MSHIKAMANO ARTS WAFANYA USAFI

Vijana wa kikundi cha MSHIKAMANO ARTS GROUP cha mjini Mpanda Waanzisha kampeni ya usafi katika Mji huo(MPANDA) ijulikanayo kwa jina la "USAFI WA MJI NI MIMI NA WEWE".

Kampeni hiyo ambayo pia inashirikisha wasanii wa kundi la muziki wa kizazi kipya KATAVI FOR REALY itakua ikifanyika kila siku ya jumamosi ili kudumisha hali ya usafi mjini kwa kila mtu kufanya usafi eneo lake la kazi na mazingira yanayomzunguka.

Sambamba na hayo kutakuwa na uzinduzi wa kampeni hiyo tarehe 12/10/2013 katika viwanja vya kashaulili, uzinduzi utakaoambatana na burudani ya muziki na michezo ya jukwaani toka makundi hayo ya sanaa.


Picha:Majaliwa Rubuye

MTANZANIA NA MWANANCHI WAFUNGIWA

Serikali imeyafungia kutochapishwa Magazeti ya MWANANCHI na MTANZANIA kuanzia 27 Septemba, 2013 kutokana na mwenendo wa magazeti hayo kuandika habari na makala za uchochezi na uhasama kwa nia ya kusababisha wananchi wakose imani kwa vyombo vya dola hivyo kuhatarisha amani na mshikamano ulipo nchini.


Gazeti la MWANANCHI limefungiwa kutochapishwa kwa siku kumi na nne(14) kuanzia 27 Septemba,2013.
Adhabu hii imetangazwa kwaTangazo la Serikali(Government Notice )Namba 333 la tarehe 27 septemba,2013.


Gazeti la MWANANCHI limepewa adhabu hiyo kutokana na hivi karibuni kuchapisha habari zenye mwelekeo wa uchochezi na uvunjifu wa amani, mfano tarehe 17 Julai, 2013 katika toleo Namba 4774 ilichapisha habari isemayo "MISHAHARA MIPYA SERIKALINI 2013" kwa kuchapisha waraka uliozuiliwa kwa matumizi ya vyombo vya habari waraka huo ulikuwa wa Siri haukupaswa kuchapishwa Magazetini.

Aidha, katika toleo la Jumamosi, tarehe 17 Agosti,2013 lilichapisha habari yenye kichwa kisemacho "WAISLAM WASALI CHINI YA ULINZI MKALI" habari hiyo ilikolezwe na picha ya mbwa mkali mwenye hasira.

Habari na picha hiyo ilitoa tafsiri ya kuwa Jeshi la Polisi lilipeleka Mbwa katika maeneo ya ibada ya waumini wa dini ya kiislam. Jambo ambalo halikuwa la ukweli.


Jeshi la Polisi katika doria siku hiyo halikupeleka mbwa katika maeneo ya Misikiti. Serikali na jeshi la Polisi linaheshimu na kuzingatia maadili ya dini ya Kiislamu na kwa hiyo Jeshi lake hakiwezi kupitisaha au kuingiza mbwa katika maeneo ya ibada.

Hivyo basi, kwa gazeti hili kuchapisha habari iliyokolezwa na picha ya mbwa ni uchochezi wa kulichonganisha Jeshi la Polisi na waumini wa dini ya kiislam mbwa ni najisi hapaswi kuingia katika maeneo ya ibada.


Gazeti la MTANZANIA limefungiwa kutochapishwa kwa siku tisini(90) kuanzia tarehe 27 Septemba,2013 kwa kuchapisha habari zenye uchochezi.

Gazeti hili limeonywa mara nyingi lirekebishe mtindo wake wa uandishi wa kichochezi na lizingatie maadili na Sheria na Kanuni za fani ya Habari.

Pamoja na kuonywa gazeti hili halikuonyesha kuzingatia maelekezo ya Msajili wa Magazeti, mfano ;katika toleo na 7262 la 20 Machi,2013 liliandika habari yenye kichwa kisemacho"URAIS WA DAMU",tarehe 12 Juni,2013,toleo Namba 7344 lilichapisha makala isemayo"MAPINDUZI HAYAEPUKIKI".

Aidha, siku ya Jumatano,tarehe 18 Septemba, 2013 katika toleo Namba 73414 ukurasa wa mbele lilichapisha Kichwa cha habari kisemacho "SERIKALI YANUKA DAMU "taarifa hiyo ilikolezwa na picha zilizo unganishwa kwa ustadi mkubwa kwa kutumia kompyuta kutapakaza rangi nyekundu mithili ya damu nyingi kumwagika.

Katika habari hiyo gazeti hilo limedai bila uthibitisho kuwa Jeshi la Polisi linahusika na wahanga waliomizwa na watu wasiojulikana kwa kumwagiwa tindikali na waliyovamiwa na kujeruhiwa vibaya.

Vile vile gazeti hilo limeishtumu serikali kuwa goigoi katika kushughulikia matukio yenye sura ya kigaidi.


Kwa ujumla wake habari hiyo ni ya kichochezi ina lengo la kuwafanya wananchi wavichukie vyombo vya ulinzi na usalama wavione kuwa haviwasaidii.

Kutokana na makosa yalitajwa hapo juu serikali imelifungia gazeti la Mtanzania kutochapishwa kwa muda wa siku tisini(90) kwaTangazo la Serikali Namba 332(Government Notice No.332) la tarehe 27 Septemba, 2013,.


Serikali inawataka wamiliki,wahariri na wanahabari kwa ujumla kuwa makini, kuzingatia weledi, miiko na madili yataaluma uandishi wa habari.


Serikali inawataka wamiliki na hasa wahariri kuhakisha kuwa habari wanazoziandika na vipindi wanavyoviandaa vinazingatia taaluma,kuweka mbele maslahi ya taifa letu kwa kuwa na uzalendo wa hali ya juu.

Serikali inavionya vyombo vya habari vinavyoutumia uhuru wa habari bila wajibu kuwa haitasita kuvichukulia hatua kali ikiwemo ya kuvifungia.

Serikali haitakubali kuona vyombo vya habari kuwa chanzo cha uvunjifu wa amani nchini.


Imetolewa na
MKURUGENZI IDARA YA HABARI
WIZARA YA HABARI,VIJANA, UTAMADUNI NA MICHEZO
28 SEPTEMBA,2013

JKT YAWATOA HOFU WANAOJIUNGA NA VYUO

JESHI la Kujenga Taifa (JKT), limewatoa hofu vijana waliotakiwa kujiunga na jeshi hilo kwa awamu yatatu, huku wakiwa tayari wamedahiliwa na kulipa ada vyuoni kwamba watachagua moja.

Vijana hao waliochaguliwa kujiunga JKT awamu ya tatu wanatakiwa kuripoti makambini Jumamosi Oktoba 28, jambo lililozua hali ya sintofahamu kwa wazazi wao ambaowalikwisha kuwalipia ada vyuoni.


Kwa mujibu wa JKT utaratibu utakuwa kwamba vijana wanaotaka kuendelea na masomo ya elimu ya juu kwa wakati huu lakini wamo kwenye orodha ya kujiunga na jeshihilo, watalazimika kuandika barua makao makuu kuomba kuahirisha mkataba wa mafunzo.

"Masharti waliyowekewa kwa ajili yakuomba kuahirisha kujiunga na JKT kwa sasa ni kuandika barua binafsi ya kuomba kuahirisha mkataba na barua iwe na picha ya mhusika anayeomba," ilisema taarifa hiyo.

Pia mhusika atatakiwa awe na nakala ya barua ya kuchaguliwa kujiunga na chuo, aeleze katika barua yake kuwa atajiunga na JKT baada ya kuhitimu masomo na kisha barua hiyo ifike makao makuukabla ya Oktoba 2, mwaka huu.

Taarifa hiyo ilisema kuwa suala la vijana wanaomaliza kidato cha sita kujiunga na JKT ni la lazima na kwamba ni wajibu wa kila mhitimu kuhudhuria mafunzo hayo.

BABU WA LOLIONDO AIBUKA TENA

Mchungaji Ambilikile Mwaisapila (Babu wa Kikombe) wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), amesema Mungu ameendelea kujifunua kwake na kumuonesha kuwa Tanzania itakuwa kioocha Afrika na dunia kwa ujumla.Alitoa kauli hiyo juzi mbele ya Waziri Mkuu Mizengo Pinda wakati akizungumzana wakazi wa kijiji cha Samunge, wilayani Ngorongoro mkoani Arusha wakati msafara wa Waziri Mkuu uliposimama nyumbani kwake ili kumsalimia akiwa njiani kurejea mjini Arusha.

Mchungaji Mstaafu Mwaisapila alisemakuna mambo mengi ambayo yameandikwa kwenye Biblia, lakini hayakutokea Israeli na sasa yatafanyika hapa Samunge.

"Mungu ametupenda sana, yanakuja mambo makubwa na wala hayako mbali. Kama mimi ni mzee na nitayaona, kwa hiyo mtarajie kuwa hayako mbali kutokea," alisema huku akishangiliwa na wananchi.Alisema katika mafunuo aliyopewa na Mungu ameoneshwa kwamba watu wengizaidi watafurika kijijini Samunge kuliko ilivyokuwa hapo awali. Alitumia fursa hiyokuishukuru Serikali kwa misaada iliyotoa wakati wa kugawa kikombe ikiwemo mahema, maji na ulinzi.

Waziri Mkuu, Pinda ambaye yuko mkoani Arusha kwa ziara maalum ya kusikiliza matatizo na migogoro ya ardhi yanayowakabili wakazi wa wilaya ya Ngorongoro, katika tarafa za Ngorongoro, Loliondo na Sale alisema anakubaliana na utabiri wa Mch. Mwaisapila kwani Tanzania imejaliwa gesi nyingi na mafuta mengi ambavyo vitabadili sura ya Taifa hili.

"Mungu ametupa gesi nyingi sana, katika miaka miwili tutakuwa na umeme kila mahali. Tuna makaa ya mawe ambayoni nishati kubwa na sasa tuna fursa ya kupata nishati ya umeme kutoka ardhini (Geo-thermal) katika Ziwa Natron," alisema.

Alisema Tanzania imekuwa kimbilio la kila mwekezaji na sababu kubwa ni amani na utulivu uliopo nchini. Aliwaeleza wakazi wa Samunge kwamba mapema mwakani mkandarasi wa barabara atakuwa katika eneo lao kwa ajili ya ujenzi wa barabara ya lami ambapo awamu ya kwanza itaanzia Wasso hadi Mto wa Mbu kupitia Samunge.

Akitoa ombi maalum kwa niaba ya vijanambele ya Waziri Mkuu, Elias Kalumbwa, alisema wanaomba kuchimbiwa bwawa iliwaweze kujiajiri kupitia kilimo cha mboga na matunda.

Kalumbwa ambaye amesomea masuala ya wanyamapori alisema eneo la kuchimba bwawa lipo katika mto wa msimu unaopita kijijini hapo.

Naye MarthaSereri (70) alimweleza Waziri Mkuu kwamba wanaomba jimbo laNgorongoro ligawanywe kwa sababu ni kubwa sana kiasi kwamba inamuwia vigumu mbunge wao kufika maeneo yote.

Aliomba pia wapatiwe walimu wa sayansi na hisabati kwa ajili ya shule 10 za sekondari zilizopo kwenye tarafa yao.

Aliomba wapatiwe mikopo ya matreka iliwaweze kuongeza ukubwa wa mashamba yao.


"Tunaomba mikopo ya matrekta na plau, haya mashamba umeyaona njiani yamelimwa na Wakenya. Ukikodisha trekta kila ekari unatozwa sh. 100,000/-. Je tutafika wapi? Mkitukopesha matrekta mtakuwa mmetusaidia zaidi," alisema.


Akijibu hoja hizo, Waziri Mkuu alisema hoja zao ni za msingi na kwamba suala la vijana kupatiwa bwawa ni jambo linalowezekana kupitia mipango ya maendeleo ya kilimo ya wilaya (DADPS)."Andaeni andiko lenu, inabidi litoke kwa wananchi na si Serikalini. Mkituletea ni jambo linalowezekana kwani liko ndani yamipango ya wilaya," alisema.

Akijibu hoja kuhusu ukubwa wa jimbo, Waziri Mkuu aliwaambia wakazi hao kwamba inawezekana kuongeza jimbo isiwe suluhisho la matatizo yao kwa sababu ya jiografia ya eneo lao.

"Kuongeza jimbo inaweza isiwe jibu la kila kitu kwani matatizo mnayopata yanatokana na jiografia ya eneo lenu, kutoka Ngorongoro, Loliondo hadi huku Sale.

Mimi nadhani tuangalie pia uwezekano wakuwapa Halmashauri ili kusogeza hudumakwa wananchi. Tutaangalia njia zote mbili na kuona ipi italeta majibu ya haraka kwenu," alisema.

AL SHABAAB WASHAMBULIA TENA

Al-Shabaab leo imevamia tena kituo cha polisi katika mji mdogo wa Mandera uliopo mpakani mwa Kenya na Somalia na kuua polisi wawili na wengine kujeruhiwa kisha kuchoma moto magari 11. Duru za uchunguzi zinaonesha hii ni sehemu tu ya mfulululizo wa mashambulizi waliyoyaandaa.

AL SHABAAB WADAI KENYA IMETUMIA SIRAHA ZA SUMU

WAKATI Serikali ya Kenya ikitangaza kukamilisha kazi ya kupambana na magaidi walioteka kituo cha bishara cha Westgate, Nairobi na kufanikiwa kuwaangamiza, mfanyakazi wa moja ya maduka ya kituo hicho, amesema mwanamke anayefanana na Samantha Lewthwaite alimmiminia risasi siku ya tukio.Shuhuda huyo alisema alikutana uso kwa uso na mwanamke mwenye rangi nyeupe na nywele ndefu nyeusi akiwa na bunduki aina ya AK-47– kama Mwingereza Mwislamu anayetuhumiwa kutoa mafunzo kwa magaidi, Lewthwaite-wakati amejificha karibu na kasha ndipo akammiminia risasi.Katika hali ya kushangaza, mwanamke huyo aliyejitambulishakwa jina moja la Caroline, hakudhurika na risasi hizo wakati magaidi hao wakivamia duka hilo Jumamosi.Alisema:

"Alikuwa juu kidogo lakinisi mbali na mimi, alikuwa karibu, kiasi kwamba niliweza kumwona akiangaliaangalia sakafuni nilikokuwa hatimaye akaniona.

Alisimama na kunilenga na kufyatua bunduki. Risasi zote hazikunipata, sijui nini kilitokea! "Ghafla aliacha kunishambulia kwa muda na kuangalia pembeni na niliruka na kukimbilia kwenye konana ndivyo nilivyoweza kutoroka.


Alikuwa na ngozi nyeupe na nywele ndefu nyeusi na alivaa baibui jeusi. Sikumbuki vizuri, lakini nakumbuka alikuwa mweupe."Ofisa wa kupambana na ugaidi wa Kenya juzi usiku alibainisha kwamba polisi wamepokea ushahidi mwingi wa mwanamke miongoni mwa magaidi hao anayefanana na mjane wa Jermaine Lindsay anayetuhumiwa kwa ugaidi wa kujitoa mhanga.Aliongeza: "Tunaamini kwamba alihusika na shambulio hilo.

Hatuna shaka na mashahidi walioshuhudia ambao wanasema walimwona akiongoza na kutoa maagizo kwa washambuliaji." Maelezo ya jinsi alivyo mwanamke huyo yalithibitishwa na kauli ya Rais Uhuru Kenyatta juzi usiku, kwamba alipokea taarifa za kiintelijensia zikisema kuwa kuna mwanamke Mwingereza ambaye alihusika katika shambulizi hilo. Waziri wa Mambo ya Nje wa Kenya,Amina Mohamed naye aliongeza:


"Mwingereza huyo alikuwa mwanamke…alishafanya matukio haya mara nyingi."Juzi, taarifa kwenye Twitter ya kikundi cha al Shabaab ilidai kuwa Lewthwaite ndiye alikuwa akiamuru magaidi kushambulia. Maofisa usalama wa Uingereza walisema bado hawajapokea uthibitisho wowote kutoka Kenya kuhusu uhusika wa Lewthwaite katika shambulizi hilo, lakini wakasema hawatashangaa wakisikiaamehusika.Ilisemekana pia juzi kwamba bibi wa Lewthwaite, Ellen Allen (85) alikimbizwa hospitalini Banbridge, Ireland Kaskazini, baada ya kuzimiakutokana na msongo wa mawazo uliosababishwa na utukutu wa mjukuu wake huyo.

Lewthwaite amekuwa akitafutwa tangu Polisi ilipozima njama zake za kulipua bomu Mombasa, Kenya mwaka 2011, juzi kesi dhidi ya mwenzake, Jermaine Grant ilianza mjini humo.Maofisa wa kupambana na ugaidi wa Uingereza -Scotland Yard-walitoa ushahidi wao katika kesi hiyo wakizungumzia kemikali zilizokutwa katika kiwanda chao kidogo cha kutengeneza mabomu.

Noel Hogan, ambaye alimhoji mwanafunzi huyo wa zamani wa sarufi muda mfupi kabla ya milipuko ya mabomu ya Julai 7, alisema:

"Kama Samantha anahusika, hainishangazi." Hogan alikodiwa na benki kuchunguza kwa nini mteja wao, mume wa Lewthwaite, Lindsay, alitumia pauni 900 kununua chupa kadhaa za marashi kwa siku chache.

Ununuzi huo unaotia shaka, ulifanyika siku chache kabla ya shambulizi hilo la Julai 7 na marashi hayo yalitumika kutengenezea milipuko nyumbani.

Waliomfahamu Lewthwaite tangu udogo nyumbani kwao Aylesbury, walieleza kushangazwa na yeye kuhusika kama mmoja wa wafadhili wa al Shabaab na mkufunzi wa utengenezaji mabomu.

Diwani Raj Khan alisema:"Alikuwa msichana kijana Mwingereza wa kawaida tu. Hakuwa anajiamini sana. Sikuwa nachochote cha kumshuku." Lewthwaite alikuwa mjamzito wa miezi saba wakati mumewe alipojilipua na kuua watu 26.

Wajifanya maiti Wakati magaidi wamepagawa wakifyatua risasi ovyo, pengine mama na wanawe wawili hisia zao zingewasukuma kukimbia na kuokoa maisha yao. Lakini familia hiyo iliepuka mauaji hayo kwa kufikiria haraka na kujifanya wamekufa ili wanusurike.


Mama na wanawe wawili walilala chini na 'kujikausha' huku akiwa amewawekea mkono wake mgongoni wanawe hao. Ni kutokana na utulivu waliokuwa naokatika mazingira hayo ya kutisha, ndipo polisi mmoja alipotambaa na kupata nafasi ya kuwaokoa. Kelele za magaidi zilisikika kwa nyuma yao, na hicho ndicho pengine kilionekana kuwashawishi kuinuka na kukimbia.Ofisa wa Polisi alimchukua msichana mkubwa na mdogo na kukimbilia nje mama akifuatia. Msichana mkubwa aliendelea kushikilia mfuko wa vitu walivyokuwa tayari wamenunua dukani hapo.

Al Shabaab yatamka Licha ya Rais Kenyatta kutangaza ushindi wa majeshi yake, al Shabaab ilidai janakuwa mateka 137 waliotekwa nao dukani hapo walikufa.

Hata hivyo, maofisa wa Serikali hawakuthibitisha idadi hiyo, ambayo iko juu kuliko iliyotangazwa na Serikali kuwa ya watu waliopotea na kuzidi pia 72 ambao ndiyo wanaodaiwa kupotezamaisha wakiwamo wapiganaji watano kama ilivyotangazwa na Rais juzi.

Wapiganaji wa al Shabaab katika ujumbe wao kupitia Twitter walisema mateka 137 waliokuwa wakishikiliwa na mujahidina walikufa na kuelekeza lawama kwa Serikali ya Kenya. Silaha za kemikali Katika ujumbe mwingine, wapiganaji hao pia wanalaumu vikosi vya Kenya kwa kutumia kemikali kumaliza sintofahamu hiyo ya siku nne, kabla ya 'kubomoa' duka hilo."Katika kitendo kinachoonekana cha uoga, vikosi vya Kenya vilivyokata tamaa viliamua kwa makusudi kutumia kemikali…na katika kuficha uhalifu wao, Serikali iliamua kuvunja jengo hilo na kufukia ushahidi na mateka wote wako chini ya kifusi." Hata hivyo msemaji wa Serikali Manoah Esipisu mara moja alikanusha madai hayo na kusisitiza hakuna silaha za kemikali zilizotumika na kwamba idadi ya raia waliouawa ni 61.

"Al Shabaab inajulikana kwa madai potofu na hakuna ukweli wowote katika wanachokisema," alisema. Esipisu alisema sakafu za duka hilo zilibomoka baada ya mashambulizikuanza na kusababisha udhaifu katika sakafu hizo na ya juu kuangukia ya tatu ambayo ni eneo la maegesho na kuangulia ya pili hadi ya kwanza na ya chini.

Juzi usiku wakati Rais Kenyatta alihutubia Taifa, milio ya bunduki iliendelea kusikika, ambapo Esipisualisema ilitoka kwa vikosi vya Kenya vilivyokuwa vikipekua chumba hadi chumba katika duka hilo, vikifyatua risasi kujihami kwani havikuwa vikijua ndani kuna hatari gani.


Alisema: "Wakati wa safishasafisha unapokuwa umedhibiti eneo unapoingia chumbani ambako hujaingia kabla unapaswa kufyatua risasi kuhakikisha kwamba hauingiimtegoni. Hakukuwa na majibizano kutoka kwa magaidi kwa zaidi ya saa 36.

"Wataalamu kusaidia uchunguzi Wakati huo huo, Serikali ya Kenya ilitangaza kwamba wataalamu kutoka Uingereza, Marekani na Israeli watasaidia uchunguzi juu ya shambulizi hilo.

"Kituo hicho kimefungwa kwa sababu ni eneo la uhalifu," alisemaEsipisu. Jana mchakato wa kuondoamiili katika duka hilo haukuwa umeanza, pengine kutokana na halikwamba haijawa salama sana, ingawa maofisa wa mochari ya Jiji la Nairobi walisema wafanyakazi wao wanajiandaa kwenda katika jengo hilo.

Kulikuwa pia na hofu kwamba baadhi ya magaidi wanaweza kuwa bado wako hai katika kifusi ndani ya jengo hilo lenye maduka mengi ya rejareja kama vile ya bidhaa za Bose, Nike na Adidas, benki, migahawa na casino.

Ofisa mwandanizi wa usalama anayehusika na uchunguzi alisema itachukua muda mrefu kupekua jengo lote kabla ya kutangaza rasmi kuwa tishio la magaidi halipotena. Siku tatu za maombolezo kitaifa zilianza jana.


Al Shabaab, ambayo inamaanisha kijana kwa Kiarabu, ilianza kutishia Kenya na shambulizi la kigaidi mwaka 2011, baada ya Kenya kupeleka vikosi vyake Somalia baada ya kutokea utekaji nyara wa raia wa mataifa ya Magharibi ndaniya Kenya.

Chanzo: Habari leo

"NYIE WATU WABAYA" KAULI ALIYOTOA MTOTO ELLIOT PRIOR KWA MAGAIDI WA AL SHABAAB

Mtoto wa miaka minne ambaye ni raia wa Uingereza, Elliott Prior ameonyesha ushujaa wa hali ya juu baada ya kuweza kuwatolea maneno makali na ya kugusa magaidi waliovamia jengo la maduka la Westgate.

Baada ya maneno hayo, baadhi ya taarifa zilizochapishwa kwenye vyombo mbalimbali vya kimataifa, vinasema magaidi hao waliomba mtoto huyo awasamehe kwa maelezo kuwa wao siyo watu wabaya.

Inaelezwa kuwa, kitendo cha mtotohuyo kilikuwa cha kishujaa kwani aliweza kuwaeleza magaidi hao maneno hayo, bila kuogopa silaha nzito walizokuwa wameshika mkononi huku baadhi ya watu wakiwa wameshauuawa.

Mtandao wa Daily Mail unasema mtoto huyo alimwambia mmoja wamagaini hao kuwa 'Nyie ni watu wabaya sana'.

Mtandao huo unasema mtoto huyo aliyasema maneno hayo kama njia ya kumkinga mama yake Amber, aliyekuwa amepigwa risasi mguuni pamoja na dada yake Amelie, mwenye umri wa miaka sita ambaye walikuwa wote ndani ya duka hilo.

Katika kile kilichotafsiriwa kuwa ni kuumizwa na maneno hayo, magaidi hao walimpa Elliott pamojana dada yake mifuko miwili miwili ya chokleti na kuwaomba msamaha. Taarifa hizo zinasema kuwa, gaidi huyo alisema "Samahani nisamehe,sisi siyo watu wabaya".

Mama huyo anasema kuwa, kabla ya kukamatwa na magaidi hao, yeye na watoto wake walikuwa wamejificha kwenye jokofu la kuhifadhi nyama lililopo ndani ya duka la Nakumatt kwa zaidi ya saa moja na nusu.

Anasema kuwa, baada ya kukamatwa na magaidi hayo, walimpiga risasi ya paja.

Mjomba wa watoto hao aliliambia gazeti la The Sun la Uingereza kuwa"Walikuwa na bahati kuweza kutokakwenye mikono ya hao magaidi. Hao magaidi walisema kuwa, kama kuna mtoto yeyote aliye hai ndani ya jengo hilo wanaweza kuondoka.

'Mama yao alisimama na kusema 'ndio' , binamu yangu aliweza kupata ujasiri wa kusimama na kuwaambia kuwa, nyie ni watu wabaya sana'.

Taarifa zaidi zinasema kuwa, baada ya magaidi hao kujua kuwa mama huyo na watoto wake hawakuwa kati ya watu waliowalenga, hawakuwaua.

VIKOSI VYA KENYA VYADHIBITI WESTGATE

Hatimaye vikosi vya usalama nchini Kenya vinasema vimelidhibiti jengozima la Westgate mjini Nairobi, ikiwa ni zaidi ya siku tatu baada ya jengo hilo kuvamiwa na wanamgambo.

Milipuko ikifuatiwa na milio ya risasi imesikika kutoka ndani ya jengo hilo asubuhi ya leo huku duruzikisema kuwa vikosi vya usalama vinaelekea kukamilisha operesheni hiyo.

Kwa mujibu wa vyombo vya habari, magaidi sita waliokuwa wamesalia wameuawa huku wengine watatu wakiuawa hapo jana.

Serikali imesema zaidi ya watu 60 wameuawa na wengine zaidi ya 170 kujeruhiwa katika shambulio hilo ambalo Al shabaab imekiri kulitekeleza.

Wizara ya mambo ya ndani imesema wanajeshi wanaendelea kulisaka jengo zima la Westgate kutoka orofa moja hadi nyengine kuhakikisha kwamba hakuna matekaaliyesaliaWakati huohuo, waziri wa mambo ya nje amesema kuwa wawili kati yawanamgambo watatu waliofanya shambulii hilo ni raia wa Marekani pamoja na mwanamke muingereza.

Kwenye mahojiano na kituo kimoja cha televisheni nchini Marekani, Amina Mohamed alisema kuwa wamarekani walikuwa kati ya umri wa miaka 18 na 19 ingawa wenye asili ya kisomali au kiarabu na waliishi mjini Minnesota.

Mshukiwa mwingine alikuwa mwanamnke Muingereza ambaye inasemekana alikuwa amefanya vitendo vingi vya aina hii kwa niaba ya Al Shabaab.

Shirika la Red Cross limeambia BBCkuwa watu 63 wangali hawajulikani waliko.

Wanajeshi wa Kenya katika juhudi zakuokoa mateka na kukomboa jengo la Westgate Haijulikani idadi ya wanamgambo waliokuwa ndani ya jengo hilo , lakini maafisa wa usalama wamesema kuwa wanamgambo watatu wameuawa.

Kundi la kigaidi la al-Shabab limekiri kutekeleza mauaji hayo, kulipiza kisasi hatua ya Kenya kujihusisha kijeshi nchini Somalia.

Operesheni hiyo iliendelea usiku kucha ingawa kwa mujibu wa waziri wa usalama wa Kenya, ilikuwa katikamkondo wake wa mwisho.

"magaidi hawa huenda wanakimbia na kujificha katika sehemu mbali mbali za jengo hilo lakini ghorofa zote za jengo hilo zimedhibitiwa na majeshi,'' alisema Ole LenkuAliongeza kuwa mateka wote walifanikiwa kuokolewa.

Jumatatu jioni moshi mkubwa ulionekana ukifuka kutoka kwenye jengo la Westgate ukiambatana na moto mkubwa.

Moto huo unasemekana uliwashwa na wanamgambo hao ili kutatiza vikosi vya usalama katika juhudi zao za kutaka kukomboa jengo hilo.

MAPIGANO YAENDELEA WESTGATE

Huku hali ya mshikemshike ikiendelea kushuhudiwa katika jengo la Westgate lenye maduka, ufyatulianaji risasi umesikika ndani ya jengo hilo lenye maduka na mikahawa zaidi ya themanini. Milio hiyo ilidumu kwa dakika tatu na kufuatiwa na moshi mkubwa juu ya jengo hilo.

Hakuna taarifa kamili kuhusu kilichosababisha moshi huo.

Wapiganaji wa Al shabaab wamewateka nyara raia ambao idadi yao haijulikani.

Walikuwemo ndani ya jengo wakiendelea na shughuli zao kuanzia Jumamosi mchana wakati wapiganaji wa Al shabaab walipowavamia na kuanza kufyatua risasi kiholela.

Inaarifiwa kuna maiti kumi katika ghorofa ya kwanza ya jengo hilo.

Aidha wapiganaji hao wanaoaminikakuwa wanachama wa Al Shabaab ni kati ya kumi na kumi na watano na bado wangali ndani ya jengo hilo.

Ripoti zinasema kuwa ufyatulianaji mkubwa wa risasi pamoja na milipuko imesikika katika jengo hilokwa takriban dakika 15.

Harakati za kuendelea kumaliza operesheni hiyo zinaendelea lakini hali ya mateka walio ndani ya jengo hilo inaendelea kudorora.

Wakenya waliofanikiwa kuondoka katika jengo la Westgate kwa usaidizi wa polisi Rais Kenyatta amesema kuwa jeshi linajitahidi kuhakikisha kuwa linakabiliana vilivyo na wanamgambo hao. Helikopta za polisi zinazunguka juu ya jengo hilo pamoja na ndege za kijeshi kushika doria.

Vikosi vya usalama vinaendelea na opereshenikujaribu kuwanusuru waathiriwa wakati hali ikiwa ni ya ati ati katika eneo la shambulizi.Awali jeshi la Kenya lilisema limeweza kudhibiti jengo hilo lote ingawa bado limetaja hali kuwa tetemno hasa katika kujaribu kuwaokoa mateka waliosalia ndani ya jengo hilo.

Ripoti zinasema kuwa watu 69 wamefariki katika shambulizi hilo laAl Shabaab kufikia sasa huku 175 wakijeruhiwa. Baadhi wametibiwa na kuondoka hospitalini. Baadhi ya majeraha waliyopata ni majereha ya risasi na kutokana na guruneti ambalo Al shabaab waliwarushia wale waliokuwa ndani ya mikahawa siku ya Jumamosi.

Kundi hilo limekiri kutekeleza shambulio hilo kutokana na hatua ya Kenya kupeleka majeshi yake nchini Somalia ili kukabiliana na wapiganaji hao.

IDADI YA WALIOKUFA SHAMBULIZI LA WASTGATE NAIROBI YAONGEZEKA

Serikali ya Kenya kupitia kwa waziri wake wa usalama Ole Lenku imesema kuwa watu 59 wamefariki katika shambulizi la kigaidi lililofanywa na wanamgambo wa Al Shabaab na wengine 175 kujeruhiwa.

Waziri Ole Lenku amesema kuwa idadi ya magaidi walio ndani ya jengo hilo ni kati ya kumi na kumi na tano na haijulikani ikiwa wanwazulia waathiriwa au waathiriwa wamjificha katika sehemu mbali mbali z jumba la Westgate. Shirika la Red Cross awali katika taarifa yake ilisema kuwa watu 43 ndio waliofariki na zaidi ya 50 kujeruhiwa huku wengine wakitekwa nyara katika mashambulizi la kigaidi Jumamosi mchana.

Milio ya risasi imeweza kusikika katika jengo la Westgate mjini Nairobi Kenya, ambako wanamgambo wa Al shabaab wanawazuilia mateka ambao idadi yao haijajulikana hadi sasa. Wanajeshi wawili walijeruhiwa katika ufyatulianaji huo na kukimbizwa hospitalini kwa matibabu huku watu wawili wakinusuriwa asubuhi ya leo.

Hadi sasa jeshi limeweza kudhibiti hali nje na ndani ya jengo hilo, magari ya kijeshi yakiwa yameletwakatika eneo hilo huku polisi na wanajeshi wakijaraibu kuwanusuru baadhi ambao wangali wanazuiliwa ndani ya jengo hilo.

Watu 39 wameuawa baada ya wanamgambo hao kushambulia jengo hilo mwanzo katika eneo la kuegeshea magari na kisha kuingia ndani ya mikahawa na maduka katika jengo hilo lenye ghorofa nne na kuwpaiga watu risasi kuholela. Kuna taarifa kuwa wanamgambo hao wako ndani ya duka moja kubwa katika jengo hilo.

Rais Kenyatta anasema kuwa baadhi ya waliofariki ni jamaa zake. Miongoni mwa waliofariki pia ni mwanadiplomasia wa Canada na raia wawili wa Ufaransa.

Rais Kenyatta anasema kuwa wale waliohusika lazima wakabiliwe na mkono wa sheria. Jamaa na marafiki waliofika kujua hali ya jamaa zao wamezuiwa kuingia ndani ya jengo hilo.

Wengi wa waathiriwa walifariki kutokana na majeraha yao.

FAMILIA YAUWAWA KINYAMA

WATU watatu wa familia moja akiwemo mtoto wa mwaka mmoja wameuawa kikatili kwa kuchinjwa nawawili kunyongwa katika Mtaa wa Ihila, Kata ya Buhongwa Wilaya ya Nyamagana mkoani Mwanza.

Watu waliouawa ni baba wa familia, Jonas Lulinga (44) aliyechinjwa, mkewake Lucia Jonas (35) aliyeuawa kwakunyongwa kama ilivyokuwa kwa mtoto wao mwenye umri wa mwaka mmoja, Eliud.Tukio hilo limethibitishwa na Mkuu wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai (RCO) katika Jeshi la Polisi mkoani Mwanza, Joseph Konyo aliyesema wanamsaka fundi ujenzi anayetuhumiwa kusababisha vifo hivyo. "Kwa sasa Polisi inaendelea na upelelezi wa kina juu ya tukio hilo na hatuwezi kumtaja jina fundi ujenzi huyo, ili kuepuka kutoroka natunawaomba wananchi wawe makinina watu ambao hawawafahamu vyema," alisema Konyo.

Naye Mwenyekiti wa Mtaa wa Ihila, Joseph Kabadi akizungumza jana eneo la tukio, alisema vifo hivyo vilitokea usiku wakati wanafamilia wakiwa wamelala.

Baadhi ya majirani walimhusisha fundi na mauaji ikielezwa huenda aliiba fedha za marehemu aliyekuwa ameuza kiwanja kingine na kuanza ujenzi wa nyumba ambayo fundi huyo alipewa jukumula kuijenga, huku tayari akiwa ameshakamilisha ujenzi wa msingi.

MADHEHEBU YA DINI KUANZA KUCHUNGUZWA

SERIKALI imesema itaanza kuchunguza madhehebu ya dini kutokana na migogoro na malalamiko ya waamini dhidi ya viongozi wao kuongezeka.

Viongozi hao ni hasa wa kigeni kutokana na vitendo vyao vya kitapeli wanavyodaiwa kuvifanya, vikiashiria kujihusisha na biashara haramu ya dawa za kulevya kwa kivuli cha dini. Aidha, baadhi ya viongozi wanaolalamikiwa ni wachungaji na wanadaiwa baadhi yao kumiliki ardhi (mashamba) na migodi ya mamilioni ya fedha nchini kinyume cha sheria na wamejiandikisha katika mchakato wa kupata vitambulisho vya Taifa kama raia wa Tanzania.


Ingawa malalamiko yapo mengi serikalini, lakini ya hivi karibuni (barua na nyaraka za malalamiko tunazo) ni ya waamini wa Kanisa la The Bible Believers Church (BBC Mission) la Pugu Kajiungeni linalomhusisha pia Mchungaji wa Kanisa la Cornerstone la Tabata, yote ya Dar es Salaam.

Wanadai pia kuwa baadhi ya wachungaji walianza kuhubiri usikuwa manane katika mitaa ya Dar es Salaam wakidai wameagizwa na Mungu kuiteka Dar es Salaam na muda mzuri ni usiku, jambo linalowapa wasiwasi wafuasi wao zaidi wa aina ya Injili wanayohubiri.

Wanadai wachungaji wao (majina tunayo), raia wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) wamekuwa sababu ya migogoro ya kifedha na mali za Kanisa isiyokwisha kwa kile walichodai wameshindwa kutoa taarifa za fedha kwa waamini pale walipotakiwa kufanya hivyo.

Aidha, waamini hao kwa barua zao walizoandika kwa nyakati tofauti kwenda Wizara ya Mambo ya Ndani(nakala tunazo), wanadai na kulalamika kuwa wachungaji hao wamejiandikisha kupata vitambulisho vya Taifa kama raia wa Tanzania waliozaliwa Kigoma naMbeya, wakati wakijua wazi kuwa siraia.

Walidai kuwa hofu kubwa ya hatima ya usalama na makanisa yao imetanda kwao na wanaiomba Serikali ichunguze wachungaji hao haraka iwezekanavyo, kuwa huenda wanatumia kivuli cha Kanisa kufanya utapeli nchini, kwa kile walichodai wanahubiri usiku wa manane katika mitaa ya Dar es Salaam.


"Tunaiomba Serikali iwachunguze watu hawa haraka, wana vibali vya kimisionari vya kufanya kazi nchini kwa muda, lakini tunashangaa kwamba wamejiandikisha kupata vitambulisho vya Taifa kama raia, hatujui nia yao hawa watu, sasa hivi wanajimilikisha ardhi kutumia watoto wao, hali si shwari kabisa," alisema muamini mmoja ambaye hakuwa tayari kutaja jina lake gazetini.

Uchunguzi uliofanywa na gazeti hili baada ya malalamiko ya waamini hao wiki chache zilizopita umebainikuwa, wapo wachungaji katika makanisa kadhaa jijini humo, wameanzisha mtindo wa kuhubiri usiku wa manane katika mitaa ya Jiji la Dar es Salaam na kufanya vikao katika majumba ya starehe (baa) na katika kuhubiri huko, hutumia magari wanayoyabadili rangi mara kwa mara.

Hali hiyo ya mashaka inahusishwa pia na matukio ya kihalifu yanayokithiri nchini, ambayo baadhi yanahusisha mpaka viongozi wa kidini ikiwamo biashara haramu ya kuuza dawa za kulevya, ukahaba na ujambazi.Kwa mujibu wa nyaraka tulizonazo, Mchungaji wa Kanisa la BBC Mission lenye namba za usajili SA 7446 anayelalamikiwa inaonesha kuwa Kanisa hilo humkatia vibali vya kufanya kazi vya muda mfupi wa miaka miwili, kwa mujibu wa taratibu za Uhamiaji lakini amejiandikisha kama raia mzaliwa wa nchini.

Askofu wa Kanisa hilo la BBC Mission, Frank Mwangende alipoulizwa kuhusu jambo hili, alikiri kuwepo kwa mgogoro katika Kanisa lao tawi la Pugu-Kajiungeni na kueleza kwa ufupi kuwa, uongozi wa Kanisa unalifanyia kazi.Pia, Askofu Mwangende alikiri waamini wake kuandika barua ya malalamiko serikalini wakitaka Serikali iingilie kati suala hilo, lakini alisema wao Kanisa, wanayafanyia kazi malalamiko hayo kwa kuzungumza na pande zote mbili husika.Wachungaji wanaolalamikiwa walitafutwa na gazeti hili kwa zaidi ya wiki tatu sasa, bila kupatikana na baadhi yao walituma wasaidizi wao kuzungumza na gazeti hili na kudai kuwa malalamiko hayo yana lengo la kuwachafulia huduma yao nchini na kwamba hakuna ardhi yoyote wala mgodi wanaomiliki kinyume cha sheria.


Lakini nyaraka tulizonazo zinaonesha kuwa, wachungaji hao wanamiliki mashamba Morogoro na wamejiingiza katika biashara ya kuchimba madini mkoani humo, kwa zaidi ya miaka miwili sasa, na kwa kuwa wameoa Watanzania, wamerithisha watoto wao ardhi baadhi zikiwa mali ya makanisa.

Aidha, wanalalamikiwa kuwa wanatumia mgongo wa uchungaji kutapeli baadhi ya waumini wanaowafanyia kazi majumbani bila kuwalipa, huku waumini wenye fedha wakiwapa uongozi wa juu ndani ya Kanisa fedha na mali zao.

Namba za simu zilizoachwa kwa gazeti hili ili kupata wachungaji haohaziwezi kupatikana kwa takribani wiki tatu sasa na eneo la Kanisa wachungaji hao hawapo kwa kipindisasa wakidaiwa wapo nje ya mkoa kwa kazi ya utumishi.


Mkurugenzi wa Sheria wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, JustusMulokozi akizungumza kwa niaba ya Wizara, alikiri kupokea malalamiko ya waamini wa makanisa hayo mawili na mengine mengi, wakiwalalamikia wachungajiwao wa ndani na nje ya nchi kuhusu masuala ya fedha na mali za makanisa."

Ni kweli, tumepokea malalamiko ya waamini wa makanisa hayo, lakini niseme si hayo tu, yapo makanisa mengi wachungaji wanalalamikiwa, Serikali tumeona ipo haja kuchunguza makanisa na madhehebu ya dini zote yanayofanya kazi hapa, upo uhuru wa kuabudu lakini, kuna mambo yanatupa wasiwasi juu ya mwenendo wa wanaotoa huduma hizo za kiroho," alisema Mulokozi.

Alisema tayari Wizara imepeleka nyaraka hizo katika Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA) na Idara ya Uhamiaji kwa ajili ya uchunguzi zaidi kutokana na malalamiko ya waumini kudai wachungaji hao wamejiandikisha kama raia wakati ni wageni na alisema ikibainika, sheria itachukua mkondo wake.

Msemaji wa Idara ya Uhamiaji nchini, Abbas Irovya aliliambia gazeti hili kuwa idara yake inashirikiana na Wizara kushughulikia suala hilo na kwamba, wameiandikia Wizara kuomba nyaraka muhimu, ili kufuatilia uraia wa wachungaji hao walioatajwa na waamini wao.


-HABARI LEO

AL SHABAAB WAJISIFIA KUFANYA SHAMBULIO NAIROBI

Afisaa mmoja mkuu wa kundi la kigaidi la Alshabaab, amefahamisha BBC kuwa kundi hilo ndilo limehusika na shambulizi dhidi ya duka la kifahari la Westage mjini Nairobi Kenya.

Kwa mujibu wa Afisaa huyo mashambulizi hayo yalikuwa ya kulipiza kisasi kwa Kenya kwa kujihusisha na vita vya Somalia ambako wanajeshi wake wanakabiliana na kundi hilo.

Wanajeshi wa Kenya wamekuwa nchini humo tangu mwaka 2011 kama sehemu ya juhudi za muungano wa Afrika kutaka kurejesha uthabiti nchini Somalia.

Afisaa mkuu wa mambo ya ndani Kenya amesema idadi ya waliofarikini kumi na moja lakini shirika la msalaba mwekundu linasema idadi hiyo imefika watu 30 huku zaidi ya hamsini wakijeruhiwa.

Taarifa kutoka Ikulu ya Rais Kenya zinasema kuwa mshukiwa mmoja aliyekamatwa alifariki kutokana na majeraha yake.

Wanamgambo wa Al Shabaab kupitia kwa mtandao wao wa Twitter, wanasema kuwa Kenya haikuchukulia kwa uzito onyo walilotoa kwa taifa hilo kwa hatua ya kuwapeleka wanajeshi wake nchini humo kupambana dhidi yao.

Kundi hilo limesema limekuwa likitoa onyo mara kwa mara kwa Kenya kuwa ikiwa haitaondoa vikosi vyake nchini Somalia, athari zitakuwa mbaya mno.


Kupitia mtandao wao wa Twitter, Al Shabaab limesema kuwa Kenya ilijidai kutosikia onyo hizo, na kuendelea kuwaua waisilamu wasio na hatia nchini Somalia.

Taarifa hiyo ya Twitter ilisema kuwaShambulio la Westgate ni tone katika bahari tu ya mfano wa yanayowakumba wasomali waisilamu nchini Somalia.Taharuki ilianza hii leo saa saba mchana wakati watu wanaokisiwa kuwa kumi walipovamia jengo la kifahari la Westgate la kuwapiga risasi kiholela wakenya waliokuwa wanaendelea na shughuli zao za kawaida.

Kwa mujibu wa shirika la msalaba mwekundu, takriban watu 30 walifariki kwa kupigwa risasi au kutokana na majeraha yao na wengine wengi wenye majeraha ya risasi kukimbizwa hospitalini kwa matibabu.

WASHUKIWA UGAIDI WATEKELEZA MAUWAJI NAIROBI

Kufuatia watu wenye silaha
kuvamia jengo la ghorofa
nne lenye maduka la
Westgate jijini Nairobi sasa
inahofiwa angalu watu 30
wameuawa na wengine zaidi
ya hamsini kujeruhiwa
vibaya.

Kwa mujibu wa taarifa za
Shirika la Msalaba
mwekunde la Kenya idadi ya
waliofariki imeongezeka
hadi 30. Washambulizi
wangali ndani ya jengo hilo
na inaaminika wangali
wamewateka nyara baadhi
ya watu waliokuwa katika
duka hilo.
Wakati huo huo taarifa
kutoka ikulu ya Rais Kenya
inasema kwamba serikali
imeanzisha oparesheni kali
ya uokozi.
Hii nikutokana na taarifa
kwamba watu hao wenye
silaha wanawashikilia
mateka watu kadhaa ndani
ya jengo hilo.

Mtu mmoja ambaye
amejificha ndani ya jengo
hilo ameiambia BBC
kwamba ameona watu
wapatao 36 wakiwa
wameshikwa mateka na
waru hao.
Hata hivyo Ikulu ya Kenya
imesema ni mapema sana
kusema kwamba tukio hilo
ni la kigaidi.
Ikulu ya Nairobi vilevile
imesema ni mapema mno
kusema kama uvamizi huo
ni tukio la kigaidi au la.
Walioshuhudia kisa hicho
wanasema watu waliovalia
magwanda yalioonekana
kama ya kijeshi huku
wengine wakiwa wamefunika
nyuso zao walivamia jengo
hilo kwa wakifyatua risasi.
Kisa hicho kimetokea katika
eneo la kifahari la Westland
jijini Nairobi.
Maduka hayo ya Westgate
hupendelewa sana na watu
matajiri na wageni.
Walioshuhudia tukio hilo,
wanasema kuwa maguruneti
piya yalitumika.

Polisi waliojihami kwa
silaha wamezingira jengo la
maduka liitwalo Westgate,
katika mtaa wa Westlands,
na kuna taarifa ya watu
waliojeruhiwa wakitolewa
hapo kwa machera.
Hadi sasa kuna watu ambao
idadi yao haijulikani wamo
ndani ya jengo hilo.

Wakati huo huo Hospitali ya
Aga Khan, ya Nairobi imetoa
ujumbe wa dharura kwamba
damu inatakikana kwa
haraka.
Hii ni kutokana na taarifa
kwamba kuna idadi kubwa
ya majeruhi ambao
wamepelekwa katka
hospitali hiyo.












MAELFU WAJITOKEZA MKUTANO WA CDM, CUF NA NCCR

Maelfu wakazi wa jiji la
Dar es salaam wengi wao
wakiwa ni wafuasi wa
vyama vya Chadema ,Cuf
na NCCR Mageuzi
wemefurika katika
viwanja vya jangwani
kuwasilikza viongozi
wakuu wa vyama hivyo
ambapo kwa pamoja
viongozi hao wanapinga
hatua ya serikali kuingiza
baadhi ya vipengele katika
mswada wa sheria ya
marekebisho ya sheria
ya mabadiliko ya katiba.


Viongozi hao wanadai
kuwa vipengele hivyo
vitapelekea kupatikana kwa
katiba ya upande mmoja
na kuongeza kuwa kama
mswada huo hautafanyiwa
marekebisho, basi wao
hawatashiriki katika bunge
la katiba.


Katika viwanja hivyo ulinzi
uliimarishwa kutoka katika
vikundi mbalimbali
vinavyomilikiwa na vyama
hivyo huku shamra
shamra za huko na kule
zikiwa hazikosekani ili
mradi kunogesha mkutano.


Mwenyekiti wa taifa wa
Chadema na ambaye ni
kiongozi wa kambi ya
upinzani bungeni Mh
Freeman Mbowe
amewataka watanzania
kuacha uoga na wasimame
imara kudai katiba bora.


Naye mwenyekiti wa Cuf
Mh Profesa Ibrahim
Lipumba amesema
Tanzani inahitaji katiba
ambayo italinda na
kusimamia rasilimali za
taifa kuweza kutimia kwa
usawa na kuzingatia
mahitaji ya watanzania
wenyewe.


Kwa upande wake
mwenyekiti wa NCCR
Mageuzi na mbuge wa
kuteuliwa amesema
hakuna haja ya kutumia
mabavu na badala yake
ameitaka serikali itumie
busara zaidi ili kuweza
kufikia mwafaka wa jambo
hili.


-ITV

JAMAA ACHARAZWA MBOKO HADHARANI

JAMAA mmoja ameonja joto
ya jiwe baada ya kucharazwa
bakora 100 hadharani kama
adhabu baada ya kufanya
uasherati.


Mtu huyo ambaye hajaoa,
aliyetambuliwa kwa jina
moja la Mallam mkazi wa
Jimbo la Borno nchini
Nigeria alipata mkong'oto
huo baada ya kulala na
msichana asiyeolewa.


Mallam alipewa adhabu hiyo
kwa vile vitendo vya ngono
kabla ya ndoa (uasherati) ni
mwiko hivyo vinapigwa vita
katika jamii hiyo.

WABUNGE WAZICHAPA KAVUKAVU BUNGENI

Wabunge wa bunge la
waakilishi Nigeria
wamerushiana ngumi wakati
wa vikao vya Jumanne
baada ya kuzuka bungeni
suitofahamu kuhusu
mrengo wa wabunge
waliojitenga na chama
tawala. Taarifa hizi ni kwa
mujibu wa vyombo vya
habari nchini humo.

Kituo kimoja cha kibinafsi
cha televisheni, pamoja na
vituo vingine vilionyesha
picha za mbunge
mwanamke akimtosa kidole
usoni kwa ghadhabu
mbunge mwenzake wakati
mbunge mwanamume
akionekana akichukua kiti
nusura kumgonga
mwenzake.
Wabunge wengine
walionekana wakipigana
ngumi.


Mgogoro inasemekana
ulianza baada ya
mwenyekiti wa mrengo wa
wabunge waliojiondoa
kutoka kwa chama tawala,
Kawu Baraje, kuingia
bungeni akiandamana na
magavana wanaomuunga
mkono.

Inaarifiwa spika wa bunge la
waakilishi ,Aminu
Tambuwal, aliambia
wabunge kuwa Baraje
aliomba ruhusa
kuwahutubia wabunge wa
mrengo wake kabla ya
bunge kuanza vikao vyake.


Lakini kuwepo kwa wabunge
hao bungeni kuliwaghabisha
mno wafuasi wa chama
tawala, PDP,kiasi cha kuzuka
sokomoko bungeni kati ya
pande hizo mbili na
kumlazimisha bwana Baraje
kukatiza hotuba yake
kutokana na kelele bungeni.


Chama tawala PDP kina
wabunge wengi zaidi
bungeni wakiwa 23 kati ya
wabunge wote 36
Aidha chama hicho
kimetawala Nigeria tangu
kupata uhuru mwaka 1999
lakini hivi kribuni
kimezongwa na migogoro ya
ndani ya chama pamoja na
kukabiliwa na upizani wenye
ushawishi.

Wananchi wanajiandaa kwa
uchaguzi mwaka 2015, lakini
wadadisi wana wasiwai ikiwa
chama tawala kitakuwa
kimesuluhisha migogoro
yake, huku kikikabiliwa na
upinzani mkali.


Mgogoro huu umekuwa
ukitokota kwa miezi kadhaa
huku baadhi ya wabunge
wakitofautiana kuhusu ikiwa
Rais Goodluck Jonathan
aidhinishwe na chama
kugombea urais kwa mara
nyingine wakati kuna
wanasiasa wengine
wanaotaka kugombea urais.

Hii ni mara ya kwanza kwa
wabunge wa Nigeria
kurushiana ngumi bungeni.

15 WADAKWA BAADA YA KUSHUKIWA KUHUSIKA NA MATUKIO YA TINDIKALI

Mkuu wa polisi nchini
humo, Mussa Ali Mussa,
alidai kuwa baadhi ya
washukiwa wana uhusiano
na kundi la wapiganaji wa Al
Shabaab nchini Somalia.

Wiki jana kasisi wa kanisa
katoliki alishambuliwa kwa
kumwagiwa tindi kali katika
mji wa kale.


Shambulizi hilo linakuja
baada ya wasichana wawili
wa uingereza kushambuliwa
mwezi jana.

Kirstie Trup na Katie Gee,
wote wenye umri wa miaka
18, walimwagiwa tindi kali
wakiwa wanatembea mjini
humo.

Maafisa nchini Zanzibari,
wametangaza kumzawadi
mtu atayetoa taarifa kuhusu
shambulizi hilo.

Katika shambulizi
lililofanyika siku ya Ijumaa,
kasisi Joseph Anselmo
Mwangamba alimwagiwa
tindi kali alipokuwa
anaondoka kwenye duka la
huduma za internet katika
mji wa kale.


Shambulizi hilo ni la tano la
aina yake visiwani humo
tangu Novemba mwaka jana.

Bwana Mussa alisema kuwa
polisi walinasa mitungi
iliyokuwa na lita 29 za Tindikali wakati wa msako wao.


Kwa mujibu wa polisi,
washukiwa walikamatwa
wakiwa katika harakati za
kujiandaa kwa mapigano
kwengineko nje ya Tanzania.

Hadi sasa polisi
wanakamilisha uchunguzi
wao kabla ya kuwafungulia
mashtaka washukiwa watatu
waliowashambulia
wasichana wawili raia wa
Uingereza.

Hata hivyo haijulikani ikiwa
washukiwa hao 15
waliokamatwa
wamehusishwa na
shambulizi walilofanyiwa
wasichana hao wawili au
ikiwa ni wao
waliomshambulia kasisi
Mwangamba.

Visiwa vya Zanzibar hupokea
watalii wengi na wenyeji
wansema kuwa
mashambulizi dhidi ya raia
wa kigeni sio jambo la
kawaida.

CHADEMA YAMSHITAKI BALOZI WA CHINA NCHINI.

CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimemshtaki Balozi wa China nchini, Dk. Lu Youging kwa Umoja wa Mataifa (UN) kwa kujihusisha na siasa katuika majukwaa nchini kitendo ambacho ni hatari katika uhusiano wa diplomasia kati ya Tanzania na China.

Pia kimemshtaki kwa Serikali ya China na ya Tanzania kikidai kitendo cha balozi huyo ni kukiuka Mkataba wa Kidiplomasia wa Vienna (Vienna Convention of Diplomatic Reletions of 1964 ibara ya 41 (1-3) ambao unasimamia sheria za nchi wanachama w Umoja wa Mataifa.

Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana, Mkurugenzi wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa wa Chadema, Ezekiel Wenje alisema kitendo cha Balozi wa China, Dk. Youging kujihusisha na siasa za uenezi katika Chama cha Mapinduzi (CCM) ni kosa kubwa kimataifa na amepoteza sifa za kushikilia nafasi hiyo.

Wenje ambaye pia ni Mbunge wa Nyamagana (CHADEMA) na Waziri Kivuli wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa alisema balozi huyo amevunja sheria za Mkataba wa Vienna ambao unasimamia sheria za nchi wanachama wa UN.

Alisema kifungu alichovunja kinakataza Balozi yeyote kujihusisha na shughuli nyingine ambazo haziendani na majukumu ya uwakilishi wa nchi na nchi.

Wenje alisema balozi huyo anapaswa kufikishwa kwenye vyombo vya sheria kama inavyoelekezwa katika mkataba wa Vienna kwamba ikiwa balozi atakiuka mkataba huo atakosa sifa na ataondolewa kinga aliyonayo na kufikishwa kwenye vyombo vya sheria.
Alisema: "Jambo hili katika macho ya diplomasia, limevunja misingi na taratibu za ushirikiano wa kimataifa, wenye nia njema kwa wananchi wa pande mbili, baina ya nchi na nchi na katika ngazi ya serikali.

"Kwanza ni taswira ya dharau ya hali ya juu ambayo Balozi wa China ameamua kuwaonyesha Watanzania, hatuamini kwamba amepungukiwa na uwezo kiasi gani lakini anapaswa kukumbushwa aweze kuheshimu mipaka ya majukumu na wajibu wa diplomasia kwa nafsi ya balozi anapokuwa nchi ya ugenini.

"Balozi huyu anapaswa kukumbushwa kuwa uhusiano wa vyama, kwa maana ya Chama cha Kikomunisti cha China na CCM hata kama ungekuwa mzuri kiasi gani hauna mwingiliano na uhusiano wa Serikali ya Tanznaia na China.


"Hatutaki kuamini kuwa serikali ya China imemtuma Balozi Youquing kuja nchini kufanya kazi za ukatibu mwenezi wa CCM, tumesikitishwa heshima aliyopewa na Watu wa China ameidharau na amevuka mstari ambao hakuna mwanadiplomasia yeyote makini anayeheshimu uhusiano baina ya nchi na nchi angejaribu kufanya hivyo.

"Mstari aliouvuka balozi huyu umefafanuliwa wazi katika Mkataba wa Vienna Convention wa 1961 hasa katika kifungu cha 41(1) na 3, katika masuala yanayohusu uhusiano na kinga za mabalozi, kwamba ni marufuku kwa mwanadiplomasia yeyote kuingilia siasa za ndani za nchi mwenyeji wake.

"Chadema tunachukua hatua dhidi ya balozi huyo kujihusisha na chama cha siasa kwa kuvaa kofia ya CCM na kuelezea mambo ambayo hayakupaswa kusemwa kwenye majukwaa ya siasa.

"Kwanza tunaandika barua tatu, moja itakwenda Serikali ya China, ya pili itakwenda UN na nyingine itakwenda Serikali ya CCM ambayo ndiyo imempeleka huko mikoani.

"Barua hizo zitakuwa zinataka kueleza msimamo wa tukio hilo la balozi wa China nchini kujihusisha na siasa za majukwaani na kuvaa nguo za CCM, tunataka kujua hatua gani zitakazochukuliwa haraka kabla ya Chadema hatujapendekeza hatua za kuchukua.


"Hii ni hatari kwa balozi huyo kujiingiza kwenye siasa kitendo kinachosababisha kuhatarisha uhusiano uliopo kati ya wawekezaji wa China nchini kwa sababu wananchi wanaweza kutafsiri vibaya.

"Kwa mfano kuna maeneo ni ngome za Chadema na pale kuna wawekezaji wa China wanaweza kukataa kutoa ushirikiano wakidai ni wapo mlengwa wa CCM, pia ni hatari chama kingine kitapokuja kushika dola hakutakuwa na uhusiano mzuri.

"Tutaambatanisha ushahidi wa kutosha katika barua hizo ikiwa ni pamoja na picha za mnato na video, maneno aliyotamka kwenye mkutano, picha inayoonyesha akiwa amveaa sare za CCM na jinsi anavyocheza".

Picha zilizonyeshwa kwa waandishi wa habari zilionyesha Balozi Youging akiwa katika mikutano mbalimbali ya CCM maeneo ya Kishapu, Shinyanga na Kahama.

Katika picha hizo balozi huyo alionekana amevaa sare za CCM, akihutubia na kuendesha baiskeli akiwa na viongozi wa chama hicho akiwamo Katibu Mkuu, Abdulrahman Kinana, Katibu wa Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye.


Kwa mara ya kwanza balozi huyo aliibukia katika mkutano waCCM uliofanyika Shinyanga huku akishangiliwa na wananchi alipojaribu kuzungumza kisukuma.

CCM yazungumza
Wakati huohuo Chama Cha Mapinduzi (CCM) kimesema kimesikitishwa na hatua ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kumshutumu Balozi wa China, Dk. . Lu Youqing kwa kuhudhuria mikutano ya CCM.)

Kimewataka watanzania kupuuza madai ya Chadema kikisema hayana msingi kwa maendeleo ya taifa na watu wake.

Katibu wa Halmashauri Kuu ya CCM, Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye alikuwa akizungumza na waandishi wa habari katika mkutano uliofanyika katika Kijiji cha Mwandoya wilayani Meatu.


Alisema ni wazi Chadema kinataka kutumia matatizo ya wananchi kuyageuza agenda ya siasa.

Chadema haina budi itambue kuwa chama tawala cha China (CPC) kimekuwa na urafiki wa muda mrefu na CCM ikizingatia Balozi Dk. Lu pia ni kiongozi wa chama hicho.


Nape alisema hatua ya Balozi huyo kuhudhuria mkutano huo ni mafanikio ya ziara ya iliyofanywa na Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana China mapema mwaka huu.

"Balozi Dk. Lu amekuja kuleta ukombozi kwa watanzania hasa wa Kanda ya Ziwa kwa kuleta wawekezaji katika Mkoa wa Shinyanga kwa kujenga viwanda wa nyuzi, pamba, nyama, maji na ngozi ambako ajira zaidi ya 1000 zitapatikana.


"Watanzania wapuuze madai haya kwani si dhambi kwa Balozi wa China kuhudhuria mkutano wa CCM…urafiki wetu hakuanza leo ni wa muda mrefu katika historia ya nchi hizi mbili tangu na baada ya Uhuru,"alisema Nape.

Nape alisema CCM imepitaka kila eneo la yakiwamo majimbo yanayoongozwa na wapinzani na kubaini kuwapo changamoto nyingi.

Aliitaka Chadema kwenda kutatua haraka matatizo hayo badala ya kufanya mikutano Dar es Salaam pekee.


Wiki iliyopita akiwa mjini Shinyanga Balozi Dk. Lu Youqing, alihudhuria mikutano ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) na kusema kuwa hakuna chama imara kama hicho.

LITA 29 ZA TINDIKALI ZAKAMATWA ZANZIBAR

SIKU chache baada ya Padri wa Kanisa Katoliki, Parokia ya Machui, Anselm Mwang'amba kumwagiwa tindikali Zanzibar, Polisi visiwani hapa imekamata lita 29 za tindikalikwenye magaloni ya ujazo tofauti.


Kamishna Mkuu wa Jeshi la Polisi Zanzibar, Mussa Ali Mussa, alisemahayo jana alipozungumza na waandishi wa habari katika makao makuu ya Jeshi hilo, Kilimani mjinihapa. "Jeshi la Polisi limekamata watu 15kwa matukio mbalimbali... wapo tunaowahoji kuhusu mtandao wa kundi la Al-Shabaab, lakini wapo wanaohusishwa na matukio ya tindikali, hawa tunataka kujua wameipata wapi na nani amewauzia," alisema.

Akizungumzia tukio la mwishoni mwa wiki la Padri Mwang'amba kumwagiwa tindikali alisema: "Hivi sasa tunazungumza tukio la kumwagiwa tindikali Padri Mwang'amba Mlandege …upelelezi unaendelea na watu kadhaa tumewakamata ingawa ni mapemamno kutaja majina yao, lakini wakati ukifika tutawafikisha mahakamani.

"Akifafanua, Kamanda Mussa alisema Polisi inakabiliwa na changamoto kubwa ya vitendo vya hujuma kwa kutumia tindikali dhidiya watu mbalimbali Zanzibar. Kuhusu matukio mawili ya kumwagiwa tindikali kwa aliyekuwaMkurugenzi wa Manispaa, Rashid Ali Juma na Katibu wa Mufti, Shekhe Fadhil Soraga, alisema upelelezi wa shauri hilo umekamilika na jalada lipo kwa Mkurugenzi wa Mashitaka na Makosa ya Jinai (DPP). Shekhe Soraga alimwagiwa tindikali mwishoni mwa mwaka jana akiwa eneo la Magogoni Msumbiji, Mkoa wa Mjini Magharibi, wakati akiwa mazoezini.


Wakati akifanya mazoezi hayo, kwamujibu wa Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai, YusufIlembo, Shekhe Soraga alimwona mtu mwingine akifanya mazoezi mbele yake kabla ya kumgeukia nakummwagia tindikali iliyomjeruhi usoni na kifuani. Baadaye mtu aliyefanya unyama huo, alitoweka na kuelekea kusikojulikana. Mbali na Shekhe Soraga, mwanzoni mwa Agosti, walimu wawili wa kujitolea raia wa Uingereza, Kate Gee (18) na Krisdtie Trup (18), walijeruhiwa kwa tindikali, wakati wakienda kulausiku.Akizungumzia upelelezi wa tukio hilo, Kamanda Mussa alisema upelelezi uko hatua za mwisho kukamilika.

Kutokana na uhalifu huo, walimu hao walikimbizwa katika Hospitali ya Aga Khan Dar esSalaam kupewa huduma na baadaye walirudishwa kwao kwa matibabu zaidi, na mmoja wao anatarajiwa kupandikizwa ngozi.

Msako Kuongezeka kwa matukio hayo, kumesababisha Polisi Zanzibar kuanza operesheni kwa kushirikiana na Ofisi ya Mkemia Mkuu wa Serikali, kwa lengo la kupunguza matumizi holela ya tindikali.

Kamanda Mussa alisema operesheni hiyo ilianza Jumamosi na inalenga waagizaji, wasambazaji na watumiaji wa tindikali kwa ujumla.

Kwa usimamizi wake, Kamanda Mussa alisema msako maalumu umeanza katika maduka yanayouzatindikali ili kujua kama wanamiliki vibali halali vya biashara hiyo.

"Msako wa tindikali umeanza na sasa tumeanza ukaguzi wa maduka ya biashara hiyo kujua kama wana leseni ya kuiendesha," alisema. Pia Polisi imeanza kukutana na wadau kuangalia sheria ya kumiliki tindikali na matumizi yake ikiwamo kudhibiti tatizo hilo.

Al-Shabaab

Kati ya watuhumiwa 15 wa kikundi cha kigaidi cha al Shabaab wanaoshikiliwa Polisi, Kamanda Mussa alisema baadhi yao ambao hakuwataja majina, wanatuhumiwakuhusika na kikundi hicho na itikadi za imani kali za kidini.

Al-Shabaab, yenye asili yake Somalia, ina lengo la kutafsiri Sheria za Kiislamu katika namna yaimani kali ya kidini. Kikundi hicho kinadaiwa kupewa mahitaji ya kifedha kutoka vikundi vya kimataifa vya kigaidi, baadhi ya nchi na wananchi wa Somalia wanaoishi nje ya nchi yao.


Wanazuoni

Taarifa ya wanazuoni wa Kiislamu Tanzania (Hay-atul Ulamaa), iliyotolewa jana kwa vyombo vya habari, ilitaka Watanzania kurejea kwenye utamaduni wa karne nyingizilizopita, wa kuvumiliana na kushirikiana kulinda amani nchini. Mwenyekiti wa wanazuoni hao nchini, Shekhe Sulaiman Kilemile, alieleza katika taarifa hiyo, kwamba kitendo cha Padri Mwang`amba kumwagiwa tindikali,hakikubaliki na ni wajibu wao kukilaani kwa nguvu zote.

"Hivi ni vitendo vinavyoashiria chuki baina ya Watanzania wenyewe kwa wenyewe, ambavyo vikiachwa viendelee vitasababisha amani, utulivu na busara kutowekanchini," alieleza Shekhe Kilemile katika taarifa hiyo.


Taarifa hiyo pia ilikemea matumiziya silaha za moto kama ilivyotumika kumwua Padri Evarist Mushi, na kumjeruhi Katibu wa Jumuiya na Taasisi za Kiislamu, Shekhe Ponda Issa Ponda. "Matukio kama hayo yote ni hatari ambayo yanaweza kubadili sura nzuri ya Tanzania…

tunachukua nafasi kuwahadharisha viongozi wa dini na wengineo wasikurupuke kuelekeza tuhuma kwa kikundi kimoja dhidi ya kingine.

"Hivyo si halali tukio kama hilo kuhusishwa na udini, uzanzibari na utanganyikakabla ya kufanya uchunguzi na kupata dalili sahihi za kutosheleza,"alisema Shekhe Kilemile.

Askofu ShaoKatika hatua nyingine, Askofu wa Kanisa Katoliki, Jimbo la Zanzibar, Augustino Shao, amesema usalamawa viongozi wa dini umekuwa mdogo Zanzibar kutokana na kuendelea kupokea vitisho.


Askofu Shao alisema hayo Dar es Salaam, alipokwenda kumjulia hali Padri Mwang'amba, ambaye amelazwa Muhimbili. Padri Mwang'amba alisema Julai alipokeavitisho kutoka kwa vijana ambao hufanya mazoezi katika njia ambayo yeye hupita kwenda kuonawazee, lakini hana uhakika kama nivijana hao ndio wameshiriki uhalifu huo. "Siwezi kusema moja kwa moja kama ni hao vijana, maana walinitolea vitisho kuwa ipo siku watanifanyia kitu kibaya kwa kuwa nawasumbua wakati wanafanya mazoezi.


"Siwezi kusema moja kwamoja kuwa ni wao ama ni mwendelezo wa matukio ya watu wanaofanya uhalifu kwa kuwamwagia wenzao tindikali," alisema Padri Mwang'amba. Aliongeza kuwa baada ya kupokea vitisho hivyo alitoa taarifa Polisi nahali ikaendelea kuwa shwari, kwanihakupokea tena vitisho mpaka alipomwagiwa tindikali.

Aliziomba mamlaka husika kuhakikisha wahusika wanatafutwa na kuchukuliwa hatua, pia kudhibitimatukio ya aina hiyo ambayo yamekuwa yakijitokeza visiwani humo.

Askofu Shao alisema vitisho wanavyopata ni vingi zaidi, pia hawawezi kujua madhumuni na makusudi ya matukio hayo, kutokana na kuwepo kwa migongano tofauti ya kisiasa, kidinina mingineyo.

Alisema asilimia kubwa ya matukioyanayotokea yamekuwa yakilenga dini moja na kufanya viongozi wa dini kuhofia usalama wao. "Kwa tukio hili hii ni ishara tosha kwamba usalama wetu ni mdogo sana, sasa hivi tunaogopa hata kutembea," alisema.


-Habari leo

WANIGERIA SITA WADAKWA KANISANI

MSAKO wa wahamiaji haramu kupitia Operesheni Kimbunga inayoendelea nchini, umejikita kanisani kutokana na wahamiaji haramu sita wa Nigeria, kubainika wakijishughulisha na kazi za kichungaji.

Akizungumza jana kwa niaba ya Ofisa Uhamiaji Mkoa wa Dar es Salaam, Grace Hokororo, Naibu Kamishna wa Uhamiaji, Sylvanus Mwakasekele, alisema wahamiaji hao walikuwa katika Kanisa la Praise la Tabata. Kwa mujibu wa Mwakasekele, Uhamiaji walipata taarifa kutoka kwa raia wema kuhusu kuwapo kwawahamiaji hao kwenye Kanisa hilo.


Baada ya taarifa hiyo, alisema maofisa Uhamiaji walifika kanisani hapo juzi saa tano asubuhi na watu hao walipogundua, waliruka madirishani kukwepa mkono wa sheria na kukimbia wakitumia gari dogo aina ya Toyota Vitz. "Walipokimbia walikuwa sita, vijanawaliokwenda kufanya kazi hiyo waliwafuatilia na walipoona wako hatarini kukamatwa walitelekeza gari na kukimbia kwa miguu na kukamatwa wanne huku wawili wakitoroka," alisema Mwakasekele na kuongeza kuwa wako katika harakati za kusaka waliokimbia.


WahusikaAliwataja waliokamatwa na jinsi walivyoingia nchini, ni Moses Opara mwenye pasipoti namba A04809965, ambaye alikuwa kiongozi wa Kanisa hilo na ameishi nchini kwa miaka mitatu.James Ateli mwenye pasipoti namba A04665804, aliyeingia nchini kama mfanyabiashara na kuishi kwa mwaka mmoja. Pia Keneth Onyebuchi aliyeingia nchinikama mfanyabiashara tangu Januari na kudai kupoteza pasipoti yake alipoingia nchini na mwingineni Augustine Ndubilisi aliyeishi nchini mwaka mmoja. "Huyu Augustine anadai anaishi na familia ya mchumba wake Mtanzania aliyetajwa kwa jina la Caro Mdegela, msichana huyu tunamshikilia kwa kuhifadhi wahamiaji haramu," alisema.

Alisema baada ya kukamilika kwa mahojiano na watu hao, watafikishwa mahakamani kwa tuhuma za kuishi nchini bila kibali muda wowote kuanzia leo. Mwishoni mwa wiki, Uhamiaji ilikamata Mchungaji wa Kanisa la Kimataifa la Life Chande Chapel lililoko Sinza E na watu wengine sita.


Wamalawi Wakati huo huo, mamia ya raia wa Malawi jana walifurika kwenye ofisiza Uhamiaji Dar es Salaam kujiorodhesha. Gazeti hili lilifika katika ofisi hizo na kushuhudia umati wa vijana wa kike na kiume wakiwa na fomu walizojaza kuelezea uraia wao na anuani ya mahali wanakoishi nchini.Watu hao ambao walionekana kutulia huku wakizungumza kwa lugha yao, walikuwa kwenye misururu mirefu kusubiri zamu za kuingia kuhudumiwa.

"Tangu asubuhi tumeanza kuwaorodhesha na mpaka sasa (saanne kasoro asubuhi) mamia ya Wamalawi wameandikishwa na kurejea kwao," alisema Mwakasekele.Alisema katika uandikishaji huo, walitoa kipaumbele kwa wajawazito na wenye watoto, ili kuwapa nafasi ya kurejea kwao mapema.

"Kumekuwa na mwitiko mkubwa na hapa tumelazimika kuacha shughuli zingine za kila siku ili kuwahudumia wao, lengo ni tumalize kazi hii mapema. Lakini bado hatujafikia uamuzi wa lini uwe mwisho wa kuwaorodhesha," alisema.

Katika kukamilisha kazi hiyo, Uhamiaji imetenga vyumba vitano vyenye maofisa watatu kila kimoja, ambao kazi yao ni kuorodhesha Wamalawi hao ambao walikuwa wakiingia kwa makundi.

Chanzo:Habari leo

POLISI WAWILI WASHIKWA NA RISASI 3000

Polisi wawili wa
Musoma, Mkoa wa Mara
na Kibaha, Pwani
wanashikiliwa kwa
tuhuma za kukutwa
wakisafirisha risasi 3,000
kutoka Musoma kwenda
Dar es Salaam.

Wanaoshikiliwa kwa
tuhuma hizo ni aliyekuwa
mtunza chumba cha silaha
Kikosi cha FFU Musoma
na mwenzake mwenye
cheo cha Koplo Wilaya ya
Kibaha, Pwani. Inadaiwa
walikamatwa Juni 2,
mwaka huu saa 11:00
alfajiri.

Watuhumiwa
wanashikiliwa Kituo cha
Polisi Musoma na
wamefunguliwa jalada
MUS/RB/2465/013 wizi wa
risasi 1,056, wanasubiri
taratibu zingine za polisi.

Habari zinadai shehena
hiyo ilisafirishwa kwa
kutumia pikipiki hadi
Kituo cha Mabasi, lakini
polisi tayari walikuwa
wameweka mtego baada
ya kupata taarifa kuhusu
wizi huo.

Taarifa kutoka vyanzo
mbalimbali ikiwamo
wahusika wa basi na
nyumba moja ya kulala
wageni iliyopo jirani na
stendi, baadhi ya askari
waliovaa kiraia
walionekana maeneo hayo
mapema.

Kwa mujibu wa habari za
uhakika kutoka ndani ya
polisi, Koplo huyo
alikutwa na shehena hiyo
karibu na kituo cha
mabasi ya Kampuni ya
Mohammed Trans,
akijiandaa kuelekea Dar es
Salaam ambako
inasemekana wana wateja
wao.

Inadaiwa koplo huyo
aliomba ruhusa ya
ugonjwa kazini kwake na
kuitumia kusafiri hadi
Musoma kuchukua mzigo
huo, inadaiwa biashara
yao hiyo ni ya muda
mrefu na wana mtandao
na watuwanaojihusisha na
uhalifu.

Mtandao huo unadaiwa
kuwagusa baadhi ya polisi
Mkoa wa Tarime na
Rorya, ambao huwauzia
watu wanaojihusisha na
uhalifu wa kutumia silaha.

Kamanda wa Polisi Mkoa
wa Mara, Absalom
Mwakyoma alipotafutwa
kwa simu zake za
mkononi licha ya kuitwa,
hazikupokewa.

Hata hivyo, aliomba
atumiwe ujumbe, licha ya
kupelekewa huo ujumbe,
hakujibu ingawa taarifa
zinadai ameanza likizo ya
kustaafu hivi karibuni.
Mkuu wa Upelelezi Mkoa
wa Mara, Jafari
Mohammed alipoulizwa
kuhusu tukio hilo,
alikanusha kufahamu
suala hilo huku akigeuka
kuwa mkali kwa
mwandishi.

"Hilo mimi silijui, nani
kakwambia wewe… askari
kukutwa na risasi mfukoni
ni jambo la kawaida
huenda ni uzembe
tunamshughulikia kwa
uzembe," alisema.

Chanzo:Mwananchi

LUKUVI KUFANYA ZIARA KATAVI, MBEYA NA RUKWA

Waziri wa Nchi Ofisi ya
Waziri Mkuu (Sera
Uratibu na Bunge) Mhe.
William V. Lukuvi (MB)
kuanza ziara rasmi leo
tarehe 16 hadi 19
Septemba, 2013 katika
Mikoa ya Katavi, Rukwa
na Mbeya.

Katika ziara hiyo Waziri
Lukuvi anatarajiwa
kutembelea baadhi ya
vituo vya Ununuzi wa
Mahindi kwa ajili ya
kuhifadhiwa kwenye
Maghala ya National
Food Reserve Agency
(NFRA), Maghala ya
NFRA ya kuhifadhi
chakula, atapokea
taarifa ya Utekelezaji
kuhusu Mradi wa
Miundo Mbinu ya
Masoko na Uongezaji wa
Thamani (MIVARF)
katika maeneo
yanayotekeleza mradi
huu.


Vilevile Mhe. Lukuvi
atapokea Taarifa ya
Utekelezaji wa Miradi
yote ya Maendeleo
ikiwemo Miradi
itokanayo na ahadi za
Mhe. Rais na Miradi
itokanayo na Ilani ya
Chama Tawala pamoja
na Miradi
inayofadhiliwa na
Taasisi mbalimbali
Mkoani humo.

MAUWAJI KATIKA KAMBI YA JESHI WASHINGTON DC

Mtu aliyewaua watu 12
katika kambi ya kijeshi
nchini Marekani na kisha
mwenyewe kuuawa, katika
makabiliano na polisi,
ametajwa kuwa mwanajeshi
wa zamaji wa jeshi la
wanamaji.

Aaron Alexis, 34, kutoka Fort
Worth, Texas, aliuawa na
polisi baada ya kuvamia
kambi hiyo na kuwaua watu
kiholela , mjini Washington
DC.

Watu wengine wanane
walijeruhiwa kwenye
uvamizi huo ulioanza
mapema asubuhi mnamo
Jumatatu.


Rais Barack Obama
aliamuru bendera
kupeperushwa nusu
mlingoti katika Ikilu ya
White House na Capitol Hill.

Alisema anaomboleza kwa
sababu ya mauaji mengine
ya halaiki na kulaani
kitendo hicho cha uoga.

Haijulikani kwa nini Aaron
Alexis aliamua kufanya
shambulizi hilo na kuwaua
watu kati ya umri wa miaka
46-73.

Awali polisi walichukua
hatua baada ya ripoti za
watu wengine kujihami
wakishirikiana na Alexis,
lakini baada ya msako mkali
wakasema kuwa hakuna
dalili kwamba Alexis alikuwa
na wenzake..

Valerie Parlave wa shirika la
ujasusi la FBI alisema kuwa
Alexis, aliyekuwa ameajiriwa
na mwanakandarasi
aliyekuwa anafanya kazi
kwenye mtandao wa
internet wa FBI, alikuwa na
pasi ya kuingia kwenye eneo
hilo.

POLISI ZANZIBAR WACHARUKA

SIKU mbili baada ya Padri
wa Kanisa Katoliki Parokia
ya Cheju, Mkoa wa Kusini
Unguja, Zanzibar, Joseph
Mwang'amba kumwagiwa
tindikali na watu
wasiofahamika, Jeshi la
Polisi li metoa tamko la
kuwasaka wahusika usiku
na mchana.


Padri Mwang'amba
ambaye amelazwa katika
Hospitali ya Taifa
Muhimbili (MNH), Dar es
Salaam, akipatiwa
matibabu, alipatwa na
tukio hilo mwishoni mwa
wiki wakati akitoka
kwenye duka linalotoa hu
duma ya mawasiliano ya
mtandao(intaneti), lililopo
eneo la Mlandege,wilayani
Ung uja.


Taarifa iliyotolewa Dar
es Salaam jana na
Msemaji wa Jeshi la Polisi
nchini, Advera Senso, alisema kutokana na
ongezeko la vitendo hivyo,
jeshi hilo, Mkemia Mkuu
wa Serikali na kikosi
Maalumu cha kuzuia
uchochezi na ugaidi,
wamejipanga kufanya
operesheni maalumu.

Operesheni hiyo ni ile ya
kuwafuatilia watu wote
wanaoingiza , kusambaza
na kuuza vimiminika vya
tindikali kama
wanazingatia sheria
zilizowekwa dhidi ya
vimiminika hivyo.

"Yeyote ambaye
itabainika kwenda
kinyume hatua za kisheria
zitachukuliwa dhidi yake
na k ufikishwa
mahakamani, tutaendelea
kuwasaka watu
wanaofanya vitendo hivi,
tunaomba wananchi
wenye taarifa nao, wazitoe
na zitakuwa siri,"alisema.

Juzi Padri Mwa ng 'amba
alitembelewa hospitali na
Rais wa Zanzibar, Dkt.Ali
Mohamed Shein na
kumwe leza kuwa, miezi
mitatu iliyopita alitishiwa
kuuawa. Katika tukio
lililomkuta mwishoni m
wa wiki, Padri
Mwang'amba alijeruhiwa
usoni, mikononi na
kifuani.

MASHAHIDI WANNE WAJITOA KESI YA KENYA HUKO ICC

Kiongozi wa mashtaka katika
mahakama ya kimataifa ya
jinai ICC, Fatou Bensouda,
amepata pigo jengine baada
ya mashahidi wengine
wanne kujiondoa katika kesi
dhidi ya Naibu Rais wa
Kenya William Ruto na
mshtakiwa mwenzake
Joshua Arap Sang.


Hili limetokesa siku moja tu
kabla ya Bensouda kuanza
kuwasilisha mashahidi
mbele ya mahakama siku ya
Jumanne kesi dhidi ya Ruto
itakapoanza tena.

Mashahidi hao
wanajumuisha manusura wa
moto ulioteketeza kanisa la
Kiambaa mkoa wa Rift
Valley na kusababisha vifo
vya watu 35 wakati wa
ghasia za baada ya
uchaguzi mkuu nchini Kenya
mwaka 2007-2008
Bwana Ruto anatuhumiwa
kwa kuchochea ghasia ili
kujinufaisha kisiasa wakati
Sang akidaiwa kumsaidia
Ruto kuafikia malengo yake
kwa kutumia kituo cha Redio
alichokuwa anafanyia kazi
wakati wa ghasia hizo.


Hii sio mara ya kwanza kwa
mashahidi kujiondoa katika
kesi dhidi ya washukiwa
hawa. Wiki mbili zilizopita
mashahidi wengine wawili
walijitokeza nchini Kenya
wakidai kuwa
wanalazimishwa na upande
wa Mashtaka kutoa ushahidi
wa uongo dhidi ya wawili
hao.

Wadadisi wanasema kuwa
kujiondoa kwa mashahidi
katika kesi hii bila shaka
kutaathiri uwezo wa
kiongozi wa Mashtaka Fatou
Bensouda lakini amewahi
kusikika akisema kuwa kwa
mashahidi kujiondoa katika
kesi yake dhidi ya Ruto na
Sang sio hoja.


Kesi dhidi ya Ruto
iliakhirishwa wiki jana
baada ya upande wa
mashtaka kusema kuwa
hawajakuwa tayari
kuwasilisha mashahidi wao
na hivyo kupewa muda na
mahakama hadi siku ya
Jumanne wiki hii.

RAIA WA RWANDA WAPIGA KURA KUCHAGUA WABUNGE

Raia milioni sita wa Rwanda
waliosajiliwa kupiga kura,
hii leo wanawachagua
wabunge katika mfumo wa
vyama vingi vya kisiasa.


Rwanda inasifika sana kwa
kuwa na wanamama wengi
kwenye nyadhifa za uongozi
wa kitaifa.

Uchaguzi huu usio na
upinzani mkubwa ni kama
kupiga muhuri tu uongozi
wa chama cha RPF chake
Rais Paul Kagame ambacho
kimekuwa uongozini tangu
kumalizika kwa mauaji ya
Kimbari mwaka 1994.

Kiongozi wa Chama rasmi
cha upinzani FDU, Victoire
Ingabire yuko jela na
wafuasi wake wanasema
kuwa serikali imefanya
mazingira kuwa magumu
sana kwao hata kusajiliwa
rasmi kama chama cha
kisiasa.


Kwa sababu ya mfumo wa
kuhakikisha kuwa wanawake
wanawakilishwa vyema
katika nyadhifa za kisiasa,
Rwanda ndiyo nchi pekee
duniani yenye wanawake
wengi bungeni.


Inasemekana kuwa wapiga
kura wengi huenda
wakajitokeza licha ya kuwa
kampeini za uchaguzi
hazikufanywa kwa kishindo
pamoja na kukosekana kwa
upinzani mkubwa kwa
chama cha RPF.

Shughuli ya kupiga kura
ilionekana kuwa tulivu ,
foleni zikiwa zimepangwa
vyema huku vipaza sauti
vikisikika kuwaambia
wananchi kutosahahu kadi
zao za kujitambulisha
wakati wakienda kupiga
kura.

Mwishoni mwa wiki, tukio
pekee la kutishia usalama
lililoripotiwa ni shambulizi
la maguruneti, katika soko
moja mjini Kigali , mji
ambao unasifika kwa
usalama wake barani
Afrikia.


Tangu kutokea kwa
shambulizi hilo, hakuna
mtu yeyote aliyekiri
kuhusika nalo, lakini serikali
ililaumu waasi wenye
uhusiano na kundi la waasi
la (FDLR), ambao huendesha
harakati zao maeneo ya
mpakani na Jamuhuri ya
kidemokrasia ya Congo
Kundi hilo linajumuisha
waasi wa zamani wa kihutu
wanaolaumiwa kwa mauaji
ya Kimbari ya mwaka 1994
ingawa waliondoshwa na
waliokuwa wanachama wa
waliokuwa wanajeshi waasi
wa RPF.

KUMI BORA AFRIKA WAPANGWA

MABINGWA wa soka wa
Afrika, Nigeria
wamepangwa na timu
isiyopewa nafasi sana,
Ethiopia, wakati Ghana
imekabidhiwa shughuli
pevu mbele ya Misri katika
mechi za mchujo za
kusaka tiketi ya fainali za
Kombe la Dunia
zitakazofanyika mwakani
Brazil.

Droo ya mechi hizo
imefanyika muda mfupi
uliopita
Ivory Coast vs Senegal,
Ethiopia vs Nigeria,
Tunisia vs Cameroon,
Ghana vs Misri, Burkina
Faso vs Algeria. Mechi za
kwanza za mchujo huo
zinatarajia kufanyika kati
ya Oktoba 11 na 15, wakati
marudiano zitakuwa kati
ya Novemba 15 na 19
mwaka huu.

UNHCR - TANZANIA HAIJAWAFUKUZA WAKIMBIZI

Shirika la Umoja wa Mataifa
la Kuhudumia Wakimbizi,
UNHCR, ofisi ya Tanzania
limekanusha taarifa katika
baadhi ya vyombo vya
habari kwamba, Tanzania
imewarejesha nyumbani
kwa nguvu, wakimbizi
25,000 wa Burundi mwezi
mmoja uliopita.
)
Vilevile serikali ya Tanzania
imesema, taarifa hiyo ni ya
uzushi ambayo haina ukweli
wowote na yenye nia ya
kuichafulia jina nchi ya
Tanzania ambayo kwa muda
mrefu imekuwa kimbilio na
makaazi ya wakimbizi wengi
kutoka nchi mbalimbali
hasa za Ukanda wa Maziwa
Makuu.

Akizungumza na BBC,
Mwakilishi Mkazi wa UNHCR
nchini Tanzania , Bi. Joyce
Mends Cole, amesema,
amewasiliana na mwakilishi
wa shirika hilo nchini
Burundi ambaye
amethibitisha kwamba
hakuna wakimbizi wa nchi
hiyo waliorejeshwa kutoka
Tanzania.

Bi. Joyce amebainisha kuwa,
tatizo lililopo ni
kuchanganywa kwa maneno
"Wakimbizi" na "Wahamiaji
Haramu".

Amefafanua kwamba, katika
operesheni inayoendelea
kwa sasa nchini Tanzania,
ya kuwasaka wahamiaji
haramu huenda baadhi ya
wakimbizi waliosalia
wamekamatwa kimakosa.

Hata hivyo Waziri wa
Mambo ya Ndani wa
Tanzania Dk. Emmanuel
Nchimbi, alimuhakikishia
kuwa operesheni hiyo
inafanyika kwa umakini
mkubwa na kwa kuzingatia
mikataba ya kimataifa ya
haki za uhamiaji.

Katika hatua nyingine,
serikali ya Tanzania kupitia
Msemaji wa Wizara ya
Mambo ya Ndani, Bw. Isaack
Nantanga, imesema hakuna
mkimbizi yeyote
aliyerejeshwa Burundi kwa
hiari wala kwa nguvu katika
kipindi kilichotajwa.

Bw. Nantanga amebainisha
kuwa, wakimbizi wote
264,000 ambao Tanzania
imewapatia "Hifadhi ya
Ukimbizi" wapo na
wanaendelea kuishi kwenye
kambi na makazi ya
wakimbizi yaliyopo katika
mikoa ya Tabora, Kigoma,
Katavi na Tanga.

Wakimbizi hao wanatoka
katika nchi za Burundi,
Jamhuri ya Kidemokrasia ya
Kongo, DRC, na Somalia.

Hadi Septemba nne mwaka
huu, zaidi ya "Wahamiaji
Haramu" 27,000
wamerejeshwa makwao kwa
hiari ambao walikuwa
wakiishi nchini Tanzania
kinyume cha sheria katika
mikoa ya Rukwa, Kigoma na
Kagera

PADRI AMWAGIWA TINDIKALI HUKO ZANZIBAR

Polisi huko visiwani
Zanzibar wanachunguza
tukio la kasisi wa kanisa
katoliki kushambuliwa kwa
tindikali.

Imeelezwa kuwa Kasisi huyo
Anselmo Mwang'amba,
alimwagiwa tindikali akitoka
mgahawa mmoja wa
kutumia mtandao mjini
Zanzibar. Tukio hilo
linatokea ndani ya mwezi
mmoja tangu wasichana
wawili wa kiingereza
kushambuliwa.

Hili ni janga jingine kwa
Zanzibar ambayo imekuwa
ikizongwa na matukio ya
aina hii kwa muda sasa.

Mkurugenzi wa upelelezi wa
Zanzibar, Yusufu Ilembo
ameieleza kuwa bado
hawajakamata mtu yoyote
kuhusika na tukio hilo
ingawa amethibitisha kuwa
uchunguzi tayari umeanza.

Ameeleza kuwa Kasisi
Mwang'amba aliungua
usoni na mabegani na
kwamba anaendelea
kutibiwa.

Katika miaka ya karibuni
Zanzibar imekabiliwa na
mikasa ya watu
kushambuliwa hivi na kuzua
hisia kuwa chuki za kidini.

Mapema mwaka huu kasisi
mwingine wa kanisa katoliki
alishambuliwa kwa risasi na
kuuawa.

Mwezi uliopita Zanzibar
ilitikisika kutokana na
wasichana wawili wangereza
kushambuliwa kwa tindikali
na watu wasiojulikana.

Kiongozi mmoja wa dini ya
kiislamu pia alimwagiwa
tindikali na watu
wasiojulikana.

PICHA YA SIKU

Kutoka kwa kipanya: Kizazi cha miadarati

MSHUKIWA WA MAUWAJI YA KIMBARI AACHIWA HURU

Mahakama moja nchini
Ufaransa imeamuru
kuachiliwa kwa aliyekuwa
Kanali wa jeshi la Rwanda ,
anayesakwa na taifa hilo
kwa kuhusika katika mauaji
ya kimbari ya mwaka 1994
nchini humo.
Rwanda iliwasilisha ombi la
kutaka Kanali huyo Laurent
Serubuga, wa kabila la
Hutu, na ambaye alihudumu
kama naibu mkuu wa
majeshi kurejeshwa nchini
humo.

Kanali Serubuga mwenye
umri wa miaka 77,
alikamatwa mwezi Julai
Kaskazini mwa Ufaransa
baada ya Rwanda kutoa
kibali cha kumkamata.

Takriban watu 800,000
wengi wao wakiwa wa kabila
la Tutsi, waliuawa na
wahutu ambao ni wengi kwa
idadi nchini Rwanda mnamo
mwaka 1994.

Mwanawe Serubuga alikuwa
mahakamani kushuhudia
kesi hiyo. Wakati jaji akitoa
uamuzi wake, alisema kuwa
wameridhishwa na uamuzi
wa kumwachilia huru
babake.

"tulirajaria kesi ya kisiasa.
Uongo wa Rwanda
haujasikika mbele ya
mahakama hii," alinukuliwa
akisema na shirika la habari
la AFP.

Mahakama iligundua kuwa
wakati wa mauaji ya
kimbari, uhalifu wa mauaji
ya halaiki na uhalifu dhidi
ya binadamu haungeweza
kuadhibiwa chini ya sheria
ya Rwanda, kwa hivyo,
bwana Serubuga hangeweza
kuchukuliwa hatua zozote
kwa makosa ambayo
hayakuwa na adhabu.

Sheria za Ufaransa,
haziruhusu mshukiwa au
mhalifu kurejeshwa kwao
hasa ambapo mshukiwa ana
wasiwasi ikiwa haki zake
zinaweza kulindwa, alisema
wakili wa Bwana Serubuga.

Wakili aliyekuwa anatetea
maslahi ya Rwanda alisema
kuwa hakushangazwa na
uamuzi huo kwani Ufaransa
mara kwa mara imekataa
kuwarejesha washukiwa wa
mauaji hayo nchini Rwanda
ili wakabiliwe na sheria.

UN YAIKOSOA TANZANIA KWA KUWARUDISHA MAKWAO WAHAMIAJI

Umoja wa Mataifa umesema
kuwa takriban wahamiaji
haramu elfu 25 kutoka
Burundi wameondoshwa
Tanzania kwa nguvu katika
mwezi mmoja uliopita.

Afisa wa shirika la Umoja
wa Mataifa la kuwahudumia
wakimbizi UNHCR amesema
malori yanayowasafirisha
warundi yamekuwa yakivuka
mpaka kila siku , huku
wahamiaji haramu wengi
wakikosa mahitaji muhimu
kama vile maji na chakula
Katika wiki za hivi karibuni,
Tanzania imekuwa
ikiwarejesha makwao kwa
nguvu wale walioelezwa
wahamiaji haramu kutoka
Burundi, Rwanda na
Jamuhuri ya Kidemokrasi ya
Congo.

Kwa miaka mingi Tanzania
iliwahifadhi mamilioni ya
wakimbizi waliokuwa
wakiyakimbia mapigano
katika nchi jirani.

Takriban watu milioni moja
walitoroka kutoka Burundi
na kuingia Tanzania wakati
wa mgogoro wa wenyewe
kwa wenyewe wakati vita
vilipozuka mwaka 1993.

Wengi walirejea kwa hiari
wakati amani ilipopatikana
mwaka 2006.

Nchi hiyo imekuwa makao
kwa mamilioni ya wakimbizi
katika kipindi cha zaidi ya
miaka kumi iliyopita
kutokana na migogoro
katika eneo la maziwa
makuu.

Maafisa wa Tanzania sasa
wameanza kutekeleza amri
ya kuwaondoa kwa nguvu
wale wanaodaiwa kuwa
wahamiaji haramu kutoka
Burundi, Rwanda, na
Jamuhuri ya kidemokrasia
ya Congo.

Shughuli hii imetokea
wakati mmoja na mgogoro
wa kidiplomasia kati ya
Tanzania na Rwanda
ambayo imekuwa ikikanusha
madai ya kuchochea vurugu
katika Jamhuri ya
Kidemokrasia ya Congo.

Mgogoro ndani ya Jamhuri
ya kidemokrasia ya Congo
nao unaendelea kuchochea
idadi ya wakimbizi
wanaotoroka vita na kuingia
katika nchi jirani.

MTANZANIA MWINGINE ADAKWA DUBAI

Kwa wiki iliyopita, tuilipekenyua maeneo yote muhimu na kukumbana na mambo mapya kuhusu habari za‘unga’huku taarifa zikionesha kuwa, hali katika viwanja vye ndege duniani kote ni tete. Tuhuma za Watanzania kukamatwa au kufariki kutokana na madawa ya kulevya bado zinaendelea kuongezeka. Kwenye hii thread kuna tuhuma tatu zinazowahusu Watanzania, mmoja inadaiwa amefariki baada ya mzigo kupasukia tumboni na wengine wawili wanadaiwa kukamatwa kwenye nchi za watu wakiwa na mzigo.
Mtanzania afia Dubai akiwa na unga tumboni
Habari zilizotufikia juzi zinadai kwamba Mtanzania aliyejulikana kwa jina moja la Chambuso amefariki dunia katika Jiji la Dubai, Falme za Kiarabu kutokana na unga aliokuwa ameubeba tumboni kuyeyuka kabla ya kufika kwenye kituo husika. Habari za uhakika kutoka chanzo chetu jijini Dar zinasema kuwa marehemu Chambuso alikuwa na‘mlinzi’wake ndani ya Ndege ya Emirate huku akiwa hamjui.
Ikazidi kudaiwa kuwa, baada ya kushuka jijini Dubai, hali ya Chambuso ilianza kubadilika akilalamikia zaidi maumivu ya tumbo, ndipo‘mlinzi’huyo alipombeba na kumpeleka hospitali (haikutajwa jina).“Baada ya kufariki dunia, jamaa (mlinzi) alijiweka mbele akitaka kufanya maarifa kwa madaktari ili tumbo la jamaa lipasuliwe atoe mzigo. Akashtukiwa, akakimbia na mpaka sasa maiti hiyo iko chini ya ulinzi wa serikali,”kilisema chanzo hicho.
Mtanzania aliyekamatwa na unga China
Tukiachana na kifo cha Chambuso huko Dubai, Septemba 2, mwaka huu zilitufikia taarifa kwamba, mchumba wa mwigizaji Pendo Mushi‘Pendo wa Maisha Plus’aliyejulikana kwa jina moja la Tasha amedakwa na unga nchini China. Kwa mujibu wa taarifa hizo, Tasha alikamatwa kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Beijing nchini humo akiwa na unga aina ya heroin (kiasi na thamani hakikutajwa).
Ili kupata uhakika wa madai hayo, juzi Ijumaa Wikienda lilimtafuta Pendo kwa njia ya simu ya mkononi na kumuuliza kuhusu madai hayo ambapo alikiri.“Yeah, ishu ni kweli. Mimi nilizipata hizo taarifa kutoka kule nikawaambia ndugu zake. Kwa mujibu wa mtu wake aliyekuwa naye kule (China) jamaa (Tasha) ameshapandishwa kortini,”alisema Pendo huku akisema uchumba wake na Tasha ulishakufa.
Msanii wa Bongo Movie adaiwa kufungwa Brazil
Wiki mbili sasa, mapaparazi wetu wamekuwa wakifuatilia kwa undani kuhusu kusambaa kwa madai kwamba, staa wa filamu za Kibongo, Aisha Bui eti kafungwa miaka 5 jela katika gereza moja nchini Brazil baada ya kukamatwa na madawa ya kulevya kwenye kibegi. Kwa mujibu wa madai ya habari hizo, eti Aisha alidakwa kwenye uwanja wa ndege wa jijini Brasilia akirejea Bongo kupitia Dubai.
Septemba 2 na 5, mwaka huu, waandishi wetu walifika nyumbani kwa baba wa Aisha, Kigamboni, Dar kutaka kujua ukweli. Septemba 2, mtu aliyekutwa nyumbani hapo alisema Aisha yupo Brazil lakini hakuna mawasiliano naye na alikwenda siku chache kabla ya Mfungo wa Mwezi Mtukufu wa Ramadhan, Julai mwaka huu. Septemba 5, hakukutwa mtu ila majirani walielekeza eneo analopatikana mzee huyo ambapo ni ufukweni. Hata hivyo, sehemu hiyo hakupatikana na waandiishi waliacha namba zao za simu.
Jioni, mzee Bui alizipata namba zilizoachwa, na saa 9:00 usiku wa kuamkia Septemba 6 alimpigia simu mwandishi wetu na kumvurumishia matusi huku akisema akome kumfuatafuata akidai yeye hana mawasiliano na binti yake tangu mwaka 2007. Mzee huyo alikwenda mbele zaidi kwa kutuma ujumbe mfupi wa simu (SMS) kwenye simu ya paparazi akitumia lugha ya Kiarabu ambapo kwa mujibu wa wataalam wa lugha hiyo ni dua ya kumwombea mabaya mwandishi huyo.
Mnaigeria aliyekamatwa na unga alitahadharishwa na wenyeji wake magomeni asipitie JNIA.
Anthonie Ojo, raia wa Nigeria aliyekamatwa Septemba 4, mwaka huu kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere, Dar (JNIA), akijaribu kusafirisha kete 99 za unga na ndege ya Shirika la Ethiopian Airways alinaswa. Mwanamke huyo aliyevalia baibui akidai anakwenda kuhiji Maka, anadaiwa aliununua mzigo huo Magomeni-Mapipa jijini Dar. Aliziweka kete hizo kwenye makopo yaliyokuwa na poda ya Johnson.
Kwa mujibu wa uchunguzi wetu, wenyeji waliomuuzia unga mwanamke huyo walimtahadharisha kuhusu hali ya ulinzi iliyopo sasa JNIA hasa baada ya Waziri wa Uchukuzi, Dk. Harrison Mwakyembe kushikia bango udhibiti wa unga lakini mtuhumiwa huyo alidaiwa kusema atapita kwa anavyojua yeye.
Nzowa azungumzia
Ili kwenda mbele zaidi, mapaparazi wetu walikwenda ofisini kwa Kamanda wa Kikosi Maalum cha Kupambana na Kudhibiti Madawa ya Kulevya Tanzania, Godfrey Nzowa ili kutaka kujua kama amesikia lolote kuhusu Aisha Bui. Alisema:"Eee, kuna habari kama hiyo lakini si rasmi kwangu, bado nafuatilia Brazil ikiwa tayari nitawajulisha tu."Tulimtafuta Aisha kwenye mitandao, hasa Facebook, Instagram na Twitter bila mafanikio. Tumemwachia ujumbe kwa kuamini kwamba akirudi hewani ataukuta na kujibu lakini wapi!

RAIS KIKWETE AMALIZA ZIARA YAKE JIJINI MWANZA

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dokta Jakaya Kikwete ameitaka mikoa nchini kuwa na mipango ya uanzishwaji viwanda jambo ambalo litasaidia kuinua maisha ya wananchi na kuchangia maendeleo.

Kauli hiyo ya Rais ameitoa katika majumuisho ya ziara yake ya siku sita mkoani Mwanza baada ya kutembelea wilaya zote na kujionea shughuli mbalimbali za maendeleo.

Mwanza unatajwa kuwa mkoa wa pili Tanzania katika kuchangia pato la Taifa kwa mwaka ambapo unachangia zaidi ya asilimia 12 ukitanguliwa na Dar es Salaam.

Rais anashangaa kuona mkoa huu hauna mipango ya kuongeza viwanda kutokana na ukweli kuwa wakazi wa mijini wanategemea ajira katika kuendesha maisha yao.

Mikoa ya Kanda ya Ziwa ni maarufukwa kulima zao la Pamba licha ya zao hili nchini kushuka thamani katika soko la kimataifa hivi karibuni.

Mfumo wa kilimo cha Mkataba unasuasua, Rais anawanyooshea kidole baadhi ya wanunuzi kwa kuwa kikwazo katika kuboresha kilimo hicho kwa kiasi kikubwa.

Katika maelezo yake Mheshimiwa Rais anahimiza kilimo cha matunda, mboga mboga na Maua kwenye ukanda huu wa ziwa hatua itakayowezesha kuwa na masoko katika nchi za Ulaya.

Katika ziara yake mkoani Mwanza Rais Kikwete amezindua na kuwekamawe ya msingi kwenye miradi mbalimbali ikiwemo ya nishati ya umeme, maji, afya na kilimo.

NDUGU WAKWARUZANA KUGOMBEA MWILI WA MAREHEMU HUKO ITENKA

NDUGU wamefarakana
wakigombea mwili wa
marehemu, Philipo
Sigare (32) aliyekuwa
Ofisa Mtendaji wa Kijiji
cha Itenka. Hali hiyo
imesababisha msiba
kuwekwa sehemu mbili
tofauti kwa wakati
mmoja mjini Mpanda
Mkoa wa Katavi. Ofisa
huyo alifariki
Septemba 9 , mwaka
huu.

Kamanda wa Polisi wa
Mkoa wa Katavi,
Dhahiri Kidavashari
alisema ilibidi aingilie
kati, kunusuru mzozo
huo katika chumba cha
kuhifadhia maiti,
ambako kila upande
ulitaka uchukue mwili.

Mzozo huo ulivuta
hisia za wakazi mjini
Mpanda baada ya
pande zinazopingana
kwenda katika chumba
cha kuhifadhia maiti
katika Hospitali ya
Wilaya mjini Mpanda,
ambako mwili
umehifadhiwa,
wakitaka kuuchukua
kwenda kuuzika.

“Nimewaasa
wanafamilia hao kama
watashindwa
kuelewana, basi
waende mahakamani
ambako ufumbuzi wa
mgogoro huo
utapatikana,” alisema
Kamanda Kidavashari.

Baadhi ya ndugu
walidai maziko
yameshindikana,
kutokana na mzozo
huo na kwamba baadhi
yao wanajipanga
kupeleka shauri hilo
mahakamani ili haki
iweze kutendeka.

“Pande mbili zilikutana
hapo hospitalini na
kuanza kutupiana
maneno makali ya
kashfa, wakidai kuwa
ndugu wa upande wa
Thobias wanataka
kuchukua msiba ili
waweze kula pesa za
rambirambi,” alisema
mmoja wa mashuhuda.

Chanzo cha mzozo huo
inadaiwa ni kutokana
na baadhi ya ndugu
kutaka maziko yasubiri
kaka mkubwa wa
marehemu, Mathias
Sigareti ambaye ni
Mwalimu wa Shule ya
Msingi kijijini Kasanga
atakapowasili huku
wengine wakipinga.

Miongoni mwa ndugu
waliopinga hilo, ni
Thobias Kizimzuri
aliyeamua kuweka
msiba nyumbani kwake
katika Mtaa wa
Makanyagio mjini
Mpanda, akidai yeye
ndiye aliyekuwa
akimhudumia mgonjwa
wakati wote alipokuwa
amelazwa hospitalini
kwa matibabu.

Wakati huo huo dada
yake Thobias, aitwaye
Magreti Francis
alipinga uamuzi wa
kaka yake, pia akaamua
msiba uwe nyumbani
kwake Mtaa wa
Majengo.

Kutokana na
mkanganyiko huo,
waombolezaji
walijikuta
wakigawanyika katika
nyumba hizo huku kila
upande ukifanya
maandalizi ya maziko.

Hata baada ya kaka
mkubwa aliyekuwa
akisubiriwa kuwasili,
iliamriwa msiba ubaki
kwa dada yao Magreth,
Mtaa wa Majengo,
lakini uamuzi huo
ulipingwa.

Kila upande uliendelea
na taratibu za
kuchimba kaburi katika
maeneo tofauti kwenye
makaburi ya Mwangaza
mjini Mpanda, kabla ya
kwenda chumba cha
maiti kuchukua mwili.

Hali hiyo ilisababisha
mzozo mkali ambao
Kamanda wa Polisi
akiwa na kundi la
askari, walifika na
kuingilia kati.

SADC WAMUONYA KAGAME

MZOZO wa kidiplomasia alioibua Rais wa Rwanda, Paul Kagame kwa Rais Jakaya Kikwete, sasa unaonekana kuchukua mwelekeo mpya, baada ya Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC), kumuonya kiongozi huyo kuacha mara moja fikra zozote mbaya dhidi ya Tanzania, MTANZANIA Jumatano limedokezwa. Habari za uhakika na za kuaminika kutoka miongoni mwa viongozi wa juu wa SADC na maofisa wa Serikali, waliokuwa katika ujumbe wa Rais Jakaya Kikwete aliyekuwa akihudhuria Mkutano wa viongozi wa Maziwa Makuu huko Uganda hivi karibuni, zinaeleza kuwa tayari Jumuiya hiyo imekwisha mpatia ujumbe huo mmoja wa mawaziri aliyekuwa ameandamana na Kagame muda mfupi baada ya kikao chake na Kikwete. Taarifa ambazo MTANZANIA Jumatano imezinasa, zinaeleza kuwa.........

kiongozi mmoja wa juu wa Msumbiji ambaye alikuwa pia Uganda, alikaririwa akimueleza Waziri huyo wa Kagame kuacha kabisa fikra za kuishambulia Tanzania, kwa sababu ya uamuzi wake wa kupeleka vikosi vyake Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo DRC.“Uamuzi wa Tanzania na Afrika Kusini kupeleka majeshi DRC, nimsimamo wa pamoja wa SADC.

Vitisho vyovyote dhidi ya Tanzania au uvamizi wa kijeshi, utachukuliwa ni uvamizi dhidi ya SADC, hivyo tutakuwa tayari kuingia vitani kupigana upande wa Tanzania,” alikaririwa akisema ofisa huyo wa juu wa Msumbiji. Inaelezwa kuwa, SADC imetoa msimamo huo baada ya kubainikuwa hasira ya sasa ya Kagamedhidi ya Rais Kikwete, msingi wake unatokana na hatua ya Tanzania kupeleka vikosi vyake nchini Kongo kwenda kupambana na vikundi vya waasi vikiwemo vile vinavyodaiwa kuwa na ushirika na majeshi ya Rwanda. Taarifa hizi zinathibitishwa na habari ambazo gazeti hili ilizinasa jana kupitia gazeti la The Namibian la nchini Namibia, ambalo liliandika kuwa Jeshi la nchi hiyo (NDF), ambalo linaunda kikosi maalumu cha SADC, lilikuwa limeanza kushiriki mazoezi huko Jangwani karibu na Walvis Bay.

Mazoezi hayo yatadumu hadi Oktoba 15 mwaka huu.Inaelezwa kuwa wakati mazoezihayo yakiendelea, Mkuu wa majeshi ya Namibia (NDF), Luteni Jenerali, Epafras Ndaitwah aliwakumbusha washiriki hao kuwa kwa sasa wanachama wenzao kama Wanajeshi wa Tanzania na Namibia, wanapambana na maadui wa amani Kongo na kwamba lazima wajiandae kwa hali yoyote ambayo haitabiriki. Hatua hiyo ya sasa ya SADC, na sifa ambazo imepata kummwagia Rais Kikwete kwa namna alivyosimamia mizozo wakati akiwa Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi, inaonyesha wazi jinsi Jumuiya hiyo ilivyotayari kuwa upande wa kiongozi huyo.

Kutokana na hilo, baadhi ya wachambuzi na wafuatiliaji wa mambo wanasema kuwa si ajabu basi Kagame na Serikali yake wakawa wanafahamu msimamo huo wa SADC, ambaohaujawekwa hadharani hasa kwa kuzingatia uamuzi wake wakuungana na Uganda na Kenya katika usharika wao wa hivi karibuni.

Pia hatua ya nchi yake kusaini mkataba wa kiusalama na nchi nyingine tano wa kusaidiana kijeshi endapo mmoja wao atavamiwa na nchi nyingine, imeelezwa kuwa na mwelekeo huo huo wa Kagame kuanza kujihami.

Nchi ambazo zimeingia mkataba huo na Rwanda ni pamoja na Ethiopia, Kenya, Uganda na Sudan Kusini. Hata hivyo wachambuzi na wafuatiliaji wa mambo, wamekosoa muungano huo wa kusaidiana kijeshi na Rwanda, wakidai kuwa ni wa mashaka ukilinganisha na ule unaounda SADC ambao unajengwa na matendo ya kihistoria.

Wameitolea mfano Ethiopia, kwamba ni rahisi kuasi kutokana na mfumo wake wa kijeshi unaoongozwa kwa mkono wa chuma, huku wanajeshi wake wakiwa katika hali mbaya ya kiuchumi. Wameulinganisha mfano huo na nchi moja tu ya Zimbambwe ambayo inaunda SADC kwamba, pamoja na matatizo yote ya migogoro ya kisiasa na kidiplomasia inayoyakabili, lakini jeshi lake lipo imara na linatunzwa vizuri.

Wakati wadadisi na wachambuzi wa mambo wakiwa na mtizamo huo, hatua ya sasa ya SADC imekuja wakatiambapo tayari Rais wa Afrika Kusini, Jacob Zuma aliwahi kuionya Rwanda akisema kuwa endapo nchi hiyo itajaribu kuigusa Tanzania, atakuwa tayari hata peke yake kupeleka jeshi lake kupambana nchini humo.

Nje ya SADC, nchi zinazounda Jumuiya hiyo kama Afrika Kusini, Msumbiji, Zimbabwe, Namibia na Angola zinaguswa moja kwa moja na hisia za Tanzania, kutokana na historia yake ya kushiriki kwenye ukombozi na uhuru wa nchi hizo.

Kutokana na hilo, wachambuzi hao wanasema kuwa si rahisi kwa wao kukaa kando pale watakapoona maslahi ya Tanzania yanachezewa, hasa linapokuja suala la kuichokoza.

Taarifa hizo za SADC zimekuja ikiwa ni siku chache baada ya Rais wa Marekani, Barack Obama, kuinyooshea kidole chalawama Rwanda, kitendo hicho kinaonekana kuungwa mkono kwa kasi na makundi mengine ya kimataifa.

Kagame ambaye kwa miaka mingi amekuwa kiongozi kipenzicha mataifa mengi tangu alipofanikiwa kumaliza mapigano yaliyosababisha mauaji ya halaiki nchini kwake mwaka 1994, katika siku za hivi karibuni taswira yake inaonekana kubadilika na kuchukua mwelekeo wa uadui zaidi kuliko urafiki.

Hilo linatokana na kile kinachodaiwa kuwa Serikali yake imekuwa ikihusika kuwasaidia waasi wa kundi la M23, wanaoendesha mapambano dhidi ya majeshi ya Serikali ya Kongo, jambo linalopingwa na Jumuiya ya Kimataifa pia wanatuhumiwa kwa ubakaji na mauaji ya watu wasiokuwa na hatia.

Tuhuma hizo ndizo ambazo zinamuweka Rais Kagame katika hatari na wingu la mashaka kwa sasa, hasa baada ya uhusiano wake na Tanzania kupita katika wakati mgumu kutokana na kuingia kwenye mgogoro na Rais Kikwete ambaye alimshauri kukaa mezamoja ya mazungumzo na waasi wa FDLR.

MWANAUME KWENYE KORODANI NDOGO ANAUWEZO KUJALI FAMILIA KULIKO MWENYE KORODANI KUBWA

Wanasayansi wanasema
kuwa kuna uhusiano kati ya
ukubwa au udogo wa
Korodani (Testicles) za baba
na uwezo wa baba
kutekeleza majukumu yake
kama mzazi wa watoto wao.

Watafiti katika chuo kikuu
cha Emory nchini Marekani,
wanasema kuwa wanaume
walio na Korodani ndogo
huenda wakayachukualia
majukumu yao kwa uzito na
hata kujihusisha na
kumbadilisha mtoto nepi,
kumlisha na hata
kumuogesha mtoto.

Pia uligundua kuwa utofauti
katika picha ya ubongo wa
baba wakitizama picha za
waoto wao, ilihusishwa na
ukubwa au udogo wa
Korodani.

Lakini mambo mengine ya
kitamaduni yanaweza
kuchangia kwenye uhusiano
kati ya Korodani na
majukumu ya baba kwa
mwanawe.

Uasherati na ukubwa wa
korodani zinajulikamna
kuwa na uhusiano mkubwa
kwa wanyama , wale walio
Korodani kubwa hujamiiana
na wanyama wengi kinyume
na walio na Korodonani
ndogo.

Watafiti walikuwa
wanachunguza nadharia
kuhusu ikiwa wanaume
hutumia muda zaidi katika
kuwa na mahusiano ya
kimapenzi au kulea watoto
wao. Wazo lao likiwa
kwamba wanaume walio na
Korodani kubwa hutumia
muda wao katika kuzaa
watoto wengi kuliko katika
kuwalea watoto hao.

Utafiti huo ulichunguza
uhusiano kati ya ukubwa wa
Korodani na mfumo wa
uzazi katika wananume 70
waliokuwa na watoto walio
kati ya umri wa mwaka
mmoja na miwili.
Watafiti waliwapiga
wanaume hao picha ya
ubongo wakiwa wanatizama
picha za wanao.

Utafiti wao ulionyesha kuwa
wanaume wenye Korodani
ndogo walionekana kuwa
makini katika malezi kuliko
wale wenye kubwa.

Wale waliokuwa na
Korodani ndogo
walionekana kuwa na wazazi
wazuri wanaojihusisha na
kubadilisha mtoto nepi na
kumuogesha, yaani
alijihusisha vyema katika
majukumu ya mzazi.
Mmoja wa watafiti alisema
kuwa uchunguzi wao
unaonyesha kwamba kuna
baadhi ya wanaume ambao
ni wazazi wazuri tu na
ambao wanajihusisha na
majukumu ya ulezi kuliko
wengine.

Watafiti hao waliona kuwa
ukubwa au udogo wa
Korodani unaweza kuathiri
tabia za mtu, lakini
haijulikani kama hatua ya
kumpata mtoto hubadili
mawazo na mienendo ya
baba.

WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA BACHELOR IFM 2013/2014

BACHELOR OF ACCOUNTING

1 FEISAL ABDALLAH
2 MWANAHAWA ABDALLAH
3 SUMAIYA ABDALLAH
4 WADH ABDALLAH
5 RAKIM ABEID
6 ISMAIL ADAM
7 HASSAN AHMED
8 RIZIKI ALBANO
9 LEOTINA ALEX
10 EMMY ALEX
11 ALLI ALLI
12 ATHUMANI ALLY
13 LEYLA ALLY
14 TAJIRI ALLY
15 ROSEMARY ALOYCE
16 PETRONILA AMMA
17 RAMONA ANCHASEIN
18 WINIEL ANDREW
19 SCOLASTICA ANTONY
20 AMANI AYUGI
21 PAUL BAINGAI
22 ELISHA BALINAGO
23 ELISHA BALONGO
24 ABDALLAH BENDE
25 ERNEST BISEKO
26 KENEDY BISEKO
27 AMANI BITOMWA
28 DONASIANI BLASI
29 DORINA BOMA
30 STEPHEN BUNDU
31 NESTORY BUYUNGU
32 MAKONGE CHACHA
33 FRANK CHALANGA
34 LILIANI CHAMI
35 AMANDO CHAMI
36 GRACE CHAMI
37 SIMON CHAMKALI
38 JOHN CHARLES
39 NEEMA CHARLES
40 OSCAR CHENGULA
41 LUCKSON CHISANZA
42 GODFREY CHISARA
43ABDULRAHMAN
CHOMBA
44 ZENAIS CHUWA
45 FATUMA DARUSI
46 JESCA DAUDI
47 NEEMA DEODATUS
48 ROSEMARY DEOGRATIUS
49 KELVIN DONALD
50 BENARD DONANT
51 LEAH EDWARD
52 ACHILEUS ELIAS
53 ZACHARIA ELIAS
54 GODLISTEN ELIMU
55 SALOME ELKANA
56 JACKSON ELPHAS
57 MARIA EMILY
58 GOODLUCKY ERASTO
59 NEEMA ERNEST
60 PROSPER EUGEN
61 KHUWAIDA FAIZI
62 DAUDI FESTO
63 ZAWADI FESTO
64 JACOB FRANCIS
65 AMOS FRANCIS
66 MUNIRA FUNDI
67 JOHA FUPPE
68 ELIASI GACHU
69 ISACK GAMBA
70 OSWALD GASPA
71 AGNES GERVAS
72 GEORGE GIBSON
73 JULIETH GODFREY
74 ADHA HAJI
75 HAJI HAJI
76 AMINA HAMISI
77 SIMON HANZI

78 HERIETH HAONGA
79 HASSAN HASSAN
80 MARIAM HASSAN
81 STUMAI HASSAN
82 YASSIN HASSAN
83 EVANCE HAULE
84 SHABANI HENGO
85 LEAH HOKORORO
86 HALIMA HUSSEIN
87 BAUSI HUSSEIN
88 HUSSEIN HUSSEIN
89 MOHAMED HUSSEIN
90 IDDI IDDI
91 JUSTINE IDDI
92 RIDHIWANI IDDI
93 SEIF IDDI
94 SIRAAJU IDI
95 MARTHA IGOGO
96 JAMES ILUNDA
97 ALICE ISAYA
98 HOSAM ISSALE
99 JAPHET JACKSON
100 MALEGELI JACKSON
101 CHARLES JACOB
102 YASINI JAFARI
103 AMINA JAFARY
104 MOHAMED JALLAS
105 HUNGU JAMES
106 VICTOR JAMES
107 MAYOMBO JARIBU
108 PRIVATUS JEMSON
109 GRACE JEREMIAH
110 MICHAEL JOACHIM
111 JOEL JOEL
112 JOHN JOHN
113 MEDANI JOHN
114 MELISSA JOHN
115 PHILEMON JOHN
116 ELIZABETH JONATHAN
117 IRENE JORAM
118 JONATHA JORAM
119 EMMANUEL JOSEPH

121 EDWIN JOSEPH
122 EMMANUEL JOSEPH
123 THEOFIL JOSEPH
124 GLORIA JULIUS
125 JANE JULIUS
126 KHALID JUMA
127 AZIZ JUMA
128 ISSA JUMA
129 KHAMIS JUMA
130 SELEMANI JUMANNE
131 COLIN KABELEGE
132 PETER KABOGO
133 AHMED KAKIVA
134 GLORYALICE KALLAGHO
135 STEPHANO KALOLO
136 LILIAN KALYANYAMA
137 NOEL KAMBALILE
138 EVANCE KAMPATE
139 AUDREY KAMUGISHA
140 BEATUS KANG'ANGA
141 DAVID KAPARA
142 ISLAM KARAMA
143 MARISELLA KASHANGAKI
144 MIHAMBO KASHINDYE
145 BOLLA KASOMI
146 FARAHA KASSIMU
147 MUHIDINI KASSIMU
148 JUDITH KATOBESI
149 GRACE KATUMBAKU
150 INNOCENT KAVISHE
151 JOYCE KENGESE
152 CHRISTINA KEREYANI
153 CHRISTINA KESSY
154 GODLISTEN KESSY
155 RISTO KHAHIMA
156 NASSOR KHALFAN
157 ASILA KHALIFA
158 BAKAR KHAMIS
159 FAIZ KHAMIS
160 NADHRA KHAMIS
161 YAKUB KHAMIS

162 REGINA KIATU
163 NEEMA KIBANDA
164 ALEX KIBONA
165 FELISTER KIBONA
166 HEZRON KIBONA
167 MOHAMEDI KIDAMUI
168 MARIA KIFERA
169 QUEEN KIHAKA
170 WARIOBA KIKANGA
171 FREDI KIKOTI
172 AGREY KILANGI
173 MUSTAPHA KILANGO
174 VICTORIA KILEO
175 RICHARD KILUWA
176 ESTHER KIMARIO
177 FRANCIS KIMARIO
178 JOSEPH KIMARIO
179 IKUNDA KIMARO
180 EMANUEL KIMARO
181 PENDO KIMEME
182 ALLY KINGAZI
183 RAMADHAN KINYAGA
184 WINIFRIDA KINYAHA
185 SECILIA KIRIA
186 WINLUCKY KISANGA
187 NURU KISSAVA
188 GEORGE KITINDI
189 ULUMBI KITUNDU
190 ASIA KIVUYO
191 YOTHAM KIWALAKA
192 PRISCA KOMBO
193 RUBEYA KOMBO
194 YUSSUF KOMBO
195 PATRICK KOOLA
196 HERIEL KOTI
197 MUSSA KULIJE
198 EVALINE KWAI
199 ROBERT KWAYU
200 HAPPINESS KWEKA
201 NEEMA KYARUZI
202 ESTER LADISLAUS
203 MONICA LAIDESON

204 NICE LEMA
205 PRINCE LODA
206 RICHARD LUANDA
207 SAMWEL LUGONGO
208 ANDREW LUHANGA
209 JAYRATU LUKAMBONA
210 ELIZABETH LUKUBO
211 DAVID LUMAMBO
212 SELESIUS LUNDERA
213 AGNES LUSELO
214 JOHN LUTUMO
215 AGNES LYAMUNDA
216 JACKSON LYIMO
217 ANITHA LYIMO
218 EMELINE LYIMO
219 JOYCE LYIMO
220 RAPHAEL MABUBU
221 ANNA MABULA
222 UPENDO MACHANGE
223 WILBERTH MACHUMU
224 ANNA MADAHA
225 LEORNAD MADANDI
226 ALPHA MADULAGO
227 INNOCENT MAGANGA
228 CHARLES MAGINDU
229 DANIEL MAGOHE
230 ABDALLA MAHENDA
231 DEUS MAKENGE
232 REGINA MAKUNGU
233 MOHAMED MAKURU
234 ELIZABETH MAKWETA
235 GODFREY MAKWINYA
236 ANNA MALLYA
237 GIFTAMEN MANFERE
238 LIGHTNESS MANJIRA
239 ISSA MANYONYI
240 HABIBU MAREGESSI
241 ANTHONY MARGWE
242 SAMSON MARO
243 ANGELINA MASAKA
244 STELLA MASALU
245 MICHAEL MASAMAKI

246 ELIYA MASAMAKI
247 MAGORI MASIKO
248 HADIJA MASOUD
249 NEWTON MASSAWE
250 SWAUMU MASSAWE
251 TABITHA MASSAWE
252 ERASMI MASSAWE
253 ISSACK MASSAWE
254 WITNESS MASSAWE
255 RONALD MATEMU
256 WILLIAM MATHIAS
257 BEATRICE MAYENGA
258 ALLY MAYUMBA
259 FESTO MBABA
260 ANANIAS MBELE
261 OSMUND MBILINYI
262 VINCENT MBILINYI
263 FADHILI MBOYA
264 NDESAMBURO MBOYA
265 NASRI MBUA
266 NSAJIGWA MBUZA
267 WILLIAM MBWAIKI
268 EDWIN MBWAMBO
269 NURU MBWILO
270 WITNESS MCHAU
271 CHARLES MDOE
272 NEEMA MDUMA
273 ZAITUNI MEMBE
274 GEOFREY MESHACK
275 GEOFREY MESHACK
276 IBRAHIM MFANANDO
277 IDDI MGALLAH
278 EVARISTA MGANGA
279 JOSIAH MGAYA
280 WITNESS MGAYA
281 ATULONGE MGINA
282 ISAYA MGOBASA
283 MICHAEL MGOBASA
284 JANETH MICHAEL
285 SHABAN MIKONGOTI
286 PHILIPO MILINGA
287 ROGERIO MINDE

288 MARTIN MINJA
289 DIANA MKAMBATI
290 BRIGHTER MKAMI
291 YUSTA MKANA
292 AGNESS MKANDE
293 IBRAHIM MKANGA
294 REHMAN MKEMWA
295 MUSA MKOBE
296 SAKINA MKUPETE
297 TITO MLEKWA
298 DICLA MMAO
299 DOROTHY MNENEY
300 RUKIA MNGODO
301 ROSEMARY MODESTY
302 MAIKO MOGELA
303 ABDUL MOHAMED
304 KHATWABI MOHAMED
305 REHEMA MOHAMED
306 SAID MOHAMMED
307 SAID MOHAMMED
308 GRACE MOLLEL
309 HUMPHREY MOSHA
310 KIRAMA MOSHA
311 GOODLUCK MOSHI
312 LENNOX MOSHY
313 SIRIPA MOSON
314 DIANA MPONDA
315 HANAFI MPYA
316 ALEX MREMI
317 YUNUS MRISHO
318 ELIAS MSEKALILE
319 ELIA MSETI
320 ELEUTER MSIGWA
321 RICHARD MSWEJI
322 SHEDRACK MTEFU
323 MOSES MTEGETU
324 VICTOR MTEI
325 DIANA MTEI
326 ALEX MTEME
327 ELLY MTIMA
328 ANNA MTOBU
329 IVON MTUI
330 BERNARD MUGOA
331 NICOLAUS MUJUNI
332 IDDI MUNGA
333 WINNIE MUNICE
334 INNOCENT MUNISHI
335 EVANCE MUNISI
336 ZUBEDA MUNISI
337 MOSSES MUNUMA
338 GODLEADER MUNUO
339 HUSSEIN MURO
340 LORD MUSHI
341 BEATRICE MUSHI
342 DOREEN MUSHI
343 ERICK MUSHI
344 JAQUALINE MUSHI
345 RICHARD MUSHI
346 SARAH MUSHI
347 UPENDO MUSHI
348 FAHMI MUSSA
349 MICHAEL MWABUKUSI
350 JESSICA MWACHALULA
351 EDGER MWAIPETA
352 ROIDA MWAKALUKWA
353 NSAJIGWA MWAKATUMA
354 JOHN MWAKIPESILE
355 LUSAJO MWAKITALIMA
356 ISAYA MWAKUNA
357 ALEX MWAMAFUPA
358 FREDRICK MWAMI
359 MEVIS MWAMPAJA
360 MACDONALD MWAMWAJA
361 KELVIN MWANG'ONDA
362 SAYANDE MWASHA
363 NOEL MWASIGALA
364 SARA MWATEBELA
365 LUCY MWINUKA
366 FRANCIS MWITA
367 RAHEL MWUMBE
368 ANET MYOVELLA
369 GERALD NALUGENDO
370 ALUNA NDELWA
371 JOSEPH NDELWA

372 KENETH NDUNGURU
373 MIRIAM NDUNGURU
374 STANLEY NDUNGURU
375 IKUPA NGALLA
376 MBOGO NGATA
377 LILIAN NGOIYA
378 NEEMA NGOLOKE
379 JACQUELINE NGONGI
380 IRENE NGOWI
381 ZUWENA NG'UMBI
382 OSWARD NICOLAUS
383 JESCA NJAU
384 COLLINS NKIFU
385 ATUPELE NORBERT
386 JANETH NSENGWA
387 CAROLINE NYALUSI
388 MARY NYANSWE
389 EDNA NYAULINGO
390 BATASHI NYIKA
391 EZEKIEL NZUKI
392 HILDERGARDER OISSO
393 EPAFRAS OLOMI
394 MADARAKA OMARI
395 ERICK OMARY
396 SADIKI OMARY
397 NADIR OTHMAN
398 ANYANGO OYUGI
399 JULIAS PATRICK
400 AARON PAUL
401 ELIAKIM PAUL
402 LEOPOLD PAUL
403 ISSACK PETER
404 GODWIN PETRO
405 JUDITH PHILEMONI
406 CASMIRY PHILIPO
407 DIANA PROSPER
408 JASTIN RABSON
409 SULEIMAN RAMADHAN
410 ADAM RAPHAEL
411 EDITHA RAPHAEL
412 SHEIKHAN RASHID
413 CECILIA RAYMOND
414 NEOFITA REUBEN
415 JANETH RICHARD
416 PATRICK RIMOY
417 JAQUILINE RINGO
418 KINGU ROBERT
419 PETER ROBERT
420 SEGAWA RUBARA
421 BERNARD RUBONDO
422 LACKSON RUGALABAMU
423 DILLON RUTAYUGA
424 ERICK RWAMGIRA
425 ANNA RWEYEMAMU
426 OMARI SAADI
427 MIRAJI SADIKI
428 ALAWI SAID
429 AMINA SAID
430 RAHIM SAID
431 SOPHIA SAID
432 DULLAH SAIDI
433 SAID SAIDI
434 ZAMDA SAIDI
435 RAMADHANI SALEHE
436 JUMA SALIMU
437 SAID SALUM
438 DENDE SALUM
439 SAID SALUM
440 PIUS SAMBI
441 JAKLINE SANANE
442 EMILY SANGA
443 MUSSA SANGA
444 NAOMI SANGA
445 NORBETHA SANGA
446 RECHO SANGA
447 BARAKA SANGULA
448 OBEDI SAWALA
449 FRANCIS SEDOYEKA
450 EMMANUEL SEKAYA
451 ALLY SELEMANI
452 KAMBI SEMDACHI
453 NEEMA SEMKUVA
454 KISAH SENGO
455 IKUA SENGUJI

456 GEORGE SEOSTINE
457 SHAMTE SHAMTE
458 SALOME SHANGARI
459 JOSEPH SHAO
460 LUCINA SHAYO
461 WILLIAM SHAYO
462 GILBERT SHEE
463 JUMA SHIJA
464 CHARLES SHUNDI
465 BARAKA SHWIRIRI
466 WESTON SIAME
467 KHAHELO SIGALLA
468 JESCA SILAYO
469 RAMADHANI SIMBANI
470 GRACE SIMON
471 PATRICK SIYOVELWA
472 BONIFACE STANSLAUS
473 DAVID SULELA
474 LOREEN SWAI
475 ABDULRAHIM TAIMUL
476 DIANA TANGIRA
477 CARLOS TARIMO
478 CLARA TARIMO
479 GETRUDA TARIMO
480 ERIC TASSEYN
481 BONIVENTURA TESHA
482 HENRY THOMAS
483 TIMONIUS TITUS
484 RIZIKI TULLY
485 RAMONA TUMBO
486 SARYA TUMBO
487 CHIDABWA TUPPA
488 MARTIN TYEAH
489 REGINA URASSA
490 BILL URIO
491 RIZIKI VALERIAN
492 WAILOS VIJEVANIA
493 FLACIAH WARWEMBO
494 AZIZA WAZIRI
495 PHARES WILSON
496 FRANCIS YUNJI

BACHELOR OF BANKING AND FINANCE
FIRST NAME SURNAME
1 ABDALLAH ABDALLAH
2 MOSSY ABDUL
3 HUSSEIN ADAMU
4 PAUL AFFAH
5 MARY ALBIN
6 SAMIHA ALI
7 FATIME ALLY
8 LIGHTNESS ALLY
9 SUDI ALLY
10 PILLY ALMAS
11 JOSEPHINE ALOYCE
12 BONIFACE AMANI
13 DAN ANDALWISYE
14 LILIAN ANOLD
15 AMANI ANYIGULILE
16 ELIAKIM ASIMULIKE
17 KIRUA ATHUMAN
18 NASRA ATHUMAN
19 SAFIA ATHUMANI
20 SAMWELI AUGUSTINO
21 HAWA AYOUB
22 HALIMA AZIZI
23 GHALIB BAKARI
24 ANTIA BALENZI
25 HAJI BANDA
26 LEOCADIA BARANYIKWA
27 BUINDA BENARD
28 MICHAEL BENEDICT
29 MICHAEL BENEDICT
30 BRIGITHA BERNAD
31 FLORIAN BESSANGO
32 ENOCK BOAZ
33 ESSAU BONIPHACE
34 SABAS BUCHINKULI
35 DENIS BUDEBA
36 MARTHA BUTA
37 AERLINE BUTOKE
38 FRANCIS BUTUBE
39 RAPHAEL BWIRE
40 MURASHANI BYALUGABA
41 MARWA CHACHA
42 VALELIANA CHAMBULILA
43 ELISHA CHAPARAMA
44 ALEX CHARLES
45 CATHERINE CHARLES
46 SALOME CHARLES
47 HALIMA CHAULEMBO
48 SADOCK CHENGULA
49 TAUSI CHILLO
50 ROBERT CHISAMBA
51 REHEMA CHITENJE
52 NURDIN CHONGWE
53 ATHUMANI CHOSO
54 MARY CHRISTIAN
55 ERNESTA CHUWA
56 ANNOCIATHA COSMA
57 DANIEL COSTANTINO
58 CASTO DAIMON
59 JESTINA DANIEL
60 RICHARD DANIEL
61 EDNA DAUDI
62 KENETH DAUDI
63 ELIZABETH DAVID
64 ANOLD DAVID
65 DERICK DEOGRATIAS
66 AGABA DERRICK
67 RAMADHANI DIGOS
68 CHRISTOPHER DISMAS
69 GEORGE DONALD
70 ESTHER EDWARD
71 JOSEPHINE ELIAFOO
72 ELIAS ELIAS
73 PETER ELIAS
74 JOHN EMILIAN
75 MICHAEL EMMANUEL
76 FABIAN FABIAN
77 BASHIRI FATAKI
78 GERALD FELICIAN
79 ANGELO FESTO
80 MICHAEL FRANCIS
81 DANIEL FUNGO
82 ELIEZA GAMA
83 NEEMA GEOFFREY
84 LIGHTNESS GHERABASTER
85 GWESSO GIBORE
86 AGNES GOODLUCK
87 RACHEL GUDA
88 HALIMA HAMISI
89 HAWA HANGO
90 SAID HASSAN
91 HASHIM HASSANI
92 PRAY HENRY
93 LEONARD HHOKO
94 MARIANNE HIZZA
95 MOSES HYERA
96 TERESIA HYERA
97 JUMA IDD
98 SALIMU IDDI
99 JUMA ILOMO
100 EDITHA ILUNGU
101 OVUMAN ISAKWISA
102 VICTORIA ISAYA
103 LILIAN ISHABAKAKI
104 ISMAIL ISMAIL
105 NAJAHU ISSA
106 EDGER JACKSON
107 WINFRIDA JACKSON
108 ALBERT JACOB
109 EDWARD JAILY
110 JAMBIA JAMBIA
111 DANIEL JAMES
112 MARIAM JAMES
113 SAMSON JAMES
114 JESCA JAPHET
115 DIANA JESSE
116 MAGRETH JIMMY
117 EMMANUEL JOELY
118 BAHATI JOHN
119 ELIZABETH JOHN
120 EMMANUEL JOHN
121 LUCAS JOHN
122 WILLIAM JONAS
123 NELSON JOSEPH
124 CHACHA JOSEPH
125 ELIZABETH JOSEPH
126 DAVID JULIUS
127 HAPPINESS JULIUS
128 ISMAIL JUMA
129 JUMA JUMA
130 JUSTINE JUMANNE
131 MGENI KABISAMA
132 ELLEN KABOTE
133 DAVID KABUCHE
134 MARIAM KABUMA
135 HABIBA KAGIRE
136 PRINCE KAGUO
137 RASHID KALINDIMYA
138 DANFORD KAMARA
139 ALLEN KAMNDE
140 HAIBA KAMPIRA
141 JENIFER KAMUKALA
142 ELIAH KAMWELA
143 KULWA KANDONGA
144 NDAGO KANESERO
145 JACKLINE KANJE
146 ANDREW KANSAPA
147 LULU KAONDO
148 ANNA KAPELA
149 ELIJAH KATABAZI
150 MARY KATALA
151 ADELBERT KAZINDUKI
152 NYANGOMA KHALFANI
153 ABDULMALIK KHALIKI
154 RAHIMA KHATIB
155 PETER KIAMBIKE
156 WEMAEL KIANGI
157 FREDRICK KIANGO
158 ZUWENA KIBAO
159 RAMADHANI KIBASA
160 SARAH KIBIKI
161 MAGINGA KIHENGU
162 MICHAEL KIHIGA
163 OLIVER KIMARIO
164 LIGHTNESS KIMARO
165 FREEMAN KIMARO
166 ROSE KIMARO
167 WINGOD KIMARO
168 AURELIA KIMARYO
169 EMMANUEL KINDOLE
170 PETER KINYAMAGOHA
171 GEORGE KIONDO
172 PROSPER KIONDO
173 VERONICA KIPIGAPASI
174 MAULID KIPINGU
175 EVAREST KISAKA
176 AMEDEUS KISIMA
177 NEEMA KISIRI
178 REGINA KITALY
179 ABUBAKARI KITWARA
180 ANGELINA KIVUYO
181 MIKIDADI KIZITO
182 HUSNA KOMBA
183 MARY KUMBEMBA
184 IBRAHIMU KUTURA
185 PASCAL KUYENGA
186 DENIS KYARA
187 GLORY KYARA
188 ANADARIA LAURENT
189 DIANAROSE LEMA
190 GLORIA LEMA
191 LOVENESS LEMUNGE
192 BARIKI LEONARD
193 BARIKI LEONARD
194 RICHARD LOMAYANI
195 HELEN LOREU
196 LAUREEN LOUX
197 ESTHER LUENA
198 MARIA LUPOLASO
199 EMMANUEL LYAKURWA
200 WINLADY LYIMO
201 ALSON LYIMO
202 DENIS LYIMO
203 MELKIZEDECK MACHA
204 VICTOR MACHA
205 ELIASI MACHIMO
206 BOBHENRY MACHIMU
207 LUBIGISA MADUKWA
208 ALLY MAFURU
209 NKWIMBA MAGAMBO
210 HASSANI MAGINA
211 SAID MAGWEGA
212 YOHANA MAJIGE
213 STEPHEN MAJULLA
214 HENRY MAJURA
215 HELLEN MAKALWE
216 MUSTAFA MAKASSY
217 JOSEPH MAKUNDI
218 ALLY MAKWANDA
219 JOSEPHINE MALANGALILA
220 BARAKA MALEMA
221 GREGORY MALEMBEKA
222 TARIQ MALIQ
223 CALVIN MALLYA
224 ANTHONY MANYANGA
225 PASCHAL MANYILIZU
226 MARY MAPESA
227 DAVID MARANDU
228 MERINA MARANDU
229 INNOCENT MARIWA
230 ERICK MARTIN
231 ERICK MARTIN
232 ANETH MARTINE
233 PASCHAL MASALU
234 ALLY MASANGULA
235 PETRO MASANYIWA
236 JACOB MASEKE
237 NAY MASHALLAH
238 PATRICK MASHENENE
239 KELVIN MASINDE
240 YUSUFU MASOUDI
241 THOMAS MASSORO
242 RASHID MASSOUD
243 STELLA MATAFU
244 STELLA MATAFU
245 MARIA MATECHI
246 SANTOS MATENDE
247 NIPANEEMA MATERU
248 MRISHO MATHEW
249 DANIEL MAWALLA
250 HAPPY MAWONA
251 ADELINA MBAWALA
252 PRISCA MBEYA
253 ANNA MBOYA
254 EDITH MBOYA
255 FRANK MBOYA
256 GRACE MBUGE
257 KIJEKINGWE MBWAGA
258 JAMES MBWILO
259 LUCAS MBWILO
260 WILKINS MCHAKI
261 NATUJWA MCHOME
262 KELVIN MDAGANU
263 DEOGRATIUS MDAVIRE
264 VIOLETH MDEMU
265 ISSA MDOHI
266 NATALIA MERERE
267 FOCUS MESANGA
268 NICODEMAS MFUNGO
269 THERESIA MGASA
270 GRACE MGAYA
271 NICHOLAUS MGODE
272 SALUM MGUHI
273 ISAYA MICHAEL
274 RAHEL MICHAEL
275 FRANK MINJA
276 MARCELINA MINJA
277 EMILIANA MISANGA
278 VENANCE MISSANA
279 DIANA MISSANGO
280 JUMA MJAILAH
281 ANGELINA MJEWA
282 HAGAI MJIRA
283 IGNAS MKAWE
284 RAYMEND MKEMBELA
285 HAMISI MKENGEMBA
286 TIZRA MKINA
287 FLORA MKOLONGO
288 JOSHUA MKUKI
289 RAYMOND MKUTTA
290 RONALD MLAY
291 DIANA MLELA
292 FLORA MMARI
293 STEPHEN MMASSY
294 STEVEN MMOLE
295 PETER MMOLE
296 STEVEN MMOLE
297 CLARA MMORO
298 FELISIA MNANDI
299 HASANI MOHAMEDI
300 HASSAN MOHAMEDY
301 AMNE MOHAMMED
302 SALIM MOH'D
303 PETER MOLLEL
304 HUSSEIN MONDO
305 LUSEKELO MOSES
306 ISACK MPILUKA
307 HAWA MPIMBI
308 HAMZA MPONDA
309 PATRICK MPUYA
310 AGNESS MREMA
311 ABBAS MRINGO
312 ANDREA MRUTU
313 WALDA MSAFIRI
314 JOSEPHINE MSANGI
315 MOHAMED MSELEM
316 WILBARD MSENDO
317 ABDALLAH MSHANA
318 HANS MSHANA
319 JOHN MSHANA
320 DENIS MSHOMBA
321 VENANCE MSIGWA
322 ISACK MSILU
323 HAPPINESS MSOKILE
324 OSMAN MSUVA
325 TUMAINI MSUYA
326 HUMPHREY MTERA
327 MSHERWA MTIRO
328 NOEL MTUI
329 ROGERS MTUI
330 JULIANA MTUTWA
331 FRANK MUDENDE
332 JUSTUS MUGANGO
333 JOYCE MUHELEJI
334 NYAMAMBALA MUKAMA
335 VIOLA MUNGURE
336 GILBERT MUNISHI
337 FARIDA MUNISI
338 LATIFA MUNISI
339 BARAKA MUNUO
340 ENIPHER MUSHI
341 JOSEPH MUSHI
342 ELLYGLORY MUSHY
343 CECILIA MUSIKULA
344 FLORAH MUSSA
345 ZENA MUSSA
346 ROGERS MUTAYABALWA
347 HUSNA MWAHU
348 VICTORIA MWAIFWANI
349 BERNAD MWAISEMBA
350 VERONICA MWAKASOLA
351 MARTIN MWAKASONDA
352 ERICA MWAKATIKA
353 STEVEN MWAKILUMA
354 ATUPELE MWAKIPESILE
355 ANDREW MWAKISU
356 FADHL MWAKITELEKO
357 CYNTHIA MWAKYUSA
358 BRENDA MWALINGO
359 JOHNSON MWALONGO
360 DORIS MWALYAJE
361 KENEDY MWAMAGEMO
362 NDIMYAKE MWAMASAGE
363 FRANK MWAMBENE
364 ALIKO MWAMBUNGU
365 JUDITH MWAMPELWA
366 GODBLESS MWANGA
367 STEVEN MWANGALABA
368 IPYANA MWANGOLOMBE
369 NEEMA MWANGOMILE
370 LUGANO MWANKENJA371 BEAUTY MWANSABA
372 JUSTINA MWANTANI
373 PHILEMON MWELEKA
374 ANDREW MWEMBE
375 MATILDE MWIGANI
376 CATHERINE MWIKOLA
377 RACHEL MZIGA
378 JULIA NALUKWAGO
379 SAAD NAMTUBWI
380 JAPHET NANGALI
381 IRENE NAPELLA
382 ELIAKIM NASHON
383 BRIGITHER NCHEMBI
384 GODFREY NDAMALYA
385 DORICE NDAPO
386 GEORGE NDEMBELE
387 BENNO NDIMBO
388 PHILEMON NDOGOTI
389 PHABIAN NDOMBA
390 ROSEMARY NDONGO
391 GLADNESS NDYAMUKAMA
392 MUSSA NGAGA
393 SHUMBANA NGAIWA
394 YOHANA NGALLO
395 MAGABIRO NG'AMBU
396 FARAJA NG'ANDU
397 ERICK NGILISHO
398 NGONGOSEKE NGONGOSEKE
399 ANGELA NGOTI
400 GOLDEN NG'OWO
401 SIMON NHYENJE
402 JANE NICHOLAUS
403 DAVID NIMROD
404 SEBASTIAN NJAU
405 SALOME NJUGULA
406 JOSEPH NKONOKI
407 SEVERIANA NKONOKI
408 VERONICA NOMBO
409 JOHNSON NTEMI
410 FOCUS NTOCHENI
411 MARIO'S NYACK
412 KABANZA NYAKALE
413 JAPHET NYAKO
414 JACOB NYAMARUNGU
415 JOSEPH NYANDA
416 JOSEPH NYAROBI
417 DEBORAH NYASIBORA
418 INNOCENT NYINDA
419 LEAH NYUDIKE
420 MAKAME OMAR
421 NURU OMERY
422 SYLVIA ORIYO
423 ROSE PARESSO
424 GEOFREY PASCHAL
425 LILYAN PASCHAL
426 THOBIAS PAUL
427 ERICK PETER
428 EMANUEL PHINIAS
429 SHARIF PILLY
430 NANCY PROSPER
431 MJUNI RAPHAEL
432 RWEGASIRA RICHARD
433 DENNIS RONJINO
434 RENATHA RUGEIHYAMU
435 CLARENCE RUGIMBANA
436 THEOPISTA RUTAYUGA
437 NIYONGERE RUTONESHA
438 KAREEN RUTTA
439 MARIA RWEYONGEZA
440 SAADAT SAADAT
441 NYAKA SAID
442 SAMMY SAIDEYA
443 ZAHRA SALEHE
444 MWAJUMA SALEHE
445 ZENA SALIM
446 SEIF SALIM
447 ZENA SALIM
448 MRISHO SALMIN
449 SUAD SALUM
450 AMANI SAMBO
451 SAID SAMWEL
452 DIANA SANGA
453 PAULO SANGA
454 YUSUPH SANGA
455 GABRIEL SAPANJO
456 IRENE SEDEDE
457 IBRAHIM SEGERE
458 VENANCE SEKIDIO
459 ASHA SELEMANI
460 ROSE SEMWAIKO
461 HANS SETONGA
462 REHEMA SHABAN
463 GWAKISA SHADRACK
464 SALMA SHAFII
465 METHUSELA SHALLUA
466 EMILIANA SHANTA
467 SAMWEL SHAYO
468 HASSAN SHEMELA
469 ALOYCE SHIRIMA
470 LIDYA SHIRIMA
471 WITNESS SHOO
472 MICHAEL SHOWE
473 HUMPHREY SICHONE
474 BEATRICE SILAYO
475 HALIMA SINGANO
476 DAUD SOLLO
477 CHRISTINA SONGALIMI
478 INTISAR SULEIMAN
479 MOZA SULEIMAN
480 ELISHIFWAYA SWAI
481 SALOME SWAI
482 HAWA SWAIBU
483 ERNEST TARIMO
484 FARAJA TARIMO
485 FEROUS TARIMO
486 PROTCHES TARIMO
487 COLETHA TEMBA
488 GEOFREY TEMENAO
489 JOHN TEMU
490 RICHARD TEMU
491 SHALIN THAVER
492 JESCA TUGARA
493 AMADEUS TUKUNJOBA
494 HALID UGASA
495 CHRISTEL ULOMI
496 SIA URIO
497 FESTO VALERY
498 SAMWEL VIANNEY
499 PROCHES VINCENT
500 ANTHONY WAMBURA
501 RAYMOND WANDEMA
502 BENJAMIN WAWA
503 RAHMA WAZIRI
504 WHELLAN WELLINGTON
505 SOPHIA YAHAYA
506 IRENE YANGE
507 ABDILLAH YUSSUF
508 YUSSUF YUSSUF
509 JOSEPH ZAWADI
510 JANETH ZONGOLO
BACHELOR OF COMPUTER SCIENCE

1 MUSLIM ABDILLAH
2 HAJI ABDULHAMID
3 TUNTUFYE ABEL
4 SAIDI ABUU
5 JOYCE ADAM
6 GODWILL AKILIMALI
7 ABUBAKAR ALI
8 SAID ALLY
9 TWALIB ATOLIGWE
10 ANGELINA BARAKA
11 BASILISA BISEKO
12 EMMANUEL BONIPHACE
13 BENEDICT DANIEL
14 FRANK EDSON
15 DOMICIANUS EMMANUEL
16 ABDALLAH FUAD
17 PATRICK GENES
18 HAMIS HAMIS
19 YUSUPH HAMISI
20 PAULO HAROLD
21 MWANAISHA HASSAN
22 MAHMOUD IBRAHIM
23 ZUBERI IDD
24 GEORGE IKOLES
25 AGOLA ISACK
26 JAIRO JACOB
27 NAHEED JAINUDIN
28 DAVID JOEL
29 ALLEN JOHN
30 LUCAS JOHN
31 INNOCENT JOSEPH
32 GERALD JULIUS
33 GODWIN JUSTINE
34 ANDREW KAHESA
35 AUGOSTINO KALUMUNA
36 MOHAMED KHAMIS
37 MOHAMED KHAMIS
38 SHARIFU KIFIKA
39 MICHAEL KIMARIO
40 MICHAEL KIMARIO
41 NELSON KIRABE
42 NATHAN KOROSSO
43 NICHOLAUS KULAMBUKA
44 COSMAS KURWA
45 MICHAEL KWEMBE
46 KENNETH LAZARO
47 LENNOX LUGOMBE
48 JUBILANT LWALI
49 DEVICE MARIA
50 REGAN MASATU
51 MASHAURI MASHAURI
52 ALAM MBUJA
53 JOSEPH MICHAEL
54 MICHAEL MLAY
55 ELIKANA MOSOZI
56 TWALIBU MSANGI
57 ERICK MSHIBA
58 ASIA MUHAJIRI
59 PATRICK MUNISHI
60 HEBRON MUSHI
61 DAVID MUTAGAYWA
62 EUGEN MWAMAFUPA
63 AMORI MWAMBUNGU
64 SALEHE MWANGA
65 KENNETH MWASE
66 BRUNO MWASENGA
67 REHEMA MWINJUMA
68 DAUDI NALOGWA
69 MOHAMMED NASSOR
70 STELLA NDUNDULU
71 JANETH NGAILO
72 GEORGE NJAU
73 NKANABO NKANABO
74 JONAS NKWABI
75 GOODLUCK NYAKEKE
76 BETHELEHEM OMARCH
77 MUKHTAR OMARY
78 GODFREY PELLA
79 CHARLES RUTATINA
80 SAIDI SAIDI
81 SAIDA SALEHE
82 MWAJUMA SALUM
83 OMARI SALUMU
84 HAGAI SAMSON
85 ISAYA SEMUNGURUKA
86 FAUSTA SEVERINE
87 ALEX SHADRACK
88 LOUIS SHOO
89 STIVIN SIMON
90 SIMON SIMUMBA
91 STEPHEN SIXBERTH
92 FLORA STEPHEN
93 PATRICK TIRA
94 DICKSON WILYSON
95 MICHAEL YONGO

BACHELOR OF SCIENCE IN INSURANCE AND RISK MANAGEMENT

1 ALLY ADAM
2 JIMIA AHMEDY
3 DICKSON ALENDWA
4 ABASI ALI
5 RAMADHAN ALLY
6 ANETH ANGELO
7 FRANCIS ASILA
8 ANDREW ASSENGA
9 LINDA ASSENGA
10 AMINA AYUBU
11 KAZEMBE BAKARI
12 SAIDA BASHIR
13 FRANCIS BENJAMIN
14 SIMON BONIFACE
15 JOSEPH BONIPHACE
16 LETICIA BWIRE
17 HOPE CHALE
18 ANDREW CHARLES
19 MABUBA CHARLES
20 WARDA CHARLES
21 NICKSON CHENGA
22 AQUINATHA CHIGANA
23 IRENE CHIMBUVU
24 JOHN CHOTA
25 TEREZA DANIEL
26 SAMWEL DAUD
27 REBECA DAVID
28 SANGWANI DAVID
29 JOSHUA DORIYE
30 TIMOTH EMILIUS
31 HAPPINESS EMMANUEL
32 GEOPHREY FRANCIS
33 BARAKA FRANS
34 JOSEPH FUE
35 EMMANUEL GEORGE
36 BARAKA GODFREY
37 NELSON GODSON
38 SAMWEL GUNDA
39 MWINGA GWAO
40 HALIDI HAMIS
41 IRENE HASSAN
42 DAVID HAULE
43 FELISTAS HONDE
44 BERTHA IBRAHIM
45 RIDHWANI IBRAHIM
46 STEVEN IGNATIUS
47 DEBORA ISDORY
48 FRANK JEREMIAH
49 YUSUPH JOSEPH
50 ILEKEBU JULIUS
51 PAUL JULIUS
52 KHADIJA JUMA
53 MERIANG'AA JUMA
54 SAIDI JUMA
55 DEBORAH KAGOROBA
56 EDWARD KAGUTA
57 DANIEL KAILA
58 ISAYA KALINDAGA
59 ELIAS KALINGA
60 IRENE KAMNDE
61 ESTHER KASANGA
62 KHALID KASIKA
63 SUBIRA KASITU
64 MOHAMEDI KASSIMU
65 JOSEPHINE KAUKI
66 EDDIBERTH KAYAWAYA
67 MASOUD KHAMIS
68 SHAMSA KHATIBU
69 PASQUINER KIBALI
70 PATRICIA KIBASA
71 EMILIUS KIFIGO
72 DAVIS KIHWELE
73 EMMANUEL KILENGIWA
74 EVANCE KIMARIO
75 ROSE KIMARO
76 GLORY KIONDO
77 CLARA KIPANGULA
78 AISHA KIRAMBI
79 ALEXANDER KIROBI
80 LATIPHA KISSIWA
81 MKAMI KISYELI
82 MARK KITALY
83 JOSEPH KOMBA
84 EZEKIEL KOMOLO
85 HASSANOUR KONDO
86 FRANK KUNAMBI
87 AMANI KUNINI
88 NORAH LAIZER
89 FRANSIS LINDI
90 ANGEL LIPUWA
91 JOHN LUKUMAY
92 JOSEPH LYAKA
93 THOBIAS MACHIMO
94 HASSAN MAGANGA
95 NAOMI MAGERE
96 STEVEN MAGHEMBE
97 ALPHA MAHEKULA
98 HADIJA MAHIMBO
99 MARWA MAKABE
100 HASSAN MAKAME
101 ERNEST MAKELELE
102 ELIAS MAKUZA
103 ANASTAZIA MALALE
104 GRACE MALISA
105 YUSUPH MALISA
106 BEATRICE MAMBETA
107 BAHATI MANENO
108 GIDEON MANG'ANA
109 JANUARY MANJI
110 FRANK MANYAMA
111 ROSSE MARISA
112 DIANA MARTIN
113 ESTER MASHINA
114 MASOUD MASOUD
115 ANNA MASSAWE
116 EMMANUEL MASSAWE
117 NELSON MASSAWE
118 JEREMIAH MASWI
119 DORIS MATARA
120 FADHILI MATELEKA
121 FORTUNATUS MAURICE
122 SILAS MBARUKU
123 FAUSTA MBILINYI
124 MARIAM MBOWE
125 DEOGRATIUS MBURI
126 IBRAHIM MDEE
127 PAULO MENGO
128 MWAJUMA MFAUME
129 LUCY MGALULA
130 SOPHIA MGAYA
131 DANIEL MGWASI
132 LILIAN MHALLY
133 STANSLAUS MICHAEL
134 ABUNASIRI MKALLI
135 FRANCE MKENDA
136 JEREMIA MKWELE
137 BENADETHA MLAY
138 MAGRETH MLOWE
139 DANIEL MLOWEZI
140 FREDRICK MLOWOLA
141 SAID MLOZI
142 ANITHA MMARY
143 PENDO MNJAGILA
144 MARYGRASIA MNYAWAMI
145 ALI MOHAMED
146 SALUM MOHAMED
147 RAJAB MOH'D
148 IRENE MOLLEL
149 SIA MONGI
150 ABDALLAH MOYO
151 ANGELA MPIGA
152 RAJABU MPILI
153 DANIEL MRINDOKO
154 WILLIAM MRUMA
155 EVONA MSACKY
156 GLORY MSAKI
157 WILSON MSSETI
158 PETER MSULAH
159 DAUDI MTEGA
160 PILI MTENDE
161 BALBINA MTONGA
162 HOLOTA MTUNGURU
163 JUSTIN MUGANYIZI
164 HAROLD MUKOMA
165 ATUPELE MUNGOME
166 AIKANDE MUSHI
167 LUCAS MUSHI
168 ROBERT MUSHI
169 TASLEEMA MUSHI
170 FELICIAN MUSSA
171 RUKIA MUSTAPHA
172 STANSLAUS MWACHA
173 ISAYA MWAKASAKA
174 JOSEPH MWAKIBINGA
175 LUGANO MWAKIBINGA
176 FREEMAN MWAKINGILI
177 CATHERINE MWALONGO
178 BUPE MWALUSANYA
179 MIRIAM MWAMBONEK
180 JOHARI MWAMBUSI
181 ESTER MWAMENGO
182 THERESIA MWANITU
183 GLADNES MWANO
184 MIRIAM MWASHUSA
185 VICTORIA MWAVILENGA
186 MUSA MWICHANDE
187 WINNA MWINUKA
188 HAPPYNESS MWITA
189 LOSIM NAIROWA
190 RAMADHANI NASSORO
191 MANSOURY NAWAB
192 DEOGRATIUS NDALI
193 ATHUMANI NDULLAH
194 JULIUS NELSON
195 THERESIA NELSON
196 IBRAHIM NGIRINI
197 JUMA NG'ITU
198 CATHERINE NJOKA
199 IDDI NOMUYO
200 PASCHAL NOVATH
201 GRACE NTIBANSIGA
202 LINDA NYAMAGENI
203 LAMECK NYAMYA
204 TUMAINI NYIKA
205 BRUNO NZALI
206 OMARY OMARY
207 SALUM OMARY
208 SOPHIA ONGA
209 ILHAM OTHMAN
210 GEOFREY PAIGHTY
211 JOHN PAUL
212 PAULO PAUL
213 YAHAYA POGWA
214 ANETH PRISCUS
215 HAWA RAMADHAN
216 THUWAIBA RAMADHAN
217 MALILO RAMADHANI
218 NASSOR RAMADHANI
219 ABDUL RASHIDI
220 FRANCIS RWAMBO
221 EDSON RWEYONGEZA
222 NASRA SAID
223 RUKIA SALEHE
224 RUWAIDA SALIM
225 RAISA SAMWANGWA
226 LEAH SAMWELY
227 CORRYS SANGU
228 SAUSI SAUSI
229 MOHAMMEDI SEIF
230 LEONARD SEKAMBA
231 OSCAR SHABAN
232 IRENE SHIJA
233 ROMANA SHIRIMA
234 HAPPINESS SHUKURU
235 IDRIS SILAYO
236 ELIZABETH SILINDE
237 EPIPHANIA SIMBA
238 NEEMA SIMON
239 NELSON SOSPETER
240 NICKSON STAMBULI
241 DIANA SWAI
242 SELINA SWEETBERT
243 HILARY TAIRO
244 JANETH TAIRO
245 SIRI TARIMO
246 LEAH TESHA
247 PASCHAL TOGOLO
248 ABDUL UGASA
249 ALBERT URIO
250 EMAKULATA WILLIAM
251 JENIF WILLIAM
252 JUSTINA YEGELA
253 FLORA ZACHARIA
254 MARY ZULU
BACHELOR OF SCIENCE IN INFORMATION TECHNOLOGY

1 NADHIR ABDALLAH
2 ZACHARIA ALEXANDER
3 AHAMEDI ALLY
4 HAMID ALLY
5 FADHILI AMRY
6 HALID ATHUMAN
7 BRENDA AYO
8 ANDREW BADELEYA
9 GLORY BALTAZAR
10 OMARY BARUTI
11 EVARISTI BENEDICTI
12 BILALI BILALI
13 JABIR BRUHANI
14 KAPANI BUHWAHWA
15 LEAH BUSUMABU
16 ELVIS CHUNGA
17 JOHN DAVID
18 ELISHA EMMANUEL
19 MONICA FRANCIS
20 EDWARD GASTONE
21 HONORATHA GERALD
22 LIGHTNESS GODFREY
23 WILLIARD GOWELE
24 ABDALLA HAMAD
25 HABIBU HAMIDU
26 WILLIAM HEKO
27 SALMA ISMAIL
28 RUTIKANGA KABWEBWE
29 ENOCK KAGUNILA
30 ESTHER KAHATANO
31 PAUL KAYUKI
32 MUGISHA KAZOBA
33 WINIFRIDA KIATU
34 CANNISYANUS KIKANGO
35 THOMAS KINYAWA
36 ALEX KIRANGI
37 JOSEPH KISIGA
38 SHABAN KIULA
39 JOSEPHINE KWIYEYA
40 PROTAS LYAPA
41 MAGRETH MAHENGE
42 RAHABU MAHENGE
43 SIMON MAHUWI
44 ALLY MASOUD
45 RASHID MASOUD
46 HONEST MASSAWE
47 JOAKIM MBELE
48 AINESS MBONEA
49 JANETH MBWIGA
50 VIOLETH METHOD
51 VINCENT MICHAEL
52 ISSA MISANGO
53 KUDRA MKINDI
54 PHILIPO MNGURE
55 SADICK MOHAMED
56 HAMIS MOHAMED
57 VERONICA MSILU
58 VICTOR MTOWA
59 VICTOR MTOWA
60 MUKAMA MUGANDA
61 REHEMA MUSSA
62 TIMOTHEO MWACHA
63 FRANK MWALULI
64 ELIZABETH MWANISAWA
65 WILLIAM MWASANDUBE
66 GWALUGANO NDILE
67 JOHN NDOJE
68 ANTHONY NGALLO
69 PHILIPO NJOWOKA
70 CHRISTINA NKYA
71 ABEDI NTABALEZI
72 PETRO NYAMAKA
73 KAITAN OSMOND
74 EDWARD PATRICK
75 JOSEPH PETER
76 MAKARIOS RAYMOND
77 ROSEMARY RWENYUMISA
78 GILBERT RWEYEMAMU
79 OMARI SAID
80 RASHID SHABAN
81 MANDELA SHAHANGA
82 KEMWEL SHAYO
83 LUIS SHEKAONEKA
84 HUMPHRAY SHUMA
85 FELICHISM SILVEST
86 SAMWEL SONGELAELI
87 BENSON SWAI
88 CRISPIN TEYE
89 NICHOLAUS UKUNGU
90 HAMIDU ULIMWENGU
91 GODFREY VALERIAN
92 DERICK VICENT
93 NYIMADI YANGE
BACHELOR OF SCIENCE IN SOCIAL PROTECTION
1 ALLY ABDALLAH
2 MBONDE ABDALLAH
3 ASHA AHMADA
4 EDWARD AMBAKISYE
5 STEPHANO ANDREW
6 GWAKISA ANGOLWISY
7 JUHUDI ASHERY
8 MAGRETH ASSENGA
9 ABUBAKAR BAKAR
10 LENATHA BARUTI
11 JIRAFRANK CHARLES
12 REVOCATUS CHARLES
13 FESTO CHIWANGU
14 DAVID CHRISTOPHER
15 CHARLES CLAUD
16 YOHANA ELISHA
17 JUDITH FRATERN
18 HALIMA GALAMBO
19 DAY GAMBA
20 PAULINA GODFREY
21 PATRICK GYINDO
22 SAUMU HAROUN
23 KHADIJAH HASHIEM
24 SUBEHA HEMED
25 JACKSON HENDRY
26 TUNGE JAMES
27 SIWANINA JAZIRI
28 REBECCA JOELY
29 KASSIAN JOSEPH
30 ESTHER JOSHUA
31 MARIA JULIUS
32 JUMA JUMA
33 AGNES KABWE
34 GEOFREY KAIZA
35 SALIM KAPORO
36 PENJAN KARUA
37 SHARIFU KASANGA
38 CHRISTINA KATUNDU
39 INNOCENT KEMBO
40 RAUHIYA KHAMIS
41 DIANA KILEO
42 RIZIKI KIMARIO
43 EVANS KISANGA
44 KALEBU KISHEPO
45 VERONICA KOMANYA
46 KENNETH KOMBA
47 MARIA KOMBA
48 HAKIM KOMBO
49 JENIFER KWANGU
50 ASMA KWEMBE
51 MONICA LAURIAN
52 FINES LEMA
53 RAJABU LILUNGULU
54 HENRY LUFEGA
55 SADICK LUGENDO
56 ZAWADI LWENA
57 MARY LWENDO
58 FAITH MAGILA
59 NEMBURIS MAINA
60 LOYCE MAJIGE
61 KENETH MAKULE
62 VICTORIA MAKYAO
63 VICTOR MALALE
64 RUFINA MALLYA
65 EDITHA MAPUNDA
66 MOHAMED MASOUD
67 EMMANUEL MASSEY
68 GODFREY MASUI
69 ODILO MATINDIKO
70 REBEKA MATITI
71 SUKUMA MAYENGA
72 GILYA MAYUNGA
73 JULIETH MBEYELLA
74 NURU MBURA
75 EPHRAIM MDOTA
76 HENOCK MELES
77 FANUEL MLAWI
78 ELISHA MMARY
79 RAHMA MOHAMED
80 ZAINABU MOHAMED
81 WISTON MOSI
82 MAOMBI MPARAZO
83 MODEST MPEKA
84 EDINA MSIGWA
85 ELIZABETH MSUYA
86 ERICK MTANGA
87 SAID MTEZO
88 PILI MUBARAK
89 ROGER MUNGEZI
90 MARYLILIAN MUSHY
91 EMMACULATE MUTAJWAHA
92 BARAKA MWAITINDA
93 BETINA MWAKISOMBOL
94 WINFREDA MWAMBAPA
95 NURU MWAMFUPE
96 MARIA MWANKENJA
97 MARY MWENDO
98 AHMED MWINYI
99 SELEMAN MZAVA
100 ALLY MZEE
101 AHMED MZUZURI
102 GRACE NDELWA
103 JOYCE NDIMILA
104 JANE NG'ENI
105 WITNESS NGOGO
106 ANOLD NG'OMA
107 DANIEL NSAJIGWA
108 GOODLUCK NUNGU
109 VERONICA NYONI
110 FAINESS NZALLI
111 DOMONICK NZELANI
112 GRADICE PETER
113 JOSEPHINE PHILIPO
114 KAFUNA PYANGA
115 HAMBAL RASHID
116 DIANA RWEZAULA
117 KATAVO SANGIWA
118 SANY SANYENGE
119 LUCY SAWE
120 GREGORY SELESTINE
121 ALLY SHEHE
122 AISHA SWALEHE
123 RIDJA UBWE
124 SAIDI USI
125 WINIFRIDA USOY
126 FILBERTH VALENTINE
127 UPENDO WAWA
128 RUBENI WILIUM
129 IDDI YAHAYA
130 IMAN ZADOCK
131 IBRAHIM ZAMBO
BACHELOR OF SCIENCE IN TAXATION

1 AUTA ABDALLAH
2 ABDUL ADIL
3 ANTHONY ADOLPH
4 SALUMU AJILI
5 AGUSTINE ALPHONCE
6 PASTORY ALPHONCE
7 JOSEPH ASHED
8 SIGFRID ASSENGA
9 ELIAS AUGUSTINO
10 KICHELE BAITA
11 TIMOTHEO BAJUNI
12 EMMANUEL BOAZ
13 CHONZA BUTOBO
14 MWITA CHACHA
15 JAMES CHALANDA
16 KULWA CHARLES
17 JAMES CHIDUO
18 JOSHUA DAUDI
19 JAMES DEOGRATIUS
20 DAVID DISMAS
21 PASCHAL EDWARD
22 MAURICE ENOCK
23 DICKSON EVARESTI
24 STEVEN FABIAN
25 ERICK FIDELIS
26 FROLIAN FREDRICK
27 JUMA GABRIEL
28 GULINJA GASPER
29 NICHOLAUS GIBOMA
30 SAYUNI GODFREY
31 YONATHAN GUMBO
32 CHRISOSTOME HAULE
33 ANAEL HUMPHREY
34 BAKARI IBRAHIM
35 JACOB ISAYA
36 TYSON JACOB
37 MUKSIN JAMAL
38 RENATUS JANUARY
39 SPIRO JASMIN
40 MUNA JINGU
41 DEVIS JOHNAS
42 ELIAZERY JONAS
43 JOVIN JOSEPH

FIRST NAME SURNAME
44 GEORGE JUBECK
45 FABIANI JUMA
46 KISAKA JUMA
47 GEORGE JUMAA
48 AMOS JUMANNE
49 VICTOR KADUVAGE
50 FIDEL KAGAYO
51 SULEIMAN KAHUMBU
52 PAUL KAJIRU
53 HERBERT KAJOBA
54 SAID KASUVI
55 EMIL KAVISHE
56 MARARA KEBOYA
57 FREDRICK KELLYA
58 JOCTAN KIBONDE
59 TUMAINI KIGANJA
60 CLEMENCE KIHWELE
61 ELIAKIM KILENGA
62 WINFRIDA KIMARO
63 MICHAEL KIMARO
64 OSCAR KISIPA
65 GERALD KOMBA
66 LAURENCE KOMBA
67 OSCAR KOMBA
68 FADHILI KULWA
69 ONOLASCO KUTIKA
70 PAMIM KYANDO
71 HUSSEIN LIKINGO
72 OLIVO LUHANGA
73 PATRICK LUYANGI
74 ISSACK MAFWENGA
75 ROBERT MAGANGA
76 CLEMENCE MAHENGE
77 MAWAZO MAKOBA
78 BRIAN MAPHURU
79 CONSTANTINE MAPUNDA
80 JOSHUA MAPUNDA
81 KURINGE MASAO
82 KELVIN MASSAWE
83 STEPHEN MATHIAS
84 SUZAN MDOE
85 DOMINICKY MELCKIHORY

FIRST NAME SURNAME
86 DANIEL MGAYA
87 AMIRI MHINA
88 JOHN MIGIRE
89 MAHUNGO MINGWA
90 SAMWEL MKALI
91 MGESI MKAMI
92 INNOCENT MLANGU
93 GOZBERT MMASSY
94 INOCENT MODESTI
95 JAMAL MOHAMED
96 YAHAYA MOHAMED
97 ERASTO MOREWA
98 COASTER MOSHA
99 SADICK MPENZWA
100 ALPHONCE MREMA
101 GODI MSAMBWA
102 ERASTO MSHANA
103 SYLVESTER MSOSSI
104 ERICK MSYALIA
105 STEPHANO MTAO
106 ANORD MTATIRO
107 DANFORD MTELEKE
108 GEOFREY MUBOFU
109 EDGAR MUMWI
110 WILBERTH MUNGO
111 PIERRE MUSHONGI
112 CALVIN MWAIPYANA
113 DEO MWAKILEMA
114 BERNADINO MWAMPOMA
115 ELIA MWANYILU
116 JOSEPH MWITA
117 RAMADHAN NAFASI
118 AMANI NASSARY
119 MKWAYU NDESEME
120 FRANK NDIMBO
121 CHARLES NGONYANI
122 AMANI NGUNYI
123 NDALAHWA NHAGA
124 GODLOVE NKYA
125 AMAN NZIKU
126 AMON OJODE
127 LOIPUKE OLEKUWAI
128 MUSA OTIENO
129 NAKAZA PETER
130 PAUL PETER
131 SALUMU RAMADHANI
132 SALUSTIAN RAYMOND
133 ALI SALUM
134 ALI SALUM
135 HANS SAMWEL
136 SAMWEL SANGA
137 SIMON SEBASTIAN
138 RAJAB SELEMANI
139 CHRISTIAN SENJE
140 KELVIN SHABAN
141 MUSSA SHABANI
142 SWAHIBU SHABANI
143 RASHID SHAIBU
144 ISIHAKA SHARRIF
145 HAJI SHAURI
146 EVANCE SIMON
147 NASSIR SONGORO
148 SALEH SULEIMAN
149 GEORGE SULUMO
150 PATRICK SWALE
151 BABUU TARIMO
152 RAMADHANI THABITI
153 DAVID THOMAS
154 THOMAS ULENDO
155 GODLOVE URIO
156 SAMWELI WAMBURA
157 ELISHA WARIOBA
158 JACKSON WELLA
159 TUMAINI WILBERT
160 BEST WILSON
161 EVANS YEGELLA
162 SALOME ALFAN
163 CECILIA ANTHONY
164 VAILETH AWICHI
165 JACQUELINE BENEDICT
166 ADELA BURCHARD
167 REBECCA BYARUFU
168 BHOKE CHACHA
169 HILDA CHACKY
FIRST NAME SURNAME
170 FRANSISCA CHARLES
171 RAHAB DANIEL
172 ANIPAE ELINIANGAZE
173 LEAH EMMANUEL
174 MELISA EPIMARCK
175 NASRA FUPE
176 PHYLIS GODWIN
177 ROZINA HENDRY
178 HERMETA HERMAN
179 ASHA JAMAL
180 MAIMUNA JUMA
181 FATIHIYA JUMANNE
182 BRIGITHA KAFANABO
183 ANETH KAGOSE
184 GLORY KAHUMBA
185 CHRISTER KEMANZI
186 GLORY KILAWE
187 SARAH KIMARO
188 GLADNESS KIMEI
189 RITHA KISANGA
190 JACKLINE KISSA
191 RACHEL KISSARH
192 IRENE KIWELU
193 HELLEN KOKA
194 FLORA LAIZER
195 SILVIA LAWRENCE
196 GLORIA LUMBUGU
197 HELLEN LUSINGU
198 NURU LWOGA
199 ESTHER MAKOTWE
200 JENIFER MAKUNDI
201 DORIS MARIWA
202 GLADNESS MASSAM
203 JACQUELINE MATUNDA
204 JOCELYN MBILINYI
205 ESTHER MBUYA
206 MGENI MBWANA
207 GLORY MELCHIOR
208 IRENE MGONHO
209 MARY MHINDI
210 ASTERIA MILLINGA
211 MWASI MLEKWANYUMA