata hivyo wakosoaji wake wanasema Pinda akiwa Waziri Mkuuhana cha kujivunia na kwamba amekuwa mzito kufanya uamuzi mara kadhaa kiasi cha kusababisha baadhi ya mambo muhimu ya nchi kukwama na kwamba kwa maana hiyo hastahili kuwa rais.

"Ni kitu gani ambacho nchi inakikumbuka kuhusu huyu bwana ambacho alikifanya katika miaka yake ya uwaziri mkuu, kama alikuwa kwenye nafasi kubwa kiasi hicho na hakuna alichofanya, atawezaje kumudu madaraka ya mkuu wa nchi?" alihoji mmoja wa makada wakongwe wa CCM.

Waziri mmoja wa sasa (jina tumelihifadhi), alisema Pinda hana uwezo wa kuongoza nchi, kwani wao wakiwa mawaziri ameshindwa kuwasaidia katika kero mbalimbali walizokuwa wakimfikishia kama kiongozi wao.

"Muulize waziri yeyote kuhusu uwezo wa jamaa, kila kukicha tunampelekea mambo tunayokutana nayo, lakini hakuna kinachowezekana kwake, atakwambia subiri leo, subiri keshona hatimaye jambo linaishia hivyohivyo," alisema.

Kwa upande mwingine, watetezi wake wanasema Pinda wanayemnadi ni yule aliyepata kuwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa – Tamisemi) kiasi cha kuonekana anafaa kuwa Waziri Mkuu.

Wanasema kushindwa kwake kufanya kazi ipasavyo ni matokeo ya sababu zilizomfanya mtangulizi wake, Lowassa kung'oka katika nafasi yake.


Chanzo: Mwananchi

CLOUDS MEDIA WAADHIBIWA

MAMLAKA ya Mawasiliano Tanzania(TCRA), imetoa onyo pamoja na kutoza faini ya takribani Sh milioni 5 kwa kituo cha redio na televisheni cha Clouds, kwa kukiuka kanuni za utangazaji za mwaka 2005.

Wakielezea uamuzi huo jana jijini Dar es Salaam, Kamati ya Maudhui ya mamlaka hiyo ikiongozwa na Mwenyekiti wake, Margaret Munyagi ilisema kuwa ukiukwaji wakanuni hizo ulifanywa kwa nyakati tofauti na vituo hivyo.

Alisema kwa upande wa kituo cha redio cha Clouds, kupitia kipindi chake cha 'Njia Panda' kilichorushwa hewani Juni 15 mwaka huu kati ya saa 8.00 mchana na saa 10.00 jioni kilikuwa na mada iliyohusu safari ya kuzimu ambapo maudhui yake yalijaa simulizi za kufikirika, za kishirikina na kichawi.

Aidha alisema kosa lingine kituo hicho hakikufuata kanuni za Utangazaji(maudhui) za mwaka 2005 zinazowataka kuwasilisha ratiba ya vipindi vyao kwa TCRA ili viidhinishwe na vilevile kuvichapisha katika gazeti kabla ya kurushwa hewani ambapo kipindi cha Njia Panda hakikuwasilishwa kwa ajili ya kuidhinishwa.

Wakati huo huo, kituo cha televisheni cha Clouds kilirusha kipindi cha 'Bibi Bomba' Mei 16 na Juni 6 mwaka huu kati ya saa 3.00 na saa 4.00 usiku ambacho kilikiuka kanuni za Utangazaji (maudhui) za mwaka 2005.

Alisema kipindi hicho kilidhalilisha mabibi hao walioshiriki pamoja na wanawake kwa ujumla kutokana namaswali ya aibu waliyokuwa wakiulizwa na waamuzi wa shindano hilo ambayo ni kinyume na kanuni hizo.

Aidha alisema kituo hicho kinatozwa faini ya Sh milioni moja na kutakiwa kuwasilisha TCRA mwongozo wa kuchuja na kusimamia maudhui yasiyofaa kabla ya kutangazwa.

TCRA imesema kama Kanuni za Utangazaji zitaendelea kukiukwa hatua kali zaidi za kisheria zitachukuliwa dhidi yao.

BODI YA MIKOPO YA WANAFUNZI(HESLB) YATOA MAJINA YA WANAFUNZI AMBAO HAWAJAKAMILISHA BAADHI YA TAARIFA

Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu(HESLB) katika mchakato wa kuhakikisha taarifa za wanafunzi walioomba mikopo katika mwaka wa masomo 2014/2015 wamegundua baadhi ya makosa katika form za waombaji, Hivyo wametoa majina ya wanafunzi wote walioomba mikopo kwa mwaka wa masomo 2014/2015 ambao hawaja kamilisha baadhi ya taarifa.

Wanafunzi ambao hawaja ambatanisha baadhi ya taarifa kama vyeti vya kuzaliwa, Picha(passport size), nakala za kitambulisho cha mpiga kura au pasi ya kusafiria wanatakiwa kutuma taarifa zao kwa The Executive Director, Higher Education Students' Loans Board, P. O. Box 76068,DAR ES SALAAM. Kwa kuambatanisha na barua ambayo itakuwa na Majina Kamili pamoja na Namba ya mtihani wa kidato cha nne(form four)

Kwa wale ambao hawajaweka sahihi ya muombaji (Applicant signature) na sahih ya mdhaming wanatakiwa kufika makao makuu ya bodi ya mikopo HESLB offices on Plot No. 8, Block No. 46 Sam Nujoma Road, Mwenge- Dar es Salaam wao wenyewe nasi mwakilishi wao.

Ili kuangalia majina ya waombaji ambao taarifa hii inawahusu watembelee link ifuatayo:-

http://www.heslb.go.tz/index.php/application-guidelines/168-call-for-loans-applicants-to-correct-their-loan-applications ??

AMCHANA MWANAE KWA WEMBE SEHEMU YA HAJA KUBWA ILI AWEZE KUJISAIDIA

Mkazi wa Kata ya Kitangiri katika Wilaya ya Ilemela jijini Mwanza, Anastazia Ngilitu, amemchana kwa wembe mtoto wake mwenye umri wa miezi miwili na wiki mbili baada ya mtoto huyo kuzaliwa bila kuwa na sehemu ya haja kubwa

Aidha, amebainisha kuwa wakati wa kujifungua, mtoto huyo alifanyiwa upasuaji katika Hospitaliya Bugando na kuwa baada ya muda mchache hali hiyo ilijirudia na kuamua kumnasua kwa kumchana bila kujua madhara ya aina yeyote ambayo yangeweza kumpata mtoto wake ambapo kwa sasa afya ya mtoto hairidhishi baada ya kuchanwa.

Wakazi wa eneo hilo wamesema wamekuwa wakimpa msaada mama huyu mara kwa mara, huku wakithibitisha maisha ya mama huyo kuwa ni magumu kutokana nakufukuzwa na mume wake na kupata kipigo.

"Kwa sasa sina fedha za kununulia chakula na fedha za matibabu za kumtibu mwanangu na mimi pia kwamaana titi langu lina uvimbe, naomba wasamaria wema wanisaidie kunichangia kwa chochote walichonacho" Alisema BiAnastazia huku akilia

BOMU LATUPWA NDANI YA HIACE LAUA WATATU

Watu watatu wamekufa, akiwemo mtoto mchanga ambaye mashuhuda wanasema "alitupwa nje," baada ya basi dogo la abiria aina ya Toyota Hiace kurushiwa bomu na watu wasiojulikana huko Kasesema, Kigoma alfajiri ya leo.

Shambulizi hilo limefanyika jirani na Kambi ya Jeshi ya Migongo wilayani Buhigwe majira ya saa 11 alfajiri, wakati basi hilo likivusha abiria toka Kilelema kwenda Kasulu Mjini.

Watu wengine 6 wamejeruhiwa vibaya katika tukio hilo la kutisha, ameeleza kamanda wa polisi (OCD) wa wilaya ya Buhigwe, Samuel Utonga.

Mashuhuda wameiambia Mwananchi kwamba, wakati Hiace hiyo ilipokuwa ikipita eneo la Migongo, alijitokeza mtu mwenye bunduki, akasimama katikati ya barabara akiishinikiza isimame.

Alipoona dereva hapunguzi mwendo, haramia huyo alilipisha hilo basi, ambalo lilosonga mbele umbali mfupi tu kabla ya mtu mwingine kujitokeza toka kusikojulikana na kulirushia bomu.

Taarifa toka wilayani humo leo mchana zinasema hali ya wahanga hao wa bomu "imezidi kuwa mbaya," hivyo imebidi wahamishwe toka hospitali ya Muyama na kupelekwa Kasulu Mjini kwa tiba zaidi.

Chanzo: Mwananchi

MJUMBE WA CCM AJIUNGA 'UKAWA'

Jana ilikuwa kama sinemapale viongozi wa Kamati Namba Moja ya Bunge Maalumu walipojikuta wakibishana na mjumbe wao mbele ya waandishi wa habari, huku siri za mambo ya ndani ya vikao zikianikwa hadharani.

Kamati hiyo inaongozwa na Naibu Waziri, Ofisi ya Makamu wa Rais, Ummy Mwalimu na makamu wake ni Waziri wa Sayansi na Teknolojia, Profesa Makame Mbarawa, huku ikiwa imesheheni vigogo wengine wakiongozwa na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda.

Viongozi wengine katika kamati hiyo ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Uhusiano na Uratibu),William Lukuvi, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Utawala Bora), George Mkuchika na Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Dk Hussein Mwinyi.

Wamo pia Waziri wa Afya na Ustawiwa Jamii, Dk Seif Rashid, Waziri wa Kazi na Ajira, Gaudensia Kabaka na Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto, Dk Pindi Chana.

Jana asubuhi, Mwalimu na Profesa Mbarawa walifika mbele ya waandishi wa habari katika Hoteli ya St Gasper wakiwa wameambatana na mmoja wa wajumbe wa kamati hiyo ambaye pia ni Mbunge wa Nkasi Kaskazini (CCM), Ally Keissy.

Lengo la mwenyekiti na makamu wake lilikuwa ni kumbana Keissy ili akanushe taarifa aliyoitoa juzi kwenye moja ya televisheni kwamba kamati hiyo inaongoza kwa kuvunja kanuni hasa katika suala la akidi ya vikao kutotimia.


Sinema ilivyoanza

Walipofika mbele ya waandishi wa habari, Keissy alipewa fursa ili akanushe taarifa yake, lakini alibadili mada na kuanza kuzungumzia masuala ya muundo wa Serikali na Bunge, huku akisemayeye ni muumini wa serikali tatu na siyo mambo ya serikali mbili zinazopendekezwa na wengi kutoka katika chama chake.

Kauli hiyo iliwashtua Mwalimu na Profesa Mbarawa ambao walianza kumkatisha ili asiendelee.

"Keissy sikukuitia mambo hayo, huu ni mkutano wangu, naomba ukanushe nilichokuitia, hayo utazungumza baadaye tafadhali sana," alisema Mwalimu.

Wakati huo Profesa Mbarawa na waandishi wa habari waliokuwapo walivunjika mbavu kwa vicheko, huku yeye akiendelea kusisitiza kwamba ni muumini wa Tanganyika.

Wakati akisema hayo, Profesa Mbarawa naye aliingilia kati na kumtaka Keissy kueleza kilichompeleka hapo huku akimtaka aache kelele za kupotosha wananchi kwa kuwa anachosema siyo kweli.

Alipopewa nafasi ya kuzungumzia jambo hilo, Keissy alisema: "Jana (juzi), mimi nilihesabu mara mbili nikaona Zanzibar hawajatimia lakini kumbe mmoja nilimfanya akawa mtu wa Tanganyika, kwa hilo nilighafilika, lakini mle ndani mambo siyo mazuri," alisema Keissy.

Kabla hajaendelea Mwalimu alidakia na kumtaka anyamaze kimya kwa kuwa huo haukuwa mkutano wake, ili yeye (Mwalimu) aendelee kueleza mambo yaliyojirindani ya kamati.

"Jamani waandishi si mnaona amekanusha, huu ni mkutano wangu na yeye sitaki azungumze mambo ya mle ndani kwa kuwa msemaji ni mimi au makamu wangu au mtu yeyote atakayeteuliwa na mwenyekiti, sasa tunaendelea," alisema Mwalimu.

Mara baada ya Mwalimu kutoa taarifa ya kamati yake kwa waandishi wa habari na kumaliza kujibu maswali, alinong'ona na Profesa Mbarawa na hapo wakampa nafasi Keissy ili azungumze kwa ufupi mambo yake lakini palepale mbele yao.


Kauli za Keissy

Akitumia fursa hiyo, Keissy alisema: "Kuna mambo yanafanywamle ndani ambayo mimi na wenzangu wengine tunalazimishwa, hatukubaliani nayo likiwamo suala la kuizika Serikali ya Tanganyika wakati wa upande wa pili (Zanzibar)wanapewa nafasi na kunufaika na rasilimali za nchi hii, ndugu zangu huu ni uonevu."

Alisema uonevu huo umekuwa mkubwa kwa wabunge wa Tanzania Bara ukilinganisha na wenzao wa Zanzibar ambao alisema wanakula fedha nyingi za bure ilihali hawafanyi kazi za Tanganyika.

"Ndugu zangu, hapa tusidanganyane, we fikiria watu zaidi ya 50 wanatoka kule Zanzibar na kuja kutuamulia mambo yetu, hii si halali hata kidogo. Haiwezekani mtu wa Zanzibar akaja kuzungumzia masuala ya Nkasi wakati hayajui," alisema.

Alisema kuwa msimamo wake siku zote ni serikali tatu na kwamba hatayumbishwa na vitisho au jambola aina yoyote hata kukiwa na kulazimishwa.

Mbunge huyo alisema kuwa kutakuwa na urahisi wa kuongoza Serikali kama Tanganyika itapewa hadhi yake kuliko ilivyo sasa kwa serikali mbili zinazopigiwa upatu.

Kwa mapendekezo yake alisema ni vyema likawepo Bunge la Tanganyika, Bunge la Zanzibar na kisha miongoni mwa wabunge hao, wachaguliwe wachache kuunda Bunge la Muungano.

Aliendelea kusisitiza kuwa wabunge kutoka Zanzibar wanawanyonya wenzao wa Tanzania Bara kwa kila kitu kauli ambayo ilionekana kumkera Profesa Mbarawa na kuamua kumkatisha asiendelee kuzungumza.

Wakati akiendelea kuzungumza, viongozi hao walimkatisha tena na kumwambia akubali waondoke pamoja kuendelea na vikao vya kamati. Baada ya hapo, Mwalimu na Profesa Mbarawa walinyanyuka na kuanza kuondoka, lakini Keissy alisimama na kuendelea kuzungumza na waandishi wa habari.

Baada ya kuona anaendelea, Profesa Mbarawa alirudi na kumshika mkono Kessy huku akisema; "Mheshimiwa Keissy twende bwana, maana ukimwacha huku huyu atazungumza mambo mengi."

Wakati akiondoka eneo hilo, Keissy alipaza sauti akiwaambia waandishi wa habari: "Angalieni tunavyodhibitiwa, lakini msimamo ni huo wala sitayumba ngoja tukaendelee lakini mimi ndiyo mtoa habari namba moja."

Msimamo wa serikali tatu ni wa Umoja wa Katiba ya Watanzania (Ukawa) waliosusia Bunge.

BOKO HARAM WATEKA CHUO CHA POLISI

Kundi la wapiganaji la kiislam la Boko Haram, wamevamia shule moja ya mafunzo ya kipolisi.

Kituo hicho cha mafunzo kilichoko kwenye kitongoji cha Gwoza kiko karibu na mpaka wa nchi ya Cameroon ambacho hufundisha maofisa wa Polisi nchini Nigeria.

Kikundi hicho Boko Haram pia kinasemekana kuudhibiti mji wa jirani na Gwoza uitwao Buni Yadi.

Nalo shirika la kutetea haki za binadamu la Human Rights Watch wametoa takwimu ya vifo vilivyosababishwa na kundi hilo kua watu zaidi ya elfu kumi mpaka sasa tangu walipoanzisha harakati za kutaka upande wa kaskazini mwa Nigeria uwe chini ya utawala wa Kiislam.

MAREKANI WAENDELEA KUWASHAMBULIA IS HUKO IRAQ

Majeshi ya Marekani yameendelea kuwashambulia wapiganaji wa Islamic State huko Iraq licha ya vitisho kutoka kwa kundi hilo kuwa watawaua mateka wengine wamarekani iwapo Obama angeendelea kuishambulia himaya hiyo kaskazini mwa Iraq.

Majeshi ya Marekani kwaushirikiano na ndege zisizikuwa na marubani zilifanya mashambulizi 14 usiku wa kuamkia leo.

Mashambulizi kumi na manne ya angani yamefanyika katika eneo karibu na bwawa la Mosul na yalilenga kuwasaidia wanajeshi wa Iraq na wa kikurdi.

Maafisa wajeshi la Marekani wamesema kuwa walifaulu kulipua magari ya kijeshi na vitu vingine vilivyokuwa vikitumiwa na wapiganajiwa IS.

Tarifa kutoka kwa wakurdi zinasema kuwa ndege ambazo hazina rubani zilikuwa angani kuwalinda wanajeshi Wakurdi wakati wapiganaji wa Pesh Merga wakisukumwa katika milima, kusini mashariki mwa bwawa kubwa la Mosul, ambalo lilitwaliwa tena kutoka kwa wapiganaji wa kiislamu wiki hii.

Pentagon imethibitisha kuwa mashambulizi kumi na manne ya angani yalifanywa katika sehemu hiyo kuliko bwawa na kuyalenga magari kadhaaya kijeshi na vitu vingine.

Televisheni ya taifa ya Iraq imesema kuwa ndege hizo za vita za Marekani zilikuwa pia zimetekeleza mashambulizi katika kambi za magaidi mkoanial-Anbar hadi magharibi mwa Baghdad, na zilikuwa zimetoa ulinzi wa angani kwa vikosi vya serikali vilivyokuwa vikielekea kuwakabili waasi wa kisuni.

Awali makao kuu ya Jeshi la Marekani limesema kuwa wanajeshi la kitengo maalum walijaribu kumuokoa mwanahabari James Foley na waamerika wengine walioshikwa mateka nchini Syria.

Habari hii imetolewa baada ya video ya aliyetekwa nyara novemba 2012 nchini Syria kuonyeshwa akiuawa kikatili na wanamgambo wa Kiislamu kutokea jumapili.

Wanamgambo hao walisema mauaji yake ilikuwa kulipiza kisasi dhidi ya Marekani kwa sababu ya kuwashambulia wapiganaji wao hewani Iraq.

Rais wa Marekani Barack Obama alikashifu mauaji hayo na kuwalinganisha wanamgambo hao na ugonjwa wa saratani na kuwa itikadi zao hazikuwa na mwelekeo aliendelea kuwa kusema tendo hilo lilishtua ulimwengu mzimaUmoja wa kitaifa,uingereza na wengine pia wameeleza huzuni yao kutokana na video hiyo.

Mamake Bwana Foley Diane alisema kuwa mwanawe aliaga dunia kwa niaba ya watu wa Syria.

Kamati inayolinda wanahabari ilisema ina wasi wasi kwa wanahabari wote waliozuiliwa na wanamgambo hawa na kusema wanahabari wajiepushe na Syria.

BABA AWACHOMA WANAE MOTO KISA KUANGALIA TV KWA JIRANI

Salum Juma, fundi gereji wilayani Temeke, mkazi wa Mbagala Kibonde Maji, jijini Dar es Salaam anadaiwa kuwachoma moto mikono watoto wake wawili kwa kutumia tambi za jiko kisa ni kuangalia TV kwa jirani.

Watoto hao, Agustino Said (7), mwanawe wa kufikia na NurdinSaid (5), wa kumzaa mwenyewe, walikutwa na mkasa huo baada ya kwenda kuangalia runinga kwa jirani na kurudi nyumbani saa 5:00 usiku

Kitendo hicho kilifanyika huku mama yao akiwa kwenye biashara zake za kukaanga mihogo.

MWANDISHI WA MAREKANI ACHINJWA NA ISLAMIC STATE

Kikosi cha kiislam cha kijeshi chenye msimamo mkali kimeachilia video inayoonesha mauaji ya mwandishi habari mwenye asili ya Marekani. James Foley alipotea tangu alipokamatwa mateka na kushikiliwa nchini Syria miaka miwili iliyopita na sasa ameuawa.

Ikulu ya Marekani imesema inaifanyia uchunguzi wa kina video hiyo na ikithibitika kwamba mwandishi huyo wa habari ni wa taifa hilo ,serikaliya Marekani itataka ufafanuziwa kina ilikuaje na kwanini James Foley auawe.

Katika mtandao wa kijamii waFacebook familia ya mwandishi huyo iliandika kuwa 'tunajua kwamba wengi wenu mnasubiri uthibitisho ama majibu ya maswali yenu,tafadhalini muwe watulivu mpaka nasi sote tupate taarifa tunazo tamia,na tunaomba muendelee kumbumbuka Foleys na kumwombea kila siku.''

Katika video hiyo iliyobeba ujumbe unaosomeka kua ujumbe kwa Marekani, mwandishi huyo pia alionekana akiwa chini ya ulinzi wa mtu aliyekua amevalia kinyago usoni, askari huyo alikua aku akizungumza ndani ya lafidhi yenye athari za Uingereza, akisema kua kifo cha mwandishi huyo ni matokeo ya mashambulizi ya magurunedi yalowalenga wa Iraq.

MWAFRIKA MWINGINE AUAWA MAREKANI

Mauaji mengine ya raia wa kiafrika yaliyofanywa na polisi katika eneo la St Louis yameongeza hali ya wasiwasi na vurugu katika eneo hilo ambalo kwa takriban siku 11 sasa kumekuwa na vurugu kutokana na mauaji yaliyotokea awali.

Jumanne wiki hii afisa mmoja wa polisi alimpiga risasi na kumuua raia wa kiafrika aliyedaiwa kuwatishia kwa kisu polisi.

Mkuu wa polisi wa St Louis Sam Dotson amesema mauaji hayo ya August 9 ya Michael Brown yameongeza hali ya machafuko katika eneo hilo.

Mwanasheria mkuu wa Marekani Eric Holder anatarajiwa kutembelea eneo la Ferguson jumatano wiki hii ili kujadili taarifa rasmi za uchunguzi wa mauaji hayo.

Mwendesha mashitaka katika kesi ya mauaji ya Michael Brown leo amewasilisha ushahidi dhidi ya afisa anayedaiwa kuhusika katika mauaji ya Michael Brown.

Vurugu zimeendelea katika mji huo huku waandamanaji wanaopinga mauaji hayo wakiwa wamepakaa maziwa usoni kujikinga na mabomu ya machozi kufuatia waandamaji wawili kuathirikana mabomu hayo.

PAPA AMRUHUSU PADRE KUOA

Kiongozi wa Kanisa Katoliki duniani, Papa Francis amekubali kumuondolea sakramenti ya upadri, RaymondMosha wa Jimbo Katoliki la Moshi ikiwa ni miaka 20 tangu padri huyo aombe kuachana nadaraja hilo.

Barua ya uamuzi wa Papa Francis ilisomwa juzi katika parokia na vigango vyote vya Kanisa Katoliki Jimbo la Moshi katika ibada zilizofanyika katika makanisa ya jimbo hilo.

Miongoni mwa parokia ambazo barua hiyo ilisomwa ni Karanga ambako Paroko wake, John Matumaini alitoa tangazo hilo katika ibada zote. Uamuzi huo ambao ni nadra kutolewa na Papa, unamaanisha kuwa sasa padri huyo yuko huru kuoa na kuwa na familia.

Hata hivyo, wakati uamuzi huo ukitangazwa rasmi juzi, tayari Padri Mosha ambaye ni profesawa falsafa na maadili katika Chuo Kikuu cha Nelson Mandela Arusha, ana mke na watoto watatu ambao kwa sasa wako vyuo vikuu.

Padri Mosha alisema aliandika barua kuomba kuondolewa daraja hilo mwaka 1994 kabla ya uamuzi kutolewa juzi.

Katika orodha ya mapadre 185 wa Kanisa Katoliki Jimbo la Moshi iliyopo katika tovuti ya jimbo hilo, jina la Padri Mosha linaonekana likiwa ni namba 23.

Akizungumzia hatua hiyo, Padri Mosha alisema: "Ninafurahi kufunguliwa kifugo hiki na hii itanifanya niishi kama Mkristo. Kwa vile hawajaniondolea sifa ya kutoa huduma kama vile ibada za mazishi, sakramenti yamwisho na ubatizo, nitaendeleakutoa kwa wahitaji kwa sababu ninaupenda ukristo."

Nashukuru sasa nimekuwa muumini wa kawaida nitaweza kufunga ndoa kanisani kwa kuwa nilikuwa nimefunga ndoa ya kisheria tu kwa DC.

"Kuhusu kwa nini aliamua kuacha upadri, Profesa Mosha alisema ni baada ya kufanya kazi hiyo kwa miaka 20 na akaona ipo haja ya kuwa na familia lakini kanisa lilikuwa haliruhusu."

Sasa kwa kuwa kanisa haliruhusu mapadri kuoa ndiyo maana nikaamua kuandika barua ambayo hata hivyo, imechukua muda mrefu kujibiwa na tayari nina watoto watatu wako chuo kikuu.

MABASI YAGONGANA USO KWA USO, YAUA NA KUJERUHI

Hali ni tete sana eneo la Mkolye, takribani km 4 toka Mjini Sikonge baada ya basi la Sabena toka Mbeya kwenda Mwanza na basi la A.M. toka Tabora kwenda Katavi kugongana uso kwa uso (head on collision).

Dereva wote wa mabasi hayo wamefariki hapo hapo, mmoja akiwa amekatika kichwa!
Nimeshuhudia abiria kadhaa wakiwa wamenasa katika mabasi hayo, baadhi wakiwa wamekatika mikono na miguu!

Abiria wapatao 18 wamefariki mpaka sasa na majeruhi zaidi ya 30 wamepelekwa katika Hospitali ya Mission ya wilayani Sikonge.

Chanzo cha ajari ni dereva wa basi la Sabena kutoka Mbeya kwenda Tabora kutaka kuovertake gari ambapo vumbi lililokuwa limetimka lilifanya ashindwe kuona na kusababisha kukumbana uso kwa uso na basi A.M kutoka Mwanza kuja Katavi

Neno langu: SUMATRA wanatakiwa kusimamia hii njia ya Mwanza-Tabora-Katavi kwa mwendo mabasi yanaoutumia ni wa hovyo na kasi sana. Mungu azilaze mahara pema peponi roho za marehemu na awatie nguvu wafiwa, Awaponye wale majeruhi wote

MWANAE JACKIE CHAN AKAMATWA NA BANGI

Mwanawe muigazaji nyota wa Hollywood Jackie Chan amekamatwa kwa madai alitumia mihadarati.

Jaycee Chan, 31, ambaye mwenyewe ni msanii pamoja na muigizaji kutoka Taiwanese Kai Ko, 23, walikamatwa alhamisi iliyopita kwa mujibu wa taarifa ya polisi mjini Beijing.

Polisi wanasema kuwa wawilihao walipatikana wamevuta bhangi huku mwanawe Chan akikabiliwa na kosa zaidi la kupatikana na dawa hiyo haramu.

Kukamatwa kwa wawili hao kunawadia wakati polisi wamekuwa wakifanya misako ya dharura na kuwakamata wasanii nyota kadhaa.

Gao Hu, 40, aliyeigiza katika filamu ya mwaka wa 2011 Zhang Yimou "The Flowers of War", alikuwa miongoni mwa wasanii wengine wakutajika waliokamatwa mapema mwezi huu.

HU alipatikana ametumia Bhangi pamoja na madawa aina ya methamphetamines.

Operesheni hizi zinafuatia agizo la rais wa China Xi Jinping mwezi juni kwa polisi la kuwataka kuimarisha juhudi za kukabiliana na matumizi ya mihadarati nchini humo.

Duru zinaarifu kuwa Kukamatwa kwa mwanawe msanii maarufu zaidi nchini humo maafisa wa polisi wanajaribu kuwadhibitishia umma kuwa hakuna atakayeepuka mtego wao.

Mwandishi wa BBC mjini Beijing Martin Patience anasema kuwa watu wenye sifa kubwa wanalengwa na maafisa wa polisi kutokana na ushawishi mkubwa walionao miongoni mwa jamii nchini humo.

Hata hivyo kiongozi wa idara ya baraza la umma la Beijing inayopambana na matumizi ya mihadarati bwana Jin Zhihai amekanusha kuwa idara yake imekuwa ikilenga wasanii na waigizaji nyota katika kampeini yao dhidi ya matumizi ya mihadarati.

"ikiwa tutaendelea na kampeini hii dhidi ya matumizi ya mihadarati ninahakika waigizaji wengi nyota watakamatwa ''Juma lililopita miungano 42 inayowakilisha wasanii walitia sahihi maagano ya kukataa kuwasajili wasanii waotumia mihadarati katika maonesho yao.

Kampuni inayomwakilisha bwana Chan iliomba msamaha kwa uma kwa niaba yake.

Kampuni hiyo ya M'Stones International iliahidi kumpeleka hospitalini ilikukomesha matumizi ya dawa hizo.

Babake Jackie Chan hajasema lolote kufikia sasa.

JAJI MAKAME AFARIKI DUNIA

ALIYEKUWA Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi (NEC), Jaji mstaafu Lewis Makame, amefariki dunia katika Hospitali ya Ami Trauma Centre iliyopo Masaki jijini Dar es Salaam, alikokuwa amelazwa kwa maradhi yaliyokuwa yakimsumbua.

Jaji Makame alifariki jana mchana katika hospitali hiyo, alikokuwa amelazwa ambapo pia Rais Jakaya Kikwete, alimtembelea kumjulia hali. Taratibu za mazishi zilikuwa zikiendelea jana nyumbani kwake Masaki.

Historia fupi iliyopatikana, inaonesha kuwa Jaji Makame alikuwa na Shahada ya Kwanza ya Sheria kutoka Chuo Kikuu cha London nchini Uingereza, ambapo baada ya kufanya mazoezi na kufanya kazi nchini humo, alirejea nchini Tanzania miaka ya 1960 na kutumikia Taifa mpaka alipofikia cheo cha Jaji wa Mahakama ya Rufaa.

Mbali na cheo hicho, Jaji Makame pia alitumikia Taifa katika nafasi yaMwenyekiti wa NEC na Mwenyekiti wa Jukwaa la Tume za Uchaguzi za Nchi Wanachama wa Jumuiya Maendeleo ya Kusini mwa Afrika (SADC-ECF).

Wakati akiwa Mwenyekiti wa NEC kwa takribani miaka 19, Jaji Makame aliweka historia ya kusimamia uchaguzi kadhaa wa vyama vingi nchini.

Alistaafu wadhifa huo baada ya mkataba wake kuisha Julai mwaka 2011. Nafasi yake ilichukuliwa na Jaji mstaafu Damian Lubuva.

MAANDAMANO YA ALBINO YASAMBARATISHWA

MAANDAMANO ya walemavu wa ngozi kwenda Kituo cha Polisi Buguruni jijini Dar es Salaam jana, yalisambaratishwa kwa mabomu yamachozi na askari Polisi, baada ya waandamanaji hao kuzingira kituo hicho na kukaidi amri ya kutawanyika.

Waandamanaji hao walitokea Mahakama ya Mwanzo Buguruni kwenda katika kituo hicho, kulalamikia uamuzi wa Mahakama hiyo kutoa dhamana kwa mshitakiwa, Ombeni Swai, mkazi wa Tabata Matumbi, anayedaiwa kutishia kumuua mwenzao.

Kabla ya maandamano hayo, Swai alifikishwa mahakamani hapo, mbele ya Hakimu Mfawidhi, Benjamini Mwakasona na kushitakiwa kwa kosa la kutishia kumuua mlemavu wa ngozi, Mwinyisi Issa.

Karani wa mahakama hiyo, Edwin Mwandawanda alidai mahakamani hapo kwamba Swai alitishia kwa maneno kumuua Issa Agosti 16 mwaka huu, saa 7 mchana katika eneo la Buguruni Wilaya ya Ilala.

Hata hivyo, mshitakiwa huyo alikana kutenda kosa hilo ambapo Hakimu Mwakasona aliahirisha kesihiyo mpaka Septemba 3, mwaka huu na kumwambia mshitakiwa kuwa dhamana ya kesi yake ipo wazi, ambapo alitakiwa kuwa wadhamini wawili waliotakiwa wote kuwa na barua zinazotambulika na serikali za mtaa.

Pamoja na dhamana hiyo kuwa wazi, mshitakiwa hakufanikiwa kutimiza masharti hayo kwa wakati, hivyo akaendelea kushikiliwa wakati akisubiri wadhamini wake kutekeleza masharti hayo.

Vurugu

Kitendo hicho cha mahakama kutangaza dhamana kwa mshitakiwa, kiliamsha hasira kwa walemavu wa ngozi waliokuwa wamekusanyika nje ya mahakama kufuatilia mwenendo wa kesi hiyo, iliyotajwa kwa mara ya kwanza.

Baadhi ya walemavu hao walifanikiwa kupenya mpaka alipokuwepo mshitakiwa na kuanzakumpiga. Kitendo hicho kilifanya Polisi kumpakia haraka kwenye gari na kumpeleka kituoni Buguruni, kwa nia ya kumnusuru.

Hatua hiyo haikuwaridhisha albino hao, ambao walijikusanya na kuandamana kwenda katika Kituo cha Polisi Buguruni, kwa lengo la kutaka kumdhuru mshitakiwa.

Mashuhuda waliozungumza na gazeti hili, walidai kuwa waandamanaji hao walipotakiwa kutawanyika, walikaidi, hatua iliyosababisha Polisi kutumia mabomu ya machozi kuwatawanya.

Walisema baadhi ya albino walidiriki kupanda ndani ya gari la polisi aina ya Land Rover 'Defender' na kuanza kumshambulia kwa mateke na ngumi mshitakiwa, jambo lililowalazimu polisi kuondoka eneo hilo hadi kituo cha polisi Buguruni.

Albino hao pia walifuata kwa nyuma huku wengine walipanda ndani ya gari hilo hadi mahali hapo. Wananchi waliokuwepo nje ya kituo cha polisi, walikumbwa kwa taharuki.

Albino hao waliendelea kumshambulia mshitakiwa huyo hadi walipofika nje ya kituo hicho, huku wakizuiliwa na polisi hao, ambao baadae walilazimika kufyatua mabomu ya machozi kwa lengo la kuwatawanya.

Gazeti hili lilimtafuta Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ilala, Marry Nzuki, ambaye alikiri kutokea kwa vuruguhizo. Alisisitiza kuwa hakuna mtu yeyote anayeshikiliwa Polisi kwa kosa hilo.

"Baada ya kutawanywa pale kituo cha Buguruni, Mkuu wa Kituo aliwaambia waje katika ofisi zangu,lakini hadi hivi sasa sijamuona mtuyeyote wala kiongozi wao kuleta mashitaka yoyote," alisema Kamanda Nzuki.

Dau la Mengi

Wakati vurugu hizo zikitokea, Mwenyekiti Mtendaji wa Makampuni ya IPP, Reginald Mengi, ametangaza kutoa Sh milioni 10 kwa mtu atakayefanikisha kukamatwa kwa watu walioshiriki kumkata mkono mlemavu wa ngozi, Susan Mungi (35) na kumuua mumewe wilayani Igunga, Tabora.

Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana, Mengi alisema pia IPP itasomesha watotowa mlemavu huyo.

Katika mkutano huo uliohudhuriwapia na baadhi ya viongozi wa Chama cha Albino Tanzania (TAS), Mengi alisema anafanya hivyo kama mwananchi wa kawaida ambaye ameguswa na vitendo hivyo vya kinyama, vinavyofanywa dhidi ya watu hao wenye ulemavu.

Aliomba Polisi kuwasaka wote waliohusika, kuwakamata na kuwapeleka mahakamani haraka.

Alisema albino ni watu kama wengine hivyo vitendo vyovyote vya kinyama dhidi yao lazima vilaaniwe na watu wote.

"Hakuna albino ambaye amependa awe hivyo, hakuna aliyemwomba Mungu ampatie ulemavu huo, hawa ni binadamu kama sisi, jamii na serikali kuendelea kukaa kimya juu ya unyama huu ni jambo linalosikitisha," alisema Mengi.

Mengi alisema waliotumwa kumkata albino huyo wakamatwe. Susan, mkazi wa Kijiji cha Buhelelekati ya Nsimbo wilayani Igunga, alikatwa kiwiko cha mkono wake nawahusika kutoweka nacho.

Katika tukio hilo, mumewe Mapambo Mashili aliuawa kwa kupigwa na kitu chenye ncha kifuani na kichwani wakati akijaribu kumnusuru mkewe asikatwe mkono wake.

Mtoto huyo hadi sasa amelazwa katika Hospitali ya Wilaya ya Urambo.

Katika tukio hilo, Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Fatma Mwasa ametangaza dau la Sh 500, 000 kwa mwananchi atakayesaidia kukamatwa kwa watu wanaofanya vitendo hivyo.

Tukio hilo limekuwepo ikiwa ni wiki baada ya mtoto, Upendo Sengerema (15) mkazi wa Kijiji cha Usinge kata ya Uganza wilayani Kaliua mkoani Tabora, kukatwa mkono na watu waliokimbia nao.

Katibu Mkuu Chama cha Albino (TAS), Ziada Nsemo alisema kati yawatanzania milioni 45, Mengi ni mmoja wa watu waliojitokeza hadharani kukemea vitendo vya kinyama wanavyofanyiwa.

Alisema licha ya polisi kuahidi kuwalinda, wameendelea kuuawa.

Alitoa mwito kwa albino nchini, kujilinda na kukaa karibu na makundi ya watu ili wanapovamiwa iwe rahisi kupata msaada kwa sababu ulinzi kwao ni wa shaka na wanawindwa kila kona.

Chanzo: Habari leo

WATU WAWILI WAFARIKI BAADA YA KUGONGWA NA GARI

Watu wawili wamefariki dunia papo hapo baada ya gari aina ya Land Cruser ilikuwa imebeba maiti 10 zikitokea hosiptali ya taifa muhimbili kwenda hospitali ya St Francis Ifakara kugonga wapanda pikipiki katika eneo la Mtego wa simba Mikese mkoani Morogoro.

Akizungumzia tukio hilo kwenye eneo la tukio mkuu wa kikosi cha usalama barabarani Bonifasi Mbao amesema gari hiyo ikiendeshwana dereva Pankrasi Pasco mkazi wa ifakara iliwagonga wapanda pikipiki Shaban Rajab na Ally Benulo wakazi wa Mikese na kufariki dunia papo hapo na chanzo cha ajali mwendo kasi na dereva anashikiliwa na jeshi la polisi, kuhusu maiti 10 zilizokuwemo katika gari hiyo amesema zilikuwa zikipelekwa hospitli ya St Fancis Ifakar kwa lengo la kufanya utafiti na mafunzo ambapo wanafanya mawasilino ya kuzifikisha katika hospitali hiyo.

Nao wananchi walioshuhudia tukio hilo wameeleleza chanzo cha ajali hiyo ni mwendo kasi huku wakilalamikia matukio ya ajali nyingi katika eneo hilo kutokana na kona na kuomba serikali kuweka matuta na vibao vya tahadhari.

AJIUNGUZA MWILI MZIMA KWA WIVU WA MAPENZI

MKAZI wa Igombe katika Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela, jijini hapa, Tausi Juma (22)amelazwa katika Hospitali ya Rufaaya Bugando baada ya kujimwagia mafuta ya taa na kujiunguza mwili mzima kutokana na wivu wa kimapenzi.

Tukio hilo ni la Agosti 9, mwaka huu saa 2 asubuhi nyumbani kwake.
Kaimu Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Mwanza, Christopher Fuime alipoulizwa, alisema ofisi yake haijapata taarifa juu ya tukio hilo.

Muuguzi wa zamu katika wadi hiyo, Pendo Muleta akizungumzia hali yamgonjwa huyo alisema si nzuri, kwani ameungua asilimia 60 ya mwili wake.

Alisema mpaka sasa wanaendelea kumpatia matibabu ikiwemo dawa za kupunguza maumivu na zinazozuia maambukizo kutokana na vidonda alivyo navyo.

Mwanamke huyo akizungumza kwatabu hospitalini hapo, alielezea kisa kwa kusema amefikia hatua hiyo baada ya kugundua mumewe alikuwa na uhusiano wa kimapenzi na mwanamke mwingine.

Alidai mwanamke huyo alituma ujumbe kwenye simu ya mkononi ya mumewe na akauona.

Akizungumza na waandishi wa habari waliofika hospitalini hapo jana, Tausi alisema aliona hana umuhimu wa kuendelea kuishi na mtu ambaye anampenda kwa dhati, lakini anakuwa na mwanamke mwingine.

Akielezea alivyojiunguza, Tausi alisema wakiwa nyumbani kwao namumewe aliyemtaja Hussein Yadunia ambaye ni polisi katika Kituo cha Polisi Igombe, wilayani Ilemela, jijini Mwanza, ujumbe wa maneno uliingia katika simu ya mume wake huyo.

Alisema hakumbuki maneno yote yaliyokuwemo kwenye ujumbe, lakini baadhi yalisomeka 'nakupenda sana honey wewe ndio chaguo la moyo wangu.'

Mwanamke huyo alisema alipomhoji mumewe ambaye pia hujishughulisha na uvuvi wa samaki, juu ya ujumbe huo, alidai kutofahamu namba iliyotuma.

"Nilipomuuliza alikataa kuwa mtu huyo hamjui na aliniambia nimpigie simu…na mie nilipopiga simu hiyo ilipokewa na mwanamke kwa hasira nilimuuliza tena mume wangu ambaye alikataa tena kwa kuniambia hamjui," alisema Tausi.

Huku akionekana kuwa na maumivu makali kutokana na sehemu kubwa ya mwili wake kuwa na majeraha ya kuungua, Tausi alisema ghafla mumewe alimbadilikia na kuanza kumgombeza kuwa amechoka na maswali yake na kumfuatilia kila siku maisha yake hivyo afungashe mizigo yake aende kwao.

"Baada ya maneno hayo, nilimuonamume wangu akiingia ndani na kuanza kunifungashia mizigo, akipakia nguo zangu kwenye mabegi nirudi kwetu na alifanya hivyo baada ya kumjua mwanamkealiyemtumia ujumbe wa maneno katika simu yake,"alisema.

Tausi ambaye aliwaambia waandishi wa habari kuwa mumewe ndiye anayemhudumia hospitalini hapo, aliendelea kusimulia, "nilimwambia mume wangu kuliko kuondoka wakati bado nakupenda bora nijiue."

Alisema moto mkubwa uliokuwa ukiwaka ulimshitua mumewe ambaye alimkimbilia na kumwagia mchanga na baada ya moto kuzimika alimvua nguo na kumkimbiza katika Kituo cha Afya cha Karume.

Kutokana na majeraha kuwa makubwa, iliamuliwa akimbizwe Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Sekou Toure ambayo pia ilimpa rufaa kwenda Bugando.

Hussein Yadunia ambaye ni mume wa mke huyo, akizungumzia tukio hilo alisema, " Sina usemi.

Tayari tukio limetokea, yote namkabidhi Mungu lakini tukio hilolimenidhihirishia kuwa mke wanguananipenda."Aliendelea kusema, "hata vyombo vikiwa kabatini huwa vinagongana lakini uamuzi aliofanya mke wangu umenishangaza."

Akizungumzia ujumbe wa simu uliosababisha mtafaruku, alisema ulitoka kwa dadake na walikuwa wakitakiana heri.

"Haikuwa meseji ya mapenzi," alisema na kusisitiza akipona ataendelea kuishi naye na atazidi kumpenda.

Chanzo: Habari leo

HAKUNA MGONJWA WA EBOLA TANZANIA

Tanzania imesema haina mgonjwa aliyethibitishwa kuwa na ugonjwa wa Ebola.

Kauli hiyo inakuja baada ya kufanyiwa uchunguzi kwa wagonjwa wawili waliotiliwa shaka kuwa na ugonjwa huo.

Waziri wa Afya wa Tanzania Seif Rashid ameiambia BBC, wagonjwa hao waliohisiwa kupata maambukizo kutokana na dalili za awali, ni wa kutoka Benin na Mtanzania, lakini vipimo vimeonesha hawana maambukizo hayo.

Amesema tayari eneo maalumu limetengwa kwa ajili ya kufanyia uchunguzi wagonjwa wanaotiliwa shaka kuwa na ugonjwa huo.

Mafunzo yametolewa pia kwa wataalamu watakao hudumia wagonjwa iwapo watatokea.

Vifaa maalumu vitakavyotumiwa na watoa huduma katika kuhudumia wagonjwa, vimewekwa pia.

Wizara ya Afya ya Tanzania inaongeza uwezo wa kufanya uchunguzi, katika Uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Nyerere, ambao wasafiri wengi kutoka nje huutumia.

NEC YATAJA MASHARTI YA DAFTARI LA WAPIGA KURA

TUME ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) imesema zoezi la uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga kura linalotarajiwa kuanza hivi karibuni linamhusu kila raia mwenye sifa yakupiga kura.

Ufafanuzi huo ulitolewa wakati kukiwa na mawazo tofauti ya nani hasa anatakiwa kushiriki katika zoezi hilo huku baadhi ya watu wakidhani kuwa jambo hili linawahusu ambao hawakuwahi kujiandikisha kupiga kura ama waliopoteza kadi na waliofikia umri wa kupiga kura.

Mwenyekiti wa NEC, Jaji mstaafu Damian Lubuva alisema juzi jijini Dar es Salaam kuwa katika kufanya maboresho hayo na kupata daftari linaloaminika zaidi, Tume inatarajia kutumia mfumo mpya wa utambuzi wa watu kwa alama zabinadamu yaani "Biometric Voters Registration System".

Alisema kwa kutumia mfumo huu, mhusika atachukuliwa alama za vidole vyote 10 vya mikono, picha,saini yake na ni tofauti na mfumo uliokuwa unatumika wa "Optical Mark Recognition" (OMR) uliohitaji kujaza fomu na alama ya kidole kimoja tu.

"Watu wote wenye sifa watatakiwa kujiandikisha upya katika mfumo huu mpya na kupatiwa kadi mpya,"alisema na kuongeza kuwa uboreshaji wa daftari hilo unatokana na matakwa ya kisheria na malalamiko ya wadau mbalimbali.

Alisema tangu uchaguzi mkuu mwaka 2010 pamekuwa na malalamiko kutoka kwa wadau kama vyama vya siasa, mashirika yasiyo ya kiserikali na wapiga kura kuhusu haja ya kuboresha daftari hilo.

Sheria inataka liboreshwe mara mbili kati ya uchaguzi uliofanyika na ujao.

Akizungumzia matayarisho ya zoezi hilo, Mkurugenzi wa Uchaguzi, Julius Mallaba alisema yanaridhisha na kuendelea vizuri.

"Sehemu kubwa ya maandalizi yamekamilika," alisema na kuongeza kuwa tayari ununuzi wa vifaa vya uandikishaji ikiwamo Biometric Voter Registration Kits umeshafanyika.

Alisema vituo katika ngazi ya vitongoji, vijiji na mitaa vimeongezeka kutoka vya awali 24,919 na kufikia vituo 40,015 nchinzima.

KAMATI ZASHAURI RAIS KUPUNGUZIWA MADARAKA

PAMOJA na Rasimu ya Katiba mpya ya Jaji Joseph Warioba kupunguza madaraka ya Rais, kamati zilizotoa taarifa ya mwenendo wake jana zimependekeza madaraka zaidi kupunguzwa.

Katika majadiliano kwenye kamati namba 10, 11 na 12, aidha imependekezwa watakaobaki kuwa wateule wa Rais ni lazima wapelekwe kuthibitishwa na Bunge au mamlaka nyingine.

Mwenyekiti wa kamati namba 12, Paul Kimiti, alisema wajumbe wengi wamejikita katika upunguzajizaidi wa madaraka ya Rais hasa katika mamlaka ya uteuzi.

Kwa kuangalia mwenendo wa majadiliano katika kamati hadi jana, inaonekana kwamba kasi ya kuchambua Rasimu ya Katiba ipo kiwango cha juu na kila Mwenyekiti aliyezungumza kuhusu akidi alisifia kutimia kwake.

Kimiti alisema wapo katika sura ya saba na wanaendelea na majadiliano na japokuwa vipengelevingi vimeshazungumzwa, wajumbe wengi wamejikita katika upunguzaji zaidi wa madaraka ya Rais.

Katika kikao hicho mjumbe wa kamati hiyo ambaye alikuwa mgonjwa kutokana na kipigo, Thomas Mgoli alisema aliomba kupiga kura kwa sababu alishiriki katika kujadili sura hizo na ilikuwa haki yake.

Alisema uamuzi huo ni tofauti na ilivyotafsiriwa kwamba ulitokana na kukosekana kwa akidi. Wakati huo huo, kamati nyingi zinaendelea kuzungumzia uraia pacha huku wakiwemo wanaopinga suala hilo.

Makamu Mwenyekiti wa kamati namba 10, Salmin Awadh Salmin alisema katika mkutano na waandishi wa habari kwamba wameshaanza kupiga kura kwa kamati 2,3 na 4 huku wakiendelea na majadiliano katika sura namba 5.

Hata hivyo alisema jana waliacha majadiliano ya sura hiyo na kuingia sura namba saba ambapo wao watawasilisha maoni ya walio wengi na wachache kutokana na jinsi mambo yalivyojiri katika majadiliano.

Alisema katika kamati yake kulikuwa na mijadala mirefu hasa kwenye mazingira yanayosababisha haki, kiasi cha kuamini kwamba kuna hitajika sura nyingine.

Alisema sura hiyo itajikita zaidi katika haki za wakulima, wavuvi na wafugaji; pia haki za kimakundi kama wanawake.
"Tutapendekeza sura nyingine ili kila mtu apate haki zake..." alisema Salmin.

Aidha alisema katika kamati yake Sura ya 7 imekuwa na mvutano mkubwa na kulazimika kuweka viporo ibara 72 na 73 zinazojadili mamlaka.

ATUHUMIWA KUMLAWITI MTOTO WA MKEWE

MKAZI wa eneo la Majengo mjini Manyoni, Juma Saidi (32) anashikiliwa na Polisi akituhumiwa kumlawiti mtoto wa mkewe. Mtoto huyo mwenye umri wa miaka 14, anasoma Kidato cha Kwanza katika shule moja ya sekondari wilayani Manyoni na inadaiwa alifanyiwa kitendo hicho juzi saa 6 usiku nyumbani kwao.

Inadaiwa baba huyo wa kambo wa mtoto huyo ambaye jina na shule anakosoma vimehifadhiwa, alifanya kitendo hicho baada ya mkewe kusafiri.

Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Singida, Geofrey Kamwela alidai mwanamume huyo alimlawiti kwa nguvu kijana huyo na kumsababishia maumivu makali sehemu zake za siri.

Katika hatua nyingine, polisi mkoani hapa inashikilia watu wengine watatu kwa tuhuma ya mauaji.

Kamanda alitaja watuhumiwa hao kuwa ni Mlani Janila (55), Nchinja Ngaja (69) na Jagali Nchinja (37); wote wakazi wa Kijiji cha Mtavira wilayani Ikungi, mkoani hapa.

Wanadaiwa Agosti 9 mwaka huu saa1.00 jioni katika kitongoji cha Muguaghana, kijiji cha Mtavira, walimuua mwanakijiji mwenzao, Kwisu Funuki (30).

Inadaiwa siku ya tukio, Kwisu alionekana akinywa pombe ya kienyeji nyumbani kwa mtuhumiwa wa kwanza Mlani Janila.

Wakati akiendelea kunywa pombe, inadaiwa ulizuka ugomvi kati ya Funuki (marehemu) na Nchinja (mtuhumiwa) ambao uliamuliwa.

Hata hivyo, baada ya muda, Funuki aliokotwa na wasamaria wema akiwa amekufa karibu na nyumbani kwake huku pembeni kwake kukiwana kopo la kunywea pombe ya kienyeji ijulikanayo kwa jina la "mtukuru".

Uchunguzi wa awali kwa mujibu wa kamanda, unaonesha alichomwa kifuani na kitu chenye ncha kali. Hivyo watu watatu aliokuwa akinywa nao pombe wanashikiliwa kwa uchunguzi.

Chanzo: Habari Leo

BARAZA LA KIISLAMU WAMUUNGA MWIGULU MKONO

Baraza la Maadili la Kiislamu nchini (BAMAKITA), limeunga mkono kauli iliyotolewa na Mbunge wa Iramba Magharibi, mkoani Singida, Bw. Mwingulu Nchemba kutaka vikao vya Bunge Maalumu la Katiba, viahirishwe ili kuokoa fedha za walipakodi nchini.

Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana, Mwenyekiti wa baraza hilo, Shekhe Athuman Mkambaku, alisema kauli ya Bw. Nchemba inaonesha ni mzalendo halisi anayelipenda Taifa lake.

Alisema hivi karibuni, Bw. Nchemba alishauri Bunge hilo liahirishwe kwani wajumbe waliopo hawawezi kuwapatia Watanzania Katiba Mpya kutokana na theluthi mbili inayotakiwa kwa mujibu wa sheria, haiwezi kupatikana kwa sababu baadhi ya wajumbe kutoka upinzani hawashiriki vikao vya Bunge hilo.

“Kuendelea kuwalipa posho wajumbe wa bunge hili ni matumizi mabaya ya fedha za umma…Nchemba ameonesha ukomavu wa kisiasa na manenoyake hayapaswi kupingwa wala kupuuzwa bali aungwe mkono na kupongezwa,” alisema.

Aliongeza kuwa, baraza hilo linapinga vikali kitendo cha baadhi ya wajumbe wa Bunge la Katiba kutoka kundi la Umoja wa Katiba ya Wananchi (UKAWA), kuendelea kususia vikao wakiamini pengine wanatumiwa na kundi la watu wasiotaka Katiba Mpya ipatikane.

“Hoja za UKAWA zilizowafanya wagomee vikao hivyo hazina mashiko kwani wao wanataka rasimu ipite kama ilivyoandaliwa na iliyokuwa Tume ya Mabadiliko ya Katiba…kama madai yao ni sahihi, kwa nini waende bungeni kuchukua posho tu?” alihoji.

Alisema lazima wajumbe wa Bunge hilo wabadili baadhi ya vifungu, waongeze na kuviboresha ndio maana ya vikao.

Shekhe Mkambaku wajumbe kutoka umoja huo hawapaswi kugoma kwa hofu kwamba, Katiba Mpya itatengenezwa kulingana na matakwa ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), kutokana na wingi wao bali watambue kuwa, chama hicho si waamuzi wa mwisho kwani mwisho wa siku rasimu hiyo itapelekwa kwa wananchi ambao ndio waamuzi wa mwisho.

“Kama rasimu hii itatoka kinyume na tulivyopendekeza, wananchi wataikataa, hivyo UKAWA wasijipe kazi ambayo siyao…kazi hiyo waiache kwa wananchi waitolee majibu kwa kupiga kura ya kuikataa au kuikubali,” alisema.

Baraza hilo pia limewapinga watu wanaomshambulia Rais wa Jakaya Kikwete wakidai amevuruga mchakato huo kutokana na hotuba yake alipolihutubia Bunge la Katiba kwani alichokisema ni ushauri tu.

“Kama Kiongozi Mkuu wa nchi, bado ana fursa ya kushauri si lazima wajumbe kufuata maoniyake ndio maana baada ya hotuba yake, vikao viliendelea,” alisema Shekhe Mkambaku

WATU WAWILI WAKAMATWA WIZI MAFUTA YA TRANSFORMER

Watu wawili wanashikiliwa na jeshi la polisi mkoa wa Morogoro baada ya kupatikana na lita 30 za mafuta ya transfoma baada yakukata nguzo za umeme kuvunja transfoma na kuiba mafuta na kusababisha wakazi wa eneo la kola mjini Morogoro kukosa huduma ya umeme kwa muda mrefu.

Kamanda wa polisi mkoa wa Morogoro Leonard Paul amethibitisha kukamatwa kwa watu hao ambapo amesema watuhumiwa walikamatwa katika eneo la kola kwa kamnyonge manispaa ya Morogoro wakihujumu miundombinu ya umeme ikiwemo kuiba mafuta ya trasfoma na kukata nguzo za umeme ambapo jeshi la polisi linaendelea kuwahoji watu hao na mara baada ya upelelezi kukamilika watafikishwa mahakamani.

Naye afisa uhusiano wa shilika na umeme Tanesco mkoa wa Morogoro Ester Msaki amsema mafuta hayo yana thamini ya zaidi ya shilingi laki tatu ambapo amewataka wananchi kuendelea kuwa na ushirikiano kwa kuwafichua wanaohujumu miundombinu ya umeme kwani shirika linaendelea kupata hasara na kusababisha baadhi ya wananchi kukosa huduma ya umeme.

Kwa upande wao wakazi wa manispaa ya Morogoro wameiomba serikali kuongeza ulinzi na kuwachukilia hatua kali watakaobainika wakihujumu miundombinu ya umeme na kusababisha wananchi kuishi gizani kwakukosa huduma ya umeme.

URAIA PACHA PASUA KICHWA

SUALA la uraia wa nchi mbili, linaonekana kupasua vichwa vya wanakamati hasa wanaotoka Zanzibar, kutokana na historia ya nchi hiyo.

Kutokana na unyeti wa suala hilo imeelezwa na Katibu wa Bunge Maalumu la Katiba, Yahya Khamis Hamad, kuwa Bunge liliruhusu mtaalamu mwakilishi wa watu waishio nje, Kadiri Singo kuwasilishawaraka ambao umejadiliwa na kamati hizo.

Akifafanua zaidi taarifa zilizoenea kwamba kulikuwa na majadiliano makali kwenye ibara inayohusu masuala ya uraia wa nchi mbili, Hamad alisema pamoja na majadiliano hayo raia walioko nje ya nchi walituma waraka maalumu ambao waliomba ujadiliwe.

"Juzi walimtuma mtaalamu wao, Singo alete waraka huo na niliomba kibali kwa mwenyekiti waraka huo uruhusiwe kujadiliwa ndani ya kamati na alipata ruhusa hiyo,'' alisema Katibu.

Alisema hadi juzi mchana kamati tatu zilikuwa zikiendelea kujadili ibara inayohusu uraia pacha na kamati nyingine zimekamilisha kujadili ibara hiyo.

Naye mwenyekiti wa kamati namba 12, Paul Kimiti alisema kamati yakeimekuwa ikijadili suala hilo la uraia pacha kwa kina, lakini kumekuwa namvutano hasa kwa upande wa Zanzibar ambapo baadhi ya wajumbe wamekuwa na hisia tofauti kuhusu uraia pacha kwa upande wao.

Kimiti alisema baadhi ya wajumbe wameonesha hofu kufuatia baadhi ya watu ambao walitoroka nje ya nchi wakati wa mapinduzi ambao wanaona kuruhusu uraia pacha kunaweza kuleta matatizo.

Lakini wajumbe walikubaliana kuwa uraia pacha kwa waliotoroka nje wakati wa mapinduzi unaweza kudhibitiwa katika sheria itakayotungwa.

Kwa maoni yake Kimiti alisema inaonesha kuwa sura zilizokuwa zikileta mgogoro ni zilizohusu muundo wa serikali kwani kwa sasa wamekuwa wakiendelea bila tatizo.

Wakati huo huo, imeelezwa kuwa majadiliano yanayoendelea kuimarika zaidi kutokana na kuzidi kuwasili kwa wabunge walikuwa wamesusia Bunge hilo.

Pamoja na kutojulikana idadi ya waliorejea, Katibu alisema kundi la wajumbe 201 waliosusia wanaendelea kurejea bungeni na kuendelea na majadiliano ya kamatikama kawaida.

ARSENAL WASAKA FURSA TANZANIA

DSC06091


Klabu ya Arsenal iliyopo kaskazini mwa jiji la London imeanza mkakati wa kujikita katika kutafuta ubia na kampuni Tanzania kwa lengo la kujitangaza na kusaidia miradi mbalimbali ya kijamii.

Katika ziara ya Balozi wa Tanzania nchini Uingereza na Ireland, Mheshimiwa Peter Kallaghe aliyoifanya jana katika Uwanja wa Emirates, na kufuatiwa na mazungumzo rasmi na maofisa wa Klabu ya Arsenal, maofisa hao walieleza kutambua umuhimu wa Tanzania katika kukua kwa Arsenal.

Ofisa Miradi ya Jamii, Samir Singh alimweleza balozi baadhi ya takwimu juu ya wapenzi wa Arsenal walioko Tanzania, akisema kuwa mtandao wa www.arsenal.com unasomwa na watu zaidi ya milioni mbili kutoka Tanzania, huku wakirudia kuutembelea zaidi ya mara laki saba; kwenye face book wanafuatwa na watu zaidi ya 120,000.
DSC06097
Arsenal wamekuwa wakitoa msaada na makocha kwa mradi wa Tanzania Street Children ulioko Mwanza kwa karibu miaka minne sasa, ambapo kupitia mradi huu watoto zaidi 1,280 wamenufaika. Arsenal wamesema wangependa kuwa na ushirikiano na kampuni mbalimbali huko nyumbani ili kusaidiana katika kuinua michezo na kutambua vipaji vya wanamichezo.

Naye Ofisa Masoko wa Arsenal, Daniel Willey, alisisitiza umuhimu wa wanachama na wapenzi wa Arsenal kujisajili na kuwa na uongozi imara utakaotambuliwa na klabu na hivyo kutoa fursa mbalimbali kwa umoja huo wa wapenzi wa Arsenal Tanzania.

“Umoja wa wanachama unaotambuliwa kwa hivi sasa ni ule wa Kasulu,  Kigoma,  ambapo kumbukumbu zetu zinaonesha kuna wapenzi 150,000, lakini tuna imani wapo wengi zaidi, tunataka tufanye nao kazi, nitaenda Tanzania hivi karibuni, nitapenda kuonana nao Dar, sitakuwa na nafasi ya kwenda nje ya Dar kwa sasa,” alisema Willey.

Kwa upande wake Balozi Kallaghe, ambaye si mpenzi wa Arsenal, alisema hiyo ni fursa muhimu sana kwa wapenzi na mashabiki wa Arsenal kuchangamkia, na kuwataka kujisajili na kuwa na viongozi wanaotambulika.
Balozi Kallaghe, akiwa pamoja na maafisa wa Arsenal uwanhani Emirates
Balozi Kallaghe, akiwa pamoja na maafisa wa Arsenal uwanjani Emirates

“Unajua kubishana bishana masuala ya mpira bila kuwa na kadi ua uanachama kumepitwa na wakati, inapendeza upotumia pesa kidogo, kwa kuvaa fulana original ya timu yako,” alisema Balozi na kuwawataka wanachama hao kuisaidia klabu yao, kuwaunganisha na kampuni kama benki, viwanda vya bia na kampuni za simu.

Balozi Kallaghe alisema hiyo italeta changamoto itakayopelekea timu ya Arsenal kwenda Tanzania siku moja, ambapo Willey alionesha hamu kubwa sana ya kufanya mazungumzo na Bodi ya Utalii Tanzania (TTB), kuona jinsi gani wanaweza kushirikiana.

“Mna vivutio vikubwa sana vya utalii; Mlima Kilimanjaro, Serengeti, Manyara -  haya ni maeneo ambayo tungependa kuyafanyia mazungumzo.

“Tunafahamu kuwa Rais Kikwete ni mpenzi sana wa michezo, na hasa soka, tunamkaribisha sana, japo hatujui yeye ni shabiki wa timu gani hapa England,” alisema Willey.

Balozi Kallaghe aliwashukuru Arsenal na kuahidi kutoa msaada pale itakapobidi, na kuwataka wasisite kumwona wakati wowote, na aliwashukuru kwa mwaliko kwa Rais Jakaya Kikwete kutembelea Emirates  wakati wowote atakapo kuwa London.

Kazi kwenu sasa, mashabiki wa Arsenal, kutaneni, chaguaneni, mchangamkie fursa.


Source: Tanzania Sports

PADRI WA KIHISPANIA AFARIKI KWA EBOLA

Liberia imetangaza kuwa hivi karibuni itapokea dozi za dawa za majaribio ya kutibu ugonjwa wa Ebola kutoka Marekani, ambazo itazitumia kwa madaktari wawili walioambukizwa virusi hivyo.

Serikali ya Marekani ilithibitisha kuwa iliwaunganisha maafisa wa Liberia na kampuni inayotengeneza dawa hiyo iitwayo ZMapp. Katika taarifa yake, kampuni hiyo ya Mapp Biopharmarceutical yenye makao yake jimboni California, ilisema kuwa katika kujibu maombi kutoka kwa taifa la Afrika magharibi ambalo halikutajwa, ilikuwa imeishiwa na ugavi wa dawa hiyo.

Habari hizo zinakuja huku ghadhabu zikiongezeka kuhusiana na ukweli kwamba watu pekee waliopatiwa dawa hiyo ya majaribio ni kutoka mataifa ya magharibi - Wamarekani wawili na Mhispania ambao wote walirudishwa nyumbani kwao kutoka Liberia.

Idadi ya vifo yaongezeka

Jumatatu jioni, shirika la afya duniani WHO, lilisema watu 1,013 wamekufa kutokana na ugonjwa wa Ebola katika mataifa ya Afrika ya Magharibi, huku serikali zikibainishawashukiwa wa ugonjwa huo 1,848. Idadi hiyo ya WHO inahusisha takwimu za kaunzia Agosti 7 hadi 9, ambapo watu 52 zaidi walikufa kutoka na ugonjwa huo, na 69 zaidi waliambukizwa.

Lakini mfanyakazi wa shirika la misaada la Madktari wasio na mipaka MSF nchini Liberia, Cokie Van Der Velde anasema hali ni mbaya kuliko inavyodhaniwa.

"Kiukweli idadi ya waliokufa na walioathirika haionyeshi hali halisi," alisema Van Der velde na kuongeza kuwa kuna vifo vijijini na nchini kote ambavyo havirekodiwi kwa sababu ukusanyajiwa data siyo mzuri kama unavyopasa kuwa.

"Nadhani nchini Liberia ugonjwa huo uko katika kaunti sita na unazidikusambaa. Na unaweza kuenea katika kanda nzima ya Afrika Magharibi, hivyo ni hali ngumu."

Bado hakuna tiba ya uhakikaHakuna chanjo wala tiba ya Ebola hadi sasa, lakini kuna dawa kadhaa za majaribio mbali na ZMapp. Tiba hiyo bado ni mpya sana kiasi kwamba haijafanyiwa majaribio ya usalama au ufanisi kwa binaadamu. Na kampuni inayoitengeneza imesema itachukuwa miezi kadhaa kutengeneza wingi wa kutosha.

Haikuwa bayana ni kiasi gani cha dawa hiyo kitapelekwa nchini Liberia. Wizara ya afya ya Marekani ilisema katika taarifa kuwa serikali ya Marekani ilisaidia kuiunganisha serikali ya Liberia na mtengenezaji wa dawa hiyo, na kuongeza kuwa kwa sababu inasafirishwa kutumiwa nje ya Marekani, taratibu zote za usafirishaji wa nje zilipaswa kufuatwa.

Taarifa ya Liberia iliyowekwa kwenye tovuti ya ofisi ya rais, ilisema nchi hiyo ilikuwa inapokea pia dawa ya majribio kutoka kwa shirika la afya duniani WHO, lakini haikubainika mara moja iwapo taarifa hiyo ilikuwa inamaanisha dawa ya ZMapp au nyingine.


*Usalama na ufanisi wa ZMapp

Katika wiki chache zilizopita, dawa hiyo ya majaribio imetumiwa kwa wafanyakazi wawili wa misaada wa Marekani walioambukizwa ugonjwa huo wakifanya kazi kwenye hospitali ya wagonjwa wa Ebola. Siku ya Jumatatu, maafisa wa Uhispania walisema tiba hiyo ilikuwa imetumika kwa Padri mmishonari wa Kihispania alieuguwa akiwa nchini Liberia.

Wamarekani wanasemekana kupata nafuu, lakini hakuna njia yoyte ya kubainisha iwapo dawa hiyo imesaidia, au wanapata nafuu kivyao kama walivyopata nafuu wengine. Karibu asilimia 40 ya walioambukizwa virusi vya Ebola wananusurika mripuko wa sasa.

BBC WAFUNGUA STUDIO DAR ES SALAAM

Wafanyakazi wa BBC wakiwa kazini kupeperusha matangazo ya Dira ya Dunia redio

Idhaa ya kiswahili ya BBC imezindua rasmi studio zake mjini Dar es Salaam kwa mbwembwe na haiba kuu.

Uzinduzi huo ni matokeo ya mkakati na uwekezaji wa miaka mingi wa shirika la BBC duniani kuhakikisha kuwa matangazo yake yanawafikia wasikilizaji katika hali ya ubora wa hali ya juu na ya kisasa zaidi.
Katika hafla hiyo iliyoandaliwa katika ofisi hizo hizo mpya zilizoko eneo la Mikocheni, mkuu wa kitengo cha uandishi wa habari katika BBC, Nicki Clarke, ameshukuru serikali ya Tanzania, kwa kuwaruhusu kujenga studio hizo za kisasa zitakazoinua tasnia ya habari nchini humo na uhuru wa habari kwa ujumla.

Naye mkuu wa ofizi ya Dar es Salaam, Hassan Mhelela mbali na kuwataka wafanyakazi wa BBC Tanzania, kuzidi kuonyesha ushirikiano pamoja na utendaji kazi wa pamoja, pia ametangaza kuanishwa rasmi kwa ushirikiano kati ya BBC na chuo kikuu cha Dar es Salaam kitengo cha uandishi wa habari.
Eric David Nampesya akizipa taabu Tumba kwenye sherehe ya ufunguzi wa ofisi za BBC Dar es Salaam

Ushirikiano huo amesema kuwa unalenga kusaidia kutoa mafunzo kwa wandishi wa habari chipukizi walioko mafunzoni katika chuo hicho, ambao kwa nyakati tofauti, watakuwa wakijiunga na BBC ili kupata mafunzo katika uandaaji vipindi vya redio na televisheni pamoja na utangazaji.

Kwa upande wa BBC, kuanzishwa kwa ofisi hii, yenye studio za kisasa kabisa za redio na televisheni mbali na kuongeza ubora wa vipindi lakini pia kutawezesha matangazo ya redio na televisheni kufanyika moja kwa moja kutokea Dar es Salaam.

Na kuanzia sasa matangazo ya Amka na BBC yatakuwa yakiandaliwa Dar es Salaam.
Itakumbukwa kuwa Tanzania mbali na kuwa na wasikilizaji wengi wa idhaa ya kiswahili ya BBC, lakini pia ndiko kunakozungumzwa zaidi lugha ya kiswahili.

Tanzania pia ina rekodi ambapo mtangazaji wa kwanza au sauti ya kwanza iliyosikika mwaka 1957, ilikuwa ya mtanzania Oscar Kambona ambapo alikuwa mwanafunzi mjini London.

SUNGUSUNGU WAFANYA MAUAJI

Mauaji ya kutisha ya watu wawili yanadaiwa kufanywa na kundi la Askari wa jadi maarufu kama Sungusungu wilayani Manyoni mkoani Singida baada ya kuwatoa nyumbani kwao usiku na kuwapeleka kichakani ambako waliwashambulia kwa kipigo kisha kumchoma moto mmoja akiwa mfu na mwingine akiwa bado hajakata roho.

Marehemu hao wanajulikana kwa majina ya Lameck Joshua (31) na Doto Kindai ( 20), na taarifa zilizozagaa kijijini hapo ni kuwa watu hao wameuawa kikatili kwa madai kuwa ni weziwa mifugo hata hivyo serikali ya kijji haina taarifa za watu hao kujihusisha na vitendo vya wizi.

POLISI AINGIA MATATANI KWA KUCHEZA MUZIKI NA SHAH RUKH KHAN

Mgogoro umeibuka nchini India baada ya polisi mwanamke nchini humo kucheza densi ukumbini na muigizaji maarufu Shah Rukh Khan katika tamasha la polisi lililofanyika katika jimbo la Bengal Magharibi.

Wanasiasa wa upinzani wamekosoa densi hiyo, wakisema afisa huyo wa polisi kucheza densi akiwa avelia sare zake, imehujumu heshima kwa polisi.

Kiongozi wa jimbo la West Bengal,Mamata Banerjee, aliyehudhuria tamasha hilo, pia alishambuliwa kwa kuruhusu tamasha hilo kufanyika.

Polisi huyo mwanamke na muigizaji Shah Rukh Khan bado hawajatoa tamko lolote kuhusu sakata hiyo.

Densi hiyo, ilifanyika katika tamasha maalum la polisi lililofanyika siku ya Jumamosi.

Shah Rukh Khan ni mmoja wawaigizaji mashuhuri nchini India na duniani , na hivi maajuzi alitajwa kama balozi wa jimbo la Bengal Magharibi.

Rais wa chama cha upinzani cha Congress katika jimbo hilo, Adhir Ranjan Chowdhury, alituhumu mkuu wa jimbo hilo Bi Banerjee kwa kukiuka, katiba kwa kumruhusu afisaa hiyo kucheza densi akiwa amevalia sare yake.

"katiba hairuhusu mtu kucheza densi akiwa amevalia sare za kazi. Ni aibutupu kwamba sifa ya idara ya polisi ilivunjiwa heshima hivyo. Kwa kuruhusu afisa wa polisi kucheza katika hali ile, alivunja katiba ya India, '' alinukuliwa akisema afisa mkuu wa upinzani jimboni humo.

Taarifa zinasema kuwa kamishna mkuu wa zamani wa polisi Nirupam Som alisema, "wakati wa muhula wangu uongozini, singeruhusuhata kidogo polisi kucheza densi kama vile. ''Lakini baadhi ya watu kwenye mitandao ya kijamii, walipuuza sakata hii iliyozua mgogoro huu wote kama kutokuwa kichekesho.

MWAKA MOJA TALAKA 1600, ZANZIBAR

TAKWIMU za Mahakama ya Kadhi Zanzibar, zimeonesha kuwa zaidi ya talaka 1,600 zimetolewa Zanzibar kati ya 2012 na 2013, huku wanawake wengi wakitelekezwa bila kupatiwa haki zao baada ya kutengana na wenza wao.

Akizungumzia hali hiyo juzi mbele ya waandishi wa habari, Naibu Kadhi Mkuu wa Zanzibar, Hassan Othman Ngwali, alisema kwa sasa peke yake kuna kesi 1,917 za talaka mbele ya Mahakama sita za Unguja.

Mbali na kuwa na kesi hizo, Ngwali alisema wanawake wamekuwa waathirika wakuu baada ya kuvunjika kwa ndoa, kwa kuwa hakuna hukumu ya kesi zilizopita, ambayo haki ya mgawanyo wa malikwa wanandoa imetolewa.

Alitaja baadhi ya sababu zinazochangia kuwepo kwa wingi wa talaka Zanzibar, kuwa ni pamoja na wanandoa wenyewe kukosa mafunzo ya ndoa na majukumu yake kwa ujumla.

"Moja ya tatizo la kuvunjika kwa ndoa katika jamii, ni wanandoa kukosa elimu ambayo itawafanya kujua haki na faida zinazopatikana katika ndoa," alisema.

Alisema Ofisi ya Mahakama ya Kadhi imeanza kutoa elimu kwa makadhi wote kuhusu haki za wanandoa katika kipindi chote wanapokuwa kwenye ndoa.

Naye Mwenyekiti wa Tume ya Kurekebisha Sheria Zanzibar, Bakari Mshibe, alisema marekebisho ya Sheria ya Mahakama ya Kadhi, yapo katika hatua za mwisho kuwasilishwa mbele ya Baraza la Wawakilishi.

Alitaja baadhi ya mambo yaliyofanyiwa marekebisho kwa lengo la kuimarisha Mahakama hizo, kuwa ni pamoja na kutoa uwezo wa kumshurutisha mwanamume kutoa matunzo ya mtoto wakati ndoa inapovunjika.

"Moja ya mambo yaliyopewa kipaumbele katika marekebisho yaSheria ya Mahakama ya Kadhi, ni kuwabana wazazi ambao hawatoi matunzo kwa watoto wakati ndoa inapovunjika," alisema.

Wanaharakati wengi Zanzibar, wanataka kuwepo kwa marekebisho makubwa katika Sheria hiyo ya Mahakama ya Kadhi,hasa katika mgawanyo wa mali kwa wanandoa wakati wanapotengana.

WANANDUGU WATANO WA FAMILIA MOJA WATEMBELEA MIKONO NA MIGUU

FAMILIA moja ya Uturuki inawapasua kichwa wanasayansi, kutokana na wanandugu watano kutokuwa na uwezo wa kutembea kama binadamu, na badala yake wanatembea mithili ya wanyama, wakitumia miguu na mikono.

Hata hivyo, katika uchunguzi wao waawali, wanasayansi hao wameeleza kuwa, hali iliyowakumba wanandugu hao haina uhusiano na mabadiliko ya binadamu, kwamba wanaanza kurudi katika zama za mwanzo ambako inaelezwa walitembea kwa miguu minne, wengine wakisema walianza kuwa nyani.

Ndugu hao watano ambao ni kaka na madada, wakiwa na umri wa miaka 16 hadi 34 kutoka kijiji cha Jimbo la Hatay, kusini mwa Uturuki,walianza kufuatiliwa na wanasayansi mwaka 2005 baada ya kugundulika na watu kutoka nje ya kijiji chao.

Wanatembea kwa mtindo wa kutambaa kama dubu kwa mikono na wanaweza kusimama tu kwa muda mfupi, kwa magoti yao.

Utafiti wa hivi karibuni ulifanywa na wanasayansi, Shapiro, Whitney Cole,Scott Robinson na Karen Adolph, wote wa Chuo Kikuu cha New York, Jessica Young wa Chuo Kikuu cha Tiba cha Northeast Ohio na David Raichlen, wa Chuo Kikuu cha Arizona.

"Lakini hawa hawana uhusiano na mgeuko wa binadamu kwamba baada ya kupitia hatua kadhaa za mabadiliko, sasa wanarudi katika hatua za awali, hilo halipo," mmoja wa wanasayansi hao amenukuliwa akisema.

Nadharia za awali zilidai familia ya Ulas ilikuwa ikitembea kama nyani, na kupendekeza kuwa huenda ni hatua ya kurudi nyuma kwa mabadiliko ya binadamu.

Lakini sasa, wanasayansi wa Kimarekani wamethibitisha kwa kusema wanandugu hao wanakabiliwa na kasoro isiyoonekana na hutokea mara chache.

Katika ripoti iliyochapishwa na PLOSOne, watafiti walisema familia hiyo wanatembea kwa namna tofauti kama nyani, ambao wakitembea huweka mikono upande mmoja na miguu upande mwingine wakijirudia rudia.

Walidai kutembea kwa wanandugu hao ni matokeo ya hali ya kurithi ambayo husababisha uwiano wa akili kutatizika.

"Nilikuwa na hamu ya kuweka rekodi sawa, kwa kuwa haya madai ya asili na sababu ya kutembea kama mnyama wa miguu minne imechapishwa mara kwa mara, bila kuwepo uchambuzi wa kwa nini wanatembea hivyo, na watafiti ambao si wataalamu wa namna mamalia wa hali ya juu wanavyotembea," Mtafiti Kiongozi Liza Shapiro wa Chuo Kikuu cha Texas alilieleza gazeti la The Washington Post.

"Tumeonesha wanyama wa miguu minne wanavyofanana na mtu mzima mwenye afya njema ambaye ameambiwa atembee kwa miguu minne wakati wa kufanya majaribio.

Mwaka 2005, watafiti wa Uingereza walikubali katika utafiti tofauti kuwautembeaji wa ndugu hao unatofautiana na baadhi ya mamalia wengine, ikizingatiwa wenyewe hubeba uzito wao wote kwenye viganja vya mkono na kifundo cha mkono na sio kiungio.

Hata hivyo, Mtaalamu wa Bayolojia wa Uturuki, Uner Tan awali alidai wanandugu hao, ambao pia wanaonekana kuwa wameathirika kwenye ubongo wanakabiliwa na hali inayoitwa Uner Tan Syndrome.

Alisema watu wanaokabiliwa na halihiyo hutembea kwa miguu minne na mara nyingine huzungumza kama wanyama na huwa na mtindio wa ubongo.

"Ghafla nimegundua wanatembea kwa mtindo kama nyani kama walivyokuwa wahenga wetu… nilikuwa wa kwanza kupendekeza kuwa kuna uwezekano wa hali ya binadamu kugeuka na kurudi enzi za zamani za ubinadamu," alisema.

Wandugu hao ambao wazazi wao wanatembea kawaida, mara ya kwanza walirushwa mwaka 2006 kwenye dokumentari ya BBC2, dokumentari hiyo ikiitwa The Family That Walks On All Fours.

Wakati mabinti wawili na mtoto mmoja wa kiume wamekuwa wakitembelea mikono miwili na miguu miwili, mtoto mwingine wa kiume na kike mara nyingine huweza kutembea wakiwa wamenyooka sawa, ingawa si kwa muda mrefu.

Profesa Nicholas Humphrey, ambaye aliitembelea familia hiyo mara mbili wakati wa dokumentari hiyo, alisema,
"inashangaza kama mfano wa kitu cha ajabu cha maendeleo ya binadamu. Lakini kinachovutia ni jinsia wanavyoweza kuishi katika ulimwengu wa kisasa."

Alisema alifikiri familia hiyo imerudi katika silika ya mfumo wa tabia iliyojikita ndani sana kwenye ubongo, lakini aliachwa wakati wa mageuko.

"Sidhani kama walitakiwa kuwa wanyama wanaotembelea miguu minne kutokana na jeni zao, lakini mfumo wa utengenezaji jeni zao zinawaruhusu kuwa hivyo," alisema.

Wanandugu hao watano ambao wana kaka na dada zao wengine 14 ambao hawajaathirika na hali hiyo, hutumia muda mwingi kukaa nje ya nyumba yao ya familia iliyoko kijijini. Hata hivyo, mmoja wao hutembea kijijini, kuchanganyika na kuzungumza na watu.

NDEGE YAANGUKA NA KUUA 40

Ndege moja iliokuwa na abiria 40 imeanguka mjini Tehran nchini Iran.

Runinga ya taifa la Iran imesema kuwa abiria wote wamefariki.

Ndege hiyo ya kampuni ya Taban Air imeripotiwa kuanguka katika makaazi baada ya kupaa kutoka uwanja wa ndege wa Mehrabad Maghribi mwa mji wa Tehran.

Ndege hiyo inayojulikana kama Iran 141 ilitengezwa nchini Iran kupitia teknologia ya Ukraine.

Uchunguzi umeanzishwa kuhusu ni nini kilichosababisha ajali hiyo.

Iran imekabiliwa na ajali kama hizo katika siku za hivi karibuni kutokana na ndege zake zilizozeeka mbali na marekebisho mabaya inazozifanyia.

MAREKANI YAENDELEZA MASHAMBULIZI IRAQ

Marekani imesema kuwa imetekeleza mashambulizi zaidi kazkazini mwa Iraq dhidiya maeneo yanayodhibitiwa na wapiganaji wa Jihad.

Taarifa kutoka Pentagon imesema kuwa ndege za Marekani pamoja na zile zisizo na rubani ziliharibu magari ya kijeshi ya wanamgambo hao likiwemo lile lilokuwa likiwashambulia raia wa Yazidi ambao wamekimbilia hifadhi katika mlima Sinjar.

Awali Rais Obama amesema kuwa kupitia washirika wake wa ulaya pamoja na wanajeshi wa Iraq watawakabili wanamgambo ambao wameuzunguka mlima huo.

Hata hivyo ameonya kuwa kampeni hiyo ya kijeshi itachukua miezi kadhaa na kwamba itachukua mda kwa jeshi la Iraq kujikusanya ili kutoa upinzani mkali dhidi ya wanamgambo hao.

Wakati huohuo Ndege za kijeshi za Marekani na zile za Uingereza zimeendelea kuangusha misaada kwa raia waliokwama katika Mlima Sinjar nchini Iraq,ijapokuwa viongozi wa mataifa hayo mawili wamekubaliana kwamba hatua hiyo sio suluhu ya kudumu.

Wamesema kuwa lazima njia ya kuwaondoa raia hao hadi katika eneo lililo salama itafutwe ili kuzuia mauaji ya kimbari.

Mfanyikazi mmoja wa shirika la Amnesty International kazkazini mwa Iraq, Donatella Rovera ameiambia BBC kwamba maelfu ya raia kazkazini na magharibi mwa mlima huo wamefanikiwa kutoroka, lakini wengi zaidi katika eneo la kusini la mlimahuo hawana mahala pa kwenda.

Amesema kuwa wale waliotoroka wako katika hali mbaya baada ya kukaa siku sita bila chakula na maji kidogo.