JESHI LA POLISI LAPATA KASHIFA

Jeshi la Polisi limeingia
katika kashfa nzito baada
ya mkuu wake, Inspekta
Jenerali Said Mwema,
kuibiwa upanga wa
dhahabu ambao ni mali
ya Shirikisho la Wakuu wa
Majeshi ya Polisi wa nchi
za Kusini mwa Afrika
(SARPCCO).

Upanga huo wenye uzito
wa takriban kilo tatu na
wenye thamani ya zaidi ya
fedha za Tanzania Sh600
milioni, ni kielelezo kwa
nchi inayokabidhiwa
uongozi wa SARPCCO.

Mwaka jana Tanzania
ilikuwa mwenyekiti wa
SARPCCO, ambapo upanga
huo ulikabidhiwa kwa IGP
Mwema na Jenerali
Magwashi Victoria ‘Riah’
Phiyega, ambaye ni
Kamishna wa Taifa wa
Polisi wa Afrika Kusini
aliyekuwa amemaliza
muda wake kwa wakati
huo.

Hilo ni tukio la pili la wizi
la mali zinazohusu ofisi ya
IGP, ambapo mwaka jana
ndani ya ofisi hiyo
kuliibwa kompyuta ndogo
(laptop), ikiwa na taarifa
muhimu za kipolisi. Hadi
sasa hakuna taarifa za
kupatikana kwa kompyuta
hiyo.

IGP Mwema alikabidhiwa
upanga huo Septemba 5,
2012, katika mkutano saba
wa SARPCCO uliofanyika
Zanzibar na kuhudhuriwa
na wakuu wa majeshi ya
Polisi kutoka nchi 13,
pamoja na mashirika ya
kimataifa.

Upanga huo ambao
unakwenda sambamba na
bendera ya SARPCCO, ni
moja ya vielelezo vya nchi
iliyochaguliwa kuwa
Mwenyekiti wa shirikisho
hilo, ambaye moja kwa
moja anakuwa ni Mkuu
wa Jeshi la Polisi katika
nchi husika.

Kwa mujibu wa taratibu
za SARPCCO, vielelezo
hivyo hutakiwa kuwekwa
ofisini kwa kiongozi
husika, ikiwa ni alama ya
kila mgeni atakayeingia
ofisini hapo kutambua
uwepo wa wadhifa huo wa
kimataifa.

Uchunguzi wa gazeti hili
ulibaini kuwa IGP
aligundua kutoweka kwa
upanga huo wiki iliyopita,
wakati akijiandaa kwenda
kuukabidhi kwa
mwenyekiti mpya wa
SARPCCO, ambaye ni IGP
wa Namibia.

Taarifa za ndani ya jeshi
hilo zilibaini kuwa, IGP
alilazimika kuondoka bila
upanga huo alipokwenda
Namibia wiki iliyopita
kuhudhuria mkutano wa
nane wa SARPCCO,
uliofanyika Jumapili
iliyopita mjini Windhoek.

Kwa mujibu wa
uchunguzi, IGP Mwema
alikabidhi upanga
unaofanana na huo ambao
siyo wa dhahabu,
alioazimwa kutoka kwa
Mkuu wa Jeshi la Polisi la
Namibia, Inspekta Jenerali,
Luteni Jenerali Sebastian
Ndeitunga, na
kukabidhiwa kama ishara
ya kukabidhiwa uenyekiti
wa SARPCCO kwa kipindi
cha mwaka mmoja.

Uchunguzi ulibaini kuwa
IGP Mwema alitoa ahadi
ya kurejesha upanga halisi
ndani ya kipindi cha
mwezi mmoja, au Serikali
ya Tanzania italazimika
kutengeneza mwingine
kulipa uliopotea.

Uchunguzi wa gazeti hili
unaonyesha kuwa kashfa
hiyo ametupiwa Mkuu wa
Polisi Zanzibar, Kamishna
Mussa Ali Mussa pamoja
na dereva wake, ikidaiwa
kuwa upanga huo baada
ya kupokewa na IGP
Mwema, Septemba mwaka
jana uliwekwa kwenye
gari la kamishna huyo.

Kamishna Mussa ndiye
alikuwa Mwenyekiti wa
Kamati ya Maandalizi ya
Mkutano wa Saba, na pia
ofisa mwenyeji kwa
wajumbe wa mkutano huo
uliofanyika Zanzibar.

Hata hivyo, taarifa zingine
zilidai kuwa IGP Mwema
naye analaumiwa kwa
kutofuatilia kwa karibu
zana za kazi, kwani baada
ya kuupokea alitakiwa
kuhakikisha unakuwepo
ofisini kwake kama alama
ya uenyekiti wake.

Gazeti hili lilipowasiliana
kwa njia ya simu na Mkuu
wa Polisi Zanzibar,
Kamishna Mussa Ali
Mussa kuhusu madai hayo
alisema, kitara (upanga)
hicho ni kweli kimepotea,
lakini yeye hahusiki kwa
kuwa kila kitu kina
utaratibu wake.

“Ni kweli kitara
kilikabidhiwa kwa afande
IGP na mimi nilishuhudia
kikikabidhiwa, na ni kweli
kitara hakijulikani kiliko,
lakini mimi sihusiki na
kupotea kwake. Ni kweli
mimi nilikuwa ofisa
mwenyeji wa mkutano
huo, lakini siku hiyo
zilitolewa zawadi nyingi,
watu walipewa mikoba,
kwa hiyo mtu akipoteza
mkoba wake niulizwe
mimi?” alihoji Kamishna
Mussa.

Alisema kila kitu kina
utaratibu wake na
kwamba taarifa kwamba
yeye amehojiwa kutokana
na upotevu wa kitara
hicho au kuna kamati
imeundwa, hazina ukweli.

“Sijawahi kuona kamati
hiyo. Kamati hiyo kwanza
imeundwa na nani na
inatoka wapi? Hayo
maneno yanatengenezwa
na watu wa nje,” alisema
Kamishna Mussa.

Alisema kinachofanyika
hivi sasa ni kukitafuta ili
kiweze kurejeshwa
kunakohusika.

Taarifa zingine zilidai hata
bendera ya mezani ya
mwenyekiti wa SARPCCO,
aliyokabidhiwa sambamba
na upanga huo nayo kuna
hatihati ilipotea.

Msemaji wa Jeshi la Polisi
nchini, Advera Senso
alipotakiwa kuzungumzia
suala hilo alisema aulizwe
kamishina wa polisi
Zanzibar.

“Suala hilo muulize
Kamishina wa Zanzibar
ndiye anayejua,” alisema
Senso.

Uchunguzi unaonyesha
kuwa maofisa katika ofisi
ya IGP na ile ya Kamishna
wa Polisi Zanzibar,
wamehojiwa akiwamo
Kamishna Mussa, na
kwamba upelelezi mkubwa
umekuwa ukiendelea
ndani ya jeshi hilo.

Hata hivyo, juhudi za
gazeti hili za kutaka
kufahamu uamuzi wa
SARPCCO katika ofisi yake
ya uratibu iliyopo kwenye
ofisi za Makao Makuu ya
Kanda ya Polisi wa
Kimataifa (INTERPOL),
Harare, Zimbabwe,
hazikuzaa matunda baada
ya baruapepe iliyotumwa
kwa ofisa mratibu wa
SARPCCO ambaye pia ni
mkuu wa ofisi ya Kanda
ya INTERPOL, C. Simfukwe
kutopata majibu.

SARPCCO ilianzishwa
mwaka 1995, Victoria Falls,
Zimbabwe, lakini kisheria
ilitambulika rasmi mwaka
2006 na lengo lake kuu ni
kupambana na uhalifu wa
kuvuka mipaka.

Uenyekiti wake ni mwaka
mmoja, ambapo kwa sasa
mwenyekiti ni Mkuu wa
Jeshi la Polisi la Namibia
Inspekta Jenerali, Luteni
Jenerali Sebastian
Ndeitunga, aliyepokea
wadhifa huo kutoka kwa
IGP Mwema.


Source:Mwananchi

MONUSCO WAWACHARAZA M23

Waasi wa M23 Mashariki
mwa Jamuhuri ya
Kidemokrasia ya Congo
wamesema kuwa
watasitisha mapigano,
kufuatia makabiliano
makali na wanajeshi wa
serikali wanaoungwa
mkono na wanajeshi wa
Umoja wa Mataifa
ikiwemo JWTZ.


Afisa mmoja wa Kundi
hilo la M23 Museveni
Sendugo, ameiambia BBC
kuwa wanajeshi wake
tayari wamerudi nyuma
umbali wa kilomita tano
kutoka eneo la
mapigano.


Wengi wa wapiganaji wa
M23 ni wanajeshi
walioasi jeshi la serikali,
wengi wao wakiwa wa
kabila la Kitutsi sawa na
uongozi wa Rwanda.

Serikali ya DRC na Umoja
wa Mataifa
zimeishutumu serikali ya
Rwanda kwa kuwaunga
mkono wapiganaji wa
kundi hilo la M23,
tuhuma ambazo
zimekanushwa na
utawala wa Kigali.


Awali, katibu mkuu wa
Umoja wa Mataifa Ban
Ki-moon ametoa wito
kwa rais wa Rwanda,
kuwa mvumilivu huku
uhasama kati yake na
nchi jirani ya Jamuhuri
ya Kidemokrasia ya
Congo, ukiendelea
kutokota katika maeneo
ya mipakani.

Bwana Ban, alizungumza
na rais Paul Kagame
baada ya serikali yake
kuishutumu Congo, kwa
kufanya shambulio
katika ardhi yake
makusudi na kumuua
mama mmoja na
kumjeruhi mtoto wake.


Msaidizi wa katibu huyo
mkuu wa Umoja wa
Mataifa, amenukuliwa
akiiambia Umoja wa
Mataifa kuwa wapiganaji
wa kundi la waasi wa
M23, wameonekana
wakirusha makombora
wakilenga Rwanda.

Serikali ya DRC na Umoja
wa Mataifa zimeshutumu
Rwanda kwa kuwaunga
mkono waasi hao wa
M23, madai ambayo
yamepingwa vikali ya
utawala wa Kigali.


Wanajeshi wa Congo
wakishirikiana na
wanajeshi wa Umoja wa
Mataifa, wamekuwa
wakifanya mashambulio
dhidi ya waasi hao wa
M23 karibu na mpaka
wa Rwanda, tangu wiki
iliyopita.

Kikosi cha Umoja wa
Mataifa cha kutunza
amani nchini DRC,
Monusco, kiliimarishwa
zaidi pale wanajeshi elfu
tatu zaidi walipotumwa
nchini humo kupambana
na waasi hao.


Waziri wa mambo ya nje
wa Rwanda Louise
Mushikiwabo, amesema
mabomu na makombora
kumi na tatu yalirushwa
katika ardhi yake siku ya
Jumatano na mengine
kumi siku ya Alhamisi.
Waziri huyo amedai
kuwa kufikia sasa
wanajeshi hao wa Congo
wamefanya mashambulio
thelathini na nne nchini
Rwanda.

Amewashutumu
wanajeshi wa DRC kwa
kuwalenga raia wake na
kusisitiza kuwa kwa sasa
wanajiepusha kulipisa
kisasi lakini hawatasita
kujibu ikiwa uchokozi
huo hautakoma.


Msemaji wa jeshi la
Congo Kanali Olivier
Hamuli ameiambia BBC
kuwa jeshi lake haliwezi
kurusha makombora
kulenga maeneo
yanayokaliwa na raia.

''Waasi ndio wanaoweza
kufanya kitendo kama
hicho, wapiganaji wa
M23 na wala sio
wanajeshi wake ndio
waliokuwa katika eneo
ambalo makombora hayo
yalirushwa'' Alisema
Kanali Hamuli.


Matamshi hayo
yaliungwa mkono na
msaidizi wa katibu mkuu
wa Umoja wa Mataifa
Bwana Mulet ambaye
aliiambia Baraza la
Usalama la Umoja wa
Mataifa kuwa, wanajeshi
wake nchini DRC
walishuhudia wapiganaji
wa M23, wakirusha
makombora wakilenga
Rwanda na wala sio
wanajeshi wa Congo.

Takriban watu laki nane
wamekimbia makwaoi
nchini Congo tangu
waasi hao wa M23
kuanzisha mashambulio
katika eneo la Mashariki
mwa Congo Aprili
mwaka wa 20120.

-BBC

WATANZANIA 247 WASHIKIRIWA KWA KUHUSIKA NA DAWA ZA KULEVYA

WATANZANIA 247
wamekamatwa katika
nchi mbalimbali
duniani na
wanashikiliwa kwa
tuhuma za kukutwa
wakisafirisha dawa za
kulevya. Waziri wa
Nchi, Ofisi ya Waziri
Mkuu, Sera na Uratibu,
William Lukuvi, alisema
hayo jana alipokuwa
akijibu swali la mbunge
wa Viti Maalumu,
Catherine Magige
(CCM).

Katika swali hilo,
Magige aliitaka Serikali
ieleze ukubwa wa
biashara ya dawa za
kulevya nchini na ukoje
na kuhoji kama haioni
kuna tatizo katika
ukaguzi wa abiria na
mizigo kwenye viwanja
vya ndege wanakopita
watuhumiwa.
Mbunge huyo pia
aliitaka Serikali, ieleze
imefanya juhudi gani
za kukabiliana na hali
ya upitishwaji wa dawa
hizo.
Akijibu swali hilo,
Lukuvi alisema ukubwa
wa biashara hiyo
nchini, unadhihirishwa
na idadi hiyo ya
watuhumiwa
Watanzania
wanaoshikiliwa nje ya
nchi kuanzia 2008 hadi
Julai 2013.
Mbali na Watanzania
hao nje ya nchi, Lukuvi
alisema nchini kuna
wageni wapatao 31
wanaoshikiliwa
mahabusu katika
magereza ya Keko na
Ukonga.
Baada ya kutoa
ufafanuzi huo, Mbunge
wa Karatu, Mchungaji
Israel Natse
(Chadema), aliomba
kuuliza swali la
nyongeza ambapo
aliitaka Serikali kutaja
kwa majina wahusika
katika biashara ya
dawa za kulevya.
Akijibu swali hilo,
Lukuvi alisema kazi ya
Serikali si kutaja
majina, bali kuyapokea
na kuyafanyia
uchunguzi na mwisho
kuchukua hatua za
kisheria.

"Si kazi ya Serikali
kutaja wahusika
bungeni, lakini
tunachofanya kwa
ambao wanatajwa ni
kuwapeleka katika
vyombo husika na
kuendelea na
uchunguzi na
wakithibitika ndipo
wanatajwa na
kuchukuliwa hatua.
"Tukisema tuwataje,
hata humu ndani
wabunge wote
watakwisha maana
wako kwengi
wanaotajatajwa. Hata
gazeti la Jamhuri
limetaja maana
wenzetu wanao
ushahidi nao, na wale
wasioridhika wanaweza
kwenda kushitaki.
Hivyo walio na majina
na vielelezo watuletee
ili tuwashughulikie.
Baadhi ya wabunge
walionekana kuguna na
kuzomea pale Lukuvi
alipokuwa akitoa
ufafanuzi wa suala
hilo, jambo
lililomfanya Spika Anne
Makinda, kukemea hali
ya zomeazomea ndani
ya Bunge.

Hivi karibuni, vita dhidi
ya dawa za kulevya,
imekuwa gumzo baada
ya Waziri wa Uchukuzi,
Dk Harrison
Mwakyembe kuapa
kuzuia uchochoro wa
kupitisha dawa hizo
katika Uwanja wa
Ndege wa Kimataifa wa
Julius Nyerere.
Kwa kuanzia, Dk
Mwakyembe alitaja
maofisa alioagiza
wafukuzwe kazi na
kufunguliwa mashitaka
ya jinai chini ya Sheria
ya Kuzuia Dawa za
Kulevya, kwa tuhuma
za kupitisha dawa za
kulevya katika uwanja
huo.
Maofisa hao ni pamoja
na Maofisa Usalama,
Yusufu Daniel Issa,
Jackson Manyonyi,
Juliana Thadei na
Mohamed Kalungwana.
Mbali na maofisa hao,
pia aliagiza Jeshi la
Polisi kumwondoa
mara moja katika
uwanja huo, askari
Polisi, Koplo Ernest na
kumchukulia hatua za
kinidhamu kwa
kushiriki kwake kwenye
njama za kupitisha
mabegi sita ya dawa za
kulevya, yaliyokamatwa
Afrika Kusini.

Pia alisema Polisi
inapaswa kumsaka
Nassoro Mangunga,
aliyekwepa vyombo vya
Dola vya Afrika Kusini
na kutoroka na mabegi
matatu ya dawa hizo.

Dk Mwakyembe alisema
mbeba mizigo katika
uwanja huo, Zahoro
Seleman, anapaswa
kufukuzwa kazi,
kukamatwa na
kufunguliwa mashitaka,
ili aunganishwe na
wenzake kujibu
mashitaka ya jinai.

Dk Mwakyembe pia
aliiagiza Idara ya
Usalama wa Taifa
kuendesha uchunguzi
wa kina kwa maofisa
wake waliokuwa zamu
siku ya tukio, kwa
kuchelewa kufikisha
mbwa wakati mwafaka
kukagua mabegi hayo
na kuliletea Taifa
fedheha kubwa.











ARSENAL YAINGIA MIAKA 16 MFURULIZO LIGI YA MABINGWA ULAYA

Aaron Ramsey alifunga
mabao mawili na kuipa
klabu yake Arsenal ushindi
wa wazi bila upinzani mkali
dhidi ya Fenerbahce ya
Uturuki.

Katika mechi iliyochezwa
hapo jana kwenye uwanja
wa Emirates, Arsenal
imefuzu kwa Ligi ya
Mabingwa kwa mwaka wa
kumi na sita mfululizo.
Wageni Fenerbahce walibaki
nyuma tangu mechi ya
awamu ya kwanza
walipofungwa mabao
matatu kwa bila na Arsenal.

Adhabu hiyo kwa
Fenerbahce imerahisisha
kazi ya shirika la kandanda
la Uropa, UEFA, kwani sasa
haitajishughulisha kuizuia
klabu hiyo kutoshiriki mechi
ya ligi za mabingwa, hii
inafuatia marufuku ya
miaka miwili ambayo inafaa
kutolewa kwa Fenerbahce
baada ya kushtumiwa na
hatia ya kupanga mechi.
Ikiwa klabu hiyo ingefaulu
kushiriki Ligi ya Mabingwa
basi kingekuwa kibarua
kigumu kwa UEFA kutekeleza
sheria na adhabu ipasavyo.

Hii leo jumatano,
mahakama ya rufaa
itasikiliza kesi hiyo.
Arsenal imewahi kushindwa
na timu za Uropa mara
mbili tu katika muda wa
miaka hamsini, huku klabu
hiyo ya Uturuki imepata
kufunga mabao mara tatu tu
katika ziara zake nane za
England.




WANAFUNZI WAFELI SEKONDARY NCHI NZIMA.

Kwa mara ya kwanza katika
historia ya Liberia,
wanafunzi wote wamefeli
mtihani wao wa mwisho wa
sekondari na hivyo
kumaanisha kuwa hakuna
hata mmoja ambaye atafuzu
kuingia chuo kikuu.

Waziri wa elimu wa Liberia
amesema ameshinda
kufahamu ni kwa nini
hakuna wanafunzi hao
wamefeli kiasi hicho.

Zaidi ya wanafunzi elfu
ishirini na watano
walianguka mtihani huo
ambao ungewapa fursa ya
kujiunga na chuo kikuu cha
Liberia ambacho ni moja ya
vyuo vikuu vinavyoendesha
na serikali.

Lakini wasimamizi wa chuo
hicho wameiambia BBC
kuwa wanafunzi hao
hawakuwa makini na
ufahamu mzuri wa lugha ya
Kiingereza ambayo
ilitumiwa kuwatahini.

Taifa la Liberia linaendelea
kujinasua kutokana na
athari za mapigano ya
wenyewe kwa wenyewe
yaliyomalizika zaidi ya
miaka kumi iliyopita.

Rais wa Liberia, Ellen
Johnson Sirleaf, ambaye pia
ni mshindi wa tuzo ya
amani ya Nobel, amekiri
kuwa mfumo wa elimu
nchini humo bado ungali
duni na unahitaji
marekebisho ya dharura.
Mwandishi wa BBC mjini
Monrovia, anasema shule
nyingi nchini humo havina
vifaa vya kimsingi na
waalimu waliohitimu.

Lakini hii ni mara ya kwanza
katika historia ya taifa hilo
kwa wanafunzi wote kufeli
mtihani huo licha ya kulipa
ada ya usajili ya dola
ishirini na tano.

Chuo hicho kikuu ambacho
kina idadi kubwa ya
wanafunzi hakitakuwa na
wanafunzi wa mwaka wa
kwanza wakati muhula mpya
utakapoanza mwezi ujao.
Lakini wanafunzi wengi
wanasema hawajaamini
matokeo ya mtihani huo na
waziri wa Elimu Etmonia
David-Tarpeh, ameiambia
BBC kuwa anatarajia
kukutana na wasimamizi wa
chuo hicho ili kujadili suala
hilo

FUNDI BAISKEL AMNAJISI MTOTO

Fundi baiskeli mmoja
mkaazi wa mtaa wa
Nsemlwa, wilaya ya
Mpanda, mkoa wa
Katavi, Athumani
Mussa (54) amefikishwa
jana katika Mahakama
ya Hakimu Mkazi ya
Wilaya ya Mpanda kwa
tuhuma za kumlawiti
(kunajisi) mdomoni
mtoto msichana (4)
baada ya kumdanganya
kumpatia mdoli wa
kuchezea.

Mtuhumiwa alifikishwa
mahakamani hapo na
kusomewa mashitaka na
mwendesha mashitaka
mkaguzi wa msaidizi wa
polisi Razalo Masembo
mbele ya Hakimu mkazi
mfawidhi wa Mahakama
ya Wilaya ya Mpanda
Chiganga Ntengwa.

Mwendesha mashitaka
aliiambia mahakama
kuwa mshitakiwa
Athumani Musa alitenda
kosa hilo Julai 24
mwaka huu majira ya
saa 12 jioni nyumbani
kwake katika mtaa wa
Nsemlwa mjini hapa.
Mtuhumiwa anadaiwa
kuwa siku hiyo ya tukio
alimwona mtoto huyo
akiwa na wenzake
wakicheza barabarani
karibu na
nyumbani kwake
ndipo alipomwita mtoto
huyo na kumwambia
amfuate nyumbani
kwake ili akampe mdoli
wa kuchezea. Mara
baada ya mtoto huyo
kuingia ndani,
mtuhumiwa alianza
kumnajisi mtoto huyo
mdomoni huku
akiwaamekaa kwenye
kochi lake sebuleni.
Ilidaiwa kuwa licha ya
mtoto huyo kupiga
mayowe ya kuomba
msaada, mtuhumiwa
hakujali mayowe ya
mtoto huyo bali
aliendelea na shughuli
yake hadi hapo
alipomaliza haja yake.

Mwendesha
mashitaka alidai kuwa
mtoto huyo alipotoka
nyumbani kwa
mtuhumiwa
alielekea nyumbani kwa
mama yake huku
akilia kwa sauti
kubwa, hali
iliyosababisha watoto
wenzake wamfuate kwa
nyuma.

Masembo alieleza mara
baada ya kufika kwa
mama yake na kuulizwa
analia nini, mtoto huyo
alitema mdomoni mbele
ya mama yake shahawa
akimweleza mama
yake alichofanyiwa na
fundi baiskeli, Musa.
Mama wa mtoto
huyo aliangua kilio na
kufanya majirani
wakusaniyike na ndipo
alipowasimulia mkasa
huo.

Majirani hao walichukua
jukumu la kwenda
kumkamata
mtuhumiwa wakiwa
wameongozwa na mtoto
huyo ambaye alikataa
kuingia ndani ya
nyumba ya mtuhumiwa
kwa kudai anaogopa
kunajisiwa tena na
mtuhumiwa.

Mtuhumiwa
Athumani Musa alikana
shitaka hilo na Hakimu
Mkazi Mfawidhi,
Chiganga Ntengwa
aliamuru mshitakiwa
apelekwe rumande hadi
Septemba 2 kesi yake
itakaposikilizwa.







POLISI FEKI WENGINE 7 WAKAMATWA.

SIKU chache baada ya
kukamatwa kwa askari
feki wa usalama
barabarani, Polisi Kanda
Maalumu ya Dar es
Salaam, imewakamata
watuhumiwa saba wa
ujambazi, wakiwa na
sare za Polisi, huku
mwingine akijifanya
ofisa Usalama wa Taifa.

Akizungumza na
waandishi wa habari
ofisini kwake jana,
Kamanda wa Polisi
Kanda Maalumu ya Dar
es Salaa, Suleiman Kova
alisema watuhumiwa
hao walikamatwa
wakiwa na sare za Polisi
jozi mbili.

Watuhumiwa hao ni
Khamis Mkalikwa (40),
Magila Werema (31),
Nurdin Bakari (46),
Materu Marko (32), Louis
Magoda (34), Amos Enock
(23) na Amiri
Mohammed (45), wote
wakazi wa jijini Dar es
Salaam.

Sare hizo, kwa mujibu
wa Kamanda Kova, ni
zenye cheo cha Sajenti
wa Kituo, huku jozi moja
ikiwa na jina
linalosomeka SSGT A.M
Mduvike.

Watuhumiwa hao
walikamatwa jana katika
eneo la Kiluvya, baada
ya askari kuweka mtego,
ambao ulifanikiwa
kuwanasa.

Alisema watu hao
walikuwa wakitumia
silaha, sare za jeshi la
Polisi na redio ya
mawasiliano katika
uhalifu wao na hivyo
kuwafanya baadhi ya
watu kutupia lawama
Jeshi la Polisi kwa
kujihusisha na uhalifu.
Alisema watuhumiwa
hao, wanahusishwa na
uhalifu katika maeneo ya
Boko, Tegeta, Mbweni,
Bahari Beach, na maeneo
mengine ya jiji. Alisema
watu hao ni hatari zaidi.
Watuhumiwa hao
walikuwa wakitumia gari
aina ya Cresta GX, 100
yenye namba T 546 BWR
na baada ya kuona
wamezingirwa na askari
maeneo hayo, walifyatua
risasi moja hewani,
lakini askari
walipambana nao na
kufanikiwa kuwakamata.
“Mbali na vitu hivyo pia
wamekamatwa na
bastola moja aina ya
Brown yenye namba
B.3901, ambayo ilikuwa
na risasi nne na ganda
moja, tunawashikilia
kwa upelelezi na baada
ya kukamilika
watafikishwa
mahakamani,” alisema
Kova.

Katika hatua nyingine,
Kamanda Kova alisema
wanamshikilia
mtuhumiwa Alquine
Masubo (42) maarufu
kama Claud, kwa kosa la
kujifanya ofisa wa
Usalama wa Taifa.
Claud ambaye ni mkazi
wa Yombo Buza,
alikamatwa akiwa na
vielelezo mbalimbali
pamoja na nyaraka za
idara hiyo, ambapo
baada ya kuhojiwa
alikiri kuwa yeye si
mfanyakazi wa idara
hiyo.

Kova alisema
mtuhumiwa huyo
alipopekuliwa zaidi,
alikutwa na bastola aina
ya Browing yenye namba
A. 956188-CZ83 ikiwa na
risasi 12 ndani ya kasha
lake.
“Alipopekuliwa
nyumbani kwake
alikutwa na bastola
nyingine aina ya
Maknov yenye namba
BA4799 ikiwa na risasi 19
na kitabu cha mmiliki
chenye namba CAR
00071678, ikiwa na jina
la P.1827 LT COL
Mohammed Ambari,
jambo ambalo
haliwezekani kwa mtu
mmoja kumiliki silaha
mbili,” alisema Kova.
Mtuhumiwa huyo pia
alikutwa na kitambulisho
cha Jeshi la Wananchi
Tanzania (JWTZ) chenye
namba 7001- E. 1075 na
kompyuta mpakato aina
ya Toshiba.

“Huyu ni tapeli wa siku
nyingi na taarifa zake
tulikuwa nazo, anatumia
kivuli cha idara ya
usalama wa taifa
kufanya utapeli, lakini
sasa ndiyo mwisho wake
na wananchi wamjue”
alisema.

-Habari leo

WANYARWANDA WAENDELEA KUICHOKONOA TANZANIA NA RAIS KIKWETE

Mtandao  wa  News  of  Rwanda  umeendelea  kutuchokonoa  watanzania  ili  kuupima  msimamo wetu..... Baada  ya  kukurupa  na  madai  kwamba  Rais  Kikwete  si  mtanzania  halisi  na  kwamba  ni  mtu  mwenye  asili  ya  Burundi, mtandao  huo  umekuja  na  kioja  kipya....Taarifa  iliyotolewa  jana  tarehe  19/08/2013  na  mtandao  huo  inadai  kwamba  mke  wa  Rais  Kikwete  aitwaye  Mama  Salma  Kikiwete  ni   mnyarwanda   wa  kabila  la  wahutu (mhutu).. Katika  maelezo  yake, mtandao  huo  umeenda  mbali  na  kudai  kuwa  Mama  Salma  Kikwete  ni  binadamu  wa  rais  wa zamani wa Rwanda, Juvenal Habyarimana  na  ndo  maana  rais Kikwete  alitoa  ushauri  wa   mazungumzo  ya  amani  kati  ya  Kagame  na  waasi.
Hiki ndicho kilichoandikwa na mtandao huo.

New details obtained byNews of Rwandamay give insight into why Tanzania’s President Jakaya Kikwete came out as the sole global leader sympathetic to Rwandan FDLR rebels based in DR Congo jungles since 1994.
According to secret US State Department cables published by whistle-blowing site Wikileaks, President Jakaya Kikwete’s wife fondly known in Tanzania as “Mama Salma Kikwete” is a cousin of former Rwanda leader Juvenal Habyarimana. The shocking details are contained in a cable sent to Washington on Thursday May 5th, 2005, by Shabyna Stillman, a seniordiplomat at the US embassy in Dar es Salaam.
The US embassy was giving update on the selection of Mr Jakaya Kikwete to be the CCM flag-bearer in the presidential election late thatyear. “For years, observers of the Great Lakes conflicts have considered Kikwete to be virulentlypro-Hutu,” reads the cable, in part.

“Kikwete’s marriage to a cousin of former Rwandan President Juvenal Habyarimana may have fueled these rumors, which are now fadingas the Burundi conflict winds down,” adds the cable, signed by Stillman.
According to the US embassy, Mr Kikwete’s love affair with “Hutus” could be seen in his spirited support for Burundian rebels at thetime fighting former President Pierre Buyoya.Since 1995, up until 2005 when Mr.Kikwete was foreign affairs ministerof Tanzania, rumours have swelled around him suggesting he sided massively with the ethnic extremistestablishment.

It is this system thatplanned and executed the genocideagainst Tutsis in 1994, and fled across to Zaire and other parts of the world. It is alleged, around 1996, Mr Kikwete suggested publicly that “Hutus” need to be armed to fight off the government in Kigali at the time. A book published by virulent critic of President Paul Kagame and historian Gérard PRUNIER writes that Tanzania did offer to train troops for Seth Sendashonga.

A former leader of the Rwanda Patriotic Front (RPF), for whom he was a minister in the government set up after the rebel movement’s victory over the army and the militias responsible for the genocide in 1994, Mr. Sendashonga was murdered in Nairobi, Kenya, on16 May 1998 by,
according to PRUNIER, “unknown assailants.

”Fast forward to May 26, 2013, President Jakaya Kikwete goes public with a suggestion that the government of President Kagame in Rwanda negotiates with rebels ofthe Democratic Forces for the Liberation of Rwanda (FDLR).

The group was formed in May 2000, butits members had been roaming DRC forests ever since they lost power in Kigali. The suggestion by a head of state ofTanzania, a country that had long been considered a friendly nation to Rwanda, caught many by surprise. Since then, the two countries are embroiled in a bitter war of words.

The ex-Rwandan Juvenal Habyarimana died on the evening of April 6th, 1994, after his plane was shot down by extremist members of inner circle who did not want the peace talks with the RPF rebels. In the same plane was Burundian counterpart Cyprien Ntaryamira and French pilots.
The death of the French crew has been the centre of legal battles in France and the United States. A French judicial inquiry did confirm that the plane was brought down bya missile fired from a military camp next to Habyarimana’s home near the airport.

MTAWA ASHAMBULIWA ZANZIBAR

Habari nilizozipata punde kutoka Zanzibar zinasema Mtawa Mkatoliki ameshambuliwa na kuumizwa vibaya Visiwani Zanzibar jirani kabisa na alipopigwa risasi Padri Mushi na kuuawa.

Chanzo ni mbwa wa masista kumng'ata kuku wa majirani. Ndipo kundi la vijana wenye mapanga na marungu wakamvamia mtawa na kumuumiza.-

Chanzo: Mwandishi wetu wa Zanzibar(Jamii forum)

MWINGINE ADAKWA NA DAWA ZA KULEVYA

Habari ambayo imeripotiwa naITV inadai kwamba baada ya siku moja ya ziara ya kushtukiza ya Waziri wa uchukuzi Dk. Harison Mwakyembe kwenye uwanja wa ndege wa kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar-es-Salaam, kiasi kikubwa cha dawa za kulevya kimekamatwauwanjani hapo katika harakati za kusafirishwa kwenda nchi zanje.

Aliekamatwa ni kijana ambae alikua anazisafirisha hizo dawa zikiwemo bangi pia akielekea nchini Italia.

MWAKYEMBE AAGIZA WAFANYAKAZI AIRPORT WATIMULIWE

Waziri wa Uchukuzi, Dkt. Harrison Mwakyembe ametoa agizo kwa Mamlaka ya Viwanjavya Ndege (TAA) kuwafukuza kazi na kuliagiza jeshi la Polisi nchini kuwaunganisha na wengine kwenye kesi mahakamani ili kujibu mashitaka ya jinai, wale wote waliohusika katika kuuwasaidia Agness Gerald na mwenziye Mellisa Edward kupitisha dawa za kulevya ainaya Crystal Methamphetamine"TIK" au "Meth" au "USAN" kilogramu 180 kuelekea Afrika Kusini Julai 5, ambako walikamatwa katika kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha O.R. Tambo nchini humo.

Waziri Mwakyembe ametoa agizo hilo leo, ofisini kwake, mbele ya waandishi wa habari wakati alipowaita ili kuufahamisha umma kuhusu hatua zilizochukuliwa na Wizaayake kuhusu suala la dawa za kulevya.
Waliofukuzwa ni Koplo Ernest,Yusuph, Jackson, Juliana Tadei na Mohamed ambao walihusika katika kuwasaidia Agnes Gerald (Masogange) na mwenzake Mellisa kupitisha dawa za kulevya kuelekea Afrika Kusini ambako walikamatwa

VODACOM WATOA TAARIFA JUU YA KUKATIKA NETWORK

TAARIFA KUTOKA VODACOM KUHUSU
TATIZO LA MTANDAO

Moto uliozuka leo katika mitambo ya
kuendesha mtandao (switch) wa
Vodacom umezimzwa jioni hii.

Akizungumza jioni hii Afisa Mkuu wa
Mawasiliano wa Vodacom, Georgia
Mutagahywa alisema moto huo
ulipelekea kusimama kwa huduma
zote za kampuni hiyo.

"Tunawaomba radhi wateja wetu wote
kutokana na usumbufu wa kukosa
mawasiliano uliosababishwa na
kuungua kwa vifaa muhimu vya
kuendesha mitambo yetu.

Ninapenda
kuwahakikishia kwamba wataalam
wetu wanafanya kila jitihada
kurudisha mawasiliano ya mtandao
wa Vodacom haraka iwezekanavyo,"

MAGENGE YASABABISHA YULE KUFUNGWA

Ongezeko la fujo na ghasia za
magenge imesababisha maafisa wa
elimu nchini Afrika kusini kufunga
kwa siku mbili shule 16 katika jimbo
la Magharibi la Cape.

Angalau watu 50 wameripotiwa
kujeruhiwa au kuuwawa baada ya
kupigwa risasi katika eneo la
Manenberg katika siku za hivi
karibuni.

Waziri Mkuu katika jimbo hilo Bi
Helen Zille ameiomba serikali kuu
kuepeka jeshi katika eneo hilo kwani
polisi wameshindwa kukabiliana na
fujo hizo za magenge.

Msimamizi katika shule mmoja eno
hilo alifariki baada ya kupigwa risasa
wiki moja iliyopita.

Uamuzi wa kufunga shule
ulichukuliwa baada ya walimu
kulalamika kwamba wanahofia
maisha yao.

Bi Aysha Ismail, ambaye ni mama ya
mmoja wa waathiriwa alisema kuna
haja ya polisi zaidi kuweko katika
eneo hilo la Manenberg,ili
kupunguza visa vya utovu wa
usalama.

Mama huyo alisema mtoto wake wa
kiume alipigwa risasi katika mahali
ambapo kwa kawaida watoto hucheza
kila siku.

Marafiki zake wanasema
kijana huyo alikuwa mwanachama wa
genge linalojulikana kama Amerika
na ambalo linahangaisha watu sana
eneo hilo.

PONDA ASOMEWA MASHITAKA AKIWA MOI

MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu, jana ilihamia kwa muda katika Taasisi ya Tiba ya Mifupa na Upasuaji wa Mishipa ya Fahamu (MOI), ambapo Katibu wa Jumuiya na Taasisi za Kiislamu, Shekhe Issa Ponda, alisomewa mashitaka ya kuhamasisha vurugu maeneo tofauti nchini.

Ponda aliyelazwa katika wodi maalumu hospitalini hapo, alisomewa mashitaka hayo na Mwendesha Mashitaka, Tumaini Kweka, mbele ya Hakimu Mkazi, Hellen Riwa. Hata hivyo waandishi wa habari hawakuruhusiwa kuingia ndani ya chumba hicho, agizo lililotolewa naaskari Polisi.

Hoja za PondaKwa mujibu wa hati ya mashitaka, ambayo waandishi wa habari walipewa na Wakili wa Shekhe Ponda, Juma Nassoro, kiongozi huyo anadaiwa kutenda kosa hilo kwa nyakati tofauti kati ya Juni 2 hadi Agosti 11 mwaka huu, katika maeneo ya Zanzibar, Dar es Salaam na Morogoro.

Akizungumza nje ya chumba cha muda cha Mahakama hospitalini hapo, Wakili Nassoro alidai kuwa watapinga mashitaka hayo, kwa kuwa baadhi ya siku zilizotajwa zinautata, ikiwemo Agosti 11 aliyodai kuwa siku hiyo Shekhe Ponda alikuwa amelazwa hospitalini akiuguza majeraha.

“Tumepanga kwenda kupinga mashitaka hayo siku ya kusikilizwa kwa kesi hiyo…ukiangalia hati ya mashitaka ina upungufu wa mambo mengi, na kwa bahati mbaya wakati akisomewa mashitaka hayo, sisi hatukuwepo ndani ya chumba hicho,” alidai Wakili Nassoro.

Kwa mujibu wa madai ya Wakili wa Ponda, kesi hiyo ilisomwa muda mfupi baada ya wao kutoka nje ya hospitali hiyo, kwa kudhani kama siku imepita.

Alidai pia mashitaka hayo yalisomwa kwa mteja wake, katika muda ambao saa za kazi zilikuwa zimekwisha, hatua aliyodai kuwa niukiukwaji wa sheria na wanajiandaakutumia hoja hiyo pia kupinga mashitaka hayo mahakamani. Hata hivyo baada ya mashitaka hayo kusomwa, Wakili Nassoro alidai aliwahi kuomba mteja wake asiondolewe hospitali hapo, kwa madai kuwa bado hali yake si nzurimbali na maumivu aliyonayo katika eneo la bega la kulia.

Ulinzi Ulinzi katika eneo hilo ulikuwa wa kutosha, huku magari matano ya Polisi yaliyokuwa yamebeba askari wa kutuliza ghasia, yakiwa katika eneo hilo tayari kwa kulinda usalama. Pia kulikuwepo gari maalumu lililokuwa limeandaliwa tayari kumbeba Shekhe Ponda.

Zaidi ya wafuasi 100 walijitokeza hospitalini hapo wakati mahakama ikiendelea na shughuli zake, hali iliyosababisha msuguano wa hapa na pale na polisi waliokuwa wakizuia wafuasi hao kwenda kumsalimia kiongozi huyo.

Mmoja wa watu waliozuiwa na polisi alipofika kumuona Shekhe Ponda wakati kesi ikiendelea, ni wakili maarufu, Profesa Abdallah Safari.Shekhe alilazwa Muhimbili baada ya kujeruhiwa bega la kulia inadaiwa katika jaribio la Polisi kutaka kumkamata mkoani Morogoro.

Hata hivyo uchunguzi wa wataalamu wa taasisi hiyo, alikolazwa Shekhe Ponda ambako alifanyiwa upasuaji upya, ulishindwa kubaini kilichomjeruhi.

“Kutokana na tiba ya awali aliyopewa, ikiwa ni pamoja na kushonwa jeraha kabla ya kufikishwa Moi, imekuwa vigumu kujua jeraha lilisababishwa na kitu gani,” taarifa ya taasisi hiyo ilieleza.

Mbali na kutojua kilichomjeruhi Ponda, Msemaji wa Moi, Jumaa Almasi, aliripotiwa akisema hali ya Shehe Ponda anaendelea vizuri, ikilinganishwa na alivyokuwa kabla ya kufikishwa hospitalini hapo Jumapili iliyopita.

Chanzo:Habarileo

DAKTARI AIBA DAWA ZA KULEVYA AINA YA HEROINE TUMBONI KWA MGONJWA

Polisi nchini Urusi wamemzuilia
daktari mmoja mpasuaji kwa madai
ya kuiba kifuko kilichokuwa na dawa
ya kulevya ya Heroin kutoka tumboni
mwa mgonjwa.

Polisi katika eneo la Siberian
walimtaka daktari kumfanyia upasuaji
mshukiwa ili waweze kunasa dawa
hiyo ambayo mgonjwa alikuwa
ameimeza.

Hata hivyo polisi
waligundua kuwa seheme ya dawa
hiyo iliyotolewa tumboni mwa
mshukiwa ilikuwa inakosekana
Maafisa wa utawala wanadai kuwa
daktari huyo alikuwa mlevi
walipomkamata.

Huenda akafungwa
jela kwa miaka 15 ikiwa atapatikana na
hatia ya wizi wa dawa za kulevya.

44 WAUWAWA MSIKITINI KWA KUPIGWA RISASI

Takriban waumini 44 wameuawa kwa
kupigwa risasi wakiwa msikitini
Kaskazini Mashariki mwa Nigeria, kwa
mujibu wa maafisa wa jimbo la
Borno.

Mauaji hayo yalifanyika wakati wa
maombi ya asubuhi Jumapili , ingawa
taarifa zimejitokeza Jumatatu ,
kutokana na hitilafu ya mawasiliano
kwani jimbo hilo liko chini ya sheria ya
hali ya hatari.

Shambulizi lilifanyika katika mji wa
Konduga, ulio umbali wa kilomita 35
kutoka mji mkuu wa jimbo hilo ,
Maiduguri.

Washambulizi wanasemekana kuwa
wanachama wa kundi la wapiganaji la
Boko Haram, ambalo liliwaua maelfu
ya watu tangu mwaka 2009.

Gazeti la Daily Post, liliripoti kuwa
watu wengine 26 walikuwa
wanatibiwa kwa majeraha waliyopata
wakati wa shambulizi hilo hospitalini
Maiduguri.

Mwanachama wa kikundi cha vijana
kinachotoa ulinzi kwa raia, aliambia
shirika la habari la Associated Press,
kuwa wapiganaji wao wannne
waliuawa walipojaribu kutoa kilio cha
kutaka usaidizi.

Raia wengine kumi na wawili,
waliuawa katika kijiji cha Ngom
kinachopakana na Maiduguri.

Rais Goodluck Jonathan alitangaza
sheria ya hali ya hatari katika majimbo
matatu Kaskazini Mashariki mwa nchi
mnamo mwezi Mei wakati wanajeshi
walipofanya operesheni dhidi ya
wapiganaji wa kiisilamu.

Boko Haram linapigania eneo la
Kaskazini mwa nchi likitaka kujitawala
kwa kutumia sheria za kiisilamu.

Mwandishi wa BBC mjini Lagos,
anasema kuwa wakati kundi hilo
limekuwa likishambulia makanisa, pia
limekuwa likishambulia misikiti.

Habari za mashambulizi hayo
zilijitokeza wakati kanda ya video ya
kiongozi wa kundi hilo Abubakar
Shekau, ilipotolewa akidai kundi hilo
kuhusika na mashambulizi hayo
ikiwemo kushambulizi dhidi ya vituo
vya polisi na kambi za jeshi.

JESHI LA POLISI LAKANUSHA UVUMI JUU YA SHEIKH PONDA KUPIGWA RISASI

Jeshi la Polisi mkoani Morogoro limekanusha kumpiga risasi Katibu wa
Jumuiya ya Taasisi za Kiislam Sheikh Ponda Issa Ponda.

Kamanda wa Polisi mkoani Morogoro ACP Faustine Shilogile amesema
polisi walikwenda kumkamata lakini kwa kusaidiwa na wafuasi wake
aliwatoroka na hawajui alipo. Jeshi hilo bado linamsaka na halina
taarifa kama yupo hai au la.

WAINGEREZA WAFANYIWA MBAYA HUKO ZANZIBAR.

Polisi katika kisiwa cha Zanzibar
wamesema wanawake wawili wa
Uingereza wamerushiwa maji ya Acid
katika nyuso zao baada ya kuvamiwa
mwendo wa usiku.


Naibu kamishna wa polisi amesema
kuwa wanaume wawili waliwatendea
wanawake hao Katie Gee na Kirstie
Trup, wote wenye umri wa miaka 18
kutoka London,kitendo hicho
walipokuwa wakitembea katika
barabara za mji wa kihistoria wa
zanzibar.

Wanawake hao ni walimu wa kujitolea
wakifanya kazi kisiwani humo
Amesema kuwa polisi tayari
wameanzisha msako dhidi ya
wanaume hao.

Katika taarifa yake shirika la usafiri la i-
to-i nchini Uingereza lilisema kuwa
wanawake hao wameondoka
hospitalini.


Kwa upande wake wizara ya mambo
ya ndani Uingereza ililezea wasiwasi
kuhusu mashambulizi dhidi ya raia
wake na kuwa tayari imetoa msaada
kwao kupitia kwa ubalozi wake.

Wanawake hao, wanasemekana
kufanyia kazi shirika moja la kujitolea
na nia ya shambulizi hilo haijulikani.


Polisi wanasema kuwa wanawake hao
wenye umri wa miaka 18 walikuwa
wakitembea katika mji wa Mawe
kisiwani Zanzibar ambao ni kivutio
kikuu cha utalii kisiwani humo, wakati
wanaume wawili waliokuwa
wamepanda piki piki
walipowamwagia Acid kwenye
mikono, vifua na nyuso zao.


Wanawake hao walipelekwa kwa
ndege hadi Dar es Salaam ambako
walipokea matibabu.
Afisa wa wizara
ya afya amesema kuwa majeraha yao
si ya kutishia maisha.


Polisi wa Zanzibar wamesema ni mara
ya kwanza kwa raia wa kigeni
kushambuliwa kwa namna hiyo na
kwamba wanawasaka wahusika.


Zanzibar ni kisiwa kinachokaliwa na
idadi kubwa ya waislam na shambulio
hilo linakuja katika kipindi cha mwisho
wa mwezi mtukufu wa Ramadhan ,
wakati watu wakisherehekea sherehe
za Eid

WASOMI WAMUUNGA RAIS KIKWETE MSIMAMO JUU YA RWANDA NA RAIS KAGAME

WASOMI na baadhi ya
wanasiasa wazalendo nchini
wameunga mkono msimamo wa
Tanzania uliotolewa na Rais Jakaya
Kikwete kuhusiana na chokochoko
zinazoanzishwa na Rwanda na
wamemtaka Rais wa nchi hiyo,
Paul Kagame, kukaa meza ya
mazungumzo na waasi wa nchi
hiyo walioko Jamhuri ya
Kidemokrasia ya Kongo (DRC),
kwani amani haiwezi kutafutwa
kwa njia ya mtutu wa bunduki.


Akizungumza na MAJIRA kwa njia
ya simu jana Mhadhiri wa Chuo
cha St. Agustino, katika kitivo cha
sayansi ya siasa, Prof. Mwesiga
Baregu, alisema ushauri alioutoa
Rais Kikwete kwa Rais Kagame ni
mzuri, hauwezi kuleta athari
zozote tofauti na kutumia mtutu
wa bunduki kukabili waasi.


"Mimi nikiwa kama mtaalam
wa kutatua migogoro suala la
mazungumzo ni njia moja
ambayo huwa inatumika mara
kwa mara na inasaidia kuleta
amani," alisema na kuongeza;

"Kutumia mtutu wa bunduki
haileti tija kwa mataifa yote
mawawili, hivyo ni busara
itumike njia ya mazungumzo."

Alitoa mwito kwa nchi jirani
kushirikiana kutatua mgogoro
uliopo kwa njia ya mazungumzo
baina ya Rwanda na DRC.


Kwa upande wake Mkuu wa Kitivo
cha Elimu Chuo Kikuu cha Dar es
Salaam (UDSM), Dkt. Kitila
Mkumbo, alisema anakubaliana na
kauli ya Rais Kikwete na
anashangazwa na Rais Kagame ni
kwa nini anachukizwa kuambiwa
azungumze na waasi.


"Maana yake inaonekana hataki
kushauriwa...ushauri huo ni
kitu kizuri kinaweza kuleta
maelewano," alisema Dkt.
Mkumbo. Alisema Rais Kagame,
anaonekana kama dikteta
kutokana na kukataa kuambiwa
ukweli na viongozi wenzake.

Alisema kauli ya Rais Kikwete,
aliyoitoa kwenye hotuba yake ya
mwisho wa mwezi wa saba
hakugusia masuala ya vita na
anaamini kwamba kwa karne hii
sio mwafaka nchi kuingia kwenye
vita kwani nchi zina matatizo
mengi ambayo yanahitajika
kupatiwa ufumbuzi.

"Alichoongea Rais Kikwete, ni
msimamo unaotakiwa kuungwa
mkono na Watanzania kwani
yeye ndiye Amiri Jeshi Mkuu na
hiyo ndiyo kauli ya nchi...hivyo
alichosema ni sawa," alisema
Dkt. Mkumbo.


Mwenyekiti wa Jukwaa la
Wahariri, Absalom Kibanda,
alisema ameridhishwa na kauli ya
Rais Kikwete, kwani ametumia
lugha sahihi katika kueleza hali
halisi, hivyo Watanzania wote
wanatakiwa kumuunga mkono.


Alisema kwa hali ilivyo ni lazima
Watanzania waungane katika
masuala kama hayo ili kuleta
mshikamano wa nchi.


Mwenyekiti wa Tanzania Labour
Party (TLP) Augustino Mrema,
alisema anamuunga mkono Rais
Kikwete, kwa kauli yake hiyo.


Alisema Rais Kagame ameanza
chokochoko dhidi ya Tanzania na
kwamba hivyo, ndivyo alivyoanza
hata Idd Amin. "Siungi mkono
vita vitokee, lakini kama
atatuchokoza basi tuwe wa
mwisho kujibu mapigo," alisema
Mrema.


Aliyekuwa Mhadhiri UDSM, Dkt.
Azaveri Lweitama, amezitaka nchi
za Afrika Mashariki kukaa chini ili
kuangalia jinsi ya kutatua mgogoro
huo.


Alisema kuipiga Rwanda ni kazi
ndogo sana, lakini hauwezi
kumaliza tatizo kwa kutumia
bunduki na badala yake ni vyema
nchi hizo zikaangalia namna ya
kumaliza mgogoro.

"Unajua mnaweza kuingia
katika vita mkamuondoa Rias
wa Rwanda, lakini bado
mkatengeneza matatizo mengine
kwa rais ajaye," alisema.


Alisema Kongo kuna waasi wa
Rwanda na hata Rwanda pia kuna
waasi wa kutoka Kongo, hivyo ni
lazima kutafuta njia nzuri ya
kutatua tatizo hilo.

Kwa upande mwingine, Dkt.
Lweitama, alivitaka vyombo vya
habari kutopotosha taarifa
zinazozungumzia vita vikitokea
hakuna mtu atakayebaki salama.


"Vyombo vya habari vijitahidi
kuandika habari zisizo za
uchochoezi, kwani hata ninyi
pia ni Watanzania, naamini vita
ikitokea hakuna mhariri wala
mwandishi atakayebaki
salama," alisema.


Alisema vyombo vya habari pia
vina nafasi ya kukaa chini na
kutafakari namna ya kumaliza
mgogoro kwa kuwa vina nafasi
kubwa kwa mustakabali wa taifa.

Uhusiano wa Tanzania na Rwanda
unaelekea kupata mtikisiko baada
ya Rais Kikwete kutoa ushauri kwa
Serikali ya Rwanda kuzungumza
na mahasimu wao.


Rais Kikwete alitoa ushauri huo
kwa nia njema kwa kuwa bado
anaamini kuwa kama jambo
linaweza kumalizwa kwa njia ya
mazungumzo njia hiyo ni vyema
itumike.

Ushauri ule aliutoa pia kwa
Serikali ya Kongo na kwa Serikali
ya Uganda. ambapo katika
mkutano ule Rais Yoweri
Museveni wa Uganda aliunga
mkono kauli hiyo.


Tangu atoe ushauri huo viongozi
wa Rwanga wamekuwa wakitoa
kauli za kejeli dhidi ya Tanzania na
Rais Jakaya Kikwete. Katika
hotuba yake Rais Kikwete, alisema
uhusiano wa Tanzania na Rwanda
unapitia katika kipindi kigumu

Credits: MAJIRA.

PICTURE OF THE DAY | PICHA YA SIKU

"TANZANIA HAWANA CHA KUAMBULIA ZIWA NYASA" PETER MUTHARIKA WA MALAWI AJINADI.

Mgombea Urais wa Democratic
Progressive Party (DPP) nchini Malawi, Peter
Mutharika, amesema hakuna sababu za kufanya
majadiliano kuhusu Ziwa Malawi ambalo
Tanzania wanaliita Ziwa Nyasa.

Mutharika, ambaye ni mwanasheria, aliyasema
hayo kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika
juzi Mkoa wa Kati.

Akikaririwa na gazeti la Nyasa Times,
Mutharika alisema Tanzania haina cha
kuambulia kwa Ziwa Malawi.

Kiongozi huyo ambaye hakuwapo katika
mkutano wa Rais Joyce Banda na wapinzani
kuzungumzia mustakabali wa ziwa,
aliwahakikishia Wamalawi kuwa wasiwe na
wasiwasi wa mvutano huo.

Mutharika ziwa lote ni mali ya Malawi na
akisisitiza kuwa, Tanzania haina hata punje ya
eneo.

“Hakuhitajiki majadiliano, Ziwa Malawi ni mali
ya Malawi, litakuwa la Malawi,” alisema
Mutharika ambaye alichukua masomo ya Sheria
Tanzania.

“Tanzania inatumia nafasi ya udhaifu wa
uongozi wetu, lakini ukweli, hawana hata tone la
eneo... Tutakapoitwa kwenye uchaguzi ujao
mwakani, tutamaliza haya yote. Nitaleta meli
nyingi kwa ajili ya maendeleo ya uchumi,
kutengeneza ajira za kutosha kwa vijana,”
alisema Mutharika huku akishangiliwa na
wafuasi wake.

Tanzania inataka kugawana ziwa, lakini Malawi
imegomea mpango huo na suala hilo liko katika
majadiliano ambayo Banda alisema kama
mwafaka haukupatikana ifikapo Septemba 30,
Malawi itapeleka suala hilo Mahakama ya Kimataifa (ICJ).

AL-BASHIR AKATALIWA SAUD ARABIA

Wakuu wa Sudan wanasema Rais
Omar al-Bashir amezuwiliwa kuingia
katika anga ya Saudi Arabia, na
amelazimika kurudi Khartoum.

Bwana al-Bashir alikuwa njiani
kuelekea Iran kwa sherehe ya
kutawazwa kwa rais mpya, Hassan
Rouhani.

Saudi Arabia - ambayo ina uhusiano
mbaya na Iran - haikutoa sababu ya
kuchukua hatua hiyo.

Bwana al-Bashir anasakwa na
Mahakama ya Jinai ya Kimataifa, ICC,
kwa uhalifu wa vitani.

Mwezi uliopita al-Bashir alipewa
heshima ya gwaride nchini Nigeria
alipohudhuria mkutano wa viongozi
wa Umoja wa Afrika.

MAREKANI YAFUNGA BALOZI ZAKE.

Marekani imeongeza mda wa
kufungwa kwa balozi 19 pamoja na
afisi zake za ujumbe wa kidiplomasia
hadi tarehe 10 Agosti.

Idara ya maswala kigeni nchini humo
imesema hatua hio ni ya kutahadhari.

Takriban afisi 22 zenye ujumbe wa
marekani wa kidiplomasia zilifungwa
kwa mda siku mbili zilizopita mbali na
kutolewa tahadhari kwa raia wa taifa
hilo kutozuru maneo ya mashariki ya
kati pamoja na kazkazini mwa afrika.

Wizara ya mambo ya nje ya Marekani
ilisema kuwa kufungwa kwa balozi
hizo ni kutokana na serikali kuchukua
tahadhari kubwa na wala sio jibu lake
kwa tisho jipya la mashambulizi.

Uingereza ilisema kuwa Ubalozi wake
nchini Yemen utasalia kufungwa hadi
mwishoni kwa sherehe za siku kuu ya
IDD siku ya Alhamisi na kufunguliwa
siku ya Jumanne.

Wakati huohuo, balozi za Marekani
katika miji ya Algiers, Kabul na
Baghdad ni miongoni mwa zile
zitakazofungwa na kutarajiwa
kufunguliwa Jumatatu wiki ijayo.

Lakini duru za kidiplomasia katika miji
ya Abu Dhabi, Amman, Cairo, Riyadh,
Dhahran, Jeddah, Doha, Dubai,
Kuwait, Manama, Muscat, Sanaa na
Tripoli zinasema kuwabalozi zitasalia
kufungwa hadi Jumamosi.

Wizara ya mambo ya nje ya Marekani
pia iliongeza kuwa balozi zake katika
miji ya Antananarivo, Bujumbura,
Djibouti, Khartoum, Kigali na Port
Louis pia zitafungwa . Idadi ya balozi
za Marekani zitakazofungwa kwa
ujumla wiki hii ni 19.

Wizara hiyo ilisema kuwa uwezekano
wa balozi hizo kushambuliwa ni
kubwa sana hususan Mashariki ya kati
na Afrika ya Kaskazini.

Hatua ya kufungwa kwa balozi hizo
imekuja baada ya kile Marekani
kusema ilinasa ujumbe kutoka kwa
kundi la wapiganaji wa kiisilamu la al-
Qaeda.

Inasemekana kuwa ujumbe huo
ulikuwa kati ya viongozi wawili wakuu
wa Al Qaeeda wakipanga
mashambulizi.

Onyo hilo pia limetoa tahadhari kwa
raia wa Marekani kuwa waangalifu
kuhusu tisho la makundi ya
wapiganaji kufanya mashambulizi
dhidi ya mifumo ya usafiri wa umma
pamoja na maeneo mengine ya kitalii.

VILABU 13 VYA VPL VYAKUBALIANA KUHUSU AZAM TV, VYAKINZANA NA YANGA

KATIKA siku za karibuni,
kumekuwapo na mjadala
kuhusiana na hatua ya klabu ya
Yanga kupinga udhamini wa Ligi
Kuu ya Tanzania unaotarajiwa
kufanywa na Azam Media.
Tumeona ni vema tukatoa
msimamo wetu wa pamoja
kuhusiana na hatua hiyo ya
wenzetu kwa lengo la kuweka
rekodi sawa.


Tunataraji hatua hii ya vilabu hivi
13 itafunga mjadala huu na
tungependa wana habari, kama
mtaamua kuuendeleza, basi
muundeleze katika mrengo
ambao wadau, yaani sisi vilabu
vinavyoshiriki mashindano hayo,
zimeamua kuufuata.


Tunapenda kukumbusha kwamba
kwa muda mrefu, kilio cha vilabu
vya Ligi Kuu ya Tanzania vilikuwa
ni ukosefu wa wadhamini na kwa
bahati nzuri kuna dalili kwamba
Mungu ameanza kukisikia kilio
hicho msimu huu.


Kwa faida ya umma, tungependa
kutoa takwimu za nchi jirani
zinazotuzunguka. Kenya, kila
klabu hupata Sh milioni saba za
Kenya (sawa na Sh milioni 125 za
Kitanzania) kwa mwaka –fedha
ambazo zimeifanya ligi ya Kenya
kuwa na uwiano na ushindani wa
kweli (fedha hizo ni mjumuisho wa
gharama za matangazo ya
televisheni na udhamini wa bia ya
Tusker).

Tanzania leo tunajivunia kuwazidi
Kenya kutokana na udhamini wa
Azam ambapo kwa mwaka huu,
kila klabu itapata zaidi ya Sh
milioni 170 (Jumla kutoka milioni
100 za Azam na milioni 70 za
Vodacom).


Hatuna sababu ya kutaja viwango
vya udhamini kwa nchi nyingine
jirani kama Uganda, Burundi,
Rwanda, Zambia nk kwa vile zote
zina udhamini wa chini kuliko
Kenya.

SuperSport, ambao wanaliliwa na
baadhi yetu, udhamini wao kwa
ligi ya Uganda ni dola 350,000
ambazo ni pungufu kulinganisha
na dola milioni moja zilizotolewa
na Azam Media hapa nchini.

Ni imani yetu kwamba udhamini
huu utaifanya ligi ya Tanzania
kuwa bora kuliko zote za Afrika
Mashariki. Hili litasaidia
kutengeneza timu bora ya Taifa ya
Tanzania.

Tungependa kutoa ufafanuzi wa
masuala machache ambayo
yaliongelewa na wenzetu wa
Yanga kama sababu za kupinga
udhamini huu.

BODI YA TPL

Kwa mujibu wa Katiba za FIFA, CAF
na TFF, Haki za Televisheni zipo
chini ya FA ya nchi husika. TFF
iliamua kukasimu shughuli ya
majadiliano kwa Kamati ya Ligi
ambayo ilishirikisha vilabu vyote
14, ikiwamo Yanga na wawakilishi
wake walihudhuria mchakato
mzima hadi mwisho.

Hoja ya Yanga kuwa bodi haina
nguvu/Mamlaka kisheria kwa
kuwa ni ya mpito inakosa mashiko
kwa sababu kimsingi ni TFF ndiyo
iliyoingia mkataba kwa sababu
ndiyo iliyopewa mrejesho na
Kamati ya Ligi kwamba mchakato
umekwenda sawasawa.

Hoja ya kuwa Bodi ya TPL iliyoko
sasa hivi haina mjumbe hata
mmoja aliyeteuliwa kutoka
YANGA.

Hili si kweli hata kidogo.

Mmoja wa wajumbe wa TPL ni Seif
Ahmed almaarufu Seif Magari;
ambaye vyeo vyake ndani ya
Yanga vinajulikana.

Kama alikuwa hahudhurii vikao
vya TPL, hilo ni suala la Wanayanga
wenyewe kumuhoji kwanini
alikuwa hahudhurii hivyo na hivyo
kuinyima klabu yake ushiriki
katika mijadala muhimu kwa
maslahi ya soka hapa nchini.


Ifahamike pia kwamba TPL
haikuhodhi mchakato huu bali
ilitoa fursa kwa vilabu vyote vya
Ligi Kuu kushiriki ambapo Yanga
ilikuwa ikiwakilishwa na Makamu
Mwenyekiti wake, Clement Sanga
na Katibu Mkuu, Lawrance
Mwalusako.
Hii maana yake ni kwamba hoja
kuwa Yanga haikushirikishwa ni
mfu.

Yanga walitumia neno UTARATIBU
WA DUNIA NZIMA wakisema eti
hakuna mahala duniani ambapo
kampuni yenye klabu inayocheza
ligi husika kupewa mkataba wa
udhamini au urushwaji wa
matangazo.


Inaonekana Yanga hawakufanya
utafiti kwani ligi ya Afrika ya
kusini ina timu inayoitwa Super
Sports United na inarushwa na
kituo cha TV cha Supersports.

Pia majirani zetu Kenya wana timu
inayoitwa Tusker FC huku ligi hiyo
ikidhaminiwa na bia ya Tusker.

Tunawashauri Yanga kuwa ni vema
kufanya utafiti kabla ya kuibuka
na hoja za namna hii ili kuepuka
kuwapotosha wanachama wao.

Yanga pia katika hoja zao
wamepinga utaratibu wa
kugawana mapato sawa.


Hoja hii ni
ya msingi na majadiliano yetu
yalilitazama hili kwa kina lakini
tukaona kwa mazingira ya
Tanzania na uchanga wa ligi
yenyewe kwa sasa ni heri
kugawana sawa ili pesa kwa usawa
ili itoke kwa wakati na kusaidia
vilabu kujiendesha. Yanga
wanakosea wanaposema eti wao
wanastahili kupewa zaidi kwa
sababu ni klabu kubwa na yenye
mashabiki wengi kwa kuwa sababu
hii haitumiki sehemu yoyote
duniani.


Tuchukulie mfano wa nchi ya
England ambako ingawa Liverpool
ina washabiki wengi kuliko
Manchester City na Chelsea,
imezidiwa kwenye mapato ya
televisheni na timu hizo.

Hii ni sababu kinachoamu mapato
mwisho wa siku ni kiasi cha mechi
za timu ambazo zimeonyeshwa na
televisheni kwenye msimu husika
na nafasi ya timu kwenye
msimamo wa ligi.


Hata hivyo, ikumbukwe kwamba
nchini England, malipo haya
hufanyika baada ya msimu
kumalizika na hapo ndipo watu
hukaa chini na kupigiana hesabu
za nini kilipatikana. Sasa ukitumia
mfumo huu, ina maada timu
zitalazimika kusubiri ligi iishe ili
kuangalia msimamo ya ligi kisha
kugawana mapato. Sote tunajua
jinsi timu zinavyoteseka kwa
kukosa nauli, posho, mishahara,
pesa za kambi nk.
Kwa mazingira yetu ya Tanzania
kwa sasa, mfumo kama huu
haufai. Hii ni kwa sababu timu
zinahitaji fedha kuanzia kwenye
maandalizi ya mechi ya kwanza na
hazikopesheki fedha kwenye
mabenki.

Tanzania inachohitaji kwa sasa ni
ligi yenye ushindani tofauti na
sasa ambapo ushindani uko kwa
timu chache zenye uwezo wa
kifedha.


Tukizijengea uwezo timu zote taifa
litakuwa na ligi nzuri na hatimaye
timu nzuri ya taifa. Pia itawezesha
wadhamini wengi zaidi kuingia
kwenye mpira na hivyo timu
nyingi zaidi kufaidika.


Tukifikia huko, tunaweza kukaa
chini na kutazama mfumo wa
kugawana mapato utakaokuwa
bora zaidi wakati huo.
Mambo ya Kuzingatia.Tangu ligi
ianze hapa nchini takribani miaka
50 iliyopita, hakuna timu iliyowahi
kulalamikia mfumo wa kugawana
mapato sawa kwa kila mechi
ambao umekuwa ukitumika.


Mfano mapato ya mlangoni
tumekuwa tukigawana sawa na
Yanga haijawahi kulalamika, Pesa
za udhamini wa Vodacom tangia
ilipokuwa ikidhaminiwa na TBL
hadi leo hii tumekuwa tukigawana
sawa na Yanga haijawahi
kulalamika kutaka kupata zaidi
kwa kuwa eti ina mashabiki wengi,
pia hata pesa za haki ya matangazo
ya Televisheni zilizowahi kutolewa
huko nyuma nailiyokuwa ikiitwa
GTV, na Star TV kwa nyakati tofauti
pesa ziligawiwa sawa kwa kila
timu.


Hii ni kwa sababu kikanuni, timu
zote zinazoshiriki kwenye ligi ni
sawa na zote zinaweza kuwa
bingwa au kushuka daraja.

Ni mdudu gani huyu aliyeingia
kwenye soka ya Tanzania na
kuanza kuleta siasa za kubaguana?
Baba wa Taifa alipata kutuasa
kwamba dhambi ya ubaguzi ni
sawa na kula nyama ya mtu.
Ikianza, haitaishia kwenye ligi
pekee na itakwenda hadi mahali
tusipotaka.


MGOGORO WA MASLAHI

Yanga imekuwa ikilalamikia
uwepo wa kiongozi mwandamizi
wa makampuni ya Bakhresa
kwenye bodi ya Ligi na kusema
inaleta mgongano wa maslahi.

Sisi vilabu tunaamini kwamba
uwepo wa kiongozi huyu ndiyo
umesaidia makampuni yake
kuwekeza fedha kwenye mpira.


Na mifano ipo hai tukianzia na
michuano ya Vijana ya Uhai Cup,
ujenzi wa kituo cha michezo cha
Chamazi ambacho kinatumiwa na
timu nyingi za Tanzania.

Na sasa tunafaidika na udhamini
huu mnono ambao haujapata
kutokea katika historia ya
Tanzania.

Tungependa viongozi wengi zaidi
wa makampuni yanayoheshimika
hapa nchini wakijitokeza kuongoza
mpira badala ya kuanza
kuwapinga.


Kwa mfano, tungependa kuona
mkurugenzi wa benki ya CRDB
akiwa kiongozi wa Ashanti, bosi wa
Barrick akiongoza Mbeya City na
Mkurugenzi wa Tanga Cement
akiongoza Coastal Union.
Hivi ndivyo namna mpira
unavyoweza kuvutia wawekezaji.

Ndiyo maana tulifurahi wakati
Yusuf Manji, alipoomba uongozi
Yanga.


Bado tunataraji kwamba naye
atajitosa kuingiza fedha zake
kwenye ligi ya Tanzania (mpira)
kama alivyofanya Bakhresa
ambaye pamoja na kutumia fedha
zake Azam FC, bado ameamua
kusaidia na timu nyingine kwa
ujumla.


Tunapenda kumuahidi Yusuf Manji
kwamba iwapo naye atataka
kudhamini Ligi Kuu iwe kibiashara
au kiufadhili, sisi tutamuunga
mkono na hatutajali suala la
mgongano wa maslahi.


UPOTEVU WA MAPATO

Wenzetu Yanga wamedai kwamba
kwa kuonyesha mechi kwenye
televisheni, mapato yake ya
mlangoni yatapungua.


Hili pia halikufanyiwa utafiti wa
kutosha. Katika siku za karibuni,
mechi zilizoingiza mapato
makubwa zaidi ya milangoni ni zile
ambazo zilionyeshwa Live kwenye
televisheni za ndani na nje ya
nchi.

Mifano ni mechi za watani wa jadi
msimu uliopita zilizoonyeshwa
Live na SuperSport na mechi za
Kombe la Kagame zilizoonyeshwa
wakati huo.


Hata mechi ya Taifa Stars na Ivory
Coast iliyoonyeshwa Live pia,
ilijaza uwanja. Ulaya ambako
karibu kila familia inamiliki
televisheni na umeme wa
uhakika, bado watu wanajaa
katika viwanja vya soka.


Mpira kuonyeshwa kwenye
televisheni unaufanya utangazike
zaidi na watu watake kuona. Kuna
faida nyingi za mpira kuonyeshwa
kwenye televisheni kuliko hasara
moja ya kufikirika ambayo Yanga
wanaiona.

Ingekuwa vema iwapo Yanga
wangetoa takwimu za kuonyesha
ni kwa namna gani mechi
kuonyeshwa kwenye televisheni
kuliwahi kupunguza mapato ya
milangoni.


Kwa faida ya umma, mpira kuwa
kwenye televisheni kuna faida
zifuatazo; jezi kuongezeka
thamani na hivyo kuvutia
makampuni makubwa kutaka
kudhamini klabu wakitumia fursa
ya kutangaza bidhaa zao,
matangazo ya viwanjani (touchline
fence) kuwa na thamani zaidi
ambapo kwa sasa vilabu havipati
chochote, kuchochea michezo ya
kubahatisha, kutabiri matokeo na
kupata habari kupitia simu za
mkononi na hivyo vilabu vitaanza
kutengeneza fedha za kutosha.


Ulaya wamesonga mbele kutokana
na televisheni. Anayekataa mpira
kuonyeshwa kwenye televisheni
ni sawa na mtu anayegoma
kutumia mfumo wa digitali katika
ulimwengu wa leo.


UWAZI KWENYE MCHAKATO WA
KUUZWA KWA HAKI ZA
MATANGAZO

Yanga wameandika kwenye taarifa
yao rasmi eti hakukuwa na uwazi
kwenye mchakato wa kuipata
kampuni ya kurusha matangazo ya
Televisheni.


Sote tunajua kuwa vituo vya
televisheni vilivyopo nchini kama
Star TV ambayo iliwahi kurusha
mechi kadhaa msimu uliopita
vilikuwa vikijua kuwa kuna nafasi
hiyo na TFF mara kadhaa
wamekuwa wakitangaza hilo
kupitia idara ya Habari ya TFF.


TFF kwa mfano walikwenda mbali
kwa kuialika Supersports kuja
kuonesha mechi bure kwa
kilichokuwa kikiitwa Super Week
ili kuwashawishi waje kuwekeza
na mara ya mwisho ni Yanga hawa
hawa walioongoza harakati za
kuikataa Supersports kuonesha
mechi bure wakisema kuwa kama
ni kuwavutia inatosha.
Katika mazingira kama haya
tunastaajabishwa na ukigeugeu wa
Yanga leo kusema eti tenda
haikuwekwa wazi. Sote tunajua
kuwa ni Super Sports pekee
tuliokuwa tukiwategemea na
kuwashawishi ambao
hawakuonesha kuhitaji kuja
kuwekeza. Kwa nini leo tuikatae
Azam TV?

Yanga wanaposema eti TFF/Kamati
ya Ligi imeipa haki za matangazo
kampuni ambayo haina ofisi wala
kituo cha televisheni kilicho
hewani kwa sasa wanasahau kuwa
huko nyuma TFF iliwahi kuwapa
haki za matangazo GTV ambao
hawakuwa na ofisi wala kitu cha
TV na baada ya miezi michache
walifungua ofisi zao na kuleta
vingamuzi na kuaza kurusha mechi
zetu. Vilabu vilifaidi udhamini ule
kabla ya ile kampuni kufilisika.

Kwa hiyo hii si mara ya kwanza
kwa jambo hili kufanyika na kama
Azam TV hawataonesha mechi za
ligi hiyo sisi kama vilabu
haituhusu kwani ni hasara yao.


Tunachowaomba Azam Media sisi
kama vilabu ni kuhakikisha
wanatulipa pesa zetu kwa haraka
ili zitusaidie kwenye
maandalizi,Tunawaomba Yanga
wasichafue hali ya hewa kwa kuwa
wao hawana shida ya Pesa.
Sisi Umoja wa Vilabu 13
vinavyoshiriki Ligi Kuu ya Tanzania
tunapinga, kwa nguvu zote, madai
ya Yanga kwamba
hatukushirikishwa kama vilabu
kwenye mchakato huu.


Mfumo wa ugawanyaji wa mapato
tuliouchagua, tuliuchagua
wenyewe bila kushurutishwa na
yeyote na tunadhani ndiyo mfumo
unaotufaa kwa sasa hadi hapo ligi
yetu itakapokuwa na nguvu maana
kwa sasa inaruhusiwa klabu
kupata fedha mwanzoni kulingana
na hali halisi ya vilabu vyetu.


Tunawashauri wenzetu wa Yanga
waanze kuamini kwenye kitu
kinachoitwa Uwajibikaji wa Pamoja
(Collective Responsibility). Mambo
yanayoamuliwa kwenye vikao
hayapaswi kupingwa nje ya vikao.


Kama hoja ililetwa kwenye vikao
na ikazidiwa nguvu na hoja
nyingine, hakuna sababu ya
kuikataa kwa sababu tu
hukubaliani nayo. Mfumo wa
kidemokrasia una kanuni moja
kuu; Wengi Wape


Imetolewa na
Vilabu 13 vya Ligi Kuu ya Tanzania

Simba SC, Azam FC, Ashanti
United, JKT Ruvu, Ruvu Shooting
Stars, Mgambo JKT, JKT Oljoro,
Rhino Rangers, Mbeya City,
Tanzania Prisons, Mtibwa Sugar,
Coastal Union na Kagera Sugar.


Chanzo:Shaffihdauda.com

DR. SLAA AWAUNGA MKONO MOVEMENT 23(M23) NA KAGAME

Katibu wa Chama cha Demokrasia
na Maendeleo (Chadema), Dk.
Wilbroad Slaa, amemkosoa Rais
Jakaya Kikwete, kuhusu kauli
yake ya kumshauri Rais wa
Rwanda, Paul Kagame,
kuzungumza na waasi wa serikali
yake.


Dk. Slaa amesema haoni busara
kwa Rais Kikwete kuwaambia
viongozi wa Rwanda, akiwamo
Rais Kagame, kuzungumza na
wafuasi wa chama cha FDRL
walioko Congo.

Slaa aliyasema hayo wakati
akizungumza katika kongamano la
vijana wa Chadema (BAVICHA) la
uchumi na ajira lililofanyika jana
jijini Dar es Salaam.


"Rais Kikwete hapa nyumbani
hawezi kuzungumza na
wapinzani na hajachukua
hatua dhidi ya wauaji wa
mwandishi Daudi Mwangosi...


"Alishauriwa amuwajibishe
Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa
Iringa Michael Kamuhanda na
badala yake amempandisha
cheo," alisema Slaa.


Kauli Dk Slaa imekuja siku moja
baada ya Rais Jakaya Kikwete
kueleza kuwa Tanzania haina
mgogoro na nchi ya Rwanda,
kutokana na kauli za kejeli na
matusi zilizokuwa zikitolewa na
viongozi wa nchi hiyo dhidi yake
na Tanzania.


Kumezuka sitofahamu ya
uhusiano wa kidiplomasia kati ya
Tanzania na Rwanda, baada ya
Rais Kikwete kuitaka Rwanza
imalize ugomvi na waasi kwa
njia ya mazungumzo ya
amani...


Rais Kikwete aliutoa ushauri
huo wakati wa mkutano wa
Umoja wa Afrika (AU) uliofanyika
Addis Ababa, Ethiopia hivi
karibuni.


Ushauri huo ulionekana
kumchukiza Rais Kagame,
anayedaiwa kuhutubia mikutano
kadhaa nchini kwake na kutumia
lugha ya matusi, kejeli na dhihaka
dhidi ya Rais Kikwete na Tanzania.


Kitendo cha Dr Slaa
kumkingia kifua Kagame
kinatia shaka uzalendo wake
na chama chake kwa taifa
hili...


Sote tumekuwa tukishuhudia
matusi ya Kagame dhidi ya
Tanzania. Iwaje Rais Kikwete
aonekane mbaya kwa kumjibu
Kagame, tena kwa lugha ya
kizalendo??

Kagame amekuwa akituhumiwa
na jumuiya mbalimbali za
kimataifa kwa kutoa misaada ya
kivita kwa waasi wa M23
ambao wamekuwa wakiua raia
na kuwabaka wanawake....


Kauli ya Dr Slaa ina mambo
mengi yaliyojificha na huenda
yeye na chama chake ni wafuasi
wa karibu wa M23 kama ilivyo
kwa Kagame.


Kuwa mpinzani, haimaanishi
ukosoe kila kitu.


Credits:Mpekuzi Huru

KANDA YA VIDEO YA SHEIKHE PONDA AKIHAMASISHA UASI YADAKWA.

SERIKALI imenasa kanda za video
zinazomuonyesha Kiongozi wa Jumuiya na
Taasisi za Kiislamu Tanzania, Sheikh Issa
Ponda, akitoa mahubiri yanayowahamasisha
waumini wa dini ya Kiislamu kuanzisha uasi
dhidi ya serikali.
Tukio la kunaswa kwa kanda hizo limekuja
ikiwa ni siku chache baada ya Jeshi la Polisi
Zanzibar kutangaza kumsaka Sheikh Ponda
kwa tuhuma za uchochezi, akingali anatumikia
kifungo cha nje cha mwaka mmoja baada ya
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu ya Dar es
Salaam kumkuta na hatia ya kosa la uchochezi.

Katika kanda hizo ambazo MTANZANIA
Jumapili imefanikiwa kuziona, Sheikh Ponda,
amerekodiwa akiwa katika Msikiti wa
Mbuyuni, Zanzibar, alikohudhuria Mhadhara
wa Dini ya Kiislamu, akiwataka waumini wa
dini hiyo kuchukua hatua za kuikomboa
Zanzibar kipindi hiki cha mfungo wa Mwezi
Mtukufu wa Ramadhani, kutoka kwenye
mikono ya utawala wa makafiri.

Huku akiitikiwa kwa neno Takbir kutoka
washiriki wa mhadhara huo, Sheikh Ponda
anasikika akisema Zanzibar ni nchi ya Kiislamu,
hivyo Waislamu wana wajibu kwa kuikomboa
kutoka mikononi mwa vibaraka wanaoiongoza,
aliodai kuwa wananyonya uchumi wake na
kuutoroshea nje ya visiwa hivyo.

Moja ya kanda hizo iliyorekodiwa kwa muda
wa saa moja na dakika ishirini na nne, ambayo
Sheikh Ponda alitumia muda mwingi kusisitiza
umuhimu wa Waislamu kuikomboa Zanzibar
kutoka mikononi mwa aliowaita makafiri,
anasikika akisema:
"Mna wajibu wa kuikomboa Zanzibar na si
mnaweka vibaraka, wanateuliwa huko halafu
wanakuja hapa kuwaongozeni, fedha zote
zinachukuliwa hapa na kupelekwa kule kwa
sababu tumepoteza nchi, tumepoteza hadhi.

"Makafiri wanatakiwa kuyaheshimu mambo
matakatifu ya Kiislamu na kuyajua, kama
hawataheshimu Mwenyezi Mungu alisema
lazima mlipize kisasi katika mambo
matakatifu. Mungu alisema ni lazima mlipize
kisasi mwezi mtakatifu kwa mwezi mtakatifu.
Mambo matakatifu yamewekewa kisasi.

"Miongoni mwa mambo matakatifu
yaliyowekewa kisasi ni haki na uadilifu
pamoja na dini ya Kiislamu,
unapozungumzia dini ni pamoja na masheikh,
hawa ni watu watakatifu, watu wenye hadhi, ni
watu wakubwa na watakatifu kuliko baba
mtakatifu kama wanavyosema wao."
Sheikh Ponda pia anasikika akieleza kuwa
Waislamu wamedhalilishwa kwa muda mrefu,
hivyo wana wajibu wa kuikomboa Zanzibar
kwa kuwa hata Mtume Mohammad aliongoza
jeshi akakomboa nchi ya Maka kipindi cha
Mwezi Ramadhani.

Alieleza kushangazwa na uteuzi wa Rais wa
Zanzibar kufanyikia Dodoma na hata uamuzi
wa kumuondoa madarakani kuchukulia
mkoani humo na kutoa mwito wa jambo hilo
kusitishwa.

Katika hili anasikika akisisitiza kuwa; "Hakuna
mtu ambaye haelewi kwamba Zanzibar ipo
mikononi mwa watu wasio stahiki, Zanzibar
ni nchi ya Waislamu. Sisi Waislamu wa
Zanzibar tuna mazingatio makubwa kuliko
watu wengine kipindi hiki cha Mwezi
Ramadhani kwa sababu mafundisho
tunayoyapata katika maisha ya Mtume
Mohammad ni sawa na mazingira ya sasa,
hivyo tunatakiwa kuyatekeleza. Zanzibar si
nchi ya watu, bali ni ya Waislamu.

Katika mahuburi yake kwenye mhadhara huo,
Sheikh Ponda anakisika akieleza kuwa
Muungano wa Zanzibar na Tanganyika umezaa
ufisadi visiwani humo na kurejea kauli aliyodai
kutolewa na Mtume iliyokuwa ikiwaonya
Wazanzibari kutoruhusu uwepo wa Muungano.
"Tangu lini bia, ukahaba ukawa hitajio la
Wazanzibari na hii ndiyo 'product'
iliyotokana na Muungano na Mapinduzi.
Maovu ambayo hamkuyapata kuyaona ni kauli
ya Mtume, alisema mkiruhusu muungano
ufisadi unatokea. Leo hii mnaona nchi ya
Zanzibar mambo ambayo si hitajio la
Wazanzibari, mmeingiza watawala waovu
katika ardhi hii.

"Zanzibar ina watu wenye akili kubwa, wenye
uwezo na ina wasomi wa fani zote na ni watu
wa kuigwa duniani kote…. hivi sasa
Mwislamu anapokwenda mahakamani
anayesikiliza shauri ni kafiri. Mwislamu
anapofunguliwa kesi, sheria hazifuatwi kwa
maana kwamba kuna utaratibu wa dhamana,
lakini hautolewi, jambo ambalo linaonyesha
wazi kuwakandamiza Waislamu.
"Leo hii viongozi wetu wanatiwa jela bila
sababu, kosa lao ni pale wanapotetea
Uislamu. Wako gerezani, tutapataje sifa ya
Ramadhani tusipowatoa hawa ndugu zetu
walioko gerezani na Mungu anasema mambo
matakatifu yanalipiziwa kisasi.

"Kila siku viongozi wa Kiislamu wanauawa,
Sheikh Hamis ameuawa anatoka msikitini,
kafa na hakuna maelezo kwa sababu kwa
mujibu wa sheria, lazima kuwe na maelekezo
na mahakama iseme. Yote hayo hakuna
maelezo yoyote utadhani kafa paka, kapigwa
risasi kafa hakuna maelezo yoyote ya serikali.
"Ndugu zangu hali ni mbaya sana, watu
wanapanga mikakati kwa ajili yenu ninyi.
Msifikirie kuwa jamii haiwezi kutoweka.
'Tujenga utayari kwa ajili ya kupigania dini ya
Mwenyezi Mungu, hilo ni jambo la msingi.

Ukimya wenu ni tatizo kubwa sana, hivi ndivyo
wanavyotaka wafike mahala wakamate
mashekh wawaweke ndani, halafu mkae kimya,
hili jambo ni kubwa na ni la dini, mnatakiwa
msimame kidete kwa ajili ya jambo hili.
"Suala la kisasi lina uhusiano na uhai,
mtapata uhai mzuri katika kulipiza kisasi
ninyi Waislamu."
Akizungumzia kukamatwa kwake hapo awali,
alisema ulikuwa ni mkakati uliopangwa
Dodoma, baada ya kusikilizwa kwa malalamiko
ya waumini wa dini ya Kikristo.

Mbali na hayo, kauli nyingine zinazoelezwa na
baadhi ya watu walioona na kusikiliza kanda
hizo kuwa zina kila dalili ya kuhatarisha amani
nchini, ni ile anayosikika akisema; "Sisi
viongozi ndio tunatoa maagizo tuingie
barabarani hata kama serikali imepiga
marufuku. Kama wataleta jeshi sisi tunakuwa
'front.'
"Kama wewe unaogopa polisi itakapofika
Jihad utatoka, hawa ni watu kama wewe,
anavyokupiga kirungu hakuna sababu ya
kumwogopa binadamu mwenzako, hizo ni
hatua za kujenga nafsi na utayari.

"Kipindi cha uchaguzi mkitumie vizuri,
muwatoe hawa madarakani, watoeni
wakatae halafu kimbembe kianze pale,
mnatoa kauli ya moja kwa moja. Waambieni
kuwa ninyi na sisi ni moto na baruti.
"Kwa upande wa Katiba, kuna suala la
kupiga kura, hakikisheni kura yenu
izingatie maslahi yenu.

Kule Bara
tulipendekeza mahakama ya kadhi
imetupwa na sasa hivi kazi zile ambazo
zinatakiwa kufanywa na mahakama ya
kadhi zinafanywa na mahakama ya
mwanzo."

--
Posted By Blogger to Michael M. Mazalla at 8/04/2013 02:46:00 PM

WANYARWANDA WAAMBIWA WARUDI KWAO

Mamia ya wahamiaji haramu kutoka nchini
Rwanda wakiwa na ng'ombe zaidi 900
wameanza kuondoka nchini kurejea kwao
kutokana na agizo la Rais Jakaya Kikwete
kuwataka waondoke Tanzania kabla ya siku
14.


Aidha, imeelezwa kuwa kumekuwapo
ongezeko la askari wa Jeshi la Wananchi wa
Tanzania (JWTZ) mkoani Kagera hasa wilayani
Ngara hali inayozua hofu kwa baadhi ya
wananchi, huku ikiongeza msukumo kwa
wahamiaji haramu kuondoka.


Akiwa katika ziara mkoani Kagera, Rais
Kikwete alitoa agizo la kuwataka wote
waliokuwa wakiishi nchini kinyume cha sheria
waondoke mapema jambo lililotakiwa
kuanza kutekelezwa Julai 29 na kukamilika
Agosti 10 mwaka huu.


Alisema kuwa wahamiaji haramu na wale
wanaoendesha ama kuhusika na ujambazi,
uhamiaji haramu na uingizaji haramu wa
mifugo waamue kuchukua hatua mwafaka za
kuondoka mapema kabla vyombo vya ulinzi na
usalama kuanza operesheni maalumu ya
kuwasaka.


Tayari idadi kubwa ya wafugaji wenye makundi
ya ng'ombe imeanza kuondoka kuelekea eneo
la mpakani la Rusumo kutoka ardhi ya
Tanzania ikiwa ni utekelezaji wa agizo hilo la
Rais Kikwete.


Akizungumza na Mwananchi Jumapili kwa njia
ya simu, Mkuu wa Wilaya ya Ngara, Costantine
Kanyasu alisema kwamba idadi kubwa ya
wafugaji waliokuwa wakiishi kinyume cha
sheria, imeitikia wito wa agizo la Rais na
kuanza kuondoka kwa hiyari yao.

Hata hivyo, alisema kuwa pamoja na idadi
kubwa ya wahamiaji kuanza kuondoka, bado
wapo ambao hawajaondoka kutokana na kudai
kuwa na vibali walivyovipata kutoka Ofisi ya
Uhamiaji na kubainisha kwamba vibali hivyo
vitakaguliwa kwa umakini wakati wa
operesheni maalumu ili kujua uhalali wake.


"Jambo hili la wahamiaji haramu lilikuwa kero
kubwa, siyo tu kwa Wilaya ya Ngara, bali mkoa
mzima wa Kagera, lakini tunashukuru sasa
wameanza kuondoka, wamebaki hao wenye
vibali. Ni lazima vibali hivyo tutavikagua
maana vipo vilivyotolewa kinamna," alieleza
Kanyasu.


Alionya kwamba jukumu la kuwaondoa kwa
nguvu wahamiaji haramu pamoja na wafugaji
linasubiri muda wa mwisho ili kuanza
kutekelezwa kama Rais Kikwete alivyoagiza.


Hofu ya Wanajeshi kuongezeka

Akizungumzia suala la wanajeshi kudaiwa
kuongezeka wilayani Ngara, Kanyasu alisema
kwamba katika wilaya yake kuna kikosi cha
dharura kinachokaa katika moja ya kambi za
JWTZ kikikuwa na idadi kubwa ya askari lakini
wananchi hawakuwa na taarifa nacho ila
kutokana na sababu za kiusalama.


"Unajua kuna kelele za hapa na pale na
haya majibizano yanayotokea baina ya
Rwanda na Tanzania. Haya ni kama
yamewastua watu na kudhani kuwa askari
wetu wa Kikosi cha Dharura waliopo hapa
Ngara wameletwa maalumu kutokana na
tahadhari," alisema na kufafanua kuwa askari
hao wapo siku zote kwa ajili ya kulinda mipaka
ya Tanzania.

Hata hivyo, mkuu huyo wa wilaya aliwataka
wananchi kutulia na kutoa ushirikiano kwa
jeshi hilo.


Rais Kikwete aliagiza operesheni hiyo ya
kuwaondoa wahamiaji haramu ifanyike katika
Mikoa ya Kigoma, Kagera na Geita kwa wakati
mmoja ikisimamiwa na vyombo vya ulinzi na
usalama yaani JWTZ, Polisi, Usalama wa Taifa
na Uhamiaji akiwaonya wahalifu kuwa
hapatakuwa na mahali pa kukimbilia wala
kujificha.


Chanzo:Mwananchi