Mchina Agongwa na Gari na Kufariki

RAIA wa China aliyetambuliwa kwa jina la Ruo Yaowu (34) amekufa papo
hapo baada ya kugongwa na gari wakati akivuka barabara.

Kamanda wa Mkoa wa Kipolisi wa Kinondoni, Charles Kenyela
alithibitisha hayo jana na kusema kuwa, ajali hiyo ilitokea juzi saa
7:00 usiku katika barabara ya Bagamoyo eneo la Boko, Kinondoni.

Alisema gari namba T865 AHB aina ya Toyota Canter, likiendeshwa na mtu
asiyefahamika akitokea Bunju kwenda Tegeta, alimgonga mtu huyo ambaye
alikufa papo hapo. Mwili wa marehemu umehifadhiwa katika Hospitali ya
Taifa Muhimbili na msako wa kumtafuta dereva aliyekimbia baada ya
ajali unaendelea.

Katika tukio jingine, maiti moja ya mwanaume aliyetambuliwa kwa jina
moja la Chalii anayekadiriwa kuwa na umri kati ya miaka 15 ba 20,
imekutwa ikiwa imelala pembezoni mwa ufukwe wa bahari ya Hindi.

Kamanda wa Mkoa wa Kipolisi wa Ilala, Marietha Minangi alisema tukio
hilo ni la juzi saa 4:10 usiku katika eneo la Ferry, wilaya ya Ilala.

Maiti hiyo ilikutwa ikiwa pembezoni huku ikiwa haina jeraha lolote
isipokuwa ilikuwa inatoka damu mdomoni na puani. Chanzo cha kifo chake
hakijafahamika na maiti imehifadhiwa hospitali ya Taifa Muhimbili.

Wanafunzi Waua Mwizi

WANAFUNZI wa Shule ya Sekondari Ntuchi wilayani Nkasi mkoani Rukwa
wanadaiwa kumuua kwa kumpiga mkazi wa kijiji cha Ifundwa wilayani
hapa, Ignas Maruku (29) wakimtuhumu kuingia kwenye bweni la wanafunzi
wa kike na kuiba nguo zao mbalimbali, zikiwemo nguo za ndani.

Akithibitisha kutokea kwa tukio hilo, Kamanda wa
Polisi Mkoa wa Rukwa, Jacob Mwaruanda amemweleza mwandishi wa habari
hizi kuwa tukio hilo lilitokea Aprili 25 mwaka huu saa 6.00mchana
wakati wanafunzi hao wakiwa darasani.

Akisimulia tukio hilo, Kamanda Mwaruanda alisema siku hiyo, mmoja wa
wanafunzi hao wakike ambaye jina lake halikuweza kufahamika mara moja
akiwa nje ya madarasa karibu na bweni lao alimwona kijana huyo
akiingia bwenini mwao hivyo alimshtukia na kuanza kupiga kelele.

Inadaiwa ndipo wanafunzi hao wa kike na wa kiume walipotoka darasani
na kuanza kumfukuza mwizi huyo kisha kumkamata na kuanza kumshambulia
kwa mawe, marungu na fimbo hadi akazimia.

Wakati wanafunzi hao wakimsulubu mwizi wao huyo ndipo walimu wao
walipoacha shughuli zao zote shuleni hapo na kukimbilia eneo la tukio
na kuamuru wanafunzi hao watawanyike na kuacha kumpiga mtuhumiwa huyo,
warejee madarasani.

Kwa mujibu wa Mwaruanda, walimu hao walitaarifu polisi ambao kwa
kushirikiana nao walimkimbiza mtuhumiwa huyo katika Hospitali Teule ya
Wilaya hiyo mjini Namanyere, lakini alifariki dunia wakati akipata
matibabu hospitalini hapo.

Kamanda Mwaruanda amedai kuwa mwalimu wa shule hiyo aliyetambuliwa
kuwa Thobias Ndunguru (26) na mkazi wa kijiji hicho cha Ntuchi, Simon
Osayi wanashikiliwa na Polisi kwamahojiano kuhusu mauaji hayo, lakini
hakuna mwanafuzi yeyote anayeshikiliwa hadi sasa huku uchunguzi zaidi
wa tukio hilo ukiendelea.

Azikwa Akiwa Hai

Mbeya. Msaidizi wa zamani wa Padri (Katekisita) katika Kigango cha
Kanisa Katoliki Kijiji cha Mkwajuni, Florian Mwamosi (70) amekufa
baada ya kuzikwa akiwa hai katika kaburi moja na mtu anayedaiwa kumuua
kwa njia ya kishirikina.
Tukio hilo limetokea katika Kitongoji cha Maweni kijijini hapo
wilayani Chunya mkoani Mbeya.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya Diwani Athumani alikiri kutokea kwa
tukio hilo akieleza kuwa lilitokea saa 9:00 mchana katika kijiji
hicho cha Maweni Mkwajuni wilayani Chunya.

"Marehemu aliuawa na wananchi wenye hasira kali kwa kupigwa na mawe
kwa tuhuma za kuhusika na uchawi na kusababisha kifo cha Peter
Robert," alisema.

Kamanda Athumani alisema kuwa uchunguzi kuhusiana na tukio hilo
unaendelea na kwamba wahusika wote wa tukio hilo wamekimbia na
kuzihamanyumba zao, hivyo polisi wanaendelea na msako wa kuwatia
mbaroni watuhumiwa na kwamba tayari kaburi hilo limefukuliwa jana
kutenganisha maiti hizo.

Mashuhuda wa tukio hilo walisema kuwa marehemu huyo ambaye alikuwa
akituhumiwa kwa ushirikina aliwahi kuwa Katekista wa kigango hicho
hadi mwaka 2007.

Wameeleza kuwa Mwamosi alikwenda kuhudhuria mazishi ya Peter Robert
(28) katika kitongoji hicho cha Maweni, baada ya kufuatwa nyumbani
kwake na watu wakitaka aende kwa sababu yeye ni mmoja wa wazee wa mila
katika kitongoji hicho.

"Bwana Mwamosi alikuwa akituhumiwa kwa uchawi kwa muda mrefu na wenzie
wawili, hivyo alipofika makaburini ilianza minong`ono ya watu na huku
wengine wakiguna na ndipo alipoombwa aingie kaburini kwa ajili ya
kupokea jeneza lililobeba mwili wa marehemu Peter Robert," alisema
mkazi mmoja wa kijiji hicho aliyejitambulisha kwa jina moja la Joseph.

Alisema kuwa baada ya kuingia kaburini akiwa na watu wengine watatu
wenzake walitoka kwa haraka na kumwacha Mwamosi peke yake ndipo kundi
la watu waliokuwa eneo hilo la makaburi walianza kumshambulia kwa
kumpiga mawe huku wakimwamuru akae chini.

Shuhuda huyo alisema kuwa baada ya kukubali kukaa chini akiwa ndani ya
kaburi hilo, walianza kumfukia naalipofukiwa nusu ya mwili wake
waliingiza jeneza la marehemu Peter na kuliweka juu yake na kuanza
kulifukia kaburi hilo.

"Baada ya kukaa chini ndani ya kaburi hilo ndipo walianza kumfukia kwa
udongo na baadaye wakachukua jeneza la marehemu na kuliweka juu yake,
kisha kumfukia na udongo na taratibu za mazishi ziliendelea kwa ajili
ya marehemu Peter,"alisema.

Alidokeza kuwa chanzo cha tukio hilo ni marehemu Robert kuugua ghafla
tumbo, ndipo ndugu zake walipoamua kumpeleka kwa mganga wa jadi kwa
ajili ya kupata matibabu na baada ya siku tatu alifariki dunia.

Kamanda huyo amewasihi wakazi wa Mkoa wa Mbeya kuacha tabia kama hizo
kwani kufanya hivyo ni kuuchafua mkoa na kuwa na sifa mbaya, hivyo
kusababisha maendeleo ya mkoa kurudi nyuma.
Januari 12, mwaka huu wakazi wawili wa Kijiji cha Karungu, Kata ya
Ivuna, Wilaya ya Momba, mkoani Mbeya walikufa baada ya kufukiwa wakiwa
hai katika kaburi moja na marehemu wanaodaiwa kumuua, tukio
linalohusishwa na imani za kishirikina.

Chanzo:Mwananchi

Godbless Lema Akamatwa

MBUNGE wa Arusha Mjini, Godbless Lema amekamatwa na Polisi usiku wa
kuamkia jana, eneo la Njiro jijini hapa. Ukamataji huo haukuhusisha
matumizi ya nguvu dhidi ya Mbunge huyo, bali mkewe alimsindikiza hadi
makao makuu ya Polisi kutoa maelezo kuhusu tukio la vurugu katika Chuo
cha Uhasibu juzi.

Kukamatwa kwa Lema ambaye ni Mbunge wa Chadema, kulithibitishwa jana
na Kamanda wa Polisi wa Mkoa, Liberatus Sabas, akisema polisi
walimkamata saa 9 alfajiri na hadi jana alikuwa akiendelea kuhojiwa na
kesho kutwa atafikishwa mahakamani kwa madai ya kusababisha
vuruguhizo.

"Tumemkamata na anahojiwa kuhusu vurugu zilizotokea chuoni juzi na
bado tunaendelea na uchunguzi wa kifo cha mwanafunzi Henry Koga (22)
aliyeuawa, lakini hatukutumia nguvu kumkamata na naomba watu watii
sheria bila shuruti," alisema Kamanda.

Aliongeza kuwa baadhi ya watu wanaojikusanyakwenye vikundi eneo la
Polisi ni vema watii sheria bila shuruti badala ya kuleta fujo hivyo
watulie ili polisi wafanye kazi zao.

Awali wafuasi wa chama hicho walionekana maeneo ya makaburini wakiwa
makini kusikilizakama Lema atapewa dhamana au la, lakini hadijana
mchana alikuwa akiendelea kuhojiwa na Polisi akiwa na wakili wake
ambaye polisi hawakumtaja jina.

Juzi Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Magesa Mulongo alisisitiza kuwa hawezi
kumtumia ujumbe mfupi wa maneno Lema wa kutaka kumbambikiza kesi bali
yeye ni kiongozi wa wananchi na anatimiza wajibu wake
kuhakikishausalama unakuwapo.

Mulongo alitoa kauli hiyo kutokana na madai ya Lema kwake kuwa
alimtumia ujumbe huo wa maandishi kwa njia ya simu ukimtishia
kumbambikia kesi. Mkuu wa Mkoa aliwapa polewanafunzi wa chuo hicho
ambao walikusanyika katika hospitali ya Mount Meru kuaga mwili wa Koga
na kabla ya kusafirishwa kwenda Iringa kwa maziko.

Mbowe ahadharisha Wakati huo huo, Mwenyekiti wa Chadema Freeman Mbowe,
ameihadharisha Serikali juu ya kukamata viongozi kwamba hali hiyo
isipodhibitiwa nchi inaweza kuchafuka. Alikuwa akizungumzia kukamatwa
kwa Lema na kufunguliwa mashitaka ya uchochezi na kuongeza kuwa
kukamatwa huko hakukuwa halali, kwa kuwa alikuwa akitimiza wajibu wake
wa ubunge.

"Napenda kuwasilisha masikitiko ya chama changu kwa Polisi Arusha
kwanza kutumia nguvu kwa kuzingira nyumba ya Lema usiku wamanane na
kumkamata kwa nguvu kama jambazi jambo ambalo halikuwa la lazima,"
alisema.

Alisema Lema alikumbwa na kadhia hiyo baadaya kuingilia kati vurugu
katika chuo cha Uhasibuambazo chanzo chake ni kuuawa na vibaka na
kuporwa kwa mwanafunzi wa chuo hicho.

"Kulitokea vurugu wanafunzi waliandamana wakitaka kuongezwa ulinzi,
Lema akiwa mbunge wa Arusha, alikwenda kuwatuliza na akiwa huko
akamwita Mkuu wa Mkoa wa Arusha wasaidiane, sasa Mkuu huyo akaharibu
wanafunzi wakazidisha jazba, wao sasa wanamkamata mbunge!" alishangaa.
Alisema pamoja na kukamatwa Lema, chama kinasikitishwa na polisi
kumvamia nyumbani usiku.

"Huyu hakuwa jambazi, kulikuwa na umuhimu gani wa kuzingira nyumba
yake na kumtaka atoke, huyu mbunge jamani ana watoto tena mmoja ana
mwaka mmoja na nusu, huku ni kumdhalilisha."

Alilitaka Jeshi la Polisi Arusha, kumpa Lema haki yake kwa kuwa
mashitaka yanayomkabili yanaruhusu dhamana na si haki kuzuia watu wake
wa karibu hadi wanasheria kumsaidia.

"Mimi naomba tu, huu utaratibu wa kukamata viongozi mara kwa mara
uangaliwe kwani utaligharimu Taifa, tuepuke kuingiza masuala ya
itikadi kwenye mambo ya usalama wa taifa, tukiendelea hivi nchi
inaweza kuchafuka," alisisitiza.
Taarifa zilizopatikana baadaye kutoka kwa Kamanda Sabas zilisema Lema
anatarajiwa kufikishwa mahakamani keshokutwa ambapo ataunganishwa na
watuhumiwa wenzake 14 waliofikishwa mahakamani juzi.


chanzo: habarileo

Vigogo Ardhi Wafikishwa Mahakamani

Dar/Korogwe. Maofisa waandamizi serikalini wamefikishwa katika
Mahakama tofauti Dar es Salaam na Korogwe jana wakituhumiwa kwa
makosa ya matumizi mabaya ya ofisi na kuhujumu uchumi.
Maofisa hao wanatoka Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi,
Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam na Halmashauri ya Wilaya ya
Korogwe.
Kesi ya Dar
Mpimaji wa Wizara ya Ardhi, Revocatus Wachawendera na Mpimaji wa
Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam, Steven Kongwa walifikishwa
katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu wakikabiliwa na mashtaka
mawili, likiwamo la matumizi mabaya ya ofisi. Kongwa aliwahi kuwa
Mkurugenzi wa Halmashauri ya Temeke na alistaafu miaka miwili
iliyopita.
Mwendesha Mashtaka wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa
(Takukuru), Wakili Hussein Mussa jana alidai mbele ya Hakimu Mkazi,
Augustina Mmbando kuwa washtakiwa hao walifanya makosa hayo kati ya
Januari 2000 na Desemba 2001. Akisomahati ya mashtaka yanayowakabili
washtakiwa hao, Wakili Mussa alidai kuwa washtakiwa hao kwa
pamojawakiwa waajiriwa wa ofisi ya umma, walitumia madaraka yao
vibaya.
Alisema walikiuka mamlaka ya ofisi zao kwa kugawa eneo la wazi
lililopo Mbezi ambalo lilitengwa kwa ajili ya bustani kinyume cha
sheria. Wakili Mussa alidai katika shtaka jingine kuwa maofisa hao kwa
pamoja walikiuka Kifungu cha 35 cha Sheria ya Mipango Miji Sura ya 355
iliyofanyiwa marekebisho mwaka 2002 kwa kuligawa eneo hilo.

Alidai kuwa washtakiwa kwa pamoja katika kipindi hicho cha Januari
2000 na Desemba 2001 wakiwa watumishi wa Halmashauri ya Jiji la Dar es
Salaam, kwa makusudi walikiuka sheria hiyo ya mipango miji na kugawa
eneo la Mbezi Kitalu L bila ya kupata kibalikutoka mipango miji. Baada
ya kusomewa mashtaka hayo, washtakiwa wote walikana na Wakili Mussa
alisema upelelezi umekamilika, hivyo aliiomba Mahakama kuipangia kesi
hiyo siku nyingine ili kuwasomea washtakiwa maelezo ya awali.

Ili kupewa dhamana, Hakimu Mmbando aliwataka kila washtakiwa kila
mmoja wao kuwa na mdhamini anayeaminika ambaye anafanya kazi katika
taasisi inayotambulika kisheria.
Sharti jingine ni la kila mdhamini kusaini bondi ya Sh10 milioni.
Washtakiwa walikamilisha masharti hayona kesi yao imeahirishwa hadi
Mei 20, mwaka huu.
Kesi ya Korogwe
Takukuru wilayani Korogwe imewashtaki vigogo watatu kwa makosa manne
likiwamo la kuhujumu uchumi na kusababishia hasara ya Sh56 milioni
kwenye Halmashauri ya Korogwe mkoani Tanga.
Mwendesha mashtaka wa Takukuru, George Magoti alimsomea mashtaka
mshtakiwa wa pili tu, Declley Nyato.
Mshtakiwa wa kwanza, ambaye ni aliyekuwa Mkurugenzi wa Halmashauri wa
wilaya hiyo, Christine Midello na mshitakiwa wa tatu, Ofisa Ardhi wa
Halmashauri ya Mji wa Korogwe, Emmanuel Ntatiye hawakuwapo mahakamani.
Mbali na kumsomea mashtaka, Magoti aliiomba Mahakama ya Wilaya ya
Korogwe kutoa hati zitakazowezesha kukamatwa kwa washtakiwa hao
wengine.
Magoti aliiambia Mahakama kuwa kati ya Julai na Agosti mwaka 2011,
Nyato na wenzake walitumia nyadhifa zao vibaya kwa kuidhinisha malipo
ya Sh15 milioni kwa Kampuni ya Concise pasipo kuishirikisha Bodi ya
Zabuni.
Katika kosa la pili, Nyato anadaiwa kuruhusu kufanyika kwa malipo ya
Sh41,050,000 kwa Kampuni ya Concise Geo Solution bila ya kuishirikisha
bodi ya zabuni na shtaka la tatu, wote wanatuhumiwa kupanga njama za
kutenda kosa namba moja na mbili.

Shitaka la nne ni la kuhujumu uchumi. Wote kwa pamoja wanadaiwa
kuisababishia Halmashauri ya Mji wa Korogwe, hasara ya Sh56,185,000 na
kuvunja Sheria ya Kuhujumu Uchumi.
Nyato aliyakana mashtaka yote. Hakimu Arnold
Kirekiano aliahirisha kesi hiyo hadi Mei 7, mwaka huu baada ya kutoa
masharti likiwamo la kuwa na mdhamini mmoja, ambaye ni mwajiriwa wa
umma au shirika linalotambuliwa ambaye ana makazi ya kudumu Korogwe au
fedha taslimu Sh9.4 milioni au hati ya mali isiyohamishika au maelezo
yatakayothibitisha mali hiyo aliyonayo mdhamini ina thamani sahihi
iliyotajwa na kusalimisha pasi za kusafiria mahakamani.



Chanzo: Mwananchi.co.tz

Vurugu zazuka Liwale Na Arusha

Liwale/Arusha. Uharibifu mkubwa wa mali ulifanywa juzi usiku Mjini
Liwale, Lindi baada ya wananchi wenyehasira kuchoma moto nyumba za
viongozi waandamizi, makao makuu ya Halmashauri ya Wilayana maghala ya
mazao kutokana na kuchukizwa kushushwa kwa bei ya korosho.
Nyumba zilizochomwa moto ni za Mbunge wa Liwale (CCM), Faith Mtambo,
Mwenyekiti wa Chama cha Msingi cha Umoja, Hassan Myao na Makamu wake,
Hassan Mpako, Diwani wa Viti Maalumu (CCM) Liwale,Amina Mnocha,
Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Liwale, Abbas Chigogola ambaye
pia ng'ombe wake tisa walikatwakatwa mapanga na kuachiwa ndama watatu.
Nyingine ni nyumba ya Mwenyekiti wa CCM wa Wilaya ya Liwale, Mohamed
Ng'omambo, Katibu Mwenezi wa CCM Mkoa wa Lindi, Mwenyekiti wa Chama
cha Msingi Minali, Mohamed Limbwilindi na Katibu wa chama hicho, Juma
Majivuno.
Wakati hayo yakitokea Lindi, huko Arusha, vurugu kubwa za wanafunzi wa
Chuo cha Uhasibu zilizuka jana baada ya kuuawa kwa mwanafunzi Henry
Kago (22), juzi usiku.
Kago, ambaye alikuwa mwanafunzi wa mwaka wa pili,anadaiwa kuwa
alifariki juzi saa nne usiku baada ya kuchomwa kisu na watu
wasiojulikana, akiwa njiani eneo la Kanisa la Wasabato akitokea chuoni
hapo kujisomea.
Ghasia za Liwale
Ghasia hizo zilianza juzi mchana katika Kijiji cha Liwale B na
ziliendelea usiku kucha hadi jana asubuhi.
Watu walioshuhudia ghasia hizo walisema chanzo ni wakulima kudai
kulipwa Sh600 na siyo Sh200 za mauzo ya korosho kwenye Chama cha
Msingi Minali.
Bei ya kilo moja ya korosho waliyokubaliana wakulimana chama hicho ni
Sh1,200 na mara ya kwanza kiliwalipa Sh600 kwa kilo na kuahidi kulipa
nusu nyingine baadaye.
Hata hivyo, viongozi wa Ushirika walibadili uamuzi na kulipa Sh200 kwa
maelezo kuwa mauzo hayakuwa mazuri kitendo ambacho kiliwakasirisha
wakulima haoambao waligoma kupokea fedha hizo.
Baadaye ilielezwa kuwa viongozi wa Minali walipeleka fedha hizo polisi
ili malipo yafanyike huko, lakini ghasia zikaibuka na wakaamua
kusitisha malipo hayo na ndipo wananchi wakaamua kuingia mitaani.
Mmoja wa mashuhuda alisema "Polisi walijaribu kuwadhibiti watu hao,
lakini walipoona wanazidiwa nguvu, wakawaachia wafanye wanavyotaka
ndiyo maana kumekuwa na uharibifu mkubwa."
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Lindi, George Mwakajinga alisema kwa kifupi:
"Hali imetulia na vurugu zimemalizika lakini bado tuko kwenye kikao
kuzungumzia suala hili."
Wakulima hao walikerwa na tamko la Limbwilindi ambaye ndiye aliyetamka
kwamba watalipwa Sh200 kwa kilo na kuamua kwenda kuchoma moto nyumba
yake na baadaye ya Katibu wake Majivuno.
Limbwilindi hakupatikana kuzungumzia tukio hilo lakini, Majivuno
alipohojiwa alisema: "Tulikubaliana kuwalipa Sh1,200 kwa kila kilo,
lakini kwa awamu.
tuliwapa Sh600 awali na nusu yake imeshindikana kwakuwa mauzo hayakuwa
mazuri. Biashara haikwenda vizuri, ndiyo maana tukawaambia tutawalipa
Sh200 lakini wakakataa wanataka fedha zote Sh600, sasa sisihatuna
fedha hizo. Kama biashara ingefanyika kwa faida tungewalipa."
Habari zilizopatikana baadaye jana zilidai kuwa mke wa Mkungura, Amina
Mmoto amelazwa katika Hospitali ya Wilaya ya Liwale baada ya kupata
shinikizo la damu kutokana na sakata hilo.
Akizungumza kwa simu kuelekea Liwale, Mbunge Mtambo alisema:
"Nimesikitishwa na ghasia hizi... wamenitia hasara kubwa. Nyumba zangu
zote mbili zimechomwa, sijui nitaishi wapi. Hakuna kingine hizi
nisiasa tu...hakukuwa na sababu ya kufanya hivyo. Kama ni kulipwa
Sh200, mbona vyama vingine wamelipwa fedha hizo na hakukuwa na vurugu?
Jana kutwa nzima, Mji wa Liwale ulikuwa na utulivu huku polisi
wakitawanya makundi ya watu waliokuwa katika vikundi kwa mabomu ya
machozi na shughuli za biashara zilisimama na hakuna maduka wala
magenge yaliyofunguliwa.

Vurugu Arusha
Kutokana na vurugu hizo, Chuo cha Uhasibu cha Arusha, kimefungwa kwa
muda usiojulikana kwa usalama huku wanafunzi wakitakiwa kuondoka
chuoni hapo hadi watakapotangaziwa tena.
Licha ya kuelezwa kwamba aliuawa kwa kisu, Mkuu wa Mkoa wa Arusha,
Magesa Mulongo alisema taarifanyingine, zinaeleza kuwa aliuawa
akitokea katika Ukumbi wa Disko wa Bugaloo jirani na chuo hicho.
Baada ya taarifa za kifo hicho, wanafunzi wa chuo hicho walikusanyika
jana asubuhi na kuanza maandamano hadi Kituo Kikuu cha Polisi
wakilalamikia ulinzi duni.
Mbunge wa Arusha Mjini (Chadema), Godbless Lema alifika na kuwatuliza
wanafunzi hao na kuzungumza nao, kwa zaidi ya saa tatu wakati
wakimsubiri Mkuu wa Mkoa.
Hata hivyo, baada ya kufika chuoni hapo, mkuu huyo wa mkoa alishindwa
kuzungumza kutokana na kutokuwa na kipaza sauti na kusababisha
wanachuo kumzomea kabla ya uongozi wa chuo kubadili eneo la mkutano.
Hata hivyo, zomeazomea iliendelea na mkutano kuvunjika na FFU kufika
na kurusha mabomuya machozi.
Akizungumza na waandishi wa habari jana mara baada ya kumalizika kwa
Kikao cha Kamati ya Ulinzi na Usalama na uongozi wa chuo hicho, mkuu
huyo wamkoa alisema polisi wanafanya uchunguzi wa suala hilo.

"Baada ya kuletewa taarifa za tukio hili na Mbunge
Lema, niliondoka na kwenda kuwasikiliza wanachuo lakini tayari nilijua
mazingira yalikuwa yamebadilishwana pale nikagundua Lema ndiyo amekuwa
msemaji mkuu badala ya uongozi wa chuo au Serikali ya wanachuo. Ndiyo
maana mkaona na zomeazomea ile," alisema Mulongo.
Alimtuhumu mbunge huyo uchochezi na ameamuru kukamatwa kwake na
wanafunzi waliohusika na vurugu zile.

Lema alieleza kusikitishwa na agizo la kutakiwa kukamatwa akisema
alizuia maandamano kufika mjini...
"Nyie waandishi wa habari mlikuwepo nimezungumza zaidi ya saa mbili na
wale wanafunzi kuwasihi watulie wasiandamane na mimi ndiye nilimpigia
simu Mkuu wa Mkoa aje kuwasikiliza wanafunzi iweje niwachochee kufanya
fujo? Ninawasubiri waje wanikamate."


Chanzo: Mwananchi

Ubalozi Wa Ufaransa Washambuliwa

Bomu limelipuka nje ya ubalozi wa Ufaransa katika mji mkuu wa Libya,
Tripoli na kuwajeruhi walinzi wawili huku ikisababisha uharibifu
mkubwa.
Mlipuko huo ulisababisha uharibifu katika sehemu moja ya ofisi hizo na
pia kuharibu nyumba jirani.
Mwandishi wa BBC mjini Tripoli, Rana Jawad anasema kuwa inaaminika
kuwa mlipuko huo ulisababishwa na gari lililokuwa na mabomu.
Rais wa Ufaransa, Francois Hollande, aliitaka serikali ya Libya
kuchukua hatua za haraka kukabiliana na waliosababisha shambulio hilo.
Aliongeza kwamba shambulizi hilo lililenga nchi za kigeni
zinazopambana dhidi ya ugaidi.

Balozi za kigeni nchini Libya zimewahi kushambuliwa katika siku
zanyuma, lakini hili ndilo shambulizi la kwanza kubwa dhidi ya ubalozi
wa kigeni mjini Tripoli.

Shambulizi liliwahi kufanywa dhidi ya ubalozi wa Marekani mjini
Benghazi mwezi Septemba mwaka jana na kusababisha kifo cha balozi
Christopher Stevens pamoja na maafisa wengine wamarekani.
Shambulio la leo lilifanyika muda mfupi baada ya saa kumi na
mojaasubuhi katika mtaa wa kifarahari mjini Tripoli.

Wakaazi wa eneo hilo walighadhabishwa sana na shambulizi hilo na
kulalamikia ukosefu wa ulinzi mzuri wa sehemu hiyo.

Waziri wa mambo ya nje wa Libya, Mohammed Abdel Aziz alilaani vikali
shambulizi hilo, ingawa hawajaeleza ni nani wanayemshuku kulifanya.

Chanzo:BBC

Ubovu Wa MiundoMbinu

Hii ni barabara Inayounganisha Mkoa wa Tabora na Katavi, Hali imekuwa
korofi baadhi ya maeneo na kusababisha magari kushindw kupita na
kusababisha msururu kusubiri kukwamua Magari yaliyo Kwama, Kabla ya
Eneo la Ipole ambako ujenzi wa Daraja Unaendelea hali ni mbaya na pia
katika Eneo mbele kidogo ya Mji wa Inyonga mkoani Katavi. Juhudi za
Hali zinahitajika kuokoa usafiri wa unaunganisa Mikoa hii ya
Magharibi. Kigoma, Tabora, Katavi na Rukwa

Wamaasai Wa Loliondo, Serikali Inafikiria Nini?

Katika kijiji kimoja Kaskazini mwa Tanzania, ndege aina ya Boeing 747
zinatua kwenye kiwanja binafsi, magari yenye nambari za usajili za
milki za kiarabu, zikiendeshwa katika eneo hilo na yeyote mwenye simu
ya mkononi anapotua hapo hupokea ujumbe ambao haukutarajiwa:
''Hujambo mgeni na karibu UAE.''

Kwa karne nyingi, (Savanna) katika eneo la Arusha lilikuwa makao kwa
watu wa jamii ya wamaasai lakini siku hizi mtu sasa anaweza kudhania
yuko Dubai moja ya nchi za milki za kiarabu.

Hii ni kwa sababu sehemu kubwa ya ardhi mjini Arusha hasa katikaeneo
la Loliondo karibu na mbuga ya kitaifa ya wanyama ya Serengeti
imekodishwa kwa kampuni ya uwindaji ya Emirati iitwayo Ortello
Tangu mwaka 1992, kampuni hiyo imekuwa ikiwapeleka kwa ndegewatalii
matajiri zaidi kuwinda simba na wanyama wengine hali
iliyowaghadhabisha wenyeji wa eneo hilo ambao ni wamaasai ambao
wamezuiwa kuwalisha mifugo wao katika maeneo ya kuwinda.

Sasa serikali ya Tanzania inataka kutoa ardhi zaidi kwa wawindaji hao
kwa lengo la kujenga barabara ya umbali wa kilomita 1,500 ambako
wanyamapori watakuwa wakipita kwa manufaa ya kampuni hiyo ya uwandaji.
Mpango huo utawaathiri takriban watu 30,000 watakaoachwa bila makao na
pia kuwaathiri maelfu ya wengine, ambao huwalisha mifugo wao katika
maeneo hayo wakati wa msimu wa kiangazi.
Wamaasai wameghadhabishwa mno na hata kufanya maandamano, wakisema
kuwa maisha yao yataathirika pakubwa.

Zaidi ya asilimia ya 90 ya wakaazi wa Loliondo ni wa Maasai
ambaohutegemea kuwalisha mifugo wao nyasi kutoka eneo ambalo serikali
inanuia kuwakodishia waarabu.
"bila Ardhi hatuwezi kuishi,'' anasema mama Naishirita Tenemeri,
mwenye watoto watatu.
Bi Tenemeri anafuga Ng'ombe na Mbuzi eneo la Loliondo, ili kuwanunulia
chakula na kuwalipia karo ya shule wanawe.

Wa Maasai wana historia ya kupoteza ardhi yao nchini Tanzaniatangu
wazungu walipowahamisha kutoka mbuga ya Serengeti mwaka 1959.

Mapema mwezi huu, Bi Tenemeri, akiwa amejifunga shuka yake nyekundu,
alijiunga na watu 1,000 wengi wao wakiwa wanawake chini ya miti ya
mivule, katika kijiji cha Olorien kupinga mipango ya serikali kuuza
ardhi yao.
Wengine walitembea kwa siku nyingi kuonyesha ghadhabu yao kwakujiondoa
katika chama tawala cha CCM kama wanachama.

"ikiwa sina ardhi, sina mahala pa kujifungulia watoto wangu,'' alisema
Bi Morkelekei Gume,akitupa kadi yake ya uwanachama wa CCM chini .
"mwanangu yuko katika shule ya upili, kwa sababu ya nyasi zinazotoka hapa.''
''Ikiwa wanataka ardhi yangu wanaweza kuniua.''
Mwanamke mmasaai anashikia bango linalosema "tutapigania ardhiyetu
hadi mwisho wake.'' Wanawake hapa ndio wamekuwa wakisikika zaidi
katika maandamano yao.
Wanawake wamekuwa wakisikika zaidi, wameathirika zaidi kutokana na
hatua ya serikali kuwafukuza, wakiachwa bila kazi kuwalea watoto wao
kwa hali ngumu wakati wanaume wakienda katika sehemu za miji ambako
wanapata kazi kama walinzi.
Pia wameongoza maandamano tangu viongozi wao wa kisiasa waliopinga
mpango wa ujenzi wa barabara waliokuwa wamesema wataondoka katika
chama tawala kukosa kutimiza ahadi zao.
Eneo la Loliondo lina wanyama wengi wa porini na hivyo kuvutia watalii
ingawa sio wengi. Linapakana na mbuga ya wanyama ya Maasai Mara
iliyoko Kenya pamoja na hifadhi ya wanyama ya Ngorongoro.
Waziri wa utalii Khamis Kagasheki anatetea hatua ya serikali kutaka
kuwaondoa wamasaai katika eneo hilo akisema kuwa mradi huo utasaidia
katika kuendeleza uhifadhi kwani Maasai wametumia ardhi hiyo vibaya.
Lakini wasomi wanasema kuwa jamii ya wamaasai kawaida hawaathiri wanyamapori.
"nina swali moja kubwa kwa wanaosema kuwa wamaasai ni tisho kubwa kwa
wanyamapori kuliko kampuni hiyo ya kiarabu ya OBC," alisema Benjamin
Gardner wa chuo kikuu cha Washington na ambaye amesomea maswala ya
ardhi miongoni mwa wamaasai kwamiongo miwili.
Ni nadra kwa wamaasai kuwinda wanyama na hutumia ardhi kuzuiabaadhi ya
wanyama kujifungulia huko kwani ni tisho kwa mifugo wao.
Mashirika 13 ya kijamii kutoka kote nchini Tanzania, yamesema kuwa
wamaasai, wana vibali vichache sana vya kumiliki ardhi, na kuwa
serikali inawapotosha watu
Viongozi wa jamii hiyo wanapanga kwenda mahakamani kuishtaki serikali,
lakini wanahofia kuwa huenda swala hilo likakosa kutatuliwa haraka
kwani kuna kesi moja iliyowasilishwa mwaka 2009 na haijapata ufumbuzi
hadi wa leo.

Ahukumiwa Maisha Jela Kwa Kumbaka Mwanae

MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi ya Wilaya ya Mpanda Mkoa wa Katavi,
imemuhukumu Abisai Joseph (40) mkazi wa Mtaa wa Kigamboni, Kata ya
Shanwe mjini hapa kifungo cha maisha jela kwa kosa la kumbaka mtoto
wake wa miaka sita.
Hukumu hiyo ilitolewa jana na Hakimu Mkazi Mfawidhi wa mahakama ya
wilaya hiyo, Chiganga Tengwa ambapo Joseph anadaiwa kutenda kosa hilo
Desemba 18 mwaka jana, saa tano usiku akiwa nyumbani kwake.
Awali, Mwendesha Mashtaka Ally Mbwijo, aliieleza mahakama kuwa siku
hiyo ya tukio Joseph alimbaka mwanaye baada ya kumvizia wakati alipo
toka kujisaidia haja ndogo.

Alidai kuwa baada ya kumkuta nje, alimvua nguo kisha alimweka sehemu
ya mapaja yake na kuanza kumfanyia kitendo hicho, na kwamba pamoja na
mtoto huyo kupiga kelele za kuomba msaada, mama yake aliyekuwa amelala
ndani hakuweza kusikia.

Mbwijo aliongeza kuwa baada ya kumaliza kufanyiwa kitendo hicho, mtoto
huyo aliingia ndani akilia, hali iliyomfanya mama yake amuulize,
lakini baba yake alijibu upesi kuwa alimkuta nje akibakwa na balozi
waowa nyumba kumi.
Alidai kuwa baada ya maelezo hayo, mama wa mtoto, Sauda Rajabu
alikwenda kwa majirani kuwapa taarifa ya kitendo hicho, lakini
walimshauri ende kutoa taarifa polisi.
"Akiwa hapo polisi mtoto huyo alikana kubakwa na balozi wao, bali
alisema aliyembaka ni baba yake mzazi," alidai.
Katika kesi hiyo, upande wa mashtaka ulikuwa na mashahidi wanne
akiwemo mtoto mwenyewe aliyebakwa na mshtakiwa hakuwa na shahidi
yeyote.

Hakimu Chiganga katika hukumu hiyo alisema mahakama imeridhika na
ushahidi uliotolewa na kwamba imemtia hatiani mshtakiwa kwa kuvunja
sheria namba 130 (1) (e) na 131 (3) kifungu cha marekebisho ya sheria
ya mwaka 2009.

Alisema kutokana na kosa hilo mahakama inamuhukumu Joseph kifungo cha
maisha jela ili liwe funzo kwa watu wengine wenye tabia kama hiyo.




Chanzo: Nassor Wazambi(fb)

Tundu Lissu Na Wabunge Watano Wa Cha Wapigwa Stop Bungeni

MNADHIMU wa Upinzani na Mbunge wa Iramba Mashariki, Tundu Lissu na
wabunge wengine watano wa Chadema wameamriwa na kiti cha
Spikakutoingia bungeni kwa siku tano kutokana na utovu wa nidhamu.
Wabunge wengine ambao wamepewa amri ya kutohudhuria kwa siku tano ni
Mbunge wa Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi; Mbunge wa Arusha Mjini,
Godbless Lema, Mbunge wa Iringa Mjini, Peter Msigwa, Mbunge wa
Ilemela, Highness Kiwia na Mbunge wa Nyamagana, Ezekiah Wenje.

Wakati wabunge hao watano wamepewa adhabu hiyokutokana na utovu wa
nidhamu wakimkinga Tundu Lissu asitolewe nje na askari, Tundu Lissu
adhabu yake inatokana na kukaidi kukaa chini, Kiti kilipomuaru kufanya
hivyo na kukataa kutoka nje alipoamriwa kutoka.

Kutolewa nje huko kulitanguliwa na kizaazaa cha dakika kadhaa katika
ukumbi wa Bunge wakati likikaribia kuahirishwa ambapo Tundu Lissu
ambaye alitaka kutoa mwongozo wakati Mbunge wa Iramba Magharibi (CCM),
Mwigulu Nchemba akichangia bajeti ya Ofisi ya Rais Menejimenti ya
Utumishi wa Umma kuamriwa na Naibu Spika Job Ndugai kukaa na kukaidi.
Wakati tukio hilo likitokea muda wa saa moja na dakika 35 usiku,
Nchemba alikuwa anaeleza kuwa kiongozi wa Chadema Willibrod Slaa
alifanya mkutano wa ndani na viongozi wa kidini, kauli ambayo
ilimfanya Lissu aamke na kutaka mwongozo ambapo Naibu Spika Ndugai
alimkatalia kwa kumwambia kwamba anaingilia muda wa wachangiaji
wengine na ameshasimama mara 20 kuomba mwongozo na kutoa taarifa.
Hata hivyo, Mbunge huyo alikaidi amri hiyo ya kukaa chini ndipo Ndugai
alipoamuru: ''Askari toa nje Tundu Lissu .. nasema toa nje'' lakini
Lissu aliendelea kugoma ndipo hali ilipobadilika katika ukumbi huo na
kuanza kusikika maneno..
" watu katika Tv wanacheka... uonevu... " na wabunge wa Chadema
wakatoka kwenda kuzuia Lissu kuondolewa katika ukumbi wa Bunge, licha
ya kwamba askari watatu walikuwa tayari wamesogea kwenda kumuondoa
Lissu.
Wabunge hao ni Msigwa, Mbilinyi , Lema , Kiwia na Wenje . Wakati
wabunge hao wakiendelea kuzozana na askari hao, Ndugai akatangaza
kuongeza adhabu nyingine kwa Tundu Lissu ya kutohudhuria Bunge kwasiku
5 baada ya kukaidi ile ya awali ya kumtaka atokenje ya Bunge na kuita
askari zaidi kutoka nje.
Wakati askari hao wakiingia kuongeza nguvu Naibu Spika alitoa adhabu
ya kutohudhuria Bunge kwa siku tano kwa wabunge watano ambao ni
Mbilinyi, Lema, Msigwa, Kiwia na Wenje kwa utovu wa nidhamu.
Kuongezeka kwa askari kuliwafanya wabunge hao waChadema kushawishi
wenzao ambao walitoka nao njeya Bunge saa moja na dakika 42, dakika
tatu kabla yakuahirishwa kwa Bunge.
Lissu akizungumza nje ya ukumbi wa Bunge alisema kwamba hakubaliani na
uamuzi wa Naibu Spika na kwamba leo atakuja bungeni kwani hakuna
kifungu cha kanuni kinachoruhusu atolewe bungeni kwa siku tano na
kinachozuia asisimame na kuongeza:
"hata kusimama mara 30 naruhusiwa". Akichangia hoja ya bajeti ya Ofisi
ya Rais, Mbunge wa Iramba Magharibi, Mwigulu Nchemba alisema Dk Slaa
alikusanya viongozi wa dini katika mkutano wa ndani badala ya
wanachama wa Chadema.
Hata hivyo, Susan Kiwanga alisimama kumpa taarifa Nchemba kuwa mkutano
huo haukuwa wa viongozi wa dini bali wa wadau wa Chadema.

Serukamba (MB) Afumua F***k(!!!!!!!!!!!) Bungeni, Spika kutumia Askari Kuwatoa Wabunge watumizi wa Lugha chafu.

PAMOJA na Spika wa Bunge, Anne Makinda, kutishia kutumia Polisi
kudhibiti wabunge wanaotukana bungeni, jana Mbunge wa Kigoma Mjini,
Peter Serukamba (CCM), alijikuta akitukana matusi ya nguoni bungeni.
Mbunge huyo alijikuta akitukana wakati wa mjadala kuhusu kusitishwa
kwa hotuba ya Kambi Rasmi ya Upinzani, kuingilia Mhimili wa Mahakama.
Awali kabla ya Serukamba kutoa tusi hilo kwa Kiingereza, akisema
'F***'(haliandikiki hapa), hotuba hiyo kuhusu makadirio ya mapato na
matumizi ya ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma, ilizua
mabishano miongoni mwa wabunge.
Ubishi huo ulitokana na hoja kwamba sehemu yake, inaingilia kesi
inayomkabili Mkurugenzi wa Ulinzi na Usalama wa Chadema, Wilfred
Lwakatare.
Kutokana na hali hiyo, hotuba hiyo ilizuiwa kusomwa jana mchana katika
muda uliokuwa imepangiwa; badala yake ililazimika kusubiri kwanza
Kamati ya Bunge ya Kanuni, kwenda kuijadili na kutoa uamuzi,
ilikukisaidia Kiti cha Spika kutoa uamuzi.
Awali Msemaji wa Kambi ya Upinzani, Profesa Kulikoyela Kahigi
alipoanza kusoma hotuba hiyo, Serukamba alisimama na kusema kurasa nne
za kwanza za hotuba hiyo, zinaingilia uhuru wa Mahakama.
Serukamba alisema katika hotuba hiyo, kunatajwa kesi ya Wilfred
Lwakatare, suala ambalo liko mahakamani na kuongeza, kwamba Mbunge wa
Mbulu, Mustafa Akunay (Chadema), wakati wa kujadilihoja ya Waziri
Mkuu, alionya kuwa kuzungumza sualahilo ambalo liko mahakamani ni
kuingilia uhuru wa Mahakama.
Kwa hoja hiyo, Serukamba aliomba Naibu Spika, Job Ndugai, amwamuru
Msemaji wa Kambi ya Upinzani, asisome kurasa za kwanza hadi nne, kwa
maelezo kuwa zina mambo mengi yanayoingilia mhimili mwingine wa Dola.
Mpambano wa hoja Wakati mjadala huo ukianza, Kiongozi wa Kambi ya
Upinzani Bungeni, Freeman Mbowe na Mnadhimu Mkuu wa Kambi hiyo, Tundu
Lissu, walikuwa wakishuhudia majadiliano wakiwa nje ya ukumbi wa
Bunge, wakaamua kurudi ndani ya ukumbi haraka, kuwahi mjadala.
Wakati Mbowe na Lissu wakiingia kwa mwendo wa haraka ndani ya ukumbi
wa Bunge, Mbunge wa Ubungo John Mnyika (Chadema), alitetea hotuba
hiyokwa maelezo kuwa hakuna suala ambalo liko kwenye hotuba hiyo
lililoko mahakamani.
Mnyika, ambaye alikuwa anatoa taarifa kwa Serukamba, alisema mambo
kwenye hotuba hiyo yanahusu vitendo vya utekaji wa Dk Steven Ulimboka
na Absalom Kibanda, ambavyo haviko mahakamani, ila vinafanywa na Idara
ya Usalama wa Taifa.
Mnadhimu Mkuu wa Serikali, William Lukuvi, alisimama kumpinga Mnyika,
akieleza kuwa kurasa zahotuba hiyo zinataka kuifanya kesi ya Lwakatare
iwe ya kisiasa, badala ya kuiachia Mahakama ifanye kazi yake.
Baada ya hoja hizo, Ndugai, alitoa uamuzi akikubaliana na hoja za
Serukamba na Lukuvi kuwa nikweli hotuba hiyo ina mambo ambayo yako
mahakamani.
"Ndugu zangu wa Chadema haya mambo mnayoleta hapa tumeshahadharishwa
kuwa yako kortini, lakini pia yanaweza kuleta mjadala wa ajabu hapa
bungeni,hivyo naomba yasisomwe," alisema Ndugai jambo ambalo
lilimfanya Mbunge wa Kawe, Halima Mdee naMbunge wa Singida Mashariki,
Lissu kusimama kupinga uamuzi huo.
Lissu katika maoni yake, alionesha Sheria ya Usalamawa Taifa namba 15
na akamtaka Lukuvi aeleze hoja zake amezitoa wapi. Alisema sheria hiyo
inakataza kuandika jina nje ya Bunge na si bungeni.
"Haya maneno ya Lukuvi ni ya kuokoteza tu mitaani, hakuna sheria
inayokataza Bunge lisijadili majina ya usalama," alisema.
Mnadhimu huyo wa Kambi ya Upinzani, alisema itakuwa ni hatari kwa
Bunge kukatazwa kujadili suala la Idara ya Usalama wa Taifa, wakati
kuna waziri anayesimama na kuomba fedha za wananchi kwa ajiliya idara
hiyo. Hoja za ajabu ajabu Lissu alisema kama kuna 'madudu' yanafanywa
na idara hiyo, Bunge linamwajibisha waziri husika, "Hivyo hizi hoja za
ajabu ajabu zinazotolewa hapa bungeni naomba Naibu Spika uzikatae,"
alisema.
Naibu Waziri wa Sheria, Angela Kairuki, alisema Lissu anapotosha Bunge
na akasoma sheria inayokataza kuwa hairuhusiwi hadi kupata kibali cha
waziri mwenye dhamana, kutangaza majina ya maofisa wa Idara ya Usalama
wa Taifa.
Mbunge wa Simanjiro, Christopher ole Sendeka (CCM), alisema hotuba ya
upinzani inazungumzia mtumishi wa Idara ya Usalama wa Taifa,
anayedaiwakughushi ushahidi dhidi ya Lwakatare, jambo ambalo liko
mahakamani.
"Bunge lijiheshimu kwa kutojadili mambo yanayoingilia uhuru wa mhimili
mwingine wa Dola, haya mambo ya kughushi ushahidi ni kuingilia
Mahakama," alisema Sendeka.
Baada ya malumbano hayo, Ndugai alisema kwa kuwa suala hilo ni la
kikanuni, akaamuru Kamati hiyo ikae na kulitolea ufumbuzi suala hilo.
Serukamba aomba radhi Bunge liliporejea jioni, Serukamba alisimama na
kuonwa na Naibu Spika ambaye alimpafursa ya kuzungumza, naye akaomba
radhi kwa kauli aliyoitoa asubuhi akisema imemfedhehesha na kwamba
ilimtoka kwa bahati mbaya.
Hata hivyo, Mbunge wa Nyamagana, Ezekiah Wenje alisimama na kutaka
agizo la Kiti la polisi wa Bunge kutumika kumtoa nje mbunge
atakayetukana, lianze kutekelezwa kwa Serukamba.
Ndugai aliahidi kulitolea uamuzi suala hilo, lakini akaruhusu Kambi ya
Upinzani kuendelea na hotuba yake, baada ya kufanyiwa marekebisho kwa
maagizo ya Kamati ya Kanuni ya Bunge.
Hilo lilifanyika. Wakati huo huo, Naibu Spika wa Bunge, amempa siku
saba Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema, athibitishe kauli yake
kwamba Rais Jakaya Kikwete, ndio kinara wa udini nchini.

Bi Kidude Afariki

Mwimbaji nguli wa muziki wa tarabu nchini Tanzania Fatma binti Baraka,
maarufu kama Bi Kidude amefariki Jumatano kisiwani Zanzibar akiwa na
umri wa zaidi ya miaka 100.
Taarifa ya kifo chake ilitolewa na mjukuu wake Fatuma Baraka ambaye
pia ni muimbaji wa Taraabu. Alisema Bi Kidude alifariki hospitalini
kutokana na maradhi ya kisukari na uvimbe kwenye Kongosho.
Bi Kidude amekuwa katika fani ya muziki wa taarab ya kiasili pamoja na
ngoma za unyago kwa zaidi ya robo tatu ya umri wake.

Katika miaka ya karibuni afya yake imekuwa ikizorota kiasi cha
serikali ya Zanzibar kumzuia kupanda majukwaani kuburudisha japokuwa
alionekana katika tamasha la Sauti za Busara mwezi Februari mwaka huu.
Mipango ya mazishi ya nguli huyu inafanywa nyumbani kwake Zanzibar.

Wengi, hasa vijana wa kizazi kipya wanamfahamu Bi. Kidude kwa uwezo
wake mkubwa wa kuimba taarabu kwa kuchanganya lugha ya kiswahili na
ile ya kiarabu. Nyimbo zake za kiarabu mara nyingi zimekuwa na ladha
kama ile ya aliyekuwa mwimbaji gwiji wa Misri Ummu Kulthumu.
Sio uimbaji tu uliomfikisha Bi. Kidude alipofika, bali uwezo wake pia
wa kutunga mashairi, kutumia ala za mziki kama vile kupiga ngoma na
hata ngoma za unyago, vyote hivi vilimuweka Bi. Kidude katika nafasi
tofauti katika jamii.
Alikuwa na tabia ya kumwita kila mtu 'mwanangu,' ingawa yeye mwenyewe
hakubahatika kupata mtoto. Katika mahojiano aliyofanyiwa na vyombo
mbali mbali vya habari, mwenyewe alisikika akisema, ingawa alikuwa na
hamu ya kupata mtoto, lakini Mwenyezi Mungu hakumjaalia.
Katika miaka ya hivi karibuni, Bi. Kidude alishirikishwa sana na
wasanii wengine katika kazi zao. Miongoni mwao ni Ahmada Amelewa, Fid
Q Juhudi za Wasiojiweza.
Mbali na hayo, mashirika mbali mbali yakiwemo ya kibiashara na yale
yasiyo ya kiserikali yaliona mvuto aliokuwa nao Bi. Kidude katika
jamii, hivyo wakamtumia katika matangazo mbali mbali maarufu likiwa
lile la kutokemeza Malaria.
Ni bibi aliyebahatika kusafiri takriban duniani kote, na vilevile
katikamaisha yake alijinyakulia tuzo lukuki. Miongoni mwa hizo ni ile
ya 2005 WOMEX ikiwa ni kutambua mchango wake mkubwa katika tasnia ya
muziki.
Katika siku zake za mwisho, Bi. Kidude alikuwa akiumwa, lakini wengi
wanahusisha kuumwa kwake na utu uzima aliokuwa nao.
Kifo chake ni pigo kubwa kwa wote, lakini zaidi ni wanamziki wa kizazi
kipya waliokuwa wakimuona Bi. Kidude ni nyanya yao.

Aliyefariki Miaka Mitano Iliyopita Afufuka

Mji wa Geita na maeneo ya jirani juzi ulikumbwa na taharuki ya aina
yake, pale mwanamke ambaye anadaiwa kwamba alifariki miaka mitano
iliyopita alipoonekana akiwa hai katika eneo la Kasamwa.
Inadaiwa kwamba Flora Onesmo (45) alifariki Februari 28, 2008 katika
Hospitali ya Wilaya ya Geita na kuzikwa katika Kijiji cha Nakasenya,
Kata ya Butundwe, lakini juzi alfajiri alikutwa ameketi nje ya nyumba
ya dada yake aitwaye Monica James, anayeishi Kasamwa.
Aliyekuwa wa kwanza kumwona Flora ni mdogo wake aitwaye Monica Onesmo
ambaye baada ya kuamka saa 11:00 alfajiri nyumbani kwa dada yake,
alimwona mwanamke aliyekuwa ameketi nje ya nyumba hiyo, lakini
alimfananisha mwanamama huyo na marehemu dada yake.
"Baada ya kumwona nilimwita mtoto wake tunayekaa naye na nikampigia
simu dada (Monica) ambaye alikuwa amelala chumba kingine nikamwambia
kwamba nimeamka na kumkuta mwanamke amekaa hapa nje, lakini kila
nikimwangalia anafanana na marehemu dada yetu,"alisema Jubili na
kuongeza kwamba alipowaita wote walitoka nje.
Alisema mtoto wa Flora (marehemu anayedaiwa kufufuka) anaitwa Rebeka
Elisha (16) na kwamba walimchukua tangu 2008 wakati mama yake huyo
alipofariki dunia katika Hospitali ya Geita ambako alikuwa amelazwa
kutokana na kusumbuliwa na ugonjwa wa ini.
Rebeka ambaye ni mtoto wa nne wa Flora alisema: "Mama mdogo alituita
sisi tulikuwa tumelala akasemakwamba nje kuna mwanamke ambaye
anafanana na marehemu mama yetu, ndipo na sisi tukatoka na kweli
kumwangalia alikuwa ni yeye kabisa."
Alisema walipomuhoji mama yake huyo kwamba ametokea wapi, aliwaeleza
kuwa ametoka eneo la Katoro kwa mganga na aliletwa na watu ambao
hakuwatambua Alhamisi saa 1:30 usiku ndani ya gari na watu hao
walimshusha kwa mtu aitwaye Juma Luchunga ambaye ni jirani na dada
zake hao.
Kauli ya Flora
Akizungumza na waandishi wa habari, Flora alisema yeye ni mkazi wa
Katoro na kwamba alitokea Katoro nyumbani kwa mganga wa jadi ambaye
hata hivyo hakumtaja kwa maelezo kwamba wataalamu wake (majini)
wamemkataza.
"Nilikuwa naishi kwa mganga wa kienyeji ila alikuja mwanaume wakati
nikiwa pale akaninywesha dawa kisha tukapakizwa kwenye gari na watu
wawili ambaosikuwatambua, mmoja mwanamke na mwingine mwanaume mpaka
hapa Kasamwa tukashushwa saa 1:00 jioni,"alisema Flora.
Alisema alipofika Kasamwa alikwenda kunywa uji kwamama mmoja ambaye
pia hakumtaja na kwamba baadaye alipelekwa nyumbani kwa mtu mwingine
saanne usiku, lakini watu wa nyumba hiyo walipomwona walimwambia:
"Hapa si kwako twende tukupeleke kwa ndugu yako" na ndipo wakampeleka
kwa dada yake ambako aliketi nje hadi alfajiri.
Flora alisema kabla ya kuishi kwa mganga alikuwa akiishi porini ambako
alitupwa na watu asiowafahamuna baadaye aliokotwa na wasamaria wema
ambao ndiyo walimpeleka kwa mganga ambako alikuwa akiishi muda wote.

Ndege Yaanguka Arusha

Arusha: Ndege ya Marehemu Wakili Nyaga Mawalla yaanguka na kuharibika
'write-off'
- Habari zilizotufikia hivi punde ni kwamba ndege iliyokuwa
inamilikiwa na Wakili maarufu Marehemu Nyaga Mawalla aliyefariki wiki
3 zilizopita na kuzikwa huko Nairobi, imeanguka ikiwa katika hatua za
mwishoza kutua (final approach) katika kiwanja cha ndege chaArusha.
- Taarifa zinasema kuwa ndege hiyo ilikuwa na rubani pekee
anayejulikana kwa jina la Jamal B S, au maarufukama "Bob Sambeke"
aliyekuwa anatokea West Kilimanjaro ambaye naye kapoteza maisha
(kafariki)!
- Inadaiwa kuwa ndege hiyo ilijaribu kutua baada ya masaa ya kawaida
ya kufunga kiwanja (saa 12.30 jioni)kupita.



Chanzo:JamiiForum

President Uhuru After Inauguration

Hapo Juu ni baadhi ya picha za Rais wa Jamuhuri ya Kenya Mh. Uhuru
Kenyatta siku chache baada ya Kuapishwa Akiwa na Makamu wake Mh.
William Ruto, Mpinzani mkuu katika Uchanguzi wa Kenya Mh. Raila Odinga
pamoja na mgombea mwenza Mh. Karonzo Musyoka.
Pia Rais wa Burundu Mh. Nkurunzinza na Mkewe na Pamoja na First lady
wa Kenya Mrs. Kenyatta

Ambwene Yesaya Awa Verified Twitter

Msanii wa muziki wa kizazi kipya Nchini Ambwene Yesaya (AY) Amekuwa
verified katika mtandao wa kijamii wa Twitter, Amekuwa msanii wa
kwanza wa Muziki Tanzania kutambuliwa na Twitter, Kwa Upande mwingine
Watanzania ambao wako verified katika Twitter ni Raiswa Jamhuri ya
Tanzania Jakaya Mrisho Kikwete (@jmkikwete), January Makamba
(@JMakamba), Hasheem Thabiti (@hasheemthedream), Flaviana Matata
(@Flavianamatata), Ambwene Yesaya (@AyTanzania)
Kwa kitendo Hicho kinaifanya Tanzania kuendelea kutambulika Duniani
Hasa kwa uwakilishi Unaofanywa na AY

Zombie Gangnam Style

Lol! Oppa Gangnam style watu na ujuzi wao now ni kw zombie style cheki video hapo juu.

CAG: Aagiza Kumbi za Harusi, M-Pesa,Tigo Pesa na Zinginezo Kutozwa Kodi

MKAGUZI na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Ludovick Utouh,
ameshauri kampuni za simu zinazotoa huduma ya utumaji fedha na kumbi
za harusi vitozwe kodi. Sambamba na hilo aliutaka uongozi wa Bunge,
kurejesha Kamati ya Ukaguzi wa Hesabu za Mashirika ya Umma (POAC).
Alisema hayo alipozungumza na waandishi wa habari baada ya kuwasilisha
taarifa yake bungeni mjini hapa jana akisema uamuzi wa kufuta kamati
hiyo na kazi zake kuunganishwa na Kamati ya Hesabu za Serikali (PAC),
hautakidhi matarajio ya wadau wa uwajibikaji.
Kwa upande wa kodi, alishauri kodi kutoka kwa wafanyabiashara wadogo,
Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) ihusishe kikamilifu makatibu kata
kutambua walipa kodi wakiwamo wamiliki wa kumbi za harusi na mikutano.
Akifafanua kuhusu kodi kwenye kampuni za simu za mkononi alitaka
zitozwe kodi ya zuio la malipo ghafi ya kamisheni, inayolipwa kwa
wanaofanya biashara hiyo ya kuhamisha fedha kwa niaba ya kampuni.
Uhamishaji fedha hizo unafaywa kwa kupitia mifumo ya M-pesa, Tigo
Pesa, Airtel Money na Easy Pesa.
Alishauri kodi hiyo ya zuio, ipunguzwe kutoka kodi ya mwisho
inayotakiwa kulipwa na kampuni za simu.
Kamati ya POAC Utouh alisema PAC itazidiwa na wingi na ukubwa wa
majukumu na akatoa mfano, kuwa hata kabla ya kamati hizo kuunganishwa,
kamati hizo mbili zilikuwa zinazidiwa.
Alisisitiza kuwa ni jambo jema POAC irejeshwe kwa jina lolote, lakini
kazi zake zibaki zile zile.
"Kuna mashirika 176, ukiweka na taasisi za Serikali mzigo unakuwa
mkubwa na PAC hii ya Zitto (Kabwe ambaye ni mwenyekiti), kama
atafanikiwa hata nusu ya kazi zake, itakuwa ni muujiza.
"Hivyo nashauri tuone uwezekano wa kurudishakamati hii hata kama
itakuwa na haja ya kubadilisha jina, iitwe ya mashirika ya umma auya
uwekezaji, lakini ifanye kazi za POAC," alisema Utouh. Wabunge na CAG
pia alisisitiza kuwa licha ya Serikali kufanya mabadiliko ya sheria ya
ukaguzi wa umma, mabadiliko hayo hayajaingilia uhuru wa ofisi yake
kutimiza wajibu wake.
Hata hivyo, Mwenyekiti wa PAC, alilalamikia sheria hiyo kuwa inawaziba
midomo wabunge kwa vile wanazuiwa kujadili ripoti ya CAG.
Zitto alisema mfumo uliokuwapo wa kuwasilisha ripoti za kamati za
Bunge, umefutwa na Serikali baada ya kutunga sheria, na Serikali
inachotaka ni Bunge kujadili ripoti hizo kupitia kamati zake kabla ya
kujadiliwa na Bunge zima.
Makamu Mwenyekiti wa PAC, Deo Filikunjombe alisema Serikali imetunga
sheria hiyo kwa vile haitaki kusimamiwa na Bunge, ila inataka Bunge
kiwe chombo cha kujadili tu. Alisema hilohalikubaliki na akasisitiza
kuwa kamwe hawataruhusu ripoti za kamati ya CAG isijadiliwe bungeni.
"Tunatumia miezi mitatu kuomba fedha za Watanzania, lakini linakuja
suala la kuhoji matumizi yake kwa sasa tunanyimwa fursa
hii…hatuikubali ni lazima ripoti hizi zijadiliwe namwenye kuwajibika
awajibike kama ilivyotokea mwaka jana," alisema Filikunjombe.
Mwenyekiti wa PAC wa zamani John Cheyo alisema sheria hiyo mpya ya
Ukaguzi wa Umma, inaifedhehesha Serikali na akashauri marekebisho hayo
yafutwe na Bunge ili kutoa fursa ya ripoti ya CAG kujadiliwa.
"Tulikuwa tunakwenda mbele sasa na mabungemengine yalikuwa yanakuja
hapa kujifunza namna tunavyoshirikiana na CAG kusimamia fedha za umma,
lakini sheria hii ya sasa inaturudisha nyuma, tusikubali ni lazima
ripoti hii ijadiliwe bungeni," alisema Cheyo.
Misamaha ya kodi Wakati huo huo, CAG alisema ataanza ukaguzi kwenye
misamaha ya kodi kwa vile fedha ambazo zingelipwa kutokana na
misamaha, ni za Serikali ambazo zinatolewa kama ruzuku kwa wanaopewa
misamaha hiyo.
"Tumeamua kuikagua kwa kina misamaha yote ya kodi kuanzia mwaka ujao
wa fedha kwa madhumuni ya kuangalia manufaa ya misamaha hiyo kwa
uchumi wa Taifa," alisema Utouh.
Lakini CAG alitaka hati za misamaha ya kodi, ziwekwe bayana kuwa
msamaha wa kodi ni wa muda gani, unaanza lini na kumalizika lini.
Alitaka misamaha ya kodi ianishwe ikionesha malengo yanayokusudiwa na
kuwa na utaratibuwa Serikali kusimamia utekelezaji wa misamaha hiyo.
Ameshauri pia mikataba yote yenye vipengele vya misamaha ya kodi,
ipitiwe na Mwanasheria Mkuu wa Serikali kwa ajili ya ushauri kabla ya
kusainiwa na pande husika.
Pia alishauri mikataba ya kuchimba madini, ijadiliwe na Kamati ya
Bunge inayoshughulikia masuala ya madini, na ushauri utolewe kwa
waziri husika kabla ya kusainiwa.



Chanzo:HabariLeo

Serikali Yagomea Ushauri Wa Wabunge

Serikali imekataa ushauri wa wabunge na kusema kuwa itaendelea
kuwaajiri wastaafu mbalimbali nchini hadi hapo soko la ajira
litakapojitosheleza.
Mbali na hilo, jana Serikali ilitangaza bungeni kuwa kazi za wakuu wa
mikoa siyo ajira rasmi, bali ni ajira za kisiasa ambazo hazipaswi
kuhesabiwa.
Akijibu swali bungeni jana, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Menejimenti
ya Utumishi wa Umma) Celina Kombani, alikiri kuwa bado Serikali
inaendelea kutoa ajira kwa watu ambao wamestaafu na kuwa itaendelea
kufanya hivyo kwa siku za usoni.
Alikuwa akijibu swali la Vicent Nyerere (Musoma-Chadema) ambaye
alitaka kujua Serikali ina mpango gani wa kusitisha kutoa mikataba kwa
wastaafu ili wahitimu wanaotoka vyuoni wapate ajira na kujenga nchi
yao.
Mbunge huyo pia alihoji nafasi za wakuu wa mikoa nchini ambao wengi
hufanya kazi wakiwa katika umri mkubwa, huku baadhi wakiwa wamestaafu
utumishi wa umma. Waziri alisema ni kweli kuwa wako wataalamu wengi
wanaohitimu vyuo vikuu hapa nchiniambao wanahitaji kuingia katika soko
la ajira, lakini hupatiwa ajira kulingana na uwezo na bajeti ya
Serikali.
Kuhusu wastaafu kuendelea kupewa ajira, alisema "Hilo linatokana na
utaalamu walionao ambao ni vigumu kuziba nafasi zao kwa kipindi cha
haraka."
Kombani alizitaja kada ambazo Serikali inatoa mikataba kwa wastaafu
kuwa ni walimu, waganga, wahandisi na wahadhiri wa vyuo ambao alisema
nafasi zao ni adimu.



Chanzo:Mwananchi.co.tz

Tanzania Yazidi Kufukuzia Namba za Juu

Tanzania na Timu ya taifa ya mpira wa miguu imeendelea kujichukulia
nafasi kupanda juu katika viwango vya FiFa na sasa Kukwea mpaka
kufikia Nafasi ya 116 kutoka 119 katika takwimu zilizotolewa mwezi
uliopita wa March. Tanzania Imepata Points 3 baada ya Kuichabanga Timu
ya Taifa ya Morocco kwa goli Tatu kwa moja Katika uwanja wa Taifa
Jijini Dar es salaam mwenzi March, ambapo ulikuwa na Mchezo wa
kutafuta Nafasi ya kufuzu Kucheza final za kombe la Dunia , Michuano
hiyo Itafanyika Nchini Brazili mwakani(2014). Tanzania Katika michuano
Hiyo Ipo Kundi moja na timu za taifa za Ivory coast Vinara wakiwa na
Points 7, Tanzania Yenyewe Points 6, Morocco points 2 na Gambia point
1 Huku zote zikiwa zimecheza Mechi Tatu kila mmoja.

Kwa Siku za Hivi Karibuni Taifa stars imekuwa wazuri zaidi katika
uwanja wa nyumbani kwa kuzifunga timu vigogo. Cameroon, Zambia na
Morocco

Picture of The Day | Picha Ya Siku

Hiyo Wikiend tayari ishafika sasa wale wa bata batani, wale wa kula
bata mpaka bata aseme bata ndo muda sasa. Enjoy Responsibly

KumbuKumbu Ya Marehemu Edward Moringe Sokoine

LEO NI KUMBUKUMBU YA MAREHEMU EDWARD MORINGE SOKOINE ALIYEFARIKI KWA
AJALI YA GARI 12/04/1984 LEO ANATIMIZA MIAKA 29

Ufuatao ni miongoni mwa maneno aliyowahi kuyatoa wakati wa Uhai wake.

"Vijana leo wengi wana mali zaidi kuliko wazee waliofanya kazi miaka
thelathini hadi arobaini. Lakini wanaitaka Serikali ndiyo iwaulize
mali hiyo wameipata wapi. Hivi kwa nini mzazi asimuulize mwanae, 'mali
hii umeipata wapi?'" - Edward Moringe Sokoine, 23 Oktoba 1983"Aliwahi
kuwa Waziri Mkuumara mbili, tangu tarehe13 Februari 1977 hadi 7
Novemba 1980, tena tangu tarehe 24 Februari 1983 hadi kifochake,
alipofariki kufuatana na ajaliya gari.
Uongozi wake ulionekana kuwa wa mfano kwa jinsi alivyokuwa na
uadilifuna kufuatilia utendaji kazi huku akikemea ulajirushwa na
ubadhirifu wa mali za umma.
Sokoine alifariki kwa ajali ya gari wakati akitoka kwenye kikao cha
bunge Dodoma kuelekea Dar es Salaam. Wengi wanashuku ajali hiyo kuwa
ilipangwa.
Kifo chake kilileta majonzi makubwa kwa Watanzania wa kawaida ambao
walikuwa wanamtarajia kuwatetea wanyonge na kuinua hali ya maisha yao.
Mwiliwa Edward Moringe Sokoine ulizikwa nyumbani kwaoMonduli, mkoaniArusha.
Chuo cha Kilimo na Mifugo Morogoro kilipewa jina la "Chuo cha Kilimo
cha Sokoine" ambacho kwa sasa ni Chuo Kikuu cha Sokoine.

Korea Kaskazini na Syria Kuzungumziwa Kwenye Mkutano wa G8

Migogoro ya Syria na Korea ndiyo itakuwa swala kuu katika agenda ya
mkutano wa nchi za G8 , baadaye hii leo mjini London Uingereza.
Duru zinasema kuwa Japan, inayoshiriki mkutano huo, inatafuta kauli
kali ambayo itaungwa mkono na nchi zote za G8 kuhusu Korea
Korea Kaskazini imekuwa ikitoa vitisho dhidi ya kambi za kijeshi za
Korea Kusini, Japan na Marekani katika eneo hilo.
Mawaziri wa mambo ya nje pia watajadiliana kuhusu mzozo wa Syria baada
ya kukutana na viongozi wa upinzani Jumatano.
Mwandishi wa BBC wa maswala ya kidiplomasia, James Robbins , anasema
kuwa mawaziri wanakubaliana kuwa vitihso vya kivita kutoka Korea
Kaskazini pamoja na maandalizi ya kufanya jaribio la makombora ni
vitisho vibaya sana
''Marekani ina msimamo mmoja na sisi kuhusu Korea Kaskazini ,'' waziri
wa mambo ya nje wa Urusi Sergei Lavrov alisema kwenye mkutano na
waziri wa mambo ya nje wa Marekani John Kerry.
Korea Kusini imetahadhari pakubwa huku kukiwa na dalili kuwa Korea
Kaskazini inajiandaa kufanya jaribio la kombora lake mpya.
Pyongyang imehamisha makombora mawili pwani mwa nchi. Makombora hayo
yanaweza kwenda umbali wa kilomita 3,000.
Inaarifiwa kuwa huenda kombora hilo likazinduliwa Jumatatu ambayo
itakuwa siku ya kuzaliwa kwa mwanzilishi wa taifa hilo KimIl-sung
Korea Kaskazini imeanza kutoa vitisho vipya baada ya kuwekewa vikwazo
vipya na Umoja wa Mataifa kufutia hatua yake ya jaribio la tatu la
nuklia.

Teknolojia ya Goli Kuanza Kutumika Ligi Kuu Uingereza

Klabu za ligi kuu soka nchini England zimepitisha sheria ya kutumia
teknolojia ya camera katika maamuzi ya mchezo wa soka kuanzia msimu
ujao.
Kampuni ya Uingereza ya Hawk-Eye imeshinda tenda na kupatiwa mkataba
wa kufunga vifaa maalumu kwenye viwanja vyote 20 vya timu za ligi kuu
nchini England.
Hawk-Eye itafunga kamera saba kwenye kila goli maalumu kwa kutambua
kama mpira umevuka mstari wa goli na kumjulisha mwamuzi wa mchezo huo
kupitia saa yake ya mkononi,na imesemainauhakika hakuna marejeo yoyote
ya matangazo ya picha ambayo yatapingana na maamuzi ya teknolojia
hiyo.
Kampuni hiyo ya Hawk-Eye inajulikana kwa kufunga teknolojia kama hiyo
kwenye mchezo wa Tenesi na Kriketi,ambapo camera maalumu huweza
kutambua iwapo mpira umegusa mstari ama la na kumjulisha mwamuzi na
wasaidizi wake ndani ya sekunde chache.
Chama cha soka nchini England FA,kitafunga vifaa hivyo kwenye uwanja
wa Wembley tayari kwa kutumika kwenye mchezo wa ngao ya jamii hapo
mwezi wa nane mwaka huu.
Vilabu vikubwa vyote nchini England vimepiga kura ya kupitisha maamuzi
hayo katika mkutano wao uliofanyika hii leo jijini London,Huku viwanja
vingine vya timu 17 zitakazosalia ligi kuu na zile 3 zitakazopanda
daraja vitawekewa teknolojia hiyo na shughuli nzima itachukua wiki
sita kukamilika.
Msukumo wa kutumia teknolojia maalumu ya kutambua goli ilipata nguvu
baada England kukataliwa goli lao la kusawazisha walipocheza na
Ukraine,Mchezo ambao England walifungwa bao moja kwa bila kwenye
michuano ya kombe la mataifa barani Ulaya mwaka 2012, Ambapo mwezi
mmoja baadaye bodi ya vyama vya soka vya kimataifa (IFAB) katika kikao
chake mjini Zurich kilipitisha teknolojia mbili ili zitumike kwenye
michezo ya soka.
Nalo shirikisho la kandanda Ulimwenguni FIFA kupitia kwa rais wake
Sepp Blater alisema kukataliwa kwa goli la Frank Lampard kwenye mechi
ya robo fainali kati ya England na Ujerumani mwaka 2010 katika
michuano ya kombe la dunia,kulichangia kwa kiasi kikubwa maamuzi ya
shirikisho hilo kupitisha sheria ya matumizi ya teknolojia ya kutambua
goli.
Chama cha soka cha England kimesema kingependa kuona teknolojia hiyo
inaanza kutumika kwa vitendo haraka iwezekanavyo.

Spika Anne Makinda Awafutia Kesi Wabunge Wa Chadema

SPIKA wa Bunge, Anne Makinda, amepata wakati mgumu kuwashawishi
wabunge wakubali mabadiliko ya kanuni mpya zitakazotumika wakati wa
mjadala wabajeti.
Hali hiyo ilitokea jana ndani ya Ukumbi wa Pius Msekwa ambapo wabunge
wote walikutana pamoja na mambo mengine kupitia mabadiliko ya kanuni
zitakazotumika kwa ajili ya utaratibu mpya wa kupitisha bajeti.
Habari kutoka ndani ya kikao hicho, zilisema kuwa kanuni iliyopingwa
na wabunge wengi, hasa wa Chama Cha Mapinduzi ni ile iliyotaka majina
ya wachangiaji wa mijadala ya bajeti za wizara mbalimbali yapitie na
kuteuliwa kwenye vyama vyao.
Kanuni hiyo ni tofauti na ya sasa ambapo majina ya wabunge wanaotaka
kuchangia, hupelekwa kwa Spikamoja kwa moja na wabunge wenyewe na
ndiye anayeteua majina ya wachangiaji.
Kwa mujibu wa habari hizo, idadi kubwa ya wabunge waliopinga ni wa
CCM, ambao walidai kuwa utaratibu huo utakuwa na upendeleo, kwani
viongozi watakaoletewa majina hayo wanaweza wasiyateua kutokana na
tofauti miongoni mwao.
"Sisi tumekataa kwa sababu majina ya wabunge wanaotaka kuchangia
yatapitia kwa viongozi wa vyama bungeni, kisha wao wanayapeleka kwa
Spika. Viongozi hao ni kina Jenister Mhagama. Kama hakupendi,
hatapeleka jina," alisema Mbunge mmoja wa CCM.
Mbunge machachari mwingie ambaye amewahi kuitwa mara kadhaa na
viongozi wa chama chake na kumtaka aache kuishambulia serikali,
alisema kuwa utaratibu huo utamnyima haki ya kuchangia bungeni kwani
anaamini hata viongozi wa CCM walio nje ya Bunge, wataingilia kati
kutaka asipewe nafasi. Mbunge huyo ambaye jina lake tunalihifadhi,
alimtakaSpika kuacha kukwepa majukumu yake.
Endapo kanuni hiyo itapita, itaanza kutumika leo baada ya Waziri Mkuu,
Mizengo Pinda, kusoma hotuba ya bajeti ya wizara yake kwa mwaka wa
fedha2013/2014.
Kabla ya Pinda kuwasilisha bajeti ya ofisi yake, wabunge wanatarajiwa
kupitisha mabadiliko machache ya kanuni na huenda kukawa na mvutano wa
kupitisha kanuni hizo.
Bunge litaanza kupitia na kujadili hotuba za bajeti za wizara
mbalimbali ambapo mwaka huu zitaanza wizara kabla ya kusomwa kwa
bajeti ya serikali.
Katika hatua nyingine, Spika wa Bunge, Makinda, amefuta kesi ya
wabunge wa CHADEMA waliodaiwa kufanya vurugu katika mkutano wa 10 wa
Bunge mjiniDodoma.
Spika aliwataka wabunge hao kusahau yaliyopita na kuanza moja, kwani
lengo la wabunge ni kuwatumikiawananchi waliowachagua.
Habari kutoka ndani ya kikao hicho, zilisema kuwa baadhi ya wabunge wa
CHADEMA walimwonya Spika kuwa kama ataendelea na staili yake ya
kuwabana wapinzani na kukiuka kanuni hawatavumilia.

Jamaa Auwa Watoto Kikatili

JESHI la Polisi mkoani Katavi, linamshikilia mkazi wa Kijiji cha Majimoto wilayani Mlele, Justine Albert (24), kwa kosa la kuwaua kikatili watoto wake wawili kwa kuwanyonga. na kisha kumjeruhi vibaya mke na kuwatumbukiza wote katika kisima kilicho karibu na kijiji hicho.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Katavi, Dhahiri Kidavashari alisema mauaji hayo yalitokea saa 11:30 alfajiri usiku wa kuamkia juzi.

Inasemekana kwa muda mrefu mtuhumiwa, alikuwa akimtuhumu mkewe kuwa na mahusiano ya kimapenzi na jirani yao na kwamba baadhi ya watoto wanadaiwa kuzaliwa nje ya ndoa yao.

Kwa mujibu wa chanzo cha kuaminika kutoka ndani ya familia, watoto walionyongwa na baba yao ni Frank Justine (6),  na Elizabeth Justine (4), na mke wa mtuhumiwa, Jackline Lwiche (21) ambaye alifariki hospitali kwa matibabu.

Akisimulia tukio hilo ndugu wa Jackline anasema mama huyo ambaye alitumbukizwa kisimani akiwa hai alifanikiwa kumuokoa mtoto wake mmoja wa mwisho, Maria Justine mwenye umri wa miezi sita kwa kumtupa nje ya kisima, Maria Justine mwenye umri wa miezi sita.

Mama huyo aliyeopolewa majini na majirani akiwa hajitambui kwa kunywa maji mengi, na mtoto aliokotwa na majirani siku moja baada ya tukio akiwa na majeraha madogo mwilini mwake

Akisimulia mkasa huo, alisema kulipopambazuka baadhi ya wakazi wa kijiji hicho waliokuwa wakielekea kwenye shughuli zao, walimwona mtoto akiwa ametelekezwa kando ya njia na kumtambua kuwa ni Maria mwenye umri wa miezi sita, ambaye ni kitindamimba wa mtuhumiwa.
Inadaiwa ndipo walipoamua kufika nyumbani kwa mtuhumiwa na kumpatia taarifa hiyo na kuhoji alipo mama yake bila kupata majibu ya msingi.

Lakini mtuhumiwa aliwaeleza kuwa alikuwa ametoroka kusikofahamika na watoto wote.

Kutokana na maelezo hayo, wananchi hao walimtilia mashaka mtuhumiwa na kuamua kutoa taarifa kituo cha Polisi.

Baada ya polisi kwenda eneo la tukio, walimkuta kichanga (Maria) na kubaini ulikuwa na miburuzo ardhini na michubuko kitendo kilichowafanya wafuatilie mpaka kisimani.

Walipofika kisimani, waliamua kufungua mfuniko wa kisima hicho ndipo walikuta miili mitatu ikielea kwenye maji.

Kutokana na hali hiyo, polisi kwa kushirikiana na wananchi walifanikiwa kuopoa miili yote, huku mama ambaye alikuwa amekunywa maji mengi akiwa taabani na kupoteza fahamu.

Kamanda Kidavashari, alisema baada ya kumuopoa mama huyo alikimbizwa kituo cha afya cha kijijini Mamba, alilazwa hapo kwa matibabu hadi mauti yalipomfika jana  jioni.



source:Katavi2date

Picha Ya Siku | Picture of the Day

Katika Picha Aliyekaa ni Rais wa Kwanza wa Jamuhuri ya Kenya Mzee Jomo
Kenyatta, na Mwanae ambaye sasa ni Rais wa Kenya Bwana Uhuru Kenyatta(Rais wa sasa wa kenya),
Walio Simama ni Rais wa Pili wa Kenya Mzee Daniel Arap Moi, na Rais
wa Tatu Ndugu Mwai Kibaki

Uhuru Kenyatta Aapishwa

Uhuru Kenyatta hii leo ameapishwa kama rais wa nne wa Jamuhuri ya
Kenya kufuatia ushindi wake dhidi ya mpinzani wake Raila Odinga katika
uchaguzi uliofanyika Machi nne.
Ushindi wake wa kwanza katika duru ya kwanza ya uchaguzi huo,
ulihalalishwa na mahakama ya juu zaidi nchini Kenya.
Kenyatta na naibu wake William Ruto, wanakabiliwa na kesi katika
mahakama ya uhalifu wa kivita iliyotokana na ghasia za baada ya
uchaguzi mkuu miaka mitano iliyopita.
Rais wa Sudan Omar al-Bashir, anayekabiliwa na kibali cha kukamatwa na
mahakama ya ICC, hatakuwepo kushiriki sherehe hizo.
Bwana Kenyatta ni mwanawe rais mwanzilishi wa Kenya, Jomo Kenyatta, na
ni mrithi wa mali nyingi sana nchini humo.
Kenyatta aliwahi kuhudumu kama naibu waziri mkuu , waziri fedha,na
waziri wa serikali za mitaa chini ya utawala wa rais
anayeondokamamlakani Mwai Kibaki.
Kenyatta mwenye urmi wa miaka 51, ni rais wa kwanza mwenye umri mdogo
zaidi kuwahi kuongoza nchi hiyo.
Raila Odinga alipinga vikali ushindi wa Kenyatta na hata kuwasilisha
kesi katika mahakama ya juu zaidi.
Baada ya uamuzi wa mahakama uliosema kuwa alichaguliwa kihalali,
Kenyatta alisema kuwa serikali yake itashirikiana na na wakenya
kuhakikisha kuwa wanawahudumia wakenya wote bila mapendeleo.
Uchaguzi huo ulikuwa wa kwanza chini ya katiba mpya na wa kwanza
katika kipindi cha miaka mitano tangu ghasia zilizoshuhudiwa baada ya
uchaguzi wa mwaka 2007.
Bwana Kenyatta anatarajiwa kufika mbele ya mahakama ya ICC kwa kesi
anayokabiliwa nayo, ya uhalifu dhidi ya binadamu.
Amekanusha madai hayo.
Kenya imetia saini mkataba wa Roma unaoishurutisha kutii mahakama ya
ICC mnamo mwaka 2002.
Lakini nchi nyingi za Afrika zimekataa kuitii mahakama hiyo na
hatakutekeleza kibali cha kumkamata rais Bashir anayetakikana na
mahakama ya ICC.

Picha Ya Siku | Picture of the Day

Kama Ukipewa Chance Kuandika Head Picha Hii Utaandika Nini?

Viboko Kurudishwa Mashuleni

Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi imesema ina mpango wa kurudisha
viboko mashuleni kama sehemuya mpango mkakati wa kuboresha na kuinua
kiwango cha elimu nchini.
Pia imepiga marufuku matumizi ya simu za mkononi kwa wanafunzi hao
kutokana na kuchangia kuporomoka kwa elimu na maadili hali inayotishia
uwepo wa taifa la mambumbu kwa miaka ijayo.
Ni katika uzinduzi wa mfumo mpya wa usomaji kwa njia ya teknolojia ya
Habari na Mawasiliano TEHAMA baina ya Walimu na Wanafunzi wa kupitia
mtandao.
Naibu Waziri na Mafunzo ya Ufundi Philipo Mulugo anabainisha mipango
mipya ya kurejesha nidhamu katika masomo…
Naibu Waziri Mulugo anasema mfumo huo wa elimu kwa mtandao utasaidia
kukabili uhaba wa vitabu na kubainisha kuwa ipo haja kwa wadau wengine
kujitokeza kusaidia sekta ya elimu badala ya kuelekezalawama kwa
serikali…
Faraja Nyalandu ni Mwanzilishi wa mfumo huo na hapa anaelezea jinsi
wanafunzi watakavyonufaik ­a na mfumo huo…
Mfumo huo ni sehemu ya mpango mkakati wa kuboresha elimu bora nchini
ikiwa ni pamoja na kwenda sambamba na ukuaji wa sayansi na teknolojia
mfumo ambao umeshika kasi kwenye sekta za maendeleo ya nchi nyingi
duniani.

Babu Wa Loliondo Aibuka na Mpya

MCHUNGAJI Ambilikile Masapila (78) ameibuka na kudai Mungu
amemuonyesha unyayo wa mtu wa 182 tangu kuumbwa kwa Adamu. Masapila
amekuwa maarufu kwa kutoa huduma ya dawa kwenye kikombe iliyodaiwa
kutibu magonjwa sugu. Maelfu ya watu walikwenda kunywa "kikombe hicho
cha Babu" mwaka juzi.
Akiwa ametanguliza sharti la kutopiga picha unyayo huo ulio kwenye
jiwe alilolihifadhi nyumbani kwake, Masapila aliwaambia waandishi wa
habari kuwa Mungu anaendelea kumuonyesha miujiza mingine.
"Nimepata unyayo wa mtu wa kale na Mungu ameniambia mtu huyo ni wa 182
tangu uumbaji wa Adamu na alikuwa binti anayeitwa Tutali.
"Tutali alikanyaga jiwe likazama kama mnavyoona huu ni unyayo wake…
awali Mungu alinionyesha mahali ulipokuwa na akanielekeza nikaenda
kuuchukua.
"Lakini mpaka sasa bado hajazungumza na mimi kwaajili ya kuuweka
hadharani hatua hiyo ni mpaka Mungu atakaponiruhusu," alidai Masapila.
Alipoulizwa kama amewasiliana na wanasayansi waukague na kujiridhisha
kama ni unyayo kweli, alisema hajafanya hivyo kwa vile anaendelea
kumsikiliza Mungu.
"Hamfahamu bustani ya Eden ilikuwa kwenye hili eneo la Ngorongoro.
Niwaombe Watanzania waendelee kusubiri na wenyenia mbaya wataona
maajabu zaidi," alisema Masapila.
Akifafanua kuhusu huduma yake kupungukiwa na watu, Masapila alisema,
mambo mengi yalichangia ikiwamo gharama za kufika nyumbani kwake
kunywa dawa.

Tanzania Yaionya Malawi

Membe amtaka Rais Banda aache kutapatapa
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe
SERIKALI ya Tanzania imetoa msimamo wake kuhusu mgogoro wa mpaka baina
yake na nchi jirani ya Malawi, huku ikitoa onyo kwa Serikali ya nchi
hiyo. Katika msimamo huo, Serikali ya Tanzania imeitaka Malawi
kutoendelea kutumia maji ya Ziwa Nyasa kabla ya mzozo wa kugombea
mpaka kumalizika.
Akitangaza msimamo huo jijini Dar es Salaam jana, Waziri wa Mambo ya
Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Benard Membe alisema Tanzania haipo
tayari kwenda Mahakama ya Kimataifa ya Haki (ICJ), ambako Malawi
imekimbilia.
Membe alisema Tanzania ipo tayari kuendelea na mazungumzo chini ya
jopo la usuluhishi wa migogoro, ambalo mwenyekiti wake ni Rais mstaafu
wa Msumbiji, Joackim Chisano.
Katika jopo hilo yumo Rais Mstaafu wa Afrika Kusini, Thabo Mbeki na
Rais Mstaafu wa Botswana, Festus Mogae, huku marais wastaafu wa nchi
hizo zenye mgogoro wakiondolewa.
Membe alimshangaa Rais wa Malawi, Joyce Banda kutokana na kitendo
chake cha kutangaza kutokuwa na imani na jopo hilo na badala yake
kufikia uamuzi wa kwenda mahakama ya ICJ na kusema kuwa hatua hiyo
haitamsaidia kupata umiliki wa ziwa hilo.
Hayo aliyasema Dar es Salaam jana, wakati akitoa msimamo wa Serikali
juu ya mzozo wa mpaka kati ya Tanzania na Malawi kwenye Ziwa Nyasa.
"Kabla ya kutoa msimamo wa Serikali, niwakumbushe kwamba mwaka jana
kati ya Novemba 15 na 17, tulikutana hapa Dar es Salaam lakini mkutano
ulimalizika kwa kuelewana na kutoelewana.
"Kutokana na hali hiyo, tulikubaliana wote na kuweka saini kwenda
kwenye jopo la usuluhishi wa migogoro linaloongozwa na marais
wastaafu.
"Katika mkutano huo, iliamuliwa kwamba marais wastaafu wa nchi mbili
zilizo na mzozo wasishiriki, pia tukakubaliana kwamba nchi zote mbili
zisitumie Ziwa Nyasa hadi hapo suluhisho litakapopatikana.
"Wakati tunasubiria kukutanishwa na jopo hilo, upande wa Malawi, Rais
Banda ametangaza kujitoa katika majadiliano hayo kwa sababu kadhaa
ikiwamo kutokuwana imani na jopo pamoja na kudai Tanzania imepokea
nyaraka za siri kutoka kwa jopo hilo, ili kujiandaa kupataushindi wa
madai yao.
"Banda amedai kwamba aliyetupatia nyaraka hizo ni Katibu Mkuu wa
Sekretarieti ya Usuluhishi wa Migogorobarani Afrika, John Tesha ambaye
ni Mtanzania.
"Tunasema hatujapokea nyaraka zozote za siri kutoka kwa Tesha, ili
kuondoa hofu hiyo tayari Tesha ameondolewa nafasi hiyo na nafasi hiyo
kushikwa na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa,
Leonard Simao wa Msumbiji.
"Pia amedai kuwa Tanzania tumebuni ramani mpya, hili si kweli bali
ramani mpya tulizonazo ni zile zinazotokanana mikoa na wilaya mpya
tulizozianzisha, sasa lazima zionyesha mpaka wao katika Ziwa Nyasa.
"Katika hali kama hiyo tunamchukulia Banda kama mchezaji wa mpira wa
miguu ambaye kabla ya dakika 90 kumalizika, anaamua kuchukua mpira na
kutoka nao nje bila mwamuzi kupuliza filimbi," alisema.
Msimamo wa Tanzania
Membe alisema hatua iliyochukuliwa na Malawi ya kulikataa jopo na
kuamua kwenda katika mahakama ya kimataifa, ni wazi kuwa Rais Banda
amekiuka makubaliano ya pamoja ya mwaka jana.
Hata hivyo Membe ambaye pia ni Mbunge wa Mtama, alisema Tanzania kamwe
haitakubali kuburuzwa na Malawi katika mzozo huo wakati sheria na
vielelezo vipo.
Membe alisema Tanzania haipo tayari kwenda ICJ hata kama ikiitwa leo
juu ya suala hilo, kabla ya jopo hilo kusikiliza mzozo huo na kutoa
uamuzi wake.
"Tunaiomba Malawi isitafute vurugu badala yake irudi katika jopo la
usuluhishi, kwani kuendelea kufanya hivyoni kutapatapa na kuashiria
madai yake kwamba si ya msingi.
"Namuomba Rais Banda aheshimu jopo la usuluhishi, kwa kuwa marais na
wanasheria wanaosikiliza madai yetu wana uzoefu mkubwa sana, imani
yetu watatenda haki.
"Tunamwomba kwa mara nyingine na ya mwisho kutoendelea kutumia maji ya
Ziwa Nyasa hadi hapo ufumbuzi utakapopatikana," alisema.
Siri za Banda zafichuka
Katika hatua nyingine, Membe alisema ameshangazwa na hatua ya Rais
Banda kuzunguka katika nchi mbalimbali duniani, akiomba msaada ili
kuikabili Tanzania.
Membe alisema katika ziara hizo, Rais Banda amekuwa akikutana na
viongozi wa mataifa makubwa, wakuu wa vikosi na viongozi maarufu
akiilalamikia Tanzania.
"Huyu Rais Banda ametushangaza kweli, yaani wakati tunasubiria jopo
yeye yupo katika mataifa makubwa kutulalamikia, sasa cha ajabu wale
wote aliokutana nao na kuwaeleza wamempigia simu Rais Kikwete wakihoji
kuhusu malalamiko yake.
"Si Rais Kikwete mwenyewe kapigiwa hata mimi nimepigiwa na kuulizwa na
mara zote tumewaeleza tulipofikia na hali ilivyo, pia tumewaeleza
kitendo cha mwenzetu kujitoa na hatua tulizochukua.
"Narudia kusema hii ni dalili za kuanza kutapatapa na mara zote
tunapokuwa tunadai haki yetu katika mipaka tumekuwa tukisingiziwa
kwamba tunapeleka boti, visababu kama hivyo vinafananishwa na madai ya
Rais Banda," alisema.
Hatua zilizochukuliwa Tanzania
Membe alisema kutokana na hali hiyo, tayari Tanzania imepeleka timu ya
wataalamu nchini Ujerumani katika jengo la makumbusho la dunia,
kutafuta nyaraka za Tanzania tangu ilipokuwa ikitawaliwa na wakoloni
ili kuona mipaka halisi.
Alisema tayari wataalamu hao wamekwisha rudi nchini na wamefanikiwa
kupata lundo la nyaraka ambazo zinaihakikishia Tanzania kuibuka na
ushindi katika mzozo huo.
Membe alisema nyaraka hizo zitawekwa hadharani palewatakapofikishana
mahakamani au watakapokutanishwapamoja mbele ya jopo hilo.
Mgogoro wa mpaka kwenye Ziwa Nyasa kati ya Tanzania na Malawi,
umechukua muda mrefu kutatuliwatangu enzi za Baba wa Taifa, Mwalimu
Julius Nyerere hadi leo.


Source:Mtanzania

Jela Miaka 10 kwa Kumbusu na Kumtomasa Mtoto wa Miaka 13

MAHAKAMA Hakimu ya Mkazi ya Wilaya ya Mpanda imemhukumu Kassim Lugendo
(41) mkazi wa kijiji chaKambanga tarafa ya Kabungu kifungo cha miaka
10 jela kwa kosa la kumnyonya ulimi mtoto wa kike mwenye umri wa miaka
13, anayesoma darasa la tano katika Shule ya Msingi Igalula, bila
ridhaa yake.
Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama hiyo, Chiganga Tengwa alitoa hukumu
hiyo jana baada ya kuridhika na ushahidi uliotolewa mahakamani hapo.
Awali katika kesi hiyo, Mwendesha Mashtaka, Mkaguzi wa Polisi, Ally
Mbwijo aliieleza mahakama hiyo kuwa mshitakiwa Lugendo alitenda kosa
hilo Machi 30 mwaka jana, saa sita mchana akiwa nyumbani kwake.
Ilidaiwa kuwa siku hiyo ya tukio mtoto huyo alikuwa akitoka shuleni
akielekea nyumbani kwao ndipo mshitakiwa alipoona anapita karibu ya
nyumba yake ambapo alimwita msichana huyo na kisha alimwingiza kwa
nguvu nyumbani kwake.
Mbwijo aliiambia mahakama kuwa, baada ya mshitakiwa kumwingiza ndani
ya nyumba yake msichana huyo, alianza kumnyonya ulimi kwa nguvu huku
akimtomasa sehemu za siri kwa vidole.
Ilielezwa mahakamani hapo kuwa wakati akimfanyia uovu huo, mtoto huyo
alikuwa akiomba msaada kwa kupiga kelele muda ambapo majirani walifika
eneo la tukio na kumkuta mshitakiwa akiwa ameshaanza kumvuta mtoto
huyo sketi yake ya shule.
Katika kesi hiyo, upande wa mashitaka ulileta mahakamani hapo
mashahidi watatu na mshitakiwa hakuwa na shahidi yeyote.
Akijitetea, Lugendo aliiomba mahakama isimpe adhabu kwa kile
alichokieleza kuwa yeye ana familia ya watoto saba na wazazi wake wote
wawili ni walemavu, hivyo ana watu wengi wanaomtegemea.
Hata hivyo, Hakimu Chiganga alisema kitendo alichokifanya mshitakiwa
ni cha kinyama na hatari kwani kina weza kumsababishia mtoto huyo
ugonjwa wa ukimwi. Alimtia hatiani na kumwadhibu kifungo cha miaka
kumi jela.

Viongozi Wa Uamsho Wafutiwa Kesi

MAHAKAMA ya Mwanakwerekwe, Zanzibar imefuta kesi iliyokuwa ikiwakabili
viongozi kumi wa Jumuiya ya Uamsho, visiwani Zanzibar.
Mahakama hiyo, imefikia uwamuzi huo leo, wakati viongozi hao
walipofikishwa Mahakamani hapo.
Kwa hivyo: Kutokana na hatua hio, viongozi hao sasa watakuwa
wanakabiliwa na kesi inayoendelea katika mahakama kuu ya Vuga, mjini
Zanzibar.
Mara ya mwisho viongozi hao wa Dini, walipofikishwa mahakama kuu,
chini ya Jaji Fatma Hamid, kesi yao ilipangwa kusikilizwa tena Aprili
11, mwaka huu.
Jaji Fatma, aliuagiza upande wa mashtaka kupeleka mahakamani kwa
maandishi, ombi la kuzuia kutolewa kwa dhamana kwa washtakiwa hao.
Jaji huyo aliongeza: Licha ya kwamba upande wa mashtaka umekata rufaa
kuzuia kusikilizwa kwa ombi la dhamana, mahakama itaendelea kusikiliza
kesi ya msingi pamoja na dhamana inayohusu viongozi hao.
Upande wa Mashtaka katika kesi hiyo unaongozwa Ramadhan Nassibu na
Raya Msellem, huku upande wautetezi unaongozwa na wakili, Salim Towfiq
na wenzake..

Mvutao Nani Wa Kuchinja Nyama Waendelea

Tunduma ambao ni makao makuu ya Wilaya ya Momba, Mkoa wa Mbeya, baada
kutokea mvutano mkali kuhusu nani anayepaswa kuchinja mifugo bainaya
waumini wa dini mbili; Waislamu na Wakristo.
Mamia ya polisi kutoka wilaya zinazouzunguka Mji wa Tunduma walimwagwa
na walilazimika kutumia mabomu ya machozi na maji ya kuwasha ili
kuwatawanya waandamanaji pia, kutuliza vurugu zilizodumu kwa zaidi ya
saa nne.
Vurugu hizo ambazo zinahatarisha amani, zimetokeasiku tatu tu tangu
Rais Jakaya Kikwete aonye kwamba kwamba vurugu zenye sura ya kidini ni
hatari na zinaweza kuvuruga amani na utulivu uliodumu kwa miaka mingi
nchini.
Mijadala kuhusu vurugu hizo ilitawala katika mitandao ya kijamii
ikiwamo facebook, Mabadiliko Forum na Jamii Forums ambako watu
mbalimbali walionyesha kukerwa nazo, huku wakiitaka Serikali ichukue
hatua za kudhibiti.
Kutokana na vurugu hizo zilizoanza saa 4:30 asubuhi,wakazi wa mji huo
walijifungia ndani kwa kuhofia usalama wa maisha yao, huku maduka na
shughuli za biashara nazo zikifungwa.
Mwandishi wa Mwananchi aliyekuwa katika eneo la tukio anaripoti kwamba
katika vurugu hizo, watu zaidiya 35 wamekamatwa wakiwamo Diwani wa
Kata ya Tunduma Frank Mwakajoka na Mchungaji wa Kanisa la Kiinjili la
Kilutheri Tanzania (KKKT), Gidion Mwamafupa.
Habari zaidi zinasema barabara za mji huo zilifungwa, umeme ulizimika
baada ya moto kulipuka kwenye moja ya nguzo za umeme. Pia mpaka wa
Tanzania na Zambia ulifungwa kwa muda.
Magari ya abiria na yale ya usafirishaji yaliyokuwa yakitoka na
kuelekea Zambia, Dar es Salaam, Sumbawanga na Mbeya Mjini pia
yalikwama na kusababisha usumbufu mkubwa kwa abiria. Msikiti ulivunjwa
na watu wawili akiwamo askari polisi walijeruhiwa.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya, Diwani Athumanalithibitisha kutokea
kwa vurugu hizo na kwamba tukio hilo limetokea wakati Serikali ikiwa
kwenye mazungumzo na baadhi ya wahusika katika mgogorowakiwamo
viongozi wa dini na wachinjaji wa nyama.
"Mgogoro wa kuchinja umedumu kwa siku tatu, jana kamati ya ulinzi na
usalama chini ya Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Abbas Kandoro ilikutana na
baadhi ya viongozi wa dini na wadau wa kuchinja nyama na kuna mambo
matatu ambayo yalitolewa katika mkutano huo," alisema Diwani.
Alisema katika mkutano huo Kandoro aliagiza kuwa wananchi wanatakiwa
kuwa wavumilivu katika kipindi hiki, ambacho Serikali ngazi ya kitaifa
inalishughulikiana kuwataka kuendelea na hali uchinjaji kama
ilivyokuwa awali na kila mmoja afanye kile anachoamini katika dini
yake wakati wa kula.
Hata hivyo, baadhi ya Wakristo waliafikia lakini wengine hawakuafiki.
Hivyo jana asubuhi walihamasisha maandamano katika mji huo ambayo
yalisababisha vurugu hizo.
"Pamoja na hayo yote uchunguzi wa kitaalamu tumebaini kuwa vurugu hizo
siyo za kidini, bali zimehusishwa siasa kwani hata viongozi wa dini
waliohusika ni baadhi siyo wote ambao wanajishughulisha na suala
hili," alisema Diwani.
source: .mwananchi

Auza Mtoto Wa Kaka Yake

MKAZI wa kijiji cha Mpemba wilayani Momba, anashikiliwa na Polisi
Mbeya, kwa tuhuma za kuuza mtoto wa kaka yake, ili apate fedha ya
kusaidia kesi ya baba wa mtoto huyo.
Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Mbeya, Diwani Athuman, alisema mwanamke
huyo, Tabu Mwashipete (40), mkulima katika kijiji hicho, alikamatwa
juzi saa 2 usiku akiwa katika harakati za kuuza mtoto huyo, Hosea
Mwashipete (5).
Kwa mujibu wa Kamanda Athumani, Hosea alikuwa akiuzwa kwa mkazi wa
kijiji cha Mpemba, John Sinyinza (64), kwa gharama ya Sh milioni moja.
Sababu ya kuuza mtoto huyo, kwa mujibu wa Kamanda Athumani, ni
kutafuta fedha kwa ajili ya kusaidia katika kesi inayomkabili baba wa
mtoto huyo, Simon Mwashipete anayekabiliwa na kesi ya mauaji nchini
Malawi.
Kamanda Athuman alisema mama wa mtoto huyo alikwishafariki dunia na
kumwacha Hosea nyumbani kwa shangazi yake huyo, ambaye aliamua kumuuza
ilikupata kiasi hicho cha fedha. Ilidawa tayari mwanamke huyo alipokea
Sh 100,000 na alikuwa katika mazungumzo ya kumaliziwa Sh 900,000
zilizobaki ili amkabidhi Hosea kwa Sinyinza.
Hata hivyo, Kamanda Athumani alisema wakati mwanamke huyo akisubiri
malipo, mteja wa biashara hiyo alitoa taarifa Polisi na kushiriki
mtego uliowezesha kukamatwa kwa mwanamke huyo.
Mtuhumiwa anaendelea kushikiliwa Polisi wakati taratibu za kisheria
zikiendelea kufanyika, ili afikishwemahakamani.
Wakati huo huo, Kamanda Athuman alisema mchomanyama, mkazi wa Iwambi
Mbeya, Leonard Kanyiki (35), ameuawa kwa kuchomwa kisu kifuani na
mkazi mwenzake Abdul Saiboko (33), katika ugomvi uliozukakwenye kilabu
cha pombe za kienyeji.
Alisema mauaji hayo yalifanyika juzi saa moja usiku katika eneo la
Iwambi, ambapo mtuhumiwa baada yakuona mwenzake amekufa, alijichoma
kisu kichwani kwa lengo la kujiua, lakini hakufanikiwa.
Kamanda Athuman alisema baada ya mtuhumiwa kujichoma kisu, alikamatwa
na watu waliokuwa eneo hilo na kupelekwa katika hospitali ya Rufaa
Mbeya ambako amelazwa na hali yake si nzuri. Chanzo cha ugomvi kati
yao hakijajulikana na uchunguzi unaendelea.

Rais Kikwete: Sibagui Dini

Rais Kikwete alisema hayo juzi katika hotuba yake ya ambayo huisoma kila mwishoni mwa mwezi, kauli ambayo imekuja wakati kukiwa na malalamiko kwamba Serikali imekuwa ikifumbia macho matukio ya uhalifu wenye sura ya uhasama wa kidini.

“Mimi binafsi sibagui, hushiriki shughuli za Waislamu na Wakristo kila ninapoalikwa labda nikose nafasi kwa sababu nyinginezo,” aliongeza Rais Kikwete.

Alisema kuna baadhi ya watu wamekuwa wakisema nchi inaendeshwa kwa mfumo wa Kikristo na kwamba amekuwa akipendelea kushiriki zaidi katika shughuli za Kikristo kuliko za Waislamu.
“Naambiwa kuwa niko mwepesi kushiriki maziko ya maaskofu kuliko ya masheikh wanapofariki.

“Kuna misikiti mitatu ya Jijini Dar es Salaam ambayo iliwahi kunisomea itikafu ili nife kwa sababu za kubagua dini yao.
“Katika itikafu hiyo waliwajumuisha Inspekta Jenerali wa Polisi, Said Mwema na Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Suleiman Kova,” alieleza Kikwete.
“Nimeshashiriki mazishi ya Masheikh kama nifanyavyo kwa maaskofu na watu mbalimbali Waislamu na Wakristo,” alisema.

Alifafanua pale ambapo hakushiriki mazishi ya sheikh au askofu itakuwa ni kwa sababu ya kubanwa na shughuli nyingine ambazo ni lazima zifanywe na yeye au taarifa ilikuwa ya muda mfupi.
“Waislamu desturi yetu ni kuzika mara mtu anapofariki, hicho ni kikwazo kwangu kushiriki mazishi ya masheikh hasa ikiwa ni nje ya Dar es Salaam kwa sababu ya taratibu za kumsafirisha Rais kutoka mahali pamoja kwenda pengine siyo nyepesi,” alisema Kikwete.

Alisema pia Waislamu wanadai kuwa kitabu chao kitakatifu, yaani Quran Tukufu, kinadhalilishwa kwa kuchanwa, kuchomwa moto na kukojolewa na Wakristo na Serikali haichukui hatua yoyote ya maana. Alisema imefika mahali viongozi na waumini wa dini hizo kubwa mbili kama hawatakubali kubadili mwelekeo wa sasa basi tunakoelekea ni kubaya
“Nchi yetu tutaivuruga na sifa yake ya miaka mingi ya Waislamu na Wakristo kuishi pamoja kama ndugu itatoweka. Tanzania itaacha kuwa kisiwa cha amani na kuingia katika orodha ya nchi zenye migogoro na hata vita ya wenyewe kwa wenyewe,” alisema Kikwete.

Alisema Serikali haifurahishwi na kitendo cha mtu kudhalilisha dini ya mwenzake ndiyo maana wapo wahadhiri wa dini ya Kiislamu na wahubiri wa dini ya Kikristo ambao wamekamatwa na kufunguliwa mashtaka katika matukio tofauti.
“Vyombo vya usalama vinatambua wajibu wao na kama havitimizi wajibu wao huo utakuwa ulegevu wao na siyo kwamba ni sera na maelekezo yangu au ya Serikali,” alisema Kikwete.

Aliongeza; “Mtakumbuka kuwa mara kadhaa nimewakumbusha wakuu wa mikoa, wilaya na vyombo vya usalama kuacha ajizi katika kutimiza wajibu wao kwenye suala hili.”

Kikwete alisema kuuawa kwa viongozi wa dini na kuchomwa makanisa kusichukuliwe kama Serikali yake imeshindwa kulinda usalama wa raia wake.

“Kama ingekuwa hivyo, tungeshuhudia mauaji ya raia, viongozi wa dini na matukio ya kuchomwa nyumba za ibada yakiwa mengi hapa nchini,” alisema Rais Kikwete.

Ajali ya Jengo la ghorofa lililoanguka

Kikwete alisema sheria zitafuata mkondo kwa waliosababisha kuanguka kwa jengo hilo baada ya uchunguzi unaofanywa na Bodi ya Usajili wa Wahandisi.

Alisema watakaobainika kuhusika watatakiwa kufikishwa mahakamani ikiwa ni pamoja na kufutiwa leseni zao za kuendesha shughuli za ujenzi.

Alitaka mikoa yote nchini kujifunza katika ajali hiyo kwa kufuata kanuni za ujenzi ili kuondokana na maafa yanayoweza kujitokeza.

source:Mwananchi

Aua Mkewe baada ya Kumfumania

Mkazi mmoja wa Kijiji cha Idubula, katika Kata ya Karitu ,wilayani Nzega, Tabora, amemuua mkewe kwa kumkatakata kwa mapanga baada ya kumfumania.
Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Tabora, Antony Lutta, alisema tukio hilo lilitokea usiku wa mkesha wa Sikukuu ya Pasaka.
Lutta alisema mtuhumiwa alimfumania mke wake Veronica Maganga (20) akiwa chumbani kwake na mwanamume mwingine .
Kwa mujibu wa kamanda huyo, mwanamume huyo alifanikiwa kukimbia.
Alisema  hasira za mtuhumiwa katika tukio hilo  ziliishia kwa kumtakata mke kwa panga hadi alipokufa.
Kamanda Lutta aliwataka wananchi kutojichukulia sheria mikononi mwao na badala yake, waviachie vyombo vya dola kuchukua hatua dhidi ya watuhumiwa.
“Watu wamekuwa na tabia ya kujichukulia sheria mikononi kwa kuwahukumu watuhumiwa, huo ni ukiukwaji mkubwa wa sheria za nchi na tunawasihi waache,” alisema kamanda huyo.
Alisema mtuhumiwa wa tukio hilo atafikishwa mahakamani mara baada ya kukamilika kwa upelelezi.

Chanzo: www.mwananchi.co.tz